<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?byline=hellen-nachilongo&#038;post_type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 01 Jul 2026 12:04:20 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0</generator>
				<item>
					<title>Aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali aondolewa adhabu ya kifungo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/#respond</comments>
					<pubDate>01 Julai 2026 12:04:12 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/29121017/meno-ya-tembo-3.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1945</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Ikolojia, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Tembo, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu uliopangwa, Uhalifu wa Mazingira, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi imemuondolea adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela Elvis Kalonga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali kwa sababu ya dosari na mkanganyiko uliobainika katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Jaji Mfawidhi, Godfrey Isaya ilitoa hukumu Juni 16,2026 baada ya kusikiliza rufani iliyowasilishwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/" data-wpel-link="internal">Aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali aondolewa adhabu ya kifungo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi imemuondolea adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela Elvis Kalonga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali kwa sababu ya dosari na mkanganyiko uliobainika katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Jaji Mfawidhi, Godfrey Isaya ilitoa hukumu Juni 16,2026 baada ya kusikiliza rufani iliyowasilishwa na Kalonga dhidi ya Jamhuri akipinga kutiwa hatiani pamoja na adhabu aliyopewa Awali, Mahakama ya Wilaya ya Mlele ilimhukumu Kalonga kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa manne ya kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria, pamoja na kosa la kuingia hifadhi ya taifa bila kibali na kubeba silaha ndani ya hifadhi. Ilidaiwa kwamba Novemba 8, 2025, askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi walimkamata Kalonga katika eneo la Kasandalala ndani ya hifadhi hiyo akiwa hana kibali na akiwa na silaha mbalimbali zikiwemo panga, shoka, vipande vya nondo, goroli na unga wa baruti. Pia alidaiwa kukutwa na nyama na viungo vya wanyamapori vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya TSh17,800,000. Sehemu ya ushahidi wa Jamhuri Upande wa mashtaka ulidai kuwa mshtakiwa alikamatwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi akiwa na nyara za Serikali na vifaa vinavyohusishwa na uwindaji haramu. Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa mahakamani, Novemba 8, 2025 askari wanyamapori Joel Kabuga ambaye alikuwa shahidi wa pili (PW2), Christian Ruyemamu (PW3) na Rahimu Hamadi Yusuf (PW4) wakiwa doria eneo la Kasandalala ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi waliona moshi ukitoka porini. Mashahidi hao kwa nyakati tofauti wakidai kuwa walipofuatilia chanzo cha moshi huo walikuta watu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/#respond</comments>
					<pubDate>01 Julai 2026 10:25:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/01114338/Screenshot-2026-07-01-144315.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1958</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Uwindaji, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na Mohammed dhidi ya Jamhuri. Sulemani anakabiliwa na mashtaka matatu, shtaka la kuongoza genge la uhalifu, kushiriki biashara haramu ya nyara na kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria, akiwa pamoja na washtakiwa wengine watatu katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 10770 ya mwaka 2026 inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam. Katika maombi yake ya dhamana, Wakili wa mshtakiwa, Meschack Dede, aliiomba Mahakama Kuu izingatie kuwa makosa yanayomkabili mteja wake yanadhaminika na kwamba thamani ya mali inayodaiwa, nusu ihesabiwe kwa kugawanywa kwa washtakiwa wote wanne. Ombi la wakili lapita Upande wa Jamhuri haukupinga ombi hilo la wakili na wala haukuwasilisha kiapo cha kupinga maombi. Wakili wa Serikali Grace Kibaki aliiomba mahakama izingatie hati ya mashtaka pamoja na masharti ya Sheria ya Uhujumu Uchumi kuhusu utoaji wa dhamana. Baada ya kusikiliza maombi hayo, Jaji Kirekiano alikubali kumpatia mwombaji dhamana kwa kuzingatia masharti ya kisheria kuhusu kiwango cha fedha kinachotakiwa kuwekwa mahakamani. Alisema kifungu cha 36(5)(a) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kinamtaka mshtakiwa kuweka fedha taslimu au mali yenye thamani ya nusu ya fedha au mali inayohusika katika kosa. Jaji alitegemea maamuzi ya awali ya mahakama, ikiwemo kesi ya Arafat&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/#respond</comments>
					<pubDate>29 Juni 2026 14:08:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/29134931/Screenshot-2026-06-29-164657-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1948</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Eneo Lililolindwa Baharini, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jinsia na Uhifadhi, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Suluhisho za Asili, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, Viwango vya Bahari, na  Wanawake katika Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi ya wavuvi walikuwa tayari wamerudi mikono mitupu. Wengine walikuwa hawajarudi kabisa. Kwa Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo kipya cha Usimamizi wa Pwani wa Mida (BMU), kusubiri kwa muda mrefu kumekuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Kitengo cha Usimamizi wa Pwani (BMU) ni mfumo wa usimamizi shirikishi wa uvuvi nchini Kenya, ukiwaleta pamoja wadau katika sekta hiyo wakiwemo wavuvi, wauza samaki na wafanyabiashara. Alice Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo cha Usimamizi wa Pwani ya Mida (BMU) kilichoanzishwa hivi karibuni huko Watamu, Kenya. Picha na David Akana/Mongabay. &#8220;Kuna wakati ambapo samaki walikuwa wengi hapa,&#8221; anasema, akionyesha mkondo wa bahari uliommzunguka. &#8220;Sasa [wavuvi] wanarudi na kilo mbili au tatu tu.&#8221; Kwa Kazungu, kupungua kwa samaki kumekuwa suala la kuishi. Akiwa ameolewa na mwenye watoto, anategemea karibu kabisa kuuza samaki ili kupata mapato. Wakati hakuna samaki, mara kwa mara anauza mnazi, aina ya mvinyo wa mitende kutoka kwa minazi. Lakini hiyo haitoshi kuchukua nafasi ya riziki iliyojengwa karibu na bahari. &#8220;Ninarejea nyumbani, watoto hutaka chakula,&#8221; anasema. &#8220;Hilo ndilo linalonitia wasiwasi.&#8221; Hadithi yake inaakisi hali ilivyo katika Mkondo wa Mida, mtandao mkubwa wa mikoko, matope na mifereji ya maji ambayo ni sehemu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Sehemu sita za hifadhi baharini zatambuliwa kama Mbuga za Buluu, nne kati yake zikiwa Afrika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>26 Juni 2026 14:25:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika Vyawahare]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/26135310/Screenshot-2026-06-26-165251.