<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=biashara&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/biashara/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sun, 20 Sep 2026 18:30:08 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.5</generator>
				<item>
					<title>Mradi wa Pemba wa majongoo ya baharini unaolenga kuoanisha biashara na uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/09/01/mradi-wa-pemba-wa-majongoo-ya-baharini-unaolenga-kuoanisha-biashara-na-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/09/01/mradi-wa-pemba-wa-majongoo-ya-baharini-unaolenga-kuoanisha-biashara-na-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>01 Septemba 2026 14:42:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/09/01142610/Screenshot-2026-09-01-172043-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2679</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Biashara ya Kilimo, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Dawa ya Jadi ya Kichina, Eneo Lililolindwa Baharini, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Uchumi wa Mazingira, Uhifadhi wa Baharini, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kama jamii nyingi za pwani kote Afrika Mashariki, wakazi wa Shamiani wamezoea kutazama bahari ikitoa mavuno yanayozidi kupungua. Maji yenye joto, makazi ya baharini yaliyoharibika na miongo kadhaa ya shinikizo la uvuvi vyote vimeathiri rasilimali ambazo hapo awali ziliendeleza riziki za wenyeji, kulingana na wanajamii. Katika Kisiwa cha Pemba cha Tanzania, kisiwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/01/mradi-wa-pemba-wa-majongoo-ya-baharini-unaolenga-kuoanisha-biashara-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mradi wa Pemba wa majongoo ya baharini unaolenga kuoanisha biashara na uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kama jamii nyingi za pwani kote Afrika Mashariki, wakazi wa Shamiani wamezoea kutazama bahari ikitoa mavuno yanayozidi kupungua. Maji yenye joto, makazi ya baharini yaliyoharibika na miongo kadhaa ya shinikizo la uvuvi vyote vimeathiri rasilimali ambazo hapo awali ziliendeleza riziki za wenyeji, kulingana na wanajamii. Katika Kisiwa cha Pemba cha Tanzania, kisiwa kinachounda sehemu ya Zanzibar, Shamiani si tofauti. Hata hivyo, hapa, wakazi wanajaribu kitu tofauti. Kamba sasa zinaweka mipaka ya maene yenye nyasi za bahari katika maji ya kina kifupi, hatua iliyofikiwa baada ya miezi kadhaa ya mikutano na majadiliano ya jamii kuhusu namna eneo hilo linapaswa kusimamiwa. Kwa vizazi vingi, maji ya pwani ya kisiwa hicho yamesaidia familia za wavuvi. Lakini katika miaka ya hivi majuzi, wakazi wengi wanasema rasilimali za karibu na pwani zimepungua kwa kasi. Majongoo ya baharini, ambayo hapo awali yalikuwa mengi na kuvunwa kwa ajili ya kusindikwa nchini, yamekuwa machache zaidi. Wavuvi na wavunaji sasa wanafanya kazi kwa bidii zaidi kwa mapato madogo, wakijaribu kupata riziki kutokana na rasilimali za pwani ambazo wengi wanasema si nyingi tena kama ilivyokuwa hapo awali. Mwonekano wa eneo la marufuku ya uvuvi linalosimamiwa na kampuni ya Asili huko Shamiani, katika Kisiwa cha Pemba; hapa, maeneo yaliyohifadhiwa yenye nyasi za bahari katika maji ya kina kifupi hutumika kufugia majongoo ya baharini. Eneo hilo lilianzishwa kufuatia miezi kadhaa ya mikutano ya jamii na majadiliano kuhusu usimamizi wake. Picha na David Akana, Mongabay. Kupungua huko ndiko kulikosukuma Asili, kampuni ya ufugaji wa viumbe vya majini yenye makao yake nchini Tanzania na inayoshirikiana na jamii za Pemba&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/01/mradi-wa-pemba-wa-majongoo-ya-baharini-unaolenga-kuoanisha-biashara-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/09/01/mradi-wa-pemba-wa-majongoo-ya-baharini-unaolenga-kuoanisha-biashara-na-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/#respond</comments>
					<pubDate>18 Agosti 2026 06:16:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Rice]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/18060350/Screenshot-2026-08-18-090213-768x492.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2511</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika ya Kati, Angola, Asia, Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Tanzania, Vietnam, na  Zambia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Cites, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Spishi, Tembo, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu uliopangwa, na  Usafirishaji wa Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo alikamatwa pia. Mshukiwa huyo alikuwa amehukumiwa mwaka 2019 kwa kumiliki zaidi ya kilo 200 (karibu paundi 441) za pembe za ndovu, na mwaka 2020 alipewa kifungo cha miaka mitano gerezani. Hata hivyo, aliachiwa huru baada ya miezi michache tu, na tangu wakati huo amekuwa akiendelea