<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=hifadhi&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/hifadhi/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sun, 20 Sep 2026 18:30:08 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.5</generator>
				<item>
					<title>Tanzania inawezaje kuendelea kunufaika na mimea ya dawa huku ikilinda spishi zilizo hatarini kutoweka?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/09/05/tanzania-inawezaje-kuendelea-kunufaika-na-mimea-ya-dawa-huku-ikilinda-spishi-zilizo-hatarini-kutoweka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/09/05/tanzania-inawezaje-kuendelea-kunufaika-na-mimea-ya-dawa-huku-ikilinda-spishi-zilizo-hatarini-kutoweka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Septemba 2026 00:00:40 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hillary Mrosso]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/09/04131104/1-mimeadawa-1-737x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2746</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Dawa ya Asili, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Ikolojia, Kuokoa Misitu, Kupambana na ujangili, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Matumizi kupita Kiasi, Mifumo ya Ikolojia, Mimea yenye Tiba, Misitu, Misitu ya Asili, Miti, Uokoaji wa Misitu, na  Uwindaji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumizi ya mimea na miti kama dawa yanaendelea kuongezeka kwa kasi, hali inayotishia uhai wa baadhi ya spishi, bioanuwai na afya ya misitu. Hali hii inazua swali muhimu: Je, jamii  nchini Tanzania zinawezaje kuendelea kunufaika na mimea ya dawa huku spishi zilizo hatarini na misitu vikiendelea kulindwa? Matumizi ya mimea dawa: Hali halisi Taarifa zilizopo zinaonyesha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/05/tanzania-inawezaje-kuendelea-kunufaika-na-mimea-ya-dawa-huku-ikilinda-spishi-zilizo-hatarini-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Tanzania inawezaje kuendelea kunufaika na mimea ya dawa huku ikilinda spishi zilizo hatarini kutoweka?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumizi ya mimea na miti kama dawa yanaendelea kuongezeka kwa kasi, hali inayotishia uhai wa baadhi ya spishi, bioanuwai na afya ya misitu. Hali hii inazua swali muhimu: Je, jamii  nchini Tanzania zinawezaje kuendelea kunufaika na mimea ya dawa huku spishi zilizo hatarini na misitu vikiendelea kulindwa? Matumizi ya mimea dawa: Hali halisi Taarifa zilizopo zinaonyesha nchi nyingi duniani sasa zinatumia  mimea kama dawa. Kwa mfano, Ripoti ya mwaka 2019 ya Shirika la Afya Duniani, (WHO) kuhusu mimea na tiba asili ilionyesha kuwa nchi wanachama (nchi ambazo WHO inafanya kazi) 170 kati ya 194, sawa na asilimia 88, zilikuwa zinatumia mimea kutibu maradhi mbalimbali. Aina mbalimbali za mimea ya dawa iliyovunwa kutoka kwenye mimea asilia ikiwa imewekwa tayari kwa kuuzwa kwenye maduka ya dawa asilia katika maeneo ya Morogoro mjini: Picha na Hillary Mrosso. Barani Afrika, ambapo kuna upatikanaji wa mimea na misitu mingi asilia, hali ya matumizi ya mimea dawa ni kubwa zaidi. Kwa mujibu wa ripoti ya Kanda ya Afrika ya Shirika la Afya Duniani (WHO) ya mwaka 2010 kuhusu matumizi ya dawa asili barani Afrika, kati ya asilimia 70 hadi 80 ya Waafrika wanategemea mimea kwa ajili ya afya zao. Nchini Tanzania, Chapisho la WHO linaonyesha kuwa kati ya asilimia 60 hadi 80 ya wananchi wanatumia mimea dawa kutibu magonjwa mbalimbali ya binadamu na wanyama wa kufugwa. Kwa mujibu wa chapisho hilo, matumizi hayo yanakwenda sambamba na uwepo wa mtandao mpana wa waganga wa jadi, wanaokadiriwa kufikia 75,000 ambao kwa kiasi kikubwa hutegemea mimea hiyo kama chanzo cha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/05/tanzania-inawezaje-kuendelea-kunufaika-na-mimea-ya-dawa-huku-ikilinda-spishi-zilizo-hatarini-kutoweka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/09/05/tanzania-inawezaje-kuendelea-kunufaika-na-mimea-ya-dawa-huku-ikilinda-spishi-zilizo-hatarini-kutoweka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Walioomba amri ya mahakama kupinga tamko la Rais kuhusu Hifadhi ya Ruaha wakwama</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/09/03/walioomba-amri-ya-mahakama-kupinga-tamko-la-rais-kuhusu-hifadhi-ya-ruaha-wakwama/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/09/03/walioomba-amri-ya-mahakama-kupinga-tamko-la-rais-kuhusu-hifadhi-ya-ruaha-wakwama/#respond</comments>
