<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=kutoweka&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/kutoweka/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 14:23:41 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Miaka 40 baada ya mpango mkubwa wa upandaji miti Burundi: Nini kilitokea? Nini kinafanyika?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/21/miaka-40-baada-ya-mpango-mkubwa-wa-upandaji-miti-burundi-nini-kilitokea-nini-kinafanyika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/21/miaka-40-baada-ya-mpango-mkubwa-wa-upandaji-miti-burundi-nini-kilitokea-nini-kinafanyika/#respond</comments>
					<pubDate>21 Agosti 2026 18:34:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Thérence Hategekimana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/21141024/3misituMiti_iliyokatwa_kwa_ajili_ya_viazi-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2565</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kutoweka, Misitu, Miti, Moto, na  Moto wa Misitu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Unapoingia ndani ya misitu iliyopandwa na Serikali ya awamu ya pili ya Burundi chini ya Rais Jean-Baptiste Bagaza, utasikitika. Misitu hiyo ambayo hapo awali ilikuwa imestawi vizuri na kuwa ya kijani kibichi, ikitoa makazi kwa aina mbalimbali za wanyama na mimea, ikilinda udongo dhidi ya mmomonyoko na kuchangia katika uhifadhi wa vyanzo vya maji, leo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/21/miaka-40-baada-ya-mpango-mkubwa-wa-upandaji-miti-burundi-nini-kilitokea-nini-kinafanyika/" data-wpel-link="internal">Miaka 40 baada ya mpango mkubwa wa upandaji miti Burundi: Nini kilitokea? Nini kinafanyika?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Unapoingia ndani ya misitu iliyopandwa na Serikali ya awamu ya pili ya Burundi chini ya Rais Jean-Baptiste Bagaza, utasikitika. Misitu hiyo ambayo hapo awali ilikuwa imestawi vizuri na kuwa ya kijani kibichi, ikitoa makazi kwa aina mbalimbali za wanyama na mimea, ikilinda udongo dhidi ya mmomonyoko na kuchangia katika uhifadhi wa vyanzo vya maji, leo hii katika baadhi ya maeneo, imepoteza sehemu kubwa ya uoto wake. Miti imetoweka, na kuacha maeneo yaliyoharibiwa, yenye miti michache na yaliyo wazi zaidi. Mpango huo mkubwa wa kitaifa wa upandaji miti nchi nzima, ulianza kutekelezwa kuanzia mwaka 1978. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Shirika la Chakula na Kilimo, (FAO), eneo lililopandwa miti katika kampeni hiyo katika kipindi cha kuanzia mwaka 1978 hadi 1991, lilikadiriwa kuwa na ukubwa jumla ya hekta 56,430. Taarifa zaidi kutoka FAO zinaonyesha kwamba takribani hekta 30,000 za misitu iliyopandwa na binadamu ziliharibiwa wakati wa mgogoro wa Oktoba 1993. Sehemu ya mti iliyokatwa katika kijiji cha Kigozi. Pichah na Thérence Hategekimana. Chapisho la FAO linaonyesha kwamba wakati wa kipindi cha upandaji miti kitaifa, takribani hekta 10,080 kati ya 12,000 zilikuwa zimepangwa kupandwa miti hasa aina za Pinus na Callitris katika eneo la Mugamba-Bututsi. Hata hivyo, utafiti wa hivi karibuni uliochapishwa na Global Forest Watch unaonyesha kwamba, kati ya mwaka 2001 na 2025, takribani hekta 760 za uoto wa miti zilipotea katika eneo hilo.Licha ya misitu ya serikali, maeneo mengine ya misitu nchini Burundi yanakabiliwa na uharibifu. Kulingana na utafiti mwingine uliochapishwa mwaka 2026, Burundi ilipoteza asilimia 40.5 ya eneo la misitu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/21/miaka-40-baada-ya-mpango-mkubwa-wa-upandaji-miti-burundi-nini-kilitokea-nini-kinafanyika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/21/miaka-40-baada-ya-mpango-mkubwa-wa-upandaji-miti-burundi-nini-kilitokea-nini-kinafanyika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Juhudi za kuondoa mikaratusi ili kumhifadhi mnyama wa kipekee asiyepatikana kwingineko duniani</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/#respond</comments>
