<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=wanyama&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/wanyama/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 07 Sep 2026 16:22:54 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mwanauhifadhi John Salehe, aliyepigania uhifadhi shirikishi Tanzaia, afariki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/#respond</comments>
					<pubDate>17 Agosti 2026 10:59:12 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Rhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/17104948/Screenshot-2026-08-17-134842-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2494</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Filosofia ya Uhifadhi, Jamii Asili, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Maendeleo ya Jamii, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro ya Ardhi, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uendelevu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kati ya Ziwa Manyara na Tarangire, mstari kwenye ramani peke yake haukuwahi kuwa wa kutosha. Tembo, nyumbu, na wanyama wengine walipita kwenye ardhi iliyotumiwa na wafugaji na wakulima, ardhi ambayo barabara, mashamba na makazi yalikuwa yakizidi kusambaa. Kulinda ushoroba huo kulihitaji zaidi ya kuweka mipaka: kulihitaji kuwashawishi watu waliokaa hapo kwamba wanyamapori walikuwa na nafasi katika mustakabali wao. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/" data-wpel-link="internal">Mwanauhifadhi John Salehe, aliyepigania uhifadhi shirikishi Tanzaia, afariki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kati ya Ziwa Manyara na Tarangire, mstari kwenye ramani peke yake haukuwahi kuwa wa kutosha. Tembo, nyumbu, na wanyama wengine walipita kwenye ardhi iliyotumiwa na wafugaji na wakulima, ardhi ambayo barabara, mashamba na makazi yalikuwa yakizidi kusambaa. Kulinda ushoroba huo kulihitaji zaidi ya kuweka mipaka: kulihitaji kuwashawishi watu waliokaa hapo kwamba wanyamapori walikuwa na nafasi katika mustakabali wao. Kulihitaji kukabiliana na hasara ya mifugo iliyouawa na wanyama wakali, migogoro kuhusu mgawanyo wa mapato, na kazi ngumu ya kuimarisha taasisi za mitaa. John Gospel Yonazi Salehe, aliyefariki tarehe 19 Juni akiwa na umri wa miaka 71, alitumia sehemu kubwa ya maisha yake ya kazi kushughulikia changamoto kama hizo. Mtanzania huyu, aliyefunzwa katika taaluma ya misitu, alifanya kazi serikalini, kisha katika FAO, UNDP, WWF, na hatimaye African Wildlife Foundation, ambako alihudumu kama mkurugenzi wa Tanzania. Alifanya kazi kwa zaidi ya miongo minne katika sekta za misitu, maeneo ya wanyamapori, na miradi ya maendeleo katika Afrika Mashariki. Kwa Salehe, uhifadhi ulikuwa wa vitendo na wenye msingi imara wa kijamii. Katika Nyanda za Maasai, alijikita katika kulinda ushoroba wa wanyamapori na kuimarisha Maeneo ya Usimamizi wa Wanyamapori yanayosimamiwa na jamii. Alitaka faida za uhifadhi ziwafikie wanajamii, akiunga mkono ujenzi wa mazizi yaliyoimarishwa ili kulinda mifugo dhidi ya wanyama wakali, na utoaji wa fidia kwa hasara zilizosababishwa na wanyamapori. Kwa mtazamo wake, jamii haikuwa hadhira inayosubiri maamuzi ya wengine; ilikuwa nguzo ya msingi ya jinsi uhifadhi unavyopaswa kufanya kazi. Mtazamo huo huo uliongoza kazi yake katika sekta ya misitu. Katika maeneo ya kati ya Tanzania, ambapo uzalishaji wa mkaa na kilimo viliongeza shinikizo kubwa kwa misitu, Salehe alisisitiza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>11 Agosti 2026 20:01:52 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/11191616/Main-Mnyama-Nguva-akiwa-baharini-Picha-na-Mtandao-wa-Jamii-Forums-Tanzania.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2426</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia wa Baharini, Mamalia Wakubwa, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tabia za Wanyama, Teknolojia na Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Ustawi wa Wanyama, Uzuri wa Kiikolojia, Wanawake katika Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo sasa ni marehemu. Siku hiyo watu walipika na kuila nyama yake. Mimi sikuweza kuila kwa sababu niliposhika nyama yake, mwili wangu ulianza kuwasha,” alisema Juma. Amiri Juma, mvuvi kutoka kijiji cha Kibuyuni Kaunti ya Kwale akiwa katika ofisi ya BMU cha Kibuyuni. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kwa mujibu wa Juma, hilo lilikuwa tukio la kawaida, kwani hakukuwa na uelewa kuhusu umuhimu wa kumhifadhi nguva. Anasema ilikuwa rahisi sana kuwaona nguva, na hii pia ilikuwa ishara nzuri kwa wavuvi kuwa bahari ilikuwa na samaki wengi. Juma anaamini kutoweka kwa mnyama huyo baharini kumechochewa na shughuli nyingi za uvuvi. “Bahari imeingiliwa sana. Zamani kulikuwa na mitego tu. Sasa watu wanaingia kila sehemu, usiku na mchana. Wanyama wengi wamepotea. Hata samaki wamepungua,” anasema. Hapo zamani nguva alikuwa kitoweo kitamu sana kwa familia nyingi eneo la pwani, kabla ya kuwekwa kwa sheria inayopiga marufuku kumkamata. Faki Kassim, mvuvi kutoka kijiji cha Bodo, Kaunti ya Kwale, anasema takriban miaka 30 iliyopita, yeye na wavuvi wenzake walikuwa wakishika nguva, kumchinja na kuuza nyama yake. “Nguva ana ngozi ngumu sana. Nyama yake ni nyekundu na yenye mafuta mengi. Miaka mingi iliyopita tulikuwa tukiuza kipande kimoja cha nyama yake kwa shilingi moja,” anasema. Anaeleza kuwa kabla ya kumchinja nguva, walilazimika kutekeleza itikadi zao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Sensa: Idadi ya tembo Tanzania bado ni chini ya nusu ya ilivyokuwa miaka 20 iliyopita</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/#respond</comments>
					<pubDate>06 Agosti 2026 18:04:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/06180552/Screenshot-2026-08-06-175346-768x497.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2393</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Matumizi ya Wanyamapori, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Idadi ya tembo nchini Tanzania sasa ni takriban asilimia 49.6 ya waliokuwepo mwaka 2005/2006, wakati idadi yao ilikuwa 134,588. Takwimu hizo zimetolewa na Ripoti ya Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025. Zoezi hili lilifanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kubaini idadi, mtawanyiko, mwenendo na hali ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/" data-wpel-link="internal">Sensa: Idadi ya tembo Tanzania bado ni chini ya nusu ya ilivyokuwa miaka 20 iliyopita</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Idadi ya tembo nchini Tanzania sasa ni takriban asilimia 49.6 ya waliokuwepo mwaka 2005/2006, wakati idadi yao ilikuwa 134,588. Takwimu hizo zimetolewa na Ripoti ya Sensa ya Taifa ya Wanyamapori ya mwaka 2024/2025. Zoezi hili lilifanywa na Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii kwa lengo la kubaini idadi, mtawanyiko, mwenendo na hali ya ustawi wa wanyamapori nchini. Ripoti ya sensa hiyo iliyofanyika kuanzia Septemba 2024 hadi Oktoba 2025 ilikabidhiwa kwa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan katika hafla iliyofanyika katika Ikulu jijini Dar es Salaam. Matokeo ya sensa hiyo yalitangazwa jijini Arusha na Mkurugenzi Mkuu wa TAWIRI, Dkt Eblate Mjingo, katika hafla iliyohudhuriwa na wadau mbalimbali wa uhifadhi. Mgeni rasmi alikuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt Ashatu Kijaji, aliyemwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, idadi ya tembo iliyopatikana mwaka 2024/2025, ambayo ni 66,714, ni asilimia 49.6 ya tembo 134,588 waliokuwepo mwaka 2005/2006. Uwepo wa mifugo kwa wingi, sambamba na makazi ya binadamu yaliyoambatana na shughuli za kilimo pembezoni/ndani ya maeneo hifadhi, ni miongoni mwa sababu zinaathiri ustawi wa wanyama. Picha kwa hisani ya Wizara ya Maliasili na Utalii. Mkurugenzi wa Utafiti wa TAWIRI Julius Keyyu alisema kuwa idadi ya tembo nchini ilishuka kutoka takriban tembo 134,000 waliokuwepo mwaka 2005/2006 hadi 46,408 mwaka 2014 kutokana na kuenea kwa ujangili unaolenga pembe za ndovu. Hata hivyo, alisema kuwa hatua mahsusi zilizochukuliwa na serikali, ikiwa ni pamoja na kupambana na ujangili na kuimarisha usimamizi wa hifadhi, zilisaidia idadi ya tembo kuanza kuongezeka tena. Aidha, Keyyu alibainisha kuwa ingawa idadi ya tembo imeongezeka,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/06/sensa-tembo-tanzania-sasa-ni-asilimia-49-ya-waliokuwepo-mwaka-2005-2006/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Shinikizo laongezeka kwa Kenya kuchunguza vifo vya tembo 15 Amboseli, ikiwemo uchimbaji dhahabu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 21:03:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05202638/1An-elephant-relocation-exercise-in-one-of-the-National-Parks-in-Kenya-in-2025.