<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=maji-ya-kunywa&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/maji-ya-kunywa/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 16 Sep 2026 17:46:29 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/#respond</comments>
					<pubDate>26 Agosti 2026 20:21:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/26193037/Screenshot-2026-08-26-222742-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2618</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Amazon, Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kati, Amerika ya Kusini, Asia, Ethiopia, India, Sri Lanka, Ukraine, Ulaya, Ulimwenguni, na  Urusi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Halijoto, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Magonjwa, Maji, Maji ya kunywa, Mazao, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, Uhamishaji, Ukame, upatikanaji wa chakula, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), yanazihimiza mataifa kujiandaa kwa hali mbaya ya hewa na athari zitakazofuata katika sekta za afya, chakula na nishati. Tayari baadhi ya mataifa yanachukua hatua: Brazil imeajiri wazima moto wengi kupambana na moto wa misitu unaotarajiwa katika Amazon. Peru, iliyokumbwa na mvua kubwa, mafuriko na maporomoko ya ardhi katika matukio ya El Niño yaliyopita, imetangaza hali ya hatari katika 40% ya maeneo ya nchi hiyo. Sri Lanka imepanga kuwapatia maji watu karibu 72,000 katika wilaya saba zinazokabiliwa na ukame, na India inalenga wilaya 300 zinazokabiliwa na ukame, ikiimarisha mipango ya dharura ya kilimo na kuongeza mipango ya umwagiliaji. Umoja wa Afrika unatoa wito kwa nchi wanachama kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema ili kulinda &#8220;maisha, riziki na uchumi katika miezi ijayo.&#8221; Ukame mkali nchini Ethiopia  wakati wa tukio la El Niño mwaka 2015 ulisababisha mgogoro wa kibinadamu uliowaathiri zaidi ya watu milioni 10. Hapa, Umoja wa Ulaya (EU) na shirika lisilo la kiserikali la Oxfam zinasambaza lori la kusafirisha maji ili kutoa maji ya dharura nayohitajika. Picha na ©EU/ECHO/Anouk Delafortrie kupitia Flickr (CC BY-NC-ND 2.0). Hata hivyo, nchi nyingi hazijajiandaa: Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetoa wito wa dharura wa $202 milioni kwa ajili ya Wito wa pamoja wa kuchukua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/#respond</comments>
					<pubDate>04 Agosti 2026 09:15:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04091305/Screenshot-2026-08-04-121218-768x440.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2324</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Maji, Maji ya kunywa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Nishati, Samaki, Samaki wa Maji safi, Shida ya Maji, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Wakenya wanaopinga kiwanda cha nyuklia wakabiliwa na uchunguzi wa ugaidi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Maandamano yaliyozuka wakati wa mkutano wa umma kuhusu mpango wa kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia nchini Kenya yalimalizika kwa mtu kupigwa risasi na watu 17 kukamatwa. Serikali ya Kenya inakusudia kujenga kiwanda cha nguvu za nyuklia chenye uwezo wa megawati 2,000 karibu na mji wa Bondo katika Kaunti ya Siaya, kando ya Ziwa Victoria. Mnamo Julai 24, 2026, maafisa wakiwemo wawakilishi wa Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) walikuwa wakiendesha mkutano wa mashauriano ya umma mjini Bondo ndipo msukosuko ulipoanza. Dickens Ochieng’, wakili na mwanaharakati wa kijamii aliyehudhuria mkutano huo, aliiambia Mongabay kwa simu kuwa wamiliki wa ardhi walioalikwa kwenye mkutano huo wakisema &#8220;Wadagi,&#8221; neno la Kidholuo linalomaanisha &#8220;tunakataa,&#8220; kuonyesha upinzani wao dhidi ya mradi wa nyuklia. &#8220;Kisha afisa mmoja wa polisi aliyekuwa akilinda mashirika ya serikali alitumia silaha yake na kumjeruhi mtu mmoja kwa risasi, na mkutano ukageuka msukosuko papo hapo,&#8221; alisema Ochieng’. Katika siku zilizofuata, watu 17 walikamatwa na kufungwa. Hati rasmi iliyopitiwa na Mongabay inaonyesha kwamba watuhumiwa hao wanachunguzwa kwa tuhuma za shambulio na makosa chini ya Sheria ya Kuzuia Ugaidi ya Kenya (Prevention of Terrorism Act). Ochieng’, ambaye amechukua jukumu la kuwatetea kisheria, alisema &#8220;kuna ukandamizaji mkubwa unaofanywa na serikali dhidi ya wanaopinga mradi huu.