<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=uchafuzi-wa-hewa&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/uchafuzi-wa-hewa/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 16 Sep 2026 17:46:29 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Wataalam wa mazingira wazungumzia athari za moto ulioteketeza maduka Burundi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/wataalam-wa-mazingira-wazungumzia-athari-za-moto-ulioteketeza-maduka-burundi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/wataalam-wa-mazingira-wazungumzia-athari-za-moto-ulioteketeza-maduka-burundi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Agosti 2026 08:06:55 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Thérence Hategekimana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/26065117/1-Duka-la-Ndayizamba-linateketea-kwa-moto.-Pica-na-Therence-Hategekimana-720x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2602</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Maji, Moto, Uchafuzi wa Hewa, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Moto mkubwa umezuka katika majengo ya maduka ya ETS Ndayizamba na Le Parisien, yaliyoko katikati ya mji wa kiuchumi, Bujumbura, Burundi. Kwa wafanyabiashara, moto huo umesababisha hasara kubwa kiuchumi lakini kwa wana mazingira, moto huo unaweza kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa hewa. Hilaire Habarugira, mtaalamu wa mazingira nchini Burundi aliiambia Mongabay kuwa moshi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/wataalam-wa-mazingira-wazungumzia-athari-za-moto-ulioteketeza-maduka-burundi/" data-wpel-link="internal">Wataalam wa mazingira wazungumzia athari za moto ulioteketeza maduka Burundi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Moto mkubwa umezuka katika majengo ya maduka ya ETS Ndayizamba na Le Parisien, yaliyoko katikati ya mji wa kiuchumi, Bujumbura, Burundi. Kwa wafanyabiashara, moto huo umesababisha hasara kubwa kiuchumi lakini kwa wana mazingira, moto huo unaweza kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa hewa. Hilaire Habarugira, mtaalamu wa mazingira nchini Burundi aliiambia Mongabay kuwa moshi wa bidhaa zilizoharibiwa na moto vikiwemo vifaa vya plastiki, nguo, viatu, vifaa vya kufungashia, betri, mafuta, kemikali pamoja na vifaa vya kielektroniki, unaweza kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa hewa. &#8220;Mabaki ya moto yanaweza kuendelea kuchafua mazingira hata baada ya moto kuzimwa,&#8221; alisema Habarugira. Pierre Nduwayo ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya mazingira, aliiambia Mongabay kuwa mabaki ya moto huo pia yanaweza kusababisha uchafuzi wa maji. &#8220;Wakati wa mvua, majivu na kemikali zenye sumu vinaweza kusombwa na maji kuingia kwenye mifereji, mito na maziwa, na hivyo kuchafua vyanzo vya maji,&#8221; alisema. Kwa kuwa baadhi ya mifereji ya maji ya Bujumbura humwaga maji yake katika Ziwa Tanganyika, mfumo wa ikolojia wa ziwa hilo unaweza kuwa hatarini iwapo hatua madhubuti hazitachukuliwa. Moto huo ambao chanzo chake hakijafahamika ulianza majira ya saa kumi na mbili asubuhi katika mojawapo ya ghorofa za majengo hayo. Walinzi wa majengo hayo walidai kuwa licha huduma za zimamoto Licha ya idara ya Zimamoto kufika haraka eneo la tukio ili kujaribu kuudhibiti, moto uliendelea kuteketeza maduka hayo kwa saa kadhaa, na kuharibu kabisa maduka yote mawili. Makamu wa Rais wa Jamhuri, Prosper Bazombanza, akiwa pamoja na Gavana wa Mkoa wa Bujumbura, walitembelea eneo la tukio.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/wataalam-wa-mazingira-wazungumzia-athari-za-moto-ulioteketeza-maduka-burundi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/wataalam-wa-mazingira-wazungumzia-athari-za-moto-ulioteketeza-maduka-burundi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/#respond</comments>
