<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?location=afrika-ya-kati&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 07 Aug 2026 18:26:45 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.3</generator>
				<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>25 Juni 2026 23:31:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/25230559/Our-Ocean-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1930</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai wa Baharini, Dawa ya Asili, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kasa wa baharini, Maji, Maliasili, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Misitu ya Asili, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhisho za Asili, Tamaduni za Kiasili, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Baharini, Urejesho wa Asili, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira si rasilimali za kutumia tu, bali ni urithi wa kulindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo. Nchini Kenya, ukanda wa pwani wenye urefu wa takriban kilomita 640 ni kitovu cha uchumi wa buluu unaojumuisha uvuvi, utalii, usafiri wa baharini na biashara nyingine zinazotegemea bahari. Karibu watu milioni nne wanaishi katika eneo la pwani, huku maelfu ya wavuvi na makumi ya maelfu ya kaya wakitegemea rasilimali za bahari kwa riziki zao. Hali hiyo inaifanya uhifadhi wa bahari kuwa muhimu si tu kwa mazingira bali pia kwa ustawi wa uchumi wa taifa. Muranga, ambaye sasa ni mvuvi na pia mwenyekiti wa kikundi cha kijamii cha kulinda misitu cha Sokoke, ana jukumu la kuhakikisha kuwa anapitisha elimu hiyo kwa jamii, hasa kwa vizazi vichanga, ili ihifadhiwe kwa vizazi vijavyo. Mwonekano wa sehemu ya Bahari ya Hindi jijini Mombasa, huku mikoko ikionekana upande wa kushoto. Picha na Malavika Vyawahare, Mongabay. Mikoko ni misitu ya kipekee inayostawi katika maeneo ya maji ya chumvi kwenye fukwe za bahari za kanda za kitropiki. Misitu hii huunganisha nchi kavu na bahari, ikifanya kazi muhimu katika kulinda mazingira na ustawi wa jamii za pwani. “Zamani tulikuwa tukikalishwa na mababu zetu tukisimuliwa hadithi na kanuni za kijamii ambazo zilikuwa zinalinda&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/#respond</comments>
					<pubDate>19 Juni 2026 16:08:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/19153844/Screenshot-2026-06-19-182917-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1891</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bioanuai, Bioanuai ya Misitu ya Mvua, Bustani za wanyama, Chakula, Cites, Elimu, Elimu ya Mazingira, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Huduma za Mazingira, Idadi ya watu, Ikolojia, Jamii Asili, Jamii ya Nyani Wakubwa, Jamii za Misitu ya Mvua, Kijani, Makazi, na  Mamalia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, ulio katikati mwa DRC. Dhamira yao ni kuwashawishi bonobo (Pan paniscus) kukubali uwepo wa binadamu kama sehemu ya asili ya mazingira yao. Kwa kupata uaminifu wa wanyama, watafiti wanatumai kuunda fursa za kuelewa vyema tabia, ikolojia na afya zao. Mchakato huu wenye bidii wa kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu unahusisha kutumia wakati karibu na nyani siku baada ya siku hadi watakapozoea watu hatua kwa hatua. Ni kazi ya polepole na inayohitaji juhudi kubwa ambayo inaweza kuchukua miaka, inayohitaji uvumilivu, uthabiti na maelfu ya masaa msituni. Muda mrefu kabla ya mapambazuko, mara nyingi karibu saa 3 alfajiri, wafuatiliaji, baadhi yao wakiwa wawindaji haramu wa zamani, ambao ujuzi wao kuhusu msitu umekuwa rasilimali muhimu ya uhifadhi, wanaanza kuelekea kwenye eneo la viota usiku uliopita. Ni lazima wafike kabla kundi hilo la bonobo halijaamka. Kisha huanza harakati za kutwa nzima kupitia moja ya misitu ya mvua iliyo mbali zaidi Duniani, kufuatia nyani kutoka alfajiri hadi wajenge viota vipya kwa ajili ya usiku. &#8220;Wazo zima la kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu ni kukutana nao kila siku kwa njia ya kirafiki sana, isiyo ya mwingiliano ili wakukubali kama sehemu ya msitu,&#8221; anasema Felix Bofeko, mtafiti msaidizi anayefanya kazi na programu ya mazoea ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 13:12:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09111629/Screenshot-2026-06-09-141545.