<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=migogoro&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/migogoro/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 14:23:41 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/#respond</comments>
					<pubDate>14 Julai 2026 13:43:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Brown]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/04134630/Screenshot-2026-08-04-164214.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2344</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ajabu, Migogoro, Sokwe, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Maadhimisho ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Heri ya Siku ya Kimataifa ya Sokwe. Tarehe 14 Julai dunia huadhimisha Siku ya Kimataifa ya Sokwe, mojawapo ya viumbe wanaokaribiana zaidi na binadamu kwa asili. Hapa chini ni muhtasari wa baadhi ya habari za hivi karibuni za Mongabay kuhusu sokwe na maisha yao: Sokwe kwenye vita katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale Kama binadamu, sokwe pia huingia katika migogoro mikubwa wao kwa wao. Mwandishi wa Mongabay, Keith Anthony Fabro, aliripoti kuhusu kile kilichoelezwa kama &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya sokwe katika Hifadhi ya Taifa ya Kibale nchini Uganda. Kabla ya mgawanyiko huo, kundi la Ngogo lilikuwa na sokwe kati ya 150 na 200, na hivyo kuwa miongoni mwa makundi makubwa zaidi ya sokwe kuwahi kurekodiwa porini. Baadaye kundi hilo liligawanyika katika makundi mawili yanayojulikana kama Kundi la Kati (Central) na Kundi la Magharibi (Western), yaliyotajwa kutokana na maeneo ya msitu walikokuwa wakipatikana. Kati ya mwaka 2018 na 2024, kundi la Magharibi lilifanya mashambulizi 24 dhidi ya kundi la Kati, na kuua angalau madume saba yaliyokomaa pamoja na sokwe wachanga 17. Migogoro hiyo bado inaendelea na inaweza kuwa na athari za muda mrefu kwa idadi ya sokwe katika eneo hilo. Utafiti unaonyesha jinsi mabadiliko ya mahusiano ya kijamii yanavyoweza kusababisha mgawanyiko na vurugu hata katika jamii za wanyama. Ni kwa namna gani sokwe na Ringo Starr wanafanana? Kupiga ngoma huku ukiimba kwa wakati mmoja ni kipaji kinachovutia, iwe kwa mwanamuzi kama Karen Carpenter au kwa Ringo Starr. Lakini inaonekana sokwe pia wana uwezo huo. Mwandishi wa Mongabay, Liz Kimbrough, alieleza kuhusu Ayumu, sokwe dume mwenye&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/14/maadhimisho-ya-siku-ya-kimataifa-ya-sokwe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/#comments</comments>
					<pubDate>08 Julai 2026 18:36:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/08182238/2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2033</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Aina Vamizi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Mazao ya kilimo kimoja, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro, Mimea, Mimea yenye Tiba, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya mandhari yameshuhudiwa hapa. Badala ya mashamba mapana ya mahindi pekee kama ilivyokuwa zamani, ardhi sasa imepambwa na rangi ya kijivu, kijani kibichi na zambarau, ya mimea hii ya manukato. Wanawake hapa wana matumaini mapya, si tu ya kulinda maisha yao, bali ya kuendeleza kilimo chenye tija ya kiuchumi. Miongoni mwa wanawake hao ni Nelly Musana kutoka Enkutoto, na mwanachama wa kikundi cha kina mama cha Oloisesiai Self Help Group. Karibu yake yupo Mama Arami Musekenya, mama wa watoto sita, mfugaji na mkulima mzaliwa wa Maasai Mara ambaye maisha yake yote ameshuhudia migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Kwa miaka mingi, wanawake