<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=mafuriko&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/mafuriko/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 06:24:00 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/#respond</comments>
					<pubDate>26 Agosti 2026 20:21:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/26193037/Screenshot-2026-08-26-222742-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2618</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Amazon, Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kati, Amerika ya Kusini, Asia, Ethiopia, India, Sri Lanka, Ukraine, Ulaya, Ulimwenguni, na  Urusi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Halijoto, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Magonjwa, Maji, Maji ya kunywa, Mazao, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, Uhamishaji, Ukame, upatikanaji wa chakula, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), yanazihimiza mataifa kujiandaa kwa hali mbaya ya hewa na athari zitakazofuata katika sekta za afya, chakula na nishati. Tayari baadhi ya mataifa yanachukua hatua: Brazil imeajiri wazima moto wengi kupambana na moto wa misitu unaotarajiwa katika Amazon. Peru, iliyokumbwa na mvua kubwa, mafuriko na maporomoko ya ardhi katika matukio ya El Niño yaliyopita, imetangaza hali ya hatari katika 40% ya maeneo ya nchi hiyo. Sri Lanka imepanga kuwapatia maji watu karibu 72,000 katika wilaya saba zinazokabiliwa na ukame, na India inalenga wilaya 300 zinazokabiliwa na ukame, ikiimarisha mipango ya dharura ya kilimo na kuongeza mipango ya umwagiliaji. Umoja wa Afrika unatoa wito kwa nchi wanachama kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema ili kulinda &#8220;maisha, riziki na uchumi katika miezi ijayo.&#8221; Ukame mkali nchini Ethiopia  wakati wa tukio la El Niño mwaka 2015 ulisababisha mgogoro wa kibinadamu uliowaathiri zaidi ya watu milioni 10. Hapa, Umoja wa Ulaya (EU) na shirika lisilo la kiserikali la Oxfam zinasambaza lori la kusafirisha maji ili kutoa maji ya dharura nayohitajika. Picha na ©EU/ECHO/Anouk Delafortrie kupitia Flickr (CC BY-NC-ND 2.0). Hata hivyo, nchi nyingi hazijajiandaa: Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetoa wito wa dharura wa $202 milioni kwa ajili ya Wito wa pamoja wa kuchukua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>22 Agosti 2026 00:16:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/21145204/Screenshot-2026-08-21-175140-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2561</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Mito, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, na  Uhalifu wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 karibu na Mto Ngong na vijito vyake, na idadi ya watu inayokadiriwa kufikia 700,000. Sehemu ya Katwekera, ndani ya Kibera, Nairobi. Picha na Mary Mwendwa, Mongabay. Katika baadhi ya maeneo ya makazi hayo, serikali ya Kenya inaendelea na ujenzi wa nyumba za bei nafuu. Mwonekano wa Kibera umeanza kubadilika. Hata hivyo, katika Gatwekera, mojawapo ya vijiji 14 vya Kibera, wakazi wa kipato cha chini wanategemea kazi za muda na biashara ndogo ndogo kando ya njia nyembamba. Asubuhi hiyo ya Jumapili, muziki mkubwa unaotoka madukani na majumbani unachanganyika na mlio wa pikipiki zinazobeba abiria na mizigo kwenye njia hizo. Licha ya msongamano huo, watu wanaonekana kuwa waangalifu. Baadhi yao walionekana kuelekea ibadani. Katikati ya msongamano huo, vijana watatu wanasukuma mkokoteni uliojaa mifuko myeusi ya plastiki iliyojaa taka, wakiteremka mteremko unaopelekea daraja la miguu ndani ya Gatwekera. Nyumba ya mwisho waliyotembelea ilikuwa ya Syprose Akinyi, iliyoko takriban mita 100 kutoka walipokuwa. Wanaelekea eneo la kukusanyia taka, ambapo taka