<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=baharini&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/baharini/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 28 Aug 2026 16:47:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Tengefu za baharini zinafunika chini ya asilimia 10 ya maeneo ya papa na papa-kolee, utafiti umebaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/tengefu-za-baharini-zinafunika-chini-ya-asilimia-10-ya-maeneo-ya-papa-na-papa-kolee-utafiti-umebaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/tengefu-za-baharini-zinafunika-chini-ya-asilimia-10-ya-maeneo-ya-papa-na-papa-kolee-utafiti-umebaini/#respond</comments>
					<pubDate>17 Agosti 2026 18:17:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Madeline Shaw]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/17180117/Screenshot-2026-08-17-205839-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2501</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Ikolojia, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Papa, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, na  Spishi Zilizo Hatarini Sana]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwaka 2022, nchi 196 ziliafiki lengo kuu la uhifadhi linaloitwa &#8220;30×30&#8221;: kutenga asilimia 30 ya maeneo ya pwani na bahari ya sayari hii kwa ajili ya uhifadhi ifikapo mwaka 2030, chini ya Mfumo wa Kimataifa wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal. Sasa, huku mwaka 2030 ukiwa umebakisha takriban miaka minne, asilimia kumi tu ya bahari ndiyo imefunikwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/tengefu-za-baharini-zinafunika-chini-ya-asilimia-10-ya-maeneo-ya-papa-na-papa-kolee-utafiti-umebaini/" data-wpel-link="internal">Tengefu za baharini zinafunika chini ya asilimia 10 ya maeneo ya papa na papa-kolee, utafiti umebaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwaka 2022, nchi 196 ziliafiki lengo kuu la uhifadhi linaloitwa &#8220;30×30&#8221;: kutenga asilimia 30 ya maeneo ya pwani na bahari ya sayari hii kwa ajili ya uhifadhi ifikapo mwaka 2030, chini ya Mfumo wa Kimataifa wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal. Sasa, huku mwaka 2030 ukiwa umebakisha takriban miaka minne, asilimia kumi tu ya bahari ndiyo imefunikwa na maeneo yaliyolindwa — hali inayoacha nchi nyingi mbali sana na lengo hilo la bioanuwai. Na hata ndani ya tengefu zilizopo, utafiti mpya unafichua mapungufu makubwa katika ulinzi wa moja ya makundi yaliyo hatarini zaidi baharini: papa na papa-kolee. Utafiti uliochapishwa katika jarida la Conservation Letters mwezi Julai unabainisha kwamba kwa spishi nyingi za papa na papa-kolee, chini ya asilimia kumi ya maeneo yao ya makazi yanaangukia ndani ya tengefu za baharini, huku spishi zilizo hatarini na karibu kutoweka zikiathirika zaidi. Uchambuzi huo pia unafichua mapungufu makubwa katika uripoti wa kiwango cha vizuizi vya uvuvi na uvunaji ndani ya tengefu hizo — kinachojulikana kama take&#8211;status — jambo muhimu katika kutathmini ufanisi wa ulinzi kwa wanyama hawa. “Kuongeza tu ukubwa wa bahari iliyolindwa hakumaanishi kwamba tunazilinda kwa kweli spishi hizo zilizo hatarini,&#8221; Amanda Arnold, mtafiti wa bayoanuwai ya baharini katika Chuo Kikuu cha Simon Fraser nchini Kanada na mwandishi mkuu wa utafiti huo, alimwambia Mongabay. &#8220;Haifuniki upana wote wa bioanuwai.&#8221; Papa-mchanga (Carcharias taurus), spishi iliyo Karibu Kutoweka kulingana na IUCN. Picha na mattdowse kupitia iNaturalist (CC BY-NC 4.0). Ili tengefu za baharini zitoe manufaa ya uhifadhi yanayopimika, zinapaswa kufunika angalau asilimia kumi ya makazi ya spishi fulani — na ufunikaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/tengefu-za-baharini-zinafunika-chini-ya-asilimia-10-ya-maeneo-ya-papa-na-papa-kolee-utafiti-umebaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/tengefu-za-baharini-zinafunika-chini-ya-asilimia-10-ya-maeneo-ya-papa-na-papa-kolee-utafiti-umebaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, rekodi za upanzi wa mikoko ni suluhu ya urejeshaji wa misitu iliyoangamia?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/15/je-rekodi-za-upanzi-wa-mikoko-ni-suluhu-ya-urejeshaji-wa-misitu-iliyoangamia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/15/je-rekodi-za-upanzi-wa-mikoko-ni-suluhu-ya-urejeshaji-wa-misitu-iliyoangamia/#respond</comments>
					<pubDate>15 Agosti 2026 00:00:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/14205646/EMMANUEL-KARISA-AKIWA-NA-JAMII-WAKIPANDA-MIKOKO-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2477</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mashirika Yanayokiuka Kanuni za Mazingira, Mazingira, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Uanaharakati, Uchumi wa Mazingira, Urejeshaji, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya imetambuliwa kimataifa baada ya kupanda miche 4,124 ya mikoko kwa muda wa chini ya sekunde 30, kwa lengo la kuhamasisha juhudi za kurejesha misitu ya mikoko iliyoharibiwa na kuchangia lengo la kitaifa la kuongeza idadi ya miti. Hatua hii iliipa nchi hiyo rekodi ya Guinness World Records. Rekodi hii iliafikiwa katika eneo la Jomvu Kuu, kaunti ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/15/je-rekodi-za-upanzi-wa-mikoko-ni-suluhu-ya-urejeshaji-wa-misitu-iliyoangamia/" data-wpel-link="internal">Je, rekodi za upanzi wa mikoko ni suluhu ya urejeshaji wa misitu iliyoangamia?