					<pubDate>24 Julai 2026 16:13:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Linah Mwamachi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/24162115/Boulengerula-niedeni_John-Measey-1000x667-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2211</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Amfibia, Ardhi iliyoharibika, Biashara ya mbao, Bioanuai, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kutoweka, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mbao, Miti, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Upandaji Miti, Urejesho wa Asili, na  Wanyama wasio na Mifupa ya Mgongo]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>TAITA TAVETA, Kenya &#8211; Kusini mashariki mwa Kenya, ndani ya msitu mnene wa Sagalla, kunapatikana mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni). Mlima huo wa Sagalla, wenye urefu wa zaidi ya mita 1,400 kutoka usawa wa bahari, una miti ya aina mbalimbali inayounda makazi ya Sagalla caecilian. Kiumbe wa kipekee ulimwenguni Kilomita 18 kutoka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/" data-wpel-link="internal">Juhudi za kuondoa mikaratusi ili kumhifadhi mnyama wa kipekee asiyepatikana kwingineko duniani</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[TAITA TAVETA, Kenya &#8211; Kusini mashariki mwa Kenya, ndani ya msitu mnene wa Sagalla, kunapatikana mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni). Mlima huo wa Sagalla, wenye urefu wa zaidi ya mita 1,400 kutoka usawa wa bahari, una miti ya aina mbalimbali inayounda makazi ya Sagalla caecilian. Kiumbe wa kipekee ulimwenguni Kilomita 18 kutoka tambarare za mji wa Voi, Mongabay ilizuru msitu huo wa Sagalla unaoweza kufikiwa kwa gari na pikipiki hadi sehemu fulani, na sehemu iliyosalia hufikiwa kwa miguu. Mnyama wa kipekee wa jamii ya amfibia anayejulikana kama Sagalla caecilian (Boulengerula niedeni. Picha na Patrick Malonza. Mongabay ilitaka kufahamu iwapo jamii inatambua spishi hii na faida zake kwa ikolojia, na ilifanikiwa kukutana na wanajiji wakiwa katika shughuli zao za kila siku shambani. “Mimi sikuwa nafahamu mnyama huyu. Nilikuwa namuona shambani kisha namkatakata kwa jembe au namgonga kwa mawe ili afe, kwa sababu anafanana na nyoka,” anasema Jemimah Mwaiga. Sasa Mwaiga anafahamisha Mongabay kuhusu umuhimu wa kiumbe huyo, na kufafanua jinsi walihusishwa katika kutafuta jina lake la kinyumbani, “kilima mrota”. “Tulijifunza kuwa kiumbe huyo husaidia katika ukulima na ubora wa mchanga kwa kuchanganya mchanga na virutubisho vilivyo mchangani na kuongeza rutuba ya asili ya mchanga,” Mwaiga anaelezea Mongabay. Mwanasayansi wa masuala ya mchanga na mazingira Kenneth Macharia wa shirika la Edge of Existence, anasema kiumbe huyu ni wa kipekee katika mlima wa Sagalla. Huishi katika mazingira yenye unyevunyevu, na mchanga wenye rutuba. Macharia anaongeza: “Jamii zinaweza kuimarisha kilimo pamoja na utunzaji wa mazingira kwa kutumia mbinu bora katika mchanga kama vile kupanda miti ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/24/juhudi-za-jamii-zaendelea-kuondoa-mikaratusi-kumhifadhi-mnyama-wa-kipekee-asiyepatikana-kwingineko-duniani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Faru 70 kutoka Afrika Kusini wawasili makao mapya nchini Rwanda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2025 13:43:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Graeme Green]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/21133633/Screenshot-2025-08-21-163555-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=125</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, na  Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Faru, Kutoweka, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Uwindaji, Uwindaji Kupita