<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=maji&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/maji/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 22 Aug 2026 21:21:12 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/#respond</comments>
					<pubDate>04 Agosti 2026 09:15:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04091305/Screenshot-2026-08-04-121218-768x440.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2324</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Maji, Maji ya kunywa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Nishati, Samaki, Samaki wa Maji safi, Shida ya Maji, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai 24, 2026, maafisa wakiwemo wawakilishi wa Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) walikuwa wakiendesha mkutano wa mashauriano ya umma mjini Bondo ndipo msukosuko ulipoanza. Dickens Ochieng’, wakili na mwanaharakati wa kijamii aliyehudhuria mkutano huo, aliiambia Mongabay kwa simu kuwa wamiliki wa ardhi walioalikwa kwenye mkutano huo wakisema &#8220;Wadagi,&#8221; neno la Kidholuo linalomaanisha &#8220;tunakataa,&#8220; kuonyesha upinzani wao dhidi ya mradi wa nyuklia. &#8220;Kisha afisa mmoja wa polisi aliyekuwa akilinda mashirika ya serikali alitumia silaha yake na kumjeruhi mtu mmoja kwa risasi, na mkutano ukageuka msukosuko papo hapo,&#8221; alisema Ochieng’. Katika siku zilizofuata, watu 17 walikamatwa na kufungwa. Hati rasmi iliyopitiwa na Mongabay inaonyesha kwamba watuhumiwa hao wanachunguzwa kwa tuhuma za shambulio na makosa chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya Kenya (Prevention of Terrorism Act). Ochieng’, ambaye amechukua jukumu la kuwatetea kisheria, alisema &#8220;kuna ukandamizaji mkubwa unaofanywa na serikali dhidi ya wanaopinga mradi huu.&#8221; &#8220;Kama wakili, ninaendelea kuiambia jamii kwamba lazima wasimame imara, kwa sababu tuhuma za ugaidi hazina uhusiano wowote na tukio lililotokea,&#8221; alisema. &#8220;Zinakusudiwa kuwatisha na kuwanyamazisha, si kuhakikisha haki inatendeka.&#8221; Hadi sasa, watuhumiwa 15 kati ya 17 wameachiwa huru baada ya wanajamii kukusanya pesa kupitia michango ya umma ili kulipia dhamana zao, zilizowekwa kati ya KSh15,000 na KSh180,000 ($116 hadi $1,391). &#8220;Katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 13:35:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Claire Asher]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/03130229/Screenshot-2026-08-03-155156-768x493.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2306</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Chembechembe ndogo za plastiki, Ikolojia, Kemikali, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Plastiki, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili dawa moja au zaidi za viuavijasumu (hali inayojulikana kama usugu dhidi ya dawa za vijiumbe, au AMR) umeongezeka kwa kasi na kuwa dharura ya afya ya umma, huku sasa ukisababisha vifo takriban milioni 5 duniani kote kila mwaka. &#8220;AMR ni tishio la kibinadamu,&#8221; anasema Tim Walsh, profesa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mkurugenzi wa biolojia katika Taasisi ya Utafiti wa Antimicrobial ya Ineos Oxford ya Uingereza, ambaye alizungumza na Mongabay kupitia njia ya simu ya video. &#8220;Itaua watu wengi zaidi [kila mwaka] kuliko Kifua Kikuu, VVU na malaria, na iwapo haitapingwa inaweza kuipita saratani kama muuaji mkubwa zaidi.&#8221; Hadi hivi karibuni, migogoro hii miwili ya kimataifa, uchafuzi wa plastiki na usugu dhidi ya viuavijasumu, ilizingatiwa tofauti na wanasayansi na watunga sera. Lakini utafiti mpya unaonyesha kuwa inahusiana kwa karibu: Taka za plastiki hukaliwa kwa haraka na vijiumbe, hivyo kuunda aina mpya ya mfumo wa ikolojia unaoitwa &#8220;plastisphere.&#8221; Aidha, bakteria wanaoishi katika mfumo huo wanastawisha uwezo mkubwa wa kustahimili viuavijasumu kwa kasi isiyo na kifani. Kipande cha plastiki ya aina ya polyethylene (kinachojulikana kama &#8220;bio-bead&#8221;), kinachotumika kusaidia kuvunja-vunja uchafu katika mitambo ya kusafisha maji taka, ambacho kimekaliwa na fangasi pamoja na vijiumbe vingine. Wakati mwingine, vipande hivi vya plastiki&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/#respond</comments>
					<pubDate>21 Julai 2026 17:56:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Kelvin Matuku]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21171918/Screenshot-2026-07-21-201312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2148</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Fedha ya mfumo wa ikolojia, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi wa Mazingira, Ufugaji Samaki, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari upya mustakabali wa uvuvi katika ziwa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi barani Afrika. “Wakati mwingine nakaa ziwani usiku mzima na kurudi na kati ya samaki 300 na 359 pekee,” anasema Otieno, ambaye amevua katika Ziwa Victoria kwa miongo kadhaa. “Samaki ni wachache na kipato pia kinapungua. Kama mvuvi, naona njia ambayo imebakia ni kukumbatia vizimba vya samaki ili tuweze kuendelea kuishi.” Ufukwe wa Paga kwenye Ziwa Victoria. Picha na Kelvin Matuku, Mongabay. Ziwa Victoria ni chanzo cha kujikimu kwa jamii za wavuvi nchini Kenya, Uganda na Tanzania, kupitia uvuvi na biashara zinazohusiana nao. Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2023, katika miaka ya hivi karibuni, Ziwa Victoria na eneo lake la vyanzo vya maji vimeathirika vibaya kutokana na “uvuvi kupita kiasi, umwagikaji wa mafuta, utiririshaji wa taka ambazo hazijatibiwa, kuenea kwa spishi vamizi, uchotaji wa maji kupita kiasi kutoka bonde la ziwa, na mabadiliko ya tabianchi, miongoni mwa sababu nyingine.” Kushuka kwa uzalishaji wa samaki Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS), uzalishaji wa samaki katika Ziwa Victoria umeshuka kutoka takriban tani za metriki 94,349 mwaka wa 2021 hadi 67,575 mwaka wa 2024. Huu ni upungufu wa zaidi ya tani 27,700 katika kipindi cha miaka mitatu. Upungufu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 17:28:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13171052/Screenshot-2026-07-13-195700-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2046</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Maji, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi wa Maji, Ufugaji Samaki, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia wangu kila siku ni kwamba naamka na mtu mwenye bidii ya kazi akichukua sehemu yangu ya kutua, akichukua eneo langu la uvuvi,&#8221; aliiambia hadhira, akielezea jinsi maendeleo ya utalii na uwekezaji mwingine wa pwani yanavyoendelea kushindana na jamii za uvuvi wa jadi kwa ajili ya kupata ufikiaji wa bahari. Kobusingye alisema wanawake wengi wanakabiliwa na hatari katika sekta ya uvuvi, mazingira duni ya kazi na shinikizo linaloongezeka kutoka kwa maendeleo yanayozidi kusukuma shughuli za uvuvi pembezoni. Katika baadhi ya jamii, haki za kitamaduni