na biashara hiyo haramu. Zambia imekuwa ikitumiwa vibaya na mitandao ya wahalifu tangu angalau mwaka 2002, na sasa iko tena chini ya mwanga wa uchunguzi. Kinachosumbua hasa ni ushiriki wa makundi ya wahalifu kutoka Kongo, ambayo yanafanya kazi kwa uhuru mkubwa ndani ya Zambia na nchi jirani. Makundi hayo yanakusanya na kusafirisha bidhaa za wanyamapori — pembe za ndovu za tembo, pembe za kifaru, magamba ya pangolin na paka wakubwa — kupitia njia ngumu za kimataifa kuelekea Asia, huku Vietnam mara nyingi ikitumika kama kituo muhimu cha kupitishia. Mitandao hii inajinufaisha na ukosefu wa nia ya kisiasa, utekelezaji dhaifu wa sheria, maafisa wafisadi na jamii zilizotengwa. Inaandaa misafara ya ujangili katika nchi jirani na kutumia wasuluhishi wa Zambia kupanua minyororo yake ya biashara haramu. Ukamataji wa Zambia — ukijumlishwa na matukio mawili ya ukamataji mkubwa uliofanywa Tanzania na Botswana mnamo Aprili na Mei mtawalia — unaleta jumla ya pembe za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka baharini hadi sokoni: Wanawake wanaoendesha biashara ya dagaa Vanga</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/#respond</comments>
					<pubDate>12 Agosti 2026 22:37:07 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asha Bekidusa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/12222728/Boti-zikiwa-katika-ufuo-wa-Vanga-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2439</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, na  Spishi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za dunia walipokongamana mjini Mombasa wakati wa Our Ocean Conference, suala la nafasi ya wanawake kama uti wa mgongo wa sekta ya bahari na uvuvi lilijitokeza pakubwa. Hii ilibainika huku utafiti kutoka WorldFish ukionyesha kuwa barani Afrika, asilimia 90 ya wanawake katika sekta ya uvuvi na ufugaji samaki wameajiriwa katika shughuli za [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/" data-wpel-link="internal">Kutoka baharini hadi sokoni: Wanawake wanaoendesha biashara ya dagaa Vanga</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Wawakilishi kutoka sehemu mbalimbali za dunia walipokongamana mjini Mombasa wakati wa Our Ocean Conference, suala la nafasi ya wanawake kama uti wa mgongo wa sekta ya bahari na uvuvi lilijitokeza pakubwa. Hii ilibainika huku utafiti kutoka WorldFish ukionyesha kuwa barani Afrika, asilimia 90 ya wanawake katika sekta ya uvuvi na ufugaji samaki wameajiriwa katika shughuli za uvunaji na uhifadhi wa samaki baada ya kuvuliwa. Mmoja wa wasaidizi wa Sauda Hassan akidondoa dagaa katika kijiji cha Jimbo, Kwale. Pamoja naye ni mfanyabiashara aliyekuja kuchukua mzigo wake. Picha na Asha Bekidusa, Mongabay. Kwa baadhi ya wanawake katika kijiji cha Vanga, hili ni jambo la kawaida. Wengi wao wanajihusisha na biashara ya dagaa, ambapo kila asubuhi hukusanyika katika ufuo wa Vanga wakisubiri boti kutoka baharini. Wanawake hao huchukua dagaa hao kuwachemsha, kuwakausha na kuwauza katika sehemu mbalimbali nchini Kenya na nje ya nchi. Miongoni mwa dagaa hao ni katashingo (Sardinella neglecta), kimalawari (Stolephorus indicus) na simsimu (ecapterus macrosoma). Kama wanawake wengine Vanga, Mwanakombo Shee alianza biashara yake takriban miaka nane iliyopita. Mtaji wake ulikuwa KSh10,000 ($77.36) ambao alipata kupitia chama cha kuweka na kukopa alichokuwa mwanachama pamoja na wenzake. “Nilianza biashara hii nilipoona wenzangu kule Jimbo wakifanya biashara,” anasema Mwanakombo. Sauda Hassan, mfanyabiashara wa dagaa kwa mwaka 10 sasa, na ambaye ni mwenyeji wa Jimbo, hakumbuki kiasi halisi cha mtaji wake. Hata hivyo, ni kupitia chama na akiba yake kidogo kidogo ambapo aliweza kuanzisha biashara yake. Biashara hii imemuwezesha kulipa karo ya shule na madrasa kwa watoto wake. “Sikumbuki ni pesa ngapi lakini tulifanya mradi wa mikoko nikapata pesa, nikaongeza na zangu nyengine kidogo kidogo,” anakumbuka&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/12/kutoka-baharini-hadi-sokoni-wanawake-wanaoendesha-biashara-ya-dagaa-vanga/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 17:58:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mazera Ndurya]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28172645/Screenshot-2026-07-28-202121-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2245</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Jinsia na Uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Ongezeko la Joto Baharini, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Teknolojia ya kisasa yabadilisha ukulima wa mwani na kuongeza kipato cha wakulima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kadri changamoto za soko zinavyoongezeka ndivyo wakulima wa mwani wanavyochangamkia mbinu mpya za uzalishaji na uuzaji wa mmea huo wa baharini. Wakisaidiwa na utafiti, ubunifu na teknolojia, wakulima wa