-Photo-courtesy-of-KWS-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2370</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Utalii, Utalii wa Mazingira, Utawala, Uthibitisho, Uwazi, Uzuri wa Kiikolojia, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyamapori, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAJIADO, Kenya &#8211; Shinikizo linaendelea kuongezeka dhidi ya Serikali ya Kenya ikitakiwa kufanya uchunguzi wa kina na huru kuhusu vifo vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli. Hii ni siku chache tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Kenya Wildlife Service (KWS) Erustus Kanga kuthibitisha kwamba wanyama hao walikufa baada ya kumeza sumu ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Shinikizo laongezeka kwa Kenya kuchunguza vifo vya tembo 15 Amboseli, ikiwemo uchimbaji dhahabu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAJIADO, Kenya &#8211; Shinikizo linaendelea kuongezeka dhidi ya Serikali ya Kenya ikitakiwa kufanya uchunguzi wa kina na huru kuhusu vifo vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli. Hii ni siku chache tu baada ya Mkurugenzi Mkuu wa Kenya Wildlife Service (KWS) Erustus Kanga kuthibitisha kwamba wanyama hao walikufa baada ya kumeza sumu ya sianidi. KWS ilithibitisha kwamba sianidi ndiyo iliyosababisha vifo hivyo, na ilisema labda tembo walipata sumu hiyo kupitia maji yaliyochafuliwa na dawa ya kuua wadudu iliyonyunyiziwa kwenye mashamba ya nyanya katika eneo la Kimana. Hata hivyo, shirika hilo bado halijabainisha kama vifo hivyo vilikuwa vya bahati mbaya au vilifanywa kwa makusudi. KWS iliiambia Mongabay kwamba uchunguzi unaendelea ili kuthibitisha matokeo ya maabara mbalimbali zinazoshiriki katika kuchunguza vifo hivyo vilivyotokea kati ya 24 Juni na 24 Julai 2026. &#8220;Maabara mbalimbali zimebadilishana sampuli ili kila moja ithibitishe matokeo ambayo tayari yanasubiriwa na umma. Maabara zinahitaji angalau siku 14 kukamilisha zoezi hili,&#8221; Mkurugenzi wa Mawasiliano wa KWS Duncan Wanyama aliiambia Mongabay kwa simu. Maabara zinazohusika ni pamoja na Maabara ya Mkemia wa Serikali na ya Chuo Kikuu cha Nairobi. Matokeo kutangazwa KWS ilisema itatangaza matokeo yoyote muhimu ya uchunguzi kutoka eneo la tukio na  vipimo vya maabara. &#8220;Wachunguzi watahakikisha wanapata kiini cha suala hili. Sampuli zinazobadilishwa ni pamoja na damu, ini na baadhi ya vimiminika vingine vya mwili vilivyokusanywa kutoka kwenye mizoga hiyo. Jana, maabara moja iliomba sampuli za damu zaidi. Kila maabara ilikuwa imechukua vielelezo tofauti vya sampuli, na sasa zinahitaji kupima zile ambazo hazikuchukuliwa awali,&#8221; Wanyama aliiambia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/hinikizo-laongezeka-kwa-serikali-ya-kenya-kuchunguza-kwa-kina-vifo-vya-tembo-15-amboseli/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 17:00:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122556/nyumbu2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2358</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Sheria, Uchumi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Serengeti iliyokuwa imemhukumu Marwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa hayo baada ya kukubali rufaa yake na hoja za Jamhuri za kuunga mkono rufani hiyo huku wakibainisha kuwa hawakuweza kuthibisha mashtaka bila kuacha shaka. Mahakama ya Wilaya Serengeti Mahakama ya Wilaya ilimtia hatiani kwa makosa matatu ambayo ni; kuingia hifadhini bila kibali, kumiliki panga ndani ya hifadhi bila kibali pamoja na kumiliki sehemu ya mguu wa nyumbu ambao haukuwa umechunwa ikiwa ni nyara ya Serikali yenye thamani ya Sh 1,586,000 (Dola za Marekani 603). Wanyama aina ya nyumbu wakirejea katika makazi yao ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakitokea katika nchi ya jirani ya Kenya, hususan kwenye mbuya ya Masai Mara. Picha kwa hisasi Blogu ya Michuzi. Upande wa mashtaka ulidai mahakamani kuwa Desemba 7, 2025, askari wa hifadhi walimkamata mshtakiwa katika eneo la Korongo la Nyamburi ndani ya Hifadhi ya Serengeti akiwa na panga na sehemu hiyo ya nyumbu. Utetezi Mahakamani Alipojitetea, Marwa Nyamhanga alidai kuwa Desemba 6, 2025 alikuwa akitoka kwenye sherehe ya harusi akiwa amelewa, ndipo askari wa hifadhi walipomkamata akiwa njiani. Alidai kuwa askari hao walimshikilia katika kituo chao usiku kucha na asubuhi yake walimbambia panga pamoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbuzi mwitu maarufu wa Ethiopia warejea kwenye hatari kubwa ya kutoweka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 12:30:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Shreya Dasgupta]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122610/Screenshot-2026-08-05-152416-768x496.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2357</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Bustani za wanyama, Ikolojia, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Matumizi ya Wanyamapori, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Spishi Zilizo Hatarini Sana, Ujangili, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mbuzi mwitu wa Walia, spishi adimu ya mbuzi anayepatikana kaskazini mwa Ethiopia pekee, kwa mara nyingine ametambuliwa kama mnyama aliye katika hatari kubwa ya kutoweka(Critically Endangered) baada ya tathmini za hivi karibuni kuonyesha idadi yake imeendelea kupungua na kushuka chini ya kiwango muhimu kinachotumiwa na wataalamu wa uhifadhi. Mnyama huyo maarufu hupatikana zaidi kwenye miamba mirefu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Mbuzi mwitu maarufu wa Ethiopia warejea kwenye hatari kubwa ya kutoweka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mbuzi mwitu wa Walia, spishi adimu ya mbuzi anayepatikana kaskazini mwa Ethiopia pekee, kwa mara nyingine ametambuliwa kama mnyama aliye katika hatari kubwa ya kutoweka(Critically Endangered) baada ya tathmini za hivi karibuni kuonyesha idadi yake imeendelea kupungua na kushuka chini ya kiwango muhimu kinachotumiwa na wataalamu wa uhifadhi. Mnyama huyo maarufu hupatikana zaidi kwenye miamba mirefu na maeneo magumu kufikika ya Hifadhi ya Taifa ya Milima ya Simien. Awali alikuwa ameorodheshwa katika kundi la wanyama walio hatarini (Vulnerable) kwenye Orodha Nyekundu ya Muungano wa Kimataifa wa Uhifadhi wa Mazingira (IUCN). Hali ya uhifadhi wa Walia ibex (Capra walie) imekuwa ikibadilika kwa miaka. Mwaka 1986, iliorodheshwa kuwa katika hatari ya kutoweka (Endangered), kisha ikawekwa katika kundi la walio katika hatari kubwa ya kutoweka (Critically Endangered) mwaka 1996, kabla ya kurejeshwa tena katika kundi la walio katika hatari ya kutoweka (Endangered) mwaka 2008. Kati ya mwaka 2009 na 2012, tafiti zilionyesha idadi ya Walia ibex iliongezeka kutoka wanyama 680 hadi 850. Kutokana na mwenendo huo, watafiti walikadiria kuwa ifikapo mwaka 2020, idadi hiyo ingefikia wanyama 975. Kwa msingi huo, walihitimisha kuwa hali ya spishi hiyo ilikuwa imeimarika na kuishusha hadi kundi la walio hatarini (Vulnerable). Hata hivyo, tathmini ya mwaka 2020 ilibaini kuwa mwaka 2019 idadi ya Walia ibex ilifikia 619 pekee, lakini ilihitimisha kuwa rekodi hiyo ya mwaka mmoja haikubadilisha mwenendo wa jumla wa ongezeko la idadi yao. “Kwa uelewa tulionao sasa, hitimisho hilo halikuwa sahihi,” alisema Paul Scholte, mshauri mwandamizi wa Mamlaka ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya Ethiopia na kiongozi wa tathmini&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/mbuzi-mwitu-maarufu-wa-ethiopia-warejea-kwenye-hatari-kubwa-ya-kutoweka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya inachunguza vifo vya kutatanisha vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/#respond</comments>
