<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=mamalia&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/mamalia/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 14:23:41 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/#respond</comments>
					<pubDate>18 Agosti 2026 06:16:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Rice]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/18060350/Screenshot-2026-08-18-090213-768x492.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2511</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika ya Kati, Angola, Asia, Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Tanzania, Vietnam, na  Zambia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Cites, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Spishi, Tembo, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu uliopangwa, na  Usafirishaji wa Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo alikamatwa pia. Mshukiwa huyo alikuwa amehukumiwa mwaka 2019 kwa kumiliki zaidi ya kilo 200 (karibu paundi 441) za pembe za ndovu, na mwaka 2020 alipewa kifungo cha miaka mitano gerezani. Hata hivyo, aliachiwa huru baada ya miezi michache tu, na tangu wakati huo amekuwa akiendelea na biashara hiyo haramu. Zambia imekuwa ikitumiwa vibaya na mitandao ya wahalifu tangu angalau mwaka 2002, na sasa iko tena chini ya mwanga wa uchunguzi. Kinachosumbua hasa ni ushiriki wa makundi ya wahalifu kutoka Kongo, ambayo yanafanya kazi kwa uhuru mkubwa ndani ya Zambia na nchi jirani. Makundi hayo yanakusanya na kusafirisha bidhaa za wanyamapori — pembe za ndovu za tembo, pembe za kifaru, magamba ya pangolin na paka wakubwa — kupitia njia ngumu za kimataifa kuelekea Asia, huku Vietnam mara nyingi ikitumika kama kituo muhimu cha kupitishia. Mitandao hii inajinufaisha na ukosefu wa nia ya kisiasa, utekelezaji dhaifu wa sheria, maafisa wafisadi na jamii zilizotengwa. Inaandaa misafara ya ujangili katika nchi jirani na kutumia wasuluhishi wa Zambia kupanua minyororo yake ya biashara haramu. Ukamataji wa Zambia — ukijumlishwa na matukio mawili ya ukamataji mkubwa uliofanywa Tanzania na Botswana mnamo Aprili na Mei mtawalia — unaleta jumla ya pembe za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>11 Agosti 2026 20:01:52 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/11191616/Main-Mnyama-Nguva-akiwa-baharini-Picha-na-Mtandao-wa-Jamii-Forums-Tanzania.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2426</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia wa Baharini, Mamalia Wakubwa, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tabia za Wanyama, Teknolojia na Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Ustawi wa Wanyama, Uzuri wa Kiikolojia, Wanawake katika Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo sasa ni marehemu. Siku hiyo watu walipika na kuila nyama yake. Mimi sikuweza kuila kwa sababu niliposhika nyama yake, mwili wangu ulianza kuwasha,” alisema Juma. Amiri Juma, mvuvi kutoka kijiji cha Kibuyuni Kaunti ya Kwale akiwa katika ofisi ya BMU cha Kibuyuni. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kwa mujibu wa Juma, hilo lilikuwa tukio la kawaida, kwani hakukuwa na uelewa kuhusu umuhimu wa kumhifadhi nguva. Anasema ilikuwa rahisi sana kuwaona nguva, na hii pia ilikuwa ishara nzuri kwa wavuvi kuwa bahari ilikuwa na samaki wengi. Juma anaamini kutoweka kwa mnyama huyo baharini kumechochewa na shughuli nyingi za uvuvi. “Bahari imeingiliwa sana. Zamani kulikuwa na mitego tu. Sasa watu wanaingia kila sehemu, usiku na mchana. Wanyama wengi wamepotea. Hata samaki wamepungua,” anasema. Hapo zamani nguva alikuwa kitoweo kitamu sana kwa familia nyingi eneo la pwani, kabla ya kuwekwa kwa sheria inayopiga marufuku kumkamata. Faki Kassim, mvuvi kutoka kijiji cha Bodo, Kaunti ya Kwale, anasema takriban miaka 30 iliyopita, yeye na wavuvi wenzake walikuwa wakishika nguva, kumchinja na kuuza nyama yake. “Nguva ana ngozi ngumu sana. Nyama yake ni nyekundu na yenye mafuta mengi. Miaka mingi iliyopita tulikuwa tukiuza kipande kimoja cha nyama yake kwa shilingi moja,” anasema. Anaeleza kuwa kabla ya kumchinja nguva, walilazimika kutekeleza itikadi zao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 12:20:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23122231/park-7-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2193</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Maliasili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira, Mgogoro wa Rasilimali, Sheria, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uanaharakati, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Kitropiki, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Misitu, Uokoaji wa Wanyamapori, Usimamizi Endelevu wa Misitu, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Utowekaji wa Misitu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande zote katika kesi hiyo ili kuandaa na kuwasilisha ripoti mahakamani. Katika taarifa iliyotumwa kwa Mongabay, shirika la Save the Nairobi National Park (SaveNNP) lililaani kile lilichokiita &#8220;vitisho na vitendo vya kutisha&#8221; kutoka kwa maafisa wa KWS, pamoja na hatua ya kuwanyima wanaharakati hao ruhusa ya kuingia katika eneo la ziara. SaveNNP ilisema hatua hiyo inapingana na mwaliko wa KWS kwa vyombo vya habari kushiriki katika ziara hiyo ya mahakama. Ujenzi unaendelea katika maeneo yanayobishaniwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nairobi huku Mahakama ya Mazingira na Ardhi ikiendelea kusikiliza kesi iliyowasilishwa na wanaharakati wa mazingira. Picha kwa hisani ya SaveNNP. Mongabay iliona barua ya KWS iliyowaalika wanahabari kuhudhuria ziara ya eneo hilo iliyoongozwa na Msajili wa Mahakama ya Mazingira. Katika taarifa yao, SaveNNP na JustAct ziliishutumu KWS kwa kutaka &#8220;kudhibiti simulizi&#8221; kuhusu mradi huo na kuhakikisha sauti za Wakenya hazisikiki mahakamani wala kupitia vyombo vya habari wakati wa ukaguzi wa eneo hilo. Madai kama hayo pia yalitolewa na Friends of Nairobi National Park. Msemaji wa KWS, Duncan Wanyama, alisema wageni hao hawakuzuiwa kuingia, na kwam ba askari wa wanyamapori walikuwa wakitekeleza tu taratibu za kawaida zinazotumika ndani ya hifadhi hiyo, vyombo vya habari vya ndani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali aondolewa adhabu ya kifungo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/#respond</comments>
					<pubDate>01 Julai 2026 12:04:12 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/29121017/meno-ya-tembo-3.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1945</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Ikolojia, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Tembo, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu uliopangwa, Uhalifu wa Mazingira, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi imemuondolea adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela Elvis Kalonga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali kwa sababu ya dosari na mkanganyiko uliobainika katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Jaji Mfawidhi, Godfrey Isaya ilitoa hukumu Juni 16,2026 baada ya kusikiliza rufani iliyowasilishwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/" data-wpel-link="internal">Aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali aondolewa adhabu ya kifungo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Masjala Ndogo ya Katavi imemuondolea adhabu ya kifungo cha miaka 20 jela Elvis Kalonga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali kwa sababu ya dosari na mkanganyiko uliobainika katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Jaji Mfawidhi, Godfrey Isaya ilitoa hukumu Juni 16,2026 baada ya kusikiliza rufani iliyowasilishwa na Kalonga dhidi ya Jamhuri akipinga kutiwa hatiani pamoja na adhabu aliyopewa Awali, Mahakama ya Wilaya ya Mlele ilimhukumu Kalonga kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa manne ya kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria, pamoja na kosa la kuingia hifadhi ya taifa bila kibali na kubeba silaha ndani ya hifadhi. Ilidaiwa kwamba Novemba 8, 2025, askari wa Hifadhi ya Taifa ya Katavi walimkamata Kalonga katika eneo la Kasandalala ndani ya hifadhi hiyo akiwa hana kibali na akiwa na silaha mbalimbali zikiwemo panga, shoka, vipande vya nondo, goroli na unga wa baruti. Pia alidaiwa kukutwa na nyama na viungo vya wanyamapori vinavyokadiriwa kuwa na thamani ya TSh17,800,000. Sehemu ya ushahidi wa Jamhuri Upande wa mashtaka ulidai kuwa mshtakiwa alikamatwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi akiwa na nyara za Serikali na vifaa vinavyohusishwa na uwindaji haramu. Kwa mujibu wa ushahidi uliotolewa mahakamani, Novemba 8, 2025 askari wanyamapori Joel Kabuga ambaye alikuwa shahidi wa pili (PW2), Christian Ruyemamu (PW3) na Rahimu Hamadi Yusuf (PW4) wakiwa doria eneo la Kasandalala ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Katavi waliona moshi ukitoka porini. Mashahidi hao kwa nyakati tofauti wakidai kuwa walipofuatilia chanzo cha moshi huo walikuta watu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/aliyetiwa-hatiani-kwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali-aondolewa-adhabu-ya-kifungo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/#respond</comments>