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1937</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Bahari ya Pasifiki, Kenya, na  Senegal]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Eneo Lililolindwa Baharini, Kasa wa baharini, Maeneo yaliyolindwa, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, Uhifadhi wa Kaboni, Uhifadhi wa Misitu, Uvuvi, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MOMBASA, Kenya — Katika kongamano la “Our Ocean” mjini Mombasa, Kenya, ujumbe ulisisitizwa katika vikao vyote: Maeneo yaliyohifadhiwa ya baharini (MPAs) ni muhimu katika kulinda bahari. Tuzo za Blue Park, zilizoanzishwa na Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari yenye makao yake makuu nchini Marekani, zinaangazia maeneo yaliyohifadhiwa yanayokidhi viwango vinavyohitajika. Mwaka huu, sita zilitambuliwa&#60;: Eneo Lililolindwa la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Sehemu sita za hifadhi baharini zatambuliwa kama Mbuga za Buluu, nne kati yake zikiwa Afrika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MOMBASA, Kenya — Katika kongamano la “Our Ocean” mjini Mombasa, Kenya, ujumbe ulisisitizwa katika vikao vyote: Maeneo yaliyohifadhiwa ya baharini (MPAs) ni muhimu katika kulinda bahari. Tuzo za Blue Park, zilizoanzishwa na Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari yenye makao yake makuu nchini Marekani, zinaangazia maeneo yaliyohifadhiwa yanayokidhi viwango vinavyohitajika. Mwaka huu, sita zilitambuliwa&lt;: Eneo Lililolindwa la Bahari la Banc-des-Américains nchini Kanada; Eneo Lililolindwa la Rapa Nui nchini Chile; eneo la turathi ya Jamii asili ya Kawawana nchini Senegali; na Hifadhi ya Kitaifa ya Nosy Hara, Mbuga ya Kitaifa ya Sahamalaza – Îles Radama, na Hifadhi ya Kitaifa ya Nosy Tanihely (pia huandikwa Tanikely) ya Madagaska. Kongamano hilo lililofanyika mjini Mombasa kuanzia Juni 16-18 lilishuhudia zaidi ya wajumbe 6,000 kutoka serikali mbalimbali, mashirika yasiyo ya faida, sekta ya kibinafsi na taasisi nyingine wakikusanyika kuzungumzia uhifadhi wa bahari. Wanachama wa ICCA wa Kawawana nchini Senegal. Picha kwa hisani ya Chama cha Wavuvi cha Jamii ya Vijijini ya Mangagoulack. Chini ya Mfumo wa Kimataifa wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal uliopitishwa na washiriki wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Anuwai wa Kibiolojia mwaka wa 2022, mataifa yalikubaliana kulinda 30% ya ardhi, maji safi na maeneo ya baharini duniani ifikapo 2030, katika kile kinachofahamika kuwa lengo la 30 kwa 30. &#8220;Kundi hili la hifadhi za buluu ni ukumbusho wa nguvu wa kile ambacho lengo la 30 kwa 30 linahitaji,&#8221; Lance Morgan, rais wa Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari, alisema katika tangazo la tuzo huko Mombasa mnamo Juni 16. &#8220;Maeneo haya sita yaliyohifadhiwa baharini, yanayolinda mifumo mbalimbali ya ikolojia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>25 Juni 2026 23:31:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/25230559/Our-Ocean-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1930</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai wa Baharini, Dawa ya Asili, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kasa wa baharini, Maji, Maliasili, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Misitu ya Asili, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhisho za Asili, Tamaduni za Kiasili, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Baharini, Urejesho wa Asili, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira si rasilimali za kutumia tu, bali ni urithi wa kulindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo. Nchini Kenya, ukanda wa pwani wenye urefu wa takriban kilomita 640 ni kitovu cha uchumi wa buluu unaojumuisha uvuvi, utalii, usafiri wa baharini na biashara nyingine zinazotegemea bahari. Karibu watu milioni nne wanaishi katika eneo la pwani, huku maelfu ya wavuvi na makumi ya maelfu ya kaya wakitegemea rasilimali za bahari kwa riziki zao. Hali hiyo inaifanya uhifadhi wa bahari kuwa muhimu si tu kwa mazingira bali pia kwa ustawi wa uchumi wa taifa. Muranga, ambaye sasa ni mvuvi na pia mwenyekiti wa kikundi cha kijamii cha kulinda misitu cha Sokoke, ana jukumu la kuhakikisha kuwa anapitisha elimu hiyo kwa jamii, hasa kwa vizazi vichanga, ili ihifadhiwe kwa vizazi vijavyo. Mwonekano wa sehemu ya Bahari ya Hindi jijini Mombasa, huku mikoko ikionekana upande wa kushoto. Picha na Malavika Vyawahare, Mongabay. Mikoko ni misitu ya kipekee inayostawi katika maeneo ya maji ya chumvi kwenye fukwe za bahari za kanda za kitropiki. Misitu hii huunganisha nchi kavu na bahari, ikifanya kazi muhimu katika kulinda mazingira na ustawi wa jamii za pwani. “Zamani tulikuwa tukikalishwa na mababu zetu tukisimuliwa hadithi na kanuni za kijamii ambazo zilikuwa zinalinda&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka uwanjani hadi jukwaa la tabianchi: Kijana wa miaka 13 aongoza vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/23/kutoka-uwanjani-hadi-jukwaa-la-tabianchi-kijana-wa-miaka-13-aongoza-vita-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/23/kutoka-uwanjani-hadi-jukwaa-la-tabianchi-kijana-wa-miaka-13-aongoza-vita-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>23 Juni 2026 18:00:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23172254/Baraka-havin-fun-at-home.-Photo-courtesy-of-Lorein-Moruri.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1905</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Elimu ya Mazingira, Haki ya Tabianchi, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uandishi wa Habari za Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Ukataji Miti, na  Upandaji Miti]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni saa moja asubuhi. Mbwa wawili aina ya Chihuahua wanaonekana kuwa waangalifu kwa uwepo wa mgeni kwenye lango la nyumba ya familia ya Moruri Baraka. Dakika chache baadaye, Baraka anashuka ngazi akiwa ameshika kichanuo mkononi na kujiandaa kwa mahojiano. Dada yake mdogo, ambaye bado hajatimiza miaka sita, anajiunga naye na mara kwa mara hujitosa kujibu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/23/kutoka-uwanjani-hadi-jukwaa-la-tabianchi-kijana-wa-miaka-13-aongoza-vita-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kutoka uwanjani hadi jukwaa la tabianchi: Kijana wa miaka 13 aongoza vita dhidi ya mabadiliko ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni saa moja asubuhi. Mbwa wawili aina ya Chihuahua wanaonekana kuwa waangalifu kwa uwepo wa mgeni kwenye lango la nyumba ya familia ya Moruri Baraka. Dakika chache baadaye, Baraka anashuka ngazi akiwa ameshika kichanuo mkononi na kujiandaa kwa mahojiano. Dada yake mdogo, ambaye bado hajatimiza miaka sita, anajiunga naye na mara kwa mara hujitosa kujibu baadhi ya maswali. Msichana huyo ni mmoja wa mashabiki wake wa karibu. Baraka, mwenye umri wa miaka 13, ameibuka kuwa mmoja wa watetezi vijana wa mazingira wanaotikisa mawimbi nchini Kenya Baraka alianza kuwa na mapenzi na masuala ya mazingira tangu alipokuwa na umri wa miaka sita. Kufikia Machi 2026, tayari alikuwa amepanda zaidi ya miti 7,600 kwa msaada wa familia na marafiki zake. “Lengo langu halina kikomo. Nataka kupanda zaidi ya miti milioni moja kabla sijafikisha umri wa miaka 18,” anasema. Mafanikio yake makubwa yamekuwa uzinduzi wa kitabu kiitwacho Go Green With Baraka, kinachosimulia shughuli zake za kuhifadhi mazingira kwa msaada wa familia yake. Kitabu hicho kimeandikwa kwa herufi kubwa na lugha rahisi ambayo mtoto anaweza kuielewa na kuhamasika kuitikia wito uliomo ndani yake. Baraka anatumaini kuwa kitabu hicho kitaingizwa katika mtaala wa elimu wa Kenya lakini pia kitapatikana katika maduka mengi zaidi ya vitabu pamoja na majukwaa ya mtandaoni kama Amazon. Baraka anasoma kitabu kiitwacho &#8216;Go Green With Baraka&#8217; anapocheza na dadake mdogo nyumbani kwao Nairobi. Picha kwa hisani ya Lawrine Moruri. Babake Baraka Arnold Warinda (kushoto), mama Lawrine Moruri na rafikiye wakati wa uzinduzi wa kitabu cha &#8216;Go Green With Baraka&#8217; jijini Nairobi mnamo Januari&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/23/kutoka-uwanjani-hadi-jukwaa-la-tabianchi-kijana-wa-miaka-13-aongoza-vita-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/23/kutoka-uwanjani-hadi-jukwaa-la-tabianchi-kijana-wa-miaka-13-aongoza-vita-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/#respond</comments>