Kiasi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Faru weupe 70 wamekamilisha safari yao kwa mafanikio kutoka Afrika Kusini hadi Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Hii ni mara ya kwanza kwa faru kuhamishwa kimataifa kutoka Platinum Rhino, mradi mkubwa wa ufugaji faru uliopitwa mnada mwaka 2023, baada ya kukumbwa na matatizo ya kifedha kwa miaka mingi. Baada ya kukosa wanunuzi, shirika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/" data-wpel-link="internal">Faru 70 kutoka Afrika Kusini wawasili makao mapya nchini Rwanda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Faru weupe 70 wamekamilisha safari yao kwa mafanikio kutoka Afrika Kusini hadi Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Hii ni mara ya kwanza kwa faru kuhamishwa kimataifa kutoka Platinum Rhino, mradi mkubwa wa ufugaji faru uliopitwa mnada mwaka 2023, baada ya kukumbwa na matatizo ya kifedha kwa miaka mingi. Baada ya kukosa wanunuzi, shirika la African Parks lilinunua eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 7,800, lililopo kilomita 160 kusini mashariki mwa Johannesburg, pamoja na faru wake 2,000 — twiga, pundamilia, na wanyama wengine — kwa kiasi cha fedha ambacho hakikutajwa. Platinum Rhino ilibadilishwa jina na kuitwa Rhino Rewild. Hii idadi ya faru waliokuwa African Parks inawakilisha takriban asilimia 15 ya idadi ya faru weupe wote duniani (Ceratotherium simum). Mpango wa African Parks wa Rhino Rewild unalenga kuwasambaza wanyama hao kwenye maeneo salama na yenye usimamizi mzuri kote Afrika, ili kuanzisha maeneo mapya ya kuwalinda na kuimarisha idadi ya waliopo tayari. Mwanzoni, faru 40 walihamishwa kutoka Rhino Rewild hadi Munywana Conservancy, ambayo ni hifadhi binafsi ya wanyamapori iliyoko mkoa wa KwaZulu Natal nchini Afrika Kusini. Hivyo uhamisho huu wa faru 70 kwenda Akagera ulikuwa wa pili. Faru mweupe akiwa kwenye makazi yake mapya katika Hifadhi ya Taifa ya Akagera nchini Rwanda. Picha na Wiktoria West. &#8220;Akagera inaweza kuhifadhi idadi kubwa ya faru weupe,&#8221; alisema Donovan Jooste,   meneja wa mradi wa Rhino Rewilding wa African Parks. &#8220;Hii, pamoja na ukweli kwamba Rwanda ni nchi thabiti na serikali yake inaunga mkono kazi zetu, inamaanisha kwamba kundi hili la faru linaweza kuwa na umuhimu sana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/06/10/faru-70-kutoka-afrika-kusini-wawasili-makao-mapya-nchini-rwanda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ugunduzi wa popo walio hatarini kutoweka nchini Rwanda waibua mazungumzo ya uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>25 Aprili 2025 00:59:44 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Aimable Twahirwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/01135959/3d1278d3-4f58-4143-82ec-1f992772db5d-1.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=285</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Rwanda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kutoweka, Mamalia, Mazingira, Popo, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Ugunduzi wa Spishi, Uhifadhi, Upotevu wa Makazi, Utafiti, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIGALI, Rwanda ― Kufuatia ugunduzi wa hivi karibuni wa popo aina ya farasi walio katika hatari ya kuangamia (au kisayansi Rhinolophus hilli) katika Mbuga ya Taifa ya Nyungwe kusini-magharibi mwa Rwanda, watafiti wanatoa wito wa kuchukua hatua na sera zinazolenga uhifadhi wao. Wanasayansi wanasema kuwa huu ni ugunduzi wa kwanza wa kuona na kurekodi popo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Ugunduzi wa popo walio hatarini kutoweka nchini Rwanda waibua mazungumzo ya uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIGALI, Rwanda ― Kufuatia ugunduzi wa hivi karibuni wa popo aina ya farasi walio katika hatari ya kuangamia (au kisayansi Rhinolophus hilli) katika Mbuga ya Taifa ya Nyungwe kusini-magharibi