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia ya wenzao. Hata hivyo, licha ya jukumu lao kuu katika kulinda bayoanuwai na baadhi ya misitu muhimu zaidi ulimwenguni, wengi wanaendelea kufanya kazi wakiwa na usaidizi mdogo, mishahara midogo, na hali hatarishi sana. Kwa Emmanuel Bahati Lukoo, ukweli huu ni wa kibinafsi sana. Aliwahi kuwa mlinzi katika mbuga ya kitaifa ya Virunga ambapo kwa sasa ni afisa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Kahuzi-Biega, alinusurika kifo katika shambulizi la kushutukizia mnamo mwaka wa 2018 na kikundi cha wanamgambo wa jamii kinachojulikana kama Mai-Mai. Wenzake kadhaa waliuawa kwa kuviziwa. Alipigwa risasi, alijeruhiwa na kupata kiwewe cha kisaikolojia, na baadaye kufunguliwa mashitaka mbele ya mahakama ya kijeshi katika kesi iliyohusishwa na ulinzi wa hifadhi, angeweza kuondoka. Badala yake, Bahati alichagua kusimulia hadithi yake katika kitabu kiitwacho Conservation at the Cost of My Youth: The Survival of a Ranger, simulizi ghafi ya dhabihu, hofu, shinikizo za kisiasa, na mara nyingi hali halisi isiyoonekana inayowakabili walinzi wa misitu mashariki mwa DRC. Kwenye mahojiano ya ana kwa ana na Mongabay, Bahati anatafakari safari yake, shambulizi lililokaribia kumuua, kiwewe walichopata walinzi, migogoro kati ya uhifadhi na maisha ya jamii ya eneo hilo, na uingiliaji wa kisiasa unaotatiza ulinzi wa maeneo yaliyohifadhiwa. Zaidi ya hadithi ya kibinafsi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/#respond</comments>
					<pubDate>10 Mei 2026 21:34:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/08205611/Screenshot-2026-05-08-235542-768x500.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1539</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Kati, na  Kusini mwa Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Biashara ya Wanyamapori ya China, Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mamalia, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu kwa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utafiti, Utawala, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Facebook imegeuka kuwa kitovu cha biashara haramu ya wanyamapori kutokana na muundo wake, ripoti yasema</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa kubonyeza tu kitufe au kutelezesha vidole kwenye simu, unaweza kununua karibu chochote mtandaoni, ikiwemo wanyama adimu au walio hatarini. Kuanzia nyara za kipekee za papa hadi ndege hai wa kigeni, pembe za faru au pembe za ndovu, wanunuzi wanaweza kwenda kwenye majukwaa ya biashara ya mtandaoni na kuzipata zote. Wasafirishaji hujificha nyuma ya skrini zao huku wakinufaika kutokana na mauzo ya mtandaoni ya spishi za wanyama wanaolindwa huku wanyama hawa wakipungua porini. &#8220;Ni soko kubwa zaidi la wanyamapori,&#8221; alisema mtafiti wa biashara ya wanyamapori Chris Shepherd kutoka Kituo cha Biolojia Anuwai. &#8220;Ni rahisi, unaweza kufanya kazi bila kujulikana ukiwa nyumbani kwako. Hakuna gharama za kuanzisha duka.