<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=sheria&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/sheria/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 22 Aug 2026 21:21:12 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/#respond</comments>
					<pubDate>05 Agosti 2026 17:00:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/05122556/nyumbu2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2358</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Sheria, Uchumi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Aliyehukumiwa miaka 20 jela kwa kukutwa na mguu wa nyumbu, aachiwa huru</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu ya Tanzania, Masjala Ndogo ya Musoma, imemwachia huru Marwa Nyamhanga aliyetiwa hatiani kwa kukutwa na nyara za Serikali, kuingia na kumiliki silaha ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti baada ya kubaini dosari zilizojitokeza katika ushahidi wa upande wa mashtaka. Mahakama hiyo Julai 20,2026 mbele ya Jaji Kamazima Kafanabo ilitengua hukumu ya Mahakama ya Wilaya ya Serengeti iliyokuwa imemhukumu Marwa kifungo cha miaka 20 jela kwa makosa hayo baada ya kukubali rufaa yake na hoja za Jamhuri za kuunga mkono rufani hiyo huku wakibainisha kuwa hawakuweza kuthibisha mashtaka bila kuacha shaka. Mahakama ya Wilaya Serengeti Mahakama ya Wilaya ilimtia hatiani kwa makosa matatu ambayo ni; kuingia hifadhini bila kibali, kumiliki panga ndani ya hifadhi bila kibali pamoja na kumiliki sehemu ya mguu wa nyumbu ambao haukuwa umechunwa ikiwa ni nyara ya Serikali yenye thamani ya Sh 1,586,000 (Dola za Marekani 603). Wanyama aina ya nyumbu wakirejea katika makazi yao ya Hifadhi ya Taifa ya Serengeti wakitokea katika nchi ya jirani ya Kenya, hususan kwenye mbuya ya Masai Mara. Picha kwa hisasi Blogu ya Michuzi. Upande wa mashtaka ulidai mahakamani kuwa Desemba 7, 2025, askari wa hifadhi walimkamata mshtakiwa katika eneo la Korongo la Nyamburi ndani ya Hifadhi ya Serengeti akiwa na panga na sehemu hiyo ya nyumbu. Utetezi Mahakamani Alipojitetea, Marwa Nyamhanga alidai kuwa Desemba 6, 2025 alikuwa akitoka kwenye sherehe ya harusi akiwa amelewa, ndipo askari wa hifadhi walipomkamata akiwa njiani. Alidai kuwa askari hao walimshikilia katika kituo chao usiku kucha na asubuhi yake walimbambia panga pamoja&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/05/aliyehukumiwa-miaka-20-jela-kwa-kukutwa-na-mguu-wa-nyumbu-aachiwa-huru/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 12:22:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30073721/Magari2-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2264</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Halijoto, Kaboni, Mabadiliko ya Tabianchi, Maliasili, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Siasa za Tabianchi, Teknolojia, Uendelevu, na  Ufanisi wa nishati]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya kuhamia matumizi ya nishati safi kwenye vyombo vya usafiri kwa kuzielekeza taasisi zote za umma kuanza kujumuisha ununuzi wa magari yanayotumia umeme na gesi asilia katika mipango na bajeti zao. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omari, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupunguza gharama kubwa za kununua mafuta. Bajaji zinazotumia umeme. Picha ya Jenifer Gilla, Mongabay. Hatua hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050  na Michango ya Taifa Iliyoamuliwa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris ambapo Tanzania imeahidi kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kupitia sekta za nishati na usafiri. Uzalishaji wa hewa ya ukaa Mpango wa kutumia nishati safi kwenye vyombo vya usafiri nchini Tanzania, iwapo utafanikiwa, utapunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi. Msololo Onditi, Mtaalam wa mabadiliko ya tabianchi na Mshauri wa Masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika Shirika la Maendeleo la Ujerumani Tanzania (GIZ), anasema kila lita moja ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:16:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28111600/Tembo-6-1.