					<pubDate>22 Juni 2026 19:12:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23161035/KESI-YA-MENO-YA-TEMBO-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1907</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu wa Mazingira, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, Wanyama Wanaowinda, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, shauri lilifutwa, lakini muda mfupi baadaye wakasomewa mashtaka upya mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustine Rwizile, ambaye sasa hivi ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Washitakiwa walikuwa 11 Wakati kesi inaanza, washitakiwa walikuwa 11, lakini idadi hiyo ilipungua baada ya washtakiwa watano kuingia kwenye maridhiano na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ambapo walikiri makosa yao na kuachiliwa baada ya kutimiza makubaliano waliyoafikiana. Washtakiwa waliobakia katika shauri hilo ni Victor Mawanda, Mussa Abdallah, Abbas Jabu, Haruna Kasa na Halfani Kahengele. Awali ilidaiwa katika hati mashtaka kuwa kati ya Januari mwaka 2006 na Juni mwaka 2016, washtakiwa walipanga njama ya kuongoza genge la uhalifu Jijini Dar es Salaam. Walidaiwa kuuza, kupokea, kununua, kuhamisha, kusafirisha na kumiliki vipande 660 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 4,656,795,000 ambayo ni nyara za serikali. Ilidaiwa pia kuwa kati ya Aprili mosi na Juni 24 mwaka 2016, maeneo ya Mbezi Msakuzi wilayani Ubungo, washtakiwa walikutwa wakimiliki vipande hivyo vya meno ya tembo bila kuwa na kibali ama leseni kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori. Washitakiwa walikana mashitaka na wako gerezani kwa kuwa kesi yao ya uhujumu uchumi haina dhamana. Korti kusikiliza shahidi wa 10 Hadi sasa shauri hilo limeshasikilizwa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Azimio la Mombasa: Nchi 15 zajitolea kushiriki taarifa za uvuvi ili kukabiliana na uvuvi haramu </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/#respond</comments>
					<pubDate>21 Juni 2026 19:47:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23195215/Screenshot-2026-06-23-225148-768x510.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1925</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Eneo Lililolindwa Baharini, Kasa wa baharini, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Msukosuko wa chakula, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sehemu za Bioanuwai, Ufugaji Samaki, Uhifadhi wa Baharini, upatikanaji wa chakula, Uvuvi, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchi 15 kutoka mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya zilipitisha Azimio la Mombasa  Azimio la Mombasa mnamo Juni 17, mwaka 2026. Kwa pamoja, mataifa hayo yalijitolea kuendeleza uwazi katika sekta ya uvuvi duniani na kuimarisha jitihada za kukabiliana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa (IUU). Tamko hilo lilipitishwa wakati wa mkutano wa 11 wa Kongamano la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/" data-wpel-link="internal">Azimio la Mombasa: Nchi 15 zajitolea kushiriki taarifa za uvuvi ili kukabiliana na uvuvi haramu </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchi 15 kutoka mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya zilipitisha Azimio la Mombasa  Azimio la Mombasa mnamo Juni 17, mwaka 2026. Kwa pamoja, mataifa hayo yalijitolea kuendeleza uwazi katika sekta ya uvuvi duniani na kuimarisha jitihada za kukabiliana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa (IUU). Tamko hilo lilipitishwa wakati wa mkutano wa 11 wa Kongamano la Kimataifa la Bahari Yetu, lililofanyika mjini Mombasa, Kenya. Bara la Afrika ilikuwa na mataifa mengi zaidi yaliyosaini yakiwemo: Cameroon, Gambia, Ghana, Guinea, Liberia, Jamhuri ya Kongo na Somalia. &#8220;Katika nchi yangu, kuwepo kwetu kunategemea sana samaki,&#8221; alisema Emelia Arthur, Waziri wa Uvuvi na Ufugaji wa samaki wa Ghana, katika taarifa iliyopeanwa na Mongabay. &#8220;Asilimia 60 ya protini ya wanyama &lt;tunayotumia inatokana na samaki, na asilimia kumi ya wakazi wetu wanategemea mnyororo wa thamani wa uvuvi ili kujipatia riziki. Uvuvi ni suala la utamaduni na usalama wa taifa kwetu. Nina furaha kuwa Ghana ni miongoni mwa mataifa ya kwanza kutia saini Azimio la Mombasa,&#8221; aliongeza. Nchi zina matumaini kwamba kwa kufanya kazi pamoja, kuoanisha kanuni na kushiriki habari kuhusu meli zinazovua katika maeneo yao ya maji, zitakuwa na ufanisi zaidi katika vita vyao dhidi ya uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa IUU. &#8220;Wahusika wa uvuvi haramu wanaendelea kuwa wa kisasa zaidi katika mbinu zao za kukwepa sheria na kanuni za nchi moja kwa kuhamia nchi nyingine,&#8221; Cephas Asare aliiambia Mongabay kupitia kwa njia ya simu. Asare ni meneja wa kanda ya Afrika Magharibi wa Wakfu wa Haki ya Mazingira (EJF), Shirika lisilo la kiserikali (NGO) la Uingereza linayofanya kazi kupambana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/#respond</comments>
					<pubDate>21 Juni 2026 17:13:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dann Okoth]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/21164857/Screenshot-2026-06-21-194344.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1898</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Filosofia ya Uhifadhi, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mamalia, na  Mamalia Wakubwa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa Barabara Kuu ya Kasi ya Nairobi-Mombasa (Nairobi Mombasa Expressway &#8211; NME), barabara ya njia mbili itakayojengwa sambamba na Reli ya Kisasa (SGR), mpango wa Twiga Tracker Initiative uliwatia alama twiga 20 (majike 11 na madume 9) ili kufuatilia mienendo na matumizi ya maeneo ya twiga wa Maasai katika ukanda wa Nairobi-Mombasa kabla, wakati na baada ya ujenzi huo ndani ya Eneo la Uhifadhi la Tsavo. Kupitia teknolojia bunifu za ufuatiliaji, na kwa ushirikiano na mfumo wa EarthRanger, programu ya wakati halisi inayosaidia juhudi za uhifadhi wa wanyamapori, watafiti waliwafunga twiga vifaa vyepesi vya GPS vilivyounganishwa na setilaiti kwenye mikia yao ili kupata taarifa muhimu kuhusu namna wanavyohama, jinsi wanavyotumia makazi yao, na athari za shughuli za binadamu kwa mienendo yao. Mpango wa Twiga Tracker, unaotekelezwa na Giraffe Conservation Foundation (GCF), kwa sasa unafuatilia twiga tisa katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki, wanane katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi na watatu katika ranchi za Taita. Shirika la GCF lilitekeleza zoezi hili kwa ushirikiano na Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS), Tsavo Trust, Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyamapori (WRTI), Wildlife Works na Sheldrick Wildlife Trust. Kwa mujibu wa GCF, Eneo la Uhifadhi la Tsavo ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/#respond</comments>
					<pubDate>19 Juni 2026 16:08:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/19153844/Screenshot-2026-06-19-182917-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1891</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bioanuai, Bioanuai ya Misitu ya Mvua, Bustani za wanyama, Chakula, Cites, Elimu, Elimu ya Mazingira, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Huduma za Mazingira, Idadi ya watu, Ikolojia, Jamii Asili, Jamii ya Nyani Wakubwa, Jamii za Misitu ya Mvua, Kijani, Makazi, na  Mamalia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, ulio katikati mwa DRC. Dhamira yao ni kuwashawishi bonobo (Pan paniscus) kukubali uwepo wa binadamu kama sehemu ya asili ya mazingira yao. Kwa kupata uaminifu wa wanyama, watafiti wanatumai kuunda fursa za kuelewa vyema tabia, ikolojia na afya zao. Mchakato huu wenye bidii wa kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu unahusisha kutumia wakati karibu na nyani siku baada ya siku hadi watakapozoea watu hatua kwa hatua. Ni kazi ya polepole na inayohitaji juhudi kubwa ambayo inaweza kuchukua miaka, inayohitaji uvumilivu, uthabiti na maelfu ya masaa msituni. Muda mrefu kabla ya mapambazuko, mara nyingi karibu saa 3 alfajiri, wafuatiliaji, baadhi yao wakiwa wawindaji haramu wa zamani, ambao ujuzi wao kuhusu msitu umekuwa rasilimali muhimu ya uhifadhi, wanaanza kuelekea kwenye eneo la viota usiku uliopita. Ni lazima wafike kabla kundi hilo la bonobo halijaamka. Kisha huanza harakati za kutwa nzima kupitia moja ya misitu ya mvua iliyo mbali zaidi Duniani, kufuatia nyani kutoka alfajiri hadi wajenge viota vipya kwa ajili ya usiku. &#8220;Wazo zima la kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu ni kukutana nao kila siku kwa njia ya kirafiki sana, isiyo ya mwingiliano ili wakukubali kama sehemu ya msitu,&#8221; anasema Felix Bofeko, mtafiti msaidizi anayefanya kazi na programu ya mazoea ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti mpya wadokeza maeneo yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia yanaweza kuathiri ustawi wa jamii za wenyeji</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 19:09:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Solomon