<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=uchafuzi&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/uchafuzi/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Tue, 01 Sep 2026 14:42:19 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Kampuni ya Kichina ya uchimbaji wa mchanga wenye madini mazito yahusishwa na uharibifu wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>31 Agosti 2026 14:18:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika Vyawahare]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/31140708/Screenshot-2026-08-31-170449-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2668</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Mashariki, na  Msumbiji]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Jukumu la Kampuni Katika Uhifadhi, Maji, Makampuni Yanayokiuka Sheria za Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Kitropiki, na  Wajibu wa Kampuni]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ZAMBEZI, Msumbiji &#8211; Uchunguzi wa Mongabay umebaini kuwa shughuli za uchimbaji wa mchanga kando ya pwani ya Mkoa wa Zambezia, katikati mwa Msumbiji, imeharibu mamia ya hekta za misitu ya mikoko katika miaka michache tu. Eneo hilo liko chini ya leseni ya kampuni ya Mozambique Heavy Sand Company VIII, ambayo inamilikiwa kwa sehemu na Jinan Yuxiao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Kampuni ya Kichina ya uchimbaji wa mchanga wenye madini mazito yahusishwa na uharibifu wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ZAMBEZI, Msumbiji &#8211; Uchunguzi wa Mongabay umebaini kuwa shughuli za uchimbaji wa mchanga kando ya pwani ya Mkoa wa Zambezia, katikati mwa Msumbiji, imeharibu mamia ya hekta za misitu ya mikoko katika miaka michache tu. Eneo hilo liko chini ya leseni ya kampuni ya Mozambique Heavy Sand Company VIII, ambayo inamilikiwa kwa sehemu na Jinan Yuxiao Group, kampuni ya uchimbaji madini ya China yenye ushawishi mkubwa, inayodai kumiliki zaidi ya hekta 500,000 (ekari milioni 1.24) za ardhi kwa ajili ya shughuli za uchimbaji nchini Msumbiji. Maeneo hayo ya uchimbaji hulenga zaidi mchanga wenye madini mazito, ambayo huwa na madini yenye titani, hasa ilmeniti na rutaili, yanayotumika katika utengenezaji wa bidhaa mbalimbali, kuanzia rangi na plastiki hadi krimu za kujikinga dhidi ya jua. Wanaharakati wa mazingira wanatoa tahadhari kuhusu hatari zinazotokana na uchimbaji wa madini mazito kando ya pwani ya Msumbiji, na vyombo vya habari vya ndani vimeandika kuhusu tishio linaloongezeka kutokana na shughuli hiyo. &#8220;Maeneo yetu yote ya pwani yana miradi hii ya mchanga wenye madini mazito,&#8221; alisema Fatima Mimbire, mtetezi wa uwazi katika sekta ya madini nchini Msumbiji katika mahojiano na Mongabay. Aliongeza kwamba kampuni nyingi zinazochimba mchanga huo wenye madini nchini Msumbiji ni za Kichina. &#8220;Kampuni hizi zinasababisha uharibifu bila kujali mazingira wala watu wanaoathiriwa.&#8221; Global Mangrove Watch (GMW) ni jukwaa lililoundwa kufuatilia maeneo ambayo mikoko inarejea na yale ambayo inapotea, ndilo lililotoa tahadhari ya kwanza kuhusu upotevu wa mikoko katika wilaya ya Chinde mkoani Zambezia. Lammert Hilarides, mtaalamu wa uchunguzi wa Dunia kwa kutumia picha za setlaiti kutoka shirika la Wetlands International (WI),&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>22 Agosti 2026 00:16:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/21145204/Screenshot-2026-08-21-175140-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2561</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Mito, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, na  Uhalifu wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 karibu na Mto Ngong na vijito vyake, na idadi ya watu inayokadiriwa kufikia 700,000. Sehemu ya Katwekera, ndani ya Kibera, Nairobi. Picha na Mary Mwendwa, Mongabay. Katika baadhi ya maeneo ya makazi hayo, serikali ya Kenya inaendelea na ujenzi wa nyumba za bei nafuu. Mwonekano wa Kibera umeanza kubadilika. Hata hivyo, katika Gatwekera, mojawapo ya vijiji 14 vya Kibera, wakazi wa kipato cha chini wanategemea kazi za muda na biashara ndogo ndogo kando ya njia nyembamba. Asubuhi hiyo ya Jumapili, muziki mkubwa unaotoka madukani na majumbani unachanganyika na mlio wa pikipiki zinazobeba abiria na mizigo kwenye njia hizo. Licha ya msongamano huo, watu wanaonekana kuwa waangalifu. Baadhi yao walionekana kuelekea ibadani. Katikati ya msongamano huo, vijana watatu wanasukuma mkokoteni uliojaa mifuko myeusi ya plastiki iliyojaa taka, wakiteremka mteremko unaopelekea daraja la miguu ndani ya Gatwekera. Nyumba ya mwisho waliyotembelea ilikuwa ya Syprose Akinyi, iliyoko takriban mita 100 kutoka walipokuwa. Wanaelekea eneo la kukusanyia taka, ambapo taka hizo zinapangwa na baadhi yake kuuzwa kwa ajili ya kuchakatwa. Taka zilizobaki husafirishwa hadi dampo la Dandora, lililo umbali wa takriban kilomita 10, kwa kutumia magari ya serikali ya kaunti. Wanachama wa West Family Group wakipanga taka zilizokusanywa kutoka majumbani huko Gatwekera. Vijana hao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakazi bado wanakabili athari za mgodi uliochafua Mto Kafue, nchini Zambia mwaka 2025</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/wakazi-bado-wanakabili-athari-za-mgodi-uliochafua-mto-kafue-nchini-zambia-mwaka-2025/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/wakazi-bado-wanakabili-athari-za-mgodi-uliochafua-mto-kafue-nchini-zambia-mwaka-2025/#respond</comments>
					<pubDate>18 Agosti 2026 11:37:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/18111439/Screenshot-2026-08-18-141220-768x439.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2525</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika na .Zambia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Makampuni Yanayokiuka Sheria za Mazingira, Mashirika Yanayokiuka Kanuni za Mazingira, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Mifumo ya Ikolojia, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mimea, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Ufujaji wa Mafuta, na  Uhalifu wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwaka mmoja na nusu baada ya kubomoka kwa bwawa la kuhifadhia mabaki ya madini katika Mkoa wa Copperbelt nchini Zambia, wakazi bado wanakabili athari za kimazingira na kibinadamu za kumwagika kwa taka zenye sumu, wanachama wa asasi za kiraia wameiambia Mongabay. Bwawa hilo, ambalo hutumika kuhifadhi taka za madini na linamilikiwa na kampuni ya China [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/wakazi-bado-wanakabili-athari-za-mgodi-uliochafua-mto-kafue-nchini-zambia-mwaka-2025/" data-wpel-link="internal">Wakazi bado wanakabili athari za mgodi uliochafua Mto Kafue, nchini Zambia mwaka 2025</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwaka mmoja na nusu baada ya kubomoka kwa bwawa la kuhifadhia mabaki ya madini katika Mkoa wa Copperbelt nchini Zambia, wakazi bado wanakabili athari za kimazingira na kibinadamu za kumwagika kwa taka zenye sumu, wanachama wa asasi za kiraia wameiambia Mongabay. Bwawa hilo, ambalo hutumika kuhifadhi taka za madini na linamilikiwa na kampuni ya China ya uchimbaji shaba, Sino-Metals Leach Zambia, lilipasuka tarehe 18 Februari 2025, katika mji wa Chambishi kaskazini-kati mwa Zambia. Lilitoa mamilioni ya lita za taka za madini zenye asidi kwenye mifumo ya maji iliyounganishwa na Mto Kafue. Ukiwa na urefu wa kilomita 1,576 (maili 979), Kafue ndiyo mto mrefu zaidi ulio ndani kabisa ya Zambia na ni tegemeo muhimu la maisha ya mamilioni ya watu nchini humo. Utafiti uliofanywa na watafiti wa Chuo Kikuu cha Copperbelt nchini Zambia na kuchapishwa katika Jarida la Journal of Hazardous Materials Advances mnamo Mei 2026 ni tathmini ya kwanza huru ya kisayansi ya athari za ikolojia za tukio hilo. Watafiti waligundua kuharibika kwa ubora wa maji, viwango vya juu vya metali nzito katika maji, samaki, mashapo na malisho, na ushahidi kwamba vitu vyenye sumu vilikuwa vimeingia kwenye mnyororo wa chakula. Mfumo mpana wa Mto Kafue ni chanzo cha maji kwa takriban nusu ya wakazi wa Zambia. Mto huo hutiririka hadi kwenye Mto Zambezi na kuhifadhi mifumo ya ikolojia ya ardhioevu yenye viumbe hai wengi, ikiwemo Kinamasi cha Lukanga na tambarare za Kafue Flats. Kwa sababu ya utafiti huo, wanasayansi walikusanya sampuli za maji kutoka maeneo matano katika eneo lililoathiriwa na sampuli moja katika eneo lisiloathiriwa lililotumiwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/wakazi-bado-wanakabili-athari-za-mgodi-uliochafua-mto-kafue-nchini-zambia-mwaka-2025/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/wakazi-bado-wanakabili-athari-za-mgodi-uliochafua-mto-kafue-nchini-zambia-mwaka-2025/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/#respond</comments>
