<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=uchimbaji-madini&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/uchimbaji-madini/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 18 Sep 2026 20:27:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.5</generator>
				<item>
					<title>Kampuni ya Kichina ya uchimbaji wa mchanga wenye madini mazito yahusishwa na uharibifu wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>31 Agosti 2026 14:18:27 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Malavika Vyawahare]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/31140708/Screenshot-2026-08-31-170449-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2668</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Mashariki, na  Msumbiji]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Jukumu la Kampuni Katika Uhifadhi, Maji, Makampuni Yanayokiuka Sheria za Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Sehemu za Bioanuwai, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Kitropiki, na  Wajibu wa Kampuni]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ZAMBEZI, Msumbiji &#8211; Uchunguzi wa Mongabay umebaini kuwa shughuli za uchimbaji wa mchanga kando ya pwani ya Mkoa wa Zambezia, katikati mwa Msumbiji, imeharibu mamia ya hekta za misitu ya mikoko katika miaka michache tu. Eneo hilo liko chini ya leseni ya kampuni ya Mozambique Heavy Sand Company VIII, ambayo inamilikiwa kwa sehemu na Jinan Yuxiao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Kampuni ya Kichina ya uchimbaji wa mchanga wenye madini mazito yahusishwa na uharibifu wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ZAMBEZI, Msumbiji &#8211; Uchunguzi wa Mongabay umebaini kuwa shughuli za uchimbaji wa mchanga kando ya pwani ya Mkoa wa Zambezia, katikati mwa Msumbiji, imeharibu mamia ya hekta za misitu ya mikoko katika miaka michache tu. Eneo hilo liko chini ya leseni ya kampuni ya Mozambique Heavy Sand Company VIII, ambayo inamilikiwa kwa sehemu na Jinan Yuxiao Group, kampuni ya uchimbaji madini ya China yenye ushawishi mkubwa, inayodai kumiliki zaidi ya hekta 500,000 (ekari milioni 1.24) za ardhi kwa ajili ya shughuli za uchimbaji nchini Msumbiji. Maeneo hayo ya uchimbaji hulenga zaidi mchanga wenye madini mazito, ambayo huwa na madini yenye titani, hasa ilmeniti na rutaili, yanayotumika katika utengenezaji wa bidhaa mbalimbali, kuanzia rangi na plastiki hadi krimu za kujikinga dhidi ya jua. Wanaharakati wa mazingira wanatoa tahadhari kuhusu hatari zinazotokana na uchimbaji wa madini mazito kando ya pwani ya Msumbiji, na vyombo vya habari vya ndani vimeandika kuhusu tishio linaloongezeka kutokana na shughuli hiyo. &#8220;Maeneo yetu yote ya pwani yana miradi hii ya mchanga wenye madini mazito,&#8221; alisema Fatima Mimbire, mtetezi wa uwazi katika sekta ya madini nchini Msumbiji katika mahojiano na Mongabay. Aliongeza kwamba kampuni nyingi zinazochimba mchanga huo wenye madini nchini Msumbiji ni za Kichina. &#8220;Kampuni hizi zinasababisha uharibifu bila kujali mazingira wala watu wanaoathiriwa.&#8221; Global Mangrove Watch (GMW) ni jukwaa lililoundwa kufuatilia maeneo ambayo mikoko inarejea na yale ambayo inapotea, ndilo lililotoa tahadhari ya kwanza kuhusu upotevu wa mikoko katika wilaya ya Chinde mkoani Zambezia. Lammert Hilarides, mtaalamu wa uchunguzi wa Dunia kwa kutumia picha za setlaiti kutoka shirika la Wetlands International (WI),&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/31/kampuni-ya-kichina-inayoongoza-uchimbaji-wa-mchanga-wenye-madini-mazito-nchini-msumbiji-yahusishwa-na-uharibifu-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>14 Agosti 2026 00:00:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/13193448/Screenshot-2026-08-13-223025-768x442.