Yimer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18185147/Screenshot-2026-06-18-215028-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1883</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Nyani, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Tabia za Wanyama, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Tembo, Ufugaji wa Uhifadhi, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ukanda wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Ustawi wa Wanyama, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Nature unaonyesha kuwa maeneo ya hifadhi ya Ethiopia yalipunguza kasi ya ukataji miti na upanuzi wa kilimo, huku yakisaidia kudumisha nyanda za malisho. Lakini utafiti pia unapendekeza kuwa faida zile zile za uhifadhi zinaweza pia kuhusishwa na kupungua kwa usalama wa chakula na ustawi kwa jamii zilizo karibu, huku ukisisitiza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/" data-wpel-link="internal">Utafiti mpya wadokeza maeneo yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia yanaweza kuathiri ustawi wa jamii za wenyeji</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Nature unaonyesha kuwa maeneo ya hifadhi ya Ethiopia yalipunguza kasi ya ukataji miti na upanuzi wa kilimo, huku yakisaidia kudumisha nyanda za malisho. Lakini utafiti pia unapendekeza kuwa faida zile zile za uhifadhi zinaweza pia kuhusishwa na kupungua kwa usalama wa chakula na ustawi kwa jamii zilizo karibu, huku ukisisitiza baadhi ya tahadhari katika matokeo yao. Utafiti huo, uliofanywa kwa ushirikiano kati ya watafiti nchini Ethiopia na Uingereza, na Mamlaka ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya Ethiopia, ulitathmini matokeo ya kimazingira na kijamii katika maeneo 25 yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia katika kipindi cha mwaka wa 2000-2020. Walipima kiwango cha misitu, upanuzi wa kilimo, nyanda za malisho, usalama wa chakula, utofauti wa lishe na ustawi wa nyenzo. Ingawa maeneo yaliyohifadhiwa yalikuwa na ufanisi mkubwa katika kupunguza uharibifu wa mazingira licha ya shinikizo kubwa kutoka kwa ukuaji wa idadi ya watu, upanuzi wa kilimo, na mahitaji ya ardhi, watafiti waligundua mchangamano wa maslahi (trade-offs) kati ya matokeo ya mazingira na kijamii katika tathmini zao. Maeneo 12 yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo mazuri ya kimazingira kwa gharama ya ustawi wa jamii. Wakati huo huo, maeneo matano kati ya maeneo yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo ya &#8220;faida kwa wote&#8221; kwa uhifadhi wa bioanuwai na ustawi wa jamii na maeneo matatu yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo ya &#8220;hasara kwa wote&#8221;. &#8220;Ethiopia ina utajiri wa viumbe hai, lakini pia inakabiliwa na changamoto kubwa kuhusu umaskini, usalama wa chakula na mahitaji ya ardhi,&#8221; alisema Sophie Jago, mwandishi mkuu wa utafiti na msaidizi wa utafiti katika Bustani za Kifalme za Mimea za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 08:35:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18080931/Screenshot-2026-06-18-110907-768x439.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1874</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Asia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Asidi ya Bahari, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Fedha za Uhifadhi, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi kubwa za kimataifa na za serikali, watu wengi wanaofanya kazi ya kila siku ya uhifadhi wa baharini ni mashirika ya kijamii yanayofanya kazi kwa bajeti ndogo katika ukanda wa pwani wa Afrika. Mara nyingi hufanya hivyo mbali na kuangaziwa, lakini mchango wao ni muhimu kwa nia ya kimataifa ya kuhifadhi nafasi za bahari. Mkataba wa Anuwai ya Kibiolojia (CBD), ambao chini yake Mfumo wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal ulipitisha malengo ya mwaka 2030, unaonyesha kuwa mafanikio yanategemea sana ushirikishwaji wa jamii. Kote nchini Kenya, Tanzania na Namibia, vikundi vinne kama hivyo &#8211; Maendeleo ya Rasilimali za Pwani na Bahari (COMRED) Action for Ocean, Mwambao Coastal Community Network na Namibia Nature Foundation (NNF) &#8211; hutoa fursa ya kufahamu jinsi uhifadhi wa bahari unaoongozwa na jamii unavyotekelezwa kwa vitendo. Kazi yao inaweza kuwa na ufadhili wa chini, kutofautiana na wakati mwingine polepole, lakini inazidi kuwa msingi wa jinsi ulinzi wa baharini unavyowaziwa katika bara. Mifumo ya ikolojia ya baharini barani Afrika inasaidia uvuvi, utalii, uchukuzi, uhifadhi wa kaboni na ulinzi wa pwani huku ikiendeleza mamilioni ya riziki kutoka Bahari ya Hindi Magharibi hadi pwani ya Afrika ya Atlantiki na Mediterania. Katika Afrika Mashariki hasa, mikoko, miamba ya matumbawe, nyasi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/#respond</comments>
					<pubDate>17 Juni 2026 13:26:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/17130445/Screenshot-2026-06-17-160345-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1868</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara ya Kilimo, Bioanuai wa Baharini, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo-ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Mimea yenye Tiba, na  Uhifadhi wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia mbadala ya kujikimu kimaisha. Kilimo cha mwani kikawa jibu lake, akaamua kujiunga na wanakijiji wenzake wanaofanya ukulima huo. Mwani ni kundi la viumbe wa majini wanaofanana na mimea inayokua katika maji ya chumvi, hasa maeneo ya pwani yenye kina kifupi. Hupandwa kwa kufungwa kwenye vitiji na kamba baharini. Mwani huchukua kati ya siku 45 na 60 kufikia kiwango cha kuvunwa. Mwani hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile vipodozi, sabuni, dawa, virutubisho vya lishe, vinywaji na malighafi za viwandani. What is seagrass and why is it important? Kwa wakulima wengi wa mwani katika eneo la Kwale, baada ya kuvuna wao huukausha kisha kuuuza kupitia chama cha ushirika cha mwani katika eneo la Kibuyuni. Ukulima wa mwani ulishirikisha wanawake wengi katika eneo la Kibuyuni ili wapate fursa ya kupata manufaa ya bahari ambayo imekuwa tegemeo la upatikanaji wa riziki kwa familia nyingi eneo la Pwani. Hii ni kutokana na kuwepo kwa mila na tamaduni zilizomwekea vikwazo mwanamke kuingia baharini kuvua samaki. Wakulima wa Mwani wakitayarisha Kamba tayari kwa mafunzo kuhusu upandaji wa Mwani eneo la Shanga, Lamu, Kenya. Picha na Mohamed Fuad Mohamed. Lakini ukulima huo sasa umeanza kuvutia hata wanaume kama Ahmed, kutokana na faida ambazo wameziona kwa wanawake, wakiwa na matumaini ya kupata kipato cha kujiendeleza kimaisha.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/#respond</comments>
					<pubDate>16 Juni 2026 15:28:54 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/16152623/Aquatic-animal-production-from-aquaculture-topped-100-million-tonnes-for-the-first-time-in-2024-according-to-FAOs-latest-State-of-World-Fisheries-and-Aquaculture-report-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1861</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Asia, na  Bahari ya Hindi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Baharini, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kasa wa baharini, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Utafiti, Uvuvi, Viwango vya Bahari, Wanyama wa Baharini, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo pia imeeleza kuwa sekta hiyo inayohusiana na uvuvi na ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa majini iliajiri wafanyakazi zaidi ya milioni 65, na hivyo kuwa tegemeo la maisha ya watu zaidi ya milioni 600 kote duniani. FAO ilizindua ripoti hiyo mpya ya Hali ya Uvuvi na Ufugaji wa Viumbe vya Majini Duniani (SOFIA 2026) kwenye mkutano wa 11 wa Bahari Yetu [11th Our Ocean Conference] uliofanyika jijini Mombasa, nchini Kenya. Ripoti hiyo imeeleza kuwa uzalishaji wa uvuvi na ufugaji wa viumbe vya majini duniani ulifikia rekodi ya tani milioni 235 kwa mwaka 2024. Pia uzalishaji wa wanyama wa majini ulifikia tani milioni 195 na umeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 3.2 kwa mwaka tangu miaka ya 1950. Pia ripoti ya shirika hilo la Umoja wa Mataifa imeonyesha kuwa uvuvi wa asili umeendelea kuwa thabiti kwa kiasi kikubwa tangu mwishoni mwa miaka ya 1980, hali inayochangiwa na juhudi za usimamizi wa uvuvi na uhifadhi wa mazingira katika baadhi ya maeneo. Aidha, ilibainika kuwa ufugaji wa viumbe vya majini ulizalisha tani milioni 103 za wanyama wa majini, rekodi ya juu zaidi kuwahi kushuhudiwa. Hii ni sawa na asilimia 53 ya uzalishaji wote wa viumbe vya majini duniani, na zaidi ya asilimia 59&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushahidi unaowahusisha popo na Ebola bado haujakamilika, mwanasayansi asema: &#8216;Suluhisho si hofu&#8217;</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/15/ushahidi-unaowahusisha-popo-na-ebola-bado-haujakamilika-mwanasayansi-asema-suluhisho-si-hofu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/15/ushahidi-unaowahusisha-popo-na-ebola-bado-haujakamilika-mwanasayansi-asema-suluhisho-si-hofu/#respond</comments>