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya imetambuliwa kimataifa baada ya kupanda miche 4,124 ya mikoko kwa muda wa chini ya sekunde 30, kwa lengo la kuhamasisha juhudi za kurejesha misitu ya mikoko iliyoharibiwa na kuchangia lengo la kitaifa la kuongeza idadi ya miti. Hatua hii iliipa nchi hiyo rekodi ya Guinness World Records. Rekodi hii iliafikiwa katika eneo la Jomvu Kuu, kaunti ya Mombasa tarehe Julai 26, 2026, ambayo ni Siku ya Mikoko Duniani. Watu 4,124 kati ya 4,196 waliojitokeza walithibitishwa na Guinness World Records kutimiza masharti ya kupanda miti hiyo kwa pamoja. Sehemu ya mikoko iliyopandwa na kutunzwa na Bidii Creek Conservancy CBO. Picha kwa hisani ya BCC. Shirika la Mpesa Foundation lilifadhili shughuli hiyo kupitia mradi wake wa mazingira, likishirikiana na jamii, huku Kenya Scouts Association ikihamasisha na kuleta maelfu ya vijana na skauti wa eneo la pwani. Bidii Creek Conservancy CBO ilishiriki katika utafutaji wa miche ya mikoko kutoka kwa jamii zinazojishughulisha na uhifadhi wa mikoko, huku serikali, kupitia Shirika la Huduma kwa Misitu (KFS), ikitoa mwongozo wa kitaalamu wa uhifadhi na upandaji wa mikoko. Rekodi za upanzi wa mikoko 2026  Mwaka 2026 umeshuhudia kuongezeka kwa kampeni za upanzi wa mikoko, huku wadau mbalimbali wakivunja rekodi na kuhamasisha juhudi za urejeshaji wa misitu hiyo. Mapema mwaka huu, mwanaharakati wa mazingira Antoine Moses alipanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 katika mkondo wa bahari wa Tudor, Mombasa kabla ya kutwaa taji la mtu aliyepanda miti mingi zaidi ya mikoko ndani ya saa 24. Wiki chache baadaye, tarehe Mei 23, Kikosi cha Ulinzi cha Kenya (KDF), kwa kushirikiana na jamii na wanafunzi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/15/je-rekodi-za-upanzi-wa-mikoko-ni-suluhu-ya-urejeshaji-wa-misitu-iliyoangamia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/15/je-rekodi-za-upanzi-wa-mikoko-ni-suluhu-ya-urejeshaji-wa-misitu-iliyoangamia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>14 Agosti 2026 00:00:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/13193448/Screenshot-2026-08-13-223025-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2467</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Madagaska, Malawi, Mauritius, na  Msumbiji]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Ikolojia, Mafuriko, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Uchimbaji Kina wa Madini ya Baharini, Uchimbaji Madini, na  Uchimbaji Madini Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari wakati wa mkutano wa mwaka wa Mamlaka ya Kimataifa ya Sakafu ya Bahari (ISA) uliofanyika Kingston, Jamaica, mwezi Julai. Zilijiunga na Malawi, Kenya na Madagaska, ambazo zilikuwa zimetangaza msimamo huo mapema. Serikali ya Mauritius ilisema wazi katika taarifa yake wakati wa mkutano huo kwamba “maendeleo endelevu ya Mauritius yanategemea kwa kiasi kikubwa bahari yenye afya na ustahimilivu”. Maafisa wake walisisitiza kwamba maamuzi kuhusu uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari lazima yafanywe kwa kuzingatia “ushahidi bora zaidi wa kisayansi unaopo na mbinu ya tahadhari, kama inavyoainishwa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari.” Malawi ilikuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari, mnamo Mei 2026. Kenya na Madagaska zilifuata msimamo huo mwezi Juni. “Msingi wa nchi hizi zote, huku zikizingatia mazingira yao ya kipekee, ni ukosefu wa ushahidi wa kutosha wa kisayansi na mapungufu ya utawala yanayoendelea,” David Willima kutoka Deep Sea Conservation Coalition (DSCC) — muungano wa mashirika zaidi ya 140 ya kiraia na asasi mbalimbali — aliiambia Mongabay kupitia barua pepe. Nchi hizo sita za Afrika ziko miongoni mwa nchi 46 duniani zinazounga mkono zuio au kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka baharini hadi sokoni: Wanawake wanaoendesha biashara ya dagaa Vanga</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/#respond</comments>
					<pubDate>12 Agosti 2026 22:37:07 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asha Bekidusa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/12222728/Boti-zikiwa-katika-ufuo-wa-Vanga-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2439</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, na  Spishi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za dunia walipokongamana mjini Mombasa wakati wa Our Ocean Conference, suala la nafasi ya wanawake kama uti wa mgongo wa sekta ya bahari na uvuvi lilijitokeza pakubwa. Hii ilibainika huku utafiti kutoka WorldFish ukionyesha kuwa barani Afrika, asilimia 90 ya wanawake katika sekta ya uvuvi na ufugaji samaki wameajiriwa katika shughuli za [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/" data-wpel-link="internal">Kutoka baharini hadi sokoni: Wanawake wanaoendesha biashara ya dagaa Vanga</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za dunia walipokongamana mjini Mombasa wakati wa Our Ocean Conference, suala la nafasi ya wanawake kama uti wa mgongo wa sekta ya bahari na uvuvi lilijitokeza pakubwa. Hii ilibainika huku utafiti kutoka WorldFish ukionyesha kuwa barani Afrika, asilimia 90 ya wanawake katika sekta ya uvuvi na ufugaji samaki wameajiriwa katika shughuli za uvunaji na uhifadhi wa samaki baada ya kuvuliwa. Mmoja wa wasaidizi wa Sauda Hassan akidondoa dagaa katika kijiji cha Jimbo, Kwale. Pamoja naye ni mfanyabiashara aliyekuja kuchukua mzigo wake. Picha na Asha Bekidusa, Mongabay. Kwa baadhi ya wanawake katika kijiji cha Vanga, hili ni jambo la kawaida. Wengi wao wanajihusisha na biashara ya dagaa, ambapo kila asubuhi hukusanyika katika ufuo wa Vanga wakisubiri boti kutoka baharini. Wanawake hao huchukua dagaa hao kuwachemsha, kuwakausha na kuwauza katika sehemu mbalimbali nchini Kenya na nje ya nchi. Miongoni mwa dagaa hao ni katashingo (Sardinella neglecta), kimalawari (Stolephorus indicus) na simsimu (ecapterus macrosoma). Kama wanawake wengine Vanga, Mwanakombo Shee alianza biashara yake takriban miaka nane iliyopita. Mtaji wake ulikuwa KSh10,000 ($77.36) ambao