<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=siasa-za-nishati&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/siasa-za-nishati/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 16 Sep 2026 17:46:29 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 12:22:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30073721/Magari2-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2264</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Halijoto, Kaboni, Mabadiliko ya Tabianchi, Maliasili, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Siasa za Tabianchi, Teknolojia, Uendelevu, na  Ufanisi wa nishati]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya kuhamia matumizi ya nishati safi kwenye vyombo vya usafiri kwa kuzielekeza taasisi zote za umma kuanza kujumuisha ununuzi wa magari yanayotumia umeme na gesi asilia katika mipango na bajeti zao. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omari, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupunguza gharama kubwa za kununua mafuta. Bajaji zinazotumia umeme. Picha ya Jenifer Gilla, Mongabay. Hatua hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050  na Michango ya Taifa Iliyoamuliwa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris ambapo Tanzania imeahidi kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kupitia sekta za nishati na usafiri. Uzalishaji wa hewa ya ukaa Mpango wa kutumia nishati safi kwenye vyombo vya usafiri nchini Tanzania, iwapo utafanikiwa, utapunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi. Msololo Onditi, Mtaalam wa mabadiliko ya tabianchi na Mshauri wa Masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika Shirika la Maendeleo la Ujerumani Tanzania (GIZ), anasema kila lita moja ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>16 Julai 2026 18:48:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Amina Chombo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/16182830/Dangote-thehabarinetwork-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2128</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mashirika, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mifumo ya Ikolojia, Misitu, Nishati, Samaki, Serikali, Siasa za Nishati, Spishi, Uanaharakati, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi, Uharakati wa Mazingira, Utawala, Uvuvi, na  Viwanda]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mradi wa kiwanda cha kusafisha mafuta Lamu wazua hofu za wanaharakati wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[LAMU, Kenya – Pendekezo la bilionea wa Nigeria Aliko Dangote kujenga kiwanda cha kusafisha mafuta cha $17 bilioni katika Kaunti ya Lamu, nchini Kenya, limezua mjadala mkali, huku serikali ikikitaja kama kichocheo cha uchumi, na wanaharakati wakionya kuhusu athari zake kwa ikolojia na maisha ya jamii za pwani. Dangote achagua Kenya Baada ya miezi kadhaa ya uvumi kuhusu iwapo kiwanda hicho kingejengwa Kenya, Uganda au Tanzania, kampuni ya Dangote Industries ilichagua Kenya kuwa mwenyeji wa uwekezaji huo. Katika ripoti iliyochapishwa na Reuters, Makamu Rais wa Kitengo cha Mafuta na Gesi wa Dangote Industries Limited, Edwin Devakumar, alithibitisha kuwa kiwanda hicho chenye uwezo wa kusafisha mapipa 700,000 ya mafuta ghafi kwa siku kitajengwa katika Kisiwa cha Lamu na kinatarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu. Mafuta ghafi yanatarajiwa kupatikana kutoka nchi za Afrika Mashariki, zikiwemo Uganda, Sudan Kusini na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Iwapo mradi huo utakamilika, utafuata mfano wa kiwanda cha Dangote kilichopo karibu na Lagos, Nigeria, chenye uwezo wa kusafisha mapipa 650,000 kwa siku, na ambacho kilianza uzalishaji mwaka 2024 na ndicho kikubwa zaidi barani Afrika. Serikali yaeleza manufaa Rais William Ruto, akimteua naibu wake Kithure Kindiki kusimamia mradi huo, alisema Kenya imefikia makubaliano na Dangote ya kuendeleza mradi wa ujenzi wa kiwanda cha kusafisha mafuta. Rais wa Kenya, William Ruto, akizungumza katika ikulu ya Nairobi mnamo Julai 8, 2026. Picha kwa hisani ya PSC. Kwa mujibu wa Ruto, kiwanda hicho kitahudumia masoko ya Afrika Mashariki na Afrika ya Kati, na kinatarajiwa kuunda takribani nafasi za ajira 60,000 wakati wa ujenzi na uendeshaji wake. Wanaharakati wapinga Wakati serikali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/16/mradi-wa-kiwanda-cha-kusafisha-mafuta-lamu-wazua-hofu-za-wanaharakati-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 