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2467</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Kenya, Madagaska, Malawi, Mauritius, na  Msumbiji]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Bioanuai wa Baharini, Ikolojia, Mafuriko, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Uchimbaji Kina wa Madini ya Baharini, Uchimbaji Madini, na  Uchimbaji Madini Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Nchi sita za Afrika sasa zinaunga mkono kusitishwa kwa uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchi tatu zaidi za Afrika zimejiunga na wito wa kusitisha kwa tahadhari uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari, hadi athari za kimazingira, kijamii na kiuchumi za shughuli hiyo zifahamike vizuri zaidi. Hatua hii inafikisha idadi ya nchi za Afrika zinazounga mkono zuio hilo kuwa sita. Mauritius, Msumbiji na Jamhuri ya Kongo zilitangaza kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari wakati wa mkutano wa mwaka wa Mamlaka ya Kimataifa ya Sakafu ya Bahari (ISA) uliofanyika Kingston, Jamaica, mwezi Julai. Zilijiunga na Malawi, Kenya na Madagaska, ambazo zilikuwa zimetangaza msimamo huo mapema. Serikali ya Mauritius ilisema wazi katika taarifa yake wakati wa mkutano huo kwamba “maendeleo endelevu ya Mauritius yanategemea kwa kiasi kikubwa bahari yenye afya na ustahimilivu”. Maafisa wake walisisitiza kwamba maamuzi kuhusu uchimbaji wa madini katika kina kirefu cha bahari lazima yafanywe kwa kuzingatia “ushahidi bora zaidi wa kisayansi unaopo na mbinu ya tahadhari, kama inavyoainishwa katika Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Sheria ya Bahari.” Malawi ilikuwa nchi ya kwanza ya Afrika kuunga mkono kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua ya tahadhari, mnamo Mei 2026. Kenya na Madagaska zilifuata msimamo huo mwezi Juni. “Msingi wa nchi hizi zote, huku zikizingatia mazingira yao ya kipekee, ni ukosefu wa ushahidi wa kutosha wa kisayansi na mapungufu ya utawala yanayoendelea,” David Willima kutoka Deep Sea Conservation Coalition (DSCC) — muungano wa mashirika zaidi ya 140 ya kiraia na asasi mbalimbali — aliiambia Mongabay kupitia barua pepe. Nchi hizo sita za Afrika ziko miongoni mwa nchi 46 duniani zinazounga mkono zuio au kusitishwa kwa shughuli hiyo kama hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/14/nchi-sita-za-afrika-sasa-zinaunga-mkono-kusitishwa-kwa-uchimbaji-wa-madini-katika-kina-kirefu-cha-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Julai 2026 11:10:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dan Yessa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/22105214/Screenshot-2026-07-22-135015-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Elimu ya Mazingira, Gesi, Haki za Kimazingira, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Maji ya kunywa, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Misitu, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati safi, Sera za Mazingira, Shida ya Maji, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uchafuzi wa Maji, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, Uchimbaji wa Mafuta, Udanganyifu wa Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uharakati wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Umeme, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utalii wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Kupinga vitalu vipya vya mafuta katika Bonde la Kongo: Mahojiano na mwanaharakati Pascal Mirindi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pascal Mirindi ni mwanaharakati wa mazingira