					<pubDate>23 Julai 2026 12:11:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ini Ekott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/23115923/Screenshot-2026-07-23-143214-768x438.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2184</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Cote D'Ivoire, Kenya, Nigeria, Uingereza, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Gesi, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Ufanisi wa nishati, na  Utoaji wa Gesi Chafu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Njia safi za kupikia zinaongezeka kwa kasi barani Afrika, lakini  bado haziendani na ongezeko la watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Eneo la kusini mwa Jangwa la Sahara liko njiani kurekodi upanuzi wake wa haraka zaidi kuwahi kutokea wa kila mwaka katika upatikanaji wa huduma za upishi safi mwaka wa 2026, kulingana na ripoti mpya ya Shirika la Nishati la Kimataifa. Lakini ukuaji wa idadi ya watu unaendelea kuzidi kasi ya maendeleo hayo, na kuwaacha zaidi ya watu bilioni moja bila huduma za upishi safi. Kanda hiyo ni nyumbani kwa idadi kubwa zaidi ya watu duniani ambayo bado inategemea kuni, mkaa na mafuta ya taa kwa ajili ya kupikia kila siku, kulingana na shirika la IEA. Shirika la Afya Duniani (WHO) linasema uchafuzi wa hewa wa makazi, ambao mwingi wake huzalishwa na nishati hizi za kupikia zinazochafua mazingira, unahusishwa na vifo vya mapema takriban milioni 2.9 kila mwaka, huku wanawake na watoto wakibeba mzigo mkubwa zaidi. &#8220;Upishi Safi Afrika 2026: Ripoti ya Maendeleo&#8221; inakadiria kuwa karibu watu milioni 15 walipata fursa ya kutumia upishi safi katika eneo la Kusini mwa Jangwa la Sahara mwaka wa 2025, karibu 35% zaidi ya wastani wa faida ya kila mwaka iliyorekodiwa kwa miaka mitano iliyopita. Ikiwa itathibitishwa, hii itakuwa ongezeko kubwa zaidi la kila mwaka kuwahi kurekodiwa. Côte d&#8217;Ivoire, Kenya na Nigeria zilipata faida kubwa zaidi. Makadirio hayo yametokana na mfumo wa hisabati unaounganisha takwimu za uingizaji wa majiko (vifaa vya kupikia vinavyochanganya jiko la kawaida na oveni) na gesi ya petroli iliyoshinikizwa (LPG), uwekezaji katika miundombinu, nishati na teknolojia zinazohitajika kwa ajili ya upikaji safi, pamoja na ufuatiliaji wa sera. Badala ya kutegemea tafiti za makazi, ambazo ndizo kipimo cha kuaminika zaidi cha upatikanaji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/23/njia-safi-za-kupikia-zinaongezeka-kwa-kasi-barani-afrika-lakini-bado-haziendani-na-ongezeko-la-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:56:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/15110719/Taka-za-kielektroniki-zikikusanywa-kwa-ajili-ya-kutengeneza-vitu-vingine-Picha-hisani-ya-WEEE-Centre-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2080</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Taka za kielektroniki ni janga hatari kwa mazingira na afya ya watu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni mchana wa Jumapili tulivu mjini Iringa. Penina Mtatifikolo anaandaa chakula kwa ajili ya familia yake. Mama huyu hana habari kuwa ugali, kambale na mchicha anaoandaa unaweza kuwa sababu ya madhara makubwa ya kiafya kwake na familia yake kwa kuwa vyakula vyote hivi huenda vina viambata-sumu. Mahindi na mchicha vililimwa katika