hawa waliishi kwa hofu kubwa. Hofu hiyo haikuja mchana; ilikuja usiku, hasa wakati mahindi yalipoanza kuzaa na kukomaa. “Tembo walikuwa wakija bila hodi,” anasema Musekenya, huku akitazama shamba lililojaa rosemary. “Kitu kibaya si kuona tembo; ni kuamka asubuhi ukute hakuna kitu kabisa.” Kiwango cha uharibifu unaofanywa na wanyama hawa wakubwa ni jambo la kutia wasiwasi mkubwa na linaloacha familia katika umaskini wa ghafla. Musekenya anasimulia kuwa kuna nyakati ambapo kundi la tembo watano tu linaweza kuingia shambani na ndani ya usiku mmoja tu, wanamaliza kabisa ekari tano za mahindi. Uharibifu huo wa kasi ya ajabu unamaanisha kuwa jasho&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>07 Julai 2026 21:50:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Clark]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/07214049/Screenshot-2026-07-08-003816-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2025</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Migogoro, Samaki, Samaki wa Maji safi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Kupanda kwa kina cha maji na shinikizo vinakutana katika Ziwa Turkana nchini Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KALOKOL, Kenya – Akiwa mwembamba sana na meno yaliyogeuka rangi ya kahawia kutokana na miongo kadhaa ya kunywa maji ya ziwa yasiyotibiwa yenye fluoride nyingi, John Esirite mwenye umri wa miaka 62, ameketi kwenye kivuli nje ya ofisi ndogo ya Kitengo cha Usimamizi wa Ufukweni cha Kalokol, au BMU, shirika linaloendeshwa na jamii linalosimamia uvuvi wa mashinani. &#8220;Ofisi ya zamani ilikuwa pale chini,&#8221; mvuvi anasema, akielekeza kuelekea ufuo wa magharibi wa Ziwa Turkana, ziwa kubwa zaidi la kudumu la jangwa duniani, linaloonekana kilomita chache tu. &#8220;Lakini sasa iko kwenye maji.&#8221; Katika kipindi cha miaka 15 iliyopita, Ziwa Turkana limeongezeka kwa takriban mita 8-10 (futi 26-33). Hii imeongeza upana wa uso wake kwa karibu 10%. Ndani na karibu na kitovu cha uvuvi cha Kalokol, mamia ya watu wamelazimika kuhama makazi yao kutokana na kuongezeka huku kwa kina cha maji. Katika kisa cha Esirite, kijiji alichokulia, Natole, kimeachwa kwa muda mrefu. Mvuvi huyo amelazimika kuhama mara tatu tangu 2014, akisukumwa mbali zaidi na ardhi ya mababu zake na maeneo ya kuzaliana ya ufukweni ambayo amevua kwa muda mrefu wa maisha yake. &#8220;Tunateseka, lakini hakuna anayetusaidia,&#8221; anasema. &#8220;Tunamuomba Mungu msaada.&#8221; Lakini hata kanisa ambalo Esirite alikuwa akisalia liko kwenye maji. Hali inayoendelea huko Kalokol ni sehemu ya mwelekeo mpana. Tangu mwanzoni mwa miaka ya 2010, maziwa mengi katika eneo lote la Bonde la Ufa la Kenya yamefurika, upanuzi wake ukiongezeka baada ya mvua kubwa sana mnamo 2020, na kulazimisha makumi ya maelfu ya watu kuacha makazi yao. Lakini hapa, katika kona hii ya kaskazini ya nchi ambayo imepuuzwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/07/kupanda-kwa-kina-cha-maji-na-shinikizo-vinakutana-katika-ziwa-turkana-nchini-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>15 Mei 2026 10:00:23 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/13194410/IMG-20260513-WA0002-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1602</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mazingira, Migogoro, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na tai na ndege kubwa za kitalii, lakini leo, kuna mlio mpya wa helikopta unaoashiria mabadiliko ya zama. Hapa ndipo ilipoanzia safari ya Wilson Sairowua &#8216;Tate&#8217;; kijana ambaye mikono yake, iliyozoea kushika fimbo ya uchungaji huku akitembea miguu peku