zinapuuzwa na serikali; huku kuongezeka kwa kina cha bahari, mmomonyoko wa udongo na kupungua kwa samaki wanaovuliwa kukifanya maisha ambayo tayari ni magumu kuwa magumu zaidi, aliwaambia waliohudhuria mkutano ulioandaliwa na Ocean Resilience Climate Alliance (ORCA). Licha ya changamoto hizi, Kobusingye alisema wanawake wanasalia kuwa muhimu katika kuendeleza uvuvi na uchumi wa pwani. Husindika samaki, huuza vyakula vya baharini na kusaidia familia zao, ikiwa ni pamoja na kulipa ada za shule, kutokana na mapato wanayopata. Hata hivyo, licha ya jukumu lao katika sekta hiyo, wanawake wengi bado hawana usemi mkubwa katika jinsi uvuvi unavyosimamiwa. Lovin Kobusingye pia ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kati Farms Ltd, kampuni ya usindikaji wa mazao ya kilimo. Picha kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Usalama wa chakula mashakani: Namna mvutano wa Ghuba unavyotikisa upatikanaji wa mbolea nchini Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>06 Julai 2026 16:53:00 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Achieng’ Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/06163255/Screenshot-2026-07-06-193237-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2014</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Kilimo, Chakula, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Maji, Mazao ya kilimo kimoja, Mimea, Msukosuko wa chakula, Safiri, Sekta ya Chakula, Siasa, upatikanaji wa chakula, na  Vita]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mzee Philip Kitur anatembea katikati ya safu nadhifu za mabua ya mahindi, huku majani yanayoanza kuchipua yakitoa ishara ya mavuno tele. Mkulima huyo mwenye umri wa miaka 72 anamiliki shamba la ekari 41 katika kijiji cha Kipkeikei, Kaunti ya Trans-Nzoia. Hata hivyo, nyuma ya tabasamu la Kitur kuna hofu ya kupoteza sehemu kubwa ya mavuno [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Usalama wa chakula mashakani: Namna mvutano wa Ghuba unavyotikisa upatikanaji wa mbolea nchini Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mzee Philip Kitur anatembea katikati ya safu nadhifu za mabua ya mahindi, huku majani yanayoanza kuchipua yakitoa ishara ya mavuno tele. Mkulima huyo mwenye umri wa miaka 72 anamiliki shamba la ekari 41 katika kijiji cha Kipkeikei, Kaunti ya Trans-Nzoia. Hata hivyo, nyuma ya tabasamu la Kitur kuna hofu ya kupoteza sehemu kubwa ya mavuno iwapo hatopata mbolea. &#8220;Mazao yanahitaji kuongezewa mbolea ya kukuzia, lakini sijapata mbolea ya aina ya urea; bila hiyo, naweza kupoteza hadi asilimia 30 ya mavuno yangu,&#8221; aliambia Mongabay. Mutahi Kagwe, Waziri wa Kilimo nchini Kenya, anasema nchi ina akiba ya kutosha ya mbolea, ikiwa ni pamoja na mifuko milioni 2 ya mbolea ya nyongeza. Anasema Kenya inatafuta vyanzo mbadala vya mbolea ili kuhakikisha usalama wa chakula licha ya misukosuko ya kimataifa iliyosababishwa na mvutano kati ya Iran na Marekani. &#8220;Ingawa hatuwezi kutabiri mgogoro wa Mashariki ya Kati utachukua muda gani, tumejadiliana kuhusu kupata mbolea ya urea kutoka Algeria na aina nyingine za mbolea kutoka Morocco,&#8221; Kagwe aliambia Mongabay katika mahojiano yaliyofanyika kwa njia ya mtandao. Shamba la mahindi linalomilikiwa na Dennis Chemonges, mkulima wa Cherengani, katika kaunti ya Trans-Nzoia nchini Kenya. Mazao hayo yanahitaji kuwekewa mbolea ya kukuzia. Picha na Achieng’ Otieno, Mongabay. Eneo kuu la uzalishaji wa chakula Kaunti ya Trans-Nzoia ni mojawapo ya maeneo makuu ya uzalishaji wa chakula nchini Kenya, hasa mahindi, ambayo ni chakula kikuu. Kulingana na Ripoti ya Kitaifa ya Uzalishaji wa Kilimo ya mwaka 2025 kutoka Shirika la Kitaifa la Takwimu za Kenya, Trans-Nzoia ilichangia tani 423,156 (asilimia 10.5) kati ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>25 Juni 2026 23:31:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/25230559/Our-Ocean-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1930</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai wa Baharini, Dawa ya Asili, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kasa wa baharini, Maji, Maliasili, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Misitu ya Asili, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhisho za Asili, Tamaduni za Kiasili, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Baharini, Urejesho wa Asili, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira si rasilimali za kutumia tu, bali ni urithi wa kulindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo. Nchini Kenya, ukanda wa pwani wenye urefu wa takriban kilomita 640 ni kitovu cha uchumi wa buluu unaojumuisha uvuvi, utalii, usafiri wa baharini na biashara nyingine zinazotegemea bahari. Karibu watu milioni nne wanaishi katika eneo la pwani, huku maelfu ya wavuvi na makumi ya maelfu ya kaya wakitegemea rasilimali za bahari kwa riziki zao. Hali hiyo inaifanya uhifadhi wa bahari kuwa muhimu si tu kwa mazingira bali pia kwa ustawi wa uchumi wa taifa. Muranga, ambaye sasa ni mvuvi na pia mwenyekiti wa kikundi cha kijamii cha kulinda misitu cha Sokoke, ana jukumu la kuhakikisha kuwa anapitisha elimu hiyo kwa jamii, hasa kwa vizazi vichanga, ili ihifadhiwe kwa vizazi vijavyo. Mwonekano wa sehemu ya Bahari ya Hindi jijini Mombasa, huku mikoko ikionekana upande wa kushoto. Picha na Malavika Vyawahare, Mongabay. Mikoko ni misitu ya kipekee inayostawi katika maeneo ya maji ya chumvi kwenye fukwe za bahari za kanda za kitropiki. Misitu hii huunganisha nchi kavu na bahari, ikifanya kazi muhimu katika kulinda mazingira na ustawi wa jamii za pwani. “Zamani tulikuwa tukikalishwa na mababu zetu tukisimuliwa hadithi na kanuni za kijamii ambazo zilikuwa zinalinda&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 19:10:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09143738/EACOP-Main-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1826</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Mimea, Samaki, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa kutumia takwimu za ramani na makadirio ya thamani ya kiuchumi, ripoti ya Earth Insight, shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Marekani, inaonyesha kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 liko karibu na maeneo muhimu kwa maisha ya mamilioni ya watu na usalama wa maji, na pia sehemu ambazo hutumika kama njia za uhamaji wa wanyama. Kutokana na uchambuzi huo, ripoti hiyo inahitimisha kuwa ujenzi wa bomba hilo tayari umeathiri jamii na mazingira, na kwamba usafirishaji wa mafuta utaleta hatari zaidi za muda mrefu. EACOP ni mradi wa ubia kati ya  kampuni ya TotalEnergies yenye asilimia 62 ya hisa, serikali za Uganda na Tanzania kila moja ikiwa na asilimia 15, pamoja na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) yenye asilimia 8. EACOP itasafirisha mafuta yanayochimbwa kutoka vitalu viwili kwenye bonde la Ziwa Albert: Kingfisher, linalomilikiwa na CNOOC; na Tilenga, linalomilikiwa na TotalEnergies. Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) nchini Uganda. Picha kwa hisani ya Thomas Lewton. Kwa mujibu wa Earth Insight, mradi huo unakaribia kukamilika na mafuta ya kwanza yataanza kusafirishwa mapema mwaka 2026. “Linapita moja kwa moja katika maeneo ya viumbe walio hatarini kutoweka, na eneo muhimu zaidi ni la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 15:09:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hellen Nachilongo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05125337/Baadhi-ya-wavuvi-katika-eneo-la-Kigambani-wakipakia-chakula-yakiwemo-mafuta-ya-kula-na-mahindi-tayari-kwenda-Mafia-kuvua-samaki.-Picha-na-Hellen-Nachilongo.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1784</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maudhui ya mazingira yanayoonyesha mabadiliko chanya, Mazingira, Maziwa, Sera za Mazingira, na  Sheria ya Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio endelevu pamoja na uharibifu wa mifumo ya ikolojia ya pwani. Hali ikoje? Remy Lema, Meneja wa Kiufundi wa mradi wa ‘Pamoja Tuhifadhi Bahari Yetu’ kutoka International Union for Conservation of Nature (IUCN), anasema sehemu kubwa ya uchafuzi wa bahari inatokana na taka ngumu. Anasema kuwa kwa sasa zaidi ya asilimia 80 ya uchafuzi unaopatikana baharini unatokana na taka ngumu, huku asilimia 10 hadi 12 ikihusishwa na vimiminika mbalimbali, yakiwemo mafuta, kemikali na taka nyingine za majimaji zinazomwagika kwenye mazingira ya bahari. “Bila hatua za haraka za kulinda bahari, Tanzania inaweza kupoteza moja ya rasilimali zake muhimu zaidi za kiikolojia na kiuchumi katika miaka ijayo,” anasema Lema. Uchafuzi wa bahari umegeuka kilio kwa wavuvi. Salum Khamis, anayefanyia kazi zake za uvuvi katika maeneo ya Kunduchi amelalamikia kuongezeka kwa uchafuzi wa bahari, akisema hali hiyo imeanza kuathiri shughuli zao za kila siku na kupunguza kipato kinachotegemea uvuvi. “Kwa sasa plastiki nyingi zinaelea baharini na nyingine huzama. Samaki wanakufa au kuhama maeneo haya…hii inaathiri sana kiasi cha samaki kinachopatikana,” anasema. Mvuvi mwingine kutoka eneo la Feri, Juma Said, anasema mara nyingi nyavu zao hunasa takataka badala ya samaki, jambo linalowaongezea gharama za matengenezo ya vifaa. “Zamani tulikuwa tukipata&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>04 Juni 2026 12:55:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/04131449/Screenshot-2026-06-04-161427.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1773</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Gesi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na kibayolojia. Ripoti hiyo iliyopewa jina la Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk ilitolewa leo, siku chache kabla ya mkutano wa 11 unaohusu masuala ya bahari, mkutano wa ‘Our Ocean Conference’ unaotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 16 hadi 18 mjini Mombasa, Kenya. Ripoti hiyo inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa kina cha bahari pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Bonde la Lamu limetajwa kuwa eneo linalopewa kipaumbele, ambapo miradi minane ya mafuta inayotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu, imepangwa kutekelezwa katika ukanda huo wa pwani wenye historia na utajiri mkubwa wa kiikolojia. “Uchambuzi wetu unaonesha kuwa asilimia 100 ya Miamba ya matumbawe na misitu ya mikoko katika eneo hili imefunikwa na vitalu vya mafuta na gesi. Kwa asilimia 100, maeneo haya ni ya hifadhi za baharini na pwani lakini pia ni muhimu kwa bayoanuwai,” ripoti hiyo imeeleza. Katika ripoti hiyo, Kenya imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Ripoti hiyo ilitolewa na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2026 21:58:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/31214131/Atuwa-akiwa-amezamia-bahari-kwenye-kazi-ya-kurekebisha-matumbawe-kwenye-bahari-ya-kisiwa-cha-Mnemba-Zanzibar.jpeg-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1733</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Barafu ya bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Upaukaji wa Matumbawe, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa bluu, njano na kijani hupita juu ya kichwa chake huku mwanga wa jua ukionekana kwa mbali ndani ya maji. Juu ya uso wa bahari, watalii huwa wanazunguka katika maji bila kufahamu kuhusu mfumo dhaifu wa ikolojia unaopambana kuendelea kuishi chini yake. Kwa mujibu wa waajiri wake, Atuwa, mwenye umri wa miaka 23, anaelezwa kuwa mwanamke pekee Zanzibar anayeshiriki kazi hiyo ya uzamiaji wa urejeshaji wa matumbawe. Mamlaka za Zanzibar zinaeleza kuwa miaka mitatu iliyopita, eneo la Mnemba ambako Atuwa hufanya kazi, ambalo lina baadhi ya miamba muhimu ya matumbawe ya Zanzibar, liliharibika. Makame Omar Makame, Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi Baharini Zanzibar, anasema eneo hilo la Mnemba liliathiriwa na shughuli za kibinadamu zilizokithiri. “Kulikuwa na shughuli nyingi za uvuvi zisizofuata utaratibu, msongamano wa watalii, ambapo takribani boti 200 zenye watalii zilikuwa zikiingia katika eneo la mita 200 za ukanda wa pwani kila siku,” Makame aliieleza Mongabay. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, ili kulinda mazingira, Serikali ya Zanzibar iliamua kupunguza idadi ya wageni hadi 80 kwa siku na kuongeza ada ya uhifadhi kutoka $3 hadi $25 kwa mtalii mmoja, kusitisha kwa muda shughuli za uvuvi na pia kutoa elimu kwa jamii. Hilo lilikuwa jambo muhimu kwa Atuwa na wenzake ambao wanaamini jamii zao zilihitaji mazingira&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mei 2026 17:35:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/26172956/Usenge-Beach-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1717</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Nishati ya Jua, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya nyuklia wenye thamani ya shilingi bilioni 500 za Kenya katika kaunti ya Siaya. “Kama wakala wa nishati ya nyuklia, tunasikia na kuheshimu sauti za wakazi wa Siaya. Ushiriki wa umma si jambo la kufuata taratibu tu. Ni haki ya kikatiba,” shirika hilo lilisema katika taarifa yake. Taarifa hiyo ilitolewa siku mbili baada ya wakazi wa Sakwa, Bondo katika Kaunti ya Siaya inayopakana na Ziwa Victoria, kuandamana kupinga mradi huo. Wakazi hao walieleza hofu kuhusu hatari za kimazingira iwapo ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika na lenye utajiri mkubwa wa ikolojia litachafuliwa. Pia walitaja hofu ya kupoteza riziki, chakula na mahitaji mengine muhimu. Katika taarifa yake ya kujibu maandamano hayo, iliyotiwa saini na Afisa Mkuu Mtendaji wa NuPEA, Justus Wabuyabom, shirika hilo lilisema kuwa ujenzi wa mradi huo hautaanza hadi wakazi wa Siaya waelimishwe kikamilifu na wakubaliane na mradi huo. NuPEA kubadili mkakati NuPEA iliongeza kuwa itabadilisha mkakati wake “kutoka mipango ya kitaasisi ya ngazi za juu kwenda katika uhamasishaji wa kina kwa wananchi wa vijijini” kuhusu mradi huo unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,000. Wakati huohuo, Power Shift Africa (PSA) imekosoa msisitizo wa kutumia nishati ya nyuklia kama chanzo cha umeme, ikisema kuwa hatua hiyo inaweza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>23 Mei 2026 21:35:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/23214326/Screenshot-2026-05-24-004210-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1696</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uhifadhi, na  Umeme]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika, ambalo linapatikana Kenya, Uganda na Tanzania. Mwisho wa Machi 2026, wakati wa kongamano la kimataifa kuhusu nishati ya nyuklia, Rais wa Kenya William Ruto alitangaza ujenzi wa kinu cha nyuklia chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,000 katika eneo hilo. Kwa sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu mpango huo kwenye tovuti ya Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA). Hata hivyo, Ruto alisema ujenzi utaanza mwaka ujao na kinu hicho kinatarajiwa kuanza kuzalisha umeme mwaka 2034. “Hakuna nchi yoyote duniani iliyowahi kufanikisha malengo yake ya maendeleo bila kuwa na nishati ya kutosha na ya kuaminika,” alisema Ruto. Pia alisisitiza kuwa nishati ya nyuklia inatambuliwa na Umoja wa Mataifa kama chanzo cha nishati chenye kiwango kidogo cha uzalishaji wa hewa ukaa na muhimu katika kufanikisha Agenda ya Maendeleo Endelevu ya 2030. “Kuunganisha nishati ya nyuklia katika gridi ya taifa ni hatua ya kimkakati ya kupata suluhisho la muda mrefu litakalokidhi ongezeko la mahitaji ya umeme nchini Kenya,” alisema. Katika hotuba yake, Ruto alifafanua kuwa tayari alikuwa ameshauriana na wakazi wa Siaya na kujiridhisha kuwa jamii za eneo hilo zinaunga mkono mradi huo. Hata hivyo, maandamano ya hivi karibuni yanaonyesha hali halisi ni tofauti. Aidha, ombi la kupinga mradi huo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yaathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi nchini Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2026 20:07:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20200154/Picture2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1672</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DODOMA, Tanzania &#8211; Mabadiliko ya tabianchi yametajwa kama changamoto kubwa iliyoathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026. Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi Tanzania, Abdallah Ulega, wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, mnamo Mei 20, katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika Makao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yaathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi nchini Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DODOMA, Tanzania &#8211; Mabadiliko ya tabianchi yametajwa kama changamoto kubwa iliyoathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026. Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi Tanzania, Abdallah Ulega, wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, mnamo Mei 20, katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika Makao Makuu ya Nchi, Dodoma. Amesema majanga yaliyosababishwa na mabadiliko ya tabianchi, kama vile mafuriko, yalisababisha uharibifu wa miundombinu ya barabara na madaraja katika maeneo mbalimbali nchini. Ili kukabiliana na hali kama hiyo, Waziri alisema wizara yake inaboresha miongozo ya usanifu na matumizi ya malighafi za ujenzi kwa kuzingatia uhimilivu wa miundombinu. Upandaji miti kando ya barabara kuu ni miongoni mwa hatua zinazochukuliwa na Serikali kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Picha kwa hisani ya Wizara ya Ujenzi Tanzania. “Vilevile, wizara imepanga kupanda miti 40,000 katika barabara kuu na barabara za mikoa, na kuanza maandalizi ya mpango wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi wa Sekta ya Ujenzi,” amesema waziri. Aidha, amesema wizara itaendelea kuchukua hatua za haraka kurejesha na kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko pamoja na athari nyingine za mabadiliko ya tabianchi. Gharama za uharibifu “Barabara na madaraja yaliyoathirika yatajengwa kwa viwango vinavyoweza kuhimili majanga hayo, ili kuepuka kuongeza mzigo kwa serikali kugharamia uharibifu unaojitokeza kila msimu wa mvua kubwa na kuhakikisha barabara zetu zinapitika majira yote ya mwaka hata wakati wa changamoto za hali ya hewa,” amesema Waziri. Kauli hiyo ya Waziri imekuja kipindi ambacho taifa bado linaugulia maumivu ya hasara kubwa zilizosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2026 12:50:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20124420/Waziri-Shemdoe-1-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1650</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Ikolojia, Maji, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Taka, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa kiwango cha chini. Kwa mujibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Tanzania huzalisha kati ya tani milioni 14.4 hadi milioni 20.7 za taka ngumu kila mwaka. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Riziki Shemdoe, jijini Dodoma katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira mijini. Mkutano huo uliwakutanisha viongozi waandamizi wa serikali, washirika wa maendeleo, na wataalamu wa mazingira kwa lengo la kutathmini maendeleo yaliyofikiwa na kuweka mikakati ya kuboresha mifumo ya usimamizi wa taka. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe na wadau wa usimamizi wa taka wakifuatilia mijadala katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Dodoma. Picha: Maktaba ya Wizara. Taka na fursa za kiuchumi Waziri Riziki alisema kuwa usimamizi wa taka unapaswa kuingizwa katika mikakati mipana ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa kuwa taka zinapaswa kuonekana kama rasilimali ya kiuchumi inayoweza kuzalisha ajira na kipato ikiwa zitasimamiwa ipasavyo. Aliziagiza mamlaka za serikali za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/#respond</comments>
					<pubDate>11 Mei 2026 15:28:34 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11150848/Lethome-5-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1551</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Umeme, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu zaidi ya 82. Mongabay ilimtembelea Sheikh Ibrahim Lethome alipokuwa kwenye mfungo wa Ramadhani ili kupata maoni yake kuhusu juhudi zake katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira. Lethome amejitaja kuwa aliyetekeleza kile ambacho huenda kilionekana kama jukumu dogo katika juhudi za kupinga mradi wa umeme wa makaa ya mawe huko Lamu, Kenya. Juhudi hizo ziliongozwa na viongozi wa Save Lamu pamoja na wawakilishi wa jamii, mawakili wa masuala ya mazingira, wanaharakati na taasisi za serikali pamoja na mamlaka za udhibiti kama NEMA na mahakama za mazingira. Hatimaye, mradi huo ulisitishwa Desemba mwaka 2025. Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano yake na Lynet Otieno wa Mongabay, yaliyofanyika katika ofisi za Msikiti wa Jamiah jijini Nairobi. Mongabay: Tafadhali tueleze kwa ufupi wewe ni nani, kama msomi, kiongozi wa kidini na mwanaharakati wa mazingira. Lethome: Mimi kitaaluma ni mwanasheria na msomi wa elimu ya Kiislamu. Ninafanya kazi katika fani zote mbili. Nimekuwa mwanachama wa Msikiti wa Jamiah kwa miaka 32 sasa. Ninaongoza Idara ya Dini. Pia ni mwanachama wa bodi ya kimataifa ya GreenFaith, na mwenyekiti wa bodi ya GreenFaith-Afrika, taasisi inayotumia mafundisho ya dini kuhamasisha uhifadhi wa mazingira. Mwelekeo wangu ni kuangalia jinsi mafundisho ya dini yanavyoweza kutumika kushughulikia changamoto nyingi ambazo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>01 Mei 2026 15:34:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/01152749/Antoine-Moses-akipanda-miche-ya-miti-ya-mikoko-katika-eneo-la-Tudor-Mombasa.-Picha-kwa-hisani-ya-Wizara-ya-Mazingira-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1485</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Mikoko, Misitu, Miti, Samaki, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini humo kwa siku 10 kabla ya tukio hilo, ambapo alipanda miti mingine 13,600 ili kujenga stamina katika maandalizi ya rekodi mpya. “Tumekuwa Kenya kwa siku 10 zilizopita tukipanda mikoko, tukijifunza kutoka kwa jamii na kutengeneza kumbukumbu zisizosahaulika na marafiki wapya,” alisema kabla ya jaribio hilo, na kuongeza: “Baada ya kufikia miti 10,000 chini ya saa nne wakati wa mazoezi, nilijua tuko tayari kusonga mbele zaidi.” Waziri wa Mazingira wa Kenya, Deborah Barasa, alimkaribisha Antoine na alikuwepo alipokuwa akipanda mche wake wa kwanza. Alisema: “Kenya imepata heshima kumkaribisha Antoine Moses… Jaribio lake la kijasiri la kupanda mikoko 40,000 ndani ya saa 24 katika eneo la Tudor Creek, Kaunti ya Mombasa, halimaanishi tu kuweka rekodi mpya, bali ni kubadili mwenendo wa uharibifu wa misitu kabla haujafikia hatua ya hatari. Uwepo wake unaimarisha nafasi ya Kenya kama kiongozi anayeaminika katika juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.” Timu iliyoratibiwa ya wanajamii, wahifadhi wa mazingira, maafisa wa Huduma ya Misitu Kenya, akiwemo Katibu Mkuu Gitonga Mugambi, pamoja na washirika kutoka Earthlungs, walimpa hamasa, wakitembea pamoja naye ili kumsaidia kutimiza malengo yake. Awali, Antoine aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba malengo yake ni kupanda miche 35,500 ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/#respond</comments>
					<pubDate>30 Aprili 2026 20:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/30202905/MTERA-6-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1470</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi wa Maji, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha mapato, lakini katika miaka ya hivi karibuni hali imebadilika, samaki wamepungua kwa kiasi kikubwa majini. Kimya kimya anaijuliza, ikiwa leo hakuna samaki, kesho kutwa, mtondo na mtondogoo hali itakuwaje? Mashaka haya hayamkabili Jamal pekee, bali pia wavuvi wengi nchini kote. Kilio cha wavuvi Kilio cha wavuvi nchini Tanzania ni matokeo ya athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo yameitikisa vibaya sekta ya uvuvi kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusababisha kiwango cha samaki kupungua huku baadhi ya aina ya samaki wakitoweka kabisa. Victor Tondelo, Mtaalamu Mtafiti wa Madiliko ya Tabianchi, aliiambia Mongabay kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimejidhihirisha zaidi katika rasilimali za maji (water resources) hasa kwenye mito, mabwawa na maziwa. “Kwa sababu ya kupungua kwa mvua inayonyesha na misimu inayotabirika, maji yamepungua na hivyo idadi ya samaki ambao maisha yao ni majini pia imepungua,” alieleza. Aliongeza kuwa kuwepo kwa maji machache pia husababisha joto kubwa wakati wa kiangazi na samaki na viumbe wengine wa majini hufa kutokana na joto kali. Uchunguzi wa Mongabay kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta ya uvuvi, ulijikita katika mikoa mitatu ya Morogoro, Iringa na Pwani. Katika mkoa wa Morogoro ulihusisha mto Kilombero, Luipa, Ruhudji na Mto&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Aprili 2026 21:25:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/22211810/Screenshot-2026-04-23-001707.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1429</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maji, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya kaya 15 zinaadhimisha siku hiyo bila kuwa na makazi baada ya kuzikimbia nyumba zao kufuatia maporomoko ya tope  yaliyokumba eneo lao hivi karibuni. Huko wilayani Rungwe, wanasherehekea siku hii huku wakiwa na majonzi mazito kufuatia kupoteza ndugu na jamaa zao zaidi ya watu 20 waliofariki katika maporomoko yaliyosababishwa na mafuriko yaliyotokea Machi 15, 2026. Kutokea kwa maporomoko ni miongoni mwa majanga yaliyoelezwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  katika taarifa yake kuhusu mwelekeo wa mvua za masika Machi-Mei, 2026. Katika taarifa hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (kanda ya Ziwa Victoria, nyanda za juu Kaskazini-mashariki, Pwani ya kaskazini pamoja na maeneo yaliyopo kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) katika kipindi cha miezi hiyo, vipindi vifupi vya mvua kubwa vingeweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi. Alisema matukio hayo yangeweza kuleta uharibifu wa miundombinu na mazingira, milipuko ya magonjwa, pamoja na upotevu wa mali na maisha. Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC ) nalo lilitoa tahadhari kuhusu hatari ya mvua kubwa na maporomoko ya ardhi ambayo yangeweza kusababisha uharibifu mkubwa. Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Immaculate Semesi, akizungumza na vyombo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 15:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Gerald Ahairwe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20185806/IMG_5205-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1409</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Maji, Mamalia, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchimbaji wa Mafuta, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru wa kuandamana. Saa nne asubuhi, ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Buganda Road, Katikati mwa jiji la Kampala nchini Uganda, wanaharakati wa mazingira na wanafunzi wanane walifikishwa kizimbani. Wanafunzi hao wanatoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini Uganda, na wamekuwa gerezani tangu Agosti 1, 2025, baada ya kukamatwa wakiandamana kupinga mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP. Nje ya Mahakama, kulikuwa na rasharasha za mvua. Wasiwasi ulitanda miongoni mwa wanafunzi wa vuguvugu la “Students Against EACOP” waliokuwa wamefika pale ili kuhudhuria hukumu ya Mahakama hiyo dhidi ya wenzao. Hakimu Mkazi alitangaza kuahirishwa kwa hukumu yao hadi saa nane mchana. Lakini nyakati za chakula cha mchana, kabla ya saa nane, wanafunzi walio nje waliambiwa kwamba wenzao wanane wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma (common nuisance). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Sylvia Muwonge katika chumba chake kwenye Mahakama ya Buganda Road. Mawakili, umma au hata waandishi wa habari hawakuhudhuria. Upande wa utetezi umepinga hukumu hiyo, ukisema kuwa wanafunzi hao wamenyimwa haki ya kupewa dhamana, na vile vile kunyimwa nafasi ya kuridhisha kujitetea. Kato Tumusiime, wakili wa wanaharakati hao, anaelekeza kidole cha lawama kwa upendeleo uliokuwepo katika kesi hiyo tangu mwanzo. “Hukumu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 17:31:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20141013/Screenshot-2026-03-20-171000-768x509.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1178</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Baharini, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maji, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii kama ilivyokuwa desturi. Nyama ya kasa ni tamu sana, na tulikuwa tunafurahia sana kitoweo chake,” alisema Abdallah. Kasa katika ufuo wa bahari Shimoni picha na Dzivula Gube Miaka 35 baadaye, Abdallah, ambaye amefanya uvuvi kwa miaka tisa sasa katika eneo la Shimoni, amekuwa mkereketwa mkubwa wa masuala ya kuhifadhi kasa katika kijiji chake. Abdallah pia anashirikiana na kikundi cha vijana cha Shimoni Turtle Watch kilichoko wadi ya Pongwe-Kikoneni, Shimoni, eneo bunge la Lunga Lunga katika Kaunti ya Kwale, ambacho kimefanya kazi hiyo ya uhifadhi wa kasa kwa miaka saba sasa. Hii ni kutokana na tishio la kupotea kwa kasa kutokana na uchafuzi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi, shughuli za uvuvi na ujenzi kwenye fuo za bahari. Wavuvi wanaochinja kasa waliokufa Zaidi, Abdallah na kikundi hicho walisema wamechukua hatua hiyo ya kumlinda kasa kutokana na tishio kwamba kuna wavuvi wengine ambao wanapokutana na kasa amekufa humchinja na kugawia watu nyama yake, hatua ambayo inahatarisha afya ya jamii. Farid Abdallah Mvuvi akionyesha aina ya karatasi za plastiki zipatikanazo baharini ambazo kasa hupenda kula na ni hatari kwao. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kasa ni aina ya kobe wakubwa wanaoishi baharini. Mnyama huyo hutaga mayai yake ardhini hasa katika ufukwe wa bahari, na kuyafukia humo kwa kati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 14:00:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20164352/Screenshot-2026-03-20-194312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1189</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Mamalia wa Baharini, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uongozi wa Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile wanachoeleza kuwa ni kupungua kwa kiasi kikubwa kwa idadi ya kasa, hasa katika pwani ya kaskazini-mashariki ya Unguja, ambako hapo awali kulishuhudiwa kasa wengi. Casper Morch, ambaye ni mwanaikolojia na msimamizi wa miradi wa Taasisi ya Under the Wave iliyopo Zanzibar, anasema kuna utafiti mdogo sana wa kisayansi kuhusu kasa wa baharini Zanzibar, lakini idadi ya kasa imepungua mara dufu katika miaka ya hivi karibuni. Morch anasema: “Tunajua kumekuwa na upungufu mkubwa wa kuonekana kwa kasa. Zamani wapiga mbizi walikuwa wanaona kasa 30 hadi 40 kwa wiki, lakini sasa wanajiona wenye bahati wakiona hata mmoja tu.” Mmoja wa kasa zaidi ya 350 wa Zanzibar waliohifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe ili kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu. Picha kwa hisani ya Under the Wave. Taasisi ya Under the Wave, ikishirikiana na mamlaka za Zanzibar, ilianza uhifadhi wa kasa mwaka 2020, mwaka ambao walibaini kuwa idadi ya kasa ilikuwa ikipungua kwa kasi. “Tulianzisha mara moja viota (aquaria) ambavyo hadi sasa vina kasa takribani 350. Lakini hawawezi kuzaliana kama walivyokuwa wakiishi kwenye makazi yao ya asilia. Hili ni jambo tunalolitambua na tutahakikisha wanarejea na kuwa salama,” anasema Morch. Taasisi hiyo inasema kasa wanahitaji kurudi walipotoka, lakini hilo litakuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>03 Mechi 2026 19:17:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/03185644/Sehemu-ya-mtambo-wa-kuzalisha-maji-wa-Ruvu-Chini-2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1074</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Maji, Maji ya kunywa, Shida ya Maji, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya plastiki yenye maji, zinapishana mtaani. Wanawake, akiwemo Mama Amina, wanazikimbilia kununua maji ambayo yanauzwa kuanzia TSh500 hadi TSh1,000 kwa dumu lenye ujazo wa lita 20. Mama Amina ni miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, lenye wakazi karibu 7,000,000, ambao mara kwa mara hukabiliwa na uhaba wa maji. Wakati viongozi wa Serikali ya Tanzania wanahaha kutembelea vyanzo vikuu vya maji vinavyohudumia Jiji la Dar es Salaam kujionea wenyewe namna vilivyokauka, watalaam wa masuala ya maji wanasema ukame huo ambao kwa kiasi kikubwa unachochewa na mabadiliko ya tabianchi, unaweza kupatiwa ufumbuzi wa kudumu iwapo ushauri wa kitalaam utafuatwa. Jiji la Dar es salaam ndilo lenye wakazi wengi zaidi nchini Tanzania. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mkoa huo ulikuwa na watu 5,380,000, ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza uliokuwa na watu 3,690,000. Kuanzia Novemba hadi Desemba mwaka 2025, Jiji la Dar es Slaam limekumbwa na uhaba mkubwa wa maji uliosababishwa na kupungua kwa kina cha maji cha Mto Ruvu &#8211; chanzo kikuu cha maji ya jiji hilo. Hali hiyo ilisababisha watu wenye visiwa kuuza maji kwa bei ya hadi TSh1,000 (takriban $0.5) kwa dumu la lita 20. Mamlaka ya Maji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake Jomvu Creek, Kenya wanasaidia kurejesha pwani inayotoweka kutokana na ufugaji wa kaa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/02/11/wanawake-jomvu-creek-kenya-wanasaidia-kurejesha-pwani-inayotoweka-kutokana-na-ufugaji-wa-kaa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/02/11/wanawake-jomvu-creek-kenya-wanasaidia-kurejesha-pwani-inayotoweka-kutokana-na-ufugaji-wa-kaa/#respond</comments>
					<pubDate>11 Februari 2026 22:36:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asha Bekidusa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/02223157/Screenshot-2026-03-03-002712-1-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1062</guid>

					