mwani katika vijiji vya Kibuyuni, Kijiweni, Mtimbwani na Changai, katika ukanda wa pwani wa Shimoni-Vanga, Kaunti ya Kwale, wameanza kuona matunda ya mbinu tofauti-tofauti wanazotumia baharini na hata katika kutafuta soko. Marinda Masudi, mwenye umri wa miaka 40, ni miongoni mwa wakulima waliojitosa katika ukulima wa mwani kama njia moja ya kukidhi mahitaji ya familia yake. Ilimchukua muda kuamua kujiingiza katika kilimo hicho, lakini biashara yake ya mahamri ilipoanza kudorora, hakuwa na la ziada. Wanawake kutoka Mwazaro, Kaunti ya Kwale, wakionyesha baadhi ya bidhaa, zikiwemo krimu na sabuni walizotengeneza kutoka kwa mwani. Picha na Mazera Ndurya, Mongabay. “Baada ya kujisajili na Kitengo cha Kusimamia Fukwe (BMU) cha Kibuyuni, nilionyeshwa sehemu ya kuanza kulima mwani, na baada ya takriban miezi miwili nilianza kuvuna mwani, kuukausha na kuuuza. Mapato niliyopata nilimsaidia mume wangu kuwasomesha watoto. Mara ya kwanza nilipovuna na kuuza mwani kutoka kwa bloki mbili, nilipata kima cha KSh30,000 ($230),” alisema Marinda. Kama ilivyokuwa na wakulima wengine, alipoanza ukulima, walikuwa wakitumia mbinu ile ambayo imetumika tangu jadi, ambayo hufanyika katika maeneo karibu na ufuo wa bahari. “Mkulima alihitajika kuingia msituni na kukata vigingi vingi vya kufungia kamba na kuweka mbegu. Kwa shamba moja la vipande sita, mtu alihitaji vigingi 300 kufanikisha ukulima wa mwani,” Marinda alieleza. Mbinu ya jadi ilijulikana kama sikio moja au mfungo mmoja, yaani kufunga mbegu moja moja kwenye kamba. Kwa mujibu wa kitabu “Sea Level Rise and Ocean Health in the&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/teknolojia-ya-kisasa-yabadilisha-ukulima-wa-mwani-na-kuongeza-kipato-cha-wakulima-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:16:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28111600/Tembo-6-1.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2227</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga baada ya kusikiliza mawasilisho ya pande zote mbili. Rufani hiyo iliyowasilishwa na Wakili wa Serikali Paulina Massawe ilitokana na uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Morogoro uliowaachia huru Yahaya Juma na Masima Mlugu waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000 bila kibali halali. Mahakama ya Wilaya Katika Mahakama ya Wilaya, upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi sita, akiwemo mtunza vielelezo, askari aliyefanya ukamataji, shahidi huru aliyeshuhudia upekuzi na ukamataji, mhifadhi wa wanyamapori aliyefanya uthamini wa meno ya tembo, askari wa TANAPA aliyeshiriki operesheni pamoja na mpelelezi wa kesi. Upande wa mashtaka uliwasilisha vielelezo saba, vikiwemo vipande 18 vya meno ya tembo, meno matatu kamili ya tembo, magunia mawili ya salfeti yaliyobebea meno hayo, pikipiki aina ya FEKON yenye namba T43 CNF, hati ya ukamataji na ripoti ya uthamini iliyoonyesha kuwa nyara hizo zilikuwa na thamani hiyo. Kwa upande wa utetezi, washtakiwa wote wawili walitoa ushahidi wao wenyewe. Mshtakiwa wa kwanza aliwasilisha pia flashi diski iliyokuwa na video ya YouTube akidai kuwa meno ya tembo yaliyoonyeshwa kwenye taarifa ya habari hayakuwa na alama, tofauti na yale yaliyowasilishwa mahakamani kama vielelezo. Mahakama ya Wilaya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:03:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28112229/ELEPHANT-3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2230</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sheria, Tembo, Uhalifu, Usafirishaji wa Wanyamapori, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama ya Wilaya ya Songwe ilimhukumu mshtakiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kukutwa na vipande 10 vya meno ya tembo vyenye thamani ya $60,000 bila kibali halali. Upande wa mashtaka uliita mashahidi sita na kuwasilisha vielelezo mbalimbali, huku mshtakiwa akikana mashtaka na kudai alikamatwa kimakosa alipokuwa amekwenda kununua mahindi na hakuwa na shahidi. Mamlaka ya mahakama Katika rufaa yake, Nchola alijiwakilisha mwenyewe, alipinga hukumu hiyo akidai miongoni mwa mambo mengine kuwa Mahakama ya Wilaya haikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo kwa kuwa kumbukumbu za kesi hazikuonyesha kuwepo kwa hati ya idhini ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) pamoja na cheti cha mamlaka vinavyotakiwa kisheria katika makosa ya uhujumu uchumi. Katika kuunga mkono rufaa yake, mrufani alidai kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha shtaka dhidi yake pasipo kuacha shaka yoyote ya msingi. Alidai kuwa ushahidi wa shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka (PW1) kuhusu uthamini wa nyara za Serikali haukuwa wa kuaminika. Pia alidai kuwa mlolongo wa utunzaji wa vielelezo haukuthibitishwa kwa sababu shahidi muhimu hakuitwa kutoa ushahidi. Aidha alidai kuwa mashahidi wa upande wa mashtaka walishindwa kuvitambua ipasavyo vielelezo walipokuwa wakitoa ushahidi mahakamani. Uhalali wa vielelezo Aliongeza kuwa hata mahakama ya mwanzo ilionyesha mashaka kuhusu uhalali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 10:40:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21195128/Raia-wa-Korea-Kaskazini.