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2227</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo: Mahakama yatupa rufaa ya Jamhuri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro imeitupilia mbali rufaa ya Jamhuri ya kupinga hukumu iliyowaachia huru Yahaya Juma na mwenzake. Washitakiwa hao walikuwa wanadaiwa kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000. Hukumu ya Mahakama hiyo ilitolewa na Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu Kanda ya Morogoro, Stephen Magoiga baada ya kusikiliza mawasilisho ya pande zote mbili. Rufani hiyo iliyowasilishwa na Wakili wa Serikali Paulina Massawe ilitokana na uamuzi wa Mahakama ya Wilaya ya Morogoro uliowaachia huru Yahaya Juma na Masima Mlugu waliokuwa wakikabiliwa na shtaka la kukutwa na vipande 18 na meno matatu ya tembo yenye thamani ya Dola za Marekani 120,000 bila kibali halali. Mahakama ya Wilaya Katika Mahakama ya Wilaya, upande wa mashtaka uliwasilisha mashahidi sita, akiwemo mtunza vielelezo, askari aliyefanya ukamataji, shahidi huru aliyeshuhudia upekuzi na ukamataji, mhifadhi wa wanyamapori aliyefanya uthamini wa meno ya tembo, askari wa TANAPA aliyeshiriki operesheni pamoja na mpelelezi wa kesi. Upande wa mashtaka uliwasilisha vielelezo saba, vikiwemo vipande 18 vya meno ya tembo, meno matatu kamili ya tembo, magunia mawili ya salfeti yaliyobebea meno hayo, pikipiki aina ya FEKON yenye namba T43 CNF, hati ya ukamataji na ripoti ya uthamini iliyoonyesha kuwa nyara hizo zilikuwa na thamani hiyo. Kwa upande wa utetezi, washtakiwa wote wawili walitoa ushahidi wao wenyewe. Mshtakiwa wa kwanza aliwasilisha pia flashi diski iliyokuwa na video ya YouTube akidai kuwa meno ya tembo yaliyoonyeshwa kwenye taarifa ya habari hayakuwa na alama, tofauti na yale yaliyowasilishwa mahakamani kama vielelezo. Mahakama ya Wilaya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-mahakama-yatupa-rufaa-ya-jamhuri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/#respond</comments>
					<pubDate>28 Julai 2026 10:03:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/28112229/ELEPHANT-3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2230</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Kimataifa, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Pembe za Ndovu, Sheria, Tembo, Uhalifu, Usafirishaji wa Wanyamapori, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kumiliki nyara za Serikali: Mahakama yabatilisha hukumu ya kifungo cha miaka 20 jela</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR-ES-SALAAM, Tanzania — Mahakama Kuu Kanda ya Mbeya imekubali rufaa ya Yegela Nchola na kubatilisha hukumu ya kutiwa hatiani na kifungo cha miaka 20 jela kwa kosa la kumiliki nyara za Serikali kinyume cha sheria. Mahakama hiyo pia mbele ya Jaji Musa Pomo imeamuru kesi hiyo isikilizwe upya mbele ya mahakama yenye mamlaka. Awali, Mahakama ya Wilaya ya Songwe ilimhukumu mshtakiwa baada ya kutiwa hatiani kwa kukutwa na vipande 10 vya meno ya tembo vyenye thamani ya $60,000 bila kibali halali. Upande wa mashtaka uliita mashahidi sita na kuwasilisha vielelezo mbalimbali, huku mshtakiwa akikana mashtaka na kudai alikamatwa kimakosa alipokuwa amekwenda kununua mahindi na hakuwa na shahidi. Mamlaka ya mahakama Katika rufaa yake, Nchola alijiwakilisha mwenyewe, alipinga hukumu hiyo akidai miongoni mwa mambo mengine kuwa Mahakama ya Wilaya haikuwa na mamlaka ya kusikiliza shauri hilo kwa kuwa kumbukumbu za kesi hazikuonyesha kuwepo kwa hati ya idhini ya Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) pamoja na cheti cha mamlaka vinavyotakiwa kisheria katika makosa ya uhujumu uchumi. Katika kuunga mkono rufaa yake, mrufani alidai kuwa upande wa mashtaka ulishindwa kuthibitisha shtaka dhidi yake pasipo kuacha shaka yoyote ya msingi. Alidai kuwa ushahidi wa shahidi wa kwanza wa upande wa mashtaka (PW1) kuhusu uthamini wa nyara za Serikali haukuwa wa kuaminika. Pia alidai kuwa mlolongo wa utunzaji wa vielelezo haukuthibitishwa kwa sababu shahidi muhimu hakuitwa kutoa ushahidi. Aidha alidai kuwa mashahidi wa upande wa mashtaka walishindwa kuvitambua ipasavyo vielelezo walipokuwa wakitoa ushahidi mahakamani. Uhalali wa vielelezo Aliongeza kuwa hata mahakama ya mwanzo ilionyesha mashaka kuhusu uhalali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/28/kesi-kumiliki-nyara-za-serikali-mahakama-yabatilisha-hukumu-ya-kifungo-cha-miaka-20-jela/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 