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Maji, Mazingira, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Misitu, Samaki, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mombasa, Kenya — Umbali kama wa dakika tano tu za kutembea kupandisha barabara ya mlimani kutoka mikoko inayozunguka eneo la tambarare la Jomvu Creek, harufu kali ya maji ya bahari imejaa hewani. Kundi la wanawake limeujaza ukumbi mdogo kwa vicheko na mazungumzo. Katika vijiji vya pwani, Kaunti ya Mombasa, mikusanyiko kama hii ya wanawake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/02/11/wanawake-jomvu-creek-kenya-wanasaidia-kurejesha-pwani-inayotoweka-kutokana-na-ufugaji-wa-kaa/" data-wpel-link="internal">Wanawake Jomvu Creek, Kenya wanasaidia kurejesha pwani inayotoweka kutokana na ufugaji wa kaa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mombasa, Kenya — Umbali kama wa dakika tano tu za kutembea kupandisha barabara ya mlimani kutoka mikoko inayozunguka eneo la tambarare la Jomvu Creek, harufu kali ya maji ya bahari imejaa hewani. Kundi la wanawake limeujaza ukumbi mdogo kwa vicheko na mazungumzo. Katika vijiji vya pwani, Kaunti ya Mombasa, mikusanyiko kama hii ya wanawake ya kusimamia vikundi visivyo rasmi vya akiba na mikopo hujulikana kama chama. Lakini hiki si chama cha kawaida. Hapa, mijadala huzungumzia mawimbi ya bahari, chakula cha kaa pamoja na ukarabati wa vizimba na miche ya mikoko. Wanawake hao, wenye umri wa kati ya miaka 35 hadi 60, ni wanachama wa Jomvu Women in Fisheries and Culture, shirika la kijamii linalolenga kubadilisha maisha na mazingira yao kupitia mradi wa ufugaji wa kaa. Miaka minne iliyopita, wanawake hawa walikuwa wametawanyika kijijini humo. Wengi wao walifanya kazi inayojulikana kwa wengi kama mama karanga, yaani wanawake wanaokaanga samaki juu ya makaa ya mawe na kuuza karibu na fukwe ambako wavuvi hushusha samaki wao. Baadhi walikuwa wakiuza samaki wabichi huku wengine wakibaki nyumbani wakilea watoto na wajukuu. Hata hivyo, kupungua kwa samaki baharini, matatizo ya kiafya yatokanayo na moshi wa kuni na kutokuwa na uhakika wa mapato ya biashara ndogondogo vilianza kuwaathiri. Mwaka 2021, mradi wa Kenya Marine Fisheries and Socio-Economic Development (KEMFSED) ulipotangaza ruzuku kwa miradi ya uchumi wa buluu, baadhi ya wanawake hawa waliamua kuchangamkia fursa hiyo. Wanawake hao wamegeuza kreti zilizokuwa zikitumika kusafirisha mikate na kuzifanya kuwa vizimba vya kufugia kaa wao. Picha na Asha Bekidusa, Mongabay. Dhana Mpya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/02/11/wanawake-jomvu-creek-kenya-wanasaidia-kurejesha-pwani-inayotoweka-kutokana-na-ufugaji-wa-kaa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/02/11/wanawake-jomvu-creek-kenya-wanasaidia-kurejesha-pwani-inayotoweka-kutokana-na-ufugaji-wa-kaa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Barafu zikififia kileleni, jamii karibu na Mlima Kenya zinatafuta suluhisho za uhifadhi na kilimo himilivu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/16/barafu-zikififia-kileleni-jamii-karibu-na-mlima-kenya-zinatafuta-suluhisho-za-uhifadhi-na-kilimo-himilivu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/16/barafu-zikififia-kileleni-jamii-karibu-na-mlima-kenya-zinatafuta-suluhisho-za-uhifadhi-na-kilimo-himilivu/#respond</comments>
					<pubDate>16 Januari 2026 13:59:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amos Kareithi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/17041951/Screenshot-2026-01-17-071935-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=958</guid>

					
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Samaki, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni nakala ya pili katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya kwanza hapa. Kumbukumbu za maisha ya utotoni za Gerald Ngatia, afisa mstaafu wa misitu, mwenye umri wa miaka 74, zimemwezesha kusimulia jinsi hapo awali Mto Sagana ungeweza kumbeba tembo na kumpelekea nyanda za chini. “Leo hata panya anaweza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/16/barafu-zikififia-kileleni-jamii-karibu-na-mlima-kenya-zinatafuta-suluhisho-za-uhifadhi-na-kilimo-himilivu/" data-wpel-link="internal">Barafu zikififia kileleni, jamii karibu na Mlima Kenya zinatafuta suluhisho za uhifadhi na kilimo himilivu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni nakala ya pili katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya kwanza hapa. Kumbukumbu za maisha ya utotoni za Gerald Ngatia, afisa mstaafu wa misitu, mwenye umri wa miaka 74, zimemwezesha kusimulia jinsi hapo awali Mto Sagana ungeweza kumbeba tembo na kumpelekea nyanda za chini. “Leo hata panya anaweza kuuvuka mto. Wakati mwingine tunafanya mikutano ya uhifadhi huku tukikalia mawe katikati ya mto uliokauka kati ya mwezi wa Septemba na mwezi Oktoba, wakati mtiririko wake wa kimazingira uko chini sana,” Ngatia, ambaye ameishi pembezoni mwa Msitu wa Hombe katika Mpango wa Makazi ya Sagana tangu utotoni, aliielezea Mongabay. Gerald Ngatia, afisa mstaafu wa misitu, mwenye umri wa miaka 74, akiwa katika ziara zake karibu na Mto Sagana. Picha na Amos Kareithi. Waendeshaji wa mitumbwi wakipita kwenye maji ya Mto Sagana wakati wa majaribio ya mashindano katika kambi ya maporomoko ya maji ya Sagana mnamo Julai 2025, wakati wa mvua. Picha na Morris Githenya. Hata hivyo, Mto Sagana sio pekee ulioko kwenye mfumo tata wa ikolojia ya Mlima Kenya, ambao viwango vyake vya maji vimepungua mara kadhaa. Mito Rigati na Thegu, ambayo hupokea maji yao kutoka Mlima Kenya na katika hatua mbalimbali kuungana na Mto Sagana, pia inajikakamua. Juu zaidi ya nyanda za juu za Laikipia, Mongabay ilipata mito mingine mikavu. Wafugaji wa mbuzi walikaa juu ya mawe yaliyopogwa kwa maji huku mifugo wao wakijaribu kunywa maji kutoka kwenye vidimbwi madogo yenye harufu kwenye mito hiyo mikavu. Ruth Waithera, anayeishi karibu na Mto Nanyuki, anahadithia kwamba alilazimika kufua nguo katika kile&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/16/barafu-zikififia-kileleni-jamii-karibu-na-mlima-kenya-zinatafuta-suluhisho-za-uhifadhi-na-kilimo-himilivu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/16/barafu-zikififia-kileleni-jamii-karibu-na-mlima-kenya-zinatafuta-suluhisho-za-uhifadhi-na-kilimo-himilivu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/#respond</comments>
					<pubDate>13 Januari 2026 21:05:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amos Kareithi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/14135833/Screenshot-2026-01-14-165633-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=931</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Barafu, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Milima, Misitu, Misitu ya Milimani, Miti, Samaki, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa kihistoria hakumaanishi tu kupotea kwa mandhari ya asili, bali pia kunafungua ukurasa mpya wa changamoto kwa mazingira, mito, na jamii zinazoutegemea. Safari ya Lewis Pugh, Msimamizi wa Mradi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), hadi kwenye barafu za mwisho za Mlima Kenya, inatoa taswira ya kusikitisha ya athari halisi za mabadiliko ya tabianchi, zinazotoka juu ya mlima na kushuka hadi mashambani, misituni na vijijini, ambako maji, imani na maisha yenyewe yako hatarini. Pugh, aliyeshikilia nafasi hiyo katika shirika la UNEP tangu mwaka 2013, aliwasili nchini Kenya kwa matumaini kuwa uwezo wake wa kutoa hotuba zenye mvuto, ulioimarishwa kwa miaka 27 iliyopita, ungezivutia hisia za dunia, kwa namna fulani, kwenye athari mbaya za ongezeko la joto duniani katika eneo la Mlima Kenya. Lewis Pugh, Mwakilishi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), aliyeukwea Mlima Kenya mnamo Desemba 2025. Picha na Duncan Moore, UNEP. Huku ulimwengu ukijiandaa kwa sikukuu ya Krismasi, kati ya tarehe 4 hadi tarehe 8 mwezi Desemba 2025, Pugh aliparaga kupitia miamba iliyomikali ya volkeno, baadhi ikiwa na umri wa miaka milioni 4, hadi urefu wa mita 4,985 (futi 16,355) juu ya kilele cha Lenana. Lengo lake kuu lilikuwa kuogelea katika Ziwa Lewis.