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2165</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Biashara ya Wanyamapori, Bustani za wanyama, Ikolojia, Matumizi ya Wanyamapori, Mifumo ya Ikolojia, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Raia wa Korea Kaskazini anayedaiwa kukutwa na meno ya tembo, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam imemwachilia huru na kuamuru aondoke nchini Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37) aliyekuwa akikabiliwa na mashtaka ya Uhujumu Uchumi baada ya Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuomba hivyo kwa maelezo kwamba upande wa Jamhuri hawana nia ya kuendelea na shauri hilo. Maombi hayo ya Jamhuri yaliwasilishwa mahakamani na Wakili wa Serikali Mkuu, Twawabu Issa mbele ya Hakimu Hakimu Mkazi Mkuu, Salome Mwasha aliyekuwa akisikiliza shauri hilo dhidi ya mshtakiwa Ra aliyedaiwa kukutwa na vipande 504 vya meno ya tembo bila kibali. Wakili Twawabu alidai kuwa DPP kwa mamlaka aliyonayo kisheria aliwasilisha uamuzi wa kusitisha mashtaka (nolle prosequi)  (chini ya Kifungu cha 92 cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai (CPA) sura ya 20 iliyofanyiwa marejeo mwaka 2023 ambapo zamani kilikuwa Kifungu cha 91 kabla ya marekebisho ya 2022) akionyesha kuwa Jamhuri haina nia ya kuendelea na shauri hilo hivyo akaomba mahakama imwachie huru mshtakiwa. Mshitakiwa atakiwa kuondoka nchini Upande wa mashtaka pia uliwasilisha maombi &#8220;persona non grata&#8221; kuonyesha kuwa mshtakiwa huyo hatakiwi kuendelea kubaki nchini Tanzania na anatakiwa kuondoka. Mahakama baada ya kusikiliza maombi hayo iliyakubali na kuamuru mshtakiwa aachiliwe huru na aondoke nchini. Katika shauri lolote la jinai na katika hatua yoyote kabla ya hukumu au uamuzi, DPP anaweza kuwasilisha nolle prosequi kwa kuitaarifu Mahakama kuwa Jamhuri haitaendelea na mashtaka lakini haizuii kumshtaki tena mshtakiwa pale inapohitajika kufanya hivyo. Ra alifikishwa mahakamani mara ya kwanza Mei 5 , 2026 akikabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/raia-wa-korea-kaskazini-anayedaiwa-kukutwa-na-meno-ya-tembo-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/#respond</comments>
					<pubDate>21 Julai 2026 17:56:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Kelvin Matuku]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21171918/Screenshot-2026-07-21-201312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2148</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Fedha ya mfumo wa ikolojia, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi wa Mazingira, Ufugaji Samaki, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari upya mustakabali wa uvuvi katika ziwa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi barani Afrika. “Wakati mwingine nakaa ziwani usiku mzima na kurudi na kati ya samaki 300 na 359 pekee,” anasema Otieno, ambaye amevua katika Ziwa Victoria kwa miongo kadhaa. “Samaki ni wachache na kipato pia kinapungua. Kama mvuvi, naona njia ambayo imebakia ni kukumbatia vizimba vya samaki ili tuweze kuendelea kuishi.” Ufukwe wa Paga kwenye Ziwa Victoria. Picha na Kelvin Matuku, Mongabay. Ziwa Victoria ni chanzo cha kujikimu kwa jamii za wavuvi nchini Kenya, Uganda na Tanzania, kupitia uvuvi na biashara zinazohusiana nao. Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2023, katika miaka ya hivi karibuni, Ziwa Victoria na eneo lake la vyanzo vya maji vimeathirika vibaya kutokana na “uvuvi kupita kiasi, umwagikaji wa mafuta, utiririshaji wa taka ambazo hazijatibiwa, kuenea kwa spishi vamizi, uchotaji wa maji kupita kiasi kutoka bonde la ziwa, na mabadiliko ya tabianchi, miongoni mwa sababu nyingine.” Kushuka kwa uzalishaji wa samaki Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS), uzalishaji wa samaki katika Ziwa Victoria umeshuka kutoka takriban tani za metriki 94,349 mwaka wa 2021 hadi 67,575 mwaka wa 2024. Huu ni upungufu wa zaidi ya tani 27,700 katika kipindi cha miaka mitatu. Upungufu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 08:18:04 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16074828/Screenshot-2026-07-16-003002-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2110</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uzuri wa Kiikolojia, na  Viwango vya Bahari]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Kuboresha uvuvi unaozidi kutapatapa, Kenya yaongeza ukusanyaji wa takwimu za boti za wavuvi wadogo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MTWAPA, Kenya — Katika asubuhi moja ya mwezi wa Machi, Mohamed Mwazigona, mwenye umri wa miaka 58, alikuwa amepata mavuno madogo sana ya samaki kwenye ufukwe wa mji wa Mtwapa, ulioko pwani ya kaskazini mwa Kenya. Wafanyakazi wake walikuwa wakilitayarisha boti kwa ajili ya safari ya pili baharini, wakitumai kupata bahati nzuri zaidi. Huku wafanyabiashara walipoanza kuwasili ili kununua samaki, Mwazigona alikaa juu ya boti iliyovunjika na kupinduliwa akitazama upeo wa bahari. Safari yake ya asubuhi ilikuwa imemletea kilo 2 pekee za samaki. Alikuwa na hofu kuhusu kupungua kwa kiasi kikubwa kwa mavuno yake ya samaki katika miaka ya hivi karibuni. &#8220;Idadi ya wavuvi imeongezeka; tumekuwa wengi mno,&#8221; alisema. Hiyo ndiyo sababu kuu iliyomfanya aondoke kijijini kwake Shariani, kilichoko umbali wa kilomita 40 kuelekea kaskazini, ili kufanyia shughuli zake za uvuvi Mtwapa; eneo aliloona kuwa na wavuvi wachache na uwezekano mzuri zaidi wa kufikia masoko. Nchini Kenya, vitengo vya usimamizi wa fukwe (BMU), kama vile Mtwapa BMU Mtwapa BMU ambayo Mwazigona ni mali yake, vina mamlaka ya kisheria ya kusaidia ukusanyaji wa takwimu za uvuvi kwa ajili ya kuwasilishwa kwa serikali: hasa aina ya samaki ambao wanachama wake huvua na uzito. Takwimu hizi zinalenga kufahamisha uamuzi wa serikali kuhusu uvuvi mdogo ili iweze kusaidia kubadilisha ushindani wa kupungua kwa samaki ambao Mwazigona na wenzake wanashuhudia. Pia zinalenga kuwasaidia wavuvi wenyewe kufanya maamuzi kuhusu wapi na wakati wa kuvua. Hata hivyo, takwimu za uvuvi mdogo za BMU hazijakuwa sahihi na haipatikani kwa wadau. Ili kushughulikia tatizo hili na kuboresha uendelevu wa uvuvi mdogo wa Kenya,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/kuboresha-uvuvi-unaoendelea-kutapatapa-kenya-yaongeza-ukusanyaji-wa-takwimu-za-boti-za-wavuvi-wadogo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:11:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14191215/Namakongoro-4-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2075</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Ikolojia, Irejeshaji wa Mfumo wa Ikolojia, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu mkubwa wa makazi ya viumbe baharini, hivyo kupunguza idadi ya samaki, pweza na viumbe wengine wanaotegemea mazingira hayo kuishi na kuzaliana. Baadhi ya viumbe walihamia kwenye maeneo yenye kina kirefu, jambo lililovuruga mfumo wa ikolojia wa bahari na kupunguza bioanuwai. Hata hivyo, tangu mwaka 2021 hali ilianza kubadilika kufuatia juhudi za pamoja za jamii, Serikali, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU) na taasisi ya Sea Sense, inayojihusisha na uhifadhi wa mazingira ya bahari na ukanda wa pwani, kuanzisha mikakati ya uhifadhi wa bahari. Wavuvi wa Namakongoro wakipewa mafunzo ya uhifadhi bahari kupitia njia za uvuvi endelevu na Maofisa wa Halmashauri ya Namakongoro pamoja na Taasisi ya Seasense. Picha kwa hisani ya SeaSense. Juhudi hizo zimeleta mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kusaidia kurejesha matumbawe, kuongeza wingi wa samaki waliokuwa wamepungua pamoja na kupungua kwa kiwango kikubwa kwa uvuvi haramu. Kurejesha uhai wa bahari Mafanikio ya kurejesha uhai wa bahari Namakongoro yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya wanakijiji, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU), Sea Sense na Serikali. Baada ya kubaini kuwa chanzo kikuu cha uharibifu huo kilikuwa ni uvuvi haramu, taasisi ya Sea Sense iliingia katika kijiji cha Namakongoro. Mratibu wa Mradi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 17:28:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13171052/Screenshot-2026-07-13-195700-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2046</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Maji, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi wa Maji, Ufugaji Samaki, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Ana kwa ana na kinara anayefungua njia na kutetea wanawake wa Uganda katika sekta ya uvuvi barani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Akizungumza kwenye mkutano wa vikundi vya uhifadhi wa bahari na wataalamu wa maendeleo huko Watamu, Kenya, Lovin Kobusingye alikuwa na ujumbe mfupi: Wanawake wanaovua, wanaosindika na wanaouza samaki bado hawako kwenye mazungumzo kuhusu uchumi wa bahari unaokua barani Afrika. Kwa Kobusingye, changamoto zinazowakabili wanawake katika uvuvi ni sehemu ya maisha yake ya kila siku. &#8220;Uhalisia wangu kila siku ni kwamba naamka na mtu mwenye bidii ya kazi akichukua sehemu yangu ya kutua, akichukua eneo langu la uvuvi,&#8221; aliiambia hadhira, akielezea jinsi maendeleo ya utalii na uwekezaji mwingine wa pwani yanavyoendelea kushindana na jamii za uvuvi wa jadi kwa ajili ya kupata ufikiaji wa bahari. Kobusingye alisema wanawake wengi wanakabiliwa na hatari katika sekta ya uvuvi, mazingira