katika mfumo huu wa ekolojia, sasa imeshika usukani wa teknolojia ya kisasa. Wilson si rubani tu, ni daraja la amani linalotumia mbingu kulinda urithi wa ardhi ambapo hatima ya binadamu na tembo zimeunganishwa. Rubani Wilson Sairowua akiwa pamoja na askari wa MEP katika makao makuu ya MEP kwenye eneo la hifadhi la Lemek wakati wa mafunzo ya matumizi ya droni. Picha kwa hisani ya MEP. Kabla hajavaa jaketi la rubani lenye nembo ya shirika la Mara Elephant Project (MEP), au kushika usukani wa helikopta, Wilson alikuwa kijana wa kawaida wa Kimaasai, mchungaji mdogo, mara nyingi akitembea miguu peku, akifuatilia mifugo chini ya jua kali la mchana. Alijua kila mti na kila njia ya siri ya maji, na alikuwa hodari wa kutafsiri nyayo za wanyamapori. Vazi lake lilikuwa shuka na kaptula. Suruali ya kwanza aliivaa akiwa na umri wa miaka 14, alipoingia shule ya upili. “Tulikuwa tunatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Wengine wetu hata hatukuwa na viatu. Nikiwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mauaji katika Ziwa Naivasha, Kenya yazua maswali kuhusu jukumu la walinzi wa pwani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>21 Agosti 2025 12:27:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joseph Maina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/01134625/Screenshot-2025-10-01-153154-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=580</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Migogoro, Samaki, Utawala, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIVASHA, Kenya — Ilikua bado ni giza simu ilipoingia. Grace Nyambura, anayejulikana kwa majirani zake eneo la Karagita Naivasha, kama Mama Chuma, alikuwa amelala alipopigiwa simu na binti yake. Ilikuwa yapata saa 11 alfajiri. Alimwambia Nyambura kuwa kuna jambo limemkumba Chuma, ambaye ni mtoto wa tano wa kiume wa Nyambura. Alimwomba mama yake afike Ziwa Naivasha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/" data-wpel-link="internal">Mauaji katika Ziwa Naivasha, Kenya yazua maswali kuhusu jukumu la walinzi wa pwani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIVASHA, Kenya — Ilikua bado ni giza simu ilipoingia. Grace Nyambura, anayejulikana kwa majirani zake eneo la Karagita Naivasha, kama Mama Chuma, alikuwa amelala alipopigiwa simu na binti yake. Ilikuwa yapata saa 11 alfajiri. Alimwambia Nyambura kuwa kuna jambo limemkumba Chuma, ambaye ni mtoto wa tano wa kiume wa Nyambura. Alimwomba mama yake afike Ziwa Naivasha haraka iwezekanavyo. Nyambura alitii wito huo. Kamau, mwanawe mkubwa, alimchukua kwa pikipiki na wakaendesha kwa kasi katika mji uliokuwa kimya, kuelekea ufuo wa ziwa. Aliyoyakuta asubuhi hiyo miaka minne iliyopita, yanampa kumbukumbu ya kuhuzunisha sana: mwanae, Samuel Mwangi Kimani – jina la utani Chuma kwa wale waliomfahamu &#8211; mwenye umri wa miaka 25 na baba wa watoto wawili, alikuwa amekufa kando ya ufukwe wa ziwa. &#8220;Alionekana kapigwa risasi mgongoni, ikiashiria kuwa alikuwa akikimbia,&#8221; Nyambura anaiambia Mongabay, akiwa ameketi kwenye sofa iliyochakaa ndani ya sebule yake yenye mwanga hafifu. &#8220;Walikuwa wakikimbia walinzi wa pwani. Walikuwa wakielekea upande mwingine.&#8221; Tukio hilo lilitokea mwezi wa Septemba mwaka 2021. Maandamano kuhusu mauaji hayo yalizuka baadaye katika makazi ya Karagita. Lakini katika kusimulia mauaji ya mwanae, Nyambura haonekani kufadhaika. Anaonekana kusumbuliwa zaidi na hilo, si kifo chake tu, bali pia miaka iliyotangulia, ambapo alishuhudia mtoto wake akihangaika kutafuta riziki. Kwa muda wa miaka miwili, Kimani alikuwa akivua samaki na kupata vibarua vya ujenzi sehemu mbalimbali mjini. Uvuvi, alisema, umekuwa hatari kila wakati. &#8220;Walikuwa wakipigwa,&#8221; Nyambura anasema. &#8220;Walinyanyaswa na maafisa wa ulinzi wa pwani.