<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=plastiki&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/plastiki/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 09 Sep 2026 10:27:30 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/#respond</comments>
					<pubDate>22 Agosti 2026 00:16:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Mwendwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/21145204/Screenshot-2026-08-21-175140-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2561</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Mito, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, na  Uhalifu wa Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Ndani ya Kibera, vijana wageuza mapambano dhidi ya taka kuwa kinga dhidi ya mafuriko </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIBERA, Kenya — Safu za paa za bati, kuta za udongo na njia nyembamba zilizojaa watu ndizo unazokutana nazo unapofika katika eneo hili mashariki mwa Mto Ngong. Hii ni Kibera, mojawapo ya makazi duni makubwa barani Afrika, yaliyoko kilomita sita kutoka katikati ya mji mkuu wa Kenya. Makazi hayo yanaenea katika eneo la hekta 225 karibu na Mto Ngong na vijito vyake, na idadi ya watu inayokadiriwa kufikia 700,000. Sehemu ya Katwekera, ndani ya Kibera, Nairobi. Picha na Mary Mwendwa, Mongabay. Katika baadhi ya maeneo ya makazi hayo, serikali ya Kenya inaendelea na ujenzi wa nyumba za bei nafuu. Mwonekano wa Kibera umeanza kubadilika. Hata hivyo, katika Gatwekera, mojawapo ya vijiji 14 vya Kibera, wakazi wa kipato cha chini wanategemea kazi za muda na biashara ndogo ndogo kando ya njia nyembamba. Asubuhi hiyo ya Jumapili, muziki mkubwa unaotoka madukani na majumbani unachanganyika na mlio wa pikipiki zinazobeba abiria na mizigo kwenye njia hizo. Licha ya msongamano huo, watu wanaonekana kuwa waangalifu. Baadhi yao walionekana kuelekea ibadani. Katikati ya msongamano huo, vijana watatu wanasukuma mkokoteni uliojaa mifuko myeusi ya plastiki iliyojaa taka, wakiteremka mteremko unaopelekea daraja la miguu ndani ya Gatwekera. Nyumba ya mwisho waliyotembelea ilikuwa ya Syprose Akinyi, iliyoko takriban mita 100 kutoka walipokuwa. Wanaelekea eneo la kukusanyia taka, ambapo taka hizo zinapangwa na baadhi yake kuuzwa kwa ajili ya kuchakatwa. Taka zilizobaki husafirishwa hadi dampo la Dandora, lililo umbali wa takriban kilomita 10, kwa kutumia magari ya serikali ya kaunti. Wanachama wa West Family Group wakipanga taka zilizokusanywa kutoka majumbani huko Gatwekera. Vijana hao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/22/ndani-ya-kibera-vijana-wageuza-mapambano-dhidi-ya-taka-kuwa-kinga-dhidi-ya-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/#respond</comments>
					<pubDate>03 Agosti 2026 13:35:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Claire Asher]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/03130229/Screenshot-2026-08-03-155156-768x493.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2306</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Chembechembe ndogo za plastiki, Ikolojia, Kemikali, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Plastiki, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Tafiti: Uchafuzi wa plastiki ndogondogo unaweza kuchochea ongezeko la usugu dhidi ya antibiotiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uchafuzi wa plastiki ni miongoni mwa majanga makubwa zaidi ya kimazingira yanayolikabili wanadamu. Uzalishaji wa plastiki tangu mwaka 1950 umezidi tani milioni 8,300, huku sehemu kubwa ya taka za plastiki ikiishia katika mazingira na kuathiri wanyamapori, utendaji kazi wa mfumo wa ikolojia, pamoja na afya ya binadamu. Sambamba na hayo, uwezo wa bakteria wanaosababisha magonjwa kustahimili dawa moja au zaidi za viuavijasumu (hali inayojulikana kama usugu dhidi ya dawa za vijiumbe, au AMR) umeongezeka kwa kasi na kuwa dharura ya afya ya umma, huku sasa ukisababisha vifo takriban milioni 5 duniani kote kila mwaka. &#8220;AMR ni tishio la kibinadamu,&#8221; anasema Tim Walsh, profesa katika Chuo Kikuu cha Oxford na mkurugenzi wa biolojia katika Taasisi ya Utafiti wa Antimicrobial ya Ineos Oxford ya Uingereza, ambaye alizungumza na Mongabay kupitia njia ya simu ya video. &#8220;Itaua watu wengi zaidi [kila mwaka] kuliko Kifua Kikuu, VVU na malaria, na iwapo haitapingwa inaweza kuipita saratani kama muuaji mkubwa zaidi.