duni ya kazi na shinikizo linaloongezeka kutoka kwa maendeleo yanayozidi kusukuma shughuli za uvuvi pembezoni. Katika baadhi ya jamii, haki za kitamaduni zinapuuzwa na serikali; huku kuongezeka kwa kina cha bahari, mmomonyoko wa udongo na kupungua kwa samaki wanaovuliwa kukifanya maisha ambayo tayari ni magumu kuwa magumu zaidi, aliwaambia waliohudhuria mkutano ulioandaliwa na Ocean Resilience Climate Alliance (ORCA). Licha ya changamoto hizi, Kobusingye alisema wanawake wanasalia kuwa muhimu katika kuendeleza uvuvi na uchumi wa pwani. Husindika samaki, huuza vyakula vya baharini na kusaidia familia zao, ikiwa ni pamoja na kulipa ada za shule, kutokana na mapato wanayopata. Hata hivyo, licha ya jukumu lao katika sekta hiyo, wanawake wengi bado hawana usemi mkubwa katika jinsi uvuvi unavyosimamiwa. Lovin Kobusingye pia ni mwanzilishi na Mkurugenzi Mtendaji wa Kati Farms Ltd, kampuni ya usindikaji wa mazao ya kilimo. Picha kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/ana-kwa-ana-na-lovin-kobusingye-kinara-anayefungua-njia-na-kutetea-wanawake-wa-uganda-katika-sekta-ya-uvuvi-barani-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>07 Julai 2026 21:50:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Clark]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/07214049/Screenshot-2026-07-08-003816-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2025</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Migogoro, Samaki, Samaki wa Maji safi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. &#8220;Ofisi ya zamani ilikuwa pale chini,&#8221; mvuvi anasema, akielekeza kuelekea ufuo wa magharibi wa Ziwa Turkana, ziwa kubwa zaidi la kudumu la jangwa duniani, linaloonekana kilomita chache tu. &#8220;Lakini sasa iko kwenye maji.&#8221; Katika kipindi cha miaka 15 iliyopita, Ziwa Turkana limeongezeka kwa takriban mita 8-10 (futi 26-33). Hii imeongeza upana wa uso wake kwa karibu 10%. Ndani na karibu na kitovu cha uvuvi cha Kalokol, mamia ya watu wamelazimika kuhama makazi yao kutokana na kuongezeka huku kwa kina cha maji. Katika kisa cha Esirite, kijiji alichokulia, Natole, kimeachwa kwa muda mrefu. Mvuvi huyo amelazimika kuhama mara tatu tangu 2014, akisukumwa mbali zaidi na ardhi ya mababu zake na maeneo ya kuzaliana ya ufukweni ambayo amevua kwa muda mrefu wa maisha yake. &#8220;Tunateseka, lakini hakuna anayetusaidia,&#8221; anasema. &#8220;Tunamuomba Mungu msaada.&#8221; Lakini hata kanisa ambalo Esirite alikuwa akisalia liko kwenye maji. Hali inayoendelea huko Kalokol ni sehemu ya mwelekeo mpana. Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2010, maziwa mengi katika eneo lote la Bonde la Ufa la Kenya yamefurika, upanuzi wake ukiongezeka baada ya mvua kubwa sana mnamo 2020, na kulazimisha makumi ya maelfu ya watu kuacha makazi yao. Lakini hapa, katika kona hii ya kaskazini ya nchi ambayo imepuuzwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 08:35:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18080931/Screenshot-2026-06-18-110907-768x439.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1874</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Asia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Asidi ya Bahari, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Fedha za Uhifadhi, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi kubwa za kimataifa na za serikali, watu wengi wanaofanya kazi ya kila siku ya uhifadhi wa baharini ni mashirika ya kijamii yanayofanya kazi kwa bajeti ndogo katika ukanda wa pwani wa Afrika. Mara nyingi hufanya hivyo mbali na kuangaziwa, lakini mchango wao ni muhimu kwa nia ya kimataifa ya kuhifadhi nafasi za bahari. Mkataba wa Anuwai ya Kibiolojia (CBD), ambao chini yake Mfumo wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal ulipitisha malengo ya mwaka 2030, unaonyesha kuwa mafanikio yanategemea sana ushirikishwaji wa jamii. Kote nchini Kenya, Tanzania na Namibia, vikundi vinne kama hivyo &#8211; Maendeleo ya Rasilimali za Pwani na Bahari (COMRED) Action for Ocean, Mwambao Coastal Community Network na Namibia Nature Foundation (NNF) &#8211; hutoa fursa ya kufahamu jinsi uhifadhi wa bahari unaoongozwa na jamii unavyotekelezwa kwa vitendo. Kazi yao inaweza kuwa na ufadhili wa chini, kutofautiana na wakati mwingine polepole, lakini inazidi kuwa msingi wa jinsi ulinzi wa baharini unavyowaziwa katika bara. Mifumo ya ikolojia ya baharini barani Afrika inasaidia uvuvi, utalii, uchukuzi, uhifadhi wa kaboni na ulinzi wa pwani huku ikiendeleza mamilioni ya riziki kutoka Bahari ya Hindi Magharibi hadi pwani ya Afrika ya Atlantiki na Mediterania. Katika Afrika Mashariki hasa, mikoko, miamba ya matumbawe, nyasi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>04 Januari 2026 19:23:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/04190953/kuruwitu1-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=871</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mazingira, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Takwimu, Ufugaji, Ufugaji Samaki, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya uhifadhi wa mazingira ya baharini?