mwa Rwanda, watafiti wanatoa wito wa kuchukua hatua na sera zinazolenga uhifadhi wao. Wanasayansi wanasema kuwa huu ni ugunduzi wa kwanza wa kuona na kurekodi popo wa aina ya Rhinolophus webalai (horseshoe bat) katika hifadhi hiyo, na pia ni mara ya kwanza kwa Rwanda kushuhudia popo wa Damara woolly bat (Kerivoula argentata) tangu walipoonekana mara ya mwisho mwaka 1981. Kwa mujibu wa Paul Webala, Mhadhiri Mwandamizi wa Biolojia ya Wanyamapori katika Idara ya Misitu na Usimamizi wa Wanyamapori katika Chuo Kikuu cha Maasai Mara nchini Kenya, wanasayansi wanachukulia popo kuwa kundi la pili lenye utofauti mkubwa zaidi miongoni mwa mamalia, baada ya panya. Anasema katika nchi kama Rwanda  ambapo misitu ya asili na maeneo ya savana yamepotea, kubadilika au kuharibika kwa kiasi kikubwa, popo wanaweza kuwakilisha “angalau asilimia 40 ya utofauti wa mamalia kwa ujumla.” Kulingana na utafiti wa mwaka mwaka 2022 (utafiti) ambao Webala alishirikiana na mtu mwingine kuufanya, popo wanaokula wadudu nchini Rwanda hutoa huduma muhimu za mfumo wa ikolojia na pia hufanywa kama wadhibiti wadudu katika maeneo ya kilimo. Hofu za kiafya na upotezaji wa makazi  &#8220;Nchini Rwanda, mojawapo ya aina [ya popo] inayotia wasiwasi, ingawa haijatishiwa kulingana na Orodha Nyekundu ya shirika la IUCN, ni popo wa Misri [Rousettus aegyptiacus] kwa sababu ametambuliwa na maafisa wa afya kama hifadhi ya asili ya ugonjwa wa virusi vya Marburg,&#8221; Webala anasema. Mnamo Februari mwaka huu, maafisa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/04/25/ugunduzi-wa-popo-walio-hatarini-kutoweka-nchini-rwanda-waibua-mazungumzo-ya-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Kama wewe, mimi pia nahofia kuangamia kwa tembo’</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>17 Desemba 2024 16:24:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/29154201/Screenshot-2025-08-29-184109-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=313</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Haki za Binadamu, Hifadhi za Taifa, Jamii Asili, Kutoweka, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Misitu, Pembe za Ndovu, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Studeo ya Data ya Mongabay, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni makala ya kwanza katika mfululizo wa habari za Mongabay kuhusu ‘Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki’. Soma sehemu ya pili na ya nne.  Mnamo Juni 13, 1959, mwindaji wa kabila la Waata, Galogalo Kafonde, alijisalimisha kwa kikosi cha kikoloni cha &#8220;Field Force&#8221; cha Kenya, kitengo cha kwanza barani Afrika cha kupambana na ujangili. Kwa karne nyingi, watu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/" data-wpel-link="internal">‘Kama wewe, mimi pia nahofia kuangamia kwa tembo’</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni makala ya kwanza katika mfululizo wa habari za Mongabay kuhusu ‘Maeneo Yaliyolindwa Afrika Mashariki’. Soma sehemu ya pili na ya nne.  Mnamo Juni 13, 1959, mwindaji wa kabila la Waata, Galogalo Kafonde, alijisalimisha kwa kikosi cha kikoloni cha &#8220;Field Force&#8221; cha Kenya, kitengo cha kwanza barani Afrika cha kupambana na ujangili. Kwa karne nyingi, watu kutoka kabila la Waata walikuwa wakiwinda tembo. Kumuua tembo mmoja ilikuwa ni ibada ya jandoni. Tofauti na majirani zao waliofuga ng’ombe, jamii ya Waata waliishi kwa kula nyama ya ng’ombe na kuvaa ngozi za tembo. Pembe za ndovu hazikuwa na manufaa kwao, lakini waliziuza kupitia ubadilishanaji wa bidhaa nyingine na wafanyabiashara wa Kiarabu huko Mombasa. Biashara ya pembe za ndovu ilipozidi kushamiri katika karne ya 17, ikichochewa na ukuaji wa soko la watumiaji wa Ulaya, sifa ya Waata iliimarika. Walikuwa miongoni mwa wafuatiliaji bora wa tembo ukanda wa Afrika Mashariki, wanaojulikana kama &#8220;watu wa upinde