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi kampeni inayoongozwa na vijana inavyorejesha uhai wa ardhi oevu ya Dunga katika Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>05 Januari 2026 15:12:10 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Achieng’ Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/05144052/PAPYRUS-REEDS-PLANTATION-AT-DUNGA-BEACH-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=886</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Kijani, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Maji, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Ndege, Samaki, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miale ya jua imechomoza na kutengeneza mwanga wa kupendeza juu ya Ziwa Victoria, Afrika Mashariki. Upepo mwanana kutoka ziwani umebeba sauti za kuvutia za ndege, huku mitumbwi ya mbao ya kawaida ikitia nanga taratibu ufukweni. Maji yametulia. Mara kwa mara, ndege aina ya African sacred ibis (Threskiornis aethiopicus) huruka kwa ustadi mkubwa na kunyakua samaki kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jinsi kampeni inayoongozwa na vijana inavyorejesha uhai wa ardhi oevu ya Dunga katika Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miale ya jua imechomoza na kutengeneza mwanga wa kupendeza juu ya Ziwa Victoria, Afrika Mashariki. Upepo mwanana kutoka ziwani umebeba sauti za kuvutia za ndege, huku mitumbwi ya mbao ya kawaida ikitia nanga taratibu ufukweni. Maji yametulia. Mara kwa mara, ndege aina ya African sacred ibis (Threskiornis aethiopicus) huruka kwa ustadi mkubwa na kunyakua samaki kwa midomo yao kisha hupaa. Mazingira ya Ufukwe wa Dunga ni ya utulivu na amani. Baada ya saa chache, wauza samaki watawasili kuanza majadiliano ya bei na wavuvi waliokesha usiku kucha wakivuta nyavu, ambazo mara nyingi hurudi zikiwa karibu tupu. Kwenye kijito kilichopo nyuma ya msururu wa vibanda vilivyojengwa kwa mbao na bati, njia nyembamba iliyozibwa na mashina ya magugu maji (water hyacinth) yaliyokaushwa imepinda kuelekea kwenye njia ya mbao iliyoinuliwa. Victor Ochieng’ Didi, mwenye umri wa miaka 32, anatembea juu ya mbao hizo akiwa na kundi la watalii wa Kenya. Watazamaji wa ndege kwa mwaka mzima wamekuwa wakipanga kutembelea eneo hilo na kushuhudia mandhari ya kuvutia yenye ndege aina ya papyrus gonolek (Laniarius mufumbiri), ambaye kwa mujibu wa Orodha Nyekundu ya IUCN, ameorodheshwa kama aliye katika hatari ya kutoweka (near threatened). Kulingana na tovuti ya ufuatiliaji wa ndege ya EBird, ndege huyo alionekana mara ya mwisho katika eneo oevu la Dunga mwaka 2024. Victor Ochieng Didi, mwanamazingira na mkazi wa Dunga, Nyalenda, ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya mazingira ya Kikundi cha Utalii wa Ikolojia na Mazingira cha Dunga (DECTTA), ambacho kimekuwa kikifanya juhudi za kufufua ardhi oevu iliyowahi kustawi. Picha na Achieng’ Otieno. Juhudi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/#respond</comments>
					<pubDate>30 Desemba 2025 14:08:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mongabay.com]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/13140426/Screenshot-2026-01-13-165604-768x482.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=922</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maji, Mazingira, Maziwa, Mito, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ulilenga kuboresha sekta ya uvuvi kwa kubadilisha boti za mbao zilizopitwa na wakati kwa vyombo vya kisasa vya kuvulia. Rais Samia alipotembelea Kilwa miezi miwili kabla ya uzinduzi wa mpango huo, aliahidi kuwa wavuvi wadogo wangepewa boti hizo kupitia mikopo yenye riba nafuu. Ahadi hiyo iliibua matumaini makubwa miongoni mwa jamii za wavuvi ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za boti chakavu na ukosefu wa mtaji wa kununua vyombo vipya. Ili kufadhili mpango huo, serikali ilishirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), ambayo hutoa mikopo nafuu kwa vikundi vya wavuvi. Mikopo hiyo ina viwango vya riba vya chini, inatoa muda mrefu kwa marejesho, na inajumuisha kipindi cha msamaha wa malipo cha takribani miaka mitano hadi kumi kabla ya kuanza kulipa. “Tunatoa tangazo linalowafikia watu nchi nzima pindi boti zinapopatikana,” alisema Mohammed Sheikh, Mkurugenzi wa Uvuvi katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi. “Vyama vya ushirika vinavyovutiwa vinatuma maombi, na vikikubaliwa, hupokea boti ambazo zinakuwa zimewekewa bima kamili na ziko tayari kwa matumizi.” Thamani ya kila boti hutegemea ukubwa wake (kwa kawaida boti yenye ukubwa wa kati ya mita 5 hadi 14, (futi 16 hadi 46), gharama yake ni takribani shilingi milioni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>10 Novemba 2025 09:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[John Cannon]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/12101218/Screenshot-2025-11-12-131027-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=769</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Hali ya Hewa, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Nishati safi, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Tabianchi, Uchafuzi, Ufadhili wa tabianchi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao pekee cha kupata nishati. Wengine wanaweza kuchangisha pesa za kutosha kwa paneli ya jua ambayo inaweza kuchajisha simu ya mkononi, kuwasha redio na kutoa mwanga kidogo kwa watoto kutwalii. Lakini kwa kawaida haitoshi kwa kazi ya msingi ya kupikia. Tofauti kubwa kati ya hali hii na ulimwengu mpana zaidi unaotumia nishati hiyo inaonekana wazi kwa walio na uwezo finyu au wasiokuwa na uwezo kabisa wa kuufikia. &#8220;Unatokea mjini &#8211; una umeme, una taa. Kwa nini wewe na sio sisi?&#8221; Mukalay Ngoyi, kiongozi kutoka kijiji cha Lukwangulo, aliiambia Mongabay. &#8220;Sisi ni wanadamu kama wewe, na tunahitaji umeme pia.&#8221; Mnamo Novemba 10, Mkutano wa 30 (COP30) wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC),utakuwa Belém, Brazili, kutathmini maendeleo ya kimataifa kuelekea kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kupunguza uzalishaji wa kaboni. Cha msingi katika kupunguza uzalishaji huo na kufikia lengo la kuweka halijoto duniani kuwa chini ya nyuzi 2° (3.6° Fahrenheit) juu ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda ni jinsi tunavyokidhi kuongezeka kwa mahitaji ya nishati, kote duniani na katika maeneo kama kijiji cha Lukwangulo. Lakini viongozi wengi wa jamii hawatakuwa Belém, badala yake wanategemea wengine kuwawakilisha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>