<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?byline=dann-okoth&#038;post_type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 06 Aug 2026 18:12:10 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Sensa: Idadi ya tembo Tanzania bado ni chini ya nusu ya ilivyokuwa miaka 20 iliyopita</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/#respond</comments>
					<pubDate>06 Agosti 2026 18:04:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/06180552/Screenshot-2026-08-06-175346-768x497.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2393</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Matumizi ya Wanyamapori, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Idadi ya tembo nchini Tanzania sasa ni takriban asilimia 49.6 ya waliokuwepo mwaka 2005/2006, wakati idadi yao ilikuwa 134,588. Takwimu hizo zimetolewa na Ripoti ya Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025. Zoezi hili lilifanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kubaini idadi, mtawanyiko, mwenendo na hali ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/" data-wpel-link="internal">Sensa: Idadi ya tembo Tanzania bado ni chini ya nusu ya ilivyokuwa miaka 20 iliyopita</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Idadi ya tembo nchini Tanzania sasa ni takriban asilimia 49.6 ya waliokuwepo mwaka 2005/2006, wakati idadi yao ilikuwa 134,588. Takwimu hizo zimetolewa na Ripoti ya Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025. Zoezi hili lilifanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kubaini idadi, mtawanyiko, mwenendo na hali ya ustawi wa wanyamapori nchini. Ripoti ya sensa hiyo iliyofanyika kuanzia Septemba 2024 hadi Oktoba 2025 ilikabidhiwa kwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika hafla iliyofanyika katika Ikulu jijini Dar es Salaam. Matokeo ya sensa hiyo yalitangazwa jijini Arusha na Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Dkt Eblate Mjingo, katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa uhifadhi. Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Ashatu Kijaji, aliyemwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, idadi ya tembo iliyopatikana mwaka 2024/2025, ambayo ni 66,714, ni asilimia 49.6 ya tembo 134,588 waliokuwepo mwaka 2005/2006. Uwepo wa mifugo kwa wingi, sambamba na makazi ya binadamu yaliyoambatana na shughuli za kilimo pembezoni/ndani ya maeneo hifadhi, ni miongoni mwa sababu zinaathiri ustawi wa wanyama. Picha kwa hisani ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Mkurugenzi wa Utafiti wa TAWIRI Julius Keyyu alisema kuwa idadi ya tembo nchini ilishuka kutoka takriban tembo 134,000 waliokuwepo mwaka 2005/2006 hadi 46,408 mwaka 2014 kutokana na kuenea kwa ujangili unaolenga pembe za ndovu. Hata hivyo, alisema kuwa hatua mahsusi zilizochukuliwa na serikali, ikiwa ni pamoja na kupambana na ujangili na kuimarisha usimamizi wa hifadhi, zilisaidia idadi ya tembo kuanza kuongezeka tena. Aidha, Keyyu alibainisha kuwa ingawa idadi ya tembo imeongezeka,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Shinikizo laongezeka kwa Kenya kuchunguza vifo vya tembo 15 Amboseli, ikiwemo uchimbaji dhahabu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 21:03:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05202638/1An-elephant-relocation-exercise-in-one-of-the-National-Parks-in-Kenya-in-2025.-Photo-courtesy-of-KWS-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2370</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Utalii, Utalii wa Mazingira, Utawala, Uthibitisho, Uwazi, Uzuri wa Kiikolojia, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyamapori, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAJIADO, Kenya &#8211; Shinikizo linaendelea kuongezeka dhidi ya Serikali ya Kenya ikitakiwa kufanya uchunguzi wa kina na huru kuhusu vifo vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli. Hii ni siku chache tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Kenya Wildlife Service (KWS) Erustus Kanga kuthibitisha kwamba wanyama hao walikufa baada ya kumeza sumu ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Shinikizo laongezeka kwa Kenya kuchunguza vifo vya tembo 15 Amboseli, ikiwemo uchimbaji dhahabu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAJIADO, Kenya &#8211; Shinikizo linaendelea kuongezeka dhidi ya Serikali ya Kenya ikitakiwa kufanya uchunguzi wa kina na huru kuhusu vifo vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli. Hii ni siku chache tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Kenya Wildlife Service (KWS) Erustus Kanga kuthibitisha kwamba wanyama hao walikufa baada ya kumeza sumu ya sianidi. KWS ilithibitisha kwamba sianidi ndiyo iliyosababisha vifo hivyo, na ilisema labda tembo walipata sumu hiyo kupitia maji yaliyochafuliwa na dawa ya kuua wadudu iliyonyunyiziwa kwenye mashamba ya nyanya katika eneo la Kimana. Hata hivyo, shirika hilo bado halijabainisha kama vifo hivyo vilikuwa vya bahati mbaya au vilifanywa kwa makusudi. KWS iliiambia Mongabay kwamba uchunguzi unaendelea ili kuthibitisha matokeo ya maabara mbalimbali zinazoshiriki katika kuchunguza vifo hivyo vilivyotokea kati ya 24 Juni na 24 Julai 2026. &#8220;Maabara mbalimbali zimebadilishana sampuli ili kila moja ithibitishe matokeo ambayo tayari yanasubiriwa na umma. Maabara zinahitaji angalau siku 14 kukamilisha zoezi hili,&#8221; Mkurugenzi wa Mawasiliano wa KWS Duncan Wanyama aliiambia Mongabay kwa simu. Maabara zinazohusika ni pamoja na Maabara ya Mkemia wa Serikali na ya Chuo Kikuu cha Nairobi. Matokeo kutangazwa KWS ilisema itatangaza matokeo yoyote muhimu ya uchunguzi kutoka eneo la tukio na  vipimo vya maabara. &#8220;Wachunguzi watahakikisha wanapata kiini cha suala hili. Sampuli zinazobadilishwa ni pamoja na damu, ini na baadhi ya vimiminika vingine vya mwili vilivyokusanywa kutoka kwenye mizoga hiyo. Jana, maabara moja iliomba sampuli za damu zaidi. Kila maabara ilikuwa imechukua vielelezo tofauti vya sampuli, na sasa zinahitaji kupima zile ambazo hazikuchukuliwa awali,&#8221; Wanyama aliiambia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 17:00:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122556/nyumbu2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2358</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Sheria, Uchumi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Serengeti iliyokuwa imemhukumu Marwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa hayo baada ya kukubali rufaa yake na hoja za Jamhuri za kuunga mkono rufani hiyo huku wakibainisha kuwa hawakuweza kuthibisha mashtaka bila kuacha shaka. Mahakama ya Wilaya Serengeti Mahakama ya Wilaya ilimtia hatiani kwa makosa matatu ambayo ni; kuingia hifadhini bila kibali, kumiliki panga ndani ya hifadhi bila kibali pamoja na kumiliki sehemu ya mguu wa nyumbu ambao haukuwa umechunwa ikiwa ni nyara ya Serikali yenye thamani ya Sh 1,586,000 (Dola za Marekani 603). Wanyama aina ya nyumbu wakirejea katika makazi yao ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakitokea katika nchi ya jirani ya Kenya, hususan kwenye mbuya ya Masai Mara. Picha kwa hisasi Blogu ya Michuzi. Upande wa mashtaka ulidai mahakamani kuwa Desemba 7, 2025, askari wa hifadhi walimkamata mshtakiwa katika eneo la Korongo la Nyamburi ndani ya Hifadhi ya Serengeti akiwa na panga na sehemu hiyo ya nyumbu. Utetezi Mahakamani Alipojitetea, Marwa Nyamhanga alidai kuwa Desemba 6, 2025 alikuwa akitoka kwenye sherehe ya harusi akiwa amelewa, ndipo askari wa hifadhi walipomkamata akiwa njiani. Alidai kuwa askari hao walimshikilia katika kituo chao usiku kucha na asubuhi yake walimbambia panga pamoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbuzi mwitu maarufu wa Ethiopia warejea kwenye hatari kubwa ya kutoweka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 12:30:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Shreya Dasgupta]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122610/Screenshot-2026-08-05-152416-768x496.