mrefu&#8221; kwa ustadi wao wa kutumia mishale yenye sumu. Lakini wawindaji wa Ulaya walikuja kuwaona jamii za Waata na jamii nyingine asilia kama ushindani. Mnamo mwaka 1897, Uingereza ilipoweka malengo yake kwa koloni la kudumu la Kenya, ilipiga marufuku uwindaji &#8220;wa asili&#8221; ambao haujaidhinishwa. Kwa saini  moja tu ya kalamu, kiini cha maisha ya Waata kiligeuka kuwa haramu. Wafanyabiashara wakipima pembe za ndovu mwaka 1935. Picha na Ewing Galloway kupitia Flickr (CC BY-NC-SA 2.0). Mnamo mwaka 1948, Waingereza waliunda Mbuga ya Taifa ya Tsavo, mojawapo ya mbuga za kwanza nchini Kenya. Lakini upande wake wa mashariki ulikuwa uwanja wa uwindaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/17/kama-wewe-mimi-pia-nahofia-kuangamia-kwa-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoonekana kwa tumbili wala gundi Tanzania kwaibua hofu ya kutoweka kwa spishi hiyo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Desemba 2024 08:06:40 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ryan Truscott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/28075239/Screenshot-2025-08-28-105201-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=297</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kutoweka, Mamalia, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Nyani, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tumbili, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hakujakuwa na taarifa zilizothibitishwa za kuonekana kwa tumbili wa kusini wa patas, ambao wako katika hatari kubwa ya kutoweka, katika makazi yao ya mwisho yanayojulikana, magharibi mwa Tanzania. Mwaka 2021, ilikadiriwa kuwa walikuwa wamebaki chini ya tumbili 200 wa aina hii wenye viungo vyepesi na virefu, wanaojulikana kitaalam kama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/" data-wpel-link="internal">Kutoonekana kwa tumbili wala gundi Tanzania kwaibua hofu ya kutoweka kwa spishi hiyo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya mwaka mmoja sasa, hakujakuwa na taarifa zilizothibitishwa za kuonekana kwa tumbili wa kusini wa patas, ambao wako katika hatari kubwa ya kutoweka, katika makazi yao ya mwisho yanayojulikana, magharibi mwa Tanzania. Mwaka 2021, ilikadiriwa kuwa walikuwa wamebaki chini ya tumbili 200 wa aina hii wenye viungo vyepesi na virefu, wanaojulikana kitaalam kama Erythrocebus baumstarki, ambao walipatikana kwenye maeneo ya misitu ya wazi katika ukanda huo na sasa wanasayansi wana hofu kuwa spishi hiyo inakaribia kutoweka kabisa. Awali, tumbili wa patas wa kusini alikuwa anachanganywa na tumbili wa patas wa mashariki, Erythrocebus patas pyrrhonotus, ambaye hupatikana kwa wingi zaidi katika maeneo mbalimbali ya Afrika Mashariki na Kati, kuanzia Kenya ya kati hadi kaskazini mashariki mwa Chad. Wanyama hawa wanafanana kwa mwonekano, na wote huishi kwenye maeneo ya misitu ya wazi yenye urefu wa mwinuko unaokaribiana. Lakini hata kabla ya mwaka 2015, wakati ambapo patas wa kusini bado walikuwepo nchini Kenya; spishi hizi mbili zilikuwa zimetenganishwa na mamia ya kilomita. Kuna uwezekano mkubwa kuwa hazijawahi kuchanganyika. Mwonekano wao unaofanana  pamoja na tabia nyingine kama vile kuwa na maeneo makubwa ya kuishi na kula gundi kutoka kwenye miti ya miiba inayojulikana kitaalam kama Acacia drepanolobium (whistling thorn); ulisababisha ukosefu wa juhudi maalum za uhifadhi kwa ajili ya kulinda tumbili wa kusini wa patas. Kutokana na ukweli kwamba aina hii ya nyani wana tabia ya uoga, na huonekana mara chache, vilifanya tafiti za kisayansi za kutambua tofauti za spishi kukosekana kwa muda mrefu. Hata hivyo, Yvonne de Jong, mtaalamu wa masuala ya jamii ya nyani&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/09/kutoonekana-kwa-tumbili-wala-gundi-tanzania-kwaibua-hofu-ya-kutoweka-kwa-spishi-hiyo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>