eneo lililo karibu na jalala ambamo zinatupwa takataka mbalimbali hatari, zikiwemo zile za kielektroniki, huku kambale akiwa amevuliwa katika bwawa lililochafuliwa na taka za aina hiyo. Fundi akitiengeneza kompyuta iliyoharibika. Picha cha Christopher Kidanka. Katika maeneo mengi, hasa mijini, wananchi hula vyakula ambavyo vina uwezekano mkubwa wa kuwa na sumu zinazotokana na taka za kielektroniki bila wao kufafahamu. Kadhalika mazingira katika maeneo hayo nayo hayako salama kutokana na taka hizo kuchafua udongo, maji, hewa na kuharibu makazi ya viumbe na kuhatarisha bioanuwai. Ongezeko la taka za kielektroniki Taka za kielektroniki ni vifaa vya elektroniki kama simu za mkononi, kompyuta, televisheni, jokofu, betri, viyoyozi, mashine za kufulia, chaja, nyaya na vifaa vingine vilivyoharibika, kupitwa na wakati au visivyotumika tena, na vinavyotupwa bila tahadhari. Kadri matumizi ya vifaa vya kielektroniki yanavyoongezeka nchini ndivyo uzalishaji wa taka hizo unavyoongezeka. Kulthum Shushu, Ofisa Mazingira wa Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC), anasema Tanzania huzalisha wastani wa tani 35,000 za taka za kielektroniki kwa mwaka, lakini ni chini ya asilimia tano tu ndiyo hurejelezwa na kuchakatwa kutokana na ukweli kuwa urejelezaji wa taka hizo hatarishi ni ghali sana. Hali hiyo, anasema, husababisha taka kujikusanya katika mazingira na mzigo wa kuzisimamia huongezeka siku&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/taka-za-kielektroniki-ni-janga-hatari-kwa-mazingira-na-afya-ya-watu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 13:46:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11131849/Screenshot-2026-06-11-161609.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1841</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Urusi, Zambia, na  Zimbabwe]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka jana, lakini uwezo wa akiba wa mitambo ya makaa ya mawe unaoweza kutumika wakati wa mahitaji makubwa ya umeme uliongezeka kwa 3.5%. Sehemu kubwa ya ongezeko hilo ilitokea nchini Uchina, ambapo uwezo wa ziada wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe unazidi kuchukuliwa kuwa chaguo mbadala ili kuhakikisha usalama wa nishati. Wakati Uchina iliongeza gigawati 78.1 za uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo 2025, matumizi yake halisi ya nishati ya makaa ya mawe yalipungua kwa 1.2%. Kupungua huku kulidhihirika wazi kwani kulikuja huku kukiwa na ongezeko la jumla la mahitaji ya nishati ya Uchina. Kulingana na ripoti hiyo, zaidi ya 90% ya ongezeko hilo la mahitaji ya nishati lilikidhiwa na nishati ya upepo na jua badala ya makaa ya mawe. Wakati Uchina inasalia kuwa mtumiaji mkubwa zaidi wa makaa ya mawe duniani, mahitaji yake zaidi ya nishati yanatimizwa kwa njia mbadala. India ilirekodi ongezeko la pili kwa ukubwa la uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo mwaka 2025, lakini pia ilionyesha harakati kuelekea gridi safi zaidi. Pamoja na nyongeza za rekodi za nishati ya jua na upepo, nishati jadidifu zilichangia zaidi ya nusu ya uwezo wa jumla wa nishati nchini kwa mara ya kwanza. Christine Shearer, mtafiti&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/#respond</comments>