					<pubDate>29 Julai 2026 14:15:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/29194917/Amboseli-KWS-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2257</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAJIADO, Kenya &#8211; Kenya inachunguza vifo vya tembo 15 vilivyotokea katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli kati ya Juni 24 na Julai 24, 2026. Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) imeiambia Mongabay kuwa uchunguzi wa awali wa maabara kuhusu vifo hivyo katika maeneo ya hifadhi ya Kimana na ranchi ya Kuku, unaonyesha huenda tembo hao walikula vitu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Kenya inachunguza vifo vya kutatanisha vya tembo 15 katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAJIADO, Kenya &#8211; Kenya inachunguza vifo vya tembo 15 vilivyotokea katika mfumo wa ikolojia wa Amboseli kati ya Juni 24 na Julai 24, 2026. Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) imeiambia Mongabay kuwa uchunguzi wa awali wa maabara kuhusu vifo hivyo katika maeneo ya hifadhi ya Kimana na ranchi ya Kuku, unaonyesha huenda tembo hao walikula vitu vyenye sumu. Sampuli zilizochunguzwa katika Maabara ya Serikali, Chuo Kikuu cha Nairobi, pamoja na maabara nyingine zinazobobea katika uchunguzi wa sumu kwenye tishu na viungo, zimetoa matokeo yanayotofautiana. Uchunguzi wa Chuo Kikuu cha Nairobi uligundua uwepo wa mabaki ya kemikali zinazoshukiwa kuwa na sumu katika sampuli zilizochukuliwa kutoka kwa baadhi ya tembo walioathirika. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Mawasiliano wa KWS, Duncan Wanyama, tembo 10 walionyesha dalili zinazofanana, ikiwemo kupooza sehemu za mwili, hali iliyowafanya washindwe kusimama kabla ya kufa ndani ya siku moja hadi mbili. Mizoga ya tembo watano wengine ilikuwa imeharibika sana au kuliwa na wanyama wala mizoga, hivyo haikuwa rahisi kubaini chanzo cha vifo vyao. Walioathirika zaidi walikuwa tembo jike wakubwa na watoto wao, huku tembo dume aliyeripotiwa kufa akiwa mmoja tu. Hata hivyo, vipimo vya Maabara ya Serikali havikuonyesha uwepo wa sumu zilizokuwa zikitafutwa, na KWS imesema “uchunguzi zaidi wa kina bado unaendelea”. Jinsi vifo hivyo viligunduliwa Wanyama aliiambia Mongabay kuwa baadhi ya vifo hivyo viligunduliwa baada ya vifaa vya kufuatilia mienendo ya baadhi ya tembo kuonyesha kuwa walikuwa hawasogei. Alisema uchunguzi wa sababu nyingine zinazoweza kusababisha vifo hivyo unaendelea ili kubaini kama tembo hao walikufa kutokana na chanzo kimoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/29/kenya-yachunguza-vifo-vya-kutatanisha-vya-tembo-15-amboseli/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:16:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28111600/Tembo-6-1.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2227</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga baada ya kusikiliza mawasilisho ya pande zote mbili. Rufani hiyo iliyowasilishwa na Wakili wa Serikali Paulina Massawe ilitokana na uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Morogoro uliowaachia huru Yahaya Juma na Masima Mlugu waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000 bila kibali halali. Mahakama ya Wilaya Katika Mahakama ya Wilaya, upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi sita, akiwemo mtunza vielelezo, askari aliyefanya ukamataji, shahidi huru aliyeshuhudia upekuzi na ukamataji, mhifadhi wa wanyamapori aliyefanya uthamini wa meno ya tembo, askari wa TANAPA aliyeshiriki operesheni pamoja na mpelelezi wa kesi. Upande wa mashtaka uliwasilisha vielelezo saba, vikiwemo vipande 18 vya meno ya tembo, meno matatu kamili ya tembo, magunia mawili ya salfeti yaliyobebea meno hayo, pikipiki aina ya FEKON yenye namba T43 CNF, hati ya ukamataji na ripoti ya uthamini iliyoonyesha kuwa nyara hizo zilikuwa na thamani hiyo. Kwa upande wa utetezi, washtakiwa wote wawili walitoa ushahidi wao wenyewe. Mshtakiwa wa kwanza aliwasilisha pia flashi diski iliyokuwa na video ya YouTube akidai kuwa meno ya tembo yaliyoonyeshwa kwenye taarifa ya habari hayakuwa na alama, tofauti na yale yaliyowasilishwa mahakamani kama vielelezo. Mahakama ya Wilaya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 10:40:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21195128/Raia-wa-Korea-Kaskazini.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2165</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Ikolojia, Matumizi ya Wanyamapori, Mifumo ya Ikolojia, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri yaliwasilishwa mahakamani na Wakili wa Serikali Mkuu, Twawabu Issa mbele ya Hakimu Hakimu Mkazi Mkuu, Salome Mwasha aliyekuwa akisikiliza shauri hilo dhidi ya mshtakiwa Ra aliyedaiwa kukutwa na vipande 504 vya meno ya tembo bila kibali. Wakili Twawabu alidai kuwa DPP kwa mamlaka aliyonayo kisheria aliwasilisha uamuzi wa kusitisha mashtaka (nolle prosequi)  (chini ya Kifungu cha 92 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2023 ambapo zamani kilikuwa Kifungu cha 91 kabla ya marekebisho ya 2022) akionyesha kuwa Jamhuri haina nia ya kuendelea na shauri hilo hivyo akaomba mahakama imwachie huru mshtakiwa. Mshitakiwa atakiwa kuondoka nchini Upande wa mashtaka pia uliwasilisha maombi &#8220;persona non grata&#8221; kuonyesha kuwa mshtakiwa huyo hatakiwi kuendelea kubaki nchini Tanzania na anatakiwa kuondoka. Mahakama baada ya kusikiliza maombi hayo iliyakubali na kuamuru mshtakiwa aachiliwe huru na aondoke nchini. Katika shauri lolote la jinai na katika hatua yoyote kabla ya hukumu au uamuzi, DPP anaweza kuwasilisha nolle prosequi kwa kuitaarifu Mahakama kuwa Jamhuri haitaendelea na mashtaka lakini haizuii kumshtaki tena mshtakiwa pale inapohitajika kufanya hivyo. Ra alifikishwa mahakamani mara ya kwanza Mei 5 , 2026 akikabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 18:14:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14175046/Omar-Shafi-akishona-nyavu-yake-yakuvulia-samaki-katika-eneo-la-Mtangawanda-kaunti-ya-LamuKenya.-Picha-na-Ruth-Keah.-2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2062</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sayansi, Sayansi ya Hali ya Tabianchi, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya uvuvi kesho yake. “Tangu nianze uvuvi miaka 40 sasa, nimekuwa nikitumia nyavu hizi za uzi kuvua samaki kwa sababu haziharibu mazingira ya bahari,” anasema Shafi. Omar Shafi akishona nyavu yake yakuvulia samaki katika eneo la Mtangawanda kaunti ya Lamu, Kenya. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kulingana naye, ujio wa zana mbalimbali za kuvulia samaki umeharibu mazingira ya bahari kiasi cha kwamba samaki na viumbe wengine baharini wamepungua sana. “Kuna zana nyingi ambazo wavuvi wanatumia, ambazo zinaharibu utulivu wa bahari. Hivyo husababisha baadhi ya viumbe baharini kupungua,” anasema. Vifaa vinavyosababisha kelele baharini ni kama meli kubwa za mizigo na abiria, boti za mwendo kasi, zana za kuvulia samaki kama trola, mitambo ya utafiti na uchimbaji na mitambo ya ujenzi wa miundombinu ya baharini. Vifaa hivi vimetajwa kusababisha kelele ambazo huathiri uwezo wa viumbe hao kuwasiliana, kusafiri na kusaka chakula. Kama anavyoeleza Shafi, nguva ni miongoni mwa wanyama baharini ambao alikuwa akikutana nao mara kwa mara alipoanza uvuvi hasa katika maeneo ya Manda na Dodori, kaunti ya Lamu. Lakini sasa imekuwa vigumu sana kwake kuwaona. Nguva bado yuko “Kwa maoni yangu, mnyama huyu nguva bado yuko, lakini kwa sababu bahari haina utulivu kutokana na kelele za vyombo vya uvuvi, nguva hukimbia, siwaoni tena,” anasema Omar. Taswira hiyo haielezwi na Shafi peke yake, bali pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 13:43:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Brown]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04134630/Screenshot-2026-08-04-164214.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2344</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ajabu, Migogoro, Sokwe, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika migogoro mikubwa wao kwa wao. Mwandishi wa Mongabay, Keith Anthony Fabro, aliripoti kuhusu kile kilichoelezwa kama &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale nchini Uganda. Kabla ya mgawanyiko huo, kundi la Ngogo lilikuwa na sokwe kati ya 150 na 200, na hivyo kuwa miongoni mwa makundi makubwa zaidi ya sokwe kuwahi kurekodiwa porini. Baadaye kundi hilo liligawanyika katika makundi mawili yanayojulikana kama Kundi la Kati (Central) na Kundi la Magharibi (Western), yaliyotajwa kutokana na maeneo ya msitu walikokuwa wakipatikana. Kati ya mwaka 2018 na 2024, kundi la Magharibi lilifanya mashambulizi 24 dhidi ya kundi la Kati, na kuua angalau madume saba yaliyokomaa pamoja na sokwe wachanga 17. Migogoro hiyo bado inaendelea na inaweza kuwa na athari za muda mrefu kwa idadi ya sokwe katika eneo hilo. Utafiti unaonyesha jinsi mabadiliko ya mahusiano ya kijamii yanavyoweza kusababisha mgawanyiko na vurugu hata katika jamii za wanyama. Ni kwa namna gani sokwe na Ringo Starr wanafanana? Kupiga ngoma huku ukiimba kwa wakati mmoja ni kipaji kinachovutia, iwe kwa mwanamuzi kama Karen Carpenter au kwa Ringo Starr. Lakini inaonekana sokwe pia wana uwezo huo. Mwandishi wa Mongabay, Liz Kimbrough, alieleza kuhusu Ayumu, sokwe dume mwenye&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/#comments</comments>