&#8221; Mongabay iliwasiliana na Shirika la Huduma ya Walinzi wa Pwani ya Kenya kuhusu tukio hilo, lakini halikuweza kuthibitisha undani wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/21/mauaji-katika-ziwa-naivasha-kenya-yazua-maswali-kuhusu-jukumu-la-walinzi-wa-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufichuaji wa uharibifu wa misitu katika hifadhi ya sokwe baada ya mashambulizi ya M23 nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2025 14:21:17 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie TotoLatoya Abulu]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/12135717/Screenshot-2025-09-12-165630-768x473.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=401</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bonde la Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na  Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Maeneo yaliyolindwa, Migogoro, Misitu, Misitu ya Mvua, Miti, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Ukataji Miti ya Msitu wa Mvua, Upotevu wa Makazi, na  Visababishi vya Ukataji Misitu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miezi sita iliyopita, kundi la waasi la M23 liliuteka mji wa Goma, moja ya miji mikubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Baada ya muda huo, wanaharakati wa ndani, na Mongabay, ambayo ilikusanya picha za satelaiti, walitambua maeneo yenye upotevu mkubwa wa misitu katika Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, kusini magharibi mwa mji wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/" data-wpel-link="internal">Ufichuaji wa uharibifu wa misitu katika hifadhi ya sokwe baada ya mashambulizi ya M23 nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miezi sita iliyopita, kundi la waasi la M23 liliuteka mji wa Goma, moja ya miji mikubwa mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Baada ya muda huo, wanaharakati wa ndani, na Mongabay, ambayo ilikusanya picha za satelaiti, walitambua maeneo yenye upotevu mkubwa wa misitu katika Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, kusini magharibi mwa mji wa Goma. Katika eneo hili kubwa la msitu wa msingi, ni nyumbani kwa sokwe wa nyanda za chini za mashariki (Gorilla beringei graueri). Watafiti wanahusisha ongezeko hili la upotevu wa misitu na upanuzi wa uzalishaji haramu wa mkaa, kuporomoka kwa utekelezaji wa uhifadhi, na migogoro ya ardhi. Mnamo Novemba mwaka 2021, kundi la waasi linaloungwa mkono na Rwanda liliibuka tena katika Jimbo la Kivu Kaskazini nchini DRC baada ya takriban muongo mmoja wa kutokuwepo katika eneo hilo. Matukio yaliongezeka mnamo Januari na Februari mwaka 2025, wakati waasi wa M23 walipoanzisha mashambulizi ya haraka na kutwaa udhibiti wa maeneo muhimu katika majimbo ya Kivu Kaskazini na Kusini, ikiwa ni pamoja na miji mikuu ya majimbo husika, Goma na Bukavu. Maeneo haya yamesalia chini ya udhibiti wa waasi M23 hadi leo. Zaidi ya miji hii mikubwa, kundi lililojihami pia linadhibiti ufikiaji wa maeneo muhimu ya uchimbaji madini na maeneo muhimu yaliyolindwa kimataifa, kama vile Hifadhi ya Taifa ya Virunga na Hifadhi ya Taifa ya Kahuzi-Biega, Maeneo ya Urithi wa Dunia wa UNESCO. Hadi sasa, mzozo huo una athari inayoonekana kwa bioanuwai kwa kuzidisha changamoto zilizopo za uhifadhi na ukataji miti, watafiti wanasema. Katika Kahuzi-Biega, picha za satelaiti kutoka&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/05/31/ufichuaji-uharibifu-misitu-katika-hifadhi-ya-sokwe-baada-ya-mashambulizi-ya-m23-nchini-drc/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jamii ya Ogiek walaumiwa na kufukuzwa kwa uharibifu wa misitu, lakini ukataji miti ovyo haujakoma</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/11/28/jamii-ya-ogiek-walaumiwa-na-kufurushwa-kwa-uharibifu-wa-misitu-lakini-ukataji-miti-ovyo-haukomi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/11/28/jamii-ya-ogiek-walaumiwa-na-kufurushwa-kwa-uharibifu-wa-misitu-lakini-ukataji-miti-ovyo-haukomi/#respond</comments>