&#8221; Hadi hivi karibuni, migogoro hii miwili ya kimataifa, uchafuzi wa plastiki na usugu dhidi ya viuavijasumu, ilizingatiwa tofauti na wanasayansi na watunga sera. Lakini utafiti mpya unaonyesha kuwa inahusiana kwa karibu: Taka za plastiki hukaliwa kwa haraka na vijiumbe, hivyo kuunda aina mpya ya mfumo wa ikolojia unaoitwa &#8220;plastisphere.&#8221; Aidha, bakteria wanaoishi katika mfumo huo wanastawisha uwezo mkubwa wa kustahimili viuavijasumu kwa kasi isiyo na kifani. Kipande cha plastiki ya aina ya polyethylene (kinachojulikana kama &#8220;bio-bead&#8221;), kinachotumika kusaidia kuvunja-vunja uchafu katika mitambo ya kusafisha maji taka, ambacho kimekaliwa na fangasi pamoja na vijiumbe vingine. Wakati mwingine, vipande hivi vya plastiki&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/03/uchafuzi-wa-plastiki-ndogondogo-unaweza-kuchochea-ongezeko-la-usugu-dhidi-ya-dawa-za-viuavijasumu-tafiti-zinaonyesha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>13 Julai 2026 16:04:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/13150952/Screenshot-2026-07-13-180713-768x466.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2039</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chembechembe ndogo za plastiki, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Plastiki, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Samaki wa Maji safi, Sehemu za Bioanuwai, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, na  Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">‘Mpito wa pekee unaowezekana ni mpito wa haki’: Mahojiano na Clemence Schmid wa WEF</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa Mkutano wa 11 wa Our Ocean uliofanyika katika jiji la pwani la Mombasa, serikali ya Kenya, pamoja na Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (GPAP) wa Jukwaa la Uchumi Duniani na UNDP Kenya, walizindua rasmi Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki wa Kenya (NPAP Kenya). Takriban tani milioni 14 za plastiki huishia baharini kila mwaka na zinachangia 80% ya uchafu wote wa baharini unaopatikana katika uso wa bahari na mashapo ya bahari kuu. Kenya inakabiliwa na changamoto kubwa za uchafuzi wa plastiki, haswa katika vituo vya mijini na kando ya pwani yake. Plastiki huchangia takriban 20% ya tani 22,000 za taka zinazozalishwa kila siku nchini Kenya, kulingana na makadirio. Ni 27% tu ya taka za plastiki zinakusanywa, ambapo 8% huchakatwa tena na 19% zilizobaki hutupwa katika majaa ya taka au madampo holela. Taka za plastiki ambazo hazijakusanywa na kusimamiwa vyema mara nyingi huishia kwenye mito na baharini. Huvuruga mifumo ikolojia, huhatarisha wanyamapori, na huathiri utalii na uvuvi. Mwaka wa 2017, Kenya ilianzisha marufuku ya matumizi, utengenezaji na uingizaji wa mifuko ya plastiki ya matumizi ya mara moja. Mnamo 2020, marufuku hiyo iliongezwa hadi plastiki zinazotumika mara moja katika maeneo yaliyohifadhiwa. Ushirikiano wa Kitaifa wa Hatua Dhidi ya Plastiki (NPAP Kenya) utasaidia kuharakisha mpito wa nchi hiyo kuelekea uchumi wa plastiki wa mviringo, kulingana na Clemence Schmid, Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua dhidi ya Plastiki (Global Plastic Action Partnership – GPAP) katika Jukwaa la Uchumi Duniani (World Economic Forum – WEF). Mkurugenzi wa Ushirikiano wa Kimataifa wa Hatua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/13/mpito-wa-pekee-unaowezekana-ni-mpito-wa-haki-mahojiano-na-clemence-schmid-wa-jukwaa-la-uchumi-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 12:56:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Penzi Nyamungumi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03130042/Screenshot-2026-06-03-160011.