					<pubDate>03 Septemba 2026 07:34:35 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/09/02181502/Hifadhi-ya-Ruaha.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2707</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Serikali, na  Sheria]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mbeya, imesema ombi la kisheria lililowasilishwa baada ya muda uliowekwa na sheria linapaswa kutupiliwa mbali (dismissed) na siyo kufutwa (struck out), hata kama shauri hilo linahusu masuala ya maslahi ya umma. Uamuzi huo ulitolewa katika Rufaa ya Madai Na.105 ya 2024, kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/03/walioomba-amri-ya-mahakama-kupinga-tamko-la-rais-kuhusu-hifadhi-ya-ruaha-wakwama/" data-wpel-link="internal">Walioomba amri ya mahakama kupinga tamko la Rais kuhusu Hifadhi ya Ruaha wakwama</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Rufani ya Tanzania Mbeya, imesema ombi la kisheria lililowasilishwa baada ya muda uliowekwa na sheria linapaswa kutupiliwa mbali (dismissed) na siyo kufutwa (struck out), hata kama shauri hilo linahusu masuala ya maslahi ya umma. Uamuzi huo ulitolewa katika Rufaa ya Madai Na.105 ya 2024, kati ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dhidi ya Mathia Mligo na wenzake watatu waliotaka ruhusa ya kuomba amri za kimahakama kupinga tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la Oktoba 20, 2023 kuhusu marekebisho ya mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha, maarufu kama “Tamko la Kurekebisha Mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha 2023.” Jopo la majaji watatu wa Mahakama hiyo, Jaji Gerald Ndika, Benhaji Masoud na Yose Mlyambina baada ya kusikiliza rufani walikubaliana kuwa Mahakama Kuu ilikosea kisheria kwa kufuta ombi badala ya kulitupilia mbali baada ya kubaini kuwa liliwasilishwa nje ya muda uliowekwa. Shauri hilo lilitokana na ombi lililowasilishwa Mahakama Kuu Aprili 9, 2024, likilenga kupata ruhusa ya kuomba amri za kimahakama kupinga tamko la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania la Oktoba 20, 2023 kuhusu marekebisho ya mipaka ya Hifadhi ya Taifa ya Ruaha. Rekodi ya shauri ilionyesha kuwa Mei 23, 2024, wakili wa walalamikaji, Jebra Kambole aliomba kuondoa ombi hilo baada ya kubaini kuwa maombi ya judicial review yalipaswa kushughulikiwa ndani ya siku 14 tangu kuwasilishwa na muda huo ulikuwa umepita. Wanyama kama hawa ni kivutio kikubwa kwenye hifadhi za wanyama. Picha kwa hisani ya Tanapa Ruaha National Park. Mahakama&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/03/walioomba-amri-ya-mahakama-kupinga-tamko-la-rais-kuhusu-hifadhi-ya-ruaha-wakwama/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/09/03/walioomba-amri-ya-mahakama-kupinga-tamko-la-rais-kuhusu-hifadhi-ya-ruaha-wakwama/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ngorongoro na mustakabali wa Wamasai: Kiongozi wa jamii ya Wamaasai Tanzania avunja ukimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/09/02/ngorongoro-na-mustakabali-wa-wamasai-kiongozi-wa-jamii-ya-wamaasai-tanzania-avunja-ukimya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/09/02/ngorongoro-na-mustakabali-wa-wamasai-kiongozi-wa-jamii-ya-wamaasai-tanzania-avunja-ukimya/#respond</comments>
