- Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, shinikizo kwaHifadhi ya Kitaifa ya Virunga huakisi mienendo ya kina ya kiuchumi na utawala, ambapo uhifadhi hushindana na mahitaji ya haraka ya maisha yanayohusiana na uzalishaji wa mkaa na kilimo.
- Emmanuel de Merode anaangazia hali ya kuzorota kwa mazingira kama matokeo ya jinsi watu wanavyopata riziki, akijadili kuwa kulinda bayoanuwai kunahitaji kushughulikia upatikanaji wa nishati, kazi, na mifumo ya kiuchumi ya ndani.
- Mbuga ya Virunga imebuni mtindo uliounganishwa unaotegemea nishati mbadala, maendeleo ya biashara ndogo ndogo, upatikanaji wa huduma zakifedha, na usalama wa ndaniunaolenga kuhamisha motisha kutoka kwa shughuli zinazohusishwa na migogoro na uchimbaji.
- Pendekezo la Mkanda wa kijani(Green Corridor) linapanua mbinu hii katika kiwango cha kitaifa, likipima iwapo mfumo wa kiuchumi unaoweza kutegemewa unaweza kujengwa ambao unategemea kutunza misitu badala ya kuisafisha, licha ya migogoro inayoendelea na vikwazo vya kisiasa.
Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, volkeno, misitu, na ardhi oevu ndani ya eneo moja lililohifadhiwa. Pia ipo ndani ya mazingira iliyoundwa kwa miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu, ambapo makundi yaliojihami kwa silaha, uchumi usio rasmi, na utawala dhaifu ni sehemu ya maisha ya kila siku.

Emmanuel de Merode, ambaye ameiongoza Virunga tangu mwaka wa 2008, haanzii na ikolojia. Mafunzo yake ni ya anthropolojia, hali inayounda namna anavyoelezea hifadhi. Anapendekeza kuwa hali ya wanyamapori hutokana na nguvu za kina. Upotevu wa misitu, ujangili, na ukosefu wa usalama sio shida za mazingira pekee. Yanatokana na namna watu wanavyopata riziki, namna mamlaka inavyofanya kazi, na jinsi pesa na rasilimali zinavyozunguka.
Katika sehemu ya Mashariki mwa Kongo, uhifadhi hauwezi kutenganishwa na uchumi. Kwa jamii nyingi zinazoizunguka Virunga, chaguo lao ni la haraka. Kuifyeka misitu kwa ajili ya ukulima au kutengeza mkaa kunaweza kuzalisha kipato cha kuendesha maisha. Faida za uhifadhi ni ngumu kuonekana na mara nyingi huonekana zaidi nje ya eneo hilo. Ukosefu wa usawa unajitokeza katika maamuzi ya kila siku kuhusu mafuta, chakula na upatikanaji wa ardhi. Kama De Merode anavyoelezea, mfumo unawalazimisha baadhi ya watu maskini zaidi kubeba gharama ya kulinda mali zinazothaminiwa kimataifa.
Shinikizo kwenye mbuga yanaimarishwa na migogoro. Tangu katikati ya miaka ya 1990, sehemu ya mashariki mwa Kongo imekuwa eneo la ghasia za muda mrefu zinazohusisha wanamgambo, makundi ya kigeni yaliojihami kwa silaha, na maslahi ya kisiasa yanayoshindana. Mienendo hii imekuwa na athari za moja kwa moja za kiikolojia. Idadi ya wanyama wakubwa ilipungua sana mwanzoni mwa miaka ya 2000. Walinzi waliopewa jukumu la kulinda mbuga hiyo, wamekuwa walengwa wa kila mara. Zaidi ya walinzi 200 wameuawa kwa miaka mingi.

Mtazamo wa De Merode ulikuzwa kutokana na muktadha huu. Mabadiliko yalikuja mwaka wa 2007, wakati wa ghasia zilizopelekea mauaji ya sokwe saba wa milimani. Uchunguzi ulihusisha matukio haya na biashara ya mkaa inayosambazwa Goma, jiji lenye takriban watu milioni mbili na njia chache mbadala za nishati. Kwenye msingi wake, mgogoro ulikuwa juu ya nishati na riziki. Matokeo hayo yalilazimisha mabadiliko katika majibu.
Katika miaka iliyofuata, mbuga ya Virunga ilijenga mfumo unaozingatia nishati mbadala, hasa mitambo midogo ya kuzalisha umeme kwa maji. Lengo lilikuwa kupunguza shinikizo kutoka kwa misitu kwa kupunguza matumizi ya mkaa huku ikijenga msingi tofauti wa kiuchumi. Umeme uliwezesha biashara ndogo ndogo, kutoka kwa uchomeleaji na kusaga hadi majokofu na usindikaji wa chakula. Shughuli hizi zilizalisha ajira. Hoja ya De Merode ni ya moja kwa moja: kwamba nishati huwezesha biashara, biashara hubuni nafasi za kazi, na kazi hubadilisha vivutio ambavyo huwavuta watu katika vikundi vilivyojihami kwa silaha au shughuli haramu.

Mtindo huo unaenea zaidi ya nishati. Huduma za kifedha zimeunganishwa kupitia mita mahiri zinazofuatilia matumizi ya umeme. Data ya matumizi hutoa rekodi ya shughuli, kuruhusu makampuni madogo kupata mikopo bila dhamana za kawaida. Malipo yanahusishwa moja kwa moja na matumizi ya nishati. Utaratibu huu ni rahisi na unashughulikia kikwazo kinachoendelea mahali ambapo mifumo rasmi ya benki ni midogo na gharama za miamala ni kubwa.
Usalama pia umefanyiwa kazi upya. Majibu ya kitamaduni, mara nyingi polepole na yenye muitiko, yaliacha jamii ikiwa wazi. Virunga imebuni mifumo ya majibu ya haraka na misingi ya uendeshaji ya mbele iliyotengezwa ili kufupisha nyakati za kukabiliana na vitisho na kuunda uthabiti uliojanibishwa. Hizi zimeunganishwa na mipango ya kiuchumi, ili maeneo yanayonufaika na usalama ulioimarishwa pia kupata nafasi za kazi na miundombinu.
Ukulima unatoa mfano mwingine. Katika sehemu za mashariki mwa Kongo, mazao kama vile kakao yamehusishwa na ufadhili wa migogoro. Vikundi vilivyojihami kwa silaha vimetumia vurugu kudhibiti uvunaji na kuelekeza uzalishaji katika mitandao ya biashara haramu. Jibu la Virunga limekuwa kufupisha mnyororo wa thamani na kuulinda. Wakulima huuza moja kwa moja kwenye mfumo ambao huchakata bidhaa ndani ya nchi, kupata thamani zaidi na kupunguza kukabiliwa na shuruti.
Vipengele hivi vinaunda kile ambacho De Merode anakielezea kama mfumo wa kiuchumi unaoshindana. Wazo ni kuwa migogoro katika mashariki mwa Kongo inadumishwa kwa sehemu na uchumi uliojengwa juu ya uchimbaji na biashara isiyo rasmi. Kubadilisha hali ilivyo kunahitaji kuanzishwa kwa njia mbadala ambayo inaweza kutumika kwa kiwango. Uingiliaji kati mdogo unaweza kuonyesha uwezo, ila haubadilishi usawa mpana. Changamoto ni kufikia mahali ambapo mbadala huanza kuondoa mfumo uliopo.
Couloir vert (Ukanda wa kijani kwa Kifaransa) Kivu-Kinshasa, au Green Corridor (kwa Kiingereza), unatazamiwa kuwa mbadala huo. Ulianzishwa kupitia sheria ya kitaifa mwaka wa 2025, ukanda huo unapanua mbinu iliyotengenezwa Virunga katika jiografia kubwa zaidi. Sio eneo lililohifadhiwa kwa maana ya kawaida. Inaihusisha miji, mashamba, na miundombinu. Lengo ni kuunganisha maeneo ya uzalishaji wa kilimo katika mashariki na mahitaji katika magharibi, hususan katika Kinshasa, huku ikidumisha uadilifu wa Msitu wa Bonde la Kongo.

Ukanda huo unachukuliwa kuwa mtandao wa vitovu vya kiuchumi, kila kimoja kikichanganya nishati, kilimo, usindikaji, vifaa na usalama. Badala ya kujaribu ukuzaji mpana wa kina mara moja, mtindo huunda fundo ambazo zinaweza kuunganishwa kwa wakati. Sehemu ya nishati inasalia kuwa mahali pa kuanzia, ikifuatiwa na uzalishaji wa ongezeko la thamani na mifumo ya usafiri. Kiwango ni kikubwa: eneo lililofunikwa ni kubwa kuliko nchi nyingi, na idadi ya watu inafikia mamilioni.
Mbinu yenyewe ina mipaka. Kuibuka upya kwa mizozo ya hivi majuzi kumetatiza sehemu za mfumo. Miundombinu inaweza kuharibiwa, ufikiaji kuzuiwa, na mapato kupunguzwa, haswa kutoka kwa utalii. De Merode anakiri kwamba uingiliaji kati wa kiuchumi pekee hauwezi kutatua mienendo mipana ya kisiasa inayounda kanda. Maslahi ya nje, mivutano ya kikanda, na changamoto za muda mrefu za utawala zinaendelea kuathiri matokeo.
Pamoja na hayo, juhudi inachukuliwa kama jaribio la lazima. Bila mtindo mbadala, mwelekeo wa Bonde la Kongo una uwezekano wa kufuata mifumo inayoonekana mahali kwingine, ambako upanuzi wa miundombinu na uchimbaji wa rasilimali husababisha kugawanyika na hasara. Ukanda huo unajaribu kubainisha kama njia tofauti inawezekana, ambayo shughuli za kiuchumi hutegemea kutunza msitu badala ya kuusafisha.
Taarifa ifuatayo imetokana na mfululizo wa mazungumzo na De Merode yaliyofanywa kwa muda wa siku kadhaa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Rhett Ayers Butler na David Akana. Mahojiano yamehaririwa na kufupishwa.