					<pubDate>08 Julai 2026 18:36:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/08182238/2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2033</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Aina Vamizi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Mazao ya kilimo kimoja, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro, Mimea, Mimea yenye Tiba, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya mandhari yameshuhudiwa hapa. Badala ya mashamba mapana ya mahindi pekee kama ilivyokuwa zamani, ardhi sasa imepambwa na rangi ya kijivu, kijani kibichi na zambarau, ya mimea hii ya manukato. Wanawake hapa wana matumaini mapya, si tu ya kulinda maisha yao, bali ya kuendeleza kilimo chenye tija ya kiuchumi. Miongoni mwa wanawake hao ni Nelly Musana kutoka Enkutoto, na mwanachama wa kikundi cha kina mama cha Oloisesiai Self Help Group. Karibu yake yupo Mama Arami Musekenya, mama wa watoto sita, mfugaji na mkulima mzaliwa wa Maasai Mara ambaye maisha yake yote ameshuhudia migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Kwa miaka mingi, wanawake hawa waliishi kwa hofu kubwa. Hofu hiyo haikuja mchana; ilikuja usiku, hasa wakati mahindi yalipoanza kuzaa na kukomaa. “Tembo walikuwa wakija bila hodi,” anasema Musekenya, huku akitazama shamba lililojaa rosemary. “Kitu kibaya si kuona tembo; ni kuamka asubuhi ukute hakuna kitu kabisa.” Kiwango cha uharibifu unaofanywa na wanyama hawa wakubwa ni jambo la kutia wasiwasi mkubwa na linaloacha familia katika umaskini wa ghafla. Musekenya anasimulia kuwa kuna nyakati ambapo kundi la tembo watano tu linaweza kuingia shambani na ndani ya usiku mmoja tu, wanamaliza kabisa ekari tano za mahindi. Uharibifu huo wa kasi ya ajabu unamaanisha kuwa jasho&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/#respond</comments>
					<pubDate>01 Julai 2026 10:25:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/01114338/Screenshot-2026-07-01-144315.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1958</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Uwindaji, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na Mohammed dhidi ya Jamhuri. Sulemani anakabiliwa na mashtaka matatu, shtaka la kuongoza genge la uhalifu, kushiriki biashara haramu ya nyara na kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria, akiwa pamoja na washtakiwa wengine watatu katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 10770 ya mwaka 2026 inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam. Katika maombi yake ya dhamana, Wakili wa mshtakiwa, Meschack Dede, aliiomba Mahakama Kuu izingatie kuwa makosa yanayomkabili mteja wake yanadhaminika na kwamba thamani ya mali inayodaiwa, nusu ihesabiwe kwa kugawanywa kwa washtakiwa wote wanne. Ombi la wakili lapita Upande wa Jamhuri haukupinga ombi hilo la wakili na wala haukuwasilisha kiapo cha kupinga maombi. Wakili wa Serikali Grace Kibaki aliiomba mahakama izingatie hati ya mashtaka pamoja na masharti ya Sheria ya Uhujumu Uchumi kuhusu utoaji wa dhamana. Baada ya kusikiliza maombi hayo, Jaji Kirekiano alikubali kumpatia mwombaji dhamana kwa kuzingatia masharti ya kisheria kuhusu kiwango cha fedha kinachotakiwa kuwekwa mahakamani. Alisema kifungu cha 36(5)(a) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kinamtaka mshtakiwa kuweka fedha taslimu au mali yenye thamani ya nusu ya fedha au mali inayohusika katika kosa. Jaji alitegemea maamuzi ya awali ya mahakama, ikiwemo kesi ya Arafat&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/#respond</comments>
					<pubDate>22 Juni 2026 19:12:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23161035/KESI-YA-MENO-YA-TEMBO-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1907</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu wa Mazingira, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, Wanyama Wanaowinda, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, shauri lilifutwa, lakini muda mfupi baadaye wakasomewa mashtaka upya mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustine Rwizile, ambaye sasa hivi ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Washitakiwa walikuwa 11 Wakati kesi inaanza, washitakiwa walikuwa 11, lakini idadi hiyo ilipungua baada ya washtakiwa watano kuingia kwenye maridhiano na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ambapo walikiri makosa yao na kuachiliwa baada ya kutimiza makubaliano waliyoafikiana. Washtakiwa waliobakia katika shauri hilo ni Victor Mawanda, Mussa Abdallah, Abbas Jabu, Haruna Kasa na Halfani Kahengele. Awali ilidaiwa katika hati mashtaka kuwa kati ya Januari mwaka 2006 na Juni mwaka 2016, washtakiwa walipanga njama ya kuongoza genge la uhalifu Jijini Dar es Salaam. Walidaiwa kuuza, kupokea, kununua, kuhamisha, kusafirisha na kumiliki vipande 660 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 4,656,795,000 ambayo ni nyara za serikali. Ilidaiwa pia kuwa kati ya Aprili mosi na Juni 24 mwaka 2016, maeneo ya Mbezi Msakuzi wilayani Ubungo, washtakiwa walikutwa wakimiliki vipande hivyo vya meno ya tembo bila kuwa na kibali ama leseni kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori. Washitakiwa walikana mashitaka na wako gerezani kwa kuwa kesi yao ya uhujumu uchumi haina dhamana. Korti kusikiliza shahidi wa 10 Hadi sasa shauri hilo limeshasikilizwa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti mpya wadokeza maeneo yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia yanaweza kuathiri ustawi wa jamii za wenyeji</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 19:09:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Solomon Yimer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18185147/Screenshot-2026-06-18-215028-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1883</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Nyani, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Tabia za Wanyama, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Tembo, Ufugaji wa Uhifadhi, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ukanda wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Ustawi wa Wanyama, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Nature unaonyesha kuwa maeneo ya hifadhi ya Ethiopia yalipunguza kasi ya ukataji miti na upanuzi wa kilimo, huku yakisaidia kudumisha nyanda za malisho. Lakini utafiti pia unapendekeza kuwa faida zile zile za uhifadhi zinaweza pia kuhusishwa na kupungua kwa usalama wa chakula na ustawi kwa jamii zilizo karibu, huku ukisisitiza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/" data-wpel-link="internal">Utafiti mpya wadokeza maeneo yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia yanaweza kuathiri ustawi wa jamii za wenyeji</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Utafiti mpya uliochapishwa katika jarida la Nature unaonyesha kuwa maeneo ya hifadhi ya Ethiopia yalipunguza kasi ya ukataji miti na upanuzi wa kilimo, huku yakisaidia kudumisha nyanda za malisho. Lakini utafiti pia unapendekeza kuwa faida zile zile za uhifadhi zinaweza pia kuhusishwa na kupungua kwa usalama wa chakula na ustawi kwa jamii zilizo karibu, huku ukisisitiza baadhi ya tahadhari katika matokeo yao. Utafiti huo, uliofanywa kwa ushirikiano kati ya watafiti nchini Ethiopia na Uingereza, na Mamlaka ya Uhifadhi wa Wanyamapori ya Ethiopia, ulitathmini matokeo ya kimazingira na kijamii katika maeneo 25 yaliyohifadhiwa nchini Ethiopia katika kipindi cha mwaka wa 2000-2020. Walipima kiwango cha misitu, upanuzi wa kilimo, nyanda za malisho, usalama wa chakula, utofauti wa lishe na ustawi wa nyenzo. Ingawa maeneo yaliyohifadhiwa yalikuwa na ufanisi mkubwa katika kupunguza uharibifu wa mazingira licha ya shinikizo kubwa kutoka kwa ukuaji wa idadi ya watu, upanuzi wa kilimo, na mahitaji ya ardhi, watafiti waligundua mchangamano wa maslahi (trade-offs) kati ya matokeo ya mazingira na kijamii katika tathmini zao. Maeneo 12 yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo mazuri ya kimazingira kwa gharama ya ustawi wa jamii. Wakati huo huo, maeneo matano kati ya maeneo yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo ya &#8220;faida kwa wote&#8221; kwa uhifadhi wa bioanuwai na ustawi wa jamii na maeneo matatu yaliyohifadhiwa yalikuwa na matokeo ya &#8220;hasara kwa wote&#8221;. &#8220;Ethiopia ina utajiri wa viumbe hai, lakini pia inakabiliwa na changamoto kubwa kuhusu umaskini, usalama wa chakula na mahitaji ya ardhi,&#8221; alisema Sophie Jago, mwandishi mkuu wa utafiti na msaidizi wa utafiti katika Bustani za Kifalme za Mimea za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/utafiti-mpya-wadokeza-maeneo-yaliyohifadhiwa-nchini-ethiopia-yanaweza-kuathiri-ustawi-wa-jamii-za-wenyeji/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 11:57:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Manuel Fonseca]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11113159/Screenshot-2026-06-11-143059.