					<pubDate>02 Septemba 2026 09:16:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Manyerere Jackton]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/09/02071800/p2-_31I4857-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2690</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi, Ikolojia, Maarifa ya Jadi, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Maliasili, Malisho ya Ng'ombe, Mashujaa wa Mazingira, Matumizi kupita Kiasi, Mazingira, Mifugo, Serikali, Uendelevu, Uhifadhi, na  Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni vigumu kuzungumzia uhifadhi katika maeneo ya Ngorongoro bila kugusia mvutano wa muda mrefu unaohusu uwiano kati ya uhifadhi wa mazingira na wanyamapori, shughuli za utalii, pamoja na haki na maisha ya jamii zinazooishi katika eneo hilo, hususan jamii ya Wamaasai. Uwiano kati ya uhifadhi na haki za jamii Msingi wa mvutano huo ni namna [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/02/ngorongoro-na-mustakabali-wa-wamasai-kiongozi-wa-jamii-ya-wamaasai-tanzania-avunja-ukimya/" data-wpel-link="internal">Ngorongoro na mustakabali wa Wamasai: Kiongozi wa jamii ya Wamaasai Tanzania avunja ukimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni vigumu kuzungumzia uhifadhi katika maeneo ya Ngorongoro bila kugusia mvutano wa muda mrefu unaohusu uwiano kati ya uhifadhi wa mazingira na wanyamapori, shughuli za utalii, pamoja na haki na maisha ya jamii zinazooishi katika eneo hilo, hususan jamii ya Wamaasai. Uwiano kati ya uhifadhi na haki za jamii Msingi wa mvutano huo ni namna ya kusawazisha mahitaji ya uhifadhi na haki za jamii kuendelea kuishi na kunufaika na ardhi ambayo imekuwa sehemu ya maisha yao kwa muda mrefu. Serikali kwa upande wake inataka baadhi ya wakazi wahame kutoka eneo la hifadhi kwenda maeneo yaliyotengwa kama Msomera, ikieleza kuwa ongezeko la watu na mifugo limeongeza shinikizo kwa ardhi, malisho, mazingira na uhifadhi wa wanyamapori. Mwenyekiti wa Jamii ya Wamaasai, Alaigwanani ole Kisongo akihutubia Baraza la Mila la Maarya jijini Arusha. Picha na Lekoko Lepilal. Kwa upande wa jamii zinazoishi eneo hilo, baadhi wanapinga kuondoka wakidai kuwa Ngorongoro ni ardhi yao ya asili, ambako wameishi na kuendesha shughuli za ufugaji kwa vizazi, huku maeneo hayo yakiwa na umuhimu wa kiutamaduni na kiimani.Mjadala ulichukua sura mpya mwaka 2022 wakati Serikali ilipoanza kutekeleza mpango wa kuwahamisha kwa hiari baadhi ya wakazi kutoka eneo la Ngorongoro kwenda maeneo mengine, ikieleza kuwa ongezeko la watu na mifugo lilikuwa linaongeza shinikizo kwenye ardhi na rasilimali za hifadhi. Hata hivyo, zoezi hilo lilikumbwa na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wakazi na wadau, waliodai kuwa uhamaji huo haukuwa wa hiari na kwamba wananchi hawakushirikishwa ipasavyo katika zoezi hilo. Tume za rais Kutokana na mvutano huo, Rais Samia Suluhu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/09/02/ngorongoro-na-mustakabali-wa-wamasai-kiongozi-wa-jamii-ya-wamaasai-tanzania-avunja-ukimya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/09/02/ngorongoro-na-mustakabali-wa-wamasai-kiongozi-wa-jamii-ya-wamaasai-tanzania-avunja-ukimya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Waliofungwa miaka 20 kwa kukutwa na nyama ya kiboko washinda rufani, waachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/13/waliofungwa-miaka-20-kwa-kukutwa-na-nyama-ya-kiboko-washinda-rufani-waachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/13/waliofungwa-miaka-20-kwa-kukutwa-na-nyama-ya-kiboko-washinda-rufani-waachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>13 Agosti 2026 17:45:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/13162200/1kibokoPicture3.