MAHOJIANO NA EMMANUEL DE MERODE
Asili yako ni ipi, na ulikujaje kufanya kazi katika mbuga ya Virunga?
Nilizaliwa Tunisia na kukulia nchini Kenya. Wazazi wangu ni Wabelgiji, ila sijawahi kuishi Ubelgiji. Kenya ndiyo ilinijenga. Huko ndiko nilikokuza uelewa wa mandhari, lakini muhimu zaidi, uelewa wa watu, namna jamii zinavyofanya kazi na jinsi zinavyohusiana na mazingira yao.
Sikuingia katika kazi hii kupitia njia ya kawaida ya uhifadhi wa jadi. Sikuwahi kuvutiwa kufuatilia kwa karibu asili kutoka kwa mtazamo wa kibaolojia au kisayansi. Kilichonivutia zaidi kilikuwa upande wa binadamu; mawasiliano, tabia, mifumo. Ndiyo maana nilisoma anthropolojia badala ya biolojia.
Mtazamo huo umesalia nami. Ukiangalia uhifadhi kupitia jicho la ikolojia, unakosa vichochezi vya msingi vya kile kinachotokea. Mara nyingi, matokeo tunayoyaona kama ukataji miti, ujangili, migogoro si kutofaulu kwa maarifa juu ya mifumo ya ikolojia. Ni kushindwa kuifahamu mifumo ya kibinadamu inayozunguka mazingira hayo.
Nimekuwa nikifanya kazi mashariki mwa Kongo tangu mwaka wa 2001, kwa hiyo takriban miaka 25 sasa. Nilipofika hapa kwa mara ya kwanza, nilitarajia uhifadhi kuwa mgumu, lakini nilishangazwa na jinsi ambavyo mara nyingi mbinu hiyo haikuendana na hali halisi.
Hiyo haifanyi kazi hapa. Muktadha ni tata sana. Unapambana na migogoro na umaskini uliokithiri, na changamoto za utawala.

Kufanya kazi katika mbuga ya Virunga kulilazimisha njia tofauti ya kufikiri. Unapowajibika si tu kwa wanyamapori bali pia kwa usalama wa watu, huwezi kumudu kuikosea. Vigingi ni vikubwa mno. Hiyo inakusukuma kuangalia mfumo mzima, si tu wanyama au msitu, bali pia uchumi, miundo ya utawala na motisha inayoipa msukumo tabia.
Baada ya muda, hiyo imeunda mtazamo tuliouchukua. Si s>uala la kutumia mbinu iliyoainishwa awali, bali ni kuhusu kuelewa mienendo mahususi ya mahali na kujenga kitu kinachojibu masharti hayo.
Hapo ndipo mtazamo huo unatoka. Sio kinadharia. Ni jibu kwa hali halisi ya ardhini.
Unaweza kuelezea Virunga namna gani, kwa maana ya umuhimu wake wa kiikolojia na mazingira iliyonayo leo?
Virunga ndiyo mbuga ya kitaifa kongwe zaidi barani Afrika, iliyoanzishwa mnamo mwaka wa 1925. Ilianzishwa kwa sababu ya thamani yake ya ajabu ya kibiolojia, na hiyo inasalia kuwa kweli leo. Ukubwa na utofauti wa mazingira ni vigumu kueleza kwa ukamilifu. Unaanzia kwenye barafu za Milima ya Rwenzori, zaidi ya futi 17,000, ukishuka kupitia maeneo ya Alpine na kwenye msitu mnene wa kitropiki, na kisha zaidi kwenye savanna na ardhioevu.
Kando ya mwinuko huo, mbuga hiyo inasaidia aina mbalimbali za kipekee za spishi. Ina utofauti wa ajabu wa mamalia na wanyama wanaotambaa, na zaidi ya spishi 700 za ndege. Pia ni moja ya maeneo machache pekee ulimwenguni ambapo unaweza kupata aina tatu za nyani wakubwa ambao ni sokwe wa milimani, sokwe, na sokwe mtu mdogo (bonobos) katika mazingira hayo.
Lakini Virunga hufafanuliwa zaidi na migogoro kama ilivyo kwa ikolojia. Tangu katikati ya miaka ya 1990, kufuatia mauaji ya kimbari ya Rwanda, eneo hilo limekuwa kitovu cha ukosefu wa utulivu wa muda mrefu.
Athari k>wa binadamu imekuwa kubwa sana. Makadirio yanaonyesha kuwa kati ya watu milioni nane hadi kumi na moja wamekufa kote mashariki mwa Kongo katika kipindi hiki.
Mgogoro huo umekuwa na athari za moja kwa moja na mbaya kwa wanyamapori. Kati ya mwishoni mwa miaka ya 1990 na mwanzoni mwa miaka ya 2000, idadi kubwa ya mamalia katika mbuga ilipungua kwa asilimia 80 hadi 95.

Sokwe wa milimani walikuwa tofauti, lakini si kwa sababu walikuwa wametengwa na mgogoro. Walinusurika kwa sababu ya kulindwa vyema na walinzi, mara nyingi kwa hatari kubwa ya kibinafsi. Zaidi ya walinzi mia mbili wameuawa wakiwa kazini.
Kinachoifanya mbuga ya Virunga kuwa mbuga isiyo ya kawaida si tu kwamba mzozo upo pamoja na bayoanuwai, lakini kwamba mambo hayo mawili yanaingiliana kwa kina.
Ndiyo maana mbuga hiyo haiwezi kueleweka kama eneo la uhifadhi. Ni mandhari ambapo mifumo ya kiikolojia, kiuchumi, na kisiasa hukutana.
Je, kulikuwa na wakati maalum au uzoefu uliobadilisha kimsingi jinsi unavyofikiri kuhusu uhifadhi katika mbuga ya Virunga?
Mnamo mwaka 2007, tulipitia kipindi kilichotulazimisha kuwazia upya kile tulichokuwa tunafanya. Kulikuwa na mfululizo wa mauaji ya sokwe wa milimani.

Wakati huohuo, walinzi wetu walikuwa wakishambuliwa kila mara. Tulikuwa tukipoteza watu, na licha ya jitihada zote tulizoziweka kwenye ulinzi, tulikuwa tukishindwa kupata aina moja ya spishi tuliyokuwa pale kulinda.
Kuna picha iliyokaa nami tangu kipindi hicho. Inaonyesha kundi la wanawake waliosimama katika mpaka wa mbuga hiyo, wakimwomba ruhusa mwanamume mwenye bunduki kuingia na kukata miti kwa ajili ya makaa.
Wanawake hao wanahitaji mkaa kupika chakula na kuchemsha maji. Bila hivyo, hawawezi kuishi.
Tulipozama zaidi, kiunga hicho kikawa wazi. Mji wa Goma, wenye wakazi wapatao milioni mbili, ulitegemea karibu kabisa mkaa kwa ajili ya nishati.
Mauaji hayakuwa ya kubahatisha. Yalikuwa ya kimkakati.
Tulipoelewa hilo tu, ilibadilisha namna tulivyofikiri kuhusu tatizo.
Chanzo kikuu kilikuwa ukosefu wa njia mbadala zinazofaa. Utambuzi huo uliashiria mabadiliko. Hilo ndilo lililopelekea kuhama kuelekea kwa nishati, na kwa upana zaidi, kuelekea kujenga mfumo mbadala wa kiuchumi.
Je, unaweza kuzungumzia makabiliano na kampuni ya SOCO, kushambuliwa kwako, na kile ambacho uzoefu huo ulikufundisha kuhusu jukumu la vyombo vya habari na uwajibikaji?
Wakati mmoja, tishio kubwa zaidi kwa mbuga ya Virunga halikutoka kwa wanamgambo au shinikizo la ndani. Lilitoka kwa kampuni ya mafuta. Kampuni ya kimataifa ya SOCO, kampuni iliyoorodheshwa nchini Uingereza, ilikuwa imepata haki za uchunguzi ambazo zilipishana na hifadhi hiyo. Iwapo wangeendelea, ingekuwa kimsingi ilibadilisha mustakabali wa mazingira.
Kilichofanya iwe vigumu hasa ni kwamba huu haukuwa tu mzozo wa kiufundi au kimazingira. Kulikuwa na ghasia karibu yake. Watu katika jamii walitishwa, waliwekwa kizuizini, na wakati fulani waliteswa. Ilibainika kuwa hili halikuwa jambo ambalo lingeweza kutatuliwa kupitia njia za kawaida pekee.
Tulitumia miaka kadhaa kujaribu kuelewa jinsi ya kujibu. Moja ya funzo kuu lilikuwa juu ya mamlaka. Ikiwa unategemea tu mifumo ya kisheria ya ndani katika mazingira tete, ni vigumu sana kuiwajibisha kampuni, hasa inapofanya kazi kimataifa.
Kampuni ya SOCO iliorodheshwa nchini Uingereza. Hiyo ilimaanisha kulikuwa na uwezekano wa njia ya kisheria kupitia mamlaka ya Uingereza, haswa kuhusu rushwa. Lakini kupata kesi katika ngazi hiyo inahitaji zaidi ya ushahidi. Inahitaji umakini.
Hapo ndipo vyombo vya habari vikawa muhimu.
Tulianza kunakili kile kinachotokea; kukusanya ushahidi, kujenga kesi. Baada ya muda, hiyo ilikua kuwa katika mkusanyiko mkubwa wa nyenzo. Lakini pia tuligundua kuwa ushahidi pekee haungetosha. Mfumo huu unabanwa na rasilimali, na kesi hupewa kipaumbele kulingana na kile kinachochukuliwa kuwa cha manufaa kwa umma. Kwa vitendo, mara nyingi hili linamaanisha kujulikana.
Kwa hivyo, tulifanya uamuzi wa kugeuza uchunguzi kuwa filamu. Hatua hiyo ikasababisha kutengenezwa kwa filamu iitwayo Virunga. Ilikuwa ni njia ya kuleta hadithi katika uwanja wa umma kwa njia ambayo ingekuwa vigumu kupuuzwa.
Tulikuwa makini katika jinsi tulivyoishughulikia. Kabla ya kuzindua filamu, tuliipa kampuni ya SOCO fursa ya kujibu. Ilikuwa muhimu kwamba mchakato ubaki wa kuaminika na wa kisheria.
Wakati huohuo, tulikusanya kesi ya kina; mamia ya kurasa za ushahidi, tulirekodi ufisadi na ukiukwaji wa haki za binadamu. Nyenzo hiyo iliwasilishwa kwa mamlaka husika.
Ni katika kipindi hiki niliposhambuliwa.
Baada ya kupeleka hati katika Mahakama ya Goma, nilikuwa nikiendesha gari kuelekea mbugani. Barabarani, watu wenye silaha walikuwa wakisubiri. Walifyatua risasi kwenye gari. Nilipigwa risasi mara mbili kifuani.
Nilifaulu kutoka kwenye gari na kuingia msituni. Wakati huo, ilikuwa ni suala la kuokoka. Wanakijiji wa eneo hilo walinipata na kunipeleka hospitalini kwa pikipiki.
Ilikuwa nusura nipoteze maisha.

