<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=uvuvi-haramu&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 06 Aug 2026 09:37:14 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Jinsi mradi wa kufunga mwamba nchini Tanzania unavyookoa ikolojia ya bahari na uchumi wa wavuvi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/jinsi-mradi-wa-kufunga-mwamba-nchini-tanzania-unavyookoa-ikolojia-ya-bahari-na-uchumi-wa-wavuvi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/jinsi-mradi-wa-kufunga-mwamba-nchini-tanzania-unavyookoa-ikolojia-ya-bahari-na-uchumi-wa-wavuvi/#respond</comments>
					<pubDate>12 Mei 2026 19:10:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/12183146/pweza2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1592</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumbawe ni miongoni mwa mifumo ya ikolojia yenye thamani kubwa duniani. Kwa mujibu wa taasisi ya National Oceanic and Atmospheric Administration (NOAA), rasilimali hiyo ya bahari hutumika kama makazi na chakula kwa takribani asilimia 25 ya viumbe wote wa baharini, wakiwemo pweza, majongoo bahari, kambakochi na changu. Tofauti na yanavyoonekana, matumbawe si mawe, bali ni viumbe hai wanaopatikana baharini, wanaoishi kwa kutegemeana na viumbe [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/jinsi-mradi-wa-kufunga-mwamba-nchini-tanzania-unavyookoa-ikolojia-ya-bahari-na-uchumi-wa-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Jinsi mradi wa kufunga mwamba nchini Tanzania unavyookoa ikolojia ya bahari na uchumi wa wavuvi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumbawe ni miongoni mwa mifumo ya ikolojia yenye thamani kubwa duniani. Kwa mujibu wa taasisi ya National Oceanic and Atmospheric Administration (NOAA), rasilimali hiyo ya bahari hutumika kama makazi na chakula kwa takribani asilimia 25 ya viumbe wote wa baharini, wakiwemo pweza, majongoo bahari, kambakochi na changu. Tofauti na yanavyoonekana, matumbawe si mawe, bali ni viumbe hai wanaopatikana baharini, wanaoishi kwa kutegemeana na viumbe wa bahari kama vile pweza, mwani na nyasi bahari. Upekee huu huifanya miamba ya matumbawe kuwa miongoni mwa mifumo tajiri zaidi ya ikolojia duniani, ikitoa makazi, sehemu za kuzaliana na chakula kwa takribani robo ya viumbe wote wa baharini. Matumbawe pia hulinda fukwe dhidi ya mawimbi makubwa na mmomonyoko wa udongo, hivyo huzuia mafuriko kwenye nyumba zilizopo karibu na bahari, kuimarisha uvuvi na kuvutia utalii, na hatimaye kusaidia maisha ya mamilioni ya watu wanaotegemea rasilimali za bahari. Hata hivyo, matumbawe yako hatarini zaidi kutoweka kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi, hasa ongezeko la joto pamoja na  shughuli mbalimbali za binadamu. Kwa mujibu wa Prof. Yunus Daud Mgaya, Mtaalamu wa Biolojia ya Bahari katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, mabadiliko ya tabianchi husababisha kuongezeka kwa kiwango cha joto baharini, na joto la maji linapofika zaidi ya nyuzi joto 30, matumbawe hushindwa kuvumilia na kupoteza mwani (algae) wanaowapa chakula kupitia usanisinuru (photosynthesis). Hali hii husababisha matumbawe hupoteza chanzo cha chakula, kudhoofika na yanapopigwa na mawimbi makali hubomoka kwa urahisi. Ripoti ya International Coral Reef Initiative iliyochapishwa mwaka 2025 inaonyesha ongezeko la joto la bahari duniani kati ya Januari 2023 hadi Machi 2025 limeathiri takribani asilimia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/jinsi-mradi-wa-kufunga-mwamba-nchini-tanzania-unavyookoa-ikolojia-ya-bahari-na-uchumi-wa-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/jinsi-mradi-wa-kufunga-mwamba-nchini-tanzania-unavyookoa-ikolojia-ya-bahari-na-uchumi-wa-wavuvi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/#respond</comments>