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2458</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi na .Hifadhi za Taifa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Watu wanne, Jastine Balali na wenzake watatu waliotiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali lakini wakapinga hukumu hiyo kwa kukata rufaa, wameshinda rufani baada ya Mahakama kukubali hoja zao kwamba kulikuwa na mapungufu makubwa kwenye mnyororo wa utunzaji vielelezo na walifikishwa mahakamani zaidi ya mwaka mmoja tangu walipokamatwa. Washitakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na makosa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/13/waliofungwa-miaka-20-kwa-kukutwa-na-nyama-ya-kiboko-washinda-rufani-waachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Waliofungwa miaka 20 kwa kukutwa na nyama ya kiboko washinda rufani, waachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Watu wanne, Jastine Balali na wenzake watatu waliotiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali lakini wakapinga hukumu hiyo kwa kukata rufaa, wameshinda rufani baada ya Mahakama kukubali hoja zao kwamba kulikuwa na mapungufu makubwa kwenye mnyororo wa utunzaji vielelezo na walifikishwa mahakamani zaidi ya mwaka mmoja tangu walipokamatwa. Washitakiwa hao walikuwa wanakabiliwa na makosa mawili; kumiliki kinyume cha sheria nyara za Serikali, likihusisha vipande 450 vya nyama ya kiboko vilivyodaiwa kuwa na thamani ya Dola za Marekani 1,500 pamoja na kumiliki silaha ndani ya hifadhi bila kibali. Hukumu hiyo ilitolewa na Mahakama Kuu ya Tanzania Kanda ya Morogoro mbele ya Jaji Aisha Sinda baada ya kusikiliza rufani iliyotokana na kesi ya Uhujumu Uchumi namba 31.2022 iliyokuwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kilombero, Ifakara. Licha ya Balali, warufani wengine ni Mohammed Mekuso, John Nyange na Gabriel Emmanuel na wajibu rufani ni Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa mujibu wa ushahidi wa upande wa mashtaka, tukio hilo lilitokea Juni 21, 2021, katika eneo la Mpanga, ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nyerere, Wilaya ya Kilombero. Mahakama ilielezwa kuwa askari wa uhifadhi walipokuwa wakifanya kazi ya kuweka mipaka kati ya vijiji na hifadhi walikutana na watu sita waliokuwa wakivuta baiskeli ya kubeba mizigo. Kiboko jike baada ya kuuawa kufuatia kuvamia maeneo ya wananchi na kutishia usalama wao. Picha kutoka kwenye blogu ya Tangajamii. Watu hao walikamatwa na baada ya kupekuliwa, inadaiwa walikutwa na nyama ya kiboko pamoja na visu viwili vya porini, mshale mmoja pamoja na baiskeli tatu. Utetezi wa washitakiwa Washitakiwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/13/waliofungwa-miaka-20-kwa-kukutwa-na-nyama-ya-kiboko-washinda-rufani-waachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/13/waliofungwa-miaka-20-kwa-kukutwa-na-nyama-ya-kiboko-washinda-rufani-waachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>11 Agosti 2026 20:01:52 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/11191616/Main-Mnyama-Nguva-akiwa-baharini-Picha-na-Mtandao-wa-Jamii-Forums-Tanzania.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2426</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Ikolojia, Jinsia na Uhifadhi, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia wa Baharini, Mamalia Wakubwa, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tabia za Wanyama, Teknolojia na Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Ustawi wa Wanyama, Uzuri wa Kiikolojia, Wanawake katika Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Nguva wanakaribia kutoweka Kenya, jamii za pwani zapambana kuwarejesha kwa kupanda nyasi bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya – Zaidi ya miaka 20 imepita tangu Amiri Juma, mvuvi kutoka Kibuyuni, Kaunti ya Kwale, alipomwona nguva (Dugong dugon) katika eneo la Mipwa, kijiji jirani cha Wasini. Hii leo, akiwa na umri wa miaka 63, Juma bado anakumbuka vizuri siku ambayo wavuvi walimnasa mnyama huyo anayejulikana kama ng&#8217;ombe wa baharini na kumchinja. &#8220;Namjua nguva; aliwahi kushikwa na jarife. Aliyemshika wakati huo sasa ni marehemu. Siku hiyo watu walipika na kuila nyama yake. Mimi sikuweza kuila kwa sababu niliposhika nyama yake, mwili wangu ulianza kuwasha,” alisema Juma. Amiri Juma, mvuvi kutoka kijiji cha Kibuyuni Kaunti ya Kwale akiwa katika ofisi ya BMU cha Kibuyuni. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kwa mujibu wa Juma, hilo lilikuwa tukio la kawaida, kwani hakukuwa na uelewa kuhusu umuhimu wa kumhifadhi nguva. Anasema ilikuwa rahisi sana kuwaona nguva, na hii pia ilikuwa ishara nzuri kwa wavuvi kuwa bahari ilikuwa na samaki wengi. Juma anaamini kutoweka kwa mnyama huyo baharini kumechochewa na shughuli nyingi za uvuvi. “Bahari imeingiliwa sana. Zamani kulikuwa na mitego tu. Sasa watu wanaingia kila sehemu, usiku na mchana. Wanyama wengi wamepotea. Hata samaki wamepungua,” anasema. Hapo zamani nguva alikuwa kitoweo kitamu sana kwa familia nyingi eneo la pwani, kabla ya kuwekwa kwa sheria inayopiga marufuku kumkamata. Faki Kassim, mvuvi kutoka kijiji cha Bodo, Kaunti ya Kwale, anasema takriban miaka 30 iliyopita, yeye na wavuvi wenzake walikuwa wakishika nguva, kumchinja na kuuza nyama yake. “Nguva ana ngozi ngumu sana. Nyama yake ni nyekundu na yenye mafuta mengi. Miaka mingi iliyopita tulikuwa tukiuza kipande kimoja cha nyama yake kwa shilingi moja,” anasema. Anaeleza kuwa kabla ya kumchinja nguva, walilazimika kutekeleza itikadi zao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/11/nguva-wanakaribia-kutoweka-kenya-jamii-za-pwani-zapambana-kuwarejesha-kwa-kupanda-nyasi-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 17:00:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122556/nyumbu2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2358</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Sheria, Uchumi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Serengeti iliyokuwa imemhukumu Marwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa hayo baada ya kukubali rufaa yake na hoja za Jamhuri za kuunga mkono rufani hiyo huku wakibainisha kuwa hawakuweza kuthibisha mashtaka bila kuacha shaka. Mahakama ya Wilaya Serengeti Mahakama ya Wilaya ilimtia hatiani kwa makosa matatu ambayo ni; kuingia hifadhini bila kibali, kumiliki panga ndani ya hifadhi bila kibali pamoja na kumiliki sehemu ya mguu wa nyumbu ambao haukuwa umechunwa ikiwa ni nyara ya Serikali yenye thamani ya Sh 1,586,000 (Dola za Marekani 603). Wanyama aina ya nyumbu wakirejea katika makazi yao ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakitokea katika nchi ya jirani ya Kenya, hususan kwenye mbuya ya Masai Mara. Picha kwa hisasi Blogu ya Michuzi. Upande wa mashtaka ulidai mahakamani kuwa Desemba 7, 2025, askari wa hifadhi walimkamata mshtakiwa katika eneo la Korongo la Nyamburi ndani ya Hifadhi ya Serengeti akiwa na panga na sehemu hiyo ya nyumbu. Utetezi Mahakamani Alipojitetea, Marwa Nyamhanga alidai kuwa Desemba 6, 2025 alikuwa akitoka kwenye sherehe ya harusi akiwa amelewa, ndipo askari wa hifadhi walipomkamata akiwa njiani. Alidai kuwa askari hao walimshikilia katika kituo chao usiku kucha na asubuhi yake walimbambia panga pamoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/#respond</comments>
					<pubDate>21 Juni 2026 17:13:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dann Okoth]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/21164857/Screenshot-2026-06-21-194344.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1898</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Filosofia ya Uhifadhi, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mamalia, na  Mamalia Wakubwa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Siku ya Twiga Duniani: Teknolojia yasaidia kufuatilia twiga wanaokabiliwa na shinikizo la maendeleo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Dunia inapoadhimisha Sikuu ya Twiga leo, siku inayolenga kusherehekea na pia kuhamasisha kuhusu changamoto zinazowakabili mamalia hawa warefu zaidi duniani, mjadala sasa unaelekezwa katika namna bora ya kuwahifadhi si kama spishi moja pekee, bali kama spishi nne tofauti, huku ongezeko la watu na maendeleo ya miundombinu yakiendelea kuwa tishio kwa maisha yao. Kufuatia pendekezo