Muda mfupi baadaye, filamu hiyo ilizinduliwa. Ilipata utambulizi wa kimataifa. Leonardo DiCaprio alihusika kama mtayarishaji mkuu, na ilifikia hadhira kubwa kupitia majukwaa makubwa ya usambazaji. Wakati huo huo, mashirika kama Human Rights Watch yalifanya uchunguzi wao wenyewe.
Mojawapo ya matokeo muhimu yalikuwa ushahidi wa moja kwa moja wa malipo kutoka kwa wawakilishi wa kampuni kwenda kwa vikundi vyenye silaha vinavyofanya kazi katika eneo hilo. Hi<lo <llibadilisha hali hiyo kwa kiasi kikubwa.
Hakukuwa na mashtaka rasmi ambayo yalifikia hitimisho. Lakini athari ilikuja kupitia njia zingine. Mchanganyiko wa ushahidi, udhihirisho wa vyombo vya habari, na hatari ya sifa iliathiri msimamo wa kampuni. Thamani yake ilishuka sana, na shinikizo likawa lisiloweza kudumu.
Hatimaye, kampuni ya SOCO ilijiondoa kwenye mbuga ya Virunga.
Matokeo hayo yaliunda namna tunavyofikiria kuhusu jukumu la vyombo vya habari. Ilionyesha kuwa uandishi wa habari na umakini wa umma unaweza kuwa na athari ya moja kwa moja kwenye matukio; si tu kuwafahamisha watu, bali pia kuishawishi mifumo inayoamua uwajibikaji.
Pia ilisisitiza umuhimu wa kujenga njia mbadala.
Kusimamisha mradi wa mafuta ilikuwa hatua moja. Lakini haikutatua tatizo la kimsingi, ambalo ni jinsi ya kutengeneza thamani ya kiuchumi bila kuharibu mazingira.
Hilo ndilo lililoongoza moja kwa moja katika awamu inayofuata ya kazi, kuwekeza katika nishati mbadala na kujenga mtindo tofauti wa kiuchumi kwenye mbuga.
Kwa maana hiyo, makabiliano na kampuni ya SOCO hayakuwa tu ya kuzuia mradi maalum. Ilikuwa ni sehemu ya mpito mpana zaidi, kutoka kutetea mbuga dhidi ya vitisho vya nje hadi kuunda mfumo ambao hufanya vitisho hivyo kutowezekana kabisa.
Je, unafikiria vipi kuhusu gharama ya uhifadhi kutoka kwenye mtazamo wa jamii zinazoishi karibu na hifadhi?
Ukitataka kuelewa ni kwa nini mapambano ya uhifadhi katika maeneo kama vile mashariki mwa Kongo, unapaswa kuangalia uchumi kutoka kwa mtazamo wa watu wanaoishi huko.
Hifadhi ya kitaifa ya Virunga ni Urithi wa dunia. Inatoa thamani katika kiwango cha kimataifa; bioanuai, hifadhi ya kaboni, huduma za mfumo wa ikolojia ambazo zinanufaisha watu mbali zaidi ya eneo. Lakini manufaa hayo si yale ambayo jamii hupata uzoefu kila siku. Wanachopitia ni gharama.
Iwapo familia itabadilisha hekta moja ya msitu kuwa ardhi ya kilimo, wanaweza kuzalisha kati ya $1,200 na $1,500 kwa mwaka. Hayo ni mapato makubwa katika muktadha huu. Unapoongeza kiwango hicho katika mbuga, mamia ya maelfu ya hekta, unaziomba jamii za wenyeji kuacha uwezekano wa kupata zaidi ya dola bilioni kila mwaka.
Hiyo sio namba ya kufikirika. Inatafsiriwa katika mabadiliko halisi. Ni tofauti kati ya kuweza kulisha familia au kutoweza kulisha familia, kulipia ada ya shule, kupata huduma za kimsingi.
Wakati huo huo, vikwazo vilivyowekwa na uhifadhi ni vya karibu sana na vinaonekana. Watu wanazuiwa kupata ardhi, kukata miti kwa ajili ya kuni, kutumia rasilimali ambazo wanazitegemea kwa ajili ya kuishi.
Kuna picha inayonasa hii kwa uwazi sana. Inaonyesha kundi la wanawake wakiwa wamesimama kando ya mbuga, wakimwomba ruhusa mwanamume mwenye bunduki kuingia na kukusanya mkaa. Kwa mtazamo wa kwanza, majukumu yanaonekana dhahiri, kwamba wanawake ni wahasiriwa, na mtu mwenye silaha ni mtekelezaji. Lakini kwa kweli, zote mbili ni sehemu ya mfumo mmoja.
Wanawake wanahitaji mkaa kupika chakula na kuchemsha maji. Bila hivyo, hawawezi kukidhi mahitaji ya kimsingi. Mtu mwenye bunduki anatekeleza sheria ambayo huenda haamini kabisa, lakini ambayo anatakiwa kuizingatia. Pia anafanya kazi ndani ya mfumo unaotokana na uhasama na uhaba.
Hapa ndipo wazo la ukosefu wa haki linapokuja. Jamii ya kimataifa inafaidika kutokana na ulinzi wa misitu, lakini gharama hiyo inabebwa mashinani na baadhi ya watu maskini zaidi duniani. Wakati usawa huo unakuwa mkubwa sana, watu huanza kukataa mfumo.
Na wanapoikataa, hawajitengi tu, wanatafuta njia mbadala. Katika muktadha huu, njia hizo mbadala mara nyingi huhusisha wanamgambo au mifumo isiyo rasmi inayoruhusu ufikiaji wa rasilimali nje ya sheria.
Ndivyo uhifadhi, usipotengezwa ipasavyo, unaweza kuchangia kukosekana kwa uthabiti. Inaunda maeneo yenye mkazo ambayo yanaweza kutumiwa na makundi yenye silaha.
Ndiyo maana suala hilo haliwezi kushughulikiwa kwa njia ya utekelezaji pekee. Unaweza kuongeza doria, kuimarisha sheria, na kuweka vikwazo, lakini iwapo uchumi wa msingi unabaki bila kubadilika, shinikizo halitoweki, bali huongezeka.

Kinachotakiwa badala yake ni kusawazisha upya gharama na manufaa. Ikiwa kulinda msitu kunaweka gharama kwa jamii za wenyeji, basi mfumo unapaswa kutoa chanzo mbadala cha mapato ambacho angalau ni cha kuvutia kama kile kinachopotea.
Huo ndio msingi wa mbinu tuliyoichukua. Lengo si tu kupunguza shughuli haramu, bali kubuni muundo wa kiuchumi ambao uhifadhi unakuwa chaguo la busara zaidi.
Hadi usawa huo upatikane, uhifadhi utaendelea kutatizika katika mazingira kama haya.
Ni jukumu lipi lililopo katika uchumi haramu katika kuendeleza mgogoro ndani na karibu na hifadhi ya Virunga?
Wanamgambo hawafanyi kazi katika mazingira yasiyo na mfumo. Wao ni sehemu ya mfumo wa kiuchumi unaofanya kazi.
Mfumo huo umejengwa juu ya uchimbaji na usafirishaji haramu wa maliasili.
Kila ripoti kutoka Kundi la Wataalamu la Umoja wa Mataifa tangu mwaka wa 2001 imetaja hii kama sababu kuu ya migogoro mashariki mwa Kongo.
Mara tulipoelewa hilo, athari yake ilikuwa moja kwa moja. Huwezi kutatua mzozo kwa utekelezaji peke yake.
Kwa nini uliangazia nishati kama kianzilishi, na hiyo imeundaje mtazamo mpana zaidi katika hifadhi ya Virunga?
Tuliporejea baada ya mzozo wa mwaka 2007, ilionekana wazi kuwa kila kitu tulichokuwa tunashughulikia; biashara ya mkaa, wanamgambo, shinikizo kwenye msitu, vilifungamanishwa na suala moja: nishati.
Mkaa haukuwa shida ya mazingira tu. Ilikuwa msingi wa uchumi wa ndani na, wakati huo huo, moja ya vyanzo vikuu vya mapato kwa vikundi vilivyo na silaha. Iwapo ulitaka kubadilisha chochote, ilikulazimu kuanzia hapo.
Hifadhi ya Virunga ni mandhari ya milima yenye mvua nyingi sana. Mito hubeba nishati nyingi. Kwa hivyo tulianza kuangalia ikiwa tunaweza kukamata hiyo na kuibadilisha kuwa umeme. Hiyo ndiyo ilikuwa hatua ya kuanzia, kujenga mitambo ya kuzalisha umeme kwa maji ambayo yanaweza kusambaza nguvu za umeme ndani ya nchi.
Mwanzoni, ilikuwa majaribio. Lakini baada ya muda, tulitengeneza mfumo. Sasa tuna mitambo mingi ya maji, na bei ya umeme imeshuka hadi kufikia kiwango ambacho ni nafuu zaidi kuliko mkaa. Hayo ndiyo mabadiliko muhimu. Mara tu umeme unapokuwa chaguo la bei nafuu zaidi, tabia hubadilika. Watu hawana haja ya kutegemea kukata msitu.
Kilichofuata hapo haikuwa mradi wa nishati tu, bali msingi wa uchumi.
Tuliiunda kama huduma, lakini inafanya kazi kama biashara ya kijamii. Tunazalisha nishati, kujenga na kudumisha miundombinu, kudhibiti gridi ya taifa na kushughulikia utozaji. Mapato yanawekwa tena kwenye mfumo, katika mbuga na katika maendeleo ya jamii.
Leo, kampuni inazalisha umeme zaidi kwa idadi ya watu kuliko shirika la kitaifa. Hilo halikuwa lengo la awali, lakini linaonyesha kiwango cha ukuaji uliopatikana.