					<pubDate>12 Mei 2026 04:00:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika VyawahareMary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11220722/671089-DSC_0303-5f9eed-original-1777544684-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1589</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Ubunifu wa Kijani, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wawili kutoka Kenya washinda tuzo ya Earth Prize kwa kubuni kichujio nafuu cha moshi wa magari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya: Wanafunzi wawili wenye umri wa miaka 17 kutoka kaunti ya Kiambu nchini Kenya, walitangazwa washindi wa Earth Prize kwa kanda ya Afrika mnamo Mei 12, kwa kubuni mfumo wa gharama nafuu wa kuchuja moshi wa magari unaotumia viguguta vya mahindi na maganda ya nazi wa magari walioubuni. Fredrick Njoroge Kariuki na Miron Onsarigo, wanafunzi wa taasisi ya Mpesa Foundation Academy, walitengeneza mfumo huo, HewaSafi, unaomaanisha “hewa ambayo ni safi” kwa Kiswahili, baada ya kuona marafiki na familia wakiugua maradhi yanayohusishwa na uchafuzi wa hewa. Shirika la Earth Foundation, lenye makao yake makuu nchini Uswizi, linatoa Tuzo ya Dunia, ambayo sasa iko katika mwaka wake wa tano, na inatambua vijana wenye umri wa miaka 13 hadi 19 wanaofanya kazi katika kutatua changamoto za mazingira. Timu ya HewaSafi sasa inawania tuzo ya kimataifa, ambayo upigaji kura kwa umma utafunguliwa tarehe 18 Mei, na kufungwa mnamo Mei 27. Mshindi wa toleo la kimataifa atatangazwa tarehe 29 Mei. &#8220;Tatizo la uchafuzi wa hewa lilikuwa la kibinafsi sana kwetu, na ndiyo maana tukaanza kufikiria kupata suluhu,&#8221; Kariuki aliiambia Mongabay. &#8220;Ilikuwa hamasa kubwa kabla ya kuwa mradi.&#8221; Kariuki, ambaye alikulia katika eneo lenye viwanda vingi katika Kaunti ya Nakuru nchini Kenya, alipata ugonjwa sugu wa mapafu akiwa na umri wa miaka 10 ambao bado unamhitaji kutumia dawa kila wiki. Onsarigo, ambaye alikulia magharibi mwa Kenya, alishuhudia vifo na magonjwa mabaya yanayohusiana na hewa chafu. Takwimu kutoka kwa Shirika la Afya Duniani (WHO) zinaonyesha kuwa uchafuzi wa hewa husababisha vifo vya mapema milioni 4.4 ulimwenguni kila mwaka. Moshi wa magari ni chanzo kikuu cha uchafuzi wa mazingira katika maeneo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/12/wanafunzi-wawili-kutoka-kenya-washinda-tuzo-ya-earth-prize-kwa-kubuni-kichujio-nafuu-cha-moshi-wa-magari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/#respond</comments>
					<pubDate>11 Mei 2026 15:28:34 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/11150848/Lethome-5-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1551</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Umeme, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Utunzaji wa mazingira kwa mtazamo wa Sheikh: Nafasi ya dini katika kuifanya dunia kuwa bora kimazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwezi Machi mwaka huu wa 2026 ulikuwa na shughuli nyingi, hasa kwa upande wa dini. Waislamu pamoja na baadhi ya waumini wa Kikristo walikuwa katika vipindi vya mfungo wa Ramadhani na Kwaresima, ambavyo vilihitimishwa kwa sikukuu za Iddi el-Fitri na Pasaka, mtawalia. Mwezi huohuo, Kenya ilikumbwa na mvua kubwa zilizosababisha mafuriko na vifo vya watu zaidi ya 82. Mongabay ilimtembelea Sheikh Ibrahim Lethome alipokuwa kwenye mfungo wa Ramadhani ili kupata maoni yake kuhusu juhudi zake katika kuhamasisha utunzaji wa mazingira. Lethome amejitaja kuwa aliyetekeleza kile ambacho huenda kilionekana kama jukumu dogo katika juhudi za kupinga mradi wa umeme wa makaa ya mawe huko Lamu, Kenya. Juhudi hizo ziliongozwa na viongozi wa Save Lamu pamoja na wawakilishi wa jamii, mawakili wa masuala ya mazingira, wanaharakati na taasisi za serikali pamoja na mamlaka za udhibiti kama NEMA na mahakama za mazingira. Hatimaye, mradi huo ulisitishwa Desemba mwaka 2025. Ifuatayo ni sehemu ya mahojiano yake na Lynet Otieno wa