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1754</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Mazingira, Plastiki, Sheria ya Mazingira, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa kwenye mifereji zimekuwa zikiziba njia za maji na kuchangia mafuriko. Aidha, chupa zinapochomwa, moshi wake husababisha maradhi na pia kuathiri mazingira kutokana na asili yake ya kuchelewa kuoza. Hata hivyo, kuibuka na kukua kwa biashara ya chupa za plastiki zilizotumika, ambayo mara nyingi hufanywa na akinamama na vijana, kunaendelea kubadilisha historia. Hivi sasa badala ya kushuhudia barabara zenye mifereji iliyojaa chupa tupu, kinachoonekana ni akinamama na vijana waliobeba viroba vikubwa vyenye chupa hizo. Wakusanyaji wadogo huuza chupa hizo kwa wakusanyaji wakubwa au kwa kampuni zinazojishughulisha na ukusanyaji na urejelezaji wa chupa hizo baada ya matumizi. Taimuru Hamad, Meneja Uzingatiaji Sheria kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), anakiri kwamba biashara hiyo imeleta faida kubwa katika ustawi na ulinzi wa mazingira. Chupa za plastiki zilizokusanywa kutoka maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam zikiwa zimefungwa kwenye mifuko mikubwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wanunuzi. Picha na Joyce Bazira. “Kuokotwa kwa hizi chupa kunasaidia sana. Kwanza, kunasaidia katika suala zima la ustawi wa mazingira, lakini pia kwenye suala la usafi. Kama zingekuwa haziokotwi, mazingira yangeendelea kuathirika sana na pia yangekuwa machafu sana,” alisema Taimuru katika mahojiano na Mongabay. Chupa za rangi Pamoja na kazi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>15 Oktoba 2025 07:04:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/07070649/Screenshot-2025-11-07-100242-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=743</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Biashara, Chakula, Chembechembe ndogo za plastiki, Kanuni, Kemikali, Magonjwa, Mazingira, Ndege, Plastiki, Taka, Uchafuzi, Uhifadhi, upatikanaji wa chakula, Utafiti, na  Utandawazi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Viwango vya ‘kutisha’ vya sumu vyapatikana kwenye mayai ya kuku wa kienyeji karibu na majaa ya taka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Utafiti wa hivi majuzi umepata kuona uwepo wa viwango &#8220;vya kutisha&#8221; vya kemikali zenye sumu katika mayai ya kuku wa kienyeji ulimwenguni. Ugunduzi huo unatokana na zaidi ya muongo mmoja wa uchanganuzi wa mayai katika mabara matano, ambayo yaligundua mayai yaliyochafuliwa na vizuia moto vilivyopigwa marufuku kimataifa, na haswa dioksini zilizo na bromini, ambazo ni sumu kwa afya ya binadamu na mazingira. Sehemu za uchafu wa kielektroniki, majaa ya taka na vichomea taka ni vyanzo muhimu vya uchafuzi huu, huku mayai yaliyofanyiwa utafiti katika maeneo jirani yakipatikana kuwa yamechafuliwa sana na kemikali zinazotolewa wakati taka za plastiki zinachomwa. Sampuli ya mayai yaliyotolewa karibu na maeneo ya taka za kielektroniki nchini Ghana mwaka wa 2019, kwa mfano, yalikuwa na viwango vya dioksini za bromini iliochanganywa na klorini mara 200 zaidi ya kiwango cha usalama cha chakula. Uzalishaji na matumizi ya kimakusudi ya dioksini umeondolewa au kuwekewa vikwazo vikali ulimwenguni kote chini ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Stockholm kuhusu vichafuzi vinavyoendelea vya kikaboni (POPs). Utafiti