anayeishi Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC), na alizaliwa mjini Goma. Aliwahi kuwa mwanachama wa vuguvugu lisilotumia nguvu la La LUCHA, ambalo lilipigania demokrasia nchini DRC. Ingawa La LUCHA ndilo lililomleta kwenye harakati zisizotumia nguvu, alitumia fursa hiyo kupigania mifumo ya ikolojia ya Kongo. Tangu mwaka 2024, Mirindi amekuwa mstari wa mbele katika kupinga uchimbaji wa madini, mafuta, na gesi katika Bonde la Kongo. Kupitia kampeni na juhudi za kuielimisha jamii, wao na wenzao walifanikiwa kuzuia mipango ya utafutaji wa mafuta ndani ya Hifadhi ya Taifa ya Virunga. Kwa sasa, Mirindi anapambana dhidi ya uchimbaji katika maeneo mapya 30 ya mafuta yanayochukua asilimia 72 ya Ukanda wa Kijani wa Kongo, mradi muhimu zaidi wa uhifadhi nchini humo unaoenea katika sehemu kubwa ya Bonde la Kongo, eneo ambalo ni makazi ya maelfu ya wanyama na tegemeo muhimu kwa jamii nyingi nchini DRC. Mnamo mwezi Juni, Mirindi alizungumza na Mongabay kuhusu anachomaanisha kupinga uharibifu akiwa ndani ya nchi husika na kuleta mabadiliko katika ngazi ya kimataifa, huku akilinda makazi ya viumbe walio hatarini kutoweka kama vile sokwe wa milimani (Gorilla beringei beringei) na okapi au twiga wa msituni (Okapia johnstoni), ambao hupatikana katika eneo hilo pekee. Ziara ya kwanza ya Pascal Mirindi kwa mkurugenzi wa Hifadhi ya Taifa ya Virunga, Emmanuel de Merode, mwaka wa 2022. Picha kwa hisani ya Pascal Mirindi. Mahojiano haya yametafsiriwa kutoka Kifaransa na kuhaririwa ili kuzingatia urefu na uwazi. Mongabay: Pascal Mirindi ni nani? Pascal Mirindi: Mimi ni raia wa Kongo; nilizaliwa Goma mnamo mwaka wa 1999.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/22/kupinga-vitalu-vipya-vya-mafuta-katika-bonde-la-kongo-mahojiano-na-mwanaharakati-pascal-mirindi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, tafiti za mara kwa mara za madini katika maeneo ya uhifadhi zinaathiri mazingira?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>03 Julai 2026 14:13:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asha Bekidusa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/03133945/George-Kimau-akionyesha-eneo-la-Mrima-ambapo-ndani-ya-ardhi-hiyo-kuna-madini-ya-niobium-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1986</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Dawa ya Asili, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kuokoa Misitu, Maeneo yaliyolindwa, Milima, Misitu, Misitu ya Asili, Misitu ya Kitropiki, Misitu ya Milimani, Miti, Nyani, Sheria, Sheria ya Mazingira, Tamaduni za Kiasili, Teknolojia, Uchimbaji Madini, Uchumi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Ukataji Miti, Utafiti, Utawala, Utekelezaji wa Sheria, Vikundi vya Jamii za Asili, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa miaka mingi, Nassir Abdallah Bege amekuwa akitembea katika njia za Msitu wa Mrima, katika Kaunti ya Kwale, akiangalia ukuaji wa miti na juhudi za jamii za eneo hilo katika kuulinda. Akiwa mwenyekiti wa Muungano wa Msitu wa Kijamii wa Mrima (Mrima Community Forest Association), amekuwa nguzo muhimu katika uhifadhi wa Mrima, ulio takriban kilomita 65 kusini-magharibi mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Je, tafiti za mara kwa mara za madini katika maeneo ya uhifadhi zinaathiri mazingira?