alipata kupitia chama cha kuweka na kukopa alichokuwa mwanachama pamoja na wenzake. “Nilianza biashara hii nilipoona wenzangu kule Jimbo wakifanya biashara,” anasema Mwanakombo. Sauda Hassan, mfanyabiashara wa dagaa kwa mwaka 10 sasa, na ambaye ni mwenyeji wa Jimbo, hakumbuki kiasi halisi cha mtaji wake. Hata hivyo, ni kupitia chama na akiba yake kidogo kidogo ambapo aliweza kuanzisha biashara yake. Biashara hii imemuwezesha kulipa karo ya shule na madrasa kwa watoto wake. “Sikumbuki ni pesa ngapi lakini tulifanya mradi wa mikoko nikapata pesa, nikaongeza na zangu nyengine kidogo kidogo,” anakumbuka&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 17:58:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mazera Ndurya]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28172645/Screenshot-2026-07-28-202121-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2245</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Jinsia na Uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Ongezeko la Joto Baharini, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti wanazotumia baharini na hata katika kutafuta soko. Marinda Masudi, mwenye umri wa miaka 40, ni miongoni mwa wakulima waliojitosa katika ukulima wa mwani kama njia moja ya kukidhi mahitaji ya familia yake. Ilimchukua muda kuamua kujiingiza katika kilimo hicho, lakini biashara yake ya mahamri ilipoanza kudorora, hakuwa na la ziada. Wanawake kutoka Mwazaro, Kaunti ya Kwale, wakionyesha baadhi ya bidhaa, zikiwemo krimu na sabuni walizotengeneza kutoka kwa mwani. Picha na Mazera Ndurya, Mongabay. “Baada ya kujisajili na Kitengo cha Kusimamia Fukwe (BMU) cha Kibuyuni, nilionyeshwa sehemu ya kuanza kulima mwani, na baada ya takriban miezi miwili nilianza kuvuna mwani, kuukausha na kuuuza. Mapato niliyopata nilimsaidia mume wangu kuwasomesha watoto. Mara ya kwanza nilipovuna na kuuza mwani kutoka kwa bloki mbili, nilipata kima cha KSh30,000 ($230),” alisema Marinda. Kama ilivyokuwa na wakulima wengine, alipoanza ukulima, walikuwa wakitumia mbinu ile ambayo imetumika tangu jadi, ambayo hufanyika katika maeneo karibu na ufuo wa bahari. “Mkulima alihitajika kuingia msituni na kukata vigingi vingi vya kufungia kamba na kuweka mbegu. Kwa shamba moja la vipande sita, mtu alihitaji vigingi 300 kufanikisha ukulima wa mwani,” Marinda alieleza. Mbinu ya jadi ilijulikana kama sikio moja au mfungo mmoja, yaani kufunga mbegu moja moja kwenye kamba. Kwa mujibu wa kitabu “Sea Level Rise and Ocean Health in the&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 08:18:04 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16074828/Screenshot-2026-07-16-003002-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2110</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uzuri wa Kiikolojia, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara walipoanza kuwasili ili kununua samaki, Mwazigona alikaa juu ya boti iliyovunjika na kupinduliwa akitazama upeo wa bahari. Safari yake ya asubuhi ilikuwa imemletea kilo 2 pekee za samaki. Alikuwa na hofu kuhusu kupungua kwa kiasi kikubwa kwa mavuno yake ya samaki katika miaka ya hivi karibuni. &#8220;Idadi ya wavuvi imeongezeka; tumekuwa wengi mno,&#8221; alisema. Hiyo ndiyo sababu kuu iliyomfanya aondoke kijijini kwake Shariani, kilichoko umbali wa kilomita 40 kuelekea kaskazini, ili kufanyia shughuli zake za uvuvi Mtwapa; eneo aliloona kuwa na wavuvi wachache na uwezekano mzuri zaidi wa kufikia masoko. Nchini Kenya, vitengo vya usimamizi wa fukwe (BMU), kama vile Mtwapa BMU Mtwapa BMU ambayo Mwazigona ni mali yake, vina mamlaka ya kisheria ya kusaidia ukusanyaji wa takwimu za uvuvi kwa ajili ya kuwasilishwa kwa serikali: hasa aina ya samaki ambao wanachama wake huvua na uzito. Takwimu hizi zinalenga kufahamisha uamuzi wa serikali kuhusu uvuvi mdogo ili iweze kusaidia kubadilisha ushindani wa kupungua kwa samaki ambao Mwazigona na wenzake wanashuhudia. Pia zinalenga kuwasaidia wavuvi wenyewe kufanya maamuzi kuhusu wapi na wakati wa kuvua. Hata hivyo, takwimu za uvuvi mdogo za BMU hazijakuwa sahihi na haipatikani kwa wadau. Ili kushughulikia tatizo hili na kuboresha uendelevu wa uvuvi mdogo wa Kenya,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 18:14:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14175046/Omar-Shafi-akishona-nyavu-yake-yakuvulia-samaki-katika-eneo-la-Mtangawanda-kaunti-ya-LamuKenya.-Picha-na-Ruth-Keah.-2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2062</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sayansi, Sayansi ya Hali ya Tabianchi, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Utafiti, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Kelele baharini: Vita vya jamii kulinda viumbe wa baharini vyapata msukumo wa kimataifa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika eneo la jeti, Mtangawanda, Kaunti ya Lamu, kwenye ufuo wa Bahari ya Hindi, mwendo wa saa sita mchana, Omar Shafi ameketi kwenye kivuli cha banda la wavuvi, akikarabati kwa makini nyavu yake ya kuvulia samaki. Ni shughuli ambayo anaifanya kila siku baada ya kutoka baharini kuvua samaki. Anapomaliza, yeye huiweka sehemu salama kwa ajili ya uvuvi kesho yake. “Tangu nianze uvuvi miaka 40 sasa, nimekuwa nikitumia nyavu hizi za uzi kuvua samaki kwa sababu haziharibu mazingira ya bahari,” anasema Shafi. Omar Shafi akishona nyavu yake yakuvulia samaki katika eneo la Mtangawanda kaunti ya Lamu, Kenya. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kulingana naye, ujio wa zana mbalimbali za kuvulia samaki umeharibu mazingira ya bahari kiasi cha kwamba samaki na viumbe wengine baharini wamepungua sana. “Kuna zana nyingi ambazo wavuvi wanatumia, ambazo zinaharibu utulivu wa bahari. Hivyo husababisha baadhi ya viumbe baharini kupungua,” anasema. Vifaa vinavyosababisha kelele baharini ni kama meli kubwa za mizigo na abiria, boti za mwendo kasi, zana za kuvulia samaki kama trola, mitambo ya utafiti na uchimbaji na mitambo ya ujenzi wa miundombinu ya baharini. Vifaa hivi vimetajwa kusababisha kelele ambazo huathiri uwezo wa viumbe hao kuwasiliana, kusafiri na kusaka chakula. Kama anavyoeleza Shafi, nguva ni miongoni mwa wanyama baharini ambao alikuwa akikutana nao mara kwa mara alipoanza uvuvi hasa katika maeneo ya Manda na Dodori, kaunti ya Lamu. Lakini sasa imekuwa vigumu sana kwake kuwaona. Nguva bado yuko “Kwa maoni yangu, mnyama huyu nguva bado yuko, lakini kwa sababu bahari haina utulivu kutokana na kelele za vyombo vya uvuvi, nguva hukimbia, siwaoni tena,” anasema Omar. Taswira hiyo haielezwi na Shafi peke yake, bali pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/kelele-baharini-vita-vya-jamii-kulinda-viumbe-wa-baharini-vyapata-msukumo-wa-kimataifa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 16:04:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13150952/Screenshot-2026-07-13-180713-768x466.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2039</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chembechembe ndogo za plastiki, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Plastiki, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, na  Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki huishia baharini kila mwaka na zinachangia 80% ya uchafu wote wa baharini unaopatikana katika uso wa bahari na mashapo ya bahari kuu. Kenya inakabiliwa na changamoto kubwa za uchafuzi wa plastiki, haswa katika vituo vya mijini na kando ya pwani yake. Plastiki huchangia takriban 20% ya tani 22,000 za taka zinazozalishwa kila siku nchini Kenya, kulingana na makadirio. Ni 27% tu ya taka za plastiki zinakusanywa, ambapo 8% huchakatwa tena na 19% zilizobaki hutupwa katika majaa ya taka au madampo holela. Taka za plastiki ambazo hazijakusanywa na kusimamiwa vyema mara nyingi huishia kwenye mito na baharini. Huvuruga mifumo ikolojia, huhatarisha wanyamapori, na huathiri utalii na uvuvi. Mwaka wa 2017, Kenya ilianzisha marufuku ya matumizi, utengenezaji na uingizaji wa mifuko ya plastiki ya matumizi ya mara moja. Mnamo 2020, marufuku hiyo iliongezwa hadi plastiki zinazotumika mara moja katika maeneo yaliyohifadhiwa. Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki (NPAP Kenya) utasaidia kuharakisha mpito wa nchi hiyo kuelekea uchumi wa plastiki wa mviringo, kulingana na Clemence Schmid, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (Global Plastic Action Partnership – GPAP) katika Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum – WEF). Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/#respond</comments>
					<pubDate>29 Juni 2026 14:08:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/29134931/Screenshot-2026-06-29-164657-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1948</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Eneo Lililolindwa Baharini, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jinsia na Uhifadhi, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Suluhisho za Asili, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, Viwango vya Bahari, na  Wanawake katika Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi ya wavuvi walikuwa tayari wamerudi mikono mitupu. Wengine walikuwa hawajarudi kabisa. Kwa Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo kipya cha Usimamizi wa Pwani wa Mida (BMU), kusubiri kwa muda mrefu kumekuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Kitengo cha Usimamizi wa Pwani (BMU) ni mfumo wa usimamizi shirikishi wa uvuvi nchini Kenya, ukiwaleta pamoja wadau katika sekta hiyo wakiwemo wavuvi, wauza samaki na wafanyabiashara. Alice Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo cha Usimamizi wa Pwani ya Mida (BMU) kilichoanzishwa hivi karibuni huko Watamu, Kenya. Picha na David Akana/Mongabay. &#8220;Kuna wakati ambapo samaki walikuwa wengi hapa,&#8221; anasema, akionyesha mkondo wa bahari uliommzunguka. &#8220;Sasa [wavuvi] wanarudi na kilo mbili au tatu tu.&#8221; Kwa Kazungu, kupungua kwa samaki kumekuwa suala la kuishi. Akiwa ameolewa na mwenye watoto, anategemea karibu kabisa kuuza samaki ili kupata mapato. Wakati hakuna samaki, mara kwa mara anauza mnazi, aina ya mvinyo wa mitende kutoka kwa minazi. Lakini hiyo haitoshi kuchukua nafasi ya riziki iliyojengwa karibu na bahari. &#8220;Ninarejea nyumbani, watoto hutaka chakula,&#8221; anasema. &#8220;Hilo ndilo linalonitia wasiwasi.&#8221; Hadithi yake inaakisi hali ilivyo katika Mkondo wa Mida, mtandao mkubwa wa mikoko, matope na mifereji ya maji ambayo ni sehemu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Sehemu sita za hifadhi baharini zatambuliwa kama Mbuga za Buluu, nne kati yake zikiwa Afrika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>26 Juni 2026 14:25:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika Vyawahare]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/26135310/Screenshot-2026-06-26-165251.