huo, uliochapishwa katika jarida la Emerging Contaminants, uliongozwa na Mtandao wa Kimataifa wa Kutokomeza Uchafuzi (IPEN), pamoja na shirika lisilo la serikali la Czech Arnika na timu ya wanasayansi wa kimataifa. Utafiti huo ulikuwa wa kina, na data ya sumu ya yai iliyokusanywa katika nchi nyingi zinazoendelea, na nchi zilizo na uchumi wa mpito, barani Afrika, Asia, Amerika Kaskazini na Kusini na Ulaya. Matokeo hayo yanahusu sana, waandishi wa utafiti wanasema, kwani mayai ni chanzo muhimu cha protini katika nchi za kipato cha chini na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/viwango-vya-kutisha-vya-sumu-vipatikanavyo-kwenye-mayai-ya-kuku-wa-kienyeji-karibu-na-majaa-ya-taka-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi vijana ndugu walivyolinusuru Ziwa Victoria kutokana na hatari ya plastiki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/#respond</comments>
					<pubDate>31 Julai 2024 19:43:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Juliet Akoth Ojwang]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23194526/Screenshot-2025-09-23-224502-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=488</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Haki ya Tabianchi, Hali ya Hewa, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Plastiki, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika miaka ya karibuni vijana kutoka ulimwenguni kote wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Vijana hawa wenye viwango mbalimbali vya elimu katika masuala hayo wamefanya kazi kubwa ya kuelimisha na kuhamasisha vijana wengine wa rika yao ili washiriki kikamilifu katika kampeni mbalimbali za kuhakikisha kuwa maisha yajayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/" data-wpel-link="internal">Jinsi vijana ndugu walivyolinusuru Ziwa Victoria kutokana na hatari ya plastiki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika miaka ya karibuni vijana kutoka ulimwenguni kote wamekuwa mstari wa mbele katika kupambana na uharibifu wa mazingira na mabadiliko ya tabianchi. Vijana hawa wenye viwango mbalimbali vya elimu katika masuala hayo wamefanya kazi kubwa ya kuelimisha na kuhamasisha vijana wengine wa rika yao ili washiriki kikamilifu katika kampeni mbalimbali za kuhakikisha kuwa maisha yajayo yanakuwa endelevu. Mfano mzuri ni vijana kutoka familia moja huko Kenya, Michelle na Jeremy Muchilwa,  wenye umri wa miaka 19 na 16, ambao walianzisha shirika la Osiepe Sango (Marafiki wa Ziwa Victoria) lenye lengo la kuondoa uchafu wa plastiki katika Ziwa Victoria ambalo ndilo kubwa kuliko maziwa yote ya maji safi barani Afrika. Ziwa hili pia limetanda katika nchi tatu za Afrika Mashariki; Kenya, Uganda na Tanzania. Wakati ugonjwa wa UVICO-19 ulipojitokeza mwaka 2020, mwezi Machi, shule nchini Kenya zilifungwa. Michelle alikuwa na umri wa miaka 15 na Jeremy miaka 12. Vijana hao waliona hii kama fursa kwao na waliporuhusiwa na wazazi wao, walijikita katika mambo waliyoyapenda badala ya kuendelea na masomo kwa njia ya mtandao. Jeremy alizama katika mambo ya teknolojia ambayo alikuwa akiyapenda, akijifunza kutengeneza programu mbalimbali. Michelle alijikita kwenye mifumo mbalimbali ya kiteknologia kupitia programu ya TED-Ed art school, ambayo ilimpa mwanga kuhusu bayoanuai, ikolojia na masuala ya mazingira katika ulimwengu. Somo moja kuhusu maji lilijadili umuhimu wa bahari, mifumo ya vyanzo vya maji baridi na kuonyesha uchafuzi unaotokana na takataka za plastiki. Michelle alihamasika na akapata habari za Ocean Heroes Boot Camp, mafunzo kuhusu uchafuzi wa mazingira unaotokana na takataka za plastiki na akaomba kushiriki. Alimshawishi pia&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/07/31/jinsi-vijana-ndugu-walivyolinusuru-ziwa-victoria-kutokana-na-hatari-ya-plastiki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>