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1834</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Misitu, Moto, Moto wa Misitu, Reptilia, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na mwonekano wa kuvutia. “Nakumbuka nilipowaona kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya wanyama, bei yao ilikuwa dola za Marekani 700 kwa kila mmoja ambazo ni sawa na zaidi ya shilingi za Tanzania milioni 1.8,” alisema Dennis Rödder, mtaalamu wa wanyama watambaao kutoka Leibniz Institute for the Analysis of Biodiversity Change nchini Ujerumani, katika mahojiano na Mongabay yaliyofanyika kwa njia ya video. “Nadhani ndani ya miaka mitatu au minne, spishi hii ilikuwa imeenea kote Ulaya. Ilikuwa ni rahisi kuinunua kutoka duka lolote la wanyama wa kufugwa.” Mijusi hawa wanaojulikana kisayansi kama (Lygodactylus williamsi) hukua hadi kufikia urefu wa sentimita 6–9 (takriban inchi 2.5–3.5). Wanapatikana tu katika maeneo mawili madogo ya misitu nchini Tanzania: Hifadhi ya Misitu ya Kimboza na Hifadhi ya Ruvu. Maeneo haya yaliyohifadhiwa yana ukubwa wa jumla ya kilomita za mraba 34 (takriban maili za mraba 13). Majike waliokomaa wana rangi ya kijani-kahawia inayofanana na majani ya miti wanayoishi, jambo linalowasaidia kujificha dhidi ya maadui. Hata hivyo, madume huwa na ngozi ya samawati ang’avu inayovutia sana. Rangi hii ni miongoni mwa rangi adimu zaidi kupatikana kiasili, na hutumika kuwavutia majike wakati wa uzazi. Mjusi mdogo wa rangi ya samawati (Lygodactylus williamsi). Picha: © Simon kupitia iNaturalist (CC&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2026 18:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/10161044/Meno-ya-tembo-2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1830</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Kupambana na ujangili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Sheria ya Mazingira, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mwasha. Akiwakilisha upande wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Florida Wenceslaus aliomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa kile alichoeleza kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika. Mshtakiwa, ambaye anaendelea kusota rumande, hakuwepo mahakamani leo kama ilivyokuwa wakati kesi hiyo ilipotajwa Mei 25, na pia hakuwa na mwakilishi. Hakimu Mwasha alikubali ombi la upande wa mashitaka na akaahirisha shauri hilo hadi Juni 23 mwaka huu, kesi itakapotajwa tena. Mshtakiwa Ra alipanda kizimbani kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa Mei mwaka huu. Shauri lilipotajwa baada ya siku 14, yaani Mei 25 mwaka huu, mshtakiwa huyo hakufikishwa mahakamani na badala yake shauri liliahirishwa bila yeye kuwepo. Kabla ya kuahirisha kesi hiyo, hakimu aliamuru hati ya kumfikisha mshtakiwa kortini itolewe ili kesi itakapotajwa Juni 9, 2026, mshtakiwa aletwe kortini. Hata hivyo leo mshtakiwa hakufikishwa kortini na hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa kwa nini mshatakiwa hakuwepo. Awali upande wa Jamhuri ulidai katika hati ya mashtaka kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali na kujihusisha na biashara hiyo bila kibali. Ilidaiwa kuwa Aprili 19, 2026 katika eneo la Hoteli ya Golden Tulip–Masaki,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 19:10:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09143738/EACOP-Main-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1826</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Mimea, Samaki, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa kutumia takwimu za ramani na makadirio ya thamani ya kiuchumi, ripoti ya Earth Insight, shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Marekani, inaonyesha kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 liko karibu na maeneo muhimu kwa maisha ya mamilioni ya watu na usalama wa maji, na pia sehemu ambazo hutumika kama njia za uhamaji wa wanyama. Kutokana na uchambuzi huo, ripoti hiyo inahitimisha kuwa ujenzi wa bomba hilo tayari umeathiri jamii na mazingira, na kwamba usafirishaji wa mafuta utaleta hatari zaidi za muda mrefu. EACOP ni mradi wa ubia kati ya  kampuni ya TotalEnergies yenye asilimia 62 ya hisa, serikali za Uganda na Tanzania kila moja ikiwa na asilimia 15, pamoja na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) yenye asilimia 8. EACOP itasafirisha mafuta yanayochimbwa kutoka vitalu viwili kwenye bonde la Ziwa Albert: Kingfisher, linalomilikiwa na CNOOC; na Tilenga, linalomilikiwa na TotalEnergies. Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) nchini Uganda. Picha kwa hisani ya Thomas Lewton. Kwa mujibu wa Earth Insight, mradi huo unakaribia kukamilika na mafuta ya kwanza yataanza kusafirishwa mapema mwaka 2026. “Linapita moja kwa moja katika maeneo ya viumbe walio hatarini kutoweka, na eneo muhimu zaidi ni la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 14:29:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Isack Dickson]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09125042/3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1810</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na Ziwa Manyara, na unaokatiza maeneo ya Babati, Monduli na Simanjiro, umeendelea kuwa kiunganishi muhimu cha mifumo ya ikolojia katika ukanda huo wenye utajiri mkubwa wa viumbe hai. Kwa miongo kadhaa umekuwa njia muhimu ya kupita kwa wanyamapori wanaohama kutoka eneo moja kwenda lingine. Wanyama aina ya pundamilia wakiwa katika ushoroba wa Kwakuchinja. Picha na Isack Dickson. Revocatus Meney, mtafiti kutoka TAWIRI, anasema ushoroba huo umekuwa ukipungua siku hadi siku kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu. Makazi, kilimo na mifugo vinaendelea kuubana mwaka hadi mwaka na kuufanya uwe finyu. Kwa mujibu wa tafiti za TAWIRI, miaka ya 1970, ushoroba wa Kwakuchinja ulikuwa na ukubwa unaofikia kilomita za mraba 600. Hata hivyo, Meney anasema kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu ikiwemo makazi, kilimo na matumizi mengine ya ardhi, eneo hilo limeendelea kupungua na kufikia takribani kilomita za mraba 274.45 kwa sasa. Kupungua huku kunamaanisha kuwa zaidi ya nusu ya eneo la awali la ushoroba limepotea ndani ya kipindi cha takribani miongo mitano. Meney anasema hakuna kiwango kimoja cha upana kinachotumika kwa ushoroba kwa sababu hutegemea aina ya wanyama wanaoutumia na mazingira husika. Hata hivyo, anasema kadri ushoroba unavyokuwa mpana na usio na vikwazo vya shughuli&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 13:12:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09111629/Screenshot-2026-06-09-141545.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia ya wenzao. Hata hivyo, licha ya jukumu lao kuu katika kulinda bayoanuwai na baadhi ya misitu muhimu zaidi ulimwenguni, wengi wanaendelea kufanya kazi wakiwa na usaidizi mdogo, mishahara midogo, na hali hatarishi sana. Kwa Emmanuel Bahati Lukoo, ukweli huu ni wa kibinafsi sana. Aliwahi kuwa mlinzi katika mbuga ya kitaifa ya Virunga ambapo kwa sasa ni afisa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Kahuzi-Biega, alinusurika kifo katika shambulizi la kushutukizia mnamo mwaka wa 2018 na kikundi cha wanamgambo wa jamii kinachojulikana kama Mai-Mai. Wenzake kadhaa waliuawa kwa kuviziwa. Alipigwa risasi, alijeruhiwa na kupata kiwewe cha kisaikolojia, na baadaye kufunguliwa mashitaka mbele ya mahakama ya kijeshi katika kesi iliyohusishwa na ulinzi wa hifadhi, angeweza kuondoka. Badala yake, Bahati alichagua kusimulia hadithi yake katika kitabu kiitwacho Conservation at the Cost of My Youth: The Survival of a Ranger, simulizi ghafi ya dhabihu, hofu, shinikizo za kisiasa, na mara nyingi hali halisi isiyoonekana inayowakabili walinzi wa misitu mashariki mwa DRC. Kwenye mahojiano ya ana kwa ana na Mongabay, Bahati anatafakari safari yake, shambulizi lililokaribia kumuua, kiwewe walichopata walinzi, migogoro kati ya uhifadhi na maisha ya jamii ya eneo hilo, na uingiliaji wa kisiasa unaotatiza ulinzi wa maeneo yaliyohifadhiwa. Zaidi ya hadithi ya kibinafsi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 15:48:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Benjamin Jumbe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03150618/Screenshot-2026-06-03-180555-768x498.