					<pubDate>04 Agosti 2026 09:15:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04091305/Screenshot-2026-08-04-121218-768x440.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2324</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Maji, Maji ya kunywa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Nishati, Samaki, Samaki wa Maji safi, Shida ya Maji, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai 24, 2026, maafisa wakiwemo wawakilishi wa Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) walikuwa wakiendesha mkutano wa mashauriano ya umma mjini Bondo ndipo msukosuko ulipoanza. Dickens Ochieng’, wakili na mwanaharakati wa kijamii aliyehudhuria mkutano huo, aliiambia Mongabay kwa simu kuwa wamiliki wa ardhi walioalikwa kwenye mkutano huo wakisema &#8220;Wadagi,&#8221; neno la Kidholuo linalomaanisha &#8220;tunakataa,&#8220; kuonyesha upinzani wao dhidi ya mradi wa nyuklia. &#8220;Kisha afisa mmoja wa polisi aliyekuwa akilinda mashirika ya serikali alitumia silaha yake na kumjeruhi mtu mmoja kwa risasi, na mkutano ukageuka msukosuko papo hapo,&#8221; alisema Ochieng’. Katika siku zilizofuata, watu 17 walikamatwa na kufungwa. Hati rasmi iliyopitiwa na Mongabay inaonyesha kwamba watuhumiwa hao wanachunguzwa kwa tuhuma za shambulio na makosa chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya Kenya (Prevention of Terrorism Act). Ochieng’, ambaye amechukua jukumu la kuwatetea kisheria, alisema &#8220;kuna ukandamizaji mkubwa unaofanywa na serikali dhidi ya wanaopinga mradi huu.&#8221; &#8220;Kama wakili, ninaendelea kuiambia jamii kwamba lazima wasimame imara, kwa sababu tuhuma za ugaidi hazina uhusiano wowote na tukio lililotokea,&#8221; alisema. &#8220;Zinakusudiwa kuwatisha na kuwanyamazisha, si kuhakikisha haki inatendeka.&#8221; Hadi sasa, watuhumiwa 15 kati ya 17 wameachiwa huru baada ya wanajamii kukusanya pesa kupitia michango ya umma ili kulipia dhamana zao, zilizowekwa kati ya KSh15,000 na KSh180,000 ($116 hadi $1,391). &#8220;Katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 13:35:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Claire Asher]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/03130229/Screenshot-2026-08-03-155156-768x493.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2306</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Chembechembe ndogo za plastiki, Ikolojia, Kemikali, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Plastiki, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili dawa moja au zaidi za viuavijasumu (hali inayojulikana kama usugu dhidi ya dawa za vijiumbe, au AMR) umeongezeka kwa kasi na kuwa dharura ya afya ya umma, huku sasa ukisababisha vifo takriban milioni 5 duniani kote kila mwaka. &#8220;AMR ni tishio la kibinadamu,&#8221; anasema Tim Walsh, profesa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mkurugenzi wa biolojia katika Taasisi ya Utafiti wa Antimicrobial ya Ineos Oxford ya Uingereza, ambaye alizungumza na Mongabay kupitia njia ya simu ya video. &#8220;Itaua watu wengi zaidi [kila mwaka] kuliko Kifua Kikuu, VVU na malaria, na iwapo haitapingwa inaweza kuipita saratani kama muuaji mkubwa zaidi.&#8221; Hadi hivi karibuni, migogoro hii miwili ya kimataifa, uchafuzi wa plastiki na usugu dhidi ya viuavijasumu, ilizingatiwa tofauti na wanasayansi na watunga sera. Lakini utafiti mpya unaonyesha kuwa inahusiana kwa karibu: Taka za plastiki hukaliwa kwa haraka na vijiumbe, hivyo kuunda aina mpya ya mfumo wa ikolojia unaoitwa &#8220;plastisphere.&#8221; Aidha, bakteria wanaoishi katika mfumo huo wanastawisha uwezo mkubwa wa kustahimili viuavijasumu kwa kasi isiyo na kifani. Kipande cha plastiki ya aina ya polyethylene (kinachojulikana kama &#8220;bio-bead&#8221;), kinachotumika kusaidia kuvunja-vunja uchafu katika mitambo ya kusafisha maji taka, ambacho kimekaliwa na fangasi pamoja na vijiumbe vingine. Wakati mwingine, vipande hivi vya plastiki&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/#respond</comments>
					<pubDate>23 Julai 2026 12:11:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ini Ekott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23115923/Screenshot-2026-07-23-143214-768x438.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2184</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Cote D'Ivoire, Kenya, Nigeria, Uingereza, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Gesi, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Ufanisi wa nishati, na  Utoaji wa Gesi Chafu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja bila huduma za upishi safi. Kanda hiyo ni nyumbani kwa idadi kubwa zaidi ya watu duniani ambayo bado inategemea kuni, mkaa na mafuta ya taa kwa ajili ya kupikia kila siku, kulingana na shirika la IEA. Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema uchafuzi wa hewa wa makazi, ambao mwingi wake huzalishwa na nishati hizi za kupikia zinazochafua mazingira, unahusishwa na vifo vya mapema takriban milioni 2.9 kila mwaka, huku wanawake na watoto wakibeba mzigo mkubwa zaidi. &#8220;Upishi Safi Afrika 2026: Ripoti ya Maendeleo&#8221; inakadiria kuwa karibu watu milioni 15 walipata fursa ya kutumia upishi safi katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara mwaka wa 2025, karibu 35% zaidi ya wastani wa faida ya kila mwaka iliyorekodiwa kwa miaka mitano iliyopita. Ikiwa itathibitishwa, hii itakuwa ongezeko kubwa zaidi la kila mwaka kuwahi kurekodiwa. Côte d&#8217;Ivoire, Kenya na Nigeria zilipata faida kubwa zaidi. Makadirio hayo yametokana na mfumo wa hisabati unaounganisha takwimu za uingizaji wa majiko (vifaa vya kupikia vinavyochanganya jiko la kawaida na oveni) na gesi ya petroli iliyoshinikizwa (LPG), uwekezaji katika miundombinu, nishati na teknolojia zinazohitajika kwa ajili ya upikaji safi, pamoja na ufuatiliaji wa sera. Badala ya kutegemea tafiti za makazi, ambazo ndizo kipimo cha kuaminika zaidi cha upatikanaji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/#respond</comments>
					<pubDate>21 Julai 2026 17:56:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Kelvin Matuku]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21171918/Screenshot-2026-07-21-201312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2148</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Fedha ya mfumo wa ikolojia, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi wa Mazingira, Ufugaji Samaki, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari upya mustakabali wa uvuvi katika ziwa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi barani Afrika. “Wakati mwingine nakaa ziwani usiku mzima na kurudi na kati ya samaki 300 na 359 pekee,” anasema Otieno, ambaye amevua katika Ziwa Victoria kwa miongo kadhaa. “Samaki ni wachache na kipato pia kinapungua. Kama mvuvi, naona njia ambayo imebakia ni kukumbatia vizimba vya samaki ili tuweze kuendelea kuishi.” Ufukwe wa Paga kwenye Ziwa Victoria. Picha na Kelvin Matuku, Mongabay. Ziwa Victoria ni chanzo cha kujikimu kwa jamii za wavuvi nchini Kenya, Uganda na Tanzania, kupitia uvuvi na biashara zinazohusiana nao. Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2023, katika miaka ya hivi karibuni, Ziwa Victoria na eneo lake la vyanzo vya maji vimeathirika vibaya kutokana na “uvuvi kupita kiasi, umwagikaji wa mafuta, utiririshaji wa taka ambazo hazijatibiwa, kuenea kwa spishi vamizi, uchotaji wa maji kupita kiasi kutoka bonde la ziwa, na mabadiliko ya tabianchi, miongoni mwa sababu nyingine.” Kushuka kwa uzalishaji wa samaki Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS), uzalishaji wa samaki katika Ziwa Victoria umeshuka kutoka takriban tani za metriki 94,349 mwaka wa 2021 hadi 67,575 mwaka wa 2024. Huu ni upungufu wa zaidi ya tani 27,700 katika kipindi cha miaka mitatu. Upungufu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:56:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/15110719/Taka-za-kielektroniki-zikikusanywa-kwa-ajili-ya-kutengeneza-vitu-vingine-Picha-hisani-ya-WEEE-Centre-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2080</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na jalala ambamo zinatupwa takataka mbalimbali hatari, zikiwemo zile za kielektroniki, huku kambale akiwa amevuliwa katika bwawa lililochafuliwa na taka za aina hiyo. Fundi akitiengeneza kompyuta iliyoharibika. Picha cha Christopher Kidanka. Katika maeneo mengi, hasa mijini, wananchi hula vyakula ambavyo vina uwezekano mkubwa wa kuwa na sumu zinazotokana na taka za kielektroniki bila wao kufafahamu. Kadhalika mazingira katika maeneo hayo nayo hayako salama kutokana na taka hizo kuchafua udongo, maji, hewa na kuharibu makazi ya viumbe na kuhatarisha bioanuwai. Ongezeko la taka za kielektroniki Taka za kielektroniki ni vifaa vya elektroniki kama simu za mkononi, kompyuta, televisheni, jokofu, betri, viyoyozi, mashine za kufulia, chaja, nyaya na vifaa vingine vilivyoharibika, kupitwa na wakati au visivyotumika tena, na vinavyotupwa bila tahadhari. Kadri matumizi ya vifaa vya kielektroniki yanavyoongezeka nchini ndivyo uzalishaji wa taka hizo unavyoongezeka. Kulthum Shushu, Ofisa Mazingira wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), anasema Tanzania huzalisha wastani wa tani 35,000 za taka za kielektroniki kwa mwaka, lakini ni chini ya asilimia tano tu ndiyo hurejelezwa na kuchakatwa kutokana na ukweli kuwa urejelezaji wa taka hizo hatarishi ni ghali sana. Hali hiyo, anasema, husababisha taka kujikusanya katika mazingira na mzigo wa kuzisimamia huongezeka siku&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 18:14:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14175046/Omar-Shafi-akishona-nyavu-yake-yakuvulia-samaki-katika-eneo-la-Mtangawanda-kaunti-ya-LamuKenya.-Picha-na-Ruth-Keah.-2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2062</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sayansi, Sayansi ya Hali ya Tabianchi, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya uvuvi kesho yake. “Tangu nianze uvuvi miaka 40 sasa, nimekuwa nikitumia nyavu hizi za uzi kuvua samaki kwa sababu haziharibu mazingira ya bahari,” anasema Shafi. Omar Shafi akishona nyavu yake yakuvulia samaki katika eneo la Mtangawanda kaunti ya Lamu, Kenya. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kulingana naye, ujio wa zana mbalimbali za kuvulia samaki umeharibu mazingira ya bahari kiasi cha kwamba samaki na viumbe wengine baharini wamepungua sana. “Kuna zana nyingi ambazo wavuvi wanatumia, ambazo zinaharibu utulivu wa bahari. Hivyo husababisha baadhi ya viumbe baharini kupungua,” anasema. Vifaa vinavyosababisha kelele baharini ni kama meli kubwa za mizigo na abiria, boti za mwendo kasi, zana za kuvulia samaki kama trola, mitambo ya utafiti na uchimbaji na mitambo ya ujenzi wa miundombinu ya baharini. Vifaa hivi vimetajwa kusababisha kelele ambazo huathiri uwezo wa viumbe hao kuwasiliana, kusafiri na kusaka chakula. Kama anavyoeleza Shafi, nguva ni miongoni mwa wanyama baharini ambao alikuwa akikutana nao mara kwa mara alipoanza uvuvi hasa katika maeneo ya Manda na Dodori, kaunti ya Lamu. Lakini sasa imekuwa vigumu sana kwake kuwaona. Nguva bado yuko “Kwa maoni yangu, mnyama huyu nguva bado yuko, lakini kwa sababu bahari haina utulivu kutokana na kelele za vyombo vya uvuvi, nguva hukimbia, siwaoni tena,” anasema Omar. Taswira hiyo haielezwi na Shafi peke yake, bali pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 19:43:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11194040/Vijana-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1846</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Fedha, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa Umoja wa Mataifa wenye makao yake nchini Uswisi unaofadhiliwa kupitia michango ya hiari kutoka kwa nchi zilizoendelea na jumuiya ya kimataifa, zitatolewa kupitia serikali na kusambazwa kwa jamii mbalimbali nchini zinazokabiliwa na majanga mbalimbali yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi. Majanga hayo ni pamoja na ukame wa mara kwa mara, mafuriko, kupungua kwa uzalishaji wa mazao, uharibifu wa mazao na matukio mengine ya hali mbaya ya hewa. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Misitu wa Kenya, Festus Ng’eno, alisema msaada huo ni hatua muhimu sana. Ng’eno alisema hatua hiyo inaifanya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na mfuko huo. Vanuatu, taifa la funguvisiwa lenye maeneo mengi ya mwinuko wa chini, ndiyo iliyokuwa nchi ya kwanza duniani kupata ufadhili huo. Ng’eno alitoa taarifa hiyo katika mazungumzo yaliyofanyika sambamba na mazungumzo ya kiufundi ya tabianchi ya UNFCCC Subsidiary Bodies (SB64) yanayoendelea huko Bonn, Ujerumani. Katika taarifa aliyochapisha mtandaoni, akithibitisha habari iliyochapishwa na gazeti la People Daily mnamo Juni 10, Dkt Ng’eno alisema kuwa licha ya Kenya kupitia baadhi ya majanga makubwa zaidi ya tabianchi katika Afrika Mashariki, nchi hiyo haijawahi kupima kikamilifu kiwango halisi cha hasara iliyopata kutokana na majanga hayo. &#8220;Hali hiyo sasa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 13:46:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11131849/Screenshot-2026-06-11-161609.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1841</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Urusi, Zambia, na  Zimbabwe]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka jana, lakini uwezo wa akiba wa mitambo ya makaa ya mawe unaoweza kutumika wakati wa mahitaji makubwa ya umeme uliongezeka kwa 3.5%. Sehemu kubwa ya ongezeko hilo ilitokea nchini Uchina, ambapo uwezo wa ziada wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe unazidi kuchukuliwa kuwa chaguo mbadala ili kuhakikisha usalama wa nishati. Wakati Uchina iliongeza gigawati 78.1 za uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo 2025, matumizi yake halisi ya nishati ya makaa ya mawe yalipungua kwa 1.2%. Kupungua huku kulidhihirika wazi kwani kulikuja huku kukiwa na ongezeko la jumla la mahitaji ya nishati ya Uchina. Kulingana na ripoti hiyo, zaidi ya 90% ya ongezeko hilo la mahitaji ya nishati lilikidhiwa na nishati ya upepo na jua badala ya makaa ya mawe. Wakati Uchina inasalia kuwa mtumiaji mkubwa zaidi wa makaa ya mawe duniani, mahitaji yake zaidi ya nishati yanatimizwa kwa njia mbadala. India ilirekodi ongezeko la pili kwa ukubwa la uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo mwaka 2025, lakini pia ilionyesha harakati kuelekea gridi safi zaidi. Pamoja na nyongeza za rekodi za nishati ya jua na upepo, nishati jadidifu zilichangia zaidi ya nusu ya uwezo wa jumla wa nishati nchini kwa mara ya kwanza. Christine Shearer, mtafiti&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 19:10:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09143738/EACOP-Main-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1826</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Mimea, Samaki, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa kutumia takwimu za ramani na makadirio ya thamani ya kiuchumi, ripoti ya Earth Insight, shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Marekani, inaonyesha kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 liko karibu na maeneo muhimu kwa maisha ya mamilioni ya watu na usalama wa maji, na pia sehemu ambazo hutumika kama njia za uhamaji wa wanyama. Kutokana na uchambuzi huo, ripoti hiyo inahitimisha kuwa ujenzi wa bomba hilo tayari umeathiri jamii na mazingira, na kwamba usafirishaji wa mafuta utaleta hatari zaidi za muda mrefu. EACOP ni mradi wa ubia kati ya  kampuni ya TotalEnergies yenye asilimia 62 ya hisa, serikali za Uganda na Tanzania kila moja ikiwa na asilimia 15, pamoja na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) yenye asilimia 8. EACOP itasafirisha mafuta yanayochimbwa kutoka vitalu viwili kwenye bonde la Ziwa Albert: Kingfisher, linalomilikiwa na CNOOC; na Tilenga, linalomilikiwa na TotalEnergies. Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) nchini Uganda. Picha kwa hisani ya Thomas Lewton. Kwa mujibu wa Earth Insight, mradi huo unakaribia kukamilika na mafuta ya kwanza yataanza kusafirishwa mapema mwaka 2026. “Linapita moja kwa moja katika maeneo ya viumbe walio hatarini kutoweka, na eneo muhimu zaidi ni la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 20:21:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05201200/Screenshot-2026-06-05-231142-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1791</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Nishati, Siasa za Nishati, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana kama “Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk” pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa sakafu ya bahari (deep-sea mining) pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Ripoti hiyo ilitolewa Juni 4, 2026 na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani inayoadhimishwa Juni 8. Ripoti iliandaliwa kutokana na utafiti uliohusisha nchi 11 kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Katika utafiti huo, Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Nchi nyingine zilizotajwa ni Kenya, Australia, Cameroon, Indonesia, Jamaica, Norway, Trinidad na Tobago, Argentina na Mexico. Kwa Tanzania, mradi huo unapangwa kujengwa katika eneo la Likong’o, kusini mwa mkoa wa Lindi. Lengo ni kuchakata gesi asilia inayopatikana baharini na kuibadilisha kuwa gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Ripoti hiyo imetolewa siku chache baada ya Waziri wa Nishati, Dkt Deogratius Ndejembi, kuliambia Bunge kwamba makubaliano ya kibiashara na kodi kati ya serikali na wawekezaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>04 Juni 2026 12:55:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/04131449/Screenshot-2026-06-04-161427.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1773</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Gesi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na kibayolojia. Ripoti hiyo iliyopewa jina la Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk ilitolewa leo, siku chache kabla ya mkutano wa 11 unaohusu masuala ya bahari, mkutano wa ‘Our Ocean Conference’ unaotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 16 hadi 18 mjini Mombasa, Kenya. Ripoti hiyo inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa kina cha bahari pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Bonde la Lamu limetajwa kuwa eneo linalopewa kipaumbele, ambapo miradi minane ya mafuta inayotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu, imepangwa kutekelezwa katika ukanda huo wa pwani wenye historia na utajiri mkubwa wa kiikolojia. “Uchambuzi wetu unaonesha kuwa asilimia 100 ya Miamba ya matumbawe na misitu ya mikoko katika eneo hili imefunikwa na vitalu vya mafuta na gesi. Kwa asilimia 100, maeneo haya ni ya hifadhi za baharini na pwani lakini pia ni muhimu kwa bayoanuwai,” ripoti hiyo imeeleza. Katika ripoti hiyo, Kenya imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Ripoti hiyo ilitolewa na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 12:56:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Penzi Nyamungumi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03130042/Screenshot-2026-06-03-160011.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1754</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Mazingira, Plastiki, Sheria ya Mazingira, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa kwenye mifereji zimekuwa zikiziba njia za maji na kuchangia mafuriko. Aidha, chupa zinapochomwa, moshi wake husababisha maradhi na pia kuathiri mazingira kutokana na asili yake ya kuchelewa kuoza. Hata hivyo, kuibuka na kukua kwa biashara ya chupa za plastiki zilizotumika, ambayo mara nyingi hufanywa na akinamama na vijana, kunaendelea kubadilisha historia. Hivi sasa badala ya kushuhudia barabara zenye mifereji iliyojaa chupa tupu, kinachoonekana ni akinamama na vijana waliobeba viroba vikubwa vyenye chupa hizo. Wakusanyaji wadogo huuza chupa hizo kwa wakusanyaji wakubwa au kwa kampuni zinazojishughulisha na ukusanyaji na urejelezaji wa chupa hizo baada ya matumizi. Taimuru Hamad, Meneja Uzingatiaji Sheria kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), anakiri kwamba biashara hiyo imeleta faida kubwa katika ustawi na ulinzi wa mazingira. Chupa za plastiki zilizokusanywa kutoka maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam zikiwa zimefungwa kwenye mifuko mikubwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wanunuzi. Picha na Joyce Bazira. “Kuokotwa kwa hizi chupa kunasaidia sana. Kwanza, kunasaidia katika suala zima la ustawi wa mazingira, lakini pia kwenye suala la usafi. Kama zingekuwa haziokotwi, mazingira yangeendelea kuathirika sana na pia yangekuwa machafu sana,” alisema Taimuru katika mahojiano na Mongabay. Chupa za rangi Pamoja na kazi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>23 Mei 2026 21:35:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/23214326/Screenshot-2026-05-24-004210-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1696</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uhifadhi, na  Umeme]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika, ambalo linapatikana Kenya, Uganda na Tanzania. Mwisho wa Machi 2026, wakati wa kongamano la kimataifa kuhusu nishati ya nyuklia, Rais wa Kenya William Ruto alitangaza ujenzi wa kinu cha nyuklia chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,000 katika eneo hilo. Kwa sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu mpango huo kwenye tovuti ya Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA). Hata hivyo, Ruto alisema ujenzi utaanza mwaka ujao na kinu hicho kinatarajiwa kuanza kuzalisha umeme mwaka 2034. “Hakuna nchi yoyote duniani iliyowahi kufanikisha malengo yake ya maendeleo bila kuwa na nishati ya kutosha na ya kuaminika,” alisema Ruto. Pia alisisitiza kuwa nishati ya nyuklia inatambuliwa na Umoja wa Mataifa kama chanzo cha nishati chenye kiwango kidogo cha uzalishaji wa hewa ukaa na muhimu katika kufanikisha Agenda ya Maendeleo Endelevu ya 2030. “Kuunganisha nishati ya nyuklia katika gridi ya taifa ni hatua ya kimkakati ya kupata suluhisho la muda mrefu litakalokidhi ongezeko la mahitaji ya umeme nchini Kenya,” alisema. Katika hotuba yake, Ruto alifafanua kuwa tayari alikuwa ameshauriana na wakazi wa Siaya na kujiridhisha kuwa jamii za eneo hilo zinaunga mkono mradi huo. Hata hivyo, maandamano ya hivi karibuni yanaonyesha hali halisi ni tofauti. Aidha, ombi la kupinga mradi huo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2026 12:50:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20124420/Waziri-Shemdoe-1-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1650</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Ikolojia, Maji, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Taka, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa kiwango cha chini. Kwa mujibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Tanzania huzalisha kati ya tani milioni 14.4 hadi milioni 20.7 za taka ngumu kila mwaka. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Riziki Shemdoe, jijini Dodoma katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira mijini. Mkutano huo uliwakutanisha viongozi waandamizi wa serikali, washirika wa maendeleo, na wataalamu wa mazingira kwa lengo la kutathmini maendeleo yaliyofikiwa na kuweka mikakati ya kuboresha mifumo ya usimamizi wa taka. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe na wadau wa usimamizi wa taka wakifuatilia mijadala katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Dodoma. Picha: Maktaba ya Wizara. Taka na fursa za kiuchumi Waziri Riziki alisema kuwa usimamizi wa taka unapaswa kuingizwa katika mikakati mipana ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa kuwa taka zinapaswa kuonekana kama rasilimali ya kiuchumi inayoweza kuzalisha ajira na kipato ikiwa zitasimamiwa ipasavyo. Aliziagiza mamlaka za serikali za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/#respond</comments>