					<pubDate>15 Juni 2026 10:35:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/15102507/Screenshot-2026-06-15-132430-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1850</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, na  Afrika Mashariki]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Aliye hatarini, Biashara ya Kilimo, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya mbao, Biashara ya Wanyamapori, Chakula, COVID 19, na  Dhoruba]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikikabiliana na mlipuko mwingine wa Ebola, popo wamechunguzwa tena kama hifadhi inayowezekana ya virusi. Lakini kulingana na mwanaikolojia wa popo Paul Webala, hakuna ushahidi kamili wa kisayansi unaowahusisha popo na Ebola na hifadhi ya asili bado haijulikani. Mlipuko wa sasa wa Ebola unasababishwa na aina ya virusi vya Bundibugyo, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/15/ushahidi-unaowahusisha-popo-na-ebola-bado-haujakamilika-mwanasayansi-asema-suluhisho-si-hofu/" data-wpel-link="internal">Ushahidi unaowahusisha popo na Ebola bado haujakamilika, mwanasayansi asema: &#8216;Suluhisho si hofu&#8217;</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ikikabiliana na mlipuko mwingine wa Ebola, popo wamechunguzwa tena kama hifadhi inayowezekana ya virusi. Lakini kulingana na mwanaikolojia wa popo Paul Webala, hakuna ushahidi kamili wa kisayansi unaowahusisha popo na Ebola na hifadhi ya asili bado haijulikani. Mlipuko wa sasa wa Ebola unasababishwa na aina ya virusi vya Bundibugyo, aina ambayo kwa sasa hakuna chanjo au matibabu yaliyoidhinishwa, kulingana na Shirika la Afya Ulimwenguni (WHO). Katika mahojiano haya na Mongabay, Webala anajadili kwa nini popo mara nyingi hawaeleweki, anaelezea huduma muhimu za kiikolojia wanazotoa, na kueleza kwa nini uharibifu wa makazi unaweza kusababisha hatari kubwa ya magonjwa yanayotokana na wanyama kuliko popo wenyewe. Webala ni mwanabiolojia wa wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Maasai Mara nchini Kenya ambaye amesomea popo kwa zaidi ya miongo miwili. Rousettus aegyptiacus, anayejulikana kama popo wa matunda wa Misri, spishi iliyoenea inayopatikana kote barani Afrika. Picha kwa hisani ya Paul Webala. Mongabay: Watu wengi hufikiria kwa haraka kuhusu popo kila kunapokuwa na mlipuko wa Ebola. Je, popo wananyanyapaliwa visivyo na haki? Paul Webala: Popo ni kundi la pili kwa ukubwa la mamalia baada ya panya. Takriban 25% ya aina zote za mamalia ni popo. Wana majukumu muhimu sana katika mifumo ikolojia na ni sehemu muhimu ya bioanuwai. Waondoe, na mifumo yote ya ikolojia inaweza kuanza kuporomoka. Kwa bahati mbaya, popo huhusishwa na hadithi nyingi na imani potofu. Baadhi ya jamii huwahusisha na kifo, pepo wachafu au ishara mbaya. Kwa sababu ya imani hizi za muda mrefu, popo mara nyingi wanateswa.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/15/ushahidi-unaowahusisha-popo-na-ebola-bado-haujakamilika-mwanasayansi-asema-suluhisho-si-hofu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/15/ushahidi-unaowahusisha-popo-na-ebola-bado-haujakamilika-mwanasayansi-asema-suluhisho-si-hofu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 19:43:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11194040/Vijana-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1846</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Fedha, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa Umoja wa Mataifa wenye makao yake nchini Uswisi unaofadhiliwa kupitia michango ya hiari kutoka kwa nchi zilizoendelea na jumuiya ya kimataifa, zitatolewa kupitia serikali na kusambazwa kwa jamii mbalimbali nchini zinazokabiliwa na majanga mbalimbali yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi. Majanga hayo ni pamoja na ukame wa mara kwa mara, mafuriko, kupungua kwa uzalishaji wa mazao, uharibifu wa mazao na matukio mengine ya hali mbaya ya hewa. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Misitu wa Kenya, Festus Ng’eno, alisema msaada huo ni hatua muhimu sana. Ng’eno alisema hatua hiyo inaifanya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na mfuko huo. Vanuatu, taifa la funguvisiwa lenye maeneo mengi ya mwinuko wa chini, ndiyo iliyokuwa nchi ya kwanza duniani kupata ufadhili huo. Ng’eno alitoa taarifa hiyo katika mazungumzo yaliyofanyika sambamba na mazungumzo ya kiufundi ya tabianchi ya UNFCCC Subsidiary Bodies (SB64) yanayoendelea huko Bonn, Ujerumani. Katika taarifa aliyochapisha mtandaoni, akithibitisha habari iliyochapishwa na gazeti la People Daily mnamo Juni 10, Dkt Ng’eno alisema kuwa licha ya Kenya kupitia baadhi ya majanga makubwa zaidi ya tabianchi katika Afrika Mashariki, nchi hiyo haijawahi kupima kikamilifu kiwango halisi cha hasara iliyopata kutokana na majanga hayo. &#8220;Hali hiyo sasa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 13:46:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11131849/Screenshot-2026-06-11-161609.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1841</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Urusi, Zambia, na  Zimbabwe]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka jana, lakini uwezo wa akiba wa mitambo ya makaa ya mawe unaoweza kutumika wakati wa mahitaji makubwa ya umeme uliongezeka kwa 3.5%. Sehemu kubwa ya ongezeko hilo ilitokea nchini Uchina, ambapo uwezo wa ziada wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe unazidi kuchukuliwa kuwa chaguo mbadala ili kuhakikisha usalama wa nishati. Wakati Uchina iliongeza gigawati 78.1 za uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo 2025, matumizi yake halisi ya nishati ya makaa ya mawe yalipungua kwa 1.2%. Kupungua huku kulidhihirika wazi kwani kulikuja huku kukiwa na ongezeko la jumla la mahitaji ya nishati ya Uchina. Kulingana na ripoti hiyo, zaidi ya 90% ya ongezeko hilo la mahitaji ya nishati lilikidhiwa na nishati ya upepo na jua badala ya makaa ya mawe. Wakati Uchina inasalia kuwa mtumiaji mkubwa zaidi wa makaa ya mawe duniani, mahitaji yake zaidi ya nishati yanatimizwa kwa njia mbadala. India ilirekodi ongezeko la pili kwa ukubwa la uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo mwaka 2025, lakini pia ilionyesha harakati kuelekea gridi safi zaidi. Pamoja na nyongeza za rekodi za nishati ya jua na upepo, nishati jadidifu zilichangia zaidi ya nusu ya uwezo wa jumla wa nishati nchini kwa mara ya kwanza. Christine Shearer, mtafiti&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 11:57:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Manuel Fonseca]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11113159/Screenshot-2026-06-11-143059.