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1759</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi ya jamii inayolenga kupunguza uharibifu wa misitu na kuongeza ufahamu wa masuala ya mazingira, pamoja na timu ya maskauti wa jamii 18 katika upande wa Kenya wa mlima, sehemu ya Mradi wa Tembo wa Mlima Elgon unaotekelezwa na Shirika la Wanyamapori la Afrika Mashariki. Mwenyekiti wa wakfu wa MEF, Chris Powles, aliiambia Mongabay kwamba mnamo mwaka 2022, maskauti walifuatilia tembo wanne wakivuka mto Suam, ambao unaashiria mpaka kati ya nchi hizo mbili. Picha za video zilizorekodiwa kwa ndege isiyo na rubani zikionyesha tembo upande wa Uganda wa Mlima Elgon. Picha kwa hisani ya UWA. Katika mahojiano kupitia barua pepe, Powles alisema sababu kadhaa zinaweza kuelezea kurudi kwa tembo, ingawa haiwezekani kusema kwa uhakika ni nini kiliwachochea kurejea katika eneo hilo. &#8220;[Hizi] ni pamoja na ongezeko la idadi ya tembo upande wa Kenya, kuongezeka kwa shinikizo la binadamu kwa upande wa Kenya, usalama wanaoupata wakiwa upande wa Uganda, ambako eneo hilo lote liko ndani ya mbuga ya taifa, tofauti na upande wa Kenya,&#8221; aliandika. &#8220;Na, labda, tembo walio hai tangu wakati wengine wao waliuawa nchini Uganda sasa wamekufa kawaida na hivyo huenda kumbukumbu ya hatari zilizowakabili nchini Uganda imefifia kadri vizazi vilivyobadilika.&#8221; Mwishoni mwa miaka ya 1970 na mwanzoni mwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mfumo wa malipo ya fidia kwa wananchi walioathirika na matukio ya uharibifu wa wanyamapori waboreshwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/#respond</comments>
					<pubDate>15 Mei 2026 14:49:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/15142508/Baadhi-ya-wanyama-wanaopatikana-katika-mbuga-nchini-Tanzania.-Picha-kutoka-tovuti-ya-TANAPA-768x500.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1629</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bustani za wanyama, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Wenyeji wa Asili, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha mfumo wa Problem Animals Information System (PAIS), mahsusi ulioundwa kusimamia taarifa za matukio ya wanyamapori wakali pamoja na kuratibu na kuwezesha ulipaji wa vifuta jasho/machozi kwa wananchi wanaoathirika na matukio hayo. Hayo yamesemwa na Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/" data-wpel-link="internal">Mfumo wa malipo ya fidia kwa wananchi walioathirika na matukio ya uharibifu wa wanyamapori waboreshwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha mfumo wa Problem Animals Information System (PAIS), mahsusi ulioundwa kusimamia taarifa za matukio ya wanyamapori wakali pamoja na kuratibu na kuwezesha ulipaji wa vifuta jasho/machozi kwa wananchi wanaoathirika na matukio hayo. Hayo yamesemwa na Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, katika kikao cha bajeti kinachoendelea makao makuu ya nchi, Dodoma. Amesema mfumo huo wa kisasa umerahisisha ukusanyaji, uwasilishwaji wa taarifa sahihi na kuepuka udanganyifu. Umeboresha pia uchakataji na utunzaji wa taarifa za matukio ya uharibifu wa wanyamapori wakali na waharibifu. Vilevile, mfumo umerahisisha malipo ya kifuta jasho na machozi kwa wananchi waliopata madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu. “Kwa sasa taratibu za malipo zinachukua siku saba hadi 14 tofauti na taratibu za awali ambapo malipo yalikuwa yakichukua miezi sita hadi 12,” amesema. Sambamba na hilo, waziri amesema mfumo umeongeza uwazi na uwajibikaji kwani unawezesha kufuatilia kila muamala. Kwa mujibu wa Waziri, hadi kufikia Aprili mwaka 2026, Wizara imelipa kiasi cha TSh8,149,314,750 ($3,134,351) ikiwa ni kifuta jasho na machozi kwa wananchi 22,696 waliopatwa na madhara ya wanyamapori katika Halmashauri za Wilaya 81 ikilinganishwa na 43 katika kipindi kama hiki cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 ambapo jumla ya TSh4,604,909,750 ($1,771,119) zililipwa kwa wananchi 16,939. Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, katika kikao cha bajeti kinachoendelea makao makuu ya nchi, Dodoma. Taarifa hiyo ya Kijazi kuhusu maboresho kwenye utaratibu wa malipo ya fidia huenda ikawa mkombozi kwa wananchi ambao wamekuwa wakitumia muda mrefu kufuatilia malipo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>15 Mei 2026 10:00:23 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/13194410/IMG-20260513-WA0002-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1602</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mazingira, Migogoro, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na tai na ndege kubwa za kitalii, lakini leo, kuna mlio mpya wa helikopta unaoashiria mabadiliko ya zama. Hapa ndipo ilipoanzia safari ya Wilson Sairowua &#8216;Tate&#8217;; kijana ambaye mikono yake, iliyozoea kushika fimbo ya uchungaji huku akitembea miguu peku katika mfumo huu wa ekolojia, sasa imeshika usukani wa teknolojia ya kisasa. Wilson si rubani tu, ni daraja la amani linalotumia mbingu kulinda urithi wa ardhi ambapo hatima ya binadamu na tembo zimeunganishwa. Rubani Wilson Sairowua akiwa pamoja na askari wa MEP katika makao makuu ya MEP kwenye eneo la hifadhi la Lemek wakati wa mafunzo ya matumizi ya droni. Picha kwa hisani ya MEP. Kabla hajavaa jaketi la rubani lenye nembo ya shirika la Mara Elephant Project (MEP), au kushika usukani wa helikopta, Wilson alikuwa kijana wa kawaida wa Kimaasai, mchungaji mdogo, mara nyingi akitembea miguu peku, akifuatilia mifugo chini ya jua kali la mchana. Alijua kila mti na kila njia ya siri ya maji, na alikuwa hodari wa kutafsiri nyayo za wanyamapori. Vazi lake lilikuwa shuka na kaptula. Suruali ya kwanza aliivaa akiwa na umri wa miaka 14, alipoingia shule ya upili. “Tulikuwa tunatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Wengine wetu hata hatukuwa na viatu. Nikiwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/#respond</comments>
					<pubDate>12 Mei 2026 04:00:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika VyawahareMary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11220722/671089-DSC_0303-5f9eed-original-1777544684-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1589</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Ubunifu wa Kijani, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya Mpesa Foundation Academy, walitengeneza mfumo huo, HewaSafi, unaomaanisha “hewa ambayo ni safi” kwa Kiswahili, baada ya kuona marafiki na familia wakiugua maradhi yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa. Shirika la Earth Foundation, lenye makao yake makuu nchini Uswizi, linatoa Tuzo ya Dunia, ambayo sasa iko katika mwaka wake wa tano, na inatambua vijana wenye umri wa miaka 13 hadi 19 wanaofanya kazi katika kutatua changamoto za mazingira. Timu ya HewaSafi sasa inawania tuzo ya kimataifa, ambayo upigaji kura kwa umma utafunguliwa tarehe 18 Mei, na kufungwa mnamo Mei 27. Mshindi wa toleo la kimataifa atatangazwa tarehe 29 Mei. &#8220;Tatizo la uchafuzi wa hewa lilikuwa la kibinafsi sana kwetu, na ndiyo maana tukaanza kufikiria kupata suluhu,&#8221; Kariuki aliiambia Mongabay. &#8220;Ilikuwa hamasa kubwa kabla ya kuwa mradi.&#8221; Kariuki, ambaye alikulia katika eneo lenye viwanda vingi katika Kaunti ya Nakuru nchini Kenya, alipata ugonjwa sugu wa mapafu akiwa na umri wa miaka 10 ambao bado unamhitaji kutumia dawa kila wiki. Onsarigo, ambaye alikulia magharibi mwa Kenya, alishuhudia vifo na magonjwa mabaya yanayohusiana na hewa chafu. Takwimu kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa uchafuzi wa hewa husababisha vifo vya mapema milioni 4.4 ulimwenguni kila mwaka. Moshi wa magari ni chanzo kikuu cha uchafuzi wa mazingira katika maeneo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/#respond</comments>