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1937</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Bahari ya Pasifiki, Kenya, na  Senegal]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Eneo Lililolindwa Baharini, Kasa wa baharini, Maeneo yaliyolindwa, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, Uhifadhi wa Kaboni, Uhifadhi wa Misitu, Uvuvi, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MOMBASA, Kenya — Katika kongamano la “Our Ocean” mjini Mombasa, Kenya, ujumbe ulisisitizwa katika vikao vyote: Maeneo yaliyohifadhiwa ya baharini (MPAs) ni muhimu katika kulinda bahari. Tuzo za Blue Park, zilizoanzishwa na Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari yenye makao yake makuu nchini Marekani, zinaangazia maeneo yaliyohifadhiwa yanayokidhi viwango vinavyohitajika. Mwaka huu, sita zilitambuliwa&#60;: Eneo Lililolindwa la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Sehemu sita za hifadhi baharini zatambuliwa kama Mbuga za Buluu, nne kati yake zikiwa Afrika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MOMBASA, Kenya — Katika kongamano la “Our Ocean” mjini Mombasa, Kenya, ujumbe ulisisitizwa katika vikao vyote: Maeneo yaliyohifadhiwa ya baharini (MPAs) ni muhimu katika kulinda bahari. Tuzo za Blue Park, zilizoanzishwa na Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari yenye makao yake makuu nchini Marekani, zinaangazia maeneo yaliyohifadhiwa yanayokidhi viwango vinavyohitajika. Mwaka huu, sita zilitambuliwa&lt;: Eneo Lililolindwa la Bahari la Banc-des-Américains nchini Kanada; Eneo Lililolindwa la Rapa Nui nchini Chile; eneo la turathi ya Jamii asili ya Kawawana nchini Senegali; na Hifadhi ya Kitaifa ya Nosy Hara, Mbuga ya Kitaifa ya Sahamalaza – Îles Radama, na Hifadhi ya Kitaifa ya Nosy Tanihely (pia huandikwa Tanikely) ya Madagaska. Kongamano hilo lililofanyika mjini Mombasa kuanzia Juni 16-18 lilishuhudia zaidi ya wajumbe 6,000 kutoka serikali mbalimbali, mashirika yasiyo ya faida, sekta ya kibinafsi na taasisi nyingine wakikusanyika kuzungumzia uhifadhi wa bahari. Wanachama wa ICCA wa Kawawana nchini Senegal. Picha kwa hisani ya Chama cha Wavuvi cha Jamii ya Vijijini ya Mangagoulack. Chini ya Mfumo wa Kimataifa wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal uliopitishwa na washiriki wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Anuwai wa Kibiolojia mwaka wa 2022, mataifa yalikubaliana kulinda 30% ya ardhi, maji safi na maeneo ya baharini duniani ifikapo 2030, katika kile kinachofahamika kuwa lengo la 30 kwa 30. &#8220;Kundi hili la hifadhi za buluu ni ukumbusho wa nguvu wa kile ambacho lengo la 30 kwa 30 linahitaji,&#8221; Lance Morgan, rais wa Taasisi ya Uhifadhi wa Bahari, alisema katika tangazo la tuzo huko Mombasa mnamo Juni 16. &#8220;Maeneo haya sita yaliyohifadhiwa baharini, yanayolinda mifumo mbalimbali ya ikolojia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/26/sehemu-sita-za-hifadhi-baharini-zatambuliwa-kama-mbuga-za-buluu-nne-kati-yake-zikiwa-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Azimio la Mombasa: Nchi 15 zajitolea kushiriki taarifa za uvuvi ili kukabiliana na uvuvi haramu </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/#respond</comments>
					<pubDate>21 Juni 2026 19:47:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/23195215/Screenshot-2026-06-23-225148-768x510.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1925</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Eneo Lililolindwa Baharini, Kasa wa baharini, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Msukosuko wa chakula, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sehemu za Bioanuwai, Ufugaji Samaki, Uhifadhi wa Baharini, upatikanaji wa chakula, Uvuvi, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchi 15 kutoka mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya zilipitisha Azimio la Mombasa  Azimio la Mombasa mnamo Juni 17, mwaka 2026. Kwa pamoja, mataifa hayo yalijitolea kuendeleza uwazi katika sekta ya uvuvi duniani na kuimarisha jitihada za kukabiliana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa (IUU). Tamko hilo lilipitishwa wakati wa mkutano wa 11 wa Kongamano la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/" data-wpel-link="internal">Azimio la Mombasa: Nchi 15 zajitolea kushiriki taarifa za uvuvi ili kukabiliana na uvuvi haramu </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchi 15 kutoka mabara ya Afrika, Asia, Amerika Kusini na Ulaya zilipitisha Azimio la Mombasa  Azimio la Mombasa mnamo Juni 17, mwaka 2026. Kwa pamoja, mataifa hayo yalijitolea kuendeleza uwazi katika sekta ya uvuvi duniani na kuimarisha jitihada za kukabiliana na uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa (IUU). Tamko hilo lilipitishwa wakati wa mkutano wa 11 wa Kongamano la Kimataifa la Bahari Yetu, lililofanyika mjini Mombasa, Kenya. Bara la Afrika ilikuwa na mataifa mengi zaidi yaliyosaini yakiwemo: Cameroon, Gambia, Ghana, Guinea, Liberia, Jamhuri ya Kongo na Somalia. &#8220;Katika nchi yangu, kuwepo kwetu kunategemea sana samaki,&#8221; alisema Emelia Arthur, Waziri wa Uvuvi na Ufugaji wa samaki wa Ghana, katika taarifa iliyopeanwa na Mongabay. &#8220;Asilimia 60 ya protini ya wanyama &lt;tunayotumia inatokana na samaki, na asilimia kumi ya wakazi wetu wanategemea mnyororo wa thamani wa uvuvi ili kujipatia riziki. Uvuvi ni suala la utamaduni na usalama wa taifa kwetu. Nina furaha kuwa Ghana ni miongoni mwa mataifa ya kwanza kutia saini Azimio la Mombasa,&#8221; aliongeza. Nchi zina matumaini kwamba kwa kufanya kazi pamoja, kuoanisha kanuni na kushiriki habari kuhusu meli zinazovua katika maeneo yao ya maji, zitakuwa na ufanisi zaidi katika vita vyao dhidi ya uvuvi haramu, usioripotiwa na usiodhibitiwa IUU. &#8220;Wahusika wa uvuvi haramu wanaendelea kuwa wa kisasa zaidi katika mbinu zao za kukwepa sheria na kanuni za nchi moja kwa kuhamia nchi nyingine,&#8221; Cephas Asare aliiambia Mongabay kupitia kwa njia ya simu. Asare ni meneja wa kanda ya Afrika Magharibi wa Wakfu wa Haki ya Mazingira (EJF), Shirika lisilo la kiserikali (NGO) la Uingereza linayofanya kazi kupambana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/azimio-la-mombasa-nchi-15-zajitolea-kushiriki-taarifa-za-uvuvi-ili-kukabiliana-na-uvuvi-haramu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 08:35:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18080931/Screenshot-2026-06-18-110907-768x439.