&#8221; &#8220;Kama wakili, ninaendelea kuiambia jamii kwamba lazima wasimame imara, kwa sababu tuhuma za ugaidi hazina uhusiano wowote na tukio lililotokea,&#8221; alisema. &#8220;Zinakusudiwa kuwatisha na kuwanyamazisha, si kuhakikisha haki inatendeka.&#8221; Hadi sasa, watuhumiwa 15 kati ya 17 wameachiwa huru baada ya wanajamii kukusanya pesa kupitia michango ya umma ili kulipia dhamana zao, zilizowekwa kati ya KSh15,000 na KSh180,000 ($116 hadi $1,391). &#8220;Katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/04/wakenya-wanaopinga-kiwanda-cha-nyuklia-wakabiliwa-na-uchunguzi-wa-ugaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 13:35:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Claire Asher]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/03130229/Screenshot-2026-08-03-155156-768x493.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2306</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Chembechembe ndogo za plastiki, Ikolojia, Kemikali, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Plastiki, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili dawa moja au zaidi za viuavijasumu (hali inayojulikana kama usugu dhidi ya dawa za vijiumbe, au AMR) umeongezeka kwa kasi na kuwa dharura ya afya ya umma, huku sasa ukisababisha vifo takriban milioni 5 duniani kote kila mwaka. &#8220;AMR ni tishio la kibinadamu,&#8221; anasema Tim Walsh, profesa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mkurugenzi wa biolojia katika Taasisi ya Utafiti wa Antimicrobial ya Ineos Oxford ya Uingereza, ambaye alizungumza na Mongabay kupitia njia ya simu ya video. &#8220;Itaua watu wengi zaidi [kila mwaka] kuliko Kifua Kikuu, VVU na malaria, na iwapo haitapingwa inaweza kuipita saratani kama muuaji mkubwa zaidi.&#8221; Hadi hivi karibuni, migogoro hii miwili ya kimataifa, uchafuzi wa plastiki na usugu dhidi ya viuavijasumu, ilizingatiwa tofauti na wanasayansi na watunga sera. Lakini utafiti mpya unaonyesha kuwa inahusiana kwa karibu: Taka za plastiki hukaliwa kwa haraka na vijiumbe, hivyo kuunda aina mpya ya mfumo wa ikolojia unaoitwa &#8220;plastisphere.&#8221; Aidha, bakteria wanaoishi katika mfumo huo wanastawisha uwezo mkubwa wa kustahimili viuavijasumu kwa kasi isiyo na kifani. Kipande cha plastiki ya aina ya polyethylene (kinachojulikana kama &#8220;bio-bead&#8221;), kinachotumika kusaidia kuvunja-vunja uchafu katika mitambo ya kusafisha maji taka, ambacho kimekaliwa na fangasi pamoja na vijiumbe vingine. Wakati mwingine, vipande hivi vya plastiki&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/#respond</comments>
					<pubDate>30 Aprili 2026 20:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/30202905/MTERA-6-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1470</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi wa Maji, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha mapato, lakini katika miaka ya hivi karibuni hali imebadilika, samaki wamepungua kwa kiasi kikubwa majini. Kimya kimya anaijuliza, ikiwa leo hakuna samaki, kesho kutwa, mtondo na mtondogoo hali itakuwaje? Mashaka haya hayamkabili Jamal pekee, bali pia wavuvi wengi nchini kote. Kilio cha wavuvi Kilio cha wavuvi nchini Tanzania ni matokeo ya athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo yameitikisa vibaya sekta ya uvuvi kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusababisha kiwango cha samaki kupungua huku baadhi ya aina ya samaki wakitoweka kabisa. Victor Tondelo, Mtaalamu Mtafiti wa Madiliko ya Tabianchi, aliiambia Mongabay kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimejidhihirisha zaidi katika rasilimali za maji (water resources) hasa kwenye