20:21:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05201200/Screenshot-2026-06-05-231142-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1791</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Nishati, Siasa za Nishati, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana kama “Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk” pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa sakafu ya bahari (deep-sea mining) pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Ripoti hiyo ilitolewa Juni 4, 2026 na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani inayoadhimishwa Juni 8. Ripoti iliandaliwa kutokana na utafiti uliohusisha nchi 11 kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Katika utafiti huo, Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Nchi nyingine zilizotajwa ni Kenya, Australia, Cameroon, Indonesia, Jamaica, Norway, Trinidad na Tobago, Argentina na Mexico. Kwa Tanzania, mradi huo unapangwa kujengwa katika eneo la Likong’o, kusini mwa mkoa wa Lindi. Lengo ni kuchakata gesi asilia inayopatikana baharini na kuibadilisha kuwa gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Ripoti hiyo imetolewa siku chache baada ya Waziri wa Nishati, Dkt Deogratius Ndejembi, kuliambia Bunge kwamba makubaliano ya kibiashara na kodi kati ya serikali na wawekezaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mei 2026 17:35:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/26172956/Usenge-Beach-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1717</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Nishati ya Jua, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya nyuklia wenye thamani ya shilingi bilioni 500 za Kenya katika kaunti ya Siaya. “Kama wakala wa nishati ya nyuklia, tunasikia na kuheshimu sauti za wakazi wa Siaya. Ushiriki wa umma si jambo la kufuata taratibu tu. Ni haki ya kikatiba,” shirika hilo lilisema katika taarifa yake. Taarifa hiyo ilitolewa siku mbili baada ya wakazi wa Sakwa, Bondo katika Kaunti ya Siaya inayopakana na Ziwa Victoria, kuandamana kupinga mradi huo. Wakazi hao walieleza hofu kuhusu hatari za kimazingira iwapo ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika na lenye utajiri mkubwa wa ikolojia litachafuliwa. Pia walitaja hofu ya kupoteza riziki, chakula na mahitaji mengine muhimu. Katika taarifa yake ya kujibu maandamano hayo, iliyotiwa saini na Afisa Mkuu Mtendaji wa NuPEA, Justus Wabuyabom, shirika hilo lilisema kuwa ujenzi wa mradi huo hautaanza hadi wakazi wa Siaya waelimishwe kikamilifu na wakubaliane na mradi huo. NuPEA kubadili mkakati NuPEA iliongeza kuwa itabadilisha mkakati wake “kutoka mipango ya kitaasisi ya ngazi za juu kwenda katika uhamasishaji wa kina kwa wananchi wa vijijini” kuhusu mradi huo unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,000. Wakati huohuo, Power Shift Africa (PSA) imekosoa msisitizo wa kutumia nishati ya nyuklia kama chanzo cha umeme, ikisema kuwa hatua hiyo inaweza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 22:09:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31212151/MSARAZA-PWANI-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1301</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Misitu, Miti, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka 1998.  Sera hii imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara ili kukabiliana na changamoto za wakati huu, na pitio la mwisho lilifanyika mwaka 2017. Miongoni mwa hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa, Kideghesho anasema ni pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kama gesi na gesi asilia, gesi inayotokana na kinyesi cha wanyama. Taarifa zaidi zinaonyesha serikali imedhamiria kurejesha misitu katika eneo la hekta milioni 5.2 ambalo ardhi yake imepoteza ubora kutokana na kukatwa miti hovyo. Kuanzia mwaka 2023, serikali kwa kushirikiana na asasi za kiraia imekuwa ikitekeleza mradi mkubwa wa mageuzi ya matumizi ya nishati itokanayo na miti wenye lengo la kuboresha usimamizi na uvunaji endelevu wa misitu. Wanakijiji wa Msaraza Wilaya ya Pangani wakiandaa udongo kwaajili ya kutengeneza vitalu vya mitiche ya miti ya asili. Picha kwa hisani ya CAN Tanzania. Mradi wa Mchakato Jumuishi wa Kuleta Mabadiliko Katika Mnyororo wa Thamani wa Nishati ya Kuni (Integrated Approach for Transformation of Tanzania Fuel Wood Value Chain Project), ni mmoja wa miradi inayolenga kuboresha ustawi wa jamii zilizo pembezoni na kuhifadhi na kulinda misitu. Mradi huo unaotekelezwa katika wilaya 16 zilizopo kwenye mikoa ya Tabora, Dar es Salaam, Mwanza, Pwani, Tanga na Morogoro, unafadhiliwa na Umoja wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>