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1874</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Asia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Asidi ya Bahari, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Fedha za Uhifadhi, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi kubwa za kimataifa na za serikali, watu wengi wanaofanya kazi ya kila siku ya uhifadhi wa baharini ni mashirika ya kijamii yanayofanya kazi kwa bajeti ndogo katika ukanda wa pwani wa Afrika. Mara nyingi hufanya hivyo mbali na kuangaziwa, lakini mchango wao ni muhimu kwa nia ya kimataifa ya kuhifadhi nafasi za bahari. Mkataba wa Anuwai ya Kibiolojia (CBD), ambao chini yake Mfumo wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal ulipitisha malengo ya mwaka 2030, unaonyesha kuwa mafanikio yanategemea sana ushirikishwaji wa jamii. Kote nchini Kenya, Tanzania na Namibia, vikundi vinne kama hivyo &#8211; Maendeleo ya Rasilimali za Pwani na Bahari (COMRED) Action for Ocean, Mwambao Coastal Community Network na Namibia Nature Foundation (NNF) &#8211; hutoa fursa ya kufahamu jinsi uhifadhi wa bahari unaoongozwa na jamii unavyotekelezwa kwa vitendo. Kazi yao inaweza kuwa na ufadhili wa chini, kutofautiana na wakati mwingine polepole, lakini inazidi kuwa msingi wa jinsi ulinzi wa baharini unavyowaziwa katika bara. Mifumo ya ikolojia ya baharini barani Afrika inasaidia uvuvi, utalii, uchukuzi, uhifadhi wa kaboni na ulinzi wa pwani huku ikiendeleza mamilioni ya riziki kutoka Bahari ya Hindi Magharibi hadi pwani ya Afrika ya Atlantiki na Mediterania. Katika Afrika Mashariki hasa, mikoko, miamba ya matumbawe, nyasi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/#respond</comments>
					<pubDate>17 Juni 2026 13:26:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/17130445/Screenshot-2026-06-17-160345-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1868</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara ya Kilimo, Bioanuai wa Baharini, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo-ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Mimea yenye Tiba, na  Uhifadhi wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia mbadala ya kujikimu kimaisha. Kilimo cha mwani kikawa jibu lake, akaamua kujiunga na wanakijiji wenzake wanaofanya ukulima huo. Mwani ni kundi la viumbe wa majini wanaofanana na mimea inayokua katika maji ya chumvi, hasa maeneo ya pwani yenye kina kifupi. Hupandwa kwa kufungwa kwenye vitiji na kamba baharini. Mwani huchukua kati ya siku 45 na 60 kufikia kiwango cha kuvunwa. Mwani hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile vipodozi, sabuni, dawa, virutubisho vya lishe, vinywaji na malighafi za viwandani. What is seagrass and why is it important? Kwa wakulima wengi wa mwani katika eneo la Kwale, baada ya kuvuna wao huukausha kisha kuuuza kupitia chama cha ushirika cha mwani katika eneo la Kibuyuni. Ukulima wa mwani ulishirikisha wanawake wengi katika eneo la Kibuyuni ili wapate fursa ya kupata manufaa ya bahari ambayo imekuwa tegemeo la upatikanaji wa riziki kwa familia nyingi eneo la Pwani. Hii ni kutokana na kuwepo kwa mila na tamaduni zilizomwekea vikwazo mwanamke kuingia baharini kuvua samaki. Wakulima wa Mwani wakitayarisha Kamba tayari kwa mafunzo kuhusu upandaji wa Mwani eneo la Shanga, Lamu, Kenya. Picha na Mohamed Fuad Mohamed. Lakini ukulima huo sasa umeanza kuvutia hata wanaume kama Ahmed, kutokana na faida ambazo wameziona kwa wanawake, wakiwa na matumaini ya kupata kipato cha kujiendeleza kimaisha.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/#respond</comments>
					<pubDate>16 Juni 2026 15:28:54 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/16152623/Aquatic-animal-production-from-aquaculture-topped-100-million-tonnes-for-the-first-time-in-2024-according-to-FAOs-latest-State-of-World-Fisheries-and-Aquaculture-report-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1861</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Asia, na  Bahari ya Hindi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Baharini, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kasa wa baharini, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Utafiti, Uvuvi, Viwango vya Bahari, Wanyama wa Baharini, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo pia imeeleza kuwa sekta hiyo inayohusiana na uvuvi na ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa majini iliajiri wafanyakazi zaidi ya milioni 65, na hivyo kuwa tegemeo la maisha ya watu zaidi ya milioni 600 kote duniani. FAO ilizindua ripoti hiyo mpya ya Hali ya Uvuvi na Ufugaji wa Viumbe vya Majini Duniani (SOFIA 2026) kwenye mkutano wa 11 wa Bahari Yetu [11th Our Ocean Conference] uliofanyika jijini Mombasa, nchini Kenya. Ripoti hiyo imeeleza kuwa uzalishaji wa uvuvi na ufugaji wa viumbe vya majini duniani ulifikia rekodi ya tani milioni 235 kwa mwaka 2024. Pia uzalishaji wa wanyama wa majini ulifikia tani milioni 195 na umeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 3.2 kwa mwaka tangu miaka ya 1950. Pia ripoti ya shirika hilo la Umoja wa Mataifa imeonyesha kuwa uvuvi wa asili umeendelea kuwa thabiti kwa kiasi kikubwa tangu mwishoni mwa miaka ya 1980, hali inayochangiwa na juhudi za usimamizi wa uvuvi na uhifadhi wa mazingira katika baadhi ya maeneo. Aidha, ilibainika kuwa ufugaji wa viumbe vya majini ulizalisha tani milioni 103 za wanyama wa majini, rekodi ya juu zaidi kuwahi kushuhudiwa. Hii ni sawa na asilimia 53 ya uzalishaji wote wa viumbe vya majini duniani, na zaidi ya asilimia 59&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 20:21:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05201200/Screenshot-2026-06-05-231142-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1791</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Nishati, Siasa