					<pubDate>12 Mei 2026 04:00:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika VyawahareMary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11220722/671089-DSC_0303-5f9eed-original-1777544684-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1589</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Ubunifu wa Kijani, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya Mpesa Foundation Academy, walitengeneza mfumo huo, HewaSafi, unaomaanisha “hewa ambayo ni safi” kwa Kiswahili, baada ya kuona marafiki na familia wakiugua maradhi yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa. Shirika la Earth Foundation, lenye makao yake makuu nchini Uswizi, linatoa Tuzo ya Dunia, ambayo sasa iko katika mwaka wake wa tano, na inatambua vijana wenye umri wa miaka 13 hadi 19 wanaofanya kazi katika kutatua changamoto za mazingira. Timu ya HewaSafi sasa inawania tuzo ya kimataifa, ambayo upigaji kura kwa umma utafunguliwa tarehe 18 Mei, na kufungwa mnamo Mei 27. Mshindi wa toleo la kimataifa atatangazwa tarehe 29 Mei. &#8220;Tatizo la uchafuzi wa hewa lilikuwa la kibinafsi sana kwetu, na ndiyo maana tukaanza kufikiria kupata suluhu,&#8221; Kariuki aliiambia Mongabay. &#8220;Ilikuwa hamasa kubwa kabla ya kuwa mradi.&#8221; Kariuki, ambaye alikulia katika eneo lenye viwanda vingi katika Kaunti ya Nakuru nchini Kenya, alipata ugonjwa sugu wa mapafu akiwa na umri wa miaka 10 ambao bado unamhitaji kutumia dawa kila wiki. Onsarigo, ambaye alikulia magharibi mwa Kenya, alishuhudia vifo na magonjwa mabaya yanayohusiana na hewa chafu. Takwimu kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa uchafuzi wa hewa husababisha vifo vya mapema milioni 4.4 ulimwenguni kila mwaka. Moshi wa magari ni chanzo kikuu cha uchafuzi wa mazingira katika maeneo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/#respond</comments>
					<pubDate>11 Mei 2026 15:28:34 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11150848/Lethome-5-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1551</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Umeme, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu zaidi ya 82. Mongabay ilimtembelea Sheikh Ibrahim Lethome alipokuwa kwenye mfungo wa Ramadhani ili kupata maoni yake kuhusu juhudi zake katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira. Lethome amejitaja kuwa aliyetekeleza kile ambacho huenda kilionekana kama jukumu dogo katika juhudi za kupinga mradi wa umeme wa makaa ya mawe huko Lamu, Kenya. Juhudi hizo ziliongozwa na viongozi wa Save Lamu pamoja na wawakilishi wa jamii, mawakili wa masuala ya mazingira, wanaharakati na taasisi za serikali pamoja na mamlaka za udhibiti kama NEMA na mahakama za mazingira. Hatimaye, mradi huo ulisitishwa Desemba mwaka 2025. Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano yake na Lynet Otieno wa Mongabay, yaliyofanyika katika ofisi za Msikiti wa Jamiah jijini Nairobi. Mongabay: Tafadhali tueleze kwa ufupi wewe ni nani, kama msomi, kiongozi wa kidini na mwanaharakati wa mazingira. Lethome: Mimi kitaaluma ni mwanasheria na msomi wa elimu ya Kiislamu. Ninafanya kazi katika fani zote mbili. Nimekuwa mwanachama wa Msikiti wa Jamiah kwa miaka 32 sasa. Ninaongoza Idara ya Dini. Pia ni mwanachama wa bodi ya kimataifa ya GreenFaith, na mwenyekiti wa bodi ya GreenFaith-Afrika, taasisi inayotumia mafundisho ya dini kuhamasisha uhifadhi wa mazingira. Mwelekeo wangu ni kuangalia jinsi mafundisho ya dini yanavyoweza kutumika kushughulikia changamoto nyingi ambazo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama ya Kenya yaruhusu kesi ya kihistoria ya taka za sumu ya BP kuendelea</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/#respond</comments>
					<pubDate>06 Mei 2026 13:26:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dalle Abraham]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/06170355/Screenshot-2026-05-06-200329-768x497.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1525</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo Kenya, imeamuru kwamba kesi ya hatua ya ngazi ya juu dhidi ya kampuni kubwa ya mafuta ya Uingereza ya BP inaweza kuendelea kusikizwa kikamilifu. Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa taka za sumu zilizoachwa kutokana na uchimbaji wa mafuta katika miaka ya 1980 zilichafua maji ya ardhini kaskazini mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/" data-wpel-link="internal">Mahakama ya Kenya yaruhusu kesi ya kihistoria ya taka za sumu ya BP kuendelea</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo Kenya, imeamuru kwamba kesi ya hatua ya ngazi ya juu dhidi ya kampuni kubwa ya mafuta ya Uingereza ya BP inaweza kuendelea kusikizwa kikamilifu. Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa taka za sumu zilizoachwa kutokana na uchimbaji wa mafuta katika miaka ya 1980 zilichafua maji ya ardhini kaskazini mwa Kenya, na kuua zaidi ya watu 500 na maelfu ya mifugo. Kesi hiyo, iliyofunguliwa Februari na walalamikaji 299 katika Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo, ilifikishwa mahakamani na wakazi wa Kargi na Kalacha, makazi mawili yaliyoko katika kaunti ya Marsabit. Inadaiwa katika kesi hiyo kuwa shughuli za uchimbaji wa mafuta zilizofanywa kati ya mwaka 1985 na mwaka 1993 kaskazini na kaskazini-magharibi mwa Kenya na Shirika la Amoco, ambalo lilinunuliwa na BP mwaka wa 1998, vichafuzi hatari na sumu vilimwagwa kwenye mazingira, na kuchafua maji ya ardhini ambayo jamii hutegemea kwa kunywa na kwa mifugo yao. Hati za korti zinadai kuwa taka za kuchimba visima zilizo na isotopu za radiamu, aseniki, madini ya risasi na nitrati, zilitupwa kwenye mashimo yaliyoachwa wazi au ambayo hayakuwekwa katika hali inayotakiwa kiusalama. Katika kesi hiyo, washitakiwa ni pamoja na kampuni ya British Petroleum PLC ambayo ni mshitakiwa wa kwanza, huku wengine 11 wakiwa ni Shirika la Kitaifa la Mafuta la Kenya; mawaziri wa mazingira, maji, afya na madini; Mamlaka ya Rasilimali za Maji; serikali ya kaunti ya Marsabit; mwanasheria mkuu; Mamlaka ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mazingira; Mamlaka ya Udhibiti wa nishati ya Nyuklia ya Kenya pamoja na Taasisi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Aprili 2026 21:25:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/22211810/Screenshot-2026-04-23-001707.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1429</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maji, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya kaya 15 zinaadhimisha siku hiyo bila kuwa na makazi baada ya kuzikimbia nyumba zao kufuatia maporomoko ya tope  yaliyokumba eneo lao hivi karibuni. Huko wilayani Rungwe, wanasherehekea siku hii huku wakiwa na majonzi mazito kufuatia kupoteza ndugu na jamaa zao zaidi ya watu 20 waliofariki katika maporomoko yaliyosababishwa na mafuriko yaliyotokea Machi 15, 2026. Kutokea kwa maporomoko ni miongoni mwa majanga yaliyoelezwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  katika taarifa yake kuhusu mwelekeo wa mvua za masika Machi-Mei, 2026. Katika taarifa hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (kanda ya Ziwa Victoria, nyanda za juu Kaskazini-mashariki, Pwani ya kaskazini pamoja na maeneo yaliyopo kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) katika kipindi cha miezi hiyo, vipindi vifupi vya mvua kubwa vingeweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi. Alisema matukio hayo yangeweza kuleta uharibifu wa miundombinu na mazingira, milipuko ya magonjwa, pamoja na upotevu wa mali na maisha. Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC ) nalo lilitoa tahadhari kuhusu hatari ya mvua kubwa na maporomoko ya ardhi ambayo yangeweza kusababisha uharibifu mkubwa. Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Immaculate Semesi, akizungumza na vyombo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 19:32:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/14182846/mawe2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1351</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Sera za Mazingira, Uchafuzi, Uharibifu wa Makazi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), bado uchimbaji holela wa mawe umeendelea kuwa jinamizi linalowaumiza wakazi jijini Mwanza. Akizungumzia sababu za hali hiyo kuendelea, Laurent Kitogo, Afisa wa Mazingira kutoka Environmental Management and Economic Development Organization (EMEDO), anataja udhaifu katika usimamizi pamoja na utekelezaji wa sheria kuwa kikwazo kikubwa. “Sheria ni eneo moja na usimamizi wake ni jambo jingine. Tunazo mamlaka kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na maeneo yote ambayo watu wanaishi. Sheria imeelekeza kabisa kwamba kutakuwa na maafisa wa mazingira kuanzia ngazi ya mtaa, lakini ukiangalia kwa uhalisia ulivyo, utaona maafisa wa mazingira wanaanzia ngazi ya halmashauri. Huwezi kumkuta afisa wa mazingira katika ngazi ya kata,” anasema. David Joseph, Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira jijini Mwanza, anasema kuwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hakuna eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa mawe, na kwamba wanaochimba, baadhi wanakuwa wanasawazisha viwanja vyao kutokana na kuwa na asili ya miamba, au ni wavamizi ambao wameona hiyo kama fursa ya ujasiriamali. “Watu wanachimba mawe katika miktadha kuu miwili. Moja, asili ya Mwanza ni milima, na sehemu nyingi zina mawe. Hata kama ni tambarare, utakuta kuna mawe…kwa hiyo watu wengine wanachimba yale mawe ili kusawazisha viwanja vyao…hayo mawe&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yakamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa umemejua wa MW 50 Kishapu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/__trashed-2__trashed/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/__trashed-2__trashed/#respond</comments>
					<pubDate>25 Mechi 2026 17:52:30 +0000</pubDate>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05125337/Baadhi-ya-wavuvi-katika-eneo-la-Kigambani-wakipakia-chakula-yakiwemo-mafuta-ya-kula-na-mahindi-tayari-kwenda-Mafia-kuvua-samaki.-Picha-na-Hellen-Nachilongo.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1227</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Misitu, Uchafuzi, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imekamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa kuzalisha umeme wa jua wenye uwezo wa kutoa megawati 50 uliogharimu Shilingi za Tanzania Bilioni 118.6 (Dola za Marekani Milioni 47.44). Mradi huo uliojengwa katika kijiji cha Ngunga, wilaya ya Kishapu, mkoa wa Shinyanga, unalenga kuongeza uzalishaji wa nishati safi na kuimarisha uthabiti wa gridi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/__trashed-2__trashed/" data-wpel-link="internal">Tanzania yakamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa umemejua wa MW 50 Kishapu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imekamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa kuzalisha umeme wa jua wenye uwezo wa kutoa megawati 50 uliogharimu Shilingi za Tanzania Bilioni 118.6 (Dola za Marekani Milioni 47.44). Mradi huo uliojengwa katika kijiji cha Ngunga, wilaya ya Kishapu, mkoa wa Shinyanga, unalenga kuongeza uzalishaji wa nishati safi na kuimarisha uthabiti wa gridi ya taifa. Ulianza kutumika rasmi Februari, mwaka huu. Hatua hiyo ni utekelezaji wa Tamko la Dar es Salaam la Misheni 300 la mwaka 2025, ambapo Tanzania iliahidi kuongeza mchango wa nishati mbadala katika uzalishaji wa umeme kwenye gridi ya taifa hadi asilimia 75 kufikia mwaka 2030, kutoka kiwango cha sasa cha  asilimia 61.8. Tamko la Misheni 300 ni utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2025, inayosisitiza matumizi ya nishati safi endelevu na Mpango wa Kitaifa wa Mchango wa Taifa (NDC) katika Mkataba wa Paris. Mkataba wa Paris ni makubaliano ya kimataifa yaliyoanzishwa mwaka 2015 chini ya Umoja wa Mataifa, yakilenga kupunguza ongezeko la joto duniani hadi chini ya nyuzi joto 2°C, na ikiwezekana 1.5°C, kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafu. Kupitia mkataba huo, nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, hutakiwa kuandaa na kutekeleza mipango yao ya kitaifa  ya kupunguza uzalishaji wa hewa chafu na kujenga ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi (NDCs). Chini ya mpango huo, Tanzania imeahidi kukuza matumizi ya teknolojia za nishati safi katika uzalishaji wa umeme na shughuli za viwanda, kwa lengo la kupunguza utegemezi wa nishati chafu kama mafuta, gesi na kuni, ambavyo huchangia uchafuzi wa mazingira na kuongeza uzalishaji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/__trashed-2__trashed/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/__trashed-2__trashed/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/#respond</comments>
					<pubDate>13 Januari 2026 21:05:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amos Kareithi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/14135833/Screenshot-2026-01-14-165633-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=931</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Barafu, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Milima, Misitu, Misitu ya Milimani, Miti, Samaki, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa kihistoria hakumaanishi tu kupotea kwa mandhari ya asili, bali pia kunafungua ukurasa mpya wa changamoto kwa mazingira, mito, na jamii zinazoutegemea. Safari ya Lewis Pugh, Msimamizi wa Mradi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), hadi kwenye barafu za mwisho za Mlima Kenya, inatoa taswira ya kusikitisha ya athari halisi za mabadiliko ya tabianchi, zinazotoka juu ya mlima na kushuka hadi mashambani, misituni na vijijini, ambako maji, imani na maisha yenyewe yako hatarini. Pugh, aliyeshikilia nafasi hiyo katika shirika la UNEP tangu mwaka 2013, aliwasili nchini Kenya kwa matumaini kuwa uwezo wake wa kutoa hotuba zenye mvuto, ulioimarishwa kwa miaka 27 iliyopita, ungezivutia hisia za dunia, kwa namna fulani, kwenye athari mbaya za ongezeko la joto duniani katika eneo la Mlima Kenya. Lewis Pugh, Mwakilishi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), aliyeukwea Mlima Kenya mnamo Desemba 2025. Picha na Duncan Moore, UNEP. Huku ulimwengu ukijiandaa kwa sikukuu ya Krismasi, kati ya tarehe 4 hadi tarehe 8 mwezi Desemba 2025, Pugh aliparaga kupitia miamba iliyomikali ya volkeno, baadhi ikiwa na umri wa miaka milioni 4, hadi urefu wa mita 4,985 (futi 16,355) juu ya kilele cha Lenana. Lengo lake kuu lilikuwa kuogelea katika Ziwa Lewis.