la ujenzi wa Barabara Kuu ya Kasi ya Nairobi-Mombasa (Nairobi Mombasa Expressway &#8211; NME), barabara ya njia mbili itakayojengwa sambamba na Reli ya Kisasa (SGR), mpango wa Twiga Tracker Initiative uliwatia alama twiga 20 (majike 11 na madume 9) ili kufuatilia mienendo na matumizi ya maeneo ya twiga wa Maasai katika ukanda wa Nairobi-Mombasa kabla, wakati na baada ya ujenzi huo ndani ya Eneo la Uhifadhi la Tsavo. Kupitia teknolojia bunifu za ufuatiliaji, na kwa ushirikiano na mfumo wa EarthRanger, programu ya wakati halisi inayosaidia juhudi za uhifadhi wa wanyamapori, watafiti waliwafunga twiga vifaa vyepesi vya GPS vilivyounganishwa na setilaiti kwenye mikia yao ili kupata taarifa muhimu kuhusu namna wanavyohama, jinsi wanavyotumia makazi yao, na athari za shughuli za binadamu kwa mienendo yao. Mpango wa Twiga Tracker, unaotekelezwa na Giraffe Conservation Foundation (GCF), kwa sasa unafuatilia twiga tisa katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Mashariki, wanane katika Hifadhi ya Taifa ya Tsavo Magharibi na watatu katika ranchi za Taita. Shirika la GCF lilitekeleza zoezi hili kwa ushirikiano na Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS), Tsavo Trust, Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyamapori (WRTI), Wildlife Works na Sheldrick Wildlife Trust. Kwa mujibu wa GCF, Eneo la Uhifadhi la Tsavo ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/21/siku-ya-twiga-duniani-teknolojia-ya-gps-yasaidia-kufuatilia-twiga-wa-maasai-wanaokabiliwa-na-shinikizo-la-maendeleo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/#respond</comments>
					<pubDate>19 Juni 2026 16:08:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/19153844/Screenshot-2026-06-19-182917-768x445.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1891</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bioanuai, Bioanuai ya Misitu ya Mvua, Bustani za wanyama, Chakula, Cites, Elimu, Elimu ya Mazingira, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Huduma ya Mifumo ya Ikolojia, Huduma za Mazingira, Idadi ya watu, Ikolojia, Jamii Asili, Jamii ya Nyani Wakubwa, Jamii za Misitu ya Mvua, Kijani, Makazi, na  Mamalia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Miaka kadhaa ya kujenga imani yao: Mazoea ya sokwe watu katika Mbuga ya Kitaifa ya Salonga, DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[HIFADHI YA KITAIFA YA SALONGA, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Kabla ya jua kuchomoza, huku sehemu kubwa ya msitu wa mvua ukiwa umefunikwa na kiza, kundi la watafiti na wafuatiliaji laondoka katika kambi ya utafiti ya Inkomu. Marudio yao ni eneo la viota ambako kundi la bonobo lililala usiku uliopita, ndani kabisa ya msitu wa Salonga, ulio katikati mwa DRC. Dhamira yao ni kuwashawishi bonobo (Pan paniscus) kukubali uwepo wa binadamu kama sehemu ya asili ya mazingira yao. Kwa kupata uaminifu wa wanyama, watafiti wanatumai kuunda fursa za kuelewa vyema tabia, ikolojia na afya zao. Mchakato huu wenye bidii wa kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu unahusisha kutumia wakati karibu na nyani siku baada ya siku hadi watakapozoea watu hatua kwa hatua. Ni kazi ya polepole na inayohitaji juhudi kubwa ambayo inaweza kuchukua miaka, inayohitaji uvumilivu, uthabiti na maelfu ya masaa msituni. Muda mrefu kabla ya mapambazuko, mara nyingi karibu saa 3 alfajiri, wafuatiliaji, baadhi yao wakiwa wawindaji haramu wa zamani, ambao ujuzi wao kuhusu msitu umekuwa rasilimali muhimu ya uhifadhi, wanaanza kuelekea kwenye eneo la viota usiku uliopita. Ni lazima wafike kabla kundi hilo la bonobo halijaamka. Kisha huanza harakati za kutwa nzima kupitia moja ya misitu ya mvua iliyo mbali zaidi Duniani, kufuatia nyani kutoka alfajiri hadi wajenge viota vipya kwa ajili ya usiku. &#8220;Wazo zima la kuwazoesha bonobo uwepo wa binadamu ni kukutana nao kila siku kwa njia ya kirafiki sana, isiyo ya mwingiliano ili wakukubali kama sehemu ya msitu,&#8221; anasema Felix Bofeko, mtafiti msaidizi anayefanya kazi na programu ya mazoea ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/19/miaka-kadhaa-ya-kujenga-imani-yao-mazoea-ya-sokwe-watu-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-salonga-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 13:12:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09111629/Screenshot-2026-06-09-141545.