					<pubDate>30 Aprili 2026 20:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/30202905/MTERA-6-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1470</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi wa Maji, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha mapato, lakini katika miaka ya hivi karibuni hali imebadilika, samaki wamepungua kwa kiasi kikubwa majini. Kimya kimya anaijuliza, ikiwa leo hakuna samaki, kesho kutwa, mtondo na mtondogoo hali itakuwaje? Mashaka haya hayamkabili Jamal pekee, bali pia wavuvi wengi nchini kote. Kilio cha wavuvi Kilio cha wavuvi nchini Tanzania ni matokeo ya athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo yameitikisa vibaya sekta ya uvuvi kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusababisha kiwango cha samaki kupungua huku baadhi ya aina ya samaki wakitoweka kabisa. Victor Tondelo, Mtaalamu Mtafiti wa Madiliko ya Tabianchi, aliiambia Mongabay kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimejidhihirisha zaidi katika rasilimali za maji (water resources) hasa kwenye mito, mabwawa na maziwa. “Kwa sababu ya kupungua kwa mvua inayonyesha na misimu inayotabirika, maji yamepungua na hivyo idadi ya samaki ambao maisha yao ni majini pia imepungua,” alieleza. Aliongeza kuwa kuwepo kwa maji machache pia husababisha joto kubwa wakati wa kiangazi na samaki na viumbe wengine wa majini hufa kutokana na joto kali. Uchunguzi wa Mongabay kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta ya uvuvi, ulijikita katika mikoa mitatu ya Morogoro, Iringa na Pwani. Katika mkoa wa Morogoro ulihusisha mto Kilombero, Luipa, Ruhudji na Mto&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>04 Januari 2026 19:23:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/04190953/kuruwitu1-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=871</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mazingira, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Takwimu, Ufugaji, Ufugaji Samaki, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya uhifadhi wa mazingira ya baharini?&#8221; aliniuliza kijana wa rika, mwendesha pikipiki. Na baada ya dakika kama saba, nilikuwa nimefika eneo hilo. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Kuruwitu Conservation Welfare and Association Daniel Mwangunya alikuwa ameshawasili tayari kuhojiwa kuhusu shughuli zao za uhifadhi wa mazingira ya bahari katika bandari ya Kinuni. Lakini kwanza aliomba tumsubiri mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa matumbawe, ambaye kwa wakati huo alikuwa amepeleka wageni kuzama na kutalii mandhari ndani ya bahari. Tengefu ni eneo la bahari lililotengwa na kusimamiwa na wanajamii kwa ajili ya uhifadhi wa viumbe na mazingira ya baharini. Eneo lililohifadhiwa na jamii ya Kuruwitu kwa ajili ya kuongeza samaki na kuhifadhi matumbawe. Picha na Ruth Keah. Katika mantiki ya tengefu, hili ni eneo ambalo uvuvi wa samaki hauruhusiwi. Eneo hili linalindwa na wanajamii, hivyo kusababisha samaki kuwa na mazingira mwafaka ya kuzaana na kuongezeka. Wanapokuwa wengi, wanamiminika hadi sehemu ambazo wavuvi wanaruhusiwa kuvua, hivyo basi kuongeza kipato. Utulivu ulionikaribisha hapo ni ishara kwamba hakuna shughuli za uvuvi zinazoendelea, bali ni pilkapilka za kupokea wageni, kutayarisha vifaa kama vile mashua na zana za kuzamia kwenye bahari. Katana Ngala ni mzaliwa wa kijiji cha Kuruwitu, na ni miongoni mwa waanzilishi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/#respond</comments>
					<pubDate>30 Desemba 2025 14:08:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mongabay.com]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/13140426/Screenshot-2026-01-13-165604-768x482.