					<pubDate>10 Mei 2026 21:34:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/08205611/Screenshot-2026-05-08-235542-768x500.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1539</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, na  Kusini mwa Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Biashara ya Wanyamapori ya China, Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mamalia, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu kwa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utafiti, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini zao huku wakinufaika kutokana na mauzo ya mtandaoni ya spishi za wanyama wanaolindwa huku wanyama hawa wakipungua porini. &#8220;Ni soko kubwa zaidi la wanyamapori,&#8221; alisema mtafiti wa biashara ya wanyamapori Chris Shepherd kutoka Kituo cha Biolojia Anuwai. &#8220;Ni rahisi, unaweza kufanya kazi bila kujulikana ukiwa nyumbani kwako. Hakuna gharama za kuanzisha duka.&#8221; Biashara ya mtandaoni katika bidhaa haramu za wanyamapori inaendelea kukua, ikihusisha spishi zaidi na jiografia pana. Ni tasnia haramu inayoendeshwa na mitandao ya uhalifu iliyopangwa vizuri, na ni vigumu kushtaki. Kukamata wahalifu mtandaoni ni changamoto sana. &#8220;Masoko ya wanyamapori yamehamia kutoka maeneo halisi hadi maeneo ya mitandaoni, na hiyo inaakisi mwelekeo mpana zaidi wa uchumi wa dunia,&#8221; alisema Simone Haysom, mkurugenzi wa programu za uhalifu wa kimazingira katika shirika lenye makao yake makuu Uswizi la Global Initiative Against Transnational Organised Crime. Katika ripoti ya hivi karibuni, Haysom na mwenzake Russell Gray walichanganua data ya biashara ya wanyamapori mtandaoni kuanzia mwezi wa Aprili 2024 hadi mwezi Machi 2026. Waliangazia mataifa 10 katika mabara matatu, mahali ambapo uhalifu wa kimazingira na matumizi ya intaneti ni mkubwa, na kuyafanya kuwa mazingira yanayochochea biashara ya wanyamapori mtandaoni. Walipata bidhaa 266,535 za wanyamapori zilizochapishwa kwenye masoko 61 ya mitandaoni, yenye thamani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>GLF: Nyanda za malisho na wafugaji ni raslimali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na si tatizo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/#respond</comments>
					<pubDate>08 Mei 2026 20:33:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/10203241/A-participant-asks-questions-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1530</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Kusini mwa Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Fedha za Uhifadhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Jinsia na Uhifadhi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Teknolojia na Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Baada ya mkutano wa siku mbili wa kujadili huduma za mifumo ya ikolojia ya nyanda za malisho na jamii za wafugaji wa kuhamahama, Mkutano wa nane wa jukwaa la Global Landscapes Forum umehitimishwa jijini Nairobi kwa tamko lililosisitiza umuhimu wa jamii ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikionekana kama kikwazo kwa maendeleo. Katika mkutano huo uliofanyika katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/" data-wpel-link="internal">GLF: Nyanda za malisho na wafugaji ni raslimali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na si tatizo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Baada ya mkutano wa siku mbili wa kujadili huduma za mifumo ya ikolojia ya nyanda za malisho na jamii za wafugaji wa kuhamahama, Mkutano wa nane wa jukwaa la Global Landscapes Forum umehitimishwa jijini Nairobi kwa tamko lililosisitiza umuhimu wa jamii ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikionekana kama kikwazo kwa maendeleo. Katika mkutano huo uliofanyika katika kituo cha CIFOR-ICRAF na kuhudhuriwa na maafisa wa serikali, wanasayansi pamoja na wawakilishi wa jamii za asili kutoka nchi 135, mjadala ulijikita katika mifumo ya ikolojia inayosaidia bioanuwai, usalama wa chakula, maisha ya watu, utamaduni, uhifadhi wa kaboni na huduma nyingine za kiikolojia bila kuvuruga maisha endelevu na tamaduni za jamii za wafugaji, badala ya kuweka msisitizo kwenye uwekezaji unaoshinikizwa na serikali kwa lengo la kupata faida. “Tunapaswa kujiuliza: Maendeleo haya yanafanywa kwa ajili ya nani? Je, jamii zinahusishwa katika maamuzi kuhusu uwekezaji unaofanywa kwenye ardhi yao? Na ni kwa manufaa ya nani miradi hii ya kibiashara inayowasilishwa kana kwamba ni juhudi za kutoa ajira na fursa nyingine kwa wakazi? Sauti zao zina umuhimu,” alisema Tahira Mohamed Shariff kutoka Jameel Observatory for Food Security Early Action siku ya kwanza ya mkutano huo. Baadhi ya waliohudhuria kongamano Nairobi, Kenya. Picha na GLF. Monicah Yator, Wakili na Mwanzilishi wa Indigenous Women and Girls Initiative, alisema kuwa ufugaji wa kuhamahama si shughuli ya mifugo pekee. “Ni mfumo wa maisha, chakula na utamaduni. Kuna sera zinazowalinda wafugaji. Sasa wafugaji wanafahamu kwamba ardhi yao inaweza kubadilishiwa matumizi,” alisema, akiongeza kuwa maarifa ya asili bado ni muhimu na yenye mchango mkubwa katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/#respond</comments>
					<pubDate>04 Mei 2026 13:28:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/04145740/Screenshot-2026-05-04-160903.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1493</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi, Asia, Asia ya Kusini-mashariki, Guinea, Indonesia, Mali, Msumbiji, Senegal, Singapore, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Magonjwa, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Ndege, Ugonjwa wa Kuambukiza wa Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano ya uimbaji wa hali ya juu. Wafugaji wa ndege aina ya vipanga na wawindaji wa michezo hukamata au kuua ndege wa porini. Matambiko ya imani za jadi katika Afrika Magharibi hujumuisha viwiliwili vya tai. Wanunuzi kutoka Marekani ya Kaskazini hutafuta hondohondo na ndege mvumaji waliokufa kama mapambo ya nyumbani. Orodha inaendelea. Biashara hii kubwa inatisha zaidi ya spishi 200 za ndege kutoweka. Sasa, huku masoko ya mtandaoni yakiongezeka, wateja wanaweza kuagiza ndege kwa kubonyeza simu zao za mkononi kutoka mahali popote katika sayari. Kusafirisha ndege kote ulimwenguni pia husambaza magonjwa hatari, kama vile homa ya ndege na virusi vwa circovirus, na wakati ndege wasio wa asili wanapotoroka au kuachiliwa, wanaweza kuongezeka kuwashinda spishi za asili. &#8220;Kuna ukosefu wa ufahamu na kuthamini ukubwa wa biashara hii, na umakini mchache sana juu ya athari ambazo hii inaweza kuwa nayo kwa wakazi wa porini au hatari za kuenea kwa viumbe vamizi na magonjwa ya kuambukiza,&#8221; Rowan Martin ni mkurugenzi wa biashara ya ndege katika shirika lisilo la faida la World Parrot Trust. &#8220;Ikiwa watu hawajui kwamba hili linafanyika, basi tutawezaje kupunguza hatari zinazohusiana nayo?&#8221; Katika kujaribu kuelewa ukubwa wa biashara ya ndege hai, Martin na wenzake walitumia hifadhidata ya Umoja wa Mataifa ya Comtrade (UN Comtrade), hifadhidata inayojumlisha taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yawapokea Swala wa milimani adimu waliorudishwa kutoka bustani za wanyama Ulaya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/#respond</comments>
					<pubDate>01 Mei 2026 10:52:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/01105311/Swala-wa-milimani-aliye-hatarini-kutoweka-akiwa-kwenye-Bustani-ya-Chester-Cheshire-Uingereza.-Picha-kwa-hisani-ya-Chester-Zoo-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1481</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Misitu, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii Kenya imepokea kundi la swala wa milimani walio katika hatari kubwa ya kutoweka, wakitokea Jamhuri ya Czech ambako walikuwa wakihifadhiwa chini ya usimamizi wa Bustani ya Wanyama ya Zoo Dvůr Králové. Urejeshaji wa swala hao wanne dume, waliokulia katika bustani mbalimbali za wanyama chini ya mpango wa uhifadhi nchini Uingereza, ni hatua muhimu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/" data-wpel-link="internal">Kenya yawapokea Swala wa milimani adimu waliorudishwa kutoka bustani za wanyama Ulaya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii Kenya imepokea kundi la swala wa milimani walio katika hatari kubwa ya kutoweka, wakitokea Jamhuri ya Czech ambako walikuwa wakihifadhiwa chini ya usimamizi wa Bustani ya Wanyama ya Zoo Dvůr Králové. Urejeshaji wa swala hao wanne dume, waliokulia katika bustani mbalimbali za wanyama chini ya mpango wa uhifadhi nchini Uingereza, ni hatua muhimu katika juhudi za Kenya kurejesha wanyama ambao kiasili wana nguvu na hupenda kuzunguka milimani kwa uhuru katika makazi yao ya asili. Hatua hii pia inaendana na mkakati wa kitaifa wa urejeshaji wa mwaka 2019–2023 unaolenga kuokoa spishi hiyo iliyokuwa hatarini kutoweka, juhudi ambazo zimeendelea hata miaka kadhaa baadaye. Swala hao watahifadhiwa katika Kituo cha Uhifadhi wa Wanyamapori cha Mount Kenya (MKWC), kilichopo katika maeneo ya milimani ya Laikipia. Uhamisho huo uliongozwa na wataalamu kutoka Bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa ushirikiano na Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) pamoja na Chama cha Ulaya cha Bustani za Wanyama na Hifadhi za Majini. Akizungumza wakati wa kupokea swala hao waliowasili kwa ndege ya mizigo ya KLM katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Waziri Mkuu Msaidizi na Waziri wa Mambo ya Nje na Masuala ya Diaspora, Musalia Mudavadi, alisema kuwa simulizi ya swala wa milimani inaakisi hali pana ya mazingira nchini humo. Alisema: “Waliwahi kustawi katika misitu ya milimani, kuanzia Aberdares hadi Mlima Kenya, Mau na Eburu, lakini sasa spishi hii ya kipekee inakabiliwa na ukweli mchungu wa kuwa katika hatari ya kutoweka kabisa.” Wadau wengine kadhaa waliokuwepo ni pamoja na Waziri&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/#respond</comments>