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia ya wenzao. Hata hivyo, licha ya jukumu lao kuu katika kulinda bayoanuwai na baadhi ya misitu muhimu zaidi ulimwenguni, wengi wanaendelea kufanya kazi wakiwa na usaidizi mdogo, mishahara midogo, na hali hatarishi sana. Kwa Emmanuel Bahati Lukoo, ukweli huu ni wa kibinafsi sana. Aliwahi kuwa mlinzi katika mbuga ya kitaifa ya Virunga ambapo kwa sasa ni afisa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Kahuzi-Biega, alinusurika kifo katika shambulizi la kushutukizia mnamo mwaka wa 2018 na kikundi cha wanamgambo wa jamii kinachojulikana kama Mai-Mai. Wenzake kadhaa waliuawa kwa kuviziwa. Alipigwa risasi, alijeruhiwa na kupata kiwewe cha kisaikolojia, na baadaye kufunguliwa mashitaka mbele ya mahakama ya kijeshi katika kesi iliyohusishwa na ulinzi wa hifadhi, angeweza kuondoka. Badala yake, Bahati alichagua kusimulia hadithi yake katika kitabu kiitwacho Conservation at the Cost of My Youth: The Survival of a Ranger, simulizi ghafi ya dhabihu, hofu, shinikizo za kisiasa, na mara nyingi hali halisi isiyoonekana inayowakabili walinzi wa misitu mashariki mwa DRC. Kwenye mahojiano ya ana kwa ana na Mongabay, Bahati anatafakari safari yake, shambulizi lililokaribia kumuua, kiwewe walichopata walinzi, migogoro kati ya uhifadhi na maisha ya jamii ya eneo hilo, na uingiliaji wa kisiasa unaotatiza ulinzi wa maeneo yaliyohifadhiwa. Zaidi ya hadithi ya kibinafsi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 17:49:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Diana Wanyonyi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://swahili.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/Screenshot-2026-03-27-200514.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1250</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Filosofia ya Uhifadhi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Hifadhi, Hifadhi za Jamii za Asili, Maendeleo ya Jamii, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Misitu ya Kitropiki, Nyani, Primates, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tumbili, Tumbili wa Msituni, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia hiyo ya asili imeundwa kupitia shughuli za kila siku za binadamu, magari, baiskeli na pikipiki zinazoitumia mara kwa mara. Pia kuna wanyamapori wanaotumia njia hiyo wakienda kutafuta maji na malisho. Mongabay iliona kinyesi cha ndovu kilichokuwa kimesambaa barabarani na kukauka, huku vingine vikiwa bado vibichi na vikitoa harufu kali. Mbegu za mimea na majani yaliyosagika yalionekana ndani ya kinyesi hicho kilichokuwa ardhini. Kwa wakazi wa Baomo, kinyesi hicho si uchafu bali ni ujumbe kuwa wanaishi kwa ukaribu na wanyamapori wakubwa zaidi barani Afrika: ndovu. Kijiji cha Baomo kilichoko katika Kaunti ya Tana River, pwani ya Kenya, kipo karibu na Mto Tana na kimezungukwa na msitu unaohifadhi wanyamapori mbalimbali, wakiwemo fisi, tumbili, ndovu, nyati, dikdik, nyani, twiga, ndege, nyoka na wanyama wengine. Mpalawasi hawezi kukudhuru Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Baomo. Picha na Diana Wanyonyi, Mongabay. Matawi ya miti yalipoanza kutikisika mbele yangu, Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, aliyekuja kunipokea, aliniambia: “Mwanangu usiogope, wala usihofu. Hao ni tumbili ambao pia ni jamii yetu. Sisi kama jamii ya Pokomo tunawaita ‘Mpalawasi’. Hatakudhuru kabisa, anasubiri nimwimbie wimbo wake afurahie aende zake. Subiri nimwimbie:&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>