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi kampeni inayoongozwa na vijana inavyorejesha uhai wa ardhi oevu ya Dunga katika Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>05 Januari 2026 15:12:10 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Achieng’ Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/05144052/PAPYRUS-REEDS-PLANTATION-AT-DUNGA-BEACH-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=886</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Kijani, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Maji, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Ndege, Samaki, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miale ya jua imechomoza na kutengeneza mwanga wa kupendeza juu ya Ziwa Victoria, Afrika Mashariki. Upepo mwanana kutoka ziwani umebeba sauti za kuvutia za ndege, huku mitumbwi ya mbao ya kawaida ikitia nanga taratibu ufukweni. Maji yametulia. Mara kwa mara, ndege aina ya African sacred ibis (Threskiornis aethiopicus) huruka kwa ustadi mkubwa na kunyakua samaki kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jinsi kampeni inayoongozwa na vijana inavyorejesha uhai wa ardhi oevu ya Dunga katika Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miale ya jua imechomoza na kutengeneza mwanga wa kupendeza juu ya Ziwa Victoria, Afrika Mashariki. Upepo mwanana kutoka ziwani umebeba sauti za kuvutia za ndege, huku mitumbwi ya mbao ya kawaida ikitia nanga taratibu ufukweni. Maji yametulia. Mara kwa mara, ndege aina ya African sacred ibis (Threskiornis aethiopicus) huruka kwa ustadi mkubwa na kunyakua samaki kwa midomo yao kisha hupaa. Mazingira ya Ufukwe wa Dunga ni ya utulivu na amani. Baada ya saa chache, wauza samaki watawasili kuanza majadiliano ya bei na wavuvi waliokesha usiku kucha wakivuta nyavu, ambazo mara nyingi hurudi zikiwa karibu tupu. Kwenye kijito kilichopo nyuma ya msururu wa vibanda vilivyojengwa kwa mbao na bati, njia nyembamba iliyozibwa na mashina ya magugu maji (water hyacinth) yaliyokaushwa imepinda kuelekea kwenye njia ya mbao iliyoinuliwa. Victor Ochieng’ Didi, mwenye umri wa miaka 32, anatembea juu ya mbao hizo akiwa na kundi la watalii wa Kenya. Watazamaji wa ndege kwa mwaka mzima wamekuwa wakipanga kutembelea eneo hilo na kushuhudia mandhari ya kuvutia yenye ndege aina ya papyrus gonolek (Laniarius mufumbiri), ambaye kwa mujibu wa Orodha Nyekundu ya IUCN, ameorodheshwa kama aliye katika hatari ya kutoweka (near threatened). Kulingana na tovuti ya ufuatiliaji wa ndege ya EBird, ndege huyo alionekana mara ya mwisho katika eneo oevu la Dunga mwaka 2024. Victor Ochieng Didi, mwanamazingira na mkazi wa Dunga, Nyalenda, ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya mazingira ya Kikundi cha Utalii wa Ikolojia na Mazingira cha Dunga (DECTTA), ambacho kimekuwa kikifanya juhudi za kufufua ardhi oevu iliyowahi kustawi. Picha na Achieng’ Otieno. Juhudi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/05/jinsi-kampeni-inayoongozwa-na-vijana-inavyorejesha-uhai-wa-ardhi-oevu-ya-dunga-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>10 Novemba 2025 09:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[John Cannon]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/12101218/Screenshot-2025-11-12-131027-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=769</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Hali ya Hewa, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Nishati safi, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Tabianchi, Uchafuzi, Ufadhili wa tabianchi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao pekee cha kupata nishati. Wengine wanaweza kuchangisha pesa za kutosha kwa paneli ya jua ambayo inaweza kuchajisha simu ya mkononi, kuwasha redio na kutoa mwanga kidogo kwa watoto kutwalii. Lakini kwa kawaida haitoshi kwa kazi ya msingi ya kupikia. Tofauti kubwa kati ya hali hii na ulimwengu mpana zaidi unaotumia nishati hiyo inaonekana wazi kwa walio na uwezo finyu au wasiokuwa na uwezo kabisa wa kuufikia. &#8220;Unatokea mjini &#8211; una umeme, una taa. Kwa nini wewe na sio sisi?&#8221; Mukalay Ngoyi, kiongozi kutoka kijiji cha Lukwangulo, aliiambia Mongabay. &#8220;Sisi ni wanadamu kama wewe, na tunahitaji umeme pia.&#8221; Mnamo Novemba 10, Mkutano wa 30 (COP30) wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC),utakuwa Belém, Brazili, kutathmini maendeleo ya kimataifa kuelekea kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kupunguza uzalishaji wa kaboni. Cha msingi katika kupunguza uzalishaji huo na kufikia lengo la kuweka halijoto duniani kuwa chini ya nyuzi 2° (3.6° Fahrenheit) juu ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda ni jinsi tunavyokidhi kuongezeka kwa mahitaji ya nishati, kote duniani na katika maeneo kama kijiji cha Lukwangulo. Lakini viongozi wengi wa jamii hawatakuwa Belém, badala yake wanategemea wengine kuwawakilisha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>15 Oktoba 2025 07:04:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/07070649/Screenshot-2025-11-07-100242-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=743</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Biashara, Chakula, Chembechembe ndogo za plastiki, Kanuni, Kemikali, Magonjwa, Mazingira, Ndege, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uhifadhi, upatikanaji wa chakula, Utafiti, na  Utandawazi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni sumu kwa afya ya binadamu na mazingira. Sehemu za uchafu wa kielektroniki, majaa ya taka na vichomea taka ni vyanzo muhimu vya uchafuzi huu, huku mayai yaliyofanyiwa utafiti katika maeneo jirani yakipatikana kuwa yamechafuliwa sana na kemikali zinazotolewa wakati taka za plastiki zinachomwa. Sampuli ya mayai yaliyotolewa karibu na maeneo ya taka za kielektroniki nchini Ghana mwaka wa 2019, kwa mfano, yalikuwa na viwango vya dioksini za bromini iliochanganywa na klorini mara 200 zaidi ya kiwango cha usalama cha chakula. Uzalishaji na matumizi ya kimakusudi ya dioksini umeondolewa au kuwekewa vikwazo vikali ulimwenguni kote chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Stockholm kuhusu vichafuzi vinavyoendelea vya kikaboni (POPs). Utafiti huo, uliochapishwa katika jarida la Emerging Contaminants, uliongozwa na Mtandao wa Kimataifa wa Kutokomeza Uchafuzi (IPEN), pamoja na shirika lisilo la serikali la Czech Arnika na timu ya wanasayansi wa kimataifa. Utafiti huo ulikuwa wa kina, na data ya sumu ya yai iliyokusanywa katika nchi nyingi zinazoendelea, na nchi zilizo na uchumi wa mpito, barani Afrika, Asia, Amerika Kaskazini na Kusini na Ulaya. Matokeo hayo yanahusu sana, waandishi wa utafiti wanasema, kwani mayai ni chanzo muhimu cha protini katika nchi za kipato cha chini na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ziwa kuu zaidi barani Afrika huenda likawa eneo la kinu cha nyuklia cha Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/08/ziwa-kuu-zaidi-barani-afrika-huenda-likawa-eneo-la-kinu-cha-nyuklia-cha-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/08/ziwa-kuu-zaidi-barani-afrika-huenda-likawa-eneo-la-kinu-cha-nyuklia-cha-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>08 Oktoba 2025 20:18:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/03202517/Screenshot-2025-11-03-232333-768x480.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=731</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Maji, Mazingira, Maziwa, Nishati, Nishati Mbadala, Samaki, Samaki wa Maji safi, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, na  Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>&#8220;Ni kamilifu!&#8221; anagutuka Anthony Kingi, mwanachama wa jamii ya kijiji cha Uyombo na mwanaharakati wa mazingira. &#8220;Kenya haiuhitaji huu. Hata hivyo, kama ni lazima waujenge, ninafurahi kuwa hauko nyuma ya nyumba yangu.&#8221; Anachoashiri “hicho” Kiwanda kinachorejelewa na Kingi ni kinu cha nyuklia cha megawati 1,000 ambacho serikali ya Kenya inapanga kujenga. Serikali imeorodhesha maeneo matatu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/08/ziwa-kuu-zaidi-barani-afrika-huenda-likawa-eneo-la-kinu-cha-nyuklia-cha-kenya/" data-wpel-link="internal">Ziwa kuu zaidi barani Afrika huenda likawa eneo la kinu cha nyuklia cha Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[&#8220;Ni kamilifu!&#8221; anagutuka Anthony Kingi, mwanachama wa jamii ya kijiji cha Uyombo na mwanaharakati wa mazingira. &#8220;Kenya haiuhitaji huu. Hata hivyo, kama ni lazima waujenge, ninafurahi kuwa hauko nyuma ya nyumba yangu.