					<pubDate>01 Julai 2026 10:25:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/01114338/Screenshot-2026-07-01-144315.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1958</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Uwindaji, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mahakama Kuu ya Tanzania yampa dhamana anayedaiwa kukutwa na nyara za Serikali</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam imempa dhamana Mohamed Hamad Sulemani, anayekabiliwa na mashtaka ya uhujumu uchumi yanayohusisha kufanya biashara haramu ya nyara za Serikali zenye thamani zaidi ya TSh bilioni 2.9 ($1,104,763). Mahakama hiyo mbele ya Jaji Amold Kirekiano ilitoa uamuzi Juni 15, 2026 baada ya kusikiliza maombi ya dhamana yaliyowasilishwa na Mohammed dhidi ya Jamhuri. Sulemani anakabiliwa na mashtaka matatu, shtaka la kuongoza genge la uhalifu, kushiriki biashara haramu ya nyara na kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria, akiwa pamoja na washtakiwa wengine watatu katika kesi ya Uhujumu Uchumi namba 10770 ya mwaka 2026 inayosikilizwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam. Katika maombi yake ya dhamana, Wakili wa mshtakiwa, Meschack Dede, aliiomba Mahakama Kuu izingatie kuwa makosa yanayomkabili mteja wake yanadhaminika na kwamba thamani ya mali inayodaiwa, nusu ihesabiwe kwa kugawanywa kwa washtakiwa wote wanne. Ombi la wakili lapita Upande wa Jamhuri haukupinga ombi hilo la wakili na wala haukuwasilisha kiapo cha kupinga maombi. Wakili wa Serikali Grace Kibaki aliiomba mahakama izingatie hati ya mashtaka pamoja na masharti ya Sheria ya Uhujumu Uchumi kuhusu utoaji wa dhamana. Baada ya kusikiliza maombi hayo, Jaji Kirekiano alikubali kumpatia mwombaji dhamana kwa kuzingatia masharti ya kisheria kuhusu kiwango cha fedha kinachotakiwa kuwekwa mahakamani. Alisema kifungu cha 36(5)(a) cha Sheria ya Uhujumu Uchumi kinamtaka mshtakiwa kuweka fedha taslimu au mali yenye thamani ya nusu ya fedha au mali inayohusika katika kosa. Jaji alitegemea maamuzi ya awali ya mahakama, ikiwemo kesi ya Arafat&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/01/mahakama-kuu-yampa-dhamana-anayedaiwa-kukutwa-na-nyara-za-serikali/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/#respond</comments>
					<pubDate>22 Juni 2026 19:12:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23161035/KESI-YA-MENO-YA-TEMBO-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1907</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Matumizi ya Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu wa Mazingira, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, Wanyama Wanaowinda, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo iliyokaa kortini kwa miaka kumi yaendelea kusikilizwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ile kesi ya kukutwa na meno ya tembo ambayo iko mahakamani kwa miaka 10 sasa huku watuhumiwa wakiendelea kusota rumande, imeendelea kusikilizwa katika Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu, Jijini Dar es Saalam. Washtakiwa walifikishwa mahakamani kwa mara ya kwanza mwaka 2018, na kusomewa mashtaka yao mbele ya Hakimu Mkazi Maira Kasonde. Baada ya kusomewa mashtaka, shauri lilifutwa, lakini muda mfupi baadaye wakasomewa mashtaka upya mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi Augustine Rwizile, ambaye sasa hivi ni Jaji wa Mahakama Kuu ya Tanzania. Washitakiwa walikuwa 11 Wakati kesi inaanza, washitakiwa walikuwa 11, lakini idadi hiyo ilipungua baada ya washtakiwa watano kuingia kwenye maridhiano na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP), ambapo walikiri makosa yao na kuachiliwa baada ya kutimiza makubaliano waliyoafikiana. Washtakiwa waliobakia katika shauri hilo ni Victor Mawanda, Mussa Abdallah, Abbas Jabu, Haruna Kasa na Halfani Kahengele. Awali ilidaiwa katika hati mashtaka kuwa kati ya Januari mwaka 2006 na Juni mwaka 2016, washtakiwa walipanga njama ya kuongoza genge la uhalifu Jijini Dar es Salaam. Walidaiwa kuuza, kupokea, kununua, kuhamisha, kusafirisha na kumiliki vipande 660 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 4,656,795,000 ambayo ni nyara za serikali. Ilidaiwa pia kuwa kati ya Aprili mosi na Juni 24 mwaka 2016, maeneo ya Mbezi Msakuzi wilayani Ubungo, washtakiwa walikutwa wakimiliki vipande hivyo vya meno ya tembo bila kuwa na kibali ama leseni kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori. Washitakiwa walikana mashitaka na wako gerezani kwa kuwa kesi yao ya uhujumu uchumi haina dhamana. Korti kusikiliza shahidi wa 10 Hadi sasa shauri hilo limeshasikilizwa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/22/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-iliyokaa-kortini-kwa-miaka-kumi-yaendelea-kusikilizwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/#respond</comments>
					<pubDate>21 Juni 2026 17:13:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dann Okoth]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/21164857/Screenshot-2026-06-21-194344.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1898</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Filosofia ya Uhifadhi, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mamalia, na  Mamalia Wakubwa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa Barabara Kuu ya Kasi ya Nairobi-Mombasa (Nairobi Mombasa Expressway &#8211; NME), barabara ya njia mbili itakayojengwa sambamba na Reli ya Kisasa (SGR), mpango wa Twiga Tracker Initiative uliwatia alama twiga 20 (majike 11 na madume 9) ili kufuatilia mienendo na matumizi ya maeneo ya twiga wa Maasai katika ukanda wa Nairobi-Mombasa kabla, wakati na baada ya ujenzi huo ndani ya Eneo la Uhifadhi la Tsavo. Kupitia teknolojia bunifu za ufuatiliaji, na kwa ushirikiano na mfumo wa EarthRanger, programu ya wakati halisi inayosaidia juhudi za uhifadhi wa wanyamapori, watafiti waliwafunga twiga vifaa vyepesi vya GPS vilivyounganishwa na setilaiti kwenye mikia yao ili kupata taarifa muhimu kuhusu namna wanavyohama, jinsi wanavyotumia makazi yao, na athari za shughuli za binadamu kwa mienendo yao. Mpango wa Twiga Tracker, unaotekelezwa na Giraffe Conservation Foundation (GCF), kwa sasa unafuatilia twiga tisa katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki, wanane katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi na watatu katika ranchi za Taita. Shirika la GCF lilitekeleza zoezi hili kwa ushirikiano na Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS), Tsavo Trust, Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyamapori (WRTI), Wildlife Works na Sheldrick Wildlife Trust. Kwa mujibu wa GCF, Eneo la Uhifadhi la Tsavo ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/#respond</comments>
					<pubDate>19 Juni 2026 16:08:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/19153844/Screenshot-2026-06-19-182917-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1891</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bioanuai, Bioanuai ya Misitu ya Mvua, Bustani za wanyama, Chakula, Cites, Elimu, Elimu ya Mazingira, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Huduma za Mazingira, Idadi ya watu, Ikolojia, Jamii Asili, Jamii ya Nyani Wakubwa, Jamii za Misitu ya Mvua, Kijani, Makazi, na  Mamalia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, ulio katikati mwa DRC. Dhamira yao ni kuwashawishi bonobo (Pan paniscus) kukubali uwepo wa binadamu kama sehemu ya asili ya mazingira yao. Kwa kupata uaminifu wa wanyama, watafiti wanatumai kuunda fursa za kuelewa vyema tabia, ikolojia na afya zao. Mchakato huu wenye bidii wa kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu unahusisha kutumia wakati karibu na nyani siku baada ya siku hadi watakapozoea watu hatua kwa hatua. Ni kazi ya polepole na inayohitaji juhudi kubwa ambayo inaweza kuchukua miaka, inayohitaji uvumilivu, uthabiti na maelfu ya masaa msituni. Muda mrefu kabla ya mapambazuko, mara nyingi karibu saa 3 alfajiri, wafuatiliaji, baadhi yao wakiwa wawindaji haramu wa zamani, ambao ujuzi wao kuhusu msitu umekuwa rasilimali muhimu ya uhifadhi, wanaanza kuelekea kwenye eneo la viota usiku uliopita. Ni lazima wafike kabla kundi hilo la bonobo halijaamka. Kisha huanza harakati za kutwa nzima kupitia moja ya misitu ya mvua iliyo mbali zaidi Duniani, kufuatia nyani kutoka alfajiri hadi wajenge viota vipya kwa ajili ya usiku. &#8220;Wazo zima la kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu ni kukutana nao kila siku kwa njia ya kirafiki sana, isiyo ya mwingiliano ili wakukubali kama sehemu ya msitu,&#8221; anasema Felix Bofeko, mtafiti msaidizi anayefanya kazi na programu ya mazoea ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2026 18:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/10161044/Meno-ya-tembo-2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1830</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Kupambana na ujangili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Sheria ya Mazingira, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mwasha. Akiwakilisha upande wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Florida Wenceslaus aliomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa kile alichoeleza kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika. Mshtakiwa, ambaye anaendelea kusota rumande, hakuwepo mahakamani leo kama ilivyokuwa wakati kesi hiyo ilipotajwa Mei 25, na pia hakuwa na mwakilishi. Hakimu Mwasha alikubali ombi la upande wa mashitaka na akaahirisha shauri hilo hadi Juni 23 mwaka huu, kesi itakapotajwa tena. Mshtakiwa Ra alipanda kizimbani kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa Mei mwaka huu. Shauri lilipotajwa baada ya siku 14, yaani Mei 25 mwaka huu, mshtakiwa huyo hakufikishwa mahakamani na badala yake shauri liliahirishwa bila yeye kuwepo. Kabla ya kuahirisha kesi hiyo, hakimu aliamuru hati ya kumfikisha mshtakiwa kortini itolewe ili kesi itakapotajwa Juni 9, 2026, mshtakiwa aletwe kortini. Hata hivyo leo mshtakiwa hakufikishwa kortini na hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa kwa nini mshatakiwa hakuwepo. Awali upande wa Jamhuri ulidai katika hati ya mashtaka kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali na kujihusisha na biashara hiyo bila kibali. Ilidaiwa kuwa Aprili 19, 2026 katika eneo la Hoteli ya Golden Tulip–Masaki,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 15:48:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Benjamin Jumbe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03150618/Screenshot-2026-06-03-180555-768x498.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1759</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi ya jamii inayolenga kupunguza uharibifu wa misitu na kuongeza ufahamu wa masuala ya mazingira, pamoja na timu ya maskauti wa jamii 18 katika upande wa Kenya wa mlima, sehemu ya Mradi wa Tembo wa Mlima Elgon unaotekelezwa na Shirika la Wanyamapori la Afrika Mashariki. Mwenyekiti wa wakfu wa MEF, Chris Powles, aliiambia Mongabay kwamba mnamo mwaka 2022, maskauti walifuatilia tembo wanne wakivuka mto Suam, ambao unaashiria mpaka kati ya nchi hizo mbili. Picha za video zilizorekodiwa kwa ndege isiyo na rubani zikionyesha tembo upande wa Uganda wa Mlima Elgon. Picha kwa hisani ya UWA. Katika mahojiano kupitia barua pepe, Powles alisema sababu kadhaa zinaweza kuelezea kurudi kwa tembo, ingawa haiwezekani kusema kwa uhakika ni nini kiliwachochea kurejea katika eneo hilo. &#8220;[Hizi] ni pamoja na ongezeko la idadi ya tembo upande wa Kenya, kuongezeka kwa shinikizo la binadamu kwa upande wa Kenya, usalama wanaoupata wakiwa upande wa Uganda, ambako eneo hilo lote liko ndani ya mbuga ya taifa, tofauti na upande wa Kenya,&#8221; aliandika. &#8220;Na, labda, tembo walio hai tangu wakati wengine wao waliuawa nchini Uganda sasa wamekufa kawaida na hivyo huenda kumbukumbu ya hatari zilizowakabili nchini Uganda imefifia kadri vizazi vilivyobadilika.&#8221; Mwishoni mwa miaka ya 1970 na mwanzoni mwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/#respond</comments>