&#8221; Biashara ya mtandaoni katika bidhaa haramu za wanyamapori inaendelea kukua, ikihusisha spishi zaidi na jiografia pana. Ni tasnia haramu inayoendeshwa na mitandao ya uhalifu iliyopangwa vizuri, na ni vigumu kushtaki. Kukamata wahalifu mtandaoni ni changamoto sana. &#8220;Masoko ya wanyamapori yamehamia kutoka maeneo halisi hadi maeneo ya mitandaoni, na hiyo inaakisi mwelekeo mpana zaidi wa uchumi wa dunia,&#8221; alisema Simone Haysom, mkurugenzi wa programu za uhalifu wa kimazingira katika shirika lenye makao yake makuu Uswizi la Global Initiative Against Transnational Organised Crime. Katika ripoti ya hivi karibuni, Haysom na mwenzake Russell Gray walichanganua data ya biashara ya wanyamapori mtandaoni kuanzia mwezi wa Aprili 2024 hadi mwezi Machi 2026. Waliangazia mataifa 10 katika mabara matatu, mahali ambapo uhalifu wa kimazingira na matumizi ya intaneti ni mkubwa, na kuyafanya kuwa mazingira yanayochochea biashara ya wanyamapori mtandaoni. Walipata bidhaa 266,535 za wanyamapori zilizochapishwa kwenye masoko 61 ya mitandaoni, yenye thamani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/10/facebook-ni-kitovu-cha-biashara-haramu-ya-wanyamapori-kutokana-na-muundo-wake-ripoti-inasema/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>GLF: Nyanda za malisho na wafugaji ni raslimali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na si tatizo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/#respond</comments>
					<pubDate>08 Mei 2026 20:33:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/10203241/A-participant-asks-questions-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1530</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Kusini mwa Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Fedha za Uhifadhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Jinsia na Uhifadhi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Teknolojia na Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Baada ya mkutano wa siku mbili wa kujadili huduma za mifumo ya ikolojia ya nyanda za malisho na jamii za wafugaji wa kuhamahama, Mkutano wa nane wa jukwaa la Global Landscapes Forum umehitimishwa jijini Nairobi kwa tamko lililosisitiza umuhimu wa jamii ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikionekana kama kikwazo kwa maendeleo. Katika mkutano huo uliofanyika katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/" data-wpel-link="internal">GLF: Nyanda za malisho na wafugaji ni raslimali katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, na si tatizo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Baada ya mkutano wa siku mbili wa kujadili huduma za mifumo ya ikolojia ya nyanda za malisho na jamii za wafugaji wa kuhamahama, Mkutano wa nane wa jukwaa la Global Landscapes Forum umehitimishwa jijini Nairobi kwa tamko lililosisitiza umuhimu wa jamii ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikionekana kama kikwazo kwa maendeleo. Katika mkutano huo uliofanyika katika kituo cha CIFOR-ICRAF na kuhudhuriwa na maafisa wa serikali, wanasayansi pamoja na wawakilishi wa jamii za asili kutoka nchi 135, mjadala ulijikita katika mifumo ya ikolojia inayosaidia bioanuwai, usalama wa chakula, maisha ya watu, utamaduni, uhifadhi wa kaboni na huduma nyingine za kiikolojia bila kuvuruga maisha endelevu na tamaduni za jamii za wafugaji, badala ya kuweka msisitizo kwenye uwekezaji unaoshinikizwa na serikali kwa lengo la kupata faida. “Tunapaswa kujiuliza: Maendeleo haya yanafanywa kwa ajili ya nani? Je, jamii zinahusishwa katika maamuzi kuhusu uwekezaji unaofanywa kwenye ardhi yao? Na ni kwa manufaa ya nani miradi hii ya kibiashara inayowasilishwa kana kwamba ni juhudi za kutoa ajira na fursa nyingine kwa wakazi? Sauti zao zina umuhimu,” alisema Tahira Mohamed Shariff kutoka Jameel Observatory for Food Security Early Action siku ya kwanza ya mkutano huo. Baadhi ya waliohudhuria kongamano Nairobi, Kenya. Picha na GLF. Monicah Yator, Wakili na Mwanzilishi wa Indigenous Women and Girls Initiative, alisema kuwa ufugaji wa