hizo zinapangwa na baadhi yake kuuzwa kwa ajili ya kuchakatwa. Taka zilizobaki husafirishwa hadi dampo la Dandora, lililo umbali wa takriban kilomita 10, kwa kutumia magari ya serikali ya kaunti. Wanachama wa West Family Group wakipanga taka zilizokusanywa kutoka majumbani huko Gatwekera. Vijana hao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>14 Agosti 2026 00:00:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/13193448/Screenshot-2026-08-13-223025-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2467</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Madagaska, Malawi, Mauritius, na  Msumbiji]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Ikolojia, Mafuriko, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Uchimbaji Kina wa Madini ya Baharini, Uchimbaji Madini, na  Uchimbaji Madini Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari wakati wa mkutano wa mwaka wa Mamlaka ya Kimataifa ya Sakafu ya Bahari (ISA) uliofanyika Kingston, Jamaica, mwezi Julai. Zilijiunga na Malawi, Kenya na Madagaska, ambazo zilikuwa zimetangaza msimamo huo mapema. Serikali ya Mauritius ilisema wazi katika taarifa yake wakati wa mkutano huo kwamba “maendeleo endelevu ya Mauritius yanategemea kwa kiasi kikubwa bahari yenye afya na ustahimilivu”. Maafisa wake walisisitiza kwamba maamuzi kuhusu uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari lazima yafanywe kwa kuzingatia “ushahidi bora zaidi wa kisayansi unaopo na mbinu ya tahadhari, kama inavyoainishwa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari.” Malawi ilikuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari, mnamo Mei 2026. Kenya na Madagaska zilifuata msimamo huo mwezi Juni. “Msingi wa nchi hizi zote, huku zikizingatia mazingira yao ya kipekee, ni ukosefu wa ushahidi wa kutosha wa kisayansi na mapungufu ya utawala yanayoendelea,” David Willima kutoka Deep Sea Conservation Coalition (DSCC) — muungano wa mashirika zaidi ya 140 ya kiraia na asasi mbalimbali — aliiambia Mongabay kupitia barua pepe. Nchi hizo sita za Afrika ziko miongoni mwa nchi 46 duniani zinazounga mkono zuio au kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/#respond</comments>
					<pubDate>17 Julai 2026 19:39:13 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ouma Elvine Tina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/17192647/Screenshot-2026-07-17-221755.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2139</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Akili Mnemba, Biashara ya Kilimo, Chakula, Jinsia na Uhifadhi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo serikali ya ukoloni ya Uingereza iliitengea jamii ya Wanubi baada ya mababu zao kutumikia kama askari kwenye jeshi la King’s African Rifles. Awali, eneo hilo lilikuwa na ukubwa wa hekta 1,698 (ekari 4,197). Leo, kutokana na ukuaji wa miji, kufukuzwa kwa nguvu, uporaji wa ardhi na miradi mbalimbali ya serikali iliyotekelezwa kwa nyakati tofauti, ni hekta 116 (ekari 288) pekee zilizosalia mikononi mwa Wanubi, bila wao kuwahi kulipwa fidia yoyote. Kupitia Mazingira Women Initiative, Hamida ametumia zaidi ya miaka 25 kujihusisha na masuala ya usimamizi wa taka, kilimo kinachotumia teknolojia za kisasa, haki za kumiliki ardhi, na uongozi wa wanawake. Pia amewahi kugombea ubunge mara tatu katika eneo bunge la Kibera na ana mpango wa kugombea tena mwaka wa 2027. Hamida alizungumza na Mongabay mchana wa Jumamosi ya baridi, wakati alipokuwa akiondoka kwenye msikiti mkubwa zaidi katika eneo bunge la Kibera. Ofisi zake zilikuwa karibu, mwendo mfupi tu kutoka hapo. Tulipokuwa tukielekea huko, watu kadhaa walimsimamisha ili kumsalimia. Aliwajibu kila mmoja kwa kusema &#8220;Assalaamu aleikum,&#8221; akasimama kidogo ili kupiga nao gumzo, na akamshika msichana mdogo usoni kwa upole. Aliniongoza kupitia lango la mabati hadi kwenye eneo tulivu lenye nyumba zenye kuta za udongo na paa za mabati. Eneo hilo lilikuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yaadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani huku vifo kutokana na mafuriko vikifikia 81</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/#respond</comments>