					<pubDate>10 Mei 2026 21:34:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/08205611/Screenshot-2026-05-08-235542-768x500.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1539</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, na  Kusini mwa Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Biashara ya Wanyamapori ya China, Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mamalia, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu kwa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utafiti, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini zao huku wakinufaika kutokana na mauzo ya mtandaoni ya spishi za wanyama wanaolindwa huku wanyama hawa wakipungua porini. &#8220;Ni soko kubwa zaidi la wanyamapori,&#8221; alisema mtafiti wa biashara ya wanyamapori Chris Shepherd kutoka Kituo cha Biolojia Anuwai. &#8220;Ni rahisi, unaweza kufanya kazi bila kujulikana ukiwa nyumbani kwako. Hakuna gharama za kuanzisha duka.&#8221; Biashara ya mtandaoni katika bidhaa haramu za wanyamapori inaendelea kukua, ikihusisha spishi zaidi na jiografia pana. Ni tasnia haramu inayoendeshwa na mitandao ya uhalifu iliyopangwa vizuri, na ni vigumu kushtaki. Kukamata wahalifu mtandaoni ni changamoto sana. &#8220;Masoko ya wanyamapori yamehamia kutoka maeneo halisi hadi maeneo ya mitandaoni, na hiyo inaakisi mwelekeo mpana zaidi wa uchumi wa dunia,&#8221; alisema Simone Haysom, mkurugenzi wa programu za uhalifu wa kimazingira katika shirika lenye makao yake makuu Uswizi la Global Initiative Against Transnational Organised Crime. Katika ripoti ya hivi karibuni, Haysom na mwenzake Russell Gray walichanganua data ya biashara ya wanyamapori mtandaoni kuanzia mwezi wa Aprili 2024 hadi mwezi Machi 2026. Waliangazia mataifa 10 katika mabara matatu, mahali ambapo uhalifu wa kimazingira na matumizi ya intaneti ni mkubwa, na kuyafanya kuwa mazingira yanayochochea biashara ya wanyamapori mtandaoni. Walipata bidhaa 266,535 za wanyamapori zilizochapishwa kwenye masoko 61 ya mitandaoni, yenye thamani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>05 Mei 2026 22:27:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David AkanaRhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/05212300/Screenshot-2026-05-06-000526-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1504</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na  Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maendeleo Endelevu, Mamalia, Mazingira, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Mvua, Uhifadhi, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, volkeno, misitu, na ardhi oevu ndani ya eneo moja lililohifadhiwa. Pia ipo ndani ya mazingira iliyoundwa kwa miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu, ambapo makundi yaliojihami kwa silaha, uchumi usio rasmi, na utawala dhaifu ni sehemu ya maisha ya kila siku. Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga. Picha kwa hisani ya Bitini Ndiyanabo Kanane. Emmanuel de Merode, ambaye ameiongoza Virunga tangu mwaka wa 2008, haanzii na ikolojia. Mafunzo yake ni ya anthropolojia, hali inayounda namna anavyoelezea hifadhi. Anapendekeza kuwa hali ya wanyamapori hutokana na nguvu za kina. Upotevu wa misitu, ujangili, na ukosefu wa usalama sio shida za mazingira pekee. Yanatokana na namna watu wanavyopata riziki, namna mamlaka inavyofanya kazi, na jinsi pesa na rasilimali zinavyozunguka. Katika sehemu ya Mashariki mwa Kongo, uhifadhi hauwezi kutenganishwa na uchumi. Kwa jamii nyingi zinazoizunguka Virunga, chaguo lao ni la haraka. Kuifyeka misitu kwa ajili ya ukulima au kutengeza mkaa kunaweza kuzalisha kipato cha kuendesha maisha. Faida za uhifadhi ni ngumu kuonekana na mara nyingi huonekana zaidi nje ya eneo hilo. Ukosefu wa usawa unajitokeza katika maamuzi ya kila siku kuhusu mafuta, chakula na upatikanaji wa ardhi. Kama De Merode anavyoelezea, mfumo unawalazimisha baadhi ya watu maskini zaidi kubeba gharama ya kulinda mali zinazothaminiwa kimataifa. Shinikizo kwenye mbuga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/#respond</comments>
					<pubDate>21 Aprili 2026 00:42:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20151506/Screenshot-2026-04-20-165755-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1399</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kaskazini mwa Kenya, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni mzunguko usiokwisha wa kutafuta malisho na maji. Lakini ndani ya moyo wa jangwa hili, kumeibuka hadithi inayopinga mantiki ya asili &#8211; ya upendo uliopitiliza, hatari iliyojificha, na mipaka inayofifia kati ya binadamu na mnyama mwitu mwenye kasi kubwa. Ni hadithi ya Bishara Abdirahman Omar, mama wa watoto tisa, ambaye kwa zaidi ya miaka miwili alifanya jambo ambalo wengi wangeliona kama hukumu ya kifo. Mama huyu aliishi na duma ndani ya nyumba kama sehemu ya familia yake. Bishara anakumbuka siku hiyo kwa uwazi kabisa, kana kwamba ilitokea jana. Ilikuwa ni asubuhi yenye joto kali, na yeye alikuwa akitembea porini kutafuta kuni na kuangalia mifugo yake. Katika kichaka kimoja cha miiba, alisikia sauti dhaifu; kilio kidogo kilichofanana na kile cha mtoto wa paka aliyeishiwa nguvu. Aliposogea, alimkuta mtoto wa duma, akiwa mdogo kiasi cha kutoshea kwenye viganja vyake, macho yake yakiwa bado na ukungu wa upofu wa utotoni. “Alikuwa hana msaada kabisa. Nilimwangalia, nikatazama huku na huko nikitarajia kumuona mama yake, lakini hapakuwa na dalili yoyote. Alikuwa ameachwa peke yake kufa kwa njaa au kuliwa na fisi,” Bishara alisimulia, huku akitazama upeo wa macho. Kwa Bishara, hakuona mnyama hatari, bali aliona kiumbe aliyehitaji maziwa na joto. Bila&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 15:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Gerald Ahairwe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20185806/IMG_5205-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1409</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Maji, Mamalia, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchimbaji wa Mafuta, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru wa kuandamana. Saa nne asubuhi, ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Buganda Road, Katikati mwa jiji la Kampala nchini Uganda, wanaharakati wa mazingira na wanafunzi wanane walifikishwa kizimbani. Wanafunzi hao wanatoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini Uganda, na wamekuwa gerezani tangu Agosti 1, 2025, baada ya kukamatwa wakiandamana kupinga mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP. Nje ya Mahakama, kulikuwa na rasharasha za mvua. Wasiwasi ulitanda miongoni mwa wanafunzi wa vuguvugu la “Students Against EACOP” waliokuwa wamefika pale ili kuhudhuria hukumu ya Mahakama hiyo dhidi ya wenzao. Hakimu Mkazi alitangaza kuahirishwa kwa hukumu yao hadi saa nane mchana. Lakini nyakati za chakula cha mchana, kabla ya saa nane, wanafunzi walio nje waliambiwa kwamba wenzao wanane wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma (common nuisance). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Sylvia Muwonge katika chumba chake kwenye Mahakama ya Buganda Road. Mawakili, umma au hata waandishi wa habari hawakuhudhuria. Upande wa utetezi umepinga hukumu hiyo, ukisema kuwa wanafunzi hao wamenyimwa haki ya kupewa dhamana, na vile vile kunyimwa nafasi ya kuridhisha kujitetea. Kato Tumusiime, wakili wa wanaharakati hao, anaelekeza kidole cha lawama kwa upendeleo uliokuwepo katika kesi hiyo tangu mwanzo. “Hukumu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/#respond</comments>
					<pubDate>07 Aprili 2026 13:39:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/15164710/Screenshot-2026-04-15-194412-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1359</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi wa Ritz-Carlton, Masai Mara Safari Camp, inayoendeshwa na Lazizi Mara Ltd. “Mahakama inaona haina mamlaka ya kushughulikia suala hili kwa sababu kuna mifumo mbadala ya utatuzi wa migogoro ambayo haikutumiwa na mlalamikaji, hivyo kesi hii iliwasilishwa kabla ya muda wake, na mahakama imeondolewa mamlaka ya kuisikiliza. Bila mamlaka, mikono ya mahakama imefungwa,” uamuzi wa mahakama unasema. Uamuzi wa mahakama unaeleza kuwa mlalamikaji, kabla ya kufungua shauri, alipaswa kuwasilisha malalamiko chini ya Kifungu cha 117 cha Sheria ya Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori, ambacho kinataka njia zote za utatuzi, ikiwa ni pamoja na zile za kijamii, zitumike, na pia kukata rufaa chini ya Kifungu cha 129 cha Sheria ya Usimamizi na Uratibu wa Mazingira. Ili kupata taarifa zaidi, Mongabay iliwasiliana na mahakama ya Narok na mamlaka za kaunti, lakini hawakujibu ombi letu la kufanyiwa mahojiano. Kwa mtazamo wa wahifadhi wa mazingira kama Johnson Yiamat, uamuzi huo unatuma ujumbe usio sahihi. “Ninahisi kwamba matokeo ya kiutaratibu hayapaswi kufunika kiini cha hoja zilizowasilishwa,” alisema kupitia ujumbe aliotuma kwa Mongabay. Yiamat ni Mmasai na mwanzilishi wa Osotua Green Alliance, shirika linaloongozwa na jamii lililojikita katika masuala ya uhifadhi wa bioanuwai, hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na uwezeshaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Shughuli za eneo la mapumziko la kifahari kisiwani Pemba zinaendelea licha ya hofu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/10/shughuli-za-eneo-la-mapumziko-la-kifahari-kisiwani-pemba-zinaendelea-licha-ya-hofu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/10/shughuli-za-eneo-la-mapumziko-la-kifahari-kisiwani-pemba-zinaendelea-licha-ya-hofu/#respond</comments>