					<pubDate>21 Aprili 2026 00:42:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20151506/Screenshot-2026-04-20-165755-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1399</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kaskazini mwa Kenya, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni mzunguko usiokwisha wa kutafuta malisho na maji. Lakini ndani ya moyo wa jangwa hili, kumeibuka hadithi inayopinga mantiki ya asili &#8211; ya upendo uliopitiliza, hatari iliyojificha, na mipaka inayofifia kati ya binadamu na mnyama mwitu mwenye kasi kubwa. Ni hadithi ya Bishara Abdirahman Omar, mama wa watoto tisa, ambaye kwa zaidi ya miaka miwili alifanya jambo ambalo wengi wangeliona kama hukumu ya kifo. Mama huyu aliishi na duma ndani ya nyumba kama sehemu ya familia yake. Bishara anakumbuka siku hiyo kwa uwazi kabisa, kana kwamba ilitokea jana. Ilikuwa ni asubuhi yenye joto kali, na yeye alikuwa akitembea porini kutafuta kuni na kuangalia mifugo yake. Katika kichaka kimoja cha miiba, alisikia sauti dhaifu; kilio kidogo kilichofanana na kile cha mtoto wa paka aliyeishiwa nguvu. Aliposogea, alimkuta mtoto wa duma, akiwa mdogo kiasi cha kutoshea kwenye viganja vyake, macho yake yakiwa bado na ukungu wa upofu wa utotoni. “Alikuwa hana msaada kabisa. Nilimwangalia, nikatazama huku na huko nikitarajia kumuona mama yake, lakini hapakuwa na dalili yoyote. Alikuwa ameachwa peke yake kufa kwa njaa au kuliwa na fisi,” Bishara alisimulia, huku akitazama upeo wa macho. Kwa Bishara, hakuona mnyama hatari, bali aliona kiumbe aliyehitaji maziwa na joto. Bila&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 15:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Gerald Ahairwe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20185806/IMG_5205-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1409</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Maji, Mamalia, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchimbaji wa Mafuta, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru wa kuandamana. Saa nne asubuhi, ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Buganda Road, Katikati mwa jiji la Kampala nchini Uganda, wanaharakati wa mazingira na wanafunzi wanane walifikishwa kizimbani. Wanafunzi hao wanatoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini Uganda, na wamekuwa gerezani tangu Agosti 1, 2025, baada ya kukamatwa wakiandamana kupinga mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP. Nje ya Mahakama, kulikuwa na rasharasha za mvua. Wasiwasi ulitanda miongoni mwa wanafunzi wa vuguvugu la “Students Against EACOP” waliokuwa wamefika pale ili kuhudhuria hukumu ya Mahakama hiyo dhidi ya wenzao. Hakimu Mkazi alitangaza kuahirishwa kwa hukumu yao hadi saa nane mchana. Lakini nyakati za chakula cha mchana, kabla ya saa nane, wanafunzi walio nje waliambiwa kwamba wenzao wanane wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma (common nuisance). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Sylvia Muwonge katika chumba chake kwenye Mahakama ya Buganda Road. Mawakili, umma au hata waandishi wa habari hawakuhudhuria. Upande wa utetezi umepinga hukumu hiyo, ukisema kuwa wanafunzi hao wamenyimwa haki ya kupewa dhamana, na vile vile kunyimwa nafasi ya kuridhisha kujitetea. Kato Tumusiime, wakili wa wanaharakati hao, anaelekeza kidole cha lawama kwa upendeleo uliokuwepo katika kesi hiyo tangu mwanzo. “Hukumu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhasama waikumba jamii adimu ya sokwe katika mbuga ya kitaifa ya Uganda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/#respond</comments>
					<pubDate>17 Aprili 2026 07:28:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Keith Anthony Fabro]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/23073935/Screenshot-2026-04-23-103518-768x507.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1433</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bustani za wanyama, Ikolojia, Magonjwa ya Zoonotiki, Mazingira, Misitu, Sokwe, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jamii ya sokwe katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale nchini Uganda iligawanyika katika makundi hasimu na kushambulia washirika wa zamani, katika kile watafiti wanakifafanua kuwa ni &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya nadra vya sokwe. Utafiti huo mpya, uliochapishwa kwenye jarida la Science, unaangazia uchunguzi wa takriban miongo mitatu kwenye tovuti ya utafiti wa sokwe wa Ngogo, ukiongozwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/" data-wpel-link="internal">Uhasama waikumba jamii adimu ya sokwe katika mbuga ya kitaifa ya Uganda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jamii ya sokwe katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale nchini Uganda iligawanyika katika makundi hasimu na kushambulia washirika wa zamani, katika kile watafiti wanakifafanua kuwa ni &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya nadra vya sokwe. Utafiti huo mpya, uliochapishwa kwenye jarida la Science, unaangazia uchunguzi wa takriban miongo mitatu kwenye tovuti ya utafiti wa sokwe wa Ngogo, ukiongozwa na mtaalamu wa wanyama Aaron A. Sandel wa Chuo Kikuu cha Texas huko Austin, nchini Marekani. Yeye na wenzake wanasema hili ni tukio la nadra linaloweza kutokea mara moja tu kila baada ya miaka 500. Limezingatiwa mara moja tu awali na wanadamu. Kabla ya mgawanyiko huo, jamii ya Ngogo ilikuwa kubwa isivyo kawaida, ikiwa na takriban sokwe 150 hadi 200 (Pan troglodytes), na kuifanya kuwa mojawapo ya makundi makubwa zaidi ya sokwe kuwahi kurekodiwa porini. Baada ya mpasuko huo, jamii iligawanyika katika makundi mawili, ambayo watafiti wameyaita makundi ya Kati na Magharibi, yaliyopewa jina la sehemu za misitu walimoishi. Kabla ya sokwe wa Ngogo kugawanywa katika makundi mawili, ilikuwa mojawapo ya makundi makubwa zaidi kuwahi kurekodiwa: kati ya wanyama 150 &#8211; 200. Picha na Aaron Sandel. Kati ya mwaka 2018 na mwaka 2024, kundi la sokwe wa Magharibi lilifanya mashambulizi 24 kwenye kundi la sokwe wa Kati, na kuua angalau wanaume wazima saba na watoto wachanga 17. Sandel aliiarifu Mongabay kuwa mzozo huo bado unaendelea na huenda ukawa na matokeo ya kudumu kwa idadi ya sokwe. &#8220;Kundi la sokwe wa Kati liko hatarini &#8211; wamekuwa na ongezeko kubwa la vifo,&#8221; Sandel alisema. &#8220;Swali kuu ni: Je,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 19:32:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/14182846/mawe2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1351</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Sera za Mazingira, Uchafuzi, Uharibifu wa Makazi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), bado uchimbaji holela wa mawe umeendelea kuwa jinamizi linalowaumiza wakazi jijini Mwanza. Akizungumzia sababu za hali hiyo kuendelea, Laurent Kitogo, Afisa wa Mazingira kutoka Environmental Management and Economic Development Organization (EMEDO), anataja udhaifu katika usimamizi pamoja na utekelezaji wa sheria kuwa kikwazo kikubwa. “Sheria ni eneo moja na usimamizi wake ni jambo jingine. Tunazo mamlaka kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na maeneo yote ambayo watu wanaishi. Sheria imeelekeza kabisa kwamba kutakuwa na maafisa wa mazingira kuanzia ngazi ya mtaa, lakini ukiangalia kwa uhalisia ulivyo, utaona maafisa wa mazingira wanaanzia ngazi ya halmashauri. Huwezi kumkuta afisa wa mazingira katika ngazi ya kata,” anasema. David Joseph, Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira jijini Mwanza, anasema kuwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hakuna eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa mawe, na kwamba wanaochimba, baadhi wanakuwa wanasawazisha viwanja vyao kutokana na kuwa na asili ya miamba, au ni wavamizi ambao wameona hiyo kama fursa ya ujasiriamali. “Watu wanachimba mawe katika miktadha kuu miwili. Moja, asili ya Mwanza ni milima, na sehemu nyingi zina mawe. Hata kama ni tambarare, utakuta kuna mawe…kwa hiyo watu wengine wanachimba yale mawe ili kusawazisha viwanja vyao…hayo mawe&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>