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=922</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maji, Mazingira, Maziwa, Mito, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ulilenga kuboresha sekta ya uvuvi kwa kubadilisha boti za mbao zilizopitwa na wakati kwa vyombo vya kisasa vya kuvulia. Rais Samia alipotembelea Kilwa miezi miwili kabla ya uzinduzi wa mpango huo, aliahidi kuwa wavuvi wadogo wangepewa boti hizo kupitia mikopo yenye riba nafuu. Ahadi hiyo iliibua matumaini makubwa miongoni mwa jamii za wavuvi ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za boti chakavu na ukosefu wa mtaji wa kununua vyombo vipya. Ili kufadhili mpango huo, serikali ilishirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), ambayo hutoa mikopo nafuu kwa vikundi vya wavuvi. Mikopo hiyo ina viwango vya riba vya chini, inatoa muda mrefu kwa marejesho, na inajumuisha kipindi cha msamaha wa malipo cha takribani miaka mitano hadi kumi kabla ya kuanza kulipa. “Tunatoa tangazo linalowafikia watu nchi nzima pindi boti zinapopatikana,” alisema Mohammed Sheikh, Mkurugenzi wa Uvuvi katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi. “Vyama vya ushirika vinavyovutiwa vinatuma maombi, na vikikubaliwa, hupokea boti ambazo zinakuwa zimewekewa bima kamili na ziko tayari kwa matumizi.” Thamani ya kila boti hutegemea ukubwa wake (kwa kawaida boti yenye ukubwa wa kati ya mita 5 hadi 14, (futi 16 hadi 46), gharama yake ni takribani shilingi milioni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mauaji katika Ziwa Naivasha, Kenya yazua maswali kuhusu jukumu la walinzi wa pwani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>21 Agosti 2025 12:27:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joseph Maina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/01134625/Screenshot-2025-10-01-153154-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=580</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Migogoro, Samaki, Utawala, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIVASHA, Kenya — Ilikua bado ni giza simu ilipoingia. Grace Nyambura, anayejulikana kwa majirani zake eneo la Karagita Naivasha, kama Mama Chuma, alikuwa amelala alipopigiwa simu na binti yake. Ilikuwa yapata saa 11 alfajiri. Alimwambia Nyambura kuwa kuna jambo limemkumba Chuma, ambaye ni mtoto wa tano wa kiume wa Nyambura. Alimwomba mama yake afike Ziwa Naivasha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/" data-wpel-link="internal">Mauaji katika Ziwa Naivasha, Kenya yazua maswali kuhusu jukumu la walinzi wa pwani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIVASHA, Kenya — Ilikua bado ni giza simu ilipoingia. Grace Nyambura, anayejulikana kwa majirani zake eneo la Karagita Naivasha, kama Mama Chuma, alikuwa amelala alipopigiwa simu na binti yake. Ilikuwa yapata saa 11 alfajiri. Alimwambia Nyambura kuwa kuna jambo limemkumba Chuma, ambaye ni mtoto wa tano wa kiume wa Nyambura. Alimwomba mama yake afike Ziwa Naivasha haraka iwezekanavyo. Nyambura alitii wito huo. Kamau, mwanawe mkubwa, alimchukua kwa pikipiki na wakaendesha kwa kasi katika mji uliokuwa kimya, kuelekea ufuo wa ziwa. Aliyoyakuta asubuhi hiyo miaka minne iliyopita, yanampa kumbukumbu ya kuhuzunisha sana: mwanae, Samuel Mwangi Kimani – jina la utani Chuma kwa wale waliomfahamu &#8211; mwenye umri wa miaka 25 na baba wa watoto wawili, alikuwa amekufa kando ya ufukwe wa ziwa. &#8220;Alionekana kapigwa risasi mgongoni, ikiashiria kuwa alikuwa akikimbia,&#8221; Nyambura anaiambia Mongabay, akiwa ameketi kwenye sofa iliyochakaa ndani ya sebule yake yenye mwanga hafifu. &#8220;Walikuwa wakikimbia walinzi wa pwani. Walikuwa wakielekea upande mwingine.&#8221; Tukio hilo lilitokea mwezi wa Septemba mwaka 2021. Maandamano kuhusu mauaji hayo yalizuka baadaye katika makazi ya Karagita. Lakini katika kusimulia mauaji ya mwanae, Nyambura haonekani kufadhaika. Anaonekana kusumbuliwa zaidi na hilo, si kifo chake tu, bali pia miaka iliyotangulia, ambapo alishuhudia mtoto wake akihangaika kutafuta riziki. Kwa muda wa miaka miwili, Kimani alikuwa akivua samaki na kupata vibarua vya ujenzi sehemu mbalimbali mjini. Uvuvi, alisema, umekuwa hatari kila wakati. &#8220;Walikuwa wakipigwa,&#8221; Nyambura anasema. &#8220;Walinyanyaswa na maafisa wa ulinzi wa pwani.&#8221; Mongabay iliwasiliana na Shirika la Huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya kuhusu tukio hilo, lakini halikuweza kuthibitisha undani wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>