za Nishati, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana kama “Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk” pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa sakafu ya bahari (deep-sea mining) pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Ripoti hiyo ilitolewa Juni 4, 2026 na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani inayoadhimishwa Juni 8. Ripoti iliandaliwa kutokana na utafiti uliohusisha nchi 11 kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Katika utafiti huo, Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Nchi nyingine zilizotajwa ni Kenya, Australia, Cameroon, Indonesia, Jamaica, Norway, Trinidad na Tobago, Argentina na Mexico. Kwa Tanzania, mradi huo unapangwa kujengwa katika eneo la Likong’o, kusini mwa mkoa wa Lindi. Lengo ni kuchakata gesi asilia inayopatikana baharini na kuibadilisha kuwa gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Ripoti hiyo imetolewa siku chache baada ya Waziri wa Nishati, Dkt Deogratius Ndejembi, kuliambia Bunge kwamba makubaliano ya kibiashara na kodi kati ya serikali na wawekezaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>04 Juni 2026 12:55:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/04131449/Screenshot-2026-06-04-161427.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1773</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Gesi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na kibayolojia. Ripoti hiyo iliyopewa jina la Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk ilitolewa leo, siku chache kabla ya mkutano wa 11 unaohusu masuala ya bahari, mkutano wa ‘Our Ocean Conference’ unaotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 16 hadi 18 mjini Mombasa, Kenya. Ripoti hiyo inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa kina cha bahari pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Bonde la Lamu limetajwa kuwa eneo linalopewa kipaumbele, ambapo miradi minane ya mafuta inayotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu, imepangwa kutekelezwa katika ukanda huo wa pwani wenye historia na utajiri mkubwa wa kiikolojia. “Uchambuzi wetu unaonesha kuwa asilimia 100 ya Miamba ya matumbawe na misitu ya mikoko katika eneo hili imefunikwa na vitalu vya mafuta na gesi. Kwa asilimia 100, maeneo haya ni ya hifadhi za baharini na pwani lakini pia ni muhimu kwa bayoanuwai,” ripoti hiyo imeeleza. Katika ripoti hiyo, Kenya imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Ripoti hiyo ilitolewa na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2026 21:58:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/31214131/Atuwa-akiwa-amezamia-bahari-kwenye-kazi-ya-kurekebisha-matumbawe-kwenye-bahari-ya-kisiwa-cha-Mnemba-Zanzibar.jpeg-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1733</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Barafu ya bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Upaukaji wa Matumbawe, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa bluu, njano na kijani hupita juu ya kichwa chake huku mwanga wa jua ukionekana kwa mbali ndani ya maji. Juu ya uso wa bahari, watalii huwa wanazunguka katika maji bila kufahamu kuhusu mfumo dhaifu wa ikolojia unaopambana kuendelea kuishi chini yake. Kwa mujibu wa waajiri wake, Atuwa, mwenye umri wa miaka 23, anaelezwa kuwa mwanamke pekee Zanzibar anayeshiriki kazi hiyo ya uzamiaji wa urejeshaji wa matumbawe. Mamlaka za Zanzibar zinaeleza kuwa miaka mitatu iliyopita, eneo la Mnemba ambako Atuwa hufanya kazi, ambalo lina baadhi ya miamba muhimu ya matumbawe ya Zanzibar, liliharibika. Makame Omar Makame, Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi Baharini Zanzibar, anasema eneo hilo la Mnemba liliathiriwa na shughuli za kibinadamu zilizokithiri. “Kulikuwa na shughuli nyingi za uvuvi zisizofuata utaratibu, msongamano wa watalii, ambapo takribani boti 200 zenye watalii zilikuwa zikiingia katika eneo la mita 200 za ukanda wa pwani kila siku,” Makame aliieleza Mongabay. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, ili kulinda mazingira, Serikali ya Zanzibar iliamua kupunguza idadi ya wageni hadi 80 kwa siku na kuongeza ada ya uhifadhi kutoka $3 hadi $25 kwa mtalii mmoja, kusitisha kwa muda shughuli za uvuvi na pia kutoa elimu kwa jamii. Hilo lilikuwa jambo muhimu kwa Atuwa na wenzake ambao wanaamini jamii zao zilihitaji mazingira&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>01 Mei 2026 15:34:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/01152749/Antoine-Moses-akipanda-miche-ya-miti-ya-mikoko-katika-eneo-la-Tudor-Mombasa.-Picha-kwa-hisani-ya-Wizara-ya-Mazingira-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1485</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Mikoko, Misitu, Miti, Samaki, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini humo kwa siku 10 kabla ya tukio hilo, ambapo alipanda miti mingine 13,600 ili kujenga stamina katika maandalizi ya rekodi mpya. “Tumekuwa Kenya kwa siku 10 zilizopita tukipanda mikoko, tukijifunza kutoka kwa jamii na kutengeneza kumbukumbu zisizosahaulika na marafiki wapya,” alisema kabla ya jaribio hilo, na kuongeza: “Baada ya kufikia miti 10,000 chini ya saa nne wakati wa mazoezi, nilijua tuko tayari kusonga mbele zaidi.” Waziri wa Mazingira wa Kenya, Deborah Barasa, alimkaribisha Antoine na alikuwepo alipokuwa akipanda mche wake wa kwanza. Alisema: “Kenya imepata heshima kumkaribisha Antoine Moses… Jaribio lake la kijasiri la kupanda mikoko 40,000 ndani ya saa 24 katika eneo la Tudor Creek, Kaunti ya Mombasa, halimaanishi tu kuweka rekodi mpya, bali ni kubadili mwenendo wa uharibifu wa misitu kabla haujafikia hatua ya hatari. Uwepo wake unaimarisha nafasi ya Kenya kama kiongozi anayeaminika katika juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.” Timu iliyoratibiwa ya wanajamii, wahifadhi wa mazingira, maafisa wa Huduma ya Misitu Kenya, akiwemo Katibu Mkuu Gitonga Mugambi, pamoja na washirika kutoka Earthlungs, walimpa hamasa, wakitembea pamoja naye ili kumsaidia kutimiza malengo yake. Awali, Antoine aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba malengo yake ni kupanda miche 35,500 ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 16:47:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/06171705/Screenshot-2026-04-06-201423-768x503.