Changamoto inayohusiana imekuwa namna ya kudumisha usambazaji wa nishati katika eneo linalotumika la migogoro. Katika miji mingi, umeme unategemea njia moja ya upitishaji wa nguvu ya juu ya umeme. Katika sehemu ya mashariki mwa Kongo, huo ni udhaifu mkubwa. Wakati mapigano yanapozidi, njia hizo mara nyingi hulengwa au kuharibiwa, na kuzirekebisha huwa ni hatari sana.
Ili kukabiliana na hili, tulisanifu upya mfumo ili kujenga upungufu katika gridi ya taifa. Badala ya kutegemea njia moja, tulitengeneza njia za upokezaji sambamba na kile tunachoita “laini za kuunganisha” kati yao. Ikiwa mstari mmoja umekatwa, nguvu inaweza kubadilishwa kwa njia ya pili.
Iwapo zote mbili zimeharibiwa, mfumo unaruhusu umeme “kupindapinda” kuzunguka maeneo yaliyoathirika, yakidumisha usambazaji wa huduma muhimu kama vile vituo vya kusukuma maji vya Goma. Ni muundo usio wa kawaida sana, gridi ya taifa iliyoundwa kufanya kazi katikati ya vita, lakini inaonyesha picha halisi ya hali wanayoendesha.
Jambo muhimu ni kwamba nishati sio tu kutoa mwangaza. Inawezesha kila kitu kingine. Mara baada ya kuwa na umeme wa kuaminika, unaweza kuanza kujenga biashara, karakana za kuchomelea vyuma, friji, useremala, viwanda vidogo. Unaanza kuona safu nzima ya shughuli za kiuchumi ambazo hazikuwezekana hapo awali.
Hapo ndipo hatua iliyofuata ilipokuja, ambayo ni fedha.
Moja ya vikwazo tulivyokutana navyo ni kwamba watu hawakuweza kupata mtaji. Licha ya umeme kupatikana, hawakuwa na uwezo wa kuwekeza kwenye vifaa au kuanzisha biashara. Mifumo ya jadi ya benki haifanyi kazi vyema katika muktadha huu. Gharama za muamala ni kubwa mno, na hatari huchukuliwa kuwa kubwa mno.
Hivyo tulianza kufikiria tena namna fedha inaweza kufanya kazi katika mazingira haya. Suluhisho tulilotengeneza lilikuwa kuunganisha huduma za kifedha moja kwa moja kwenye mfumo wa nishati kupitia mita za kidijitali.
Kila muunganisho kwenye gridi ya taifa hufuatiliwa kupitia mita inayofuatilia matumizi ya umeme. Data hiyo inakuwa mwakilishi wa shughuli za kiuchumi. Iwapo una miezi sita ya matumizi thabiti, moja kwa moja una rekodi ya utendaji wa biashara yako. Hiyo inaweza kutumika kama njia ya kustahili mikopo.
Badala ya kupitia benki ya kawaida, biashara ndogo inaweza kupata mkopo kupitia mfumo. Kisha malipo yanahusishwa moja kwa moja na matumizi yao ya umeme. Ikiwa watalipa mkopo, wanaendelea kupokea nguvu za umeme. Ikiwa hawana, mfumo unaweza kuzima usambazaji.
Inaondoa uhitaji wa dhamana na inapunguza kwa kiasi kikubwa gharama ya kusimamia mikopo.
Uchumi wake ni muhimu. Gharama ya umeme mbadala ni chini sana kuliko umeme unaozalishwa kwa dizeli. Hata unapoongeza malipo ya ziada ili kurejesha mkopo, jumla ya gharama inasalia chini ya ile ambayo watu wangelipa kwa nishati.
Hiyo inatengeza tatizo la hali ambapo daima ni kwa maslahi ya akopaye hulipa. Ni nafuu kukaa ndani ya mfumo kuliko kuanguka nje yake.
Hii imeturuhusu kupanua ufadhili kwa watu ambao wangetengwa kabisa. Pia huharakisha maendeleo ya biashara ndogo ndogo, ambazo huongeza mahitaji ya umeme. Mifumo miwili inaimarisha kila mmoja.
Tumeunda hili kupitia shirika la ufadhili mdogo, ushirikiano ambao hubadilisha gridi ya nishati kuwa jukwaa la kifedha. Malipo yanaweza kufanywa moja kwa moja kupitia mita za kidijitali. Katika baadhi ya matukio, inafanya kazi karibu kama benki ndani ya makazi.
Hii inachokifanya ni kuanza kuvunja kile unachoweza kukiita mtego wa umaskini. Watu wanapata nishati, kisha mitaji, kisha shughuli za kujiongezea kipato. Hatua hiyo inaunda njia ya kutoka kwa utegemezi wa shughuli za uchimbaji au haramu.
Kwa kiwango kikubwa, mfumo wa nishati pia unasimamia upande wa uchumi wa viwanda. Inaturuhusu kukuza vifaa vya usindikaji kwa mfano, katika kilimo ili thamani iundwe ndani badala ya kuuzwa nje.
Hii yote inachangia kuhamisha usawa kutoka kwa uchumi wa vita. Wanamgambo wanategemea kudhibiti rasilimali kama vile makaa na mazao ya kilimo. Unapozindua mfumo mbadala ambao ni bora na wenye faida zaidi, unaanza kuharibu udhibiti huo.
Sio mara moja, na haujakamilika. Lakini baada ya muda, athari zake huongezeka.
Lengo pana ni kujenga uchumi unaojitegemea. Kwa makusudi, tumeachana na kutegemea ruzuku pekee. Ruzuku zina kikomo. Zinapoisha, mfumo huanguka ikiwa haujaweza kutumika peke yake.
Kwa kujenga miundombinu ya kuzalisha mapato, nishati, fedha, sekta; unaunda muundo ambao unaweza kuendelea kufanya kazi na kupanuka.
Kiukweli, huo ndio msingi wa mbinu.
Unaanza na nishati. Nishati huwezesha biashara. Biashara hutengeneza ajira. Ajira hupunguza motisha ya migogoro.
Na yote hayo, iwapo imeundwa vyema, hupunguza shinikizo katika msitu.
Ni vipi uundaji wa nafasi za ajira unaendana na mkakati wako wa kupunguza migogoro na kuwaunganisha tena watu ambao pengine wanaweza kujiunga na makundi yenye silaha?
Moja ya mambo muhimu tuliyojifunza ni kwamba migogoro, katika muktadha huu, sio tu ya kiitikadi au kisiasa, bali ni ya kiuchumi. Watu hawajiungi na vikundi vyenye silaha kwa sababu wanataka kupigana. Wanajiunga kwa sababu hakuna njia mbadala. Iwapo unataka kupunguza vurugu kwa njia ya kudumu, unapaswa kushindana katika soko la ajira.
Hiyo ilijitokeza wazi mara tulipoanza kutengeza mfumo wa nishati. Umeme hautumiki tu katika makazi; inawezesha shughuli za kiuchumi. Biashara ndogo ndogo huanza kuibuka; uchomeleaji wa vyuma, useremala, kusaga nafaka, matumizi ya friji, usindikaji wa vyakula. Kisha unaanza kuona shughuli kubwa zaidi kama vile viwanda, karakana, watoa huduma. Kila safu hutengeneza ajira.
Tulianza kupima hili kwa muda, na uhusiano ni thabiti kabisa. Kwa kila megawati ya umeme inayoletwa katika uchumi wa ndani, unabuni kati ya ajira 800 na 1,000. Hiyo sio ya kinadharia, tumeifuatilia kwa miaka mingi ya operesheni.
Unapoanza kuongeza hiyo, idadi zinakuwa muhimu. Mfumo tunaojenga una uwezo wa kuzalisha makumi kwa maelfu ya ajira, na katika miaka kadhaa iliyopita, tayari tumeunda idadi kubwa.
Kinachokuwa na umuhimu zaidi ni nani anajaza kazi hizo. Tulipokagua wafanyikazi, tuligundua kuwa sehemu ya maana, karibu mtu mmoja kati ya kumi, walikuwa watu ambao hapo awali walikuwa wanachama wa makundi yaliojihami kwa silaha.
Hayo ni mabadiliko muhimu. Inaonyesha kuwa wakati njia mbadala zinapatikana, watu hujitenga na uhamasa. Sio kwa sababu ya itikadi, ila kwa sababu gharama ya fursa inabadilika. Kama unaweza kupata mapato thabiti, kusaidia familia yako, na kuishi bila hatari ya kila wakati, hilo linakuwa chaguo la busara.
Muundo wa kazi hizi pia ni muhimu. Si nafasi za muda mfupi au zinazofadhiliwa na watu wa nje. Zimefungamana na mifumo ya kiuchumi inayofanya kazi; uzalishaji wa nishati, kilimo, usindikaji, vifaa. Hiyo inawafanya kudumu.
Wakati huo huo, tumelazimika kufikiria kwa makini namna ya kuunganisha watu katika mifumo hii. Haitoshi kubuni kazi; ni sharti ujenge uwezo wa kuzijaza. Ndiyo maana mafunzo ni sehemu kuu ya kielelzo kutoka kwa ujuzi wa kiufundi katika uhandisi na matengenezo hadi majukumu katika utengenezaji na huduma.
Katika baadhi ya matukio, mabadiliko ni ya moja kwa moja kabisa. Mtu ambaye anaweza kivyengine kuvutiwa katika shughuli za wanamgambo badala yake anaingia kwenye programu ya mafunzo, kisha anahamia kwenye ajira kwenye mojawapo ya sekta hizi. Baada ya muda, hiyo inaunda aina tofauti ya muundo wa kijamii, ambapo ushiriki wa kiuchumi unachukua nafasi ya kutegemea vikundi vilivyo na silaha.