					<pubDate>24 Mechi 2026 17:49:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/24174838/Vehicles-partially-submerged-in-at-a-flooded-parking-lot-in-Nairobi-Kenya-after-days-of-heavy-rainfall-on-March-06-2026.-Photo-Courtesy-of-AA.com_.tr_-1-768x487.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1212</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, na  Uhifadhi wa Misitu wa Mvua]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Machi 23, 2026 ni siku ya kuadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani kwa kutambua mchango wa sayansi katika kusaidia binadamu kuelewa na kutabiri hali ya hewa. Huku maadhimisho haya yakiendelea, familia kadhaa kutoka Mashariki mwa Kenya zinaomboleza vifo vya ndugu zao. Watu wawili waliopoteza maisha baada ya ukuta uliolowa kwa maji ya mvua kuwaangukia, na msichana mdogo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/" data-wpel-link="internal">Kenya yaadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani huku vifo kutokana na mafuriko vikifikia 81</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Machi 23, 2026 ni siku ya kuadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani kwa kutambua mchango wa sayansi katika kusaidia binadamu kuelewa na kutabiri hali ya hewa. Huku maadhimisho haya yakiendelea, familia kadhaa kutoka Mashariki mwa Kenya zinaomboleza vifo vya ndugu zao. Watu wawili waliopoteza maisha baada ya ukuta uliolowa kwa maji ya mvua kuwaangukia, na msichana mdogo pia akachukuliwa na maji alipokuwa akichunga mifugo katika eneo hilo. Katika Kaunti ya Baringo, iliyoko Bonde la Ufa, mwanamke mmoja na mtoto wa miaka minne walifariki baada ya maporomoko ya ardhi kuisomba nyumba yao. Vifo vingine vinavyohusishwa na msimu huu wa mvua vinaendelea kuripotiwa kote nchini, huku matukio ya karibuni yakifanya idadi ya vifo vilivyotokea hadi sasa kufikia 81. Kwa mujibu wa taarifa za ReliefWeb, takribani kaunti 21 kati ya 47 za nchini humo, ukiwemo mji mkuu Nairobi, zimeathirika. Taarifa hiyo imefafanua kuwa “takribani watu 70,000 wamehamishwa makazi yao”. Kabla ya kuanza kwa msimu wa mvua, Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya ilitoa tahadhari. Idara hiyo ilitabiri mvua kubwa, zaidi ya milimita 20 ndani ya saa 24 katika maeneo mbalimbali, na kutoa onyo kuhusu mafuriko, maporomoko ya ardhi, na mwonekano hafifu. Idara hiyo imeendelea kutoa utabiri zaidi wa hali ya hewa kila siku. Athari za mvua kubwa zinahusishwa na sababu mbalimbali, ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upangaji wa miji, na mabadiliko ya matumizi ya ardhi. Pia kumekuwepo madai ya mapungufu katika utawala bora, kama ilivyoripotiwa Gazeti la The Daily Nation. Wakati wa maadhimisho ya jana, Edward Muriuki, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya, alisema taasisi hiyo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>03 Mechi 2026 19:17:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/03185644/Sehemu-ya-mtambo-wa-kuzalisha-maji-wa-Ruvu-Chini-2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1074</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Maji, Maji ya kunywa, Shida ya Maji, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya plastiki yenye maji, zinapishana mtaani. Wanawake, akiwemo Mama Amina, wanazikimbilia kununua maji ambayo yanauzwa kuanzia TSh500 hadi TSh1,000 kwa dumu lenye ujazo wa lita 20. Mama Amina ni miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, lenye wakazi karibu 7,000,000, ambao mara kwa mara hukabiliwa na uhaba wa maji. Wakati viongozi wa Serikali ya Tanzania wanahaha kutembelea vyanzo vikuu vya maji vinavyohudumia Jiji la Dar es Salaam kujionea wenyewe namna vilivyokauka, watalaam wa masuala ya maji wanasema ukame huo ambao kwa kiasi kikubwa unachochewa na mabadiliko ya tabianchi, unaweza kupatiwa ufumbuzi wa kudumu iwapo ushauri wa kitalaam utafuatwa. Jiji la Dar es salaam ndilo lenye wakazi wengi zaidi nchini Tanzania. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mkoa huo ulikuwa na watu 5,380,000, ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza uliokuwa na watu 3,690,000. Kuanzia Novemba hadi Desemba mwaka 2025, Jiji la Dar es Slaam limekumbwa na uhaba mkubwa wa maji uliosababishwa na kupungua kwa kina cha maji cha Mto Ruvu &#8211; chanzo kikuu cha maji ya jiji hilo. Hali hiyo ilisababisha watu wenye visiwa kuuza maji kwa bei ya hadi TSh1,000 (takriban $0.5) kwa dumu la lita 20. Mamlaka ya Maji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kwenye mafuriko yanayohusiana na tabianchi, mto nchini Uganda wageuka kuwa sumu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/#respond</comments>
					<pubDate>05 Februari 2024 11:41:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23103154/Screenshot-2025-09-23-133105-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=426</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Hali Mbaya ya Hewa, Kemikali, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mazingira, Mito, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu majanga yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Magharibi mwa Uganda. Soma Sehemu ya Kwanza hapa.   KASESE, Uganda – Mara tu Mto Nyamwamba unapopita katika miteremko ya Milima ya Rwenzori magharibi mwa Uganda, na hatimaye kuanza kutiririka kuelekea kwenye savanna, unapita kwenye eneo la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/" data-wpel-link="internal">Kwenye mafuriko yanayohusiana na tabianchi, mto nchini Uganda wageuka kuwa sumu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu majanga yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Magharibi mwa Uganda. Soma Sehemu ya Kwanza hapa.   KASESE, Uganda – Mara tu Mto Nyamwamba unapopita katika miteremko ya Milima ya Rwenzori magharibi mwa Uganda, na hatimaye kuanza kutiririka kuelekea kwenye savanna, unapita kwenye eneo la kushangaza. Katika upande wa pili wa mto kutoka barabarani, hupita marundo ya mawe yaliyopauka kwa jua kwenye mto uliokauka, ardhi iliyoharibiwa. Kuta ndefu zinasimama wazi, zikichomoza katikati ya vilima, kana kwamba mkono wenye nguvu umechukua sehemu ya mandhari hiyo. Miamba mikali huchomoza ghafla kutoka kwenye vichaka vya kijani juu, ikishuka hadi  kwenye shimo tambarare la mchanga na mawe ya rangi ya hudhurungi. Hili ni bwawa la mabaki ya shaba. Pamoja na mabwawa mingine, linatia sumu kwenye sehemu hii ya Uganda. Mabwawa hayo yalijengwa kuhifadhi taka kutoka kwenye mgodi wa shamba uliokuwa unamilikiwa na Falconbridge, kampuni ya Canada ambayo iliendesha shughuli zake katika miteremko ya Milima ya Rwenzori kuanzia miaka ya 1950 hadi mwishoni mwa miaka ya 1970. Wakati wa enzi zake, mgodi wa shaba wa Falconbridge, ulioko kando ya barabara katika mji mdogo wa Kilembe, ulikuwa injini kuu ya uchumi wa Uganda. Mgodi huo uliwahi kuajiri zaidi ya watu 6,000 na ulichangia karibu theluthi moja ya Pato la Taifa. Falconbridge ilifukuzwa nchini Uganda na Idi Amin mwaka 1977, ambaye alitaifisha mgodi huo katika miaka ya mwisho ya utawala wake, akiwa na imani kwamba serikali yake inaweza kuuendesha pamoja na Wakanada na kuweka thamani zaidi ya shaba nyumbani.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>