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1312</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Sheria ya Mazingira, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana zaidi, ambao kulingana na wahifadhi wa mazingira, unaoonyesha jinsi hatma ya papa na samaki jamii ya pweza walio hatarini, ilivyofungamana kwa karibu na maisha ya wavuvi wanaojitafutia kipato katika Bahari ya Hindi ya Magharibi. Mnamo Februari, ili kuweka mpango kazi unaotekelezeka wa uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza nchini Kenya, kundi la watunga sera, wanasayansi na viongozi wa jamii walichapisha mkakati wenye malengo 19. Kati ya hayo, zaidi ya malengo 12 yanawahusisha moja kwa moja wavuvi wadogo au yanakusudia kuwashirikisha ili kuhakikisha mafanikio yake. Malengo hayo yanajumuisha kuanzisha maeneo zaidi ya bahari yanayosimamiwa na jamii, kuwashirikisha wavuvi katika maamuzi ya uhifadhi, na kuimarisha utekelezaji wa sheria kuhusu zana za uvuvi na uvuvi wa spishi zilizo hatarini. Tangu mwaka 2023, Kenya tayari ina sera ya uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza — Mpango wa Kitaifa wa Hatua za Uhifadhi na Usimamizi wa Papa (NPOA-Sharks). Hata hivyo, mpango huo bado unasubiri kuidhinishwa rasmi na serikali. Mkakati uliopendekezwa na wadau unatoa njia ya jinsi ya kuutekeleza. Papa aina ya scalloped hammerhead (Sphyrna lewini), aliyepigwa picha Yonaguni, Japan. Kulingana na utafiti, spishi hii huvuliwa mara kwa mara na wavuvi wadogo nchini Kenya. Picha na Masayuki Agawa kupitia Ocean Image Bank.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 17:31:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20141013/Screenshot-2026-03-20-171000-768x509.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1178</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Baharini, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maji, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii kama ilivyokuwa desturi. Nyama ya kasa ni tamu sana, na tulikuwa tunafurahia sana kitoweo chake,” alisema Abdallah. Kasa katika ufuo wa bahari Shimoni picha na Dzivula Gube Miaka 35 baadaye, Abdallah, ambaye amefanya uvuvi kwa miaka tisa sasa katika eneo la Shimoni, amekuwa mkereketwa mkubwa wa masuala ya kuhifadhi kasa katika kijiji chake. Abdallah pia anashirikiana na kikundi cha vijana cha Shimoni Turtle Watch kilichoko wadi ya Pongwe-Kikoneni, Shimoni, eneo bunge la Lunga Lunga katika Kaunti ya Kwale, ambacho kimefanya kazi hiyo ya uhifadhi wa kasa kwa miaka saba sasa. Hii ni kutokana na tishio la kupotea kwa kasa kutokana na uchafuzi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi, shughuli za uvuvi na ujenzi kwenye fuo za bahari. Wavuvi wanaochinja kasa waliokufa Zaidi, Abdallah na kikundi hicho walisema wamechukua hatua hiyo ya kumlinda kasa kutokana na tishio kwamba kuna wavuvi wengine ambao wanapokutana na kasa amekufa humchinja na kugawia watu nyama yake, hatua ambayo inahatarisha afya ya jamii. Farid Abdallah Mvuvi akionyesha aina ya karatasi za plastiki zipatikanazo baharini ambazo kasa hupenda kula na ni hatari kwao. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kasa ni aina ya kobe wakubwa wanaoishi baharini. Mnyama huyo hutaga mayai yake ardhini hasa katika ufukwe wa bahari, na kuyafukia humo kwa kati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>04 Januari 2026 19:23:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/04190953/kuruwitu1-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=871</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mazingira, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Takwimu, Ufugaji, Ufugaji Samaki, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya uhifadhi wa mazingira ya baharini?&#8221; aliniuliza kijana wa rika, mwendesha pikipiki. Na baada ya dakika kama saba, nilikuwa nimefika eneo hilo. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Kuruwitu Conservation Welfare and Association Daniel Mwangunya alikuwa ameshawasili tayari kuhojiwa kuhusu shughuli zao za uhifadhi wa mazingira ya bahari katika bandari ya Kinuni. Lakini kwanza aliomba tumsubiri mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa matumbawe, ambaye kwa wakati huo alikuwa amepeleka wageni kuzama na kutalii mandhari ndani ya bahari. Tengefu ni eneo la bahari lililotengwa na kusimamiwa na wanajamii kwa ajili ya uhifadhi wa viumbe na mazingira ya baharini. Eneo lililohifadhiwa na jamii ya Kuruwitu kwa ajili ya kuongeza samaki na kuhifadhi matumbawe. Picha na Ruth Keah. Katika mantiki ya tengefu, hili ni eneo ambalo uvuvi wa samaki hauruhusiwi. Eneo hili linalindwa na wanajamii, hivyo kusababisha samaki kuwa na mazingira mwafaka ya kuzaana na kuongezeka. Wanapokuwa wengi, wanamiminika hadi sehemu ambazo wavuvi wanaruhusiwa kuvua, hivyo basi kuongeza kipato. Utulivu ulionikaribisha hapo ni ishara kwamba hakuna shughuli za uvuvi zinazoendelea, bali ni pilkapilka za kupokea wageni, kutayarisha vifaa kama vile mashua na zana za kuzamia kwenye bahari. Katana Ngala ni mzaliwa wa kijiji cha Kuruwitu, na ni miongoni mwa waanzilishi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>