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1834</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Misitu, Moto, Moto wa Misitu, Reptilia, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na mwonekano wa kuvutia. “Nakumbuka nilipowaona kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya wanyama, bei yao ilikuwa dola za Marekani 700 kwa kila mmoja ambazo ni sawa na zaidi ya shilingi za Tanzania milioni 1.8,” alisema Dennis Rödder, mtaalamu wa wanyama watambaao kutoka Leibniz Institute for the Analysis of Biodiversity Change nchini Ujerumani, katika mahojiano na Mongabay yaliyofanyika kwa njia ya video. “Nadhani ndani ya miaka mitatu au minne, spishi hii ilikuwa imeenea kote Ulaya. Ilikuwa ni rahisi kuinunua kutoka duka lolote la wanyama wa kufugwa.” Mijusi hawa wanaojulikana kisayansi kama (Lygodactylus williamsi) hukua hadi kufikia urefu wa sentimita 6–9 (takriban inchi 2.5–3.5). Wanapatikana tu katika maeneo mawili madogo ya misitu nchini Tanzania: Hifadhi ya Misitu ya Kimboza na Hifadhi ya Ruvu. Maeneo haya yaliyohifadhiwa yana ukubwa wa jumla ya kilomita za mraba 34 (takriban maili za mraba 13). Majike waliokomaa wana rangi ya kijani-kahawia inayofanana na majani ya miti wanayoishi, jambo linalowasaidia kujificha dhidi ya maadui. Hata hivyo, madume huwa na ngozi ya samawati ang’avu inayovutia sana. Rangi hii ni miongoni mwa rangi adimu zaidi kupatikana kiasili, na hutumika kuwavutia majike wakati wa uzazi. Mjusi mdogo wa rangi ya samawati (Lygodactylus williamsi). Picha: © Simon kupitia iNaturalist (CC&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2026 18:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/10161044/Meno-ya-tembo-2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1830</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Kupambana na ujangili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Sheria ya Mazingira, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mwasha. Akiwakilisha upande wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Florida Wenceslaus aliomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa kile alichoeleza kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika. Mshtakiwa, ambaye anaendelea kusota rumande, hakuwepo mahakamani leo kama ilivyokuwa wakati kesi hiyo ilipotajwa Mei 25, na pia hakuwa na mwakilishi. Hakimu Mwasha alikubali ombi la upande wa mashitaka na akaahirisha shauri hilo hadi Juni 23 mwaka huu, kesi itakapotajwa tena. Mshtakiwa Ra alipanda kizimbani kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa Mei mwaka huu. Shauri lilipotajwa baada ya siku 14, yaani Mei 25 mwaka huu, mshtakiwa huyo hakufikishwa mahakamani na badala yake shauri liliahirishwa bila yeye kuwepo. Kabla ya kuahirisha kesi hiyo, hakimu aliamuru hati ya kumfikisha mshtakiwa kortini itolewe ili kesi itakapotajwa Juni 9, 2026, mshtakiwa aletwe kortini. Hata hivyo leo mshtakiwa hakufikishwa kortini na hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa kwa nini mshatakiwa hakuwepo. Awali upande wa Jamhuri ulidai katika hati ya mashtaka kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali na kujihusisha na biashara hiyo bila kibali. Ilidaiwa kuwa Aprili 19, 2026 katika eneo la Hoteli ya Golden Tulip–Masaki,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 19:10:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09143738/EACOP-Main-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1826</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Mimea, Samaki, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa kutumia takwimu za ramani na makadirio ya thamani ya kiuchumi, ripoti ya Earth Insight, shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Marekani, inaonyesha kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 liko karibu na maeneo muhimu kwa maisha ya mamilioni ya watu na usalama wa maji, na pia sehemu ambazo hutumika kama njia za uhamaji wa wanyama. Kutokana na uchambuzi huo, ripoti hiyo inahitimisha kuwa ujenzi wa bomba hilo tayari umeathiri jamii na mazingira, na kwamba usafirishaji wa mafuta utaleta hatari zaidi za muda mrefu. EACOP ni mradi wa ubia kati ya  kampuni ya TotalEnergies yenye asilimia 62 ya hisa, serikali za Uganda na Tanzania kila moja ikiwa na asilimia 15, pamoja na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) yenye asilimia 8. EACOP itasafirisha mafuta yanayochimbwa kutoka vitalu viwili kwenye bonde la Ziwa Albert: Kingfisher, linalomilikiwa na CNOOC; na Tilenga, linalomilikiwa na TotalEnergies. Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) nchini Uganda. Picha kwa hisani ya Thomas Lewton. Kwa mujibu wa Earth Insight, mradi huo unakaribia kukamilika na mafuta ya kwanza yataanza kusafirishwa mapema mwaka 2026. “Linapita moja kwa moja katika maeneo ya viumbe walio hatarini kutoweka, na eneo muhimu zaidi ni la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 14:29:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Isack Dickson]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09125042/3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1810</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na Ziwa Manyara, na unaokatiza maeneo ya Babati, Monduli na Simanjiro, umeendelea kuwa kiunganishi muhimu cha mifumo ya ikolojia katika ukanda huo wenye utajiri mkubwa wa viumbe hai. Kwa miongo kadhaa umekuwa njia muhimu ya kupita kwa wanyamapori wanaohama kutoka eneo moja kwenda lingine. Wanyama aina ya pundamilia wakiwa katika ushoroba wa Kwakuchinja. Picha na Isack Dickson. Revocatus Meney, mtafiti kutoka TAWIRI, anasema ushoroba huo umekuwa ukipungua siku hadi siku kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu. Makazi, kilimo na mifugo vinaendelea kuubana mwaka hadi mwaka na kuufanya uwe finyu. Kwa mujibu wa tafiti za TAWIRI, miaka ya 1970, ushoroba wa Kwakuchinja ulikuwa na ukubwa unaofikia kilomita za mraba 600. Hata hivyo, Meney anasema kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu ikiwemo makazi, kilimo na matumizi mengine ya ardhi, eneo hilo limeendelea kupungua na kufikia takribani kilomita za mraba 274.45 kwa sasa. Kupungua huku kunamaanisha kuwa zaidi ya nusu ya eneo la awali la ushoroba limepotea ndani ya kipindi cha takribani miongo mitano. Meney anasema hakuna kiwango kimoja cha upana kinachotumika kwa ushoroba kwa sababu hutegemea aina ya wanyama wanaoutumia na mazingira husika. Hata hivyo, anasema kadri ushoroba unavyokuwa mpana na usio na vikwazo vya shughuli&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 13:12:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09111629/Screenshot-2026-06-09-141545.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia ya wenzao. Hata hivyo, licha ya jukumu lao kuu katika kulinda bayoanuwai na baadhi ya misitu muhimu zaidi ulimwenguni, wengi wanaendelea kufanya kazi wakiwa na usaidizi mdogo, mishahara midogo, na hali hatarishi sana. Kwa Emmanuel Bahati Lukoo, ukweli huu ni wa kibinafsi sana. Aliwahi kuwa mlinzi katika mbuga ya kitaifa ya Virunga ambapo kwa sasa ni afisa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Kahuzi-Biega, alinusurika kifo katika shambulizi la kushutukizia mnamo mwaka wa 2018 na kikundi cha wanamgambo wa jamii kinachojulikana kama Mai-Mai. Wenzake kadhaa waliuawa kwa kuviziwa. Alipigwa risasi, alijeruhiwa na kupata kiwewe cha kisaikolojia, na baadaye kufunguliwa mashitaka mbele ya mahakama ya kijeshi katika kesi iliyohusishwa na ulinzi wa hifadhi, angeweza kuondoka. Badala yake, Bahati alichagua kusimulia hadithi yake katika kitabu kiitwacho Conservation at the Cost of My Youth: The Survival of a Ranger, simulizi ghafi ya dhabihu, hofu, shinikizo za kisiasa, na mara nyingi hali halisi isiyoonekana inayowakabili walinzi wa misitu mashariki mwa DRC. Kwenye mahojiano ya ana kwa ana na Mongabay, Bahati anatafakari safari yake, shambulizi lililokaribia kumuua, kiwewe walichopata walinzi, migogoro kati ya uhifadhi na maisha ya jamii ya eneo hilo, na uingiliaji wa kisiasa unaotatiza ulinzi wa maeneo yaliyohifadhiwa. Zaidi ya hadithi ya kibinafsi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yatishia ikolojia ya bahari Zanzibar &#8211; Serikali</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 11:55:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09103711/ZANZIBAR-ECOLOGY.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1795</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Huduma za Mazingira, Ikolojia, Irejeshaji wa Mfumo wa Ikolojia, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Licha ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhifadhi ikolojia ya bahari kupitia usimamizi endelevu wa rasilimali zake, mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuwa tishio kubwa kwa mazingira hayo na ustawi wa jamii zinazoyategemea. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, amesema athari za mabadiliko ya tabianchi zinahatarisha mafanikio ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yatishia ikolojia ya bahari Zanzibar &#8211; Serikali</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Licha ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhifadhi ikolojia ya bahari kupitia usimamizi endelevu wa rasilimali zake, mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuwa tishio kubwa kwa mazingira hayo na ustawi wa jamii zinazoyategemea. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, amesema athari za mabadiliko ya tabianchi zinahatarisha mafanikio ya uchumi wa buluu kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari, kupauka kwa miamba ya matumbawe, dhoruba kali pamoja na kupungua kwa samaki baharini. Kulinda ikolojia ya Zanzibar ni hatua muhimu katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kujenga uchumi wa buluu wenye tija. Picha kutoka mtandaoni. Aliyasema hayo katika Warsha ya 29 ya Mwaka ya Utafiti iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti na Kupunguza Umasikini [REPOA], iliyowaweka pamoja serikali za Tanzania bara na Zanzibar pamoja na wadau wa bahari kujadili namna ya kuimarisha ikolojia hiyo. Abdulla alisema Zanzibar imekuwa kivutio kikubwa cha utalii duniani kutokana na utajiri wa ikolojia yake ya bahari, utamaduni wa watu wake na mazingira ya amani na utulivu lakini ongezeko la joto duniani linaendelea kuathiri mifumo ya bahari inayochangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa Zanzibar kupitia utalii, uvuvi na shughuli nyingine za kiuchumi zinazotegemea bahari. Nini kifanyike Makamu wa Pili wa Rais alishauri kujengwa kwa miundombinu himilivu  na mifumo madhubuti ya tahadhari ya mapema ili kulinda ikolojia ya bahari na maisha ya wananchi. Alishauri kuwepo ushirikiano kati ya taasisi za mafunzo ya uvuvi na bahari pamoja na vyuo vikuu katika kuendeleza uchumi wa buluu kwa muda mrefu, sambamba na kuingiza elimu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 20:21:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05201200/Screenshot-2026-06-05-231142-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1791</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Nishati, Siasa za Nishati, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana kama “Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk” pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa sakafu ya bahari (deep-sea mining) pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Ripoti hiyo ilitolewa Juni 4, 2026 na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani inayoadhimishwa Juni 8. Ripoti iliandaliwa kutokana na utafiti uliohusisha nchi 11 kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Katika utafiti huo, Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Nchi nyingine zilizotajwa ni Kenya, Australia, Cameroon, Indonesia, Jamaica, Norway, Trinidad na Tobago, Argentina na Mexico. Kwa Tanzania, mradi huo unapangwa kujengwa katika eneo la Likong’o, kusini mwa mkoa wa Lindi. Lengo ni kuchakata gesi asilia inayopatikana baharini na kuibadilisha kuwa gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Ripoti hiyo imetolewa siku chache baada ya Waziri wa Nishati, Dkt Deogratius Ndejembi, kuliambia Bunge kwamba makubaliano ya kibiashara na kodi kati ya serikali na wawekezaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 15:09:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hellen Nachilongo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05125337/Baadhi-ya-wavuvi-katika-eneo-la-Kigambani-wakipakia-chakula-yakiwemo-mafuta-ya-kula-na-mahindi-tayari-kwenda-Mafia-kuvua-samaki.-Picha-na-Hellen-Nachilongo.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1784</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maudhui ya mazingira yanayoonyesha mabadiliko chanya, Mazingira, Maziwa, Sera za Mazingira, na  Sheria ya Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio endelevu pamoja na uharibifu wa mifumo ya ikolojia ya pwani. Hali ikoje? Remy Lema, Meneja wa Kiufundi wa mradi wa ‘Pamoja Tuhifadhi Bahari Yetu’ kutoka International Union for Conservation of Nature (IUCN), anasema sehemu kubwa ya uchafuzi wa bahari inatokana na taka ngumu. Anasema kuwa kwa sasa zaidi ya asilimia 80 ya uchafuzi unaopatikana baharini unatokana na taka ngumu, huku asilimia 10 hadi 12 ikihusishwa na vimiminika mbalimbali, yakiwemo mafuta, kemikali na taka nyingine za majimaji zinazomwagika kwenye mazingira ya bahari. “Bila hatua za haraka za kulinda bahari, Tanzania inaweza kupoteza moja ya rasilimali zake muhimu zaidi za kiikolojia na kiuchumi katika miaka ijayo,” anasema Lema. Uchafuzi wa bahari umegeuka kilio kwa wavuvi. Salum Khamis, anayefanyia kazi zake za uvuvi katika maeneo ya Kunduchi amelalamikia kuongezeka kwa uchafuzi wa bahari, akisema hali hiyo imeanza kuathiri shughuli zao za kila siku na kupunguza kipato kinachotegemea uvuvi. “Kwa sasa plastiki nyingi zinaelea baharini na nyingine huzama. Samaki wanakufa au kuhama maeneo haya…hii inaathiri sana kiasi cha samaki kinachopatikana,” anasema. Mvuvi mwingine kutoka eneo la Feri, Juma Said, anasema mara nyingi nyavu zao hunasa takataka badala ya samaki, jambo linalowaongezea gharama za matengenezo ya vifaa. “Zamani tulikuwa tukipata&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>04 Juni 2026 12:55:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/04131449/Screenshot-2026-06-04-161427.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1773</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Gesi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na kibayolojia. Ripoti hiyo iliyopewa jina la Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk ilitolewa leo, siku chache kabla ya mkutano wa 11 unaohusu masuala ya bahari, mkutano wa ‘Our Ocean Conference’ unaotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 16 hadi 18 mjini Mombasa, Kenya. Ripoti hiyo inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa kina cha bahari pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Bonde la Lamu limetajwa kuwa eneo linalopewa kipaumbele, ambapo miradi minane ya mafuta inayotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu, imepangwa kutekelezwa katika ukanda huo wa pwani wenye historia na utajiri mkubwa wa kiikolojia. “Uchambuzi wetu unaonesha kuwa asilimia 100 ya Miamba ya matumbawe na misitu ya mikoko katika eneo hili imefunikwa na vitalu vya mafuta na gesi. Kwa asilimia 100, maeneo haya ni ya hifadhi za baharini na pwani lakini pia ni muhimu kwa bayoanuwai,” ripoti hiyo imeeleza. Katika ripoti hiyo, Kenya imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Ripoti hiyo ilitolewa na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 15:48:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Benjamin Jumbe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03150618/Screenshot-2026-06-03-180555-768x498.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1759</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi ya jamii inayolenga kupunguza uharibifu wa misitu na kuongeza ufahamu wa masuala ya mazingira, pamoja na timu ya maskauti wa jamii 18 katika upande wa Kenya wa mlima, sehemu ya Mradi wa Tembo wa Mlima Elgon unaotekelezwa na Shirika la Wanyamapori la Afrika Mashariki. Mwenyekiti wa wakfu wa MEF, Chris Powles, aliiambia Mongabay kwamba mnamo mwaka 2022, maskauti walifuatilia tembo wanne wakivuka mto Suam, ambao unaashiria mpaka kati ya nchi hizo mbili. Picha za video zilizorekodiwa kwa ndege isiyo na rubani zikionyesha tembo upande wa Uganda wa Mlima Elgon. Picha kwa hisani ya UWA. Katika mahojiano kupitia barua pepe, Powles alisema sababu kadhaa zinaweza kuelezea kurudi kwa tembo, ingawa haiwezekani kusema kwa uhakika ni nini kiliwachochea kurejea katika eneo hilo. &#8220;[Hizi] ni pamoja na ongezeko la idadi ya tembo upande wa Kenya, kuongezeka kwa shinikizo la binadamu kwa upande wa Kenya, usalama wanaoupata wakiwa upande wa Uganda, ambako eneo hilo lote liko ndani ya mbuga ya taifa, tofauti na upande wa Kenya,&#8221; aliandika. &#8220;Na, labda, tembo walio hai tangu wakati wengine wao waliuawa nchini Uganda sasa wamekufa kawaida na hivyo huenda kumbukumbu ya hatari zilizowakabili nchini Uganda imefifia kadri vizazi vilivyobadilika.&#8221; Mwishoni mwa miaka ya 1970 na mwanzoni mwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 12:56:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Penzi Nyamungumi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03130042/Screenshot-2026-06-03-160011.