Mongabay, yaliyofanyika katika ofisi za Msikiti wa Jamiah jijini Nairobi. Mongabay: Tafadhali tueleze kwa ufupi wewe ni nani, kama msomi, kiongozi wa kidini na mwanaharakati wa mazingira. Lethome: Mimi kitaaluma ni mwanasheria na msomi wa elimu ya Kiislamu. Ninafanya kazi katika fani zote mbili. Nimekuwa mwanachama wa Msikiti wa Jamiah kwa miaka 32 sasa. Ninaongoza Idara ya Dini. Pia ni mwanachama wa bodi ya kimataifa ya GreenFaith, na mwenyekiti wa bodi ya GreenFaith-Afrika, taasisi inayotumia mafundisho ya dini kuhamasisha uhifadhi wa mazingira. Mwelekeo wangu ni kuangalia jinsi mafundisho ya dini yanavyoweza kutumika kushughulikia changamoto nyingi ambazo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/11/utunzaji-wa-mazingira-kwa-mtazamo-wa-sheikh-nafasi-ya-dini-katika-kuifanya-dunia-kuwa-bora-kimazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yaanzisha mabasi ya umeme kukabili uchafuzi wa hewa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/#respond</comments>
					<pubDate>12 Desemba 2024 17:05:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Stephanie Wangari]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/25105127/c2bb7b40-27ce-4f07-b856-41df9afa1f36-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=249</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Dioksidi ya kaboni, Maendeleo, Maendeleo Endelevu, Mafuta, Mazingira, na  Uchafuzi wa Hewa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI — Zaidi ya mabasi 22,000 huwa kwenye mitaa yenye msongamano jijini Nairobi, yakibeba sehemu kubwa ya wakazi milioni 5.3 wa mji huo mkuu wa Kenya. Mabasi ya abiria, maarufu kama matatu ya Nairobi, ambayo ni mali ya watu binafsi, yanajulikana kwa kupambwa kwa rangi kali na picha za wasanii wa muziki wa rap au [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/" data-wpel-link="internal">Kenya yaanzisha mabasi ya umeme kukabili uchafuzi wa hewa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI — Zaidi ya mabasi 22,000 huwa kwenye mitaa yenye msongamano jijini Nairobi, yakibeba sehemu kubwa ya wakazi milioni 5.3 wa mji huo mkuu wa Kenya. Mabasi ya abiria, maarufu kama matatu ya Nairobi, ambayo ni mali ya watu binafsi, yanajulikana kwa kupambwa kwa rangi kali na picha za wasanii wa muziki wa rap au vilabu vya soka vya Uingereza. Miongoni mwa haya magari yanayotumia dizeli yenye kelele nyingi na kutoa moshi mzito, sasa kuna wageni wapya 35 ambao hawana kelele; wageni hao ni mabasi ya umeme yaliyounganishwa na kampuni ya humo humo nchini iitwayo BasiGo. Kwa miaka sita sasa, Isaac Kamau amekuwa akihudumu kama dereva wa basi jijini Nairobi, akisafirisha abiria kutoka katikati mwa jiji hadi maeneo ya makazi. Mwaka 2022, alipata fursa ya kupewa mafunzo maalum ya kuendesha basi la umeme. “Kila mhitimu alitakiwa kuwa na historia nzuri ya kazi ili kupata nafasi kama hii,” Kamau aliiambia Mongabay. Mafunzo yake yalilenga zaidi uendeshaji rafiki kwa mazingira na usalama, na sasa anafurahia gari lake jipya. “Abiria wanapendelea mabasi ya umeme kuliko yale yanayotumia mafuta. Hawahitaji kushawishiwa kupanda. Yanafariji zaidi, ni ya haraka na hayana kelele.” Basi la Kamau ni miongoni mwa mabasi 35 ya umeme yanayofanya kazi jijini, huku mengine 14 yakitarajiwa kuongezwa mjini humo mwishoni mwa mwaka 2024. Kampuni ya BasiGo, ambayo huunganisha mabasi nchini Kenya kwa kutumia sehemu zinazotengenezwa na kampuni ya China ya CHTC, inasema tayari imepokea maagizo ya awali 500 kutoka kwa waendeshaji wa mabasi. Matatu za Nairobi ni zaidi ya chombo cha usafiri wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>