12:20:20 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23122231/park-7-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2193</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Maliasili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira, Mgogoro wa Rasilimali, Sheria, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uanaharakati, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Kitropiki, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Misitu, Uokoaji wa Wanyamapori, Usimamizi Endelevu wa Misitu, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Utowekaji wa Misitu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mahakama yakagua eneo linalobishaniwa Nairobi, huku KWS ikishutumiwa kwa kuwazuia wanaharakati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya – Shirika la Huduma za Wanyamapori Kenya (KWS) limeshutumiwa kwa kuwazuia na kuwanyanyasa walalamikaji wenza katika kesi inayopinga uhamishaji wa Kituo cha Kuhifadhi Wanyama Yatima cha Nairobi (Nairobi Animal Orphanage). Mnamo Julai 16, Mahakama ya Mazingira na Ardhi jijini Nairobi ilimwagiza Naibu Msajili wake, Vincent Kiplagat, kutembelea eneo linalobishaniwa akiwa pamoja na pande zote katika kesi hiyo ili kuandaa na kuwasilisha ripoti mahakamani. Katika taarifa iliyotumwa kwa Mongabay, shirika la Save the Nairobi National Park (SaveNNP) lililaani kile lilichokiita &#8220;vitisho na vitendo vya kutisha&#8221; kutoka kwa maafisa wa KWS, pamoja na hatua ya kuwanyima wanaharakati hao ruhusa ya kuingia katika eneo la ziara. SaveNNP ilisema hatua hiyo inapingana na mwaliko wa KWS kwa vyombo vya habari kushiriki katika ziara hiyo ya mahakama. Ujenzi unaendelea katika maeneo yanayobishaniwa ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Nairobi huku Mahakama ya Mazingira na Ardhi ikiendelea kusikiliza kesi iliyowasilishwa na wanaharakati wa mazingira. Picha kwa hisani ya SaveNNP. Mongabay iliona barua ya KWS iliyowaalika wanahabari kuhudhuria ziara ya eneo hilo iliyoongozwa na Msajili wa Mahakama ya Mazingira. Katika taarifa yao, SaveNNP na JustAct ziliishutumu KWS kwa kutaka &#8220;kudhibiti simulizi&#8221; kuhusu mradi huo na kuhakikisha sauti za Wakenya hazisikiki mahakamani wala kupitia vyombo vya habari wakati wa ukaguzi wa eneo hilo. Madai kama hayo pia yalitolewa na Friends of Nairobi National Park. Msemaji wa KWS, Duncan Wanyama, alisema wageni hao hawakuzuiwa kuingia, na kwam ba askari wa wanyamapori walikuwa wakitekeleza tu taratibu za kawaida zinazotumika ndani ya hifadhi hiyo, vyombo vya habari vya ndani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/pande-zapingana-wakati-mahakama-yatembelea-eneo-la-ujenzi-katika-hifadhi-ya-taifa-ya-nairobi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, tafiti za mara kwa mara za madini katika maeneo ya uhifadhi zinaathiri mazingira?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>03 Julai 2026 14:13:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asha Bekidusa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/03133945/George-Kimau-akionyesha-eneo-la-Mrima-ambapo-ndani-ya-ardhi-hiyo-kuna-madini-ya-niobium-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1986</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Dawa ya Asili, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Milima, Misitu, Misitu ya Asili, Misitu ya Kitropiki, Misitu ya Milimani, Miti, Nyani, Sheria, Sheria ya Mazingira, Tamaduni za Kiasili, Teknolojia, Uchimbaji Madini, Uchumi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Ukataji Miti, Utafiti, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Vikundi vya Jamii za Asili, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa miaka mingi, Nassir Abdallah Bege amekuwa akitembea katika njia za Msitu wa Mrima, katika Kaunti ya Kwale, akiangalia ukuaji wa miti na juhudi za jamii za eneo hilo katika kuulinda. Akiwa mwenyekiti wa Muungano wa Msitu wa Kijamii wa Mrima (Mrima Community Forest Association), amekuwa nguzo muhimu katika uhifadhi wa Mrima, ulio takriban kilomita 65 kusini-magharibi mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Je, tafiti za mara kwa mara za madini katika maeneo ya uhifadhi zinaathiri mazingira?