Nchi 15 kutoka mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya zilipitisha Azimio la Mombasa Azimio la Mombasa mnamo Juni 17, mwaka 2026. Kwa pamoja, mataifa hayo yalijitolea kuendeleza uwazi katika sekta ya uvuvi duniani na kuimarisha jitihada za kukabiliana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa (IUU).
Tamko hilo lilipitishwa wakati wa mkutano wa 11 wa Kongamano la Kimataifa la Bahari Yetu, lililofanyika mjini Mombasa, Kenya. Bara la Afrika ilikuwa na mataifa mengi zaidi yaliyosaini yakiwemo: Cameroon, Gambia, Ghana, Guinea, Liberia, Jamhuri ya Kongo na Somalia.
“Katika nchi yangu, kuwepo kwetu kunategemea sana samaki,” alisema Emelia Arthur, Waziri wa Uvuvi na Ufugaji wa samaki wa Ghana, katika taarifa iliyopeanwa na Mongabay. “Asilimia 60 ya protini ya wanyama <tunayotumia inatokana na samaki, na asilimia kumi ya wakazi wetu wanategemea mnyororo wa thamani wa uvuvi ili kujipatia riziki. Uvuvi ni suala la utamaduni na usalama wa taifa kwetu. Nina furaha kuwa Ghana ni miongoni mwa mataifa ya kwanza kutia saini Azimio la Mombasa,” aliongeza.
Nchi zina matumaini kwamba kwa kufanya kazi pamoja, kuoanisha kanuni na kushiriki habari kuhusu meli zinazovua katika maeneo yao ya maji, zitakuwa na ufanisi zaidi katika vita vyao dhidi ya uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa IUU.
“Wahusika wa uvuvi haramu wanaendelea kuwa wa kisasa zaidi katika mbinu zao za kukwepa sheria na kanuni za nchi moja kwa kuhamia nchi nyingine,” Cephas Asare aliiambia Mongabay kupitia kwa njia ya simu.
Asare ni meneja wa kanda ya Afrika Magharibi wa Wakfu wa Haki ya Mazingira (EJF), Shirika lisilo la kiserikali (NGO) la Uingereza linayofanya kazi kupambana na uvuvi haramu. “Hii inahitaji kukomeshwa. Ndiyo maana tunahitaji kushughulikia suala hilo kwa pamoja, kuwa wazi zaidi, kuimarisha ufuatiliaji na hatimaye kuukomesha uvuvi haramu haramu,” Asare alisema.
Miongoni mwa hatua zilizopendekezwa na tamko la azimio hilo, nchi zilizotia saini zimejitolea kupitisha Mkataba wa Kimataifa wa Uwazi wa Uvuvi. Mkataba unatoa wito wa uchapishaji wa leseni za uvuvi, uidhinishaji, mikataba ya ufikiaji na mgao wa kiasi cha uvuvi. Pia unahimiza nchi kuhakikisha kuwa meli zote za uvuvi wa kibiashara zina vitambulisho vya kipekee vya meli (UVIs) na kutekeleza hatua kwa hatua za leseni za UVI kwa meli ndogo ndogo.
Wakati wa mkutano na wanahabari mjini Mombasa, nchi zilizotia saini zilitoa wito kwa wawakilishi kutoka mataifa mengine ya pwani pia kupitisha tamko la azimio hilo.
Asare aliiambia Mongabay kuwa uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa unagharimu nchi za Afrika Magharibi mamilioni ya dola kila mwaka, unatishia hifadhi ya samaki na kudhohofisha usalama wa chakula kwa mamilioni ya watu.
Picha ya bango: Sehemu ya mitumbwi baada ya kuvua samaki huko Marshall, Liberia. Picha na Edward Blamo wa Mongabay.