kuhamahama si shughuli ya mifugo pekee. “Ni mfumo wa maisha, chakula na utamaduni. Kuna sera zinazowalinda wafugaji. Sasa wafugaji wanafahamu kwamba ardhi yao inaweza kubadilishiwa matumizi,” alisema, akiongeza kuwa maarifa ya asili bado ni muhimu na yenye mchango mkubwa katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/08/nyanda-za-malisho-na-wafugaji-ni-raslimali-katika-kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-na-si-tatizo-mkutano-wa-kimataifa-watangaza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>05 Mei 2026 22:27:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David AkanaRhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/05212300/Screenshot-2026-05-06-000526-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1504</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na  Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maendeleo Endelevu, Mamalia, Mazingira, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Mvua, Uhifadhi, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, volkeno, misitu, na ardhi oevu ndani ya eneo moja lililohifadhiwa. Pia ipo ndani ya mazingira iliyoundwa kwa miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu, ambapo makundi yaliojihami kwa silaha, uchumi usio rasmi, na utawala dhaifu ni sehemu ya maisha ya kila siku. Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga. Picha kwa hisani ya Bitini Ndiyanabo Kanane. Emmanuel de Merode, ambaye ameiongoza Virunga tangu mwaka wa 2008, haanzii na ikolojia. Mafunzo yake ni ya anthropolojia, hali inayounda namna anavyoelezea hifadhi. Anapendekeza kuwa hali ya wanyamapori hutokana na nguvu za kina. Upotevu wa misitu, ujangili, na ukosefu wa usalama sio shida za mazingira pekee. Yanatokana na namna watu wanavyopata riziki, namna mamlaka inavyofanya kazi, na jinsi pesa na rasilimali zinavyozunguka. Katika sehemu ya Mashariki mwa Kongo, uhifadhi hauwezi kutenganishwa na uchumi. Kwa jamii nyingi zinazoizunguka Virunga, chaguo lao ni la haraka. Kuifyeka misitu kwa ajili ya ukulima au kutengeza mkaa kunaweza kuzalisha kipato cha kuendesha maisha. Faida za uhifadhi ni ngumu kuonekana na mara nyingi huonekana zaidi nje ya eneo hilo. Ukosefu wa usawa unajitokeza katika maamuzi ya kila siku kuhusu mafuta, chakula na upatikanaji wa ardhi. Kama De Merode anavyoelezea, mfumo unawalazimisha baadhi ya watu maskini zaidi kubeba gharama ya kulinda mali zinazothaminiwa kimataifa. Shinikizo kwenye mbuga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kasuku wa Kiafrika waliookolewa warudishwa katika misitu ya DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/#respond</comments>
					<pubDate>21 Oktoba 2025 12:30:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Didier Makal]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/03123238/Screenshot-2025-11-03-152749-768x474.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=714</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Ndege, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Sheria ya Mazingira, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LUBUMBASHI, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo &#8211; kasuku 50 wa Kiafrika wa kijivu wameachiliwa na kurejea porini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia kuokolewa kutoka kwa biashara haramu ya wanyamapori. Kuachiliwa kwao, katika mkoa wa kati wa Maniema mwezi huu wa Oktoba, kulikuja baada ya mwaka mmoja kurekebiswa katika hifadhi inayoendeshwa na Wakfu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/" data-wpel-link="internal">Kasuku wa Kiafrika waliookolewa warudishwa katika misitu ya DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LUBUMBASHI, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo &#8211; kasuku 50 wa Kiafrika wa