Pia kuna athari pana katika ngazi ya jamii. Kadiri ajira inavyoongezeka, uchumi wa ndani unaimarika. Hali hiyo inapunguza motisha ya kuhama na kurahisisha watu kubaki mahali. Pia huimarisha uhalali wa mifumo inayotoa fursa hizo iwe hiyo ni bustani, serikali, au sekta ya kibinafsi inayoibuka.
Kati ya haya si ya papo hapo. Inachukua muda kujenga shughuli za kutosha za kiuchumi ili kuhamisha usawa. Lakini mara tu inapofikia kiwango fulani, athari huongezeka.
Hifadhi, kwa maana hiyo, si tena eneo lililohifadhiwa. Inakuwa sehemu ya mfumo mkubwa wa kiuchumi ambao hutoa njia mbadala kwa miundo inayoendeleza migogoro.
Na hatimaye, hivyo ndivyo ujumuishaji upya unavyoonekana katika muktadha huu. Sio programu tofauti. Ni matokeo ya kujenga uchumi ambao watu wanaweza kuingia badala ya mgambo.
Ni mabadiliko gani ya kiusalama uliyoyafanya, na vipi mifumo kama vituo vya uendeshaji wa mbele na majibu ya haraka yanavyolingana na mbinu yako viwanjani?
Usalama ndio msingi kwa kila kitu tunachojaribu kufanya. Bila usalama, hakuna mfumo wowote wa kiuchumi unaozuia. Uwekezaji hauji, biashara hazifanyi kazi, na watu hurudi kwenye mikakati ya kuishi ambayo mara nyingi huimarisha uhasama.
Tulichopata mapema ni kwamba mbinu ya kawaida ya usalama katika maeneo haya haikuwa ikifanya kazi. Nyakati za majibu zilikuwa polepole sana, mara nyingi saa sita, wakati mwingine siku kadhaa. Kufikia wakati uingiliaji kati wowote ulipofika, uharibifu ulikuwa tayari umefanyika. Hilo huleta hali ambapo jamii huhisi kuachwa, na imani hiyo inapopotea, ni vigumu sana kuijenga upya.
Kwa hivyo, tulizingatia kupunguza wakati huo wa majibu ya kasi. Hatua ya kwanza ilikuwa kubuni mfumo ambapo jamii yenyewe huanzisha majibu. Tulisambaza makumi kwa maelfu ya “vitufe vya dharura” vilivyounganishwa kupitia mtandao wa redio wa masafa marefu. Mtu anapobonyeza kitufe, huenda moja kwa moja kwenye kituo kikuu cha usalama. Kuanzia hapo, tuna itifaki kali: kubali ndani ya dakika chache, tumana haraka, na fika eneo la tukio ndani ya takriban dakika ishirini.
Hilo pekee linabadilisha nguvu. Wakati watu wanajua kwamba msaada utafika haraka, mazingira ya kisaikolojia hubadilika. Inajenga hisia ya ulinzi ambayo hapo awali haikuwepo.
Lakini majibu ya haraka ni sehemu moja tu ya mfumo. Ya pili ni namna nguvu zinavyowekwa na kusimamiwa ardhini. Hapo ndipo misingi ya Uendeshaji Mbele; (Forward Operating Bases – FOBs)< kwa kimombo inapoingia.
Hii sio mitambo ya kawaida ya kijeshi. Imeundwa mahsusi kwa muktadha huu. Kimwili, ni misombo iliyoimarishwa, iliyojengwa kwa kuta zilizoimarishwa zenye uwezo wa kuhimili mashambulizi, ikiwemo silaha nzito nzito. Ndani, huweka vitengo vya jeshi katika mazingira yaliyodhibitiwa.
Sababu ya kubuni hiyo ni muhimu. Katika maeneo mengi ya vijijini, wakati askari wamewekwa moja kwa moja ndani ya jamii, husababisha mvutano na mara kwa mara husababisha unyanyasaji au utumiaji mbaya. Kwa kuziweka ndani ya sehemu salama, zinazojitosheleza, unaunda utengano kati ya wanajeshi na raia. Wanajeshi wanalindwa, wanasambaziwa vizuri zaidi, na wana nidhamu zaidi, na jamii haidhulumiwi kutokana na uwepo wao wa kila siku.
Wakati huo huo, muundo wa amri ni tofauti. Jeshi lipo, lakini linafanya kazi chini ya mfumo unaotanguliza ulinzi wa raia. Mamlaka ya hifadhi za taifa, kupitia walinzi wake, hudumisha uangalizi katika vituo hivi, na mfumo umeundwa ili uingiliaji kati uchochewe na jamii badala ya kulazimishwa nje.
Kwa maneno ya vitendo, kila misingi ya Uendeshaji Mbele, yaani FOBs inakuwa sehemu ya msingi ya mfumo mpana. Inatoa ulinzi wa usalama kwa eneo lililobainishwa, inasaidia mwitikio wa haraka, na kuunda hali ambayo shughuli za kiuchumi zinaweza kufanyika.
Mfano wa Mutwanga unaonyesha jinsi hii inavyofanya kazi. Kabla ya mfumo huo kuwekwa, mji ulikuwa chini ya mashambulizi ya mara kwa mara. Katika kipindi kifupi, makumi ya watu waliuawa, na idadi kubwa ya watu walikimbia. Mwitikio wa jeshi ulikuwa polepole na hauendani.
Tulifanya kazi na jamii, viongozi wa kidini, na wanajeshi kuanzisha kituo na mfumo unaohusika wa kukabiliana. Jamii ilichangia kazi kuijenga, maelfu ya watu walijitokeza, na msingi ulijengwa kwa muda wa siku chache.
Mara tu ilipoanza kufanya kazi, tofauti ilikuwa haraka. Mchanganyiko wa uwezo wa mwitikio wa haraka na uwepo wa kudumu na salama ulibadilisha motisha kwa vikundi vilivyojihami. Mashambulizi yakawa magumu zaidi kutekelezwa, na kiwango cha ghasia kilipungua sana. Katika kipindi cha tangu mfumo huo uanzishwe, hakujakuwa na vifo vingine vya raia katika eneo hilo.
Lakini misingi ya Uendeshaji Mbele, yaani FOBs sio tu muundo wa kujihami. Ni sehemu ya mtindo mpana zaidi unaounganisha usalama na uchumi. Karibu na kila kituo, tunakuza shughuli za kiuchumi kama kilimo, usindikaji, viwanda vidogo. Wazo ni kwamba kituo kinaunda eneo la utulivu, na ndani ya eneo hilo, uchumi unaweza kuanza kufanya kazi.
Hii wakati mwingine huelezewa kama njia ya “tuzo na adhabu”. “Adhabu” ni uwezo wa kujibu haraka na kuzuia vurugu. “Tuzo” ni maendeleo ya njia mbadala ya kiuchumi ambayo ni kazi, mapato, miundombinu.
Vitu hivyo viwili ni sharti vifanye kazi kwa pamoja. Iwapo unatoa usalama tu, hautashughulikia vichochezi vya msingi vya migogoro. Iwapo unatoa fursa za kiuchumi tu bila usalama, uwekezaji huo unakamatwa au kuharibiwa.