					<pubDate>10 Mechi 2026 20:26:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/22203304/Screenshot-2026-04-22-233211-768x474.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1423</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Bioanuai ya Misitu ya Mvua, Haki za Kimazingira, Kijani, Mabadiliko ya Tabianchi, Mamalia, Mazingira, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Misitu ya Mvua, Miti, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utawala, Wadudu, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mapema mwaka huu, wafanyakazi walijenga ukuta wa mzunguko kwa ajili ya hoteli ya kifahari katika kisiwa cha Pemba kando ya pwani ya Tanzania. Kuna taarifa chache za umma kuhusu maendeleo ya Mantuli, lakini ukuta huo upo mita mia chache tu magharibi mwa ardhi ya hekta 1,440 (sawa na ekari 3,558) ya Hifadhi ya Asili ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/10/shughuli-za-eneo-la-mapumziko-la-kifahari-kisiwani-pemba-zinaendelea-licha-ya-hofu/" data-wpel-link="internal">Shughuli za eneo la mapumziko la kifahari kisiwani Pemba zinaendelea licha ya hofu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mapema mwaka huu, wafanyakazi walijenga ukuta wa mzunguko kwa ajili ya hoteli ya kifahari katika kisiwa cha Pemba kando ya pwani ya Tanzania. Kuna taarifa chache za umma kuhusu maendeleo ya Mantuli, lakini ukuta huo upo mita mia chache tu magharibi mwa ardhi ya hekta 1,440 (sawa na ekari 3,558) ya Hifadhi ya Asili ya Msitu wa Ngezi-Vumawimbi, ambako wanasayansi wamegundua zaidi ya aina 80 za mimea katika miaka ya hivi karibuni, ambazo baadhi wanahofia zitatoweka kutokana na maendeleo hayo. Kulingana na bao la matangazo karibu na msitu na mipango iliyochapishwa awali kwenye tovuti ya kampuni ya Acoarch Architects iliyo na makao yake makuu Afrika Kusini, vyumba vya mapumziko, madimbwi ya kuogelea, kituo cha mazoezi ya mwili na sehemu za kahawa vitaenea kando ya umbali wa kilomita 3 (karibu maili 2) ya fukwe za Vumawimbi, kuwanyima wakazi wa kijiji cha Makangale kilicho karibu na bahari ufikiaji wa bahari hiyo. Baadhi ya maudhui ya mtandaoni yametolewa, na kampuni ya usanifu majengo haikujibu maswali ya Mongabay. Tim Caro ni mwanaikolojia wa mageuzi ambaye amefanya utafiti katika eneo hilo na ni mwanachama wa shirika la hisani lililosajiliwa nchini Uingereza, kwa jina la Friends of Ngezi, ambalo hufanya kazi na jamii na kukuza uhifadhi wa msitu. Alisema karibu theluthi moja ya wakazi wa Makangale hujihusisha na shughuli za uvuvi, wakifanya safari za kuvua na boti zao kutoka fukwe za Vumawimbi, ambazo pia ni sehemu maarufu ya kubarizi na burudani kwa wakazi wa kisiwani humo. &#8220;Kulingana na ripoti za kila wiki tunazozipokea kutoka kwa jamii,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/10/shughuli-za-eneo-la-mapumziko-la-kifahari-kisiwani-pemba-zinaendelea-licha-ya-hofu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/10/shughuli-za-eneo-la-mapumziko-la-kifahari-kisiwani-pemba-zinaendelea-licha-ya-hofu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yaomboleza Craig, jitu mpole aliyekuwa mmoja wa &#8216;Super tuskers&#8217; waliosalia barani Afrika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/kenya-yaaga-craig-jitu-mpole-aliyekuwa-mmoja-wa-super-tuskers-waliosalia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/kenya-yaaga-craig-jitu-mpole-aliyekuwa-mmoja-wa-super-tuskers-waliosalia/#respond</comments>
					<pubDate>04 Januari 2026 10:22:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/05163629/Screenshot-2026-01-05-193539.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=865</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Huduma za Mazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Maudhui ya mazingira yanayoonyesha mabadiliko chanya, Mazingira, Sera za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Tembo mashuhuri Craig, aliyekuwa mmoja wa wachache wanaojulikana kama “super tuskers” barani Afrika, ameaga dunia. Craig alifariki kwenye mbuga ya kitaifa ya Amboseli, kutokana na sababu za kiasili. Craig alizaliwa mwaka 1972 na tembo jike aliyefahamika kama Cassandra. Aliishi maisha yake yote katika tambarare za Amboseli, na kuwa jitu, pembe zake zikiwa na uzito wa zaidi ya kilo 45. Kila alipokuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/kenya-yaaga-craig-jitu-mpole-aliyekuwa-mmoja-wa-super-tuskers-waliosalia/" data-wpel-link="internal">Kenya yaomboleza Craig, jitu mpole aliyekuwa mmoja wa &#8216;Super tuskers&#8217; waliosalia barani Afrika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Tembo mashuhuri Craig, aliyekuwa mmoja wa wachache wanaojulikana kama “super tuskers” barani Afrika, ameaga dunia. Craig alifariki kwenye mbuga ya kitaifa ya Amboseli, kutokana na sababu za kiasili. Craig alizaliwa mwaka 1972 na tembo jike aliyefahamika kama Cassandra. Aliishi maisha yake yote katika tambarare za Amboseli, na kuwa jitu, pembe zake zikiwa na uzito wa zaidi ya kilo 45. Kila alipokuwa akitembea, pembe hizo zilipinda chini na kukaribia kugusa ardhi, hali iliyompa hadhi adimu ya “super tusker.” Taarifa ya rambirambi iliyotolewa na Shirika la Huduma za Wanyamapori la Kenya (KWS), ilisisitiza ulinzi maksudi na ushirikiano kati ya washirika wa uhifadhi na jamii asilia. “Ufuatiliaji wa mara kwa mara, juhudi za kupambana na ujangili, ulinzi wa makazi ya wanyamapori, pamoja na usimamizi na ulinzi kutoka kwa jamii, vilihakikisha kuwa Craig aliishi kwa uhuru na usalama,” KWS ilisema katika tovuti yake. Shirika hilo pia lilimtaja Craig kama “mnara hai wa urithi wa asili wa Kenya na Afrika.&#8221; African Wildlife Foundation (AWF) pia ilitoa heshima zake kupitia mitandao ya kijamii, huku ikigusia hisia za wengi waliomwomboleza. “Leo mandhari ya Amboseli inaonekana kimya zaidi. Kifo cha Craig kinaashiria mwisho wa enzi ya balozi wa kweli wa pori super tusker aliyekumbusha dunia kile kilicho hatarini katika juhudi za uhifadhi,” AWF iliandika. Hata ingawa mabadiliko ya tabianchi yanazidi kubana mandhari ya asili, na upotevu wa makazi ya wanyamapori kuwasukuma katika maeneo madogo zaidi, simulizi ya Craig ilileta matumaini. Akiwa hai, Craig aliwaunganisha watu. Tembo huyu amefanya vivyo hivyo hata katika kifo chake kwa jinsi alivyoingia katika fikra za umma. Kabla hajafa, wapiga picha na watalii walivuka mipaka na mabara&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/kenya-yaaga-craig-jitu-mpole-aliyekuwa-mmoja-wa-super-tuskers-waliosalia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/kenya-yaaga-craig-jitu-mpole-aliyekuwa-mmoja-wa-super-tuskers-waliosalia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Toka uhai hadi kifo: Maana ya maisha marefu ya Craig kwa uhifadhi wa tembo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/03/toka-uhai-hadi-kifo-maana-ya-maisha-marefu-ya-craig-kwa-uhifadhi-wa-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/03/toka-uhai-hadi-kifo-maana-ya-maisha-marefu-ya-craig-kwa-uhifadhi-wa-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>03 Januari 2026 14:40:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Rhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/07144420/Screenshot-2026-01-07-174336-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=907</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kifo cha mnyamapori maarufu huwa habari ya ajabu. Ni tukio linalogusa kwa karibu, kwa sababu kupitia picha na video, wengi walihisi kana kwamba walikuwa wamemfahamu. Hata hivyo, ukaribu huo huambatana na umbali fulani, kwani mnyama hana maisha ya umma zaidi ya simulizi na maana ambazo wanadamu humjengea. Kwa tembo, mvutano huo unachochewa na historia. Miili yao imegeuzwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/03/toka-uhai-hadi-kifo-maana-ya-maisha-marefu-ya-craig-kwa-uhifadhi-wa-tembo/" data-wpel-link="internal">Toka uhai hadi kifo: Maana ya maisha marefu ya Craig kwa uhifadhi wa tembo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kifo cha mnyamapori maarufu huwa habari ya ajabu. Ni tukio linalogusa kwa karibu, kwa sababu kupitia picha na video, wengi walihisi kana kwamba walikuwa wamemfahamu. Hata hivyo, ukaribu huo huambatana na umbali fulani, kwani mnyama hana maisha ya umma zaidi ya simulizi na maana ambazo wanadamu humjengea. Kwa tembo, mvutano huo unachochewa na historia. Miili yao imegeuzwa na kuwa bidhaa za anasa, makazi yao yamegeuzwa na kuwa maeneo ya maendeleo, na kuendelea kwao kuishi kumetumiwa kama kipimo ili kubaini kama uhifadhi unawezekana kwa kiwango kikubwa. Kwa sababu hii, habari za leo kutoka Kenya zilisambaa upesi. Craig, dume wa Amboseli aliyejulikana kwa pembe zake zilizokaribia kugusa ardhi, aliaga dunia akiwa na umri wa miaka 54. Makundi ya uhifadhi na mamlaka za wanyamapori yalisema tembo huyo alifariki kwa sababu za kawaida, baada ya kuonyesha dalili za dhiki usiku mzima, huku walinzi wakimfuatilia. Hatua zake za mwisho zilionekana kuashiria uzee wake zaidi kuliko vurugu, kwani alianguka mara kwa mara, huku akijaribu kusimama na kutembea kwa muda mfupi. Pia magego yake yaliyochakaa yalionyesha kwamba hakuwa tena akitafuna vizuri. Katika maisha ya tembo, meno mara nyingi huchora sura ya mwisho ya hadithi yao. Craig alikuwa mnyama maarufu. Kwa simulizi nyingi, alikuwa mmoja wa tembo walionaswa na kamera zaidi barani Afrika, na pengine “super tusker” anayejulikana zaidi. Craig alikuwa mmoja wa madume machache adimu yenye pembe zenye uzito wa zaidi ya kilo 45 kila moja. Mnyama huyo pia alijulikana kwa tabia. Alikuwa mtulivu karibu na magari na mvumilivu mbele ya kamera. Alivumilia umakini uliomfuata kwa namna ya kipekee. Sifa hiyo, pamoja na pembe alizobeba, ilimfanya kuwa ishara ya kile ambacho&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/03/toka-uhai-hadi-kifo-maana-ya-maisha-marefu-ya-craig-kwa-uhifadhi-wa-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/03/toka-uhai-hadi-kifo-maana-ya-maisha-marefu-ya-craig-kwa-uhifadhi-wa-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tembo wanaohama wapata nafasi ya kuzurura kupitia juhudi za uhifadhi wa jamii</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/14/tembo-wanaohama-wapata-nafasi-ya-kuzurura-kupitia-juhudi-za-uhifadhi-wa-jamii/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/14/tembo-wanaohama-wapata-nafasi-ya-kuzurura-kupitia-juhudi-za-uhifadhi-wa-jamii/#respond</comments>