&#8221; aliniuliza kijana wa rika, mwendesha pikipiki. Na baada ya dakika kama saba, nilikuwa nimefika eneo hilo. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Kuruwitu Conservation Welfare and Association Daniel Mwangunya alikuwa ameshawasili tayari kuhojiwa kuhusu shughuli zao za uhifadhi wa mazingira ya bahari katika bandari ya Kinuni. Lakini kwanza aliomba tumsubiri mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa matumbawe, ambaye kwa wakati huo alikuwa amepeleka wageni kuzama na kutalii mandhari ndani ya bahari. Tengefu ni eneo la bahari lililotengwa na kusimamiwa na wanajamii kwa ajili ya uhifadhi wa viumbe na mazingira ya baharini. Eneo lililohifadhiwa na jamii ya Kuruwitu kwa ajili ya kuongeza samaki na kuhifadhi matumbawe. Picha na Ruth Keah. Katika mantiki ya tengefu, hili ni eneo ambalo uvuvi wa samaki hauruhusiwi. Eneo hili linalindwa na wanajamii, hivyo kusababisha samaki kuwa na mazingira mwafaka ya kuzaana na kuongezeka. Wanapokuwa wengi, wanamiminika hadi sehemu ambazo wavuvi wanaruhusiwa kuvua, hivyo basi kuongeza kipato. Utulivu ulionikaribisha hapo ni ishara kwamba hakuna shughuli za uvuvi zinazoendelea, bali ni pilkapilka za kupokea wageni, kutayarisha vifaa kama vile mashua na zana za kuzamia kwenye bahari. Katana Ngala ni mzaliwa wa kijiji cha Kuruwitu, na ni miongoni mwa waanzilishi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>15 Oktoba 2025 07:04:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/07070649/Screenshot-2025-11-07-100242-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=743</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Biashara, Chakula, Chembechembe ndogo za plastiki, Kanuni, Kemikali, Magonjwa, Mazingira, Ndege, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uhifadhi, upatikanaji wa chakula, Utafiti, na  Utandawazi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni sumu kwa afya ya binadamu na mazingira. Sehemu za uchafu wa kielektroniki, majaa ya taka na vichomea taka ni vyanzo muhimu vya uchafuzi huu, huku mayai yaliyofanyiwa utafiti katika maeneo jirani yakipatikana kuwa yamechafuliwa sana na kemikali zinazotolewa wakati taka za plastiki zinachomwa. Sampuli ya mayai yaliyotolewa karibu na maeneo ya taka za kielektroniki nchini Ghana mwaka wa 2019, kwa mfano, yalikuwa na viwango vya dioksini za bromini iliochanganywa na klorini mara 200 zaidi ya kiwango cha usalama cha chakula. Uzalishaji na matumizi ya kimakusudi ya dioksini umeondolewa au kuwekewa vikwazo vikali ulimwenguni kote chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Stockholm kuhusu vichafuzi vinavyoendelea vya kikaboni (POPs). Utafiti huo, uliochapishwa katika jarida la Emerging Contaminants, uliongozwa na Mtandao wa Kimataifa wa Kutokomeza Uchafuzi (IPEN), pamoja na shirika lisilo la serikali la Czech Arnika na timu ya wanasayansi wa kimataifa. Utafiti huo ulikuwa wa kina, na data ya sumu ya yai iliyokusanywa katika nchi nyingi zinazoendelea, na nchi zilizo na uchumi wa mpito, barani Afrika, Asia, Amerika Kaskazini na Kusini na Ulaya. Matokeo hayo yanahusu sana, waandishi wa utafiti wanasema, kwani mayai ni chanzo muhimu cha protini katika nchi za kipato cha chini na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatimaye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imechukua hatua kuwalinda kasuku wa kijivu wa Afrika kutokana na biashara haramu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/#respond</comments>
					<pubDate>02 Septemba 2025 11:37:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dider Makal]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/01113941/Screenshot-2025-10-01-143917-768x470.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=575</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, na  Afrika ya Kati]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya Wanyamapori, Cites, Ikolojia, Kijani, Misitu, Ndege, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LUBUMBASHI, DRC — Idadi ya kasuku wa kijivu wa Afrika inaendelea kupungua maeneo ya katikati na kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.Takwimu zilizokusanywa wakati wa doria na Lukuru Foundation katika eneo la Lomami Luidjo, jimbo la Maniema zinaonyesha kuwa idadi ya ndege hao aina ya Psittacus erithacus imepungua kati ya mwaka 2016 na 2021. Hali hii inatia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/" data-wpel-link="internal">Hatimaye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imechukua hatua kuwalinda kasuku wa kijivu wa Afrika kutokana na biashara