kijivu wameachiliwa na kurejea porini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia kuokolewa kutoka kwa biashara haramu ya wanyamapori. Kuachiliwa kwao, katika mkoa wa kati wa Maniema mwezi huu wa Oktoba, kulikuja baada ya mwaka mmoja kurekebiswa katika hifadhi inayoendeshwa na Wakfu wa Lukuru wenye makao yake nchini humo, ambao umewatunza na kuwaachilia karibu kasuku 400 waliopatikana kutoka kwa wafanyabiashara haramu. Wakati utekelezaji wa amri mpya iliyochapishwa na wizara ya mazingira ya DRC inapoanza, vituo vya urekebishaji wa taasisi hiyo vinatarajia kazi nyingi zaidi za kufanya. Mnamo Julai 31, 2025, DRC ilichapisha amri inayokataza kukamata, kumiliki au kufanya biashara ya kasuku wa Kiafrika wa kijivu (Psittacus erithacus). Marufuku hiyo ilitanguliwa na hatua kama hiyo iliyopitishwa awali na mamlaka katika mkoa wa Tshopo, kaskazini mwa DRC, ambao mji mkuu wake, Kisangani, unatumika kama kitovu kikuu cha biashara ya kasuku. Lakini mwezi mmoja baadaye, kasuku waliokamatwa bado walikuwepo katika jamii za Ngungwa na Kimwachi huko Maniema, kulingana na Corneille Kalume, meneja wa taasisi isiokuwa ya  kiserikali ya Action for Environmental Management (Action Communautaire pour la Gestion de l’Environnement) yenye makao yake makuu Kindu, mji mkuu wa mkoa. &#8220;Wawindaji haramu bado wanawawinda na kuwakamata kasuku,&#8221; Kalume aliiambia Mongabay kwa njia ya simu. &#8220;Ni vizuri kuwa na agizo la mawaziri la kupiga marufuku ujangili, lakini kuna haja ya kuchukuliwa hatua za kuzuia watu kuwatega ndege.&#8221; Kasuku wa kijivu walinaswa katika operesheni ya kupambana na biashara haramu ya binadamu huko Lodja, DRC. Picha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mjini Kivu nchini DRC, Moringa unatoa manufaa muhimu kiafya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/#respond</comments>
					<pubDate>09 Oktoba 2025 19:27:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Blaise Kasereka Makuta]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/03193952/Screenshot-2025-11-03-223837-768x473.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=725</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Ikolojia, Kilimo, Kilimo-ikolojia, Maarifa ya Jadi, Mazingira, Mimea, Mimea yenye Tiba, Misitu, Miti, Sheria ya Mazingira, Ufugaji, Ufugaji wa Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Moringa, mti ambao mara nyingi huhusishwa na eneo lake la asili la taifa la India, pia ni mmea wenye thamani unaopatikana maelfu ya maili kutoka eneo la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ndani ya nchi, mti wa Moringa huchukua jukumu muhimu la utengenezaji wa dawa za jadi, za jadi-kileo (mchanganyiko wa dawa za [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/" data-wpel-link="internal">Mjini Kivu nchini DRC, Moringa unatoa manufaa muhimu kiafya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Moringa, mti ambao mara nyingi huhusishwa na eneo lake la asili la taifa la India, pia ni mmea wenye thamani unaopatikana maelfu ya maili kutoka eneo la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ndani ya nchi, mti wa Moringa huchukua jukumu muhimu la utengenezaji wa dawa za jadi, za jadi-kileo (mchanganyiko wa dawa za zamani na mpya) na za kisasa. Kulingana na watabibu na wagonjwa kadhaa wa kienyeji, kutokana na sifa zake za matibabu, moringa unaweza kutumika kutibu magonjwa mbalimbali kama vile kisukari, maumivu ya misuli, udhaifu wa kijinsia na mengine mengi. &#8220;Kando na sifa zake za dawa, moringa una faida nyingi; ni mti wa asili unaorutubisha,&#8221; Jackeline Muderwa, mwanamke mwenye umri wa miaka 69 na mtabibu kutoka mtaa wa Mugunga huko Goma, alielezea katika mahojiano na Mongabay. Anaihusisha na kipindi cha ukoloni wa Ubelgiji karibu katikati ya karne ya 20. &#8220;Wabelgiji waliipanda miti ya moringa kwenye bustani zao na kuitumia kutibu magonjwa yao fulani. Naamini hapo ndipo tulipofahamu manufaa yake. Mara nyingi hata msituni, uwepo wake ulidhihirisha uwepo wa babu wa mtu mahali hapo ambaye huenda alihama.