Kipengele kingine muhimu ni uendelevu. Vituo hivi vimeundwa ili kujifadhili baada ya muda kupitia shughuli za kiuchumi zinazounga mkono. Hiyo ni tofauti muhimu kutoka kwa mifumo ya jadi ya kulinda amani, ambayo inategemea ufadhili endelezi wa nje.
Kwa kiwango kikubwa, Ukanda huo unatazamia mtandao wa Uendeshaji Mbele, yaani FOBs hizi, kila moja ikioanishwa na kitovu cha uchumi. Kwa pamoja, wanaunda mfumo uliosambazwa wa usalama na maendeleo katika mazingira yote.
Ni mfano usio wa kawaida. Shirika la uhifadhi kwa kawaida halihusiani na kujenga na kusimamia miundombinu ya usalama katika ngazi hii. Lakini katika muktadha huu, ambapo vichochezi vya migogoro vinahusishwa moja kwa moja na maliasili, inakuwa ni nyongeza ya lazima ya mamlaka.
Hatimaye, lengo si kuweka ujeshi kwenye uhifadhi. Ni kuunda hali ambapo watu na mifumo ikolojia inaweza kuwepo bila tishio la kila mara.
Bila msingi huo, hakuna kitu kingine kinachoshikilia.
Je, unaweza kufafanua namna kitu kama vile uzalishaji wa kakao unavyohusishwa na migogoro, na ulichokifanya kubadilisha hali hiyo?
Kakao ni mfano mzuri wa jinsi uchumi unavyohusishwa na ghasia mashariki mwa Kongo. Inaonekana kama bidhaa ya kawaida ya kilimo kutoka nje, lakini mashinani, imenaswa sana na migogoro.
Katika maeneo yanayodhibitiwa na wanamgambo wa ADF, mfumo mzima umeundwa katika kulazimishwa. Mpangilio huo ni thabiti sana. Mwanzoni mwa msimu wa mavuno kwa kawaida karibu na mwezi wa Agosti, na tena mwezi wa Februari,kuna kupanda kwa vurugu. Wanamgambo hao hufanya mashambulizi kwenye vijiji na mashamba. Watu wanauawa, au wanakimbia. Lengo sio la kubahatisha; ni kusafisha mashamba.
Pindi wakulima wakiondoka wote, kakao inaachwa imesimama. Wanamgambo kisha huingia na kuwalazimisha watu kuvuna, kuchachusha na kukausha kokwa za kakao. Mchakato huo wa uvunaji, uchachushaji na ukaushaji unachukua wiki kadhaa. Baada ya hapo, bidhaa hiyo husafirishwa kuvuka mpaka, mara nyingi hadi Uganda, ambako huingia kwenye mnyororo wa usambazwaji wa kimataifa chini ya uasili tofauti.
Kwa hivyo, kile kinachoonekana kama bidhaa ya kawaida ya kuuza nje ni, kwa kweli, kufadhili mojawapo ya makundi yenye ghasia zaidi katika eneo hilo.
Changamoto ni kwamba udhaifu umejengwa katika muundo wa mnyororo wa thamani. Kakao inahitaji muda, maganda yake huvunwa, kisha kuchachushwa na kukaushwa kwa wiki kadhaa. Katika kipindi hicho, bidhaa hukaa kwenye shamba, jambo linalowafanya wakulima kuwa na walengwa.
Hatua tuliyoanzisha ilikuwa ni kuondoa athari hiyo kwa haraka iwezekanavyo. Badala ya wakulima kuhifadhi mavuno yao, timu zetu hutoka kila siku na kununua maganda moja kwa moja. Bidhaa hiyo kisha husafirishwa kwa haraka hadi mahali salama kwa usindikaji.
Hiyo hufanya mambo mawili. Kwanza, inapunguza udhihirisho wa wakulima, kwa sababu hawana tena mazao ya thamani kwenye ardhi yao. Pili, inakataza ufikiaji wa wanamgambo kwa bidhaa hiyo. Kama hakuna kitu chochte cha kukamata, kichocheo cha mashambulizi hupungua.
Wakati huo huo, tulijenga uwezo wa usindikaji ndani ya nchi. Badala ya kuuza nje kakao mbichi, tulianza kuhifadhi zaidi ya mnyororo wa thamani kwa kuugeuza kuwa bidhaa zilizokamilishwa, chokoleti. Hilo lilihitaji utaalam tofauti, kwa hivyo tukaleta mtengenezaji wa chokoleti wa Ubelgiji ili kusaidia kuweka viwango vya uzalishaji na kutoa mafunzo kwa timu za ndani. Wazo sio tu kusindika kokwa za kakao, bali kuzalisha bidhaa ambayo inaweza kushindana kwa ubora katika masoko ya kimataifa. Hii inatengeza thamani zaidi kwa kila kitengo cha kakao na kukaza thamani yake ndani ya eneo. Pia hubadilisha asili ya ajira. Badala ya kufanya kazi tu katika kiwango cha kilimo au usindikaji wa kimsingi, watu wanahusika katika uzalishaji wenye ujuzi ikiwa ni pamoja na wanawake kutoka jamii zilizoathiriwa na migogoro, kama vile wajane wa walinzi waliouawa, ambao wamefunzwa kama watengenezaji wa bidhaa za uza chokoleti. Kwa maana hiyo, kiwanda kinakuwa zaidi ya kituo cha viwanda; ni sehemu ya kujenga upya mfumo wa kiuchumi unaoenea zaidi ya uziduaji hadi kwenye uzalishaji na ufundi.