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa miaka mingi, Nassir Abdallah Bege amekuwa akitembea katika njia za Msitu wa Mrima, katika Kaunti ya Kwale, akiangalia ukuaji wa miti na juhudi za jamii za eneo hilo katika kuulinda. Akiwa mwenyekiti wa Muungano wa Msitu wa Kijamii wa Mrima (Mrima Community Forest Association), amekuwa nguzo muhimu katika uhifadhi wa Mrima, ulio takriban kilomita 65 kusini-magharibi mwa Mombasa. Anakumbuka mashimo yaliyoachwa baada ya baadhi ya sehemu za msitu kukatwa wakati kampuni zilipokuwa zikifanya tafiti za kutafuta madini. Zaidi ya mwongo mmoja baadaye, anasema, mashimo hayo yanaendelea kujiziba yenyewe. Ukitembea msituni, si rahisi kuona mashimo hayo madogo kwani yamefinikwa, baada ya mimea ya asili kuota tena kwa zaidi ya muongo mmoja. Mrima. Picha na Asha Bekidusa, Mongabay. Neno ‘Mrima’ linatoka katika jamii ya Wadigo, kumaanisha mlima. Msitu huu wa Mrima una rutuba kubwa na bioanuwai ya kipekee. Kadri unavyozidi kupanda mlimani, msitu huwa mnene zaidi na mwanga hupungua. Eneo hili liko kimya, isipokuwa sauti za wanyama, wadudu na miti ambayo mara kwa mara inatikisika kutokana na upepo unaovuma. Kwa mujibu wa Key Biodiversity Areas (KBA), eneo la Mrima lenye umuhimu wa bioanuwai lina ukubwa wa takriban kilomita za mraba 3.76 (sawa na takriban hekta 376), ambapo asilimia 95.77 ya eneo hilo iko chini ya hadhi mbalimbali za ulinzi wa kisheria. Utafiti na uharibifu wa misitu Kutokea miaka ya 1950, wataalamu wa jiolojia na makampuni ya madini wamekuwa wakifanya tafiti katika eneo la Mrima kutathmini uwepo wa madini ya niobium na madini adimu mengine. Stakabadhi za rekodi za kesi ya kampuni ya Cortec zinaonyesha kuwa utafiti wa awali ulifanywa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kasuku wa Kiafrika waliookolewa warudishwa katika misitu ya DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/#respond</comments>
					<pubDate>21 Oktoba 2025 12:30:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Didier Makal]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/03123238/Screenshot-2025-11-03-152749-768x474.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=714</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Ndege, Sehemu za Bioanuwai, Sheria, Sheria ya Mazingira, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LUBUMBASHI, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo &#8211; kasuku 50 wa Kiafrika wa kijivu wameachiliwa na kurejea porini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia kuokolewa kutoka kwa biashara haramu ya wanyamapori. Kuachiliwa kwao, katika mkoa wa kati wa Maniema mwezi huu wa Oktoba, kulikuja baada ya mwaka mmoja kurekebiswa katika hifadhi inayoendeshwa na Wakfu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/" data-wpel-link="internal">Kasuku wa Kiafrika waliookolewa warudishwa katika misitu ya DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LUBUMBASHI, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo &#8211; kasuku 50 wa Kiafrika wa kijivu wameachiliwa na kurejea porini katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kufuatia kuokolewa kutoka kwa biashara haramu ya wanyamapori. Kuachiliwa kwao, katika mkoa wa kati wa Maniema mwezi huu wa Oktoba, kulikuja baada ya mwaka mmoja kurekebiswa katika hifadhi inayoendeshwa na Wakfu wa Lukuru wenye makao yake nchini humo, ambao umewatunza na kuwaachilia karibu kasuku 400 waliopatikana kutoka kwa wafanyabiashara haramu. Wakati utekelezaji wa amri mpya iliyochapishwa na wizara ya mazingira ya DRC inapoanza, vituo vya urekebishaji wa taasisi hiyo vinatarajia kazi nyingi zaidi za kufanya. Mnamo Julai 31, 2025, DRC ilichapisha amri inayokataza kukamata, kumiliki au kufanya biashara ya kasuku wa Kiafrika wa kijivu (Psittacus erithacus). Marufuku hiyo ilitanguliwa na hatua kama hiyo iliyopitishwa awali na mamlaka katika mkoa wa Tshopo, kaskazini mwa DRC, ambao mji mkuu wake, Kisangani, unatumika kama kitovu kikuu cha biashara ya kasuku. Lakini mwezi mmoja baadaye, kasuku waliokamatwa bado walikuwepo katika jamii za Ngungwa na Kimwachi huko Maniema, kulingana na Corneille Kalume, meneja wa taasisi isiokuwa ya  kiserikali ya Action for Environmental Management (Action Communautaire pour la Gestion de l’Environnement) yenye makao yake makuu Kindu, mji mkuu wa mkoa. &#8220;Wawindaji haramu bado wanawawinda na kuwakamata kasuku,&#8221; Kalume aliiambia Mongabay kwa njia ya simu. &#8220;Ni vizuri kuwa na agizo la mawaziri la kupiga marufuku ujangili, lakini kuna haja ya kuchukuliwa hatua za kuzuia watu kuwatega ndege.