					<pubDate>14 Oktoba 2025 06:11:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hillary Rosner]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/14073639/Screenshot-2025-11-14-092343-768x482.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kaskazini mwa Kenya, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Maendeleo ya Jamii, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Miundombinu, Tembo, Uhamishaji, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uwanja wa ndege unaotumika kila mara nje ya mji wa Archers Post, kaskazini mwa Kenya, ulifungwa baada ya kuharibiwa na mvua kubwa, kwa hiyo ndege yangu ilitua katika uwanja mdogo wenye vumbi ulio upande mwingine wa hifadhi ya kitaifa ya Samburu. Kutoka hapo, barabara ilielekea kusini kupitia ardhi ya malisho inayomilikiwa na jamii hadi lango [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/14/tembo-wanaohama-wapata-nafasi-ya-kuzurura-kupitia-juhudi-za-uhifadhi-wa-jamii/" data-wpel-link="internal">Tembo wanaohama wapata nafasi ya kuzurura kupitia juhudi za uhifadhi wa jamii</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uwanja wa ndege unaotumika kila mara nje ya mji wa Archers Post, kaskazini mwa Kenya, ulifungwa baada ya kuharibiwa na mvua kubwa, kwa hiyo ndege yangu ilitua katika uwanja mdogo wenye vumbi ulio upande mwingine wa hifadhi ya kitaifa ya Samburu. Kutoka hapo, barabara ilielekea kusini kupitia ardhi ya malisho inayomilikiwa na jamii hadi lango la magharibi la hifadhi, kando ya Mto Ewaso Ng’iro. Ilikuwa ni wiki moja tu kabla ya 2024, na Januari kwa kawaida ni mwanzo wa msimu wa kiangazi, lakini mvua bado ilikuwa haijapungua. Hifadhi hiyo, eneo linalolindwa lenye ukubwa wa Jimbo la Washington DC, &#8211; sehemu ya eneo kubwa zaidi la ardhi ya uhifadhi &#8211; ilikuwa utafiti wa kijani kibichi, ardhi ya tambarare na vilima vyake vilivyofunikwa na msukosuko wa mimea. Mara tu tulipovuka mpaka wa hifadhi, tulikuwa miongoni mwa tembo, kuanzia watoto wa umri mdogo wa miezi kadhaa hadi vijana wadogo na wachangamfu, wazee wanaoongoza, na fahali wakubwa. Walitanga huku na huku kwa miguu yao iliyofunikwa na ngozi na kwato za mviringo, wakisinzia, wakinyonyesha, wakipita mtoni, huku wakijimwagia vumbi. Kwenye joto la adhuhuri, walisimama kwenye vivuli vya miti ya migunga na kwa uvivu kung&#8217;oa vijiti vya kijani kibichi na vigogo vyao, kisha wakavitupa vinywani mwao. Bila ya wasiwasi na uwepo wa gari aina ya Land Cruiser niliyopanda; walitangatanga hadi kwenye gari, wengine wakiwa na urefu wa chini ya shina moja. Hizi zilikuwa siku za kutojali kwa tembo wa Samburu. Ilikuwa ni miaka miwili mirefu, migumu, yenye mauti kutokana na ukame uliokithiri, wakati wanyama wenye njaa walipokufa katika mazingira yaliyochakaa.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/14/tembo-wanaohama-wapata-nafasi-ya-kuzurura-kupitia-juhudi-za-uhifadhi-wa-jamii/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/14/tembo-wanaohama-wapata-nafasi-ya-kuzurura-kupitia-juhudi-za-uhifadhi-wa-jamii/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi Akili Bandia inavyosaidia wahifadhi kuwaelewa vizuri twiga na kuwalinda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/09/16/jinsi-akili-bandia-inavyosaidia-wahifadhi-kuwaelewa-vizuri-twiga-na-kuwalinda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/09/16/jinsi-akili-bandia-inavyosaidia-wahifadhi-kuwaelewa-vizuri-twiga-na-kuwalinda/#respond</comments>
					<pubDate>16 Septemba 2025 10:42:30 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Abhishyant Kidangoor]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/01104407/Screenshot-2025-10-01-134332-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=570</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Akili Mnemba, Mamalia, Mazingira, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Teknolojia, Teknolojia na Uhifadhi, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Uhifadhi, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Monica Bond na Derek Lee walianza kujenga mapenzi makubwa kwa twiga mnamo mwaka 2005, wakati walipotembelea nchi ya Uganda. Tangu wakati huo, wanasema dhamira yao ilikuwa wazi: kurudi Afrika na kuongoza “tafiti kubwa zaidi duniani kuhusu twiga.” Miaka mitano baadaye, wawili hao walishirikiana kuanzisha shirika lisilo la kiserikali la Wild Nature Institute, lenye makao yake nchini Tanzania, ambako twiga [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/16/jinsi-akili-bandia-inavyosaidia-wahifadhi-kuwaelewa-vizuri-twiga-na-kuwalinda/" data-wpel-link="internal">Jinsi Akili Bandia inavyosaidia wahifadhi kuwaelewa vizuri twiga na kuwalinda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Monica Bond na Derek Lee walianza kujenga mapenzi makubwa kwa twiga mnamo mwaka 2005, wakati walipotembelea nchi ya Uganda. Tangu wakati huo, wanasema dhamira yao ilikuwa wazi: kurudi Afrika na kuongoza “tafiti kubwa zaidi duniani kuhusu twiga.” Miaka mitano baadaye, wawili hao walishirikiana kuanzisha shirika lisilo la kiserikali la Wild Nature Institute, lenye makao yake nchini Tanzania, ambako twiga wa Masai (Giraffa tippelskirchi) ni mnyama wa taifa. Hapa, timu yao imejikita katika kutambua na kuwatambua twiga mmoja mmoja kwa kutumia muundo wa kipekee wa madoa kwenye miili yao. Kwa miaka kadhaa, timu yao ilikuwa inafanya kazi kwa mikono, lakini baadaye wakaanza kujaribu teknolojia mbalimbali. Hata hivyo, njia zote mbili hazikuwapa matokeo waliyokuwa wakiyatarajia. Kwa sasa, mifumo ya akili bandia (AI), iliyotengenezwa kwa ushirikiano na Microsoft kupitia maabara yao ya AI For Good Lab inawasaidia kuharakisha kazi hiyo. Mradi huo unaoitwa Project GIRAFFE (Generalized Image-based Re-identification using AI for Fauna Feature Extraction) ni nyenzo ya wazi ya akili bandia inayowawezesha Bond na Lee kuwatambua twiga mmoja mmoja kwa ufanisi mkubwa zaidi. “Sasa kazi hii inaweza kufanyika ndani ya dakika chache, na tunaweza kupata matokeo siku hiyohiyo tunapokusanya takwimu,” Lee aliiambia Mongabay katika mahojiano kupitia njia ya video. Kuwatambua twiga mmoja mmoja, na kuweza kuwatambua tena baadaye, ni jambo muhimu sana ili kuelewa maeneo ambayo ni ya msingi kwa ustawi na uhai wao. Hili ni jukumu la dharura, hasa ikizingatiwa kwamba idadi ya twiga imepungua sana katika miongo ya hivi karibuni, hasa kutokana na upotevu wa makazi yao ya asili na ujangili. Zaidi ya hayo, kulinda makazi ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/16/jinsi-akili-bandia-inavyosaidia-wahifadhi-kuwaelewa-vizuri-twiga-na-kuwalinda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/09/16/jinsi-akili-bandia-inavyosaidia-wahifadhi-kuwaelewa-vizuri-twiga-na-kuwalinda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya: Utata waibuka kuhusu hoteli ya Ritz-Carlton iliyomo kwenye Hifadhi ya Maasai Mara, katikati ya shoruba ya uhamaji wa wanyama</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/12/kenya-utata-waibuka-kuhusu-hoteli-ya-ritz-carlton-iliyomo-kwenye-hifadhi-ya-maasai-mara-katikati-ya-shoruba-ya-uhamaji-wa-wanyama/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/12/kenya-utata-waibuka-kuhusu-hoteli-ya-ritz-carlton-iliyomo-kwenye-hifadhi-ya-maasai-mara-katikati-ya-shoruba-ya-uhamaji-wa-wanyama/#respond</comments>
					<pubDate>12 Agosti 2025 06:41:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/28064805/Screenshot-2025-11-28-093928-768x481.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=819</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Jamii Asili, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika hifadhi ya kitaifa ya Maasai Mara iliyoko nchini Kenya, ujenzi wa hoteli ya kifahari umeibua utata mkubwa. Hoteli hiyo inayojulikana kama Ritz-Carlton Masai Mara Safari Camp, inasimamiwa na kundi la hoteli la Marriott International. Hoteli hii ya kifahari inayotarajia kufunguliwa katikati ya mwezi Agosti, ina idadi ya vyumba binafsi 20, bwawa la kuogelea lisilo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/12/kenya-utata-waibuka-kuhusu-hoteli-ya-ritz-carlton-iliyomo-kwenye-hifadhi-ya-maasai-mara-katikati-ya-shoruba-ya-uhamaji-wa-wanyama/" data-wpel-link="internal">Kenya: Utata waibuka kuhusu hoteli ya Ritz-Carlton iliyomo kwenye Hifadhi ya Maasai Mara, katikati ya shoruba ya uhamaji wa wanyama</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika hifadhi ya kitaifa ya Maasai Mara iliyoko nchini Kenya, ujenzi wa hoteli ya kifahari umeibua utata mkubwa. Hoteli hiyo inayojulikana kama Ritz-Carlton Masai Mara Safari Camp, inasimamiwa na kundi la hoteli la Marriott International. Hoteli hii ya kifahari inayotarajia kufunguliwa katikati ya mwezi Agosti, ina idadi ya vyumba binafsi 20, bwawa la kuogelea lisilo na ukingo, spa na huduma nyingine nyingi. Gharama za chini za kulala kwenye hoteli hiyo ni Dola za Kimarekani 3,500 kwa usiku mmoja tu. Hata hivyo kinacholeta utata hapa si hali ya kifahari ya hoteli hiyo bali mahali ilipojengwa, yaani kandokando ya Mto Sand, kwenye njia muhimu inayotumiwa na wanyamapori katika uhamaji wao. “Mahali walipojenga ni eneo linalosifika sana kwa uhamaji mkubwa wa wanyama aina ya nyumbu kati ya Tanzania na Kenya. Kila mwaka, kipindi kama hiki, mamilioni ya wanyama