Ukubwa wa jambo hili ni muhimu. Kwa kiasi kidogo, mfumo una athari ndogo. Lakini unapokua, huanza kuunda upya mnyororo mzima wa thamani. Uzalishaji umeongezeka kwa kasi, na lengo ni kufikia kiwango ambapo sehemu kubwa ya kakao ya eneo hilo inachakatwa kupitia njia salama na za uwazi.
Hivi ndivyo tunamaanisha kwa kuchanganya usalama na uchumi. Unabuni ulinzi kwa upande mmoja kupitia vituo vya uendeshaji mbele na mifumo ya majibu ya haraka na kwa upande mwingine, unaunda uchumi mbadala ambao unavutia zaidi na thabiti zaidi kuliko ule unaodhibitiwa na vikundi vilivyojihami.
Ni njia ya “tuzo na adhabu”, lakini vipengele vyote viwili ni muhimu. Bila usalama, uchumi haufanyi kazi. Bila uchumi, usalama haushiki.
Ni jukumu gani teknolojia na mifumo ya fedha lina nafasi katika kufanya kielelezo hiki kufanya kazi kwa kiwango kikubwa?
Kwetu sisi, teknolojia, si safu dhahania, ndiyo inayoruhusu mfumo kufanya kazi kwa kiwango na kwa uwajibikaji. Mojawapo ya changamoto kubwa katika eneo kama la Kongo mashariki si ukosefu wa habari; ni pengo kati ya habari na vitendo.
Tumejaribu kuziba pengo hilo kwa kujenga mifumo inayotafsiri kile kinachotokea ardhini kuwa jibu lililoundwa. Kwa mfano, wakati mlinzi au kitambuzi kinaripoti tukio, hutoa kile tunachoita “tiketi.” Tiketi hiyo inasalia wazi na kuonekana hadi suala litatuliwe. Inapitia katika msururu wa uwajibikaji, na ikiwa haitashughulikiwa ndani ya muda uliotarajiwa, mtu anayehusika atawajibishwa. Hatimaye, kila kitu kinasonga, iwapo mfumo unashindwa, ninawajibika.
Hiyo inaweza kuonekana kama kitu cha msingi, lakini katika mazingira ya kiwango hiki na mamia ya walinzi wanaofanya kazi katika maeneo makubwa na ya mbali, aina hiyo ya muundo ni muhimu. Inaunda aina ya utawala ambayo inaweza kufuatiliwa na kutekelezeka.
Muunganisho ni sehemu nyingine muhimu. Bila hiyo, hakuna chochote cha hii kinafanya kazi. Tulipoanza kutengeneza ukanda wa kijani, tulisisitiza kuwa na huduma ya mtandao wa kasi katika mandhari yote. Hiyo ilijumuisha kupata ufikiaji wa mifumo inayotegemea satelaiti. Sio tu kuhusu mawasiliano; huwezesha mfumo mzima wa usimamizi kufuatilia doria, kuratibu majibu, kudhibiti data, na kudumisha uangalizi.
Pia tumeunganisha mifumo hii katika jukwaa pana la usimamizi, kimsingi mfumo wa upangaji wa rasilimali za biashara uliorekebishwa kwa muktadha huu. Inaturuhusu kuleta pamoja data ya uendeshaji, mtiririko wa kifedha, vifaa, na mifumo ya uzalishaji katika mfumo mmoja. Kuanzia hapo, tumeanza kutengeneza zana za ufuatiliaji, haswa katika sekta kama vile kakao na mafuta ya mchikichi. Kwa kutumia data ya setilaiti na ramani, tunaweza kubaini kama shamba mahususi lilikuwa na misitu hapo awali. Hilo linazidi kuwa muhimu kwa kufuata kanuni za kimataifa, kama vile sheria za ukataji miti za Ulaya. Inamaanisha kuwa bidhaa zinazosonga kupitia mfumo zinaweza kuthibitishwa kwa njia inayoafiki viwango vya nje.
Kinachoshangaza ni namna uwezo wa ndani unavyokua kwa haraka karibu na vifaa hivi. Tumeunda timu za mafundi vijana wa Kongo ambao wanajifunza kwa kasi ya ajabu. Ujuzi ambao kwa kawaida ungechukua miaka kupata unaendelezwa kwa muda mfupi zaidi. Tumeweka nafasi za kazi ambapo zinachanganya kazi ya kiufundi ya kufanya kazi kwa mikono na kujifunza kila mara, kwa ufanisi kujenga msingi wa teknolojia ya ndani kuanzia mwanzo hadi mwisho.
Maendeleo yanayohusiana yamekuwa ni matumizi ya akili unde yaani akili bandia (AI) kama kifaa cha mafunzo. Mojawapo ya vikwazo vinavyotukabili ni muda gani inachukua kujenga uwezo wa kiufundi, iwe ni mekanika, mafundi umeme, au ufundi mwingine wenye ujuzi ambao ni muhimu kudumisha miundombinu. Kizamani, aina hiyo ya mafunzo ingechukua miaka. Tulichoanza kujaribu ni kutumia akili unde (AI) kutengeneza nyenzo za mafunzo ambazo zinaweza kuharakisha mchakato huo. Kwa mfano, tunaweza kutoa mwongozo wa vitendo kuhusu jinsi ya kuwa mekanika, iliyoundwa kulingana na vifaa na hali maalum hapa, na kuifanya ipatikane na mafundi wa mashinani. Haichukui nafasi ya uzoefu wa vitendo, lakini inafupisha mkondo wa kujifunza kwa kiasi kikubwa. Katika muktadha ambapo tunajaribu kuunda mifumo yote kwa upesi; nishati, usafiri, na viwanda, aina hiyo ya kuongeza kasi ni muhimu sana.
Hii ni muhimu kwa sababu lengo si kuagiza utaalamu kutoka nje kwa muda usiojulikana. Mfumo lazima umilikiwe na kuendeshwa kutoka mashinani. Vinginevyo, haina kiwango, na haidumu.
Fedha, kama sehemu ya hii, imeunganishwa kwa undani katika miundombinu. Mfumo wa mita za kidijitali ni mfano mmoja, lakini kwa upana zaidi, wazo ni kupunguza msuguano ambao kwa kawaida huzuia mtaji kufikia mazingira haya. Mifumo ya zamani ya kifedha haijaundwa kwa uchumi mdogo, uliosambazwa katika mazingira hatarishi.
Kwa kuingiza huduma za kifedha katika mifumo ya uendeshaji iwe kupitia nishati, uzalishaji, au vifaa, unaunda mifumo ambayo ni bora zaidi na inayolingana zaidi na jinsi uchumi unavyofanya kazi. Gharama ya kusimamia miamala inashuka, hatari inakuwa rahisi zaidi kupimika, na ufikiaji unapanuka.
Pia kuna mabadiliko mapana zaidi ya kifikra. Tumeachana na kutegemea ruzuku pekee na kuelekea miundo inayojumuisha mapato, madeni na uwekezaji. Hiyo haifurahishi kila wakati, haswa katika mazingira ya migogoro ambapo malipo ya hatari ni ya juu, lakini ni muhimu. Iwapo mfumo unategemea zaidi ufadhili wa nje, unasalia kuwa tete.
Kinyume chake, kama unaweza kujenga kitu kinachozalisha mapato yake yenyewe iwe kupitia nishati, kilimo, au usindikaji basi kinaweza kujiendeleza na kukua. Jukumu la teknolojia na fedha ni kufanya hilo liwezekane kwa kiwango kikubwa, huku tukidumisha uwazi na uwajibikaji.
Mwishowe, mifumo hii sio tofauti na lengo pana. Hiyo ni sehemu ya juhudi sawa za kujenga uchumi unaofanya kazi, thabiti, na wenye uwezo wa kushindana na miundo inayoendesha migogoro kwa sasa.
Ni maono gani yaliwajia katika wazo la Ukanda wa Kijani, na kwa ni nini ni muhimu sana kwa kile unachojaribu kufikia?
Wazo la ukanda wa kijani lilitokana na kile tulichokuwa tukifanya huko Virunga. Tuliona kwamba ikiwa unaweza kujenga kielelezo cha kiuchumi karibu na eneo lililohifadhiwa ambalo hutoa nafasi za ajira, hutoa nishati, na kuleta utulivu wa jamii, basi uhifadhi unawezekana. Swali lilikuwa kama hiyo inaweza kupunguzwa.
Rais alituomba tuwazie kwenye ngazi ya kitaifa. Hilo lilipelekea sheria iliyopitishwa mapema mwaka 2025 kuanzisha kile tunachokiita ukanda wa Mto Kongo, au Couloir Vert kwa kifaransa ikimaanisha ukanda wa kijani. Sio eneo la jadi lililohifadhiwa. Ni msitu uliohifadhiwa unaojumuisha miji, vimiji, na mandhari ya kilimo. Lengo si kulinda tu asili; bali kujenga uchumi unaowezesha ulinzi.
Katika msingi wake, Ukanda unahusu kuunganisha hali halisi mbili ambazo kwa sasa zipo katika hatari ya kutengwa. Katika Mashariki ya nchi, kuna ardhi yenye rutuba ya ajabu yenye uwezo wa kuzalisha chakula. Huko Kinshasa, ambayo ni mojawapo ya miji mikubwa zaidi barani Afrika, kuna mahitaji makubwa, lakini jiji linategemea sana uagizaji bidhaa kutoka Brazil, Ulaya, na kwingineko.
Kimsingi, mji wa Kinshasa uko kwenye kipima muda. Mji huo uppo katika upungufu mmoja tu wa chakula mbali na mzozo mkubwa. Iwapo minyororo ya ugavi itakatizwa, matokeo yatakuwa ya haraka na makali. Udhaifu huo haueleweki kwa upana, lakini ni msingi wa uharaka wa kile tunachojaribu kufanya.
Ukiunganisha matoleo hayo mawili ya Mashariki na mahitaji ya Kinshasa, unaunda mfumo wa ndani wa uchumi. Mfumo huo unazalisha utulivu kwa sababu ya kutegemeana. Maeneo ambayo hapo awali yalikatwa huanza kutegemeana. Hiyo ni moja ya misingi ya amani.
Lakini pia kuna uharaka mpana wa mazingira. Bonde la Kongo ndio msitu pekee wa kitropiki ulimwenguni ambao bado ni shimo la kaboni. Inafyonza kaboni zaidi kuliko inavyotoa. Wakati huo huo, shinikizo ambazo tayari zimebadilisha maeneo mingine ya kitropiki zinaanza kuibuka hapa kama barabara, miji, miundombinu ya kikanda.
Kugawanyika ni tishio kubwa. Sio tu ufyekaji wa msitu; ni kugawanyika kwa mifumo ikolojia katika vipande vidogo na vidogo. Pindi mchakato huo unapoharakishwa, inakuwa vigumu sana kuupindua.
Tunachokiona kwa sasa ni mbio kati ya mifumo miwili. Kwa upande mmoja, una miundombinu inayoendelezwa kupitia uwekezaji kutoka nje kama barabara, reli, na njia za biashara zilizounganishwa na minyororo ya kimataifa ya usambazaji. Hii ni muhimu kwa maendeleo, lakini pia hufungua msitu kwa utumiaji mbaya wa haraka. Kwa upande mwingine, una uwezekano wa kujenga uchumi ambao una mizizi ndani ya nchi, unaotumia msitu bila kuharibu.
Ukanda ni jaribio la kuunda matokeo hayo. Umeundwa kama mtandao wa vitovu vya kiuchumi vinavyosambazwa katika mazingira yote. Kila kitovu huchanganya vipengele kadhaa: miundombinu ya nishati, usindikaji wa kilimo, vifaa, na usalama. Wazo sio kujaribu kukuza kila kitu mara moja, lakini kujenga nodi au vifundo, sehemu ambazo shughuli za kiuchumi zinaweza kushikilia na kisha kuziunganisha kwa wakati.
Kwenye nishati ndio mahali pa kuanzia. Bila nishati, hakuna kitu kinachofanya kazi. Hatua ya kwanza ni kujenga mifumo ya nishati mbadala ambayo inaweza kuwezesha mabadiliko ya chakula na viwanda vya ndani. Ukishapata hiyo, unaweza kuanza kusindika mazao ya kilimo ndani ya nchi badala ya kuisafirisha malighafi nje ya nchi. Hiyo inajenga thamani ndani ya nchi na kuzalisha ajira.
Safu inayofuata ni vifaa. Kongo inatambulika kwa mito yake, lakini usafiri bado ni mgumu sana. Ikiwa huwezi kuhamisha bidhaa kwa ufanisi, mfumo mzima utaharibika. Kwa hivyo, sehemu ya Ukanda huo inahusu kujenga mifumo ya usafiri inayotegemewa; usafiri wa mto, hifadhi ya baridi, na minyororo ya usambazaji ambayo inaweza kuhamisha chakula kutoka mahali kinapozalishwa hadi kinapohitajika.
Usalama ni sehemu nyingine muhimu. Katika mengi ya maeneo haya, uchumi bado unahusishwa na migogoro. Vikundi vilivyojihami kwa silaha vyajishughulisha sababu wanadhibiti minyororo ya thamani. Ikiwa hutashughulikia usalama, uwekezaji haushiki. Ndiyo maana kila kitovu cha uchumi kinaunganishwa na mfumo wa ulinzi sio tu kijeshi, lakini mifumo ya kijamii ambayo inaruhusu watu kuishi na kufanya kazi kwa usalama.
Yote haya yameundwa ili kujiimarisha yenyewe. Ajira hupunguza kivutio cha kujiunga namaikundi yenye silaha. Utulivu huvutia uwekezaji. Uwekezaji huimarisha uchumi, jambo ambalo hupunguza uharibifu kwenye misitu.
Utulivu huvutia uwekezaji. Uwekezaji huimarisha uchumi, jambo ambalo hupunguza shinikizo la uharibifu wa misitu.
Kiwango ni muhimu. Ukanda huu unachukua eneo kubwa kuliko nchi nyingi na linajumuisha mamilioni ya watu. Malengo yanaakisi kiwango hicho, idadi kubwa ya kazi, ongezeko kubwa la uzalishaji wa chakula, na ulinzi wa maeneo makubwa ya misitu.
Pia ni mradi wa muda mrefu. Bado tuko katika hatua za awali kimsingi hatua ya uthibitisho wa dhana. Lengo sasa ni kuonyesha kuwa kielelezo kinaweza kufanya kazi kwa kiwango. Ikiwa inafanya hivyo, kinaweza kupanuliwa katika mazingira yote.
Wakati huo huo, unapaswa kushindana na vikosi vingine. Kuna miradi mikubwa ya miundombinu ambayo tayari inaendelea katika eneo lote, ikiungwa mkono na uwekezaji wa Uchina na Magharibi. Haya yataunda mustakabali wa Bonde la Kongo. Ikiwa hatutajenga kielelezo mbadala haraka vya kutosha, mifumo hiyo itafafanua matokeo na hatari yake ni kuwa msitu unafuata njia ile ile ambayo tumeona mahali pengine.
Hatimaye, kanuni ni rahisi. Unaunda uchumi unaotegemea afya ya msitu badala ya uharibifu wake.
Iwapo unaweza kuoanisha mambo hayo mawili, basi ulinzi unakuwa chaguo la busara.
Hilo ndilo tunalojaribu kulifanya.
Ni kipi kikomo cha kielelezo hiki, hasa katika hali ya migogoro inayoendelea na ukosefu wa utulivu wa kisiasa?
Kwa muda mrefu, tulihisi ni kama tunaanza kuigeuza kona. Mfumo wa nishati ulikuwa ukipanuka, biashara zilikuwa zikiibuka, nafasi za ajira zilikuwa zikiundwa, na katika baadhi ya maeneo, vurugu zilikuwa zikipungua. Kulikuwa na hisia kwamba kielelezo hicho kilianza kufanya kazi, kwamba kwa kushughulikia vichochezi vya kiuchumi vya migogoro, tunaweza kuanza kuimarisha mfumo.
Kisha, karibu miaka mitatu iliyopita, hali ikawa mbaya tena. Kuibuka tena kwa mzozo, haswa wa kundi la waasi wa M23, kulivuruga sehemu kubwa za kile tulichokuwa tumejenga. Miundombinu iliharibiwa, ufikiaji ulizuiwa, na maeneo yote yakawa na migogoro au kutoweza kufikiwa.
Ilikuwa ni wakati wa kugutusha sana. Ilionyesha wazi kuwa uchumi ni chombo chenye nguvu, hakitoshi peke yake. Unaweza kujenga miundombinu, kubuni nafasi za ajira, na kukuza minyororo mbadala ya thamani, lakini faida hizo zitasalia kuwa hatarini kama muktadha mpana wa kisiasa hauko thabiti.
Kwa maneno ya vitendo, imemaanisha kufanya kazi katika hali ngumu sana. Sehemu za hifadhi hiyo sasa ziko chini ya udhibiti wa makundi yaliojihami kwa silaha. Chini ya sheria za Kongo, tunatakiwa kuendelea kufanya kazi bila kujali ni nani anayedhibiti eneo. Sheria inatufafanua sisi kuwa wasio wapiganaji sawa na shirika la kibinadamu, ambalo huturuhusu kudumisha uwepo hata katika maeneo yanayoshikiliwa na waasi.
Hiyo inajenga usawa wa udhaifu. Tunasalia mahali, tukiendelea kulinda mbuga na kuunga mkono mifumo ya kijamii, lakini tunapaswa kuangazia athari za kisiasa kwa uangalifu sana. Itakuwa si sahihi kusema “tunafanya kazi na” makundi yenye silaha, lakini tunafanya kazi katika maeneo ambayo wako. Wakati huo huo, tunapaswa kuhakikisha kuwa kazi yetu haitumiki, kwamba haitumiwi na chama chochote kuhalalisha msimamo wao.
Licha ya vikwazo hivi, baadhi ya vipengele vya mfumo vina mshiko. Operesheni za walinzi zimeendelea katika maeneo mengi, mara nyingi kwa msaada kutoka kwa skauti za jamii ambao hubakia mahali hata wakati hali ni ngumu. Katika baadhi ya matukio, idadi ya wanyamapori hasa sokwe wa milimani, wameendelea kukua kwa kasi ya asili.