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa miaka mingi, Nassir Abdallah Bege amekuwa akitembea katika njia za Msitu wa Mrima, katika Kaunti ya Kwale, akiangalia ukuaji wa miti na juhudi za jamii za eneo hilo katika kuulinda. Akiwa mwenyekiti wa Muungano wa Msitu wa Kijamii wa Mrima (Mrima Community Forest Association), amekuwa nguzo muhimu katika uhifadhi wa Mrima, ulio takriban kilomita 65 kusini-magharibi mwa Mombasa. Anakumbuka mashimo yaliyoachwa baada ya baadhi ya sehemu za msitu kukatwa wakati kampuni zilipokuwa zikifanya tafiti za kutafuta madini. Zaidi ya mwongo mmoja baadaye, anasema, mashimo hayo yanaendelea kujiziba yenyewe. Ukitembea msituni, si rahisi kuona mashimo hayo madogo kwani yamefinikwa, baada ya mimea ya asili kuota tena kwa zaidi ya muongo mmoja. Mrima. Picha na Asha Bekidusa, Mongabay. Neno ‘Mrima’ linatoka katika jamii ya Wadigo, kumaanisha mlima. Msitu huu wa Mrima una rutuba kubwa na bioanuwai ya kipekee. Kadri unavyozidi kupanda mlimani, msitu huwa mnene zaidi na mwanga hupungua. Eneo hili liko kimya, isipokuwa sauti za wanyama, wadudu na miti ambayo mara kwa mara inatikisika kutokana na upepo unaovuma. Kwa mujibu wa Key Biodiversity Areas (KBA), eneo la Mrima lenye umuhimu wa bioanuwai lina ukubwa wa takriban kilomita za mraba 3.76 (sawa na takriban hekta 376), ambapo asilimia 95.77 ya eneo hilo iko chini ya hadhi mbalimbali za ulinzi wa kisheria. Utafiti na uharibifu wa misitu Kutokea miaka ya 1950, wataalamu wa jiolojia na makampuni ya madini wamekuwa wakifanya tafiti katika eneo la Mrima kutathmini uwepo wa madini ya niobium na madini adimu mengine. Stakabadhi za rekodi za kesi ya kampuni ya Cortec zinaonyesha kuwa utafiti wa awali ulifanywa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/03/je-tafiti-za-mara-kwa-mara-za-madini-katika-maeneo-ya-uhifadhi-zinaathiri-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kufutwa kwa leseni 40 za utafiti wa madini Tanzania kwafichua ukweli wa athari za mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/#respond</comments>
					<pubDate>28 Aprili 2026 21:53:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Nkwimba Nkwimba]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/28213333/Madini-3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1452</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Ikolojia, Kijani, Mazingira, Misitu, Uchimbaji Dhahabu, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Sekta ya madini nchini Tanzania imetikiswa na hatua ya Serikali kuzifutia leseni za utafiti wa madini kampuni 40 huku ikitoa muda wa siku 30 kwa kampuni nyingine 43 kurekebisha mapungufu yao, la sivyo nazo zitapoteza leseni zao. Wakati watu wengi wameunga mkono hatua hiyo kwa kuangalia matokeo ya uamuzi huo kwa mtazamo wa kiuchumi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/" data-wpel-link="internal">Kufutwa kwa leseni 40 za utafiti wa madini Tanzania kwafichua ukweli wa athari za mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Sekta ya madini nchini Tanzania imetikiswa na hatua ya Serikali kuzifutia leseni za utafiti wa madini kampuni 40 huku ikitoa muda wa siku 30 kwa kampuni nyingine 43 kurekebisha mapungufu yao, la sivyo nazo zitapoteza leseni zao. Wakati watu wengi wameunga mkono hatua hiyo kwa kuangalia matokeo ya uamuzi huo kwa mtazamo wa kiuchumi na uwajibikaji, watetezi wa mazingira wameibua hoja nzito kuhusu uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokea pindi leseni za utafiti zinapotelekezwa. Waziri wa Madini Antony Mavunde, katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika makao makuu ya Tanzania, jijini Dodoma, alitaja mambo kadhaa ambayo kampuni hizo zimeshindwa kutekeleza licha ya kupewa onyo na muda wa kurekebisha kasoro zilizobainishwa. Alibainisha kuwa leseni hizo zilifutwa kufuatia ukiukwaji mkubwa wa masharti, ikiwemo kuhodhi maeneo bila kuyaendeleza, kushindwa kulipa ada stahiki, kutotekeleza wajibu wa ushirikishwaji wa Watanzania pamoja na kupuuza miradi ya uwajibikaji kwa jamii. “Tunashuhudia baadhi