&#8221; Moringa, kwa jina la kibayolojia Moringa oleifera, ni mti unaokua kwa haraka wa familia ya Moringaceae; jina la kibayolojia. Ingawa umeainishwa kimataifa kama spishi isiyojali sana kwenye Orodha Nyekundu ya shirika la IUCN, mti huu unahitaji uangalizi maalum. Hulimwa hasa katika maeneo ya nusu-kame, kitropiki na maeneo ya nusu-tropiki. (Kushoto) Spishi ya Moringa, kwa jina la kibayolojia Moringa oleifera, ni spishi ya miti asili wa India lakini pia inatumika DRC kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, tunaitambuaje bayoanuwai? Tunaweza kuiona na kuisikia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/09/04/je-tunaitambuaje-bayoanuwai-tunaweza-kuiona-na-kuisikia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/09/04/je-tunaitambuaje-bayoanuwai-tunaweza-kuiona-na-kuisikia/#respond</comments>
					<pubDate>04 Septemba 2025 12:30:10 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Blaise Kasereka Makuta]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/03123446/Screenshot-2025-10-03-153401-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=601</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Jamii Asili, Mazingira, Misitu, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utafiti, Wanyamapori, Watu wa Jadi, na  Wenza]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika kina kirefu na chenye kupendeza cha mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo sauti za ndege zilizoambatana na msukosuko wa majani, watu kadhaa wa jamii za asili wanathibitisha matokeo ya utafiti uliochapishwa mwezi Julai. Wanasayansi wa bayoanuwai, waliovutiwa na jinsi binadamu wanavyotambua mazingira ya asili, walianzisha utafiti wenye kichwa cha habari; &#8220;Bayoanuwai inayoonekana: [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/04/je-tunaitambuaje-bayoanuwai-tunaweza-kuiona-na-kuisikia/" data-wpel-link="internal">Je, tunaitambuaje bayoanuwai? Tunaweza kuiona na kuisikia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika kina kirefu na chenye kupendeza cha mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo sauti za ndege zilizoambatana na msukosuko wa majani, watu kadhaa wa jamii za asili wanathibitisha matokeo ya utafiti uliochapishwa mwezi Julai. Wanasayansi wa bayoanuwai, waliovutiwa na jinsi binadamu wanavyotambua mazingira ya asili, walianzisha utafiti wenye kichwa cha habari; &#8220;Bayoanuwai inayoonekana: Je, kile tunachokipima ndicho tunachokiona na kukisikia?&#8221; Wazo lililokuwa nyuma ya utafiti huo lilikuwa rahisi: Katika awamu ya kwanza, washiriki waliombwa kusikiliza sauti zilizorekodiwa msituni kutoka maeneo yenye viwango tofauti vya bayoanuwai. Katika awamu nyingine, washiriki walionyeshwa picha za mazingira ya asili. Lengo ? Ili kujua kile ambacho watu hutambua pale wanapoona au kusikia viwango tofauti vya bayoanuwai, na ni kwa kiwango gani bayoanuwai halisi inalingana na ile inayotambulika na binadamu. Inavutia, siyo? Ili kulifumbua fumbo hili, watafiti walichunguza washiriki 48 katika kila kikundi ambao walionyeshwa alama za kuona (picha 57 zilizopigwa kwenye misitu yenye viwango tofauti vya bayoanuwai) au vidokezo vya sauti (rekodi 16 za sekunde 10 kila moja kutoka katika mazingira ya asili), kisha wakatakiwa kuainisha picha na sauti kulingana na kiwango cha bayoanuwai waliyoitambua. Kevin Rozario, mmoja wa waandishi wa utafiti huo, katika ujumbe wa sauti kwa Mongabay, alieleza hivi; “Tuliwaambia tu, ‘Tazama picha hizi, sikilizeni sauti hizi. Tuambieni mnaona nini na