mito, mabwawa na maziwa. “Kwa sababu ya kupungua kwa mvua inayonyesha na misimu inayotabirika, maji yamepungua na hivyo idadi ya samaki ambao maisha yao ni majini pia imepungua,” alieleza. Aliongeza kuwa kuwepo kwa maji machache pia husababisha joto kubwa wakati wa kiangazi na samaki na viumbe wengine wa majini hufa kutokana na joto kali. Uchunguzi wa Mongabay kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta ya uvuvi, ulijikita katika mikoa mitatu ya Morogoro, Iringa na Pwani. Katika mkoa wa Morogoro ulihusisha mto Kilombero, Luipa, Ruhudji na Mto&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>03 Mechi 2026 19:17:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/03185644/Sehemu-ya-mtambo-wa-kuzalisha-maji-wa-Ruvu-Chini-2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1074</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Maji, Maji ya kunywa, Shida ya Maji, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya plastiki yenye maji, zinapishana mtaani. Wanawake, akiwemo Mama Amina, wanazikimbilia kununua maji ambayo yanauzwa kuanzia TSh500 hadi TSh1,000 kwa dumu lenye ujazo wa lita 20. Mama Amina ni miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, lenye wakazi karibu 7,000,000, ambao mara kwa mara hukabiliwa na uhaba wa maji. Wakati viongozi wa Serikali ya Tanzania wanahaha kutembelea vyanzo vikuu vya maji vinavyohudumia Jiji la Dar es Salaam kujionea wenyewe namna vilivyokauka, watalaam wa masuala ya maji wanasema ukame huo ambao kwa kiasi kikubwa unachochewa na mabadiliko ya tabianchi, unaweza kupatiwa ufumbuzi wa kudumu iwapo ushauri wa kitalaam utafuatwa. Jiji la Dar es salaam ndilo lenye wakazi wengi zaidi nchini Tanzania. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mkoa huo ulikuwa na watu 5,380,000, ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza uliokuwa na watu 3,690,000. Kuanzia Novemba hadi Desemba mwaka 2025, Jiji la Dar es Slaam limekumbwa na uhaba mkubwa wa maji uliosababishwa na kupungua kwa kina cha maji cha Mto Ruvu &#8211; chanzo kikuu cha maji ya jiji hilo. Hali hiyo ilisababisha watu wenye visiwa kuuza maji kwa bei ya hadi TSh1,000 (takriban $0.5) kwa dumu la lita 20. Mamlaka ya Maji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/#respond</comments>
					<pubDate>13 Januari 2026 21:05:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amos Kareithi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/14135833/Screenshot-2026-01-14-165633-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=931</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Barafu, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Milima, Misitu, Misitu ya Milimani, Miti, Samaki, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Wito wa mkwea milima wa UNEP Lewis baada ya kushuhudia barafu za mwisho za Mlima Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ndiyo nakala ya kwanza katika Mfululizo wa Mongabay – Kinachotokea mlimani hakisalii mlimani. Soma nakala ya pili hapa. Juu ya vilele vya Mlima Kenya, ambako barafu iliwahi kuonekana kama ya milele, na mito kutiririka kwa uhakika kuelekea mabonde yaliyojaa uhai, kuna ishara za hatari zinazoonekana wazi leo. Kupungua kwa barafu za mlima huu wa kihistoria hakumaanishi tu kupotea kwa mandhari ya asili, bali pia kunafungua ukurasa mpya wa changamoto kwa mazingira, mito, na jamii zinazoutegemea. Safari ya Lewis Pugh, Msimamizi wa Mradi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), hadi kwenye barafu za mwisho za Mlima Kenya, inatoa taswira ya kusikitisha ya athari halisi za mabadiliko ya tabianchi, zinazotoka juu ya mlima na kushuka hadi mashambani, misituni na vijijini, ambako maji, imani na maisha yenyewe yako hatarini. Pugh, aliyeshikilia nafasi hiyo katika shirika la UNEP tangu mwaka 2013, aliwasili nchini Kenya kwa matumaini kuwa uwezo wake wa kutoa hotuba zenye mvuto, ulioimarishwa kwa miaka 27 iliyopita, ungezivutia hisia za dunia, kwa namna fulani, kwenye athari mbaya za ongezeko la joto duniani katika eneo la Mlima Kenya. Lewis Pugh, Mwakilishi wa Bahari katika Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa (UNEP), aliyeukwea Mlima Kenya mnamo Desemba 2025. Picha na Duncan Moore, UNEP. Huku ulimwengu ukijiandaa kwa sikukuu ya Krismasi, kati ya tarehe 4 hadi tarehe 8 mwezi Desemba 2025, Pugh aliparaga kupitia miamba iliyomikali ya volkeno, baadhi ikiwa na umri wa miaka milioni 4, hadi urefu wa mita 4,985 (futi 16,355) juu ya kilele cha Lenana. Lengo lake kuu lilikuwa kuogelea katika Ziwa Lewis.