wakiwemo pundamilia na swala, huvuka mto huu. Kwa kawaida, wanyama hawa huvuka kupitia maeneo maalum. Kwa hiyo ujenzi wa hoteli hiyo maeneo hayo, unavuruga sana mwenendo wao,” anaeleza Meitamei Ole Dapash, Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu, Utafiti na Uhifadhi ya Wamasai (MERC), ambaye pia ni mwanachama wa jamii ya Waamasai. Uhamaji mkubwa wa wanyama hutokea katika kipindi kinachoanzia mwezi Juni hadi Oktoba kila mwaka ambapo wanyama wanaoishi kwa kula majani, kutoka Hifadhi ya Serengeti nchini Tanzania huhama kwenda kufuata malisho. Ili kufanikisha safari hii, makundi makubwa huvuka mito kadhaa na hatimaye kufika Hifadhi ya Kitaifa ya Maasai Mara nchini Kenya. Tukio hili la kiasili huvutia maelfu ya watalii, kwa sababu ya muonekano wa makundi makubwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/12/kenya-utata-waibuka-kuhusu-hoteli-ya-ritz-carlton-iliyomo-kwenye-hifadhi-ya-maasai-mara-katikati-ya-shoruba-ya-uhamaji-wa-wanyama/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/12/kenya-utata-waibuka-kuhusu-hoteli-ya-ritz-carlton-iliyomo-kwenye-hifadhi-ya-maasai-mara-katikati-ya-shoruba-ya-uhamaji-wa-wanyama/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Faru 70 kutoka Afrika Kusini wawasili makao mapya nchini Rwanda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2025 13:43:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Graeme Green]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/21133633/Screenshot-2025-08-21-163555-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=125</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, na  Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Faru, Kutoweka, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Uwindaji, Uwindaji Kupita Kiasi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Faru weupe 70 wamekamilisha safari yao kwa mafanikio kutoka Afrika Kusini hadi Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Hii ni mara ya kwanza kwa faru kuhamishwa kimataifa kutoka Platinum Rhino, mradi mkubwa wa ufugaji faru uliopitwa mnada mwaka 2023, baada ya kukumbwa na matatizo ya kifedha kwa miaka mingi. Baada ya kukosa wanunuzi, shirika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/" data-wpel-link="internal">Faru 70 kutoka Afrika Kusini wawasili makao mapya nchini Rwanda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Faru weupe 70 wamekamilisha safari yao kwa mafanikio kutoka Afrika Kusini hadi Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Hii ni mara ya kwanza kwa faru kuhamishwa kimataifa kutoka Platinum Rhino, mradi mkubwa wa ufugaji faru uliopitwa mnada mwaka 2023, baada ya kukumbwa na matatizo ya kifedha kwa miaka mingi. Baada ya kukosa wanunuzi, shirika la African Parks lilinunua eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 7,800, lililopo kilomita 160 kusini mashariki mwa Johannesburg, pamoja na faru wake 2,000 — twiga, pundamilia, na wanyama wengine — kwa kiasi cha fedha ambacho hakikutajwa. Platinum Rhino ilibadilishwa jina na kuitwa Rhino Rewild. Hii idadi ya faru waliokuwa African Parks inawakilisha takriban asilimia 15 ya idadi ya faru weupe wote duniani (Ceratotherium simum). Mpango wa African Parks wa Rhino Rewild unalenga kuwasambaza wanyama hao kwenye maeneo salama na yenye usimamizi mzuri kote Afrika, ili kuanzisha maeneo mapya ya kuwalinda na kuimarisha idadi ya waliopo tayari. Mwanzoni, faru 40 walihamishwa kutoka Rhino Rewild hadi Munywana Conservancy, ambayo ni hifadhi binafsi ya wanyamapori iliyoko mkoa wa KwaZulu Natal nchini Afrika Kusini. Hivyo uhamisho huu wa faru 70 kwenda Akagera ulikuwa wa pili. Faru mweupe akiwa kwenye makazi yake mapya katika Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Picha na Wiktoria West. &#8220;Akagera inaweza kuhifadhi idadi kubwa ya faru weupe,&#8221; alisema Donovan Jooste,   meneja wa mradi wa Rhino Rewilding wa African Parks. &#8220;Hii, pamoja na ukweli kwamba Rwanda ni nchi thabiti na serikali yake inaunga mkono kazi zetu, inamaanisha kwamba kundi hili la faru linaweza kuwa na umuhimu sana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatari, ustahimilivu vyaelezea maisha ya wahifadhi Afrika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/06/03/hatari-ustahimilivu-vyaelezea-maisha-ya-wahifadhi-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/06/03/hatari-ustahimilivu-vyaelezea-maisha-ya-wahifadhi-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2025 21:33:55 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Orji Sunday]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/21212807/Screenshot-2025-08-19-134647-1-768x508.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=162</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Kenya, Nigeria, na  Sierra Leone]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Mamalia, Mazingira, Misitu ya Kitropiki, Siasa za Mazingira, Sokwe, Uanaharakati, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jioni ya Mei 9, 2019, mhifadhi na mwalimu Itakwu Innocent alinusurika jaribio la mauaji nje ya nyumba yake huko Kubong-Bette, kijiji kidogo cha wakulima katika jimbo la Cross River kusini mashariki mwa Nigeria. &#8220;Baba! Bunduki!&#8221; Innocent anakumbuka mwanawe akipiga kelele sekunde chache kabla ya risasi kufyatuliwa. Risasi hiyo ilipasua nyumba yake na kuchana sikio lake na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/03/hatari-ustahimilivu-vyaelezea-maisha-ya-wahifadhi-afrika/" data-wpel-link="internal">Hatari, ustahimilivu vyaelezea maisha ya wahifadhi Afrika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jioni ya Mei 9, 2019, mhifadhi na mwalimu Itakwu Innocent alinusurika jaribio la mauaji nje ya nyumba yake huko Kubong-Bette, kijiji kidogo cha wakulima katika jimbo la Cross River kusini mashariki mwa Nigeria. &#8220;Baba! Bunduki!&#8221; Innocent anakumbuka mwanawe akipiga kelele sekunde chache kabla ya risasi kufyatuliwa. Risasi hiyo ilipasua nyumba yake na kuchana sikio lake na kuliacha likiwa vipande vipande vinavyoning’inia. “Walidhani nimekufa,” Innocent anasema. Jaribio la kumaliza maisha ya Innocent linatoa muhtasari wa vitisho vinavyowakabili wanasayansi wa Kiafrika walio mstari wa mbele katika uhifadhi vijijini. Ushirikishwaji unaotatanisha wa Innocent kwenye mfumo wa ikolojia wa maeneo ya vijijini mashinani humpa ufahamu wa kina kuhusu ardhi na watu wanaomzunguka. Hata hivyo, uhusiano huu unamweka kwenye mashambulizi na vitisho. Tofauti na wanasayansi wa kigeni au wa mijini, yeye anakosa mbinu za kukabiliana na hatari hiyo. &#8220;Mtu hawezi kutoroka kutoka nyumbani kwake,&#8221; anasema. &#8220;Hii ndiyo nyumba yangu pekee. Na nisipoihifadhi, nani ataihifadhi?” Zaidi ya ukosefu wa usalama, wanasayansi kama Innocent wanakabiliwa na changamoto nyingi zaidi za kitaaluma, anasema Babafemi Ogunjemite, profesa wa usimamizi wa wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Teknolojia cha Akure, kusini magharibi mwa Nigeria. Kwa kiasi kikubwa wanasahaulika na wanafadhiliwa kidogo. Uwakilishi, nafasi za kupata ushauri na mchango wao kuonekana, viko chini na zaidi ya hayo, ubaguzi wa kijinsia ni kikwazo cha ziada kwa wanawake. Kutokana na hilo, Ogunjemite anasema, &#8220;vipaji vyetu bora havitumiwi ipasavyo na sekta ya uhifadhi.&#8221; Innocent Itakwu akiwa ameketi mbele ya baraza la nyumba yake ambapo muuaji alikaribia kumuua miaka sita iliyopita. Picha na Orji Sunday. Anaonekana kama&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/03/hatari-ustahimilivu-vyaelezea-maisha-ya-wahifadhi-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/06/03/hatari-ustahimilivu-vyaelezea-maisha-ya-wahifadhi-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ugunduzi wa popo walio hatarini kutoweka nchini Rwanda waibua mazungumzo ya uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>25 Aprili 2025 00:59:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Aimable Twahirwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/01135959/3d1278d3-4f58-4143-82ec-1f992772db5d-1.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=285</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Rwanda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kutoweka, Mamalia, Mazingira, Popo, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Ugunduzi wa Spishi, Uhifadhi, Upotevu wa Makazi, Utafiti, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIGALI, Rwanda ― Kufuatia ugunduzi wa hivi karibuni wa popo aina ya farasi walio katika hatari ya kuangamia (au kisayansi Rhinolophus hilli) katika Mbuga ya Taifa ya Nyungwe kusini-magharibi mwa Rwanda, watafiti wanatoa wito wa kuchukua hatua na sera zinazolenga uhifadhi wao. Wanasayansi wanasema kuwa huu ni ugunduzi wa kwanza wa kuona na kurekodi popo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Ugunduzi wa popo walio hatarini kutoweka nchini Rwanda waibua mazungumzo ya uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIGALI, Rwanda ― Kufuatia ugunduzi wa hivi karibuni wa popo aina ya farasi walio katika hatari ya kuangamia (au kisayansi Rhinolophus hilli) katika Mbuga ya Taifa ya Nyungwe kusini-magharibi mwa Rwanda, watafiti wanatoa wito wa kuchukua hatua na sera zinazolenga uhifadhi wao. Wanasayansi wanasema kuwa huu ni ugunduzi wa kwanza wa kuona na kurekodi popo wa aina ya Rhinolophus webalai (horseshoe bat) katika hifadhi hiyo, na pia ni mara ya kwanza kwa Rwanda kushuhudia popo wa Damara woolly bat (Kerivoula argentata) tangu walipoonekana mara ya mwisho mwaka 1981. Kwa mujibu wa Paul Webala, Mhadhiri Mwandamizi wa Biolojia ya Wanyamapori katika Idara ya Misitu na Usimamizi wa Wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Maasai Mara nchini Kenya, wanasayansi wanachukulia popo kuwa kundi la pili lenye utofauti mkubwa zaidi miongoni mwa mamalia, baada ya panya. Anasema katika nchi kama Rwanda  ambapo misitu ya asili na maeneo ya savana yamepotea, kubadilika au kuharibika kwa kiasi kikubwa, popo wanaweza kuwakilisha “angalau asilimia 40 ya utofauti wa mamalia kwa ujumla.” Kulingana na utafiti wa mwaka mwaka 2022 (utafiti) ambao Webala alishirikiana na mtu