&#8221; Anachoashiri “hicho” Kiwanda kinachorejelewa na Kingi ni kinu cha nyuklia cha megawati 1,000 ambacho serikali ya Kenya inapanga kujenga. Serikali imeorodhesha maeneo matatu ambayo yanaweza kutumika kwa mradi huo wenye thamani ya dola bilioni 3.8. &#8220;Kwa sasa Kenya ipo katika awamu ya pili ya maendeleo ya mpango wa nishati ya nyuklia, ikiwa na lengo la wazi la kuunganisha nishati ya nyuklia kwenye gridi ya kitaifa ifikapo mwaka 2034,&#8221; Shirika la Nishati ya Nyuklia la Kenya (NuPEA) lilisema katika taarifa kwa Mongabay. Mashauriano ya awali kuhusu mradi yalijikita katika sehemu ya Uyombo, kijiji cha wavuvi katika Kaunti ya Kilifi kwenye pwani ya kusini mashariki mwa Kenya. Uamuzi huo ulisababisha upinzani mkubwa kutoka kwa wanakijiji wa Uyombo na wataalam wa mazingira. Kwa miaka mingi, maandamano yalipoongezeka, waandamanaji walivamiwa na polisi, na wengine walikamatwa. Mnamo Juni 27 mwaka huu, kukiwa na shamrashamra ndogo sana, Wizara ya Kawi na Petroli ilitangaza katika Kongamano la Nishati ya Nyuklia katika Chuo Kikuu cha Sayansi na Teknolojia cha Jaramogi Oginga Odinga (JOOUST), kilichoko kaunti ya Siaya kwamba inafikiria kujenga kiwanda hicho huko Luanda Kotieno, katika eneo la Bondo kaunti ya Siaya, upande wa pili wa nchi. Sehemu zinazowezekana kuanzishwa kwa mradi wa kinu cha nyuklia kilichopendekezwa cha Kenya. Mbunge wa Rarieda Paul Otiende Amollo, mojawapo ya maeneo bunge sita ya kaunti ya Siaya, alisema wakati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/08/ziwa-kuu-zaidi-barani-afrika-huenda-likawa-eneo-la-kinu-cha-nyuklia-cha-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/08/ziwa-kuu-zaidi-barani-afrika-huenda-likawa-eneo-la-kinu-cha-nyuklia-cha-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi vijana ndugu walivyolinusuru Ziwa Victoria kutokana na hatari ya plastiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/#respond</comments>
					<pubDate>31 Julai 2024 19:43:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Juliet Akoth Ojwang]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23194526/Screenshot-2025-09-23-224502-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=488</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Haki ya Tabianchi, Hali ya Hewa, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Plastiki, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika miaka ya karibuni vijana kutoka ulimwenguni kote wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Vijana hawa wenye viwango mbalimbali vya elimu katika masuala hayo wamefanya kazi kubwa ya kuelimisha na kuhamasisha vijana wengine wa rika yao ili washiriki kikamilifu katika kampeni mbalimbali za kuhakikisha kuwa maisha yajayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/" data-wpel-link="internal">Jinsi vijana ndugu walivyolinusuru Ziwa Victoria kutokana na hatari ya plastiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika miaka ya karibuni vijana kutoka ulimwenguni kote wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Vijana hawa wenye viwango mbalimbali vya elimu katika masuala hayo wamefanya kazi kubwa ya kuelimisha na kuhamasisha vijana wengine wa rika yao ili washiriki kikamilifu katika kampeni mbalimbali za kuhakikisha kuwa maisha yajayo yanakuwa endelevu. Mfano mzuri ni vijana kutoka familia moja huko Kenya, Michelle na Jeremy Muchilwa,  wenye umri wa miaka 19 na 16, ambao walianzisha shirika la Osiepe Sango (Marafiki wa Ziwa Victoria) lenye lengo la kuondoa uchafu wa plastiki katika Ziwa Victoria ambalo ndilo kubwa kuliko maziwa yote ya maji safi barani Afrika. Ziwa hili pia limetanda katika nchi tatu za Afrika Mashariki; Kenya, Uganda na Tanzania. Wakati ugonjwa wa UVICO-19 ulipojitokeza mwaka 2020, mwezi Machi, shule nchini Kenya zilifungwa. Michelle alikuwa na umri wa miaka 15 na Jeremy miaka 12. Vijana hao waliona hii kama fursa kwao na waliporuhusiwa na wazazi wao, walijikita katika mambo waliyoyapenda badala ya kuendelea na masomo kwa njia ya mtandao. Jeremy alizama katika mambo ya teknolojia ambayo alikuwa akiyapenda, akijifunza kutengeneza programu mbalimbali. Michelle alijikita kwenye mifumo mbalimbali ya kiteknologia kupitia programu ya TED-Ed art school, ambayo ilimpa mwanga kuhusu bayoanuai, ikolojia na masuala ya mazingira katika ulimwengu. Somo moja kuhusu maji lilijadili umuhimu wa bahari, mifumo ya vyanzo vya maji baridi na kuonyesha uchafuzi unaotokana na takataka za plastiki. Michelle alihamasika na akapata habari za Ocean Heroes Boot Camp, mafunzo kuhusu uchafuzi wa mazingira unaotokana na takataka za plastiki na akaomba kushiriki. Alimshawishi pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Bomba la mafuta la Afrika Mashariki latupiwa lawama kwa kuharibu makaburi </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/11/14/bomba-la-mafuta-la-africa-mashariki-latupiwa-lawama-kwa-kuharibu-makaburi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/11/14/bomba-la-mafuta-la-africa-mashariki-latupiwa-lawama-kwa-kuharibu-makaburi/#respond</comments>
					<pubDate>14 Novemba 2023 13:40:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Justin Catanoso]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/24140752/Screenshot-2025-09-24-164647-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=495</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira, Miti, Miundombinu, Nishati, Siasa, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uchumi, Ukataji Miti, Utawala, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti ya hivi karibuni illiyochapishwa na shirika la kimataifa linalojumuisha watu wa imani tofauti na linalotetea haki sawa ya kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi, GreenFaith, linadai kuwa Bomba la Mafuta la Afrika Mashariki (EACOP) litaharibu au kunajisi makaburi yapatayo 2,000 katika maeneo litakapopita kutoka Ziwa Albert nchini Uganda hadi bandari ya Tanga iliyopo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/11/14/bomba-la-mafuta-la-africa-mashariki-latupiwa-lawama-kwa-kuharibu-makaburi/" data-wpel-link="internal">Bomba la mafuta la Afrika Mashariki latupiwa lawama kwa kuharibu makaburi </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti ya hivi karibuni illiyochapishwa na shirika la kimataifa linalojumuisha watu wa imani tofauti na linalotetea haki sawa ya kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi, GreenFaith, linadai kuwa Bomba la Mafuta la Afrika Mashariki (EACOP) litaharibu au kunajisi makaburi yapatayo 2,000 katika maeneo litakapopita kutoka Ziwa Albert nchini Uganda hadi bandari ya Tanga iliyopo nchini Tanzania. Lakini kampuni ya mafuta ya Kifaransa, TotalEnergies, inapinga madai hayo na kusema kwamba inafuata taratibu za kimataifa za kubaini, kutambua na kushughulikia makaburi, na maeneo mengine muhimu ingawa jamii zinazoishi katika njia litakazopita bomba hilo wamelieleza GreenFaith kuwa kampuni hiyo haisikilizi wala kutilia maanani maoni na wasiwasi wao kuhusu utunzaji wa makaburi. Kuanzia Januari hadi Septemba mwaka huu, GreenFaith walifanya uchunguzi katika wilaya sita nchini Uganda na wilaya tatu nchini Tanzania katika njia yenye urefu wa kilometa 1,441 (maili 895) na kuongea na wakazi wengi ambao ni wenyeji wa maeneo hayo. Katika ripoti yenye kurasa 37, ambayo ilichapisha mwezi Novemmba, shirika hilo linadai kuwa wanaosimamia mradi huo wa bomba la mafuta wanafahamu kuwa mradi huo utaathiri maelfu ya makaburi na sehemu “takatifu” na wametoa majibu yasiyoridhisha au kulipa fidia ndogo kwa waathirika. “Wenyeji wametueleza kuwa TotalEnergies wamekuwa wakiharibu makaburi ya familia zao au ya ukoo mara kwa mara. Uharibifu huu umekuwa ukiendelea hata baada ya wenyeji kuwatahadharisha TotalEnergies kuhusu makaburi hayo na kutoridhishwa kwao na kinachoendelea,” ripoti hiyo inaeleza. EACOP inakiri kuwa makaburi zaidi ya 2,000 yataathiriwa na ujenzi wa bomba hilo la mafuta. Wenyeji wanasema hiyo ni idadi ndogo kwani huenda kuna&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/11/14/bomba-la-mafuta-la-africa-mashariki-latupiwa-lawama-kwa-kuharibu-makaburi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/11/14/bomba-la-mafuta-la-africa-mashariki-latupiwa-lawama-kwa-kuharibu-makaburi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>