ya watu wanamiliki leseni kwa miaka mingi bila uwekezaji wowote unaoonekana. Hii si tu inapoteza fursa za kiuchumi bali pia inachochea uharibifu wa mazingira na migogoro katika jamii,” alisema Waziri. Kwa mujibu wa waziri huyo, leseni 40 za utafiti wa madini zilizofutwa ni sawa na eneo lenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 900 sawa na hekari 188,163. Uharibirifu wa mazingira Simulizi za watu tofauti wakiwemo wachimbaji wadogo katika maeneo mbalimbali zinaonyesha jinsi mazingira yanavyoharibiwa iwe katika hatua ya utafiti wa madini ama uchimbaji wenyewe. “Usiku mvua ikinyesha kidogo tu… asubuhi tunakuta shimo limejaa maji na kuta zimeporomoka,” anasema Emmanuel Joseph, mchimbaji mdogo katika Mkoa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kwenye mafuriko yanayohusiana na tabianchi, mto nchini Uganda wageuka kuwa sumu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/#respond</comments>
					<pubDate>05 Februari 2024 11:41:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23103154/Screenshot-2025-09-23-133105-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=426</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Hali Mbaya ya Hewa, Kemikali, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mazingira, Mito, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu majanga yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Magharibi mwa Uganda. Soma Sehemu ya Kwanza hapa.   KASESE, Uganda – Mara tu Mto Nyamwamba unapopita katika miteremko ya Milima ya Rwenzori magharibi mwa Uganda, na hatimaye kuanza kutiririka kuelekea kwenye savanna, unapita kwenye eneo la [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/" data-wpel-link="internal">Kwenye mafuriko yanayohusiana na tabianchi, mto nchini Uganda wageuka kuwa sumu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni sehemu ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu majanga yanayohusiana na mabadiliko ya tabianchi katika maeneo ya Magharibi mwa Uganda. Soma Sehemu ya Kwanza hapa.   KASESE, Uganda – Mara tu Mto Nyamwamba unapopita katika miteremko ya Milima ya Rwenzori magharibi mwa Uganda, na hatimaye kuanza kutiririka kuelekea kwenye savanna, unapita kwenye eneo la kushangaza. Katika upande wa pili wa mto kutoka barabarani, hupita marundo ya mawe yaliyopauka kwa jua kwenye mto uliokauka, ardhi iliyoharibiwa. Kuta ndefu zinasimama wazi, zikichomoza katikati ya vilima, kana kwamba mkono wenye nguvu umechukua sehemu ya mandhari hiyo. Miamba mikali huchomoza ghafla kutoka kwenye vichaka vya kijani juu, ikishuka hadi  kwenye shimo tambarare la mchanga na mawe ya rangi ya hudhurungi. Hili ni bwawa la mabaki ya shaba. Pamoja na mabwawa mingine, linatia sumu kwenye sehemu hii ya Uganda. Mabwawa hayo yalijengwa kuhifadhi taka kutoka kwenye mgodi wa shamba uliokuwa unamilikiwa na Falconbridge, kampuni ya Canada ambayo iliendesha shughuli zake katika miteremko ya Milima ya Rwenzori kuanzia miaka ya 1950 hadi mwishoni mwa miaka ya 1970. Wakati wa enzi zake, mgodi wa shaba wa Falconbridge, ulioko kando ya barabara katika mji mdogo wa Kilembe, ulikuwa injini kuu ya uchumi wa Uganda. Mgodi huo uliwahi kuajiri zaidi ya watu 6,000 na ulichangia karibu theluthi moja ya Pato la Taifa. Falconbridge ilifukuzwa nchini Uganda na Idi Amin mwaka 1977, ambaye alitaifisha mgodi huo katika miaka ya mwisho ya utawala wake, akiwa na imani kwamba serikali yake inaweza kuuendesha pamoja na Wakanada na kuweka thamani zaidi ya shaba nyumbani.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/02/05/kwenye-mafuriko-yanayohusiana-na-tabianchi-mto-nchini-uganda-wageuka-kuwa-sumu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>