mwingine kuufanya, popo wanaokula wadudu nchini Rwanda hutoa huduma muhimu za mfumo wa ikolojia na pia hufanywa kama wadhibiti wadudu katika maeneo ya kilimo. Hofu za kiafya na upotezaji wa makazi  &#8220;Nchini Rwanda, mojawapo ya aina [ya popo] inayotia wasiwasi, ingawa haijatishiwa kulingana na Orodha Nyekundu ya shirika la IUCN, ni popo wa Misri [Rousettus aegyptiacus] kwa sababu ametambuliwa na maafisa wa afya kama hifadhi ya asili ya ugonjwa wa virusi vya Marburg,&#8221; Webala anasema. Mnamo Februari mwaka huu, maafisa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Auawa akiwinda kiharamu’: Utekelezaji wa sheria za wanyamapori unapogeuka vurugu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/03/27/auawa-akiwinda-haramu-utekelezaji-wa-sheria-za-wanyamapori-unapogeuka-vurugu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/03/27/auawa-akiwinda-haramu-utekelezaji-wa-sheria-za-wanyamapori-unapogeuka-vurugu/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2025 14:56:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/03140900/Screenshot-2025-09-03-170809-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=363</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Jamii Asili, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Siasa za Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyamapori, na  Watu wa Jadi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni hadithi ya pili katika mfululizo wa Mongabay – Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki. Soma Sehemu ya Kwanza hapa. KITABU, Uganda — Ni saa sita mchana katika sehemu ya Kitabu, mji mdogo ulio kwenye vilima vya magharibi mwa Uganda chini ya milima ya Rwenzori. Mashamba yaliyotunzwa vyema ya maharage na mihogo yako kando ya barabara [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/27/auawa-akiwinda-haramu-utekelezaji-wa-sheria-za-wanyamapori-unapogeuka-vurugu/" data-wpel-link="internal">‘Auawa akiwinda kiharamu’: Utekelezaji wa sheria za wanyamapori unapogeuka vurugu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni hadithi ya pili katika mfululizo wa Mongabay – Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki. Soma Sehemu ya Kwanza hapa. KITABU, Uganda — Ni saa sita mchana katika sehemu ya Kitabu, mji mdogo ulio kwenye vilima vya magharibi mwa Uganda chini ya milima ya Rwenzori. Mashamba yaliyotunzwa vyema ya maharage na mihogo yako kando ya barabara inayoelekea huko. Wanawake na watoto wadogo wanaonekana wakiwa wamebeba mizigo ya kuni vichwani mwao chini ya jua kali la Oktoba. Chini kabisa, mandhari ya savanna ya kijani kibichi na kahawia inaambaa kwa umbali, na kuenea hadi upeo wa macho ikiwa na maziwa na mito inayomeremeta. Hii ni mbuga ya Taifa ya Malkia Elizabeth, &#8220;kivutio maarufu zaidi cha watalii” nchini Uganda, na mojawapo ya mifumo muhimu zaidi ya ikolojia katika Afrika Mashariki. Misitu yake, mabwawa na nyasi vimeenea katika eneo la karibu kilomita za mraba 2,000 (takribani maili za mraba 765). Kuna tembo wa savanna hapa, pamoja na simba ambao hulala kwenye matawi ya miti, nyati, chui, swala, sokwe, viboko, na zaidi ya aina 600 za ndege tofauti. &#8220;Malkia,&#8221; kama wasimamizi wa mbuga wanavyoiita, ni &#8220;mhifadhi wa binadamu na eneo la uhai&#8221; la UNESCO &#8211; moja ya makazi machache ya wanyamapori yaliyohifadhiwa kwa kiwango hiki ambacho kimebaki barani Afrika. Ramani ya Mbuga ya Taifa ya Malkia Elizabeth nchini Uganda. Shule iliyoko hapa mji wa Kitabusi ya kawaida. Ilianzishwa mwaka 2018 na kundi la waliokuwa wawindaji haramu, na ni moja ya shule chache zilizo karibu na Mbuga ya Malkia Elizabeth ambazo zinapata usaidizi kutoka kwa wafadhili nje ya nchi au, mara kwa mara, kutoka kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/27/auawa-akiwinda-haramu-utekelezaji-wa-sheria-za-wanyamapori-unapogeuka-vurugu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/03/27/auawa-akiwinda-haramu-utekelezaji-wa-sheria-za-wanyamapori-unapogeuka-vurugu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutafuta amani, kupata tumaini: Filamu mpya yachunguza migogoro vijijini mwa Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/03/14/kutafuta-amani-kupata-tumaini-filamu-mpya-yachunguza-migogoro-vijijini-mwa-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/03/14/kutafuta-amani-kupata-tumaini-filamu-mpya-yachunguza-migogoro-vijijini-mwa-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>14 Mechi 2025 05:51:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Leonie Joubert]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/22053734/Screenshot-2025-08-22-083501-768x470.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=173</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Maendeleo, Maeneo yaliyolindwa, Makazi, Mamalia, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni hadithi ya kusisimua kuhusu vijana wawili wa Kenya ambao urafiki wao unatokana na tukio la mauaji. Filamu hii ya makala, “Searching for Amani”, inaweka wazi mvutano mgumu iliyo kati ya wanahifadhi, wakulima wa mazao na wafugaji nchini Kenya, huku kipindi kirefu cha ukame kikisababisha migogoro juu ya rasilimali zinazozidi kupungua. “Wakati kuna amani, huwa watu hawauawi,” anasema [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/14/kutafuta-amani-kupata-tumaini-filamu-mpya-yachunguza-migogoro-vijijini-mwa-kenya/" data-wpel-link="internal">Kutafuta amani, kupata tumaini: Filamu mpya yachunguza migogoro vijijini mwa Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni hadithi ya kusisimua kuhusu vijana wawili wa Kenya ambao urafiki wao unatokana na tukio la mauaji. Filamu hii ya makala, “Searching for Amani”, inaweka wazi mvutano mgumu iliyo kati ya wanahifadhi, wakulima wa mazao na wafugaji nchini Kenya, huku kipindi kirefu cha ukame kikisababisha migogoro juu ya rasilimali zinazozidi kupungua. “Wakati kuna amani, huwa watu hawauawi,” anasema Simon Ali, mwenye umri wa miaka 18, ambaye baba yake, aliyekuwa mwongoza watalii, aliuwawa kazini kwenye hifadhi ya wanyamapori miaka mitano iliyopita. “Kama mmoja wa wahanga wa migogoro, ninajua umuhimu wa amani.” Sauti ya Ali inafichua taswira ya muda ambao umepita tangu alipopata habari kwamba baba yake alipigwa risasi akiwaongoza watalii katika eneo la pori la Kaunti ya Laikipia, Kenya ya Kati. Simon Ali, akiwa Kaunti ya Laikipia, Kenya. Picha na Backroads Pictures. Miaka mitano baadaye, Ali amepitia majonzi kwenye ujana wake, huku akifanya kazi kwenye mradi wa filamu uliotayarishwa na Backroads Pictures na Nicole Gormley Films, ambamo amekuwa akitafuta majibu kuhusu jinsi, na sababu ya baba yake kuuawa, pamoja muuaji. Wakati huo huo, usuli wa simulizi hili ni ukame sugu, ambao umetajwa kama mbaya zaidi kuwahi kuikumba eneo hilo katika kipindi cha miaka 40. Ali anapojitokeza mbele ya kamera katika filamu ya “Searching for Amani”, anashika kamera yake na kuchukua jukumu la mwandishi chipukizi wa uchunguzi. Akiwa chini ya ulezi wa kikosi cha filamu, anafunzwa mbinu za uandishi wa habari, zinazomwezesha kuwa na ukakamavu anapowahoji watu wengi waliokuwa na taarifa kuhusu mauaji ya baba yake, Stephen Ali, na hatimaye kupata utulivu kiasi kwa ajili yake na familia yake. Kenya imeshuhudia migogoro kati ya wanaoshikilia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/14/kutafuta-amani-kupata-tumaini-filamu-mpya-yachunguza-migogoro-vijijini-mwa-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/03/14/kutafuta-amani-kupata-tumaini-filamu-mpya-yachunguza-migogoro-vijijini-mwa-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Kama wewe, mimi pia nahofia kuangamia kwa tembo’</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>17 Desemba 2024 16:24:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/29154201/Screenshot-2025-08-29-184109-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=313</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Haki za Binadamu, Hifadhi za Taifa, Jamii Asili, Kutoweka, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Misitu, Pembe za Ndovu, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Studeo ya Data ya Mongabay, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni makala ya kwanza katika mfululizo wa habari za Mongabay kuhusu ‘Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki’. Soma sehemu ya pili na ya nne.  Mnamo Juni 13, 1959, mwindaji wa kabila la Waata, Galogalo Kafonde, alijisalimisha kwa kikosi cha kikoloni cha &#8220;Field Force&#8221; cha Kenya, kitengo cha kwanza barani Afrika cha kupambana na ujangili. Kwa karne nyingi, watu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/" data-wpel-link="internal">‘Kama wewe, mimi pia nahofia kuangamia kwa tembo’</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni makala ya kwanza katika mfululizo wa habari za Mongabay kuhusu ‘Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki’. Soma sehemu ya pili na ya nne.  