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2357</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Bustani za wanyama, Ikolojia, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Matumizi ya Wanyamapori, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Spishi Zilizo Hatarini Sana, Ujangili, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mbuzi mwitu wa Walia, spishi adimu ya mbuzi anayepatikana kaskazini mwa Ethiopia pekee, kwa mara nyingine ametambuliwa kama mnyama aliye katika hatari kubwa ya kutoweka(Critically Endangered) baada ya tathmini za hivi karibuni kuonyesha idadi yake imeendelea kupungua na kushuka chini ya kiwango muhimu kinachotumiwa na wataalamu wa uhifadhi. Mnyama huyo maarufu hupatikana zaidi kwenye miamba mirefu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Mbuzi mwitu maarufu wa Ethiopia warejea kwenye hatari kubwa ya kutoweka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mbuzi mwitu wa Walia, spishi adimu ya mbuzi anayepatikana kaskazini mwa Ethiopia pekee, kwa mara nyingine ametambuliwa kama mnyama aliye katika hatari kubwa ya kutoweka(Critically Endangered) baada ya tathmini za hivi karibuni kuonyesha idadi yake imeendelea kupungua na kushuka chini ya kiwango muhimu kinachotumiwa na wataalamu wa uhifadhi. Mnyama huyo maarufu hupatikana zaidi kwenye miamba mirefu na maeneo magumu kufikika ya Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Simien. Awali alikuwa ameorodheshwa katika kundi la wanyama walio hatarini (Vulnerable) kwenye Orodha Nyekundu ya Muungano wa Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN). Hali ya uhifadhi wa Walia ibex (Capra walie) imekuwa ikibadilika kwa miaka. Mwaka 1986, iliorodheshwa kuwa katika hatari ya kutoweka (Endangered), kisha ikawekwa katika kundi la walio katika hatari kubwa ya kutoweka (Critically Endangered) mwaka 1996, kabla ya kurejeshwa tena katika kundi la walio katika hatari ya kutoweka (Endangered) mwaka 2008. Kati ya mwaka 2009 na 2012, tafiti zilionyesha idadi ya Walia ibex iliongezeka kutoka wanyama 680 hadi 850. Kutokana na mwenendo huo, watafiti walikadiria kuwa ifikapo mwaka 2020, idadi hiyo ingefikia wanyama 975. Kwa msingi huo, walihitimisha kuwa hali ya spishi hiyo ilikuwa imeimarika na kuishusha hadi kundi la walio hatarini (Vulnerable). Hata hivyo, tathmini ya mwaka 2020 ilibaini kuwa mwaka 2019 idadi ya Walia ibex ilifikia 619 pekee, lakini ilihitimisha kuwa rekodi hiyo ya mwaka mmoja haikubadilisha mwenendo wa jumla wa ongezeko la idadi yao. “Kwa uelewa tulionao sasa, hitimisho hilo halikuwa sahihi,” alisema Paul Scholte, mshauri mwandamizi wa Mamlaka ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya Ethiopia na kiongozi wa tathmini&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Sensa yaonyesha ongezekelo la spishi nyingi za wanyama, tishio jipya kwa wanyamapori Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/sensa-ya-wanyamapori-tanzania-yaonyesha-ongezekelo-la-spishi-nyingi-za-wanyama-tishio-jipya-kwa-wanyamapori/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/sensa-ya-wanyamapori-tanzania-yaonyesha-ongezekelo-la-spishi-nyingi-za-wanyama-tishio-jipya-kwa-wanyamapori/#respond</comments>
					<pubDate>04 Agosti 2026 18:43:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Manyerere Jackton]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04121219/Twiga2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2330</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kupambana na ujangili, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Mifumo ya Ikolojia, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Spishi Zilizo Hatarini Sana, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025 imetoa ripoti yake ambayo inatoa picha mchanganyiko: upande mmoja kuna mafanikio makubwa katika kudhibiti ujangili na kuongeza idadi ya baadhi ya wanyama muhimu. Upande mwingine kuna tishio jipya la uvamizi wa maeneo ya hifadhi, na hivyo kuibua migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Zoezi hilo lilifanywa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/sensa-ya-wanyamapori-tanzania-yaonyesha-ongezekelo-la-spishi-nyingi-za-wanyama-tishio-jipya-kwa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Sensa yaonyesha ongezekelo la spishi nyingi za wanyama, tishio jipya kwa wanyamapori Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025 imetoa ripoti yake ambayo inatoa picha mchanganyiko: upande mmoja kuna mafanikio makubwa katika kudhibiti ujangili na kuongeza idadi ya baadhi ya wanyama muhimu. Upande mwingine kuna tishio jipya la uvamizi wa maeneo ya hifadhi, na hivyo kuibua migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Zoezi hilo lilifanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii ili kubaini idadi, mtawanyiko, mwenendo na hali ya ustawi wa wanyamapori nchini. Kati ya spishi mahsusi za wanyamapori zilizofanyiwa tathmini, spishi moja ya Swala twiga – gerenuk ilionyesha kupungua kwa kiwango kikubwa. Picha kwa hisani ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Ripoti ya sensa hiyo iliyofanyika kuanzia Septemba 2024 hadi Oktoba 2025, ilikabidhiwa kwa Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika hafla iliyofanyika ikulu jijini Dar es Salaam. Matokeo ya sensa hiyo yalitangazwa jijini Arusha na Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Dkt Eblate Mjingo, katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa uhifadhi. Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Ashatu Kijaji, aliyemwakilisha Rais Suluhu. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, spishi nyingi zimeongezeka kwa idadi, huku nyingine zikibaki katika viwango vinavyoonyesha uthabiti. Spishi 28 zathibitishwa Matokeo yanaonyesha kuwa Tanzania kwa sasa ina spishi 28 za wanyamapori wakubwa na wa kati, ambazo zimethibitishwa katika mifumo yote mikubwa ya ikolojia iliyofanyiwa utafiti. Hata hivyo, ripoti hiyo, inaonyesha mafanikio hayo hayajasambaa kwa kiwango kinachofanana katika maeneo yote ya nchi. Baadhi ya spishi zimeongezeka kwa kasi, nyingine zimeongezeka kwa kiwango kidogo, huku nyingine zikionyesha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/sensa-ya-wanyamapori-tanzania-yaonyesha-ongezekelo-la-spishi-nyingi-za-wanyama-tishio-jipya-kwa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/sensa-ya-wanyamapori-tanzania-yaonyesha-ongezekelo-la-spishi-nyingi-za-wanyama-tishio-jipya-kwa-wanyamapori/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/#respond</comments>
					<pubDate>04 Agosti 2026 09:15:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04091305/Screenshot-2026-08-04-121218-768x440.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2324</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Maji, Maji ya kunywa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Nishati, Samaki, Samaki wa Maji safi, Shida ya Maji, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai 24, 2026, maafisa wakiwemo wawakilishi wa Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) walikuwa wakiendesha mkutano wa mashauriano ya umma mjini Bondo ndipo msukosuko ulipoanza. Dickens Ochieng’, wakili na mwanaharakati wa kijamii aliyehudhuria mkutano huo, aliiambia Mongabay kwa simu kuwa wamiliki wa ardhi walioalikwa kwenye mkutano huo wakisema &#8220;Wadagi,&#8221; neno la Kidholuo linalomaanisha &#8220;tunakataa,&#8220; kuonyesha upinzani wao dhidi ya mradi wa nyuklia. &#8220;Kisha afisa mmoja wa polisi aliyekuwa akilinda mashirika ya serikali alitumia silaha yake na kumjeruhi mtu mmoja kwa risasi, na mkutano ukageuka msukosuko papo hapo,&#8221; alisema Ochieng’. Katika siku zilizofuata, watu 17 walikamatwa na kufungwa. Hati rasmi iliyopitiwa na Mongabay inaonyesha kwamba watuhumiwa hao wanachunguzwa kwa tuhuma za shambulio na makosa chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya Kenya (Prevention of Terrorism Act). Ochieng’, ambaye amechukua jukumu la kuwatetea kisheria, alisema &#8220;kuna ukandamizaji mkubwa unaofanywa na serikali dhidi ya wanaopinga mradi huu.&#8221; &#8220;Kama wakili, ninaendelea kuiambia jamii kwamba lazima wasimame imara, kwa sababu tuhuma za ugaidi hazina uhusiano wowote na tukio lililotokea,&#8221; alisema. &#8220;Zinakusudiwa kuwatisha na kuwanyamazisha, si kuhakikisha haki inatendeka.&#8221; Hadi sasa, watuhumiwa 15 kati ya 17 wameachiwa huru baada ya wanajamii kukusanya pesa kupitia michango ya umma ili kulipia dhamana zao, zilizowekwa kati ya KSh15,000 na KSh180,000 ($116 hadi $1,391). &#8220;Katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 13:35:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Claire Asher]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/03130229/Screenshot-2026-08-03-155156-768x493.