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1754</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Mazingira, Plastiki, Sheria ya Mazingira, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa kwenye mifereji zimekuwa zikiziba njia za maji na kuchangia mafuriko. Aidha, chupa zinapochomwa, moshi wake husababisha maradhi na pia kuathiri mazingira kutokana na asili yake ya kuchelewa kuoza. Hata hivyo, kuibuka na kukua kwa biashara ya chupa za plastiki zilizotumika, ambayo mara nyingi hufanywa na akinamama na vijana, kunaendelea kubadilisha historia. Hivi sasa badala ya kushuhudia barabara zenye mifereji iliyojaa chupa tupu, kinachoonekana ni akinamama na vijana waliobeba viroba vikubwa vyenye chupa hizo. Wakusanyaji wadogo huuza chupa hizo kwa wakusanyaji wakubwa au kwa kampuni zinazojishughulisha na ukusanyaji na urejelezaji wa chupa hizo baada ya matumizi. Taimuru Hamad, Meneja Uzingatiaji Sheria kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), anakiri kwamba biashara hiyo imeleta faida kubwa katika ustawi na ulinzi wa mazingira. Chupa za plastiki zilizokusanywa kutoka maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam zikiwa zimefungwa kwenye mifuko mikubwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wanunuzi. Picha na Joyce Bazira. “Kuokotwa kwa hizi chupa kunasaidia sana. Kwanza, kunasaidia katika suala zima la ustawi wa mazingira, lakini pia kwenye suala la usafi. Kama zingekuwa haziokotwi, mazingira yangeendelea kuathirika sana na pia yangekuwa machafu sana,” alisema Taimuru katika mahojiano na Mongabay. Chupa za rangi Pamoja na kazi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 10:41:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Naina Rao]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03103608/Screenshot-2026-06-03-132733-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1749</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Amerika ya Kaskazini, Marekani, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Halijoto, Kudhibiti Ongezeko la Joto Duniani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila nusu ya kila mchezo &#8220;ili kuhakikisha hali bora zaidi kwa wachezaji&#8221;. Hata hivyo, uchambuzi wa hivi majuzi unasema Kombe la Dunia la 2026, lililoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Meksiko na Kanada, litakuwa na joto kali zaidi kuliko mashindano ya Marekani ya &#8217;94. Wanasayansi kutoka World Weather Attribution (WWA), mtandao wa kimataifa wa watafiti wanaochunguza mchango wa mabadiliko ya tabianchi katika matukio ya hali mbaya ya hewa, wanaonya kuwa mabadiliko ya tabianchi yameongeza karibu mara mbili uwezekano wa joto kali tangu wakati huo. Hiyo inafanya iwe vigumu zaidi kuondoa joto mwilini, alisema Chris Mullington, mshauri wa kutia ganzi na mhadhiri mkuu wa kliniki katika Imperial College London. &#8220;Hiyo ni muhimu kwa sababu wanasoka huzalisha kiasi kikubwa cha joto mwilini wanapokimbia mara kwa mara, kuongeza kasi na kucheza kwa kiwango cha juu cha ushindani,&#8221; alisema katika mkutano na waandishi wa habari. &#8220;WBGT inapoongezeka, mifumo ya kawaida ya kupoeza ya mwili inakuwa dhaifu.&#8221; WBGT ni kipimo cha joto kinachojumuisha halijoto ya hewa, unyevunyevu, mionzi ya jua na kasi ya upepo, na hutoa &#8220;hisia halisi&#8221; ya joto kwenye mwili wa mwanadamu. Mullington alisema viwango vya juu vya WBGT vinaweza kulazimisha wachezaji &#8220;kupunguza kasi ya kukimbia mara kwa mara, kujiendesha kwa uangalifu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, akili bandia inaweza kubadilisha miradi ya kaboni barani Afrika? </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>02 Juni 2026 09:54:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/02094948/Screenshot-2026-06-02-124936-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1742</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kaboni, Fedha za Kaboni, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kaboni, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Mikopo ya Kaboni, Siasa za Mazingira, Soko ya Kaboni, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Naito Leshao alionyesha hisia za kuchoshwa na miradi ya biashara ya fidia ya hewa ukaa katika mkutano wa kimataifa uitwao Global Landscapes Forum (GLF) wa mwaka 2026 uliofanyika Nairobi, Kenya. Akiwa na hisia kali, Leshao aliuliza maswali kadhaa: kwa nini miradi mikubwa ya kaboni inayodaiwa kuwa kwa ajili ya watu waliolinda ardhi kwa miaka mingi hupitia mikononi mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Je, akili bandia inaweza kubadilisha miradi ya kaboni barani Afrika? </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Naito Leshao alionyesha hisia za kuchoshwa na miradi ya biashara ya fidia ya hewa ukaa katika mkutano wa kimataifa uitwao Global Landscapes Forum (GLF) wa mwaka 2026 uliofanyika Nairobi, Kenya. Akiwa na hisia kali, Leshao aliuliza maswali kadhaa: kwa nini miradi mikubwa ya kaboni inayodaiwa kuwa kwa ajili ya watu waliolinda ardhi kwa miaka mingi hupitia mikononi mwa watu wengi kiasi kwamba malipo yanapowafikia wanajamii, wanapata kiasi kidogo sana? Leshao, aliyekuwa akiwakilisha jamii yake kutoka Maasai Mara, aliendelea kwa swali jingine: Je, mnatarajia jamii za kiasili ziendelee kuhifadhi ardhi huku zikilinda mifumo yao ya malisho, wakati matatizo yao hayasikilizwi kuhusu namna mabadiliko ya tabianchi yanavyowaathiri? Maswali tata Maswali yake si mapya katika mijadala ya uhifadhi wa mazingira. Yameendelea kujitokeza tangu Mkataba wa Paris ulipoweka msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika biashara ya kaboni kupitia Kifungu cha 6 kama njia ya kupambana na ongezeko la joto duniani huku ukiwa na lengo la kupambana na ongezeko la joto duniani na kuzalisha mapato. Hata hivyo, vigezo vya mfumo huo mara nyingi vimekuwa vikionekana kuwa vya upendeleo, vikiegemea zaidi kwa waendelezaji wa miradi katika mnyororo wa biashara ya kaboni. “Wanakuja na asilimia fulani, lakini nani anaamua hizo asilimia? Nani anasema kwamba jamii hii inapaswa kupata asilimia 10 au 15? Unajuaje kwamba hicho ndicho kiasi kinachokidhi uendeshaji wa jamii hii? Pamoja na kukosekana kwa usawa katika mchakato huu, bado dunia inazihitaji jamii za kiasili kuhifadhi mazingira,” alisema Leshao. Hakukuwa na majibu ya haraka kwa maswali yake, licha ya makadirio mapya kuonyesha kwamba mapato yanayotokana na soko la kimataifa la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2026 21:58:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/31214131/Atuwa-akiwa-amezamia-bahari-kwenye-kazi-ya-kurekebisha-matumbawe-kwenye-bahari-ya-kisiwa-cha-Mnemba-Zanzibar.jpeg-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1733</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Barafu ya bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Upaukaji wa Matumbawe, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa bluu, njano na kijani hupita juu ya kichwa chake huku mwanga wa jua ukionekana kwa mbali ndani ya maji. Juu ya uso wa bahari, watalii huwa wanazunguka katika maji bila kufahamu kuhusu mfumo dhaifu wa ikolojia unaopambana kuendelea kuishi chini yake. Kwa mujibu wa waajiri wake, Atuwa, mwenye umri wa miaka 23, anaelezwa kuwa mwanamke pekee Zanzibar anayeshiriki kazi hiyo ya uzamiaji wa urejeshaji wa matumbawe. Mamlaka za Zanzibar zinaeleza kuwa miaka mitatu iliyopita, eneo la Mnemba ambako Atuwa hufanya kazi, ambalo lina baadhi ya miamba muhimu ya matumbawe ya Zanzibar, liliharibika. Makame Omar Makame, Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi Baharini Zanzibar, anasema eneo hilo la Mnemba liliathiriwa na shughuli za kibinadamu zilizokithiri. “Kulikuwa na shughuli nyingi za uvuvi zisizofuata utaratibu, msongamano wa watalii, ambapo takribani boti 200 zenye watalii zilikuwa zikiingia katika eneo la mita 200 za ukanda wa pwani kila siku,” Makame aliieleza Mongabay. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, ili kulinda mazingira, Serikali ya Zanzibar iliamua kupunguza idadi ya wageni hadi 80 kwa siku na kuongeza ada ya uhifadhi kutoka $3 hadi $25 kwa mtalii mmoja, kusitisha kwa muda shughuli za uvuvi na pia kutoa elimu kwa jamii. Hilo lilikuwa jambo muhimu kwa Atuwa na wenzake ambao wanaamini jamii zao zilihitaji mazingira&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>