Lakini mazingira mapana yanasalia kutokuwa thabiti. Utalii, ambao hapo awali ulikuwa chanzo kikubwa cha mapato, sasa umetoweka kabisa. Hilo limeweka matatizo ya ziada kwenye mfumo, na kuongeza utegemezi wa ufadhili kutoka nje na kufanya kuwa vigumu kuendeleza shughuli.
Kimsingi, mzozo wenyewe sio usumbufu wa muda mfupi. Ni sehemu ya mchakato mrefu zaidi, miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu inayofungamana na siasa za kikanda, ushindani wa rasilimali, na maslahi ya nje. Kuna mienendo mingi inayochangia hali fulani, ikijumuisha mivutano inayohusishwa na harakati za kuvuka mpaka, kanda za kiuchumi zinazoshindana, na umuhimu wa kimkakati wa maliasili.
Katika muktadha huo, suluhisho lolote linapaswa kufanya kazi katika viwango vingi. Muundo wa kiuchumi ambao tumeutengeza unashughulikia safu moja, vivutio vinavyochochea ushiriki wa wenyeji katika migogoro. Lakini haisuluhishi nguvu kubwa za kisiasa zinazoiendeleza.
Hicho ndio kikomo.
Wakati huo huo, haimaanishi kuwa kielelezo hakifanyi kazi. Kinachofanya ni kutengeza mifuko ya utulivu ndani ya mazingira mapana ya kutokuwa na utulivu. Kinatoa njia mbadala ambapo haikuwepo awali. Inaonyesha kuwa matokeo tofauti yanawezekana chini ya hali fulani.
Changamoto ni jinsi ya kuongeza kiwango hicho kwa njia ambayo inaweza kuhimili nguvu kubwa zinazocheza.
Hatimaye, somo ni kwamba uhifadhi katika muktadha huu hauwezi kutenganishwa na siasa. Unaweza kuunda mifumo ya kisasa zaidi kama nishati, fedha, usalama lakini mazingira ya kisiasa yakibadilika, mifumo hiyo itafichuliwa.
Kwa hiyo, kazi zinakuwa mara mbili: kuendelea kujenga msingi wa kiuchumi, wakati pia kutambua kwamba mafanikio yake yanategemea mambo ambayo yanaenea zaidi yake.
Huo ndio ukweli tunaoendesha.
Kutokana na uzoefu wako, unadhani ni kwa nini uhifadhi kama uwanja unakuwa mbaya na ni nini kinachohitajika kubadilishwa?
Mojawapo ya mambo yaliyonivutia mapema ni mara ngapi uhifadhi unashughulikiwa kwa njia ambayo haijaunganishwa na hali halisi.
Pia kuna suala pana zaidi kuhusu namna uhifadhi unavyojiwasilisha.
Matokeo yake ni kwamba uwanja unaweza kupoteza mwelekeo wa kile unachojaribu kufikia.

Sehemu ya shida ni kwamba uhifadhi mara nyingi umechukuliwa kama kitu tofauti na mifumo inayoizunguka.
Kinachotakiwa badala yake ni mbinu iliyojumuishwa zaidi.
Kutoka hapo, unajenga kitu ambacho kinajibu kwa hali hizo.
Pia inahitaji mabadiliko katika jinsi mafanikio yanavyopimwa.
Ukirudi nyuma kutoka kwa kila kitu ambacho umejenga katika mbuga ya Virunga, ni wazo gani la msingi au kanuni inayosisitiza mbinu yako?
Ukirudi nyuma kutoka kwa haya yote, mifumo ya nishati, miundo ya usalama, mipango ya kiuchumi, sababu za msingi ni rahisi sana.
Tunachopambana nacho sehemu ya mashariki mwa Kongo sio ukosefu wa rasilimali au hata ukosefu wa uwezo. Ni mfumo ambapo mtindo mkuu wa uchumi umejengwa juu ya uchimbaji na migogoro. Maliasili huchukuliwa, mara nyingi kinyume cha sheria, na mchakato huo huzalisha mapato kwa makundi yenye silaha. Mapato hayo yanaendeleza mzozo huo, ambao unaruhusu uchimbaji kuendelea. Ni mzunguko wa kujiimarisha.
Ikiwa unataka kubadilisha hayo, unastahili kuanzisha mfumo wa ushindani. Ni sharti ujenge uchumi ambao una nguvu ya kutosha kuondoa ule unaoendesha migogoro. Hilo ndilo wazo la msingi.
Hiyo inamaanisha kufanya kazi katika viwango kadhaa mara moja. Lazima upeane usalama, kwa sababu bila hiyo hakuna kitu kingine kinachoshikilia. Lazima ujenge miundombinu, kwa sababu bila hiyo hakuna uchumi unaofanya kazi. Lazima utengeneze ajira, kwa sababu bila wao watu wataendelea kugeukia makundi yenye silaha. Na lazima ufanye yote hayo kwa njia ambayo inalinda mifumo ya asili unayojaribu kuhifadhi.
Sio mchakato unaofwata mtiririko wa moja kwa moja. Hutatua kipande kimoja na kisha uende kwa kingine. Kila kitu kinapaswa kuendeleza pamoja, na kila sehemu inategemea wengine.
Pia kuna swali la kiwango. Uingiliaji kati mdogo unaweza kuonyesha kile kinachowezekana, lakini haubadilishi mfumo wa jumla. Ili kufanya hivyo, unapaswa kufikia kiwango ambacho uchumi mbadala ni mkubwa wa kutosha kushindana. Hivyo ndivyo tunajaribu kufanya na Ukanda, kuiondokea mifano iliyotengwa hadi kitu ambacho kinaweza kufanya kazi katika mazingira yote.
Wakati huo huo, kuna mipaka kwa kila mbinu inayoweza kufikia peke yake. Muktadha mpana wa kisiasa bado unatengeza mazingira tunayofanyia kazi. Shinikizo za nje, mienendo ya kikanda, na mizozo ya muda mrefu yote huathiri matokeo.
Lakini hiyo haifanyi juhudi kuwa zisizo na maana. Inachofanya ni kufafanua jukumu lake.

Tunachoweza kufanya ni kuunda hali ambapo mwelekeo tofauti unawezekana. Tunaweza kuonyesha kwamba inawezekana kujenga uchumi ambao hautegemei uharibifu, unaotoa utulivu badala ya kuimarisha migogoro, na unaoruhusu watu na mifumo ikolojia kuendelea.
Ikiwa hilo hatimaye litakuwepo inategemea nguvu zaidi ya mpango wowote. Lakini bila kujenga mbadala huo, hakuna njia ya mbele hata kidogo.
Kwa hivyo, kwa maana hiyo, kazi ni ya vitendo na ya muda. Inahusu kutatua matatizo ya mara moja ya nishati, usalama, riziki huku pia ikijaribu kuhamisha mwelekeo wa mfumo kwa wakati.
Ikiwa mabadiliko hayo yanatokea, basi uhifadhi unakuwa kitu cha kudumu zaidi. Sio tena kitu kinachopaswa kulazimishwa au kutetewa kila mara. Inakuwa iliyoingia kwenye namna uchumi unavyofanya kazi.
Na hilo ndilo lengo hasa.
Kufikia mahali ambapo kulinda msitu sio kikwazo, lakini ni matokeo ya jinsi mfumo unavyofanya kazi.
Habari hii ilichapishwa kwa mara ya kwanza hapa kwa lugha ya Kiingereza mnamo tarehe 13/04/2026