Mnamo Juni 13, 1959, mwindaji wa kabila la Waata, Galogalo Kafonde, alijisalimisha kwa kikosi cha kikoloni cha &#8220;Field Force&#8221; cha Kenya, kitengo cha kwanza barani Afrika cha kupambana na ujangili. Kwa karne nyingi, watu kutoka kabila la Waata walikuwa wakiwinda tembo. Kumuua tembo mmoja ilikuwa ni ibada ya jandoni. Tofauti na majirani zao waliofuga ng’ombe, jamii ya Waata waliishi kwa kula nyama ya ng’ombe na kuvaa ngozi za tembo. Pembe za ndovu hazikuwa na manufaa kwao, lakini waliziuza kupitia ubadilishanaji wa bidhaa nyingine na wafanyabiashara wa Kiarabu huko Mombasa. Biashara ya pembe za ndovu ilipozidi kushamiri katika karne ya 17, ikichochewa na ukuaji wa soko la watumiaji wa Ulaya, sifa ya Waata iliimarika. Walikuwa miongoni mwa wafuatiliaji bora wa tembo ukanda wa Afrika Mashariki, wanaojulikana kama &#8220;watu wa upinde mrefu&#8221; kwa ustadi wao wa kutumia mishale yenye sumu. Lakini wawindaji wa Ulaya walikuja kuwaona jamii za Waata na jamii nyingine asilia kama ushindani. Mnamo mwaka 1897, Uingereza ilipoweka malengo yake kwa koloni la kudumu la Kenya, ilipiga marufuku uwindaji &#8220;wa asili&#8221; ambao haujaidhinishwa. Kwa saini  moja tu ya kalamu, kiini cha maisha ya Waata kiligeuka kuwa haramu. Wafanyabiashara wakipima pembe za ndovu mwaka 1935. Picha na Ewing Galloway kupitia Flickr (CC BY-NC-SA 2.0). Mnamo mwaka 1948, Waingereza waliunda Mbuga ya Taifa ya Tsavo, mojawapo ya mbuga za kwanza nchini Kenya. Lakini upande wake wa mashariki ulikuwa uwanja wa uwindaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoonekana kwa tumbili wala gundi Tanzania kwaibua hofu ya kutoweka kwa spishi hiyo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Desemba 2024 08:06:40 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ryan Truscott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/28075239/Screenshot-2025-08-28-105201-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=297</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kutoweka, Mamalia, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Nyani, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tumbili, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hakujakuwa na taarifa zilizothibitishwa za kuonekana kwa tumbili wa kusini wa patas, ambao wako katika hatari kubwa ya kutoweka, katika makazi yao ya mwisho yanayojulikana, magharibi mwa Tanzania. Mwaka 2021, ilikadiriwa kuwa walikuwa wamebaki chini ya tumbili 200 wa aina hii wenye viungo vyepesi na virefu, wanaojulikana kitaalam kama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/" data-wpel-link="internal">Kutoonekana kwa tumbili wala gundi Tanzania kwaibua hofu ya kutoweka kwa spishi hiyo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hakujakuwa na taarifa zilizothibitishwa za kuonekana kwa tumbili wa kusini wa patas, ambao wako katika hatari kubwa ya kutoweka, katika makazi yao ya mwisho yanayojulikana, magharibi mwa Tanzania. Mwaka 2021, ilikadiriwa kuwa walikuwa wamebaki chini ya tumbili 200 wa aina hii wenye viungo vyepesi na virefu, wanaojulikana kitaalam kama Erythrocebus baumstarki, ambao walipatikana kwenye maeneo ya misitu ya wazi katika ukanda huo na sasa wanasayansi wana hofu kuwa spishi hiyo inakaribia kutoweka kabisa. Awali, tumbili wa patas wa kusini alikuwa anachanganywa na tumbili wa patas wa mashariki, Erythrocebus patas pyrrhonotus, ambaye hupatikana kwa wingi zaidi katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki na Kati, kuanzia Kenya ya kati hadi kaskazini mashariki mwa Chad. Wanyama hawa wanafanana kwa mwonekano, na wote huishi kwenye maeneo ya misitu ya wazi yenye urefu wa mwinuko unaokaribiana. Lakini hata kabla ya mwaka 2015, wakati ambapo patas wa kusini bado walikuwepo nchini Kenya; spishi hizi mbili zilikuwa zimetenganishwa na mamia ya kilomita. Kuna uwezekano mkubwa kuwa hazijawahi kuchanganyika. Mwonekano wao unaofanana  pamoja na tabia nyingine kama vile kuwa na maeneo makubwa ya kuishi na kula gundi kutoka kwenye miti ya miiba inayojulikana kitaalam kama Acacia drepanolobium (whistling thorn); ulisababisha ukosefu wa juhudi maalum za uhifadhi kwa ajili ya kulinda tumbili wa kusini wa patas. Kutokana na ukweli kwamba aina hii ya nyani wana tabia ya uoga, na huonekana mara chache, vilifanya tafiti za kisayansi za kutambua tofauti za spishi kukosekana kwa muda mrefu. Hata hivyo, Yvonne de Jong, mtaalamu wa masuala ya jamii ya nyani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uwindaji pembe za ndovu wa Amboseli Tanzania wazua hasira, watu wataka usitishwe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/07/22/uwindaji-pembe-za-ndovu-wa-amboseli-tanzania-wazua-hasira-watu-wataka-usitishwe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/07/22/uwindaji-pembe-za-ndovu-wa-amboseli-tanzania-wazua-hasira-watu-wataka-usitishwe/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2024 15:29:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika Vyawahare]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/24153059/Screenshot-2025-09-24-183022-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=506</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Misitu, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wanaharakati wa uhifadhi wametoa wito wa kusitishwa kwa uwindaji wa nyara zinazotokana na tembo kutoka Hifadhi ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya wanaovuka mpaka kuingia Tanzania, kufuatia kuuawa kwa zaidi ya tembo dume watano wenye mapembe makubwa isivyo kawaida na wawindaji nchini Tanzania. Uwindaji wa nyara unaruhusiwa nchini Tanzania lakini ni kinyume cha sheria nchini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/22/uwindaji-pembe-za-ndovu-wa-amboseli-tanzania-wazua-hasira-watu-wataka-usitishwe/" data-wpel-link="internal">Uwindaji pembe za ndovu wa Amboseli Tanzania wazua hasira, watu wataka usitishwe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wanaharakati wa uhifadhi wametoa wito wa kusitishwa kwa uwindaji wa nyara zinazotokana na tembo kutoka Hifadhi ya Taifa ya Amboseli nchini Kenya wanaovuka mpaka kuingia Tanzania, kufuatia kuuawa kwa zaidi ya tembo dume watano wenye mapembe makubwa isivyo kawaida na wawindaji nchini Tanzania. Uwindaji wa nyara unaruhusiwa nchini Tanzania lakini ni kinyume cha sheria nchini Kenya. Chini ya kile wanaharakati wa uhifadhi walichoita “makubaliano ya kiungwana,” hadi sasa wawindaji hawatakiwi kuwagusa tembo wa Amboseli wanaozunguka mpakani mwa Kenya na Tanzania. Utaratibu huo ulikuwa ni utambuzi wa umuhimu wa kundi hili la tembo wa savanna wa Afrika (Loxodonta africana), ambao wako katika hatari kubwa na idadi yao inaendelea kupungua. Mradi wa Utafiti wa Tembo wa Amboseli uliodumu kwa miaka 51 “ndio utafiti wa muda mrefu zaidi wa tembo duniani’’, jambo linalowafanya tembo wa Amboseli kuwa miongoni mwa tembo wanaojulikana zaidi duniani, waliopigwa picha mara nyingi na watalii, na wanaofahamika kwa undani na wanasayansi. Kwa Cynthia Moss, anayeongoza Mradi wa Utafiti wa Tembo wa Amboseli, na Joyce Poole, mwanzilishi mwenza na mkurugenzi mwenza wa shirika lisilo la kiserikali la ElephantVoices, mauaji haya yaliwagusa moja kwa moja  kwa kiasi kikubwa. Wote wawili walianza taaluma zao za kisayansi kwa kuchunguza kundi hili la tembo takriban miongo mitano iliyopita. Wanasayansi wamewapa majina karibu ya tembo wote 2,000 kutoka familia 69 wanaopatikana katika eneo hilo, wengi wao walizaliwa na kukua chini ya uangalizi wao wa karibu. Maikoni wa Amboseli, Tim na Kilimanjaro, Hifadhi ya Taifa ya Amboseli, 2016, Kenya. Picha kwa hisani ya ElephantVoices. Matokeo ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/22/uwindaji-pembe-za-ndovu-wa-amboseli-tanzania-wazua-hasira-watu-wataka-usitishwe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/07/22/uwindaji-pembe-za-ndovu-wa-amboseli-tanzania-wazua-hasira-watu-wataka-usitishwe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kipunji: Nyani adimu anayehifadhiwa nchini Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/07/07/kipunjinyani-adimu-anayehifadhiwa-tanzania/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/07/07/kipunjinyani-adimu-anayehifadhiwa-tanzania/#respond</comments>
					<pubDate>07 Julai 2023 10:12:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Kamnitzer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/29101352/Screenshot-2025-09-29-131113-768x469.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=546</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Jamii ya Nyani Wakubwa, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Nyani, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Ukataji Miti ya Msitu wa Mvua, Uwindaji, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Januari 2003, watafiti kutoka Shirika la Kuhifadhi Wanyamapori (Wildlife Conservation Society) waliokuwa wakifanya kazi huko Nyanda za Juu Kusini nchini Tanzania walikutana na wawindaji ambao waliwaeleza kuwa kulikuwa na nyani anayeitwa kipunji katika misitu ya Mlima Rungwe. Walishangaa kwa kuwa hawakuwahi kuwaona nyani hao lakini wenyeji wa huko ambao ni Wanyakyusa ni wasimulizi wazuri wa hadithi, ingawa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/07/07/kipunjinyani-adimu-anayehifadhiwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Kipunji: Nyani adimu anayehifadhiwa nchini Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Januari 2003, watafiti kutoka Shirika la Kuhifadhi Wanyamapori (Wildlife Conservation Society) waliokuwa wakifanya kazi huko Nyanda za Juu Kusini nchini Tanzania walikutana na wawindaji ambao waliwaeleza kuwa kulikuwa na nyani anayeitwa kipunji katika misitu ya Mlima Rungwe. Walishangaa kwa kuwa hawakuwahi kuwaona nyani hao lakini wenyeji wa huko ambao ni Wanyakyusa ni wasimulizi wazuri wa hadithi, ingawa wakati mwingine ni vigumu kujua ukweli wa simulizi za asili za wenyeji. Mwezi Mei mwaka huo huo, wakati watafiti hao wakishughulika na mambo ya bioanuai maeneo ya Nyanda za Juu Kusini, waliwaona kwa mara ya kwanza nyani ambao si wa kawaida. Ilichukua miezi mingi kuwafuatilia nyani hao ambao mara nyingi hupenda kujificha kabla ya kuwaona vizuri na kupata picha. Hapo ndipo walithibitisha bila shaka yoyote kuwepo kwa nyani aina ya kipunji mwenye rangi ya kahawia, uso mweusi, mdomo kama wa kima na sauti ya juu. Hii ilikuwa aina mpya ya nyani kwa wanasayansi wa nchi za magharibi. Kwa bahati ya pekee, mwezi Julai 2004 watafiti waliokuwa wakifanya kazi eneo la Milima ya Udzungwa takriban kilometa 350 (maili 220) upande wa kaskazini mashariki, waliwaona aina ya nyani ambao waliamini hawajawahi kuonekana na watafiti wengine. Mwaka uliofuata, yaani 2005, makundi hayo mawili ya watafiti kwa pamoja yalichapisha taarifa ya utafiti wao katika jarida la Science wakielezea aina hiyo mpya ya nyani. Mwanzoni waliwaita mangabey wa milimani (Lophocepus kipunji), lakini baada ya uchambuzi wa vinasaba vya mnyama aliyekufa wakawapa jina la kipunji (Rungwecebus kipunji), ambalo ni utambulisho wa kipekee kwa kuwa hawakufanana na nyani mwingine wa aina yoyote. Utafiti huo ulifanya kipunji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/07/07/kipunjinyani-adimu-anayehifadhiwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/07/07/kipunjinyani-adimu-anayehifadhiwa-tanzania/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>