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/13/mkwea-milima-wa-unep-lewis-ashuhudia-barafu-za-mwisho-za-mlima-kenya-na-kutabiri-kuwa-zitafifia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kurejesha mto nchini Kenya wajigharimia na kuleta faida zaidi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/10/29/mradi-wa-kurejesha-mto-nchini-kenya-wajigharimia-na-kuleta-faida-zaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/10/29/mradi-wa-kurejesha-mto-nchini-kenya-wajigharimia-na-kuleta-faida-zaidi/#respond</comments>
					<pubDate>29 Oktoba 2024 00:23:43 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ochieng Ogodo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/28001801/Screenshot-2025-08-28-031539-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=280</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Maji ya kunywa, Mazingira, Misitu, Mito, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi, na  Upangaji wa Miji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ugavi wa maji kwa wakazi zaidi ya milioni tano wa mji wa Nairobi na wengine milioni nne pembezoni mwa mji unategemea Mto Tana. Kwa miongo mingi sasa, upanuzi wa kilimo kwenye maeneo ya juu ya bonde la Tana umechochea ukataji wa miti na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo ambao umeharibu mashamba na kushusha ubora wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/10/29/mradi-wa-kurejesha-mto-nchini-kenya-wajigharimia-na-kuleta-faida-zaidi/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kurejesha mto nchini Kenya wajigharimia na kuleta faida zaidi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ugavi wa maji kwa wakazi zaidi ya milioni tano wa mji wa Nairobi na wengine milioni nne pembezoni mwa mji unategemea Mto Tana. Kwa miongo mingi sasa, upanuzi wa kilimo kwenye maeneo ya juu ya bonde la Tana umechochea ukataji wa miti na hivyo kusababisha mmomonyoko wa udongo ambao umeharibu mashamba na kushusha ubora wa maji ambayo wakaaji wa jiji hilo wanategemea. Kila mara udongo unaposombwa kwa kasi kipindi cha mvua kubwa, mchanga huingia mtoni na kusababisha kupungua kwa rutuba ya mashamba, huku ukiziba mabwawa ya kuzalisha umeme na miundombinu ya kusambaza maji. Mto huu unasafiri kutoka magharibi kuelekea mashariki, kupitia eneo la tambarare na milima ya Kaunti ya Garissa, ambako wafugaji wanafuga mifugo katika mazingira ya ukame ambayo pia hutegemewa na wanyamapori walio hatarini kama swala wa gerenuk na twiga wa Rothschild. Baadaye mto huo hupitia kwenye maeneo yenye misitu kabla ya kuishia kwenye delta kubwa katika Ghuba ya Ungwana. Shida zinazosababishwa na ukosefu wa misitu zimeenea na kuathiri watu wengi kwenye bonde la Tana na kwingineko. Wakazi wengi wa Nairobi hulazimika kununua maji kwa madumu ili kupata ya kunywa, kupikia na kuoga, huku viwanda na biashara vikilazimika kuwa na mipango ya dharura. Kadri idadi ya watu inavyoongezeka na mabadiliko ya tabianchi kuathiri upatikanaji wa mvua, usalama wa maji unazidi kuwa changamoto kubwa. Naabia Ofosu-Amaah, mshauri mwandamizi wa shirika la The Nature Conservancy, anasema iwapo mifumo ya maji safi haina afya, haiwezi kuwa na msingi unaohitajika na binadamu, mimea, wanyama, miji na hata uchumi. Wanyama kama swala wa gerenuk,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/10/29/mradi-wa-kurejesha-mto-nchini-kenya-wajigharimia-na-kuleta-faida-zaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/10/29/mradi-wa-kurejesha-mto-nchini-kenya-wajigharimia-na-kuleta-faida-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>