haramu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LUBUMBASHI, DRC — Idadi ya kasuku wa kijivu wa Afrika inaendelea kupungua maeneo ya katikati na kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.Takwimu zilizokusanywa wakati wa doria na Lukuru Foundation katika eneo la Lomami Luidjo, jimbo la Maniema zinaonyesha kuwa idadi ya ndege hao aina ya Psittacus erithacus imepungua kati ya mwaka 2016 na 2021. Hali hii inatia wasiwasi. Mwezi Agosti mwaka 2023, aliyekuwa waziri wa Mazingira wa nchi hiyo, JKK (DRC), Eve Bazaïba, alitia saini amri ya  kuwalinda aina ya ndege hao kwa namna yoyote ile. Kupungua kwa idadi ya ndege hao kunawiana na ongezeko la biashara ya ndege wanaotumika kama mapambo ya majumbani. Biashara hiyo imekuwa ikiongezeka kuanzia mwaka 2012 na ongezeko hili linasababishwa na udhaifu wa usimamizi na uangalizi wa biashara ya kimataifa na rushwa miongoni mwa maafisa ambao wanatakiwa kusimamia biashara hiyo chini ya mkataba wa CITES. Kasuku wa Kijivu waliokamatwa wakati wa operesheni ya kuzuia biashara ya kimataifa ya ndege hao, iliyoendeshwa mjini Lodja, JKK.(Picha: Adams Cassinga). Kasuku wa aina hii waliingizwa katika Kiambatanisho Namba 1 cha CITES (CITES Appendix I in 2016) na hii ilikuwa na maana kuwa mamlaka zilitakiwa kufanya usimamizi mkali wa biashara ya kimataifa ya ndege hao. Hata hivyo serikali ya Kongo ilipinga ndege hao kuingizwa kwenye Kiambatanisho hicho  kwa madai kwamba ndege hao hawakutishiwa uhai kiasi cha kuwekwa katika jedwali hilo, jambo ambalo liliungwa mkono za serikali ya Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao ndiyo walikuwa wanunuzi wakubwa wa ndege hao. Kwa sasa, serikali za Saudi Arabia na Umoja wa Falme&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufichuaji wa uharibifu wa misitu katika hifadhi ya sokwe baada ya mashambulizi ya M23 nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2025 14:21:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie TotoLatoya Abulu]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/12135717/Screenshot-2025-09-12-165630-768x473.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=401</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bonde la Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na  Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Maeneo yaliyolindwa, Migogoro, Misitu, Misitu ya Mvua, Miti, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Ukataji Miti ya Msitu wa Mvua, Upotevu wa Makazi, na  Visababishi vya Ukataji Misitu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miezi sita iliyopita, kundi la waasi la M23 liliuteka mji wa Goma, moja ya miji mikubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Baada ya muda huo, wanaharakati wa ndani, na Mongabay, ambayo ilikusanya picha za satelaiti, walitambua maeneo yenye upotevu mkubwa wa misitu katika Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, kusini magharibi mwa mji wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/" data-wpel-link="internal">Ufichuaji wa uharibifu wa misitu katika hifadhi ya sokwe baada ya mashambulizi ya M23 nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miezi sita iliyopita, kundi la waasi la M23 liliuteka mji wa Goma, moja ya miji mikubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Baada ya muda huo, wanaharakati wa ndani, na Mongabay, ambayo ilikusanya picha za satelaiti, walitambua maeneo yenye upotevu mkubwa wa misitu katika Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, kusini magharibi mwa mji wa Goma. Katika eneo hili kubwa la msitu wa msingi, ni nyumbani kwa sokwe wa nyanda za chini za mashariki (Gorilla beringei graueri). Watafiti wanahusisha ongezeko hili la upotevu wa misitu na upanuzi wa uzalishaji haramu wa mkaa, kuporomoka kwa utekelezaji wa uhifadhi, na migogoro ya ardhi. Mnamo Novemba mwaka 2021, kundi la waasi linaloungwa mkono na Rwanda liliibuka tena katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini DRC baada ya takriban muongo mmoja wa kutokuwepo katika eneo hilo. Matukio yaliongezeka mnamo Januari na Februari mwaka 2025, wakati waasi wa M23 walipoanzisha mashambulizi ya haraka na kutwaa udhibiti wa maeneo muhimu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini, ikiwa ni pamoja na miji mikuu ya majimbo husika, Goma na Bukavu. Maeneo haya yamesalia chini ya udhibiti wa waasi M23 hadi leo. Zaidi ya miji hii mikubwa, kundi lililojihami pia linadhibiti ufikiaji wa maeneo muhimu ya uchimbaji madini na maeneo muhimu yaliyolindwa kimataifa, kama vile Hifadhi ya Taifa ya Virunga na Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, Maeneo ya Urithi wa Dunia wa UNESCO. Hadi sasa, mzozo huo una athari inayoonekana kwa bioanuwai kwa kuzidisha changamoto zilizopo za uhifadhi na ukataji miti, watafiti wanasema. Katika Kahuzi-Biega, picha za satelaiti kutoka&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>