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2306</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Chembechembe ndogo za plastiki, Ikolojia, Kemikali, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Plastiki, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili dawa moja au zaidi za viuavijasumu (hali inayojulikana kama usugu dhidi ya dawa za vijiumbe, au AMR) umeongezeka kwa kasi na kuwa dharura ya afya ya umma, huku sasa ukisababisha vifo takriban milioni 5 duniani kote kila mwaka. &#8220;AMR ni tishio la kibinadamu,&#8221; anasema Tim Walsh, profesa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mkurugenzi wa biolojia katika Taasisi ya Utafiti wa Antimicrobial ya Ineos Oxford ya Uingereza, ambaye alizungumza na Mongabay kupitia njia ya simu ya video. &#8220;Itaua watu wengi zaidi [kila mwaka] kuliko Kifua Kikuu, VVU na malaria, na iwapo haitapingwa inaweza kuipita saratani kama muuaji mkubwa zaidi.&#8221; Hadi hivi karibuni, migogoro hii miwili ya kimataifa, uchafuzi wa plastiki na usugu dhidi ya viuavijasumu, ilizingatiwa tofauti na wanasayansi na watunga sera. Lakini utafiti mpya unaonyesha kuwa inahusiana kwa karibu: Taka za plastiki hukaliwa kwa haraka na vijiumbe, hivyo kuunda aina mpya ya mfumo wa ikolojia unaoitwa &#8220;plastisphere.&#8221; Aidha, bakteria wanaoishi katika mfumo huo wanastawisha uwezo mkubwa wa kustahimili viuavijasumu kwa kasi isiyo na kifani. Kipande cha plastiki ya aina ya polyethylene (kinachojulikana kama &#8220;bio-bead&#8221;), kinachotumika kusaidia kuvunja-vunja uchafu katika mitambo ya kusafisha maji taka, ambacho kimekaliwa na fangasi pamoja na vijiumbe vingine. Wakati mwingine, vipande hivi vya plastiki&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Magugumaji ya Salvinia yaendelea kuhatarisha mazingira na ikolojia ya Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/magugumaji-ya-salvinia-yaendelea-kuhatarisha-mazingira-na-ikolojia-ya-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/magugumaji-ya-salvinia-yaendelea-kuhatarisha-mazingira-na-ikolojia-ya-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 08:34:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/31183729/magugu6PXL_20260520_094206516.PORTRAIT%40-1513612770-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2289</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mimea]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Victoria, ziwa kubwa zaidi Barani Afrika linalopatikana Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisifika kwa kuwa kitovu cha bioanuwai ya maji baridi na makazi bora ya viumbe wa majini, huenda likapoteza sifa hizo iwapo uvamizi wa magugumaji aina ya Salvinia, hautadhibitiwa haraka. Wataalam wanabainisha kuwa iwapo magugumaji hayo yataendelea kuenea katika ziwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/magugumaji-ya-salvinia-yaendelea-kuhatarisha-mazingira-na-ikolojia-ya-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Magugumaji ya Salvinia yaendelea kuhatarisha mazingira na ikolojia ya Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Victoria, ziwa kubwa zaidi Barani Afrika linalopatikana Kaskazini Magharibi mwa Tanzania, ambalo kwa muda mrefu limekuwa likisifika kwa kuwa kitovu cha bioanuwai ya maji baridi na makazi bora ya viumbe wa majini, huenda likapoteza sifa hizo iwapo uvamizi wa magugumaji aina ya Salvinia, hautadhibitiwa haraka. Wataalam wanabainisha kuwa iwapo magugumaji hayo yataendelea kuenea katika ziwa hilo, mazingira ya majini, ikolojia pamoja na shughuli za kiuchumi kwa mamilioni ya wakazi wa Afrika Mashariki, vinaweza kuathirika. Hata hivyo Serikali ilinukuliwa ikisema kuwa magugu hayo yamedhibitiwa kikamilifu. Licha ya Tanzania, Ziwa hilo linapakana katika nchi za Kenya na Uganda. Kwa upande wa Tanzania, linazungukwa na mikoa ya Mwanza, Mara, Kagera, Simiyu na Geita. Chanzo cha magugumaji vamizi Kwa mujibu wa hifadhidata ya mimea duniani, Salvinia ni mimea vamizi hatari zaidi ya majini yenye uwezo wa kuzaliana na kukua haraka sana hadi kutengeneza jamvi zito juu ya maji. Salvinia ina aina kuu za Salvinia molesta – Spishi vamizi inayojulikana kwa kutengeneza magugu mengi kwenye maziwa na mito, Salvinia minima – Spishi ndogo inayotumika pia kwenye mapambo ya majini na Salvinia natans – Spishi ya asili inayoelea kwenye maji matulivu. Jarome Kayombo, Meneja wa Kanda ya Ziwa wa Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) alinukuliwa na vyombo vya habari akisema kuwa wavuvi katika maeneo ya Buyagu (Sengerema), Chole, Nyahiti na Mbarika (Misungwi) walianza kuona magugumaji aina ya Salvinia katika Ziwa Victoria mwezi Agosti 2024. Baadhi ya watu wakivua samaki kwa kutumia chandarua huku kilimo kikiendelea kandokando ya mto Mirongo ambao huingiza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/magugumaji-ya-salvinia-yaendelea-kuhatarisha-mazingira-na-ikolojia-ya-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/magugumaji-ya-salvinia-yaendelea-kuhatarisha-mazingira-na-ikolojia-ya-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Siku ya Walinzi wa Wanyamapori: Walinzi wa jamii wabeba mzigo wa uhifadhi huku ufadhili ukipungua</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/siku-ya-walinzi-wa-wanyamapori-duniani-walinzi-wa-jamii-wabeba-mzigo-wa-uhifadhi-huku-ufadhili-ukipungua/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/siku-ya-walinzi-wa-wanyamapori-duniani-walinzi-wa-jamii-wabeba-mzigo-wa-uhifadhi-huku-ufadhili-ukipungua/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 21:38:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jack Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
		<category><![CDATA[Afrika]]></category>
		<category><![CDATA[Afrika Mashariki]]></category>
		<category><![CDATA[Mazingira]]></category>
		<category><![CDATA[Sera ya mazingira]]></category>
		<category><![CDATA[Utawala]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30212751/Photo-from-Jack-Otieno-6-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2280</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bustani za wanyama, Huduma za Mazingira, Mazingira, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Tabia za Wanyama, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Walinzi wa Pori, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAJIADO, Kenya — Purity Lakara hajutii chaguo lake la kuwa askari wa wanyamapori. Katika miaka saba ya kuhudumu katika Team Lioness, kikosi cha askari wanawake nchini Kenya, amepanda vyeo vitatu, kutoka constable hadi senior sergeant wa sasa. Mwaka 2021, Lakara alikuwa miongoni mwa askari wawili waliosafiri Madrid kupokea Tuzo ya Kimataifa ya Ustawi wa Wanyama kutoka kwa Serikali [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/siku-ya-walinzi-wa-wanyamapori-duniani-walinzi-wa-jamii-wabeba-mzigo-wa-uhifadhi-huku-ufadhili-ukipungua/" data-wpel-link="internal">Siku ya Walinzi wa Wanyamapori: Walinzi wa jamii wabeba mzigo wa uhifadhi huku ufadhili ukipungua</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAJIADO, Kenya — Purity Lakara hajutii chaguo lake la kuwa askari wa wanyamapori. Katika miaka saba ya kuhudumu katika Team Lioness, kikosi cha askari wanawake nchini Kenya, amepanda vyeo vitatu, kutoka constable hadi senior sergeant wa sasa. Mwaka 2021, Lakara alikuwa miongoni mwa askari wawili waliosafiri Madrid kupokea Tuzo ya Kimataifa ya Ustawi wa Wanyama kutoka kwa Serikali ya Uhispania, tuzo iliyotambua mchango wa kikosi hicho katika uhifadhi wa wanyamapori na mazingira. Katika Hifadhi ya Jamii ya Olgulului/Ololarashi, iliyopakana na Hifadhi ya Taifa ya Amboseli, siku yake ya kawaida inajumuisha kuratibu askari kutoka kambi tatu katika shughuli za doria, ukusanyaji wa taarifa za kiintelijensia, ufuatiliaji wa wanyamapori, na usuluhishi wa migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. &#8220;Nililelewa karibu na Amboseli na maeneo yaliyolindwa, na nikapata shauku ya uhifadhi wa wanyamapori tangu utotoni. Niliangalia jamii ya eneo hili ikiishi pamoja na wanyamapori, na wakati mwingine wakikabiliwa na changamoto katika kufanya hivyo. Ninafurahi kuwa na kazi inayonipa fursa ya kuhifadhi wanyamapori na kusaidia jamii yangu,&#8221; Lakara aliiambia Mongabay. Wanachama wa Team Lioness wako miongoni mwa askari zaidi ya 80 wa jamii ya Olgulului wanaopata msaada kutoka kwa International Fund for Animal Welfare (IFAW), shirika la kimataifa lisilo la faida, linalojikita katika uhifadhi wa wanyamapori. Kikundi cha walinzi wa wanyamapori wanawake pekee kikiwaelimisha wanafunzi wa shule moja ya msingi nchini Kenya kuhusu uhifadhi wa mazingira na usalama porini. Picha kwa hisani ya IFAW. IFAW hulipa mishahara ya askari hao kwa wakati na kuwapa mgao wa chakula, bima ya afya, sare, magari, redio, pamoja na vifaa vya ufuatiliaji na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/siku-ya-walinzi-wa-wanyamapori-duniani-walinzi-wa-jamii-wabeba-mzigo-wa-uhifadhi-huku-ufadhili-ukipungua/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/siku-ya-walinzi-wa-wanyamapori-duniani-walinzi-wa-jamii-wabeba-mzigo-wa-uhifadhi-huku-ufadhili-ukipungua/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 12:22:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30073721/Magari2-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2264</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Halijoto, Kaboni, Mabadiliko ya Tabianchi, Maliasili, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Siasa za Tabianchi, Teknolojia, Uendelevu, na  Ufanisi wa nishati]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya kuhamia matumizi ya nishati safi kwenye vyombo vya usafiri kwa kuzielekeza taasisi zote za umma kuanza kujumuisha ununuzi wa magari yanayotumia umeme na gesi asilia katika mipango na bajeti zao. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omari, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupunguza gharama kubwa za kununua mafuta. Bajaji zinazotumia umeme. Picha ya Jenifer Gilla, Mongabay. Hatua hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050  na Michango ya Taifa Iliyoamuliwa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris ambapo Tanzania imeahidi kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kupitia sekta za nishati na usafiri. Uzalishaji wa hewa ya ukaa Mpango wa kutumia nishati safi kwenye vyombo vya usafiri nchini Tanzania, iwapo utafanikiwa, utapunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi. Msololo Onditi, Mtaalam wa mabadiliko ya tabianchi na Mshauri wa Masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika Shirika la Maendeleo la Ujerumani Tanzania (GIZ), anasema kila lita moja ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya inachunguza vifo vya kutatanisha vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/#respond</comments>
					<pubDate>29 Julai 2026 14:15:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/29194917/Amboseli-KWS-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2257</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAJIADO, Kenya &#8211; Kenya inachunguza vifo vya tembo 15 vilivyotokea katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli kati ya Juni 24 na Julai 24, 2026. Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) imeiambia Mongabay kuwa uchunguzi wa awali wa maabara kuhusu vifo hivyo katika maeneo ya hifadhi ya Kimana na ranchi ya Kuku, unaonyesha huenda tembo hao walikula vitu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Kenya inachunguza vifo vya kutatanisha vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAJIADO, Kenya &#8211; Kenya inachunguza vifo vya tembo 15 vilivyotokea katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli kati ya Juni 24 na Julai 24, 2026. Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) imeiambia Mongabay kuwa uchunguzi wa awali wa maabara kuhusu vifo hivyo katika maeneo ya hifadhi ya Kimana na ranchi ya Kuku, unaonyesha huenda tembo hao walikula vitu vyenye sumu. Sampuli zilizochunguzwa katika Maabara ya Serikali, Chuo Kikuu cha Nairobi, pamoja na maabara nyingine zinazobobea katika uchunguzi wa sumu kwenye tishu na viungo, zimetoa matokeo yanayotofautiana. Uchunguzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi uligundua uwepo wa mabaki ya kemikali zinazoshukiwa kuwa na sumu katika sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa baadhi ya tembo walioathirika. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa KWS, Duncan Wanyama, tembo 10 walionyesha dalili zinazofanana, ikiwemo kupooza sehemu za mwili, hali iliyowafanya washindwe kusimama kabla ya kufa ndani ya siku moja hadi mbili. Mizoga ya tembo watano wengine ilikuwa imeharibika sana au kuliwa na wanyama wala mizoga, hivyo haikuwa rahisi kubaini chanzo cha vifo vyao. Walioathirika zaidi walikuwa tembo jike wakubwa na watoto wao, huku tembo dume aliyeripotiwa kufa akiwa mmoja tu. Hata hivyo, vipimo vya Maabara ya Serikali havikuonyesha uwepo wa sumu zilizokuwa zikitafutwa, na KWS imesema “uchunguzi zaidi wa kina bado unaendelea”. Jinsi vifo hivyo viligunduliwa Wanyama aliiambia Mongabay kuwa baadhi ya vifo hivyo viligunduliwa baada ya vifaa vya kufuatilia mienendo ya baadhi ya tembo kuonyesha kuwa walikuwa hawasogei. Alisema uchunguzi wa sababu nyingine zinazoweza kusababisha vifo hivyo unaendelea ili kubaini kama tembo hao walikufa kutokana na chanzo kimoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 17:58:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mazera Ndurya]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28172645/Screenshot-2026-07-28-202121-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2245</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Jinsia na Uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Ongezeko la Joto Baharini, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti wanazotumia baharini na hata katika kutafuta soko. Marinda Masudi, mwenye umri wa miaka 40, ni miongoni mwa wakulima waliojitosa katika ukulima wa mwani kama njia moja ya kukidhi mahitaji ya familia yake. Ilimchukua muda kuamua kujiingiza katika kilimo hicho, lakini biashara yake ya mahamri ilipoanza kudorora, hakuwa na la ziada. Wanawake kutoka Mwazaro, Kaunti ya Kwale, wakionyesha baadhi ya bidhaa, zikiwemo krimu na sabuni walizotengeneza kutoka kwa mwani. Picha na Mazera Ndurya, Mongabay. “Baada ya kujisajili na Kitengo cha Kusimamia Fukwe (BMU) cha Kibuyuni, nilionyeshwa sehemu ya kuanza kulima mwani, na baada ya takriban miezi miwili nilianza kuvuna mwani, kuukausha na kuuuza. Mapato niliyopata nilimsaidia mume wangu kuwasomesha watoto. Mara ya kwanza nilipovuna na kuuza mwani kutoka kwa bloki mbili, nilipata kima cha KSh30,000 ($230),” alisema Marinda. Kama ilivyokuwa na wakulima wengine, alipoanza ukulima, walikuwa wakitumia mbinu ile ambayo imetumika tangu jadi, ambayo hufanyika katika maeneo karibu na ufuo wa bahari. “Mkulima alihitajika kuingia msituni na kukata vigingi vingi vya kufungia kamba na kuweka mbegu. Kwa shamba moja la vipande sita, mtu alihitaji vigingi 300 kufanikisha ukulima wa mwani,” Marinda alieleza. Mbinu ya jadi ilijulikana kama sikio moja au mfungo mmoja, yaani kufunga mbegu moja moja kwenye kamba. Kwa mujibu wa kitabu “Sea Level Rise and Ocean Health in the&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:16:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28111600/Tembo-6-1.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2227</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga baada ya kusikiliza mawasilisho ya pande zote mbili. Rufani hiyo iliyowasilishwa na Wakili wa Serikali Paulina Massawe ilitokana na uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Morogoro uliowaachia huru Yahaya Juma na Masima Mlugu waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000 bila kibali halali. Mahakama ya Wilaya Katika Mahakama ya Wilaya, upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi sita, akiwemo mtunza vielelezo, askari aliyefanya ukamataji, shahidi huru aliyeshuhudia upekuzi na ukamataji, mhifadhi wa wanyamapori aliyefanya uthamini wa meno ya tembo, askari wa TANAPA aliyeshiriki operesheni pamoja na mpelelezi wa kesi. Upande wa mashtaka uliwasilisha vielelezo saba, vikiwemo vipande 18 vya meno ya tembo, meno matatu kamili ya tembo, magunia mawili ya salfeti yaliyobebea meno hayo, pikipiki aina ya FEKON yenye namba T43 CNF, hati ya ukamataji na ripoti ya uthamini iliyoonyesha kuwa nyara hizo zilikuwa na thamani hiyo. Kwa upande wa utetezi, washtakiwa wote wawili walitoa ushahidi wao wenyewe. Mshtakiwa wa kwanza aliwasilisha pia flashi diski iliyokuwa na video ya YouTube akidai kuwa meno ya tembo yaliyoonyeshwa kwenye taarifa ya habari hayakuwa na alama, tofauti na yale yaliyowasilishwa mahakamani