&#8221; Kasuku wa kijivu walinaswa katika operesheni ya kupambana na biashara haramu ya binadamu huko Lodja, DRC. Picha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/21/kasuku-wa-kiafrika-waliokolewa-warudishwa-katika-misitu-ya-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wafichua taarifa wahusisha kampuni ya uwindaji wa kifahari na ujangili Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/08/22/kampuni-ya-uwindaji-wa-kifahari-yahusishwa-na-ujangili-tanzania-wafichua-taarifa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/08/22/kampuni-ya-uwindaji-wa-kifahari-yahusishwa-na-ujangili-tanzania-wafichua-taarifa/#respond</comments>
					<pubDate>22 Agosti 2024 20:24:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mongabay.com]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2024/08/25121514/Screenshot-2025-09-25-151400-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=151</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Biashara ya Wanyamapori, Jamii Asili, Migogoro ya Ardhi, Nyama ya Porini, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Ujangili, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utawala, Uwindaji, na  Watu wa Jadi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LOLIONDO, Tanzania — Kampuni ya uwindaji wa kifahari inayotoa huduma kwa watu wa tabaka la juu kutoka Falme za Kiarabu na familia ya kifalme, inadaiwa kuhusika na matukio ya ujangili yaliyodumu kwa miongo kadhaa hapa Tanzania, wafichua taarifa wameiambia Mongabay. Wadau wa ndani wanatoka kampuni ya Ortello &#8211; wakati mwingine huandikwa Otterlo &#8211; Business Corporation (OBC), [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/08/22/kampuni-ya-uwindaji-wa-kifahari-yahusishwa-na-ujangili-tanzania-wafichua-taarifa/" data-wpel-link="internal">Wafichua taarifa wahusisha kampuni ya uwindaji wa kifahari na ujangili Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LOLIONDO, Tanzania — Kampuni ya uwindaji wa kifahari inayotoa huduma kwa watu wa tabaka la juu kutoka Falme za Kiarabu na familia ya kifalme, inadaiwa kuhusika na matukio ya ujangili yaliyodumu kwa miongo kadhaa hapa Tanzania, wafichua taarifa wameiambia Mongabay. Wadau wa ndani wanatoka kampuni ya Ortello &#8211; wakati mwingine huandikwa Otterlo &#8211; Business Corporation (OBC), ambayo inaendesha shughuli zake huko Loliondo, wilaya ya Ngorongoro kaskazini mwa Tanzania. Mahojiano na vyanzo vya habari, ambavyo viliomba majina bandia kwa sababu za kiusalama, yanatoa mwanga kuhusu safari za uwindaji zilizopangwa na kampuni ya OBC, ambazo zilivutia ndugu wa familia ya kifalme ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) na washirika wao wa karibu angalau mara moja au mbili kwa mwaka kuanzia miaka ya 1990 hadi mwishoni mwa mwaka 2016. Wanaripoti kwamba baadhi ya safari hizi zilisababisha wanyamapori hai kusafirishwa kwenda nchi za nje kwa ndege. Usafirishaji wa wanyamapori hai umepigwa marufuku nchini Tanzania tangu mwaka 2016 ili kulinda wanyama na ndege adimu. Mnamo mwaka 2022, wabunge walibatilisha haraka uamuzi wa kutatanisha wa kuondoa marufuku ambayo ilikuwa imewekwa kwa miaka sita. Ushahidi wa vyanzo hivyo umekuja wakati mamlaka ya Tanzania imetoa notisi za kuwaondoa wafugaji wa Kimasai ndani na nje ya Loliondo, kama sehemu ya juhudi za kukodisha eneo la kilomita za mraba 1,500 (maili za mraba 580) kwa kampuni ya OBC. Mwaka 2023, ripoti ya shirika la kutetea haki la Amnesty International ililaani vikosi vya serikali kwa vurugu na ukamataji wa watu wengi ambao uliwaacha wastani wa Wamasai 70,000 bila maeneo yao ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/08/22/kampuni-ya-uwindaji-wa-kifahari-yahusishwa-na-ujangili-tanzania-wafichua-taarifa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/08/22/kampuni-ya-uwindaji-wa-kifahari-yahusishwa-na-ujangili-tanzania-wafichua-taarifa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>