mnasikia nini’ Na wao wakaanza kulinganisha kwa uhuru, wakitumia kumbukumbu na uzoefu wao binafsi.” Msitu katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Wanajamii wanaoishi karibu na Virunga wanasema wanaweza kutambua habari kuhusu wanyama, muda , hali ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/04/je-tunaitambuaje-bayoanuwai-tunaweza-kuiona-na-kuisikia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/09/04/je-tunaitambuaje-bayoanuwai-tunaweza-kuiona-na-kuisikia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatimaye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imechukua hatua kuwalinda kasuku wa kijivu wa Afrika kutokana na biashara haramu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/#respond</comments>
					<pubDate>02 Septemba 2025 11:37:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dider Makal]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/01113941/Screenshot-2025-10-01-143917-768x470.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=575</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, na  Afrika ya Kati]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya Wanyamapori, Cites, Ikolojia, Kijani, Misitu, Ndege, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LUBUMBASHI, DRC — Idadi ya kasuku wa kijivu wa Afrika inaendelea kupungua maeneo ya katikati na kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.Takwimu zilizokusanywa wakati wa doria na Lukuru Foundation katika eneo la Lomami Luidjo, jimbo la Maniema zinaonyesha kuwa idadi ya ndege hao aina ya Psittacus erithacus imepungua kati ya mwaka 2016 na 2021. Hali hii inatia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/" data-wpel-link="internal">Hatimaye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo imechukua hatua kuwalinda kasuku wa kijivu wa Afrika kutokana na biashara haramu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LUBUMBASHI, DRC — Idadi ya kasuku wa kijivu wa Afrika inaendelea kupungua maeneo ya katikati na kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo.Takwimu zilizokusanywa wakati wa doria na Lukuru Foundation katika eneo la Lomami Luidjo, jimbo la Maniema zinaonyesha kuwa idadi ya ndege hao aina ya Psittacus erithacus imepungua kati ya mwaka 2016 na 2021. Hali hii inatia wasiwasi. Mwezi Agosti mwaka 2023, aliyekuwa waziri wa Mazingira wa nchi hiyo, JKK (DRC), Eve Bazaïba, alitia saini amri ya  kuwalinda aina ya ndege hao kwa namna yoyote ile. Kupungua kwa idadi ya ndege hao kunawiana na ongezeko la biashara ya ndege wanaotumika kama mapambo ya majumbani. Biashara hiyo imekuwa ikiongezeka kuanzia mwaka 2012 na ongezeko hili linasababishwa na udhaifu wa usimamizi na uangalizi wa biashara ya kimataifa na rushwa miongoni mwa maafisa ambao wanatakiwa kusimamia biashara hiyo chini ya mkataba wa CITES. Kasuku wa Kijivu waliokamatwa wakati wa operesheni ya kuzuia biashara ya kimataifa ya ndege hao, iliyoendeshwa mjini Lodja, JKK.(Picha: Adams Cassinga). Kasuku wa aina hii waliingizwa katika Kiambatanisho Namba 1 cha CITES (CITES Appendix I in 2016) na hii ilikuwa na maana kuwa mamlaka zilitakiwa kufanya usimamizi mkali wa biashara ya kimataifa ya ndege hao. Hata hivyo serikali ya Kongo ilipinga ndege hao kuingizwa kwenye Kiambatanisho hicho  kwa madai kwamba ndege hao hawakutishiwa uhai kiasi cha kuwekwa katika jedwali hilo, jambo ambalo liliungwa mkono za serikali ya Saudi Arabia na Umoja wa Falme za Kiarabu ambao ndiyo walikuwa wanunuzi wakubwa wa ndege hao. Kwa sasa, serikali za Saudi Arabia na Umoja wa Falme&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/09/02/hatimaye-jamhuri-ya-kidemokrasi-ya-kongo-imechukua-hatua-kuwalinda-kasuku-wa-kijivu-wa-afrika-kutokana-na-biashara-haramu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>