kama vielelezo. Mahakama ya Wilaya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:03:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28112229/ELEPHANT-3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2230</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sheria, Tembo, Uhalifu, Usafirishaji wa Wanyamapori, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama ya Wilaya ya Songwe ilimhukumu mshtakiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kukutwa na vipande 10 vya meno ya tembo vyenye thamani ya $60,000 bila kibali halali. Upande wa mashtaka uliita mashahidi sita na kuwasilisha vielelezo mbalimbali, huku mshtakiwa akikana mashtaka na kudai alikamatwa kimakosa alipokuwa amekwenda kununua mahindi na hakuwa na shahidi. Mamlaka ya mahakama Katika rufaa yake, Nchola alijiwakilisha mwenyewe, alipinga hukumu hiyo akidai miongoni mwa mambo mengine kuwa Mahakama ya Wilaya haikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo kwa kuwa kumbukumbu za kesi hazikuonyesha kuwepo kwa hati ya idhini ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) pamoja na cheti cha mamlaka vinavyotakiwa kisheria katika makosa ya uhujumu uchumi. Katika kuunga mkono rufaa yake, mrufani alidai kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha shtaka dhidi yake pasipo kuacha shaka yoyote ya msingi. Alidai kuwa ushahidi wa shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka (PW1) kuhusu uthamini wa nyara za Serikali haukuwa wa kuaminika. Pia alidai kuwa mlolongo wa utunzaji wa vielelezo haukuthibitishwa kwa sababu shahidi muhimu hakuitwa kutoa ushahidi. Aidha alidai kuwa mashahidi wa upande wa mashtaka walishindwa kuvitambua ipasavyo vielelezo walipokuwa wakitoa ushahidi mahakamani. Uhalali wa vielelezo Aliongeza kuwa hata mahakama ya mwanzo ilionyesha mashaka kuhusu uhalali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Juhudi za kuondoa mikaratusi ili kumhifadhi mnyama wa kipekee asiyepatikana kwingineko duniani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>24 Julai 2026 16:13:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Linah Mwamachi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/24162115/Boulengerula-niedeni_John-Measey-1000x667-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2211</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Amfibia, Ardhi iliyoharibika, Biashara ya mbao, Bioanuai, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kutoweka, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mbao, Miti, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Upandaji Miti, Urejesho wa Asili, na  Wanyama wasio na Mifupa ya Mgongo]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>TAITA TAVETA, Kenya &#8211; Kusini mashariki mwa Kenya, ndani ya msitu mnene wa Sagalla, kunapatikana mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni). Mlima huo wa Sagalla, wenye urefu wa zaidi ya mita 1,400 kutoka usawa wa bahari, una miti ya aina mbalimbali inayounda makazi ya Sagalla caecilian. Kiumbe wa kipekee ulimwenguni Kilomita 18 kutoka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/" data-wpel-link="internal">Juhudi za kuondoa mikaratusi ili kumhifadhi mnyama wa kipekee asiyepatikana kwingineko duniani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[TAITA TAVETA, Kenya &#8211; Kusini mashariki mwa Kenya, ndani ya msitu mnene wa Sagalla, kunapatikana mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni). Mlima huo wa Sagalla, wenye urefu wa zaidi ya mita 1,400 kutoka usawa wa bahari, una miti ya aina mbalimbali inayounda makazi ya Sagalla caecilian. Kiumbe wa kipekee ulimwenguni Kilomita 18 kutoka tambarare za mji wa Voi, Mongabay ilizuru msitu huo wa Sagalla unaoweza kufikiwa kwa gari na pikipiki hadi sehemu fulani, na sehemu iliyosalia hufikiwa kwa miguu. Mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni. Picha na Patrick Malonza. Mongabay ilitaka kufahamu iwapo jamii inatambua spishi hii na faida zake kwa ikolojia, na ilifanikiwa kukutana na wanajiji wakiwa katika shughuli zao za kila siku shambani. “Mimi sikuwa nafahamu mnyama huyu. Nilikuwa namuona shambani kisha namkatakata kwa jembe au namgonga kwa mawe ili afe, kwa sababu anafanana na nyoka,” anasema Jemimah Mwaiga. Sasa Mwaiga anafahamisha Mongabay kuhusu umuhimu wa kiumbe huyo, na kufafanua jinsi walihusishwa katika kutafuta jina lake la kinyumbani, “kilima mrota”. “Tulijifunza kuwa kiumbe huyo husaidia katika ukulima na ubora wa mchanga kwa kuchanganya mchanga na virutubisho vilivyo mchangani na kuongeza rutuba ya asili ya mchanga,” Mwaiga anaelezea Mongabay. Mwanasayansi wa masuala ya mchanga na mazingira Kenneth Macharia wa shirika la Edge of Existence, anasema kiumbe huyu ni wa kipekee katika mlima wa Sagalla. Huishi katika mazingira yenye unyevunyevu, na mchanga wenye rutuba. Macharia anaongeza: “Jamii zinaweza kuimarisha kilimo pamoja na utunzaji wa mazingira kwa kutumia mbinu bora katika mchanga kama vile kupanda miti ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/#respond</comments>
					<pubDate>23 Julai 2026 12:11:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ini Ekott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23115923/Screenshot-2026-07-23-143214-768x438.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2184</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Cote D'Ivoire, Kenya, Nigeria, Uingereza, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Gesi, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Ufanisi wa nishati, na  Utoaji wa Gesi Chafu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja bila huduma za upishi safi. Kanda hiyo ni nyumbani kwa idadi kubwa zaidi ya watu duniani ambayo bado inategemea kuni, mkaa na mafuta ya taa kwa ajili ya kupikia kila siku, kulingana na shirika la IEA. Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema uchafuzi wa hewa wa makazi, ambao mwingi wake huzalishwa na nishati hizi za kupikia zinazochafua mazingira, unahusishwa na vifo vya mapema takriban milioni 2.9 kila mwaka, huku wanawake na watoto wakibeba mzigo mkubwa zaidi. &#8220;Upishi Safi Afrika 2026: Ripoti ya Maendeleo&#8221; inakadiria kuwa karibu watu milioni 15 walipata fursa ya kutumia upishi safi katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara mwaka wa 2025, karibu 35% zaidi ya wastani wa faida ya kila mwaka iliyorekodiwa kwa miaka mitano iliyopita. Ikiwa itathibitishwa, hii itakuwa ongezeko kubwa zaidi la kila mwaka kuwahi kurekodiwa. Côte d&#8217;Ivoire, Kenya na Nigeria zilipata faida kubwa zaidi. Makadirio hayo yametokana na mfumo wa hisabati unaounganisha takwimu za uingizaji wa majiko (vifaa vya kupikia vinavyochanganya jiko la kawaida na oveni) na gesi ya petroli iliyoshinikizwa (LPG), uwekezaji katika miundombinu, nishati na teknolojia zinazohitajika kwa ajili ya upikaji safi, pamoja na ufuatiliaji wa sera. Badala ya kutegemea tafiti za makazi, ambazo ndizo kipimo cha kuaminika zaidi cha upatikanaji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 12:20:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23122231/park-7-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2193</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Maliasili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira, Mgogoro wa Rasilimali, Sheria, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uanaharakati, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Kitropiki, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Misitu, Uokoaji wa Wanyamapori, Usimamizi Endelevu wa Misitu, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Utowekaji wa Misitu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande zote katika kesi hiyo ili kuandaa na kuwasilisha ripoti mahakamani. Katika taarifa iliyotumwa kwa Mongabay, shirika la Save the Nairobi National Park (SaveNNP) lililaani kile lilichokiita &#8220;vitisho na vitendo vya kutisha&#8221; kutoka kwa maafisa wa KWS, pamoja na hatua ya kuwanyima wanaharakati hao ruhusa ya kuingia katika eneo la ziara. SaveNNP ilisema hatua hiyo inapingana na mwaliko wa KWS kwa vyombo vya habari kushiriki katika ziara hiyo ya mahakama. Ujenzi unaendelea katika maeneo yanayobishaniwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nairobi huku Mahakama ya Mazingira na Ardhi ikiendelea kusikiliza kesi iliyowasilishwa na wanaharakati wa mazingira. Picha kwa hisani ya SaveNNP. Mongabay iliona barua ya KWS iliyowaalika wanahabari kuhudhuria ziara ya eneo hilo iliyoongozwa na Msajili wa Mahakama ya Mazingira. Katika taarifa yao, SaveNNP na JustAct ziliishutumu KWS kwa kutaka &#8220;kudhibiti simulizi&#8221; kuhusu mradi huo na kuhakikisha sauti za Wakenya hazisikiki mahakamani wala kupitia vyombo vya habari wakati wa ukaguzi wa eneo hilo. Madai kama hayo pia yalitolewa na Friends of Nairobi National Park. Msemaji wa KWS, Duncan Wanyama, alisema wageni hao hawakuzuiwa kuingia, na kwam ba askari wa wanyamapori walikuwa wakitekeleza tu taratibu za kawaida zinazotumika ndani ya hifadhi hiyo, vyombo vya habari vya ndani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 10:40:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21195128/Raia-wa-Korea-Kaskazini.