					<pubDate>28 Novemba 2024 16:54:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Caroline Chebet]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/29163845/Screenshot-2025-08-29-193750-768x469.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=329</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Maeneo yaliyolindwa, Maji, Mazingira, Migogoro, Migogoro ya Ardhi, Misitu, Misitu ya Asili, Misitu ya Kitropiki, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uharibifu wa Misitu, na  Vikundi vya Jamii za Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika uamuzi wa kihistoria wa Mei mwaka 2017, Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ilithibitisha hadhi ya jamii asili ya WaOgiek kama wamiliki tangu mababu wa Msitu wa Mau nchini Kenya na kuamuru serikali kulilipa kundi hilo kwa hasara ya nyenzo na maadili, kuwapa hati miliki ya pamoja ya ardhi ya mababu zao, na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/11/28/jamii-ya-ogiek-walaumiwa-na-kufurushwa-kwa-uharibifu-wa-misitu-lakini-ukataji-miti-ovyo-haukomi/" data-wpel-link="internal">Jamii ya Ogiek walaumiwa na kufukuzwa kwa uharibifu wa misitu, lakini ukataji miti ovyo haujakoma</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika uamuzi wa kihistoria wa Mei mwaka 2017, Mahakama ya Afrika ya Haki za Binadamu ilithibitisha hadhi ya jamii asili ya WaOgiek kama wamiliki tangu mababu wa Msitu wa Mau nchini Kenya na kuamuru serikali kulilipa kundi hilo kwa hasara ya nyenzo na maadili, kuwapa hati miliki ya pamoja ya ardhi ya mababu zao, na kurekebisha sera na sheria zinazowanyima watu hao asili haki zao. Novemba 12 mwaka huu, miaka saba na nusu tangu uamuzi huo, mahakama hiyo yenye makao yake makuu nchini Tanzania iliipa Kenya muda wa miezi mitatu kuripoti kuhusu hatua iliyochukua kutekeleza uamuzi huo. Kumekuwa na ushahidi mdogo wa utekelezaji wa uamuzi huo tangu ulipotolewa &#8211; kwa mfano Mamlaka ya Misitu Kenya iliruhusu baadhi ya WaOgiek kuingia katika maeneo ya msitu na kufanya doria za pamoja katika sehemu ya msitu huo katika kaunti ya Nakurue. Hata hivyo, mamlaka za Kenya ziliendesha awamu kadhaa za kuwafukuza wanajamii wa Ogiek na jamii nyingine kutoka msituni, ya hivi karibuni ikiwa mwezi Novemba mwaka 2023, katika Kaunti ya Narok. Katika tukio hilo, walinzi wa Mamlaka ya Misitu ya Kenya waliwaondoa   zaidi ya watu 700 wa jamii ya Ogiek kutoka kwenye makazi yao eneo la Sasimwani, ndani ya sehemu ya Maasai Mau ya kundi hili la misitu, na wakaharibu mali zao. Kiwanja cha Msitu wa Mau chenye ukubwa wa kilomita za mraba 2,700 (maili 1,040 za mraba) ni mfumo muhimu wa ikolojia, mazingira muhimu kwa kuendeleza mito na maziwa mengi ambayo yanasaidia kilimo na misitu mbali nje ya mipaka yake. Msitu huu pia ni kitovu muhimu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/11/28/jamii-ya-ogiek-walaumiwa-na-kufurushwa-kwa-uharibifu-wa-misitu-lakini-ukataji-miti-ovyo-haukomi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/11/28/jamii-ya-ogiek-walaumiwa-na-kufurushwa-kwa-uharibifu-wa-misitu-lakini-ukataji-miti-ovyo-haukomi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>