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2165</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Ikolojia, Matumizi ya Wanyamapori, Mifumo ya Ikolojia, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri yaliwasilishwa mahakamani na Wakili wa Serikali Mkuu, Twawabu Issa mbele ya Hakimu Hakimu Mkazi Mkuu, Salome Mwasha aliyekuwa akisikiliza shauri hilo dhidi ya mshtakiwa Ra aliyedaiwa kukutwa na vipande 504 vya meno ya tembo bila kibali. Wakili Twawabu alidai kuwa DPP kwa mamlaka aliyonayo kisheria aliwasilisha uamuzi wa kusitisha mashtaka (nolle prosequi)  (chini ya Kifungu cha 92 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2023 ambapo zamani kilikuwa Kifungu cha 91 kabla ya marekebisho ya 2022) akionyesha kuwa Jamhuri haina nia ya kuendelea na shauri hilo hivyo akaomba mahakama imwachie huru mshtakiwa. Mshitakiwa atakiwa kuondoka nchini Upande wa mashtaka pia uliwasilisha maombi &#8220;persona non grata&#8221; kuonyesha kuwa mshtakiwa huyo hatakiwi kuendelea kubaki nchini Tanzania na anatakiwa kuondoka. Mahakama baada ya kusikiliza maombi hayo iliyakubali na kuamuru mshtakiwa aachiliwe huru na aondoke nchini. Katika shauri lolote la jinai na katika hatua yoyote kabla ya hukumu au uamuzi, DPP anaweza kuwasilisha nolle prosequi kwa kuitaarifu Mahakama kuwa Jamhuri haitaendelea na mashtaka lakini haizuii kumshtaki tena mshtakiwa pale inapohitajika kufanya hivyo. Ra alifikishwa mahakamani mara ya kwanza Mei 5 , 2026 akikabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/#respond</comments>
					<pubDate>21 Julai 2026 17:56:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Kelvin Matuku]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21171918/Screenshot-2026-07-21-201312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2148</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Fedha ya mfumo wa ikolojia, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi wa Mazingira, Ufugaji Samaki, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari upya mustakabali wa uvuvi katika ziwa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi barani Afrika. “Wakati mwingine nakaa ziwani usiku mzima na kurudi na kati ya samaki 300 na 359 pekee,” anasema Otieno, ambaye amevua katika Ziwa Victoria kwa miongo kadhaa. “Samaki ni wachache na kipato pia kinapungua. Kama mvuvi, naona njia ambayo imebakia ni kukumbatia vizimba vya samaki ili tuweze kuendelea kuishi.” Ufukwe wa Paga kwenye Ziwa Victoria. Picha na Kelvin Matuku, Mongabay. Ziwa Victoria ni chanzo cha kujikimu kwa jamii za wavuvi nchini Kenya, Uganda na Tanzania, kupitia uvuvi na biashara zinazohusiana nao. Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2023, katika miaka ya hivi karibuni, Ziwa Victoria na eneo lake la vyanzo vya maji vimeathirika vibaya kutokana na “uvuvi kupita kiasi, umwagikaji wa mafuta, utiririshaji wa taka ambazo hazijatibiwa, kuenea kwa spishi vamizi, uchotaji wa maji kupita kiasi kutoka bonde la ziwa, na mabadiliko ya tabianchi, miongoni mwa sababu nyingine.” Kushuka kwa uzalishaji wa samaki Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS), uzalishaji wa samaki katika Ziwa Victoria umeshuka kutoka takriban tani za metriki 94,349 mwaka wa 2021 hadi 67,575 mwaka wa 2024. Huu ni upungufu wa zaidi ya tani 27,700 katika kipindi cha miaka mitatu. Upungufu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/#respond</comments>
					<pubDate>17 Julai 2026 19:39:13 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ouma Elvine Tina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/17192647/Screenshot-2026-07-17-221755.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2139</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Akili Mnemba, Biashara ya Kilimo, Chakula, Jinsia na Uhifadhi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo serikali ya ukoloni ya Uingereza iliitengea jamii ya Wanubi baada ya mababu zao kutumikia kama askari kwenye jeshi la King’s African Rifles. Awali, eneo hilo lilikuwa na ukubwa wa hekta 1,698 (ekari 4,197). Leo, kutokana na ukuaji wa miji, kufukuzwa kwa nguvu, uporaji wa ardhi na miradi mbalimbali ya serikali iliyotekelezwa kwa nyakati tofauti, ni hekta 116 (ekari 288) pekee zilizosalia mikononi mwa Wanubi, bila wao kuwahi kulipwa fidia yoyote. Kupitia Mazingira Women Initiative, Hamida ametumia zaidi ya miaka 25 kujihusisha na masuala ya usimamizi wa taka, kilimo kinachotumia teknolojia za kisasa, haki za kumiliki ardhi, na uongozi wa wanawake. Pia amewahi kugombea ubunge mara tatu katika eneo bunge la Kibera na ana mpango wa kugombea tena mwaka wa 2027. Hamida alizungumza na Mongabay mchana wa Jumamosi ya baridi, wakati alipokuwa akiondoka kwenye msikiti mkubwa zaidi katika eneo bunge la Kibera. Ofisi zake zilikuwa karibu, mwendo mfupi tu kutoka hapo. Tulipokuwa tukielekea huko, watu kadhaa walimsimamisha ili kumsalimia. Aliwajibu kila mmoja kwa kusema &#8220;Assalaamu aleikum,&#8221; akasimama kidogo ili kupiga nao gumzo, na akamshika msichana mdogo usoni kwa upole. Aliniongoza kupitia lango la mabati hadi kwenye eneo tulivu lenye nyumba zenye kuta za udongo na paa za mabati. Eneo hilo lilikuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka hadi rasilimali: Jinsi lava wa nzi chuma wanavyopunguza tatizo la taka oza jijini Dar es Salaam</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/taka-hadi-rasilimali-jinsi-lava-wa-nzi-chuma-wanavyopunguza-tatizo-la-taka-oza-jijini-dar-es-salaam/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/taka-hadi-rasilimali-jinsi-lava-wa-nzi-chuma-wanavyopunguza-tatizo-la-taka-oza-jijini-dar-es-salaam/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 08:37:04 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/15210008/Taka1-1.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2103</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Mashujaa wa Mazingira, Maudhui ya mazingira yanayoonyesha mabadiliko chanya, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Taka, na  Uchumi wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Katika moja ya eneo la uzalishaji wa lava wa nzi chuma (Black Soldier Fly Larvae) Jijini Dar es Salaam, yanaonekana matenga yaliyopangwa kwa safu, maelfu ya lava wenye rangi ya kijivu wakijongea juu ya mabaki ya chakula yaliyooza. Ingawa wadudu hawa wanaonekana kama funza wa kawaida, lava wa nzi chuma [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/taka-hadi-rasilimali-jinsi-lava-wa-nzi-chuma-wanavyopunguza-tatizo-la-taka-oza-jijini-dar-es-salaam/" data-wpel-link="internal">Taka hadi rasilimali: Jinsi lava wa nzi chuma wanavyopunguza tatizo la taka oza jijini Dar es Salaam</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Katika moja ya eneo la uzalishaji wa lava wa nzi chuma (Black Soldier Fly Larvae) Jijini Dar es Salaam, yanaonekana matenga yaliyopangwa kwa safu, maelfu ya lava wenye rangi ya kijivu wakijongea juu ya mabaki ya chakula yaliyooza. Ingawa wadudu hawa wanaonekana kama funza wa kawaida, lava wa nzi chuma wameanza kuchukuliwa kama sehemu ya suluhisho la tatizo linalozidi kukua la udhibiti wa taka oza katika maeneo ya miji mikubwa kama Dar es Salaam. Kadri miji inavyoendelea kupanuka, ndivyo changamoto ya usimamizi wa taka inavyozidi kuwa kubwa. Dar es Salaam, jiji kubwa zaidi nchini Tanzania na moja ya miji inayokua kwa kasi zaidi Afrika Mashariki, ni mfano halisi wa changamoto hiyo, ambapo kwa mujibu wa ripoti ya Dar es Salaam Urban Resilience Programme (DURP) ya mwaka 2024, jiji hilo huzalisha takribani tani 5,300 za taka ngumu kila siku. Lori likimwaga taka oza maeneo ya kiwanda cha Mabwepande kwa ajili ya kuchakata taka hizo na kuwalisha lava wa nzi chuma pamoja na kutengeneza mbolea. Picha kwa hisani ya Kiwanda cha Mabwepande. Asilimia 72 ya taka hizo, sawa na takribani tani 3,800 huishia katika madampo au maeneo yasiyo rasmi ya kutupia taka. Matokeo yake imekuwa kuongezeka kwa harufu mbaya, kuzaliana kwa wadudu, kuziba kwa mifereji ya maji na uzalishaji wa gesi chafu zinazochangia mabadiliko ya tabianchi. Lakini wakati mamlaka za mijini zikihangaika kutafuta njia za kukabiliana na tatizo hilo, teknolojia inayotumia lava wa nzi chuma inaanza kuonyesha uwezekano wa kubadili taka oza kuwa rasilimali. Kutoka taka za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/taka-hadi-rasilimali-jinsi-lava-wa-nzi-chuma-wanavyopunguza-tatizo-la-taka-oza-jijini-dar-es-salaam/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/taka-hadi-rasilimali-jinsi-lava-wa-nzi-chuma-wanavyopunguza-tatizo-la-taka-oza-jijini-dar-es-salaam/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 08:18:04 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16074828/Screenshot-2026-07-16-003002-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2110</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uzuri wa Kiikolojia, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara walipoanza kuwasili ili kununua samaki, Mwazigona alikaa juu ya boti iliyovunjika na kupinduliwa akitazama upeo wa bahari. Safari yake ya asubuhi ilikuwa imemletea kilo 2 pekee za samaki. Alikuwa na hofu kuhusu kupungua kwa kiasi kikubwa kwa mavuno yake ya samaki katika miaka ya hivi karibuni. &#8220;Idadi ya wavuvi imeongezeka; tumekuwa wengi mno,&#8221; alisema. Hiyo ndiyo sababu kuu iliyomfanya aondoke kijijini kwake Shariani, kilichoko umbali wa kilomita 40 kuelekea kaskazini, ili kufanyia shughuli zake za uvuvi Mtwapa; eneo aliloona kuwa na wavuvi wachache na uwezekano mzuri zaidi wa kufikia masoko. Nchini Kenya, vitengo vya usimamizi wa fukwe (BMU), kama vile Mtwapa BMU Mtwapa BMU ambayo Mwazigona ni mali yake, vina mamlaka ya kisheria ya kusaidia ukusanyaji wa takwimu za uvuvi kwa ajili ya kuwasilishwa kwa serikali: hasa aina ya samaki ambao wanachama wake huvua na uzito. Takwimu hizi zinalenga kufahamisha uamuzi wa serikali kuhusu uvuvi mdogo ili iweze kusaidia kubadilisha ushindani wa kupungua kwa samaki ambao Mwazigona na wenzake wanashuhudia. Pia zinalenga kuwasaidia wavuvi wenyewe kufanya maamuzi kuhusu wapi na wakati wa kuvua. Hata hivyo, takwimu za uvuvi mdogo za BMU hazijakuwa sahihi na haipatikani kwa wadau. Ili kushughulikia tatizo hili na kuboresha uendelevu wa uvuvi mdogo wa Kenya,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:56:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/15110719/Taka-za-kielektroniki-zikikusanywa-kwa-ajili-ya-kutengeneza-vitu-vingine-Picha-hisani-ya-WEEE-Centre-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2080</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na jalala ambamo zinatupwa takataka mbalimbali hatari, zikiwemo zile za kielektroniki, huku kambale akiwa amevuliwa katika bwawa lililochafuliwa na taka za aina hiyo. Fundi akitiengeneza kompyuta iliyoharibika. Picha cha Christopher Kidanka. Katika maeneo mengi, hasa mijini, wananchi hula vyakula ambavyo vina uwezekano mkubwa wa kuwa na sumu zinazotokana na taka za kielektroniki bila wao kufafahamu. Kadhalika mazingira katika maeneo hayo nayo hayako salama kutokana na taka hizo kuchafua udongo, maji, hewa na kuharibu makazi ya viumbe na kuhatarisha bioanuwai. Ongezeko la taka za kielektroniki Taka za kielektroniki ni vifaa vya elektroniki kama simu za mkononi, kompyuta, televisheni, jokofu, betri, viyoyozi, mashine za kufulia, chaja, nyaya na vifaa vingine vilivyoharibika, kupitwa na wakati au visivyotumika tena, na vinavyotupwa bila tahadhari. Kadri matumizi ya vifaa vya kielektroniki yanavyoongezeka nchini ndivyo uzalishaji wa taka hizo unavyoongezeka. Kulthum Shushu, Ofisa Mazingira wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), anasema Tanzania huzalisha wastani wa tani 35,000 za taka za kielektroniki kwa mwaka, lakini ni chini ya asilimia tano tu ndiyo hurejelezwa na kuchakatwa kutokana na ukweli kuwa urejelezaji wa taka hizo hatarishi ni ghali sana. Hali hiyo, anasema, husababisha taka kujikusanya katika mazingira na mzigo wa kuzisimamia huongezeka siku&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:11:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14191215/Namakongoro-4-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2075</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Ikolojia, Irejeshaji wa Mfumo wa Ikolojia, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu mkubwa wa makazi ya viumbe baharini, hivyo kupunguza idadi ya samaki, pweza na viumbe wengine wanaotegemea mazingira hayo kuishi na kuzaliana. Baadhi ya viumbe walihamia kwenye maeneo yenye kina kirefu, jambo lililovuruga mfumo wa ikolojia wa bahari na kupunguza bioanuwai. Hata hivyo, tangu mwaka 2021 hali ilianza kubadilika kufuatia juhudi za pamoja za jamii, Serikali, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU) na taasisi ya Sea Sense, inayojihusisha na uhifadhi wa mazingira ya bahari na ukanda wa pwani, kuanzisha mikakati ya uhifadhi wa bahari. Wavuvi wa Namakongoro wakipewa mafunzo ya uhifadhi bahari kupitia njia za uvuvi endelevu na Maofisa wa Halmashauri ya Namakongoro pamoja na Taasisi ya Seasense. Picha kwa hisani ya SeaSense. Juhudi hizo zimeleta mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kusaidia kurejesha matumbawe, kuongeza wingi wa samaki waliokuwa wamepungua pamoja na kupungua kwa kiwango kikubwa kwa uvuvi haramu. Kurejesha uhai wa bahari Mafanikio ya kurejesha uhai wa bahari Namakongoro yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya wanakijiji, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU), Sea Sense na Serikali. Baada ya kubaini kuwa chanzo kikuu cha uharibifu huo kilikuwa ni uvuvi haramu, taasisi ya Sea Sense iliingia katika kijiji cha Namakongoro. Mratibu wa Mradi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 18:14:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14175046/Omar-Shafi-akishona-nyavu-yake-yakuvulia-samaki-katika-eneo-la-Mtangawanda-kaunti-ya-LamuKenya.-Picha-na-Ruth-Keah.-2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2062</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sayansi, Sayansi ya Hali ya Tabianchi, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya uvuvi kesho yake. “Tangu nianze uvuvi miaka 40 sasa, nimekuwa nikitumia nyavu hizi za uzi kuvua samaki kwa sababu haziharibu mazingira ya bahari,” anasema Shafi. Omar Shafi akishona nyavu yake yakuvulia samaki katika eneo la Mtangawanda kaunti ya Lamu, Kenya. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kulingana naye, ujio wa zana mbalimbali za kuvulia samaki umeharibu mazingira ya bahari kiasi cha kwamba samaki na viumbe wengine baharini wamepungua sana. “Kuna zana nyingi ambazo wavuvi wanatumia, ambazo zinaharibu utulivu wa bahari. Hivyo husababisha baadhi ya viumbe baharini kupungua,” anasema. Vifaa vinavyosababisha kelele baharini ni kama meli kubwa za mizigo na abiria, boti za mwendo kasi, zana za kuvulia samaki kama trola, mitambo ya utafiti na uchimbaji na mitambo ya ujenzi wa miundombinu ya baharini. Vifaa hivi vimetajwa kusababisha kelele ambazo huathiri uwezo wa viumbe hao kuwasiliana, kusafiri na kusaka chakula. Kama anavyoeleza Shafi, nguva ni miongoni mwa wanyama baharini ambao alikuwa akikutana nao mara kwa mara alipoanza uvuvi hasa katika maeneo ya Manda na Dodori, kaunti ya Lamu. Lakini sasa imekuwa vigumu sana kwake kuwaona. Nguva bado yuko “Kwa maoni yangu, mnyama huyu nguva bado yuko, lakini kwa sababu bahari haina utulivu kutokana na kelele za vyombo vya uvuvi, nguva hukimbia, siwaoni tena,” anasema Omar. Taswira hiyo haielezwi na Shafi peke yake, bali pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 13:43:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Brown]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04134630/Screenshot-2026-08-04-164214.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2344</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ajabu, Migogoro, Sokwe, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika migogoro mikubwa wao kwa wao. Mwandishi wa Mongabay, Keith Anthony Fabro, aliripoti kuhusu kile kilichoelezwa kama &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale nchini Uganda. Kabla ya mgawanyiko huo, kundi la Ngogo lilikuwa na sokwe kati ya 150 na 200, na hivyo kuwa miongoni mwa makundi makubwa zaidi ya sokwe kuwahi kurekodiwa porini. Baadaye kundi hilo liligawanyika katika makundi mawili yanayojulikana kama Kundi la Kati (Central) na Kundi la Magharibi (Western), yaliyotajwa kutokana na maeneo ya msitu walikokuwa wakipatikana. Kati ya mwaka 2018 na 2024, kundi la Magharibi lilifanya mashambulizi 24 dhidi ya kundi la Kati, na kuua angalau madume saba yaliyokomaa pamoja na sokwe wachanga 17. Migogoro hiyo bado inaendelea na inaweza kuwa na athari za muda mrefu kwa idadi ya sokwe katika eneo hilo. Utafiti unaonyesha jinsi mabadiliko ya mahusiano ya kijamii yanavyoweza kusababisha mgawanyiko na vurugu hata katika jamii za wanyama. Ni kwa namna gani sokwe na Ringo Starr wanafanana? Kupiga ngoma huku ukiimba kwa wakati mmoja ni kipaji kinachovutia, iwe kwa mwanamuzi kama Karen Carpenter au kwa Ringo Starr. Lakini inaonekana sokwe pia wana uwezo huo. Mwandishi wa Mongabay, Liz Kimbrough, alieleza kuhusu Ayumu, sokwe dume mwenye&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 17:28:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13171052/Screenshot-2026-07-13-195700-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2046</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Maji, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi wa Maji, Ufugaji Samaki, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia wangu kila siku ni kwamba naamka na mtu mwenye bidii ya kazi akichukua sehemu yangu ya kutua, akichukua eneo langu la uvuvi,&#8221; aliiambia hadhira, akielezea jinsi maendeleo ya utalii na uwekezaji mwingine wa pwani yanavyoendelea kushindana na jamii za uvuvi wa jadi kwa ajili ya kupata ufikiaji wa bahari. Kobusingye alisema wanawake wengi wanakabiliwa na hatari katika sekta ya uvuvi, mazingira duni ya kazi na shinikizo linaloongezeka kutoka kwa maendeleo yanayozidi kusukuma shughuli za uvuvi pembezoni. Katika baadhi ya jamii, haki za kitamaduni zinapuuzwa na serikali; huku kuongezeka kwa kina cha bahari, mmomonyoko wa udongo na kupungua kwa samaki wanaovuliwa kukifanya maisha ambayo tayari ni magumu kuwa magumu zaidi, aliwaambia waliohudhuria mkutano ulioandaliwa na Ocean Resilience Climate Alliance (ORCA). Licha ya changamoto hizi, Kobusingye alisema wanawake wanasalia kuwa muhimu katika kuendeleza uvuvi na uchumi wa pwani. Husindika samaki, huuza vyakula vya baharini na kusaidia familia zao, ikiwa ni pamoja na kulipa ada za shule, kutokana na mapato wanayopata. Hata hivyo, licha ya jukumu lao katika sekta hiyo, wanawake wengi bado hawana usemi mkubwa katika jinsi uvuvi unavyosimamiwa. Lovin Kobusingye pia ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kati Farms Ltd, kampuni ya usindikaji wa mazao ya kilimo. Picha kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 16:04:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13150952/Screenshot-2026-07-13-180713-768x466.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2039</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chembechembe ndogo za plastiki, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Plastiki, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, na  Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki huishia baharini kila mwaka na zinachangia 80% ya uchafu wote wa baharini unaopatikana katika uso wa bahari na mashapo ya bahari kuu. Kenya inakabiliwa na changamoto kubwa za uchafuzi wa plastiki, haswa katika vituo vya mijini na kando ya pwani yake. Plastiki huchangia takriban 20% ya tani 22,000 za taka zinazozalishwa kila siku nchini Kenya, kulingana na makadirio. Ni 27% tu ya taka za plastiki zinakusanywa, ambapo 8% huchakatwa tena na 19% zilizobaki hutupwa katika majaa ya taka au madampo holela. Taka za plastiki ambazo hazijakusanywa na kusimamiwa vyema mara nyingi huishia kwenye mito na baharini. Huvuruga mifumo ikolojia, huhatarisha wanyamapori, na huathiri utalii na uvuvi. Mwaka wa 2017, Kenya ilianzisha marufuku ya matumizi, utengenezaji na uingizaji wa mifuko ya plastiki ya matumizi ya mara moja. Mnamo 2020, marufuku hiyo iliongezwa hadi plastiki zinazotumika mara moja katika maeneo yaliyohifadhiwa. Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki (NPAP Kenya) utasaidia kuharakisha mpito wa nchi hiyo kuelekea uchumi wa plastiki wa mviringo, kulingana na Clemence Schmid, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (Global Plastic Action Partnership – GPAP) katika Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum – WEF). Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/#comments</comments>
					<pubDate>08 Julai 2026 18:36:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/08182238/2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2033</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Aina Vamizi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Mazao ya kilimo kimoja, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro, Mimea, Mimea yenye Tiba, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya mandhari yameshuhudiwa hapa. Badala ya mashamba mapana ya mahindi pekee kama ilivyokuwa zamani, ardhi sasa imepambwa na rangi ya kijivu, kijani kibichi na zambarau, ya mimea hii ya manukato. Wanawake hapa wana matumaini mapya, si tu ya kulinda maisha yao, bali ya kuendeleza kilimo chenye tija ya kiuchumi. Miongoni mwa wanawake hao ni Nelly Musana kutoka Enkutoto, na mwanachama wa kikundi cha kina mama cha Oloisesiai Self Help Group. Karibu yake yupo Mama Arami Musekenya, mama wa watoto sita, mfugaji na mkulima mzaliwa wa Maasai Mara ambaye maisha yake yote ameshuhudia migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Kwa miaka mingi, wanawake hawa waliishi kwa hofu kubwa. Hofu hiyo haikuja mchana; ilikuja usiku, hasa wakati mahindi yalipoanza kuzaa na kukomaa. “Tembo walikuwa wakija bila hodi,” anasema Musekenya, huku akitazama shamba lililojaa rosemary. “Kitu kibaya si kuona tembo; ni kuamka asubuhi ukute hakuna kitu kabisa.” Kiwango cha uharibifu unaofanywa na wanyama hawa wakubwa ni jambo la kutia wasiwasi mkubwa na linaloacha familia katika umaskini wa ghafla. Musekenya anasimulia kuwa kuna nyakati ambapo kundi la tembo watano tu linaweza kuingia shambani na ndani ya usiku mmoja tu, wanamaliza kabisa ekari tano za mahindi. Uharibifu huo wa kasi ya ajabu unamaanisha kuwa jasho&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>07 Julai 2026 21:50:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Clark]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/07214049/Screenshot-2026-07-08-003816-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2025</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Migogoro, Samaki, Samaki wa Maji safi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. &#8220;Ofisi ya zamani ilikuwa pale chini,&#8221; mvuvi anasema, akielekeza kuelekea ufuo wa magharibi wa Ziwa Turkana, ziwa kubwa zaidi la kudumu la jangwa duniani, linaloonekana kilomita chache tu. &#8220;Lakini sasa iko kwenye maji.&#8221; Katika kipindi cha miaka 15 iliyopita, Ziwa Turkana limeongezeka kwa takriban mita 8-10 (futi 26-33). Hii imeongeza upana wa uso wake kwa karibu 10%. Ndani na karibu na kitovu cha uvuvi cha Kalokol, mamia ya watu wamelazimika kuhama makazi yao kutokana na kuongezeka huku kwa kina cha maji. Katika kisa cha Esirite, kijiji alichokulia, Natole, kimeachwa kwa muda mrefu. Mvuvi huyo amelazimika kuhama mara tatu tangu 2014, akisukumwa mbali zaidi na ardhi ya mababu zake na maeneo ya kuzaliana ya ufukweni ambayo amevua kwa muda mrefu wa maisha yake. &#8220;Tunateseka, lakini hakuna anayetusaidia,&#8221; anasema. &#8220;Tunamuomba Mungu msaada.&#8221; Lakini hata kanisa ambalo Esirite alikuwa akisalia liko kwenye maji. Hali inayoendelea huko Kalokol ni sehemu ya mwelekeo mpana. Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2010, maziwa mengi katika eneo lote la Bonde la Ufa la Kenya yamefurika, upanuzi wake ukiongezeka baada ya mvua kubwa sana mnamo 2020, na kulazimisha makumi ya maelfu ya watu kuacha makazi yao. Lakini hapa, katika kona hii ya kaskazini ya nchi ambayo imepuuzwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>