<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=uendelevu&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/uendelevu/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 06:24:00 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mwanauhifadhi John Salehe, aliyepigania uhifadhi shirikishi Tanzaia, afariki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/#respond</comments>
					<pubDate>17 Agosti 2026 10:59:12 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Rhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/17104948/Screenshot-2026-08-17-134842-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2494</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Filosofia ya Uhifadhi, Jamii Asili, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Maendeleo ya Jamii, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro ya Ardhi, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uendelevu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kati ya Ziwa Manyara na Tarangire, mstari kwenye ramani peke yake haukuwahi kuwa wa kutosha. Tembo, nyumbu, na wanyama wengine walipita kwenye ardhi iliyotumiwa na wafugaji na wakulima, ardhi ambayo barabara, mashamba na makazi yalikuwa yakizidi kusambaa. Kulinda ushoroba huo kulihitaji zaidi ya kuweka mipaka: kulihitaji kuwashawishi watu waliokaa hapo kwamba wanyamapori walikuwa na nafasi katika mustakabali wao. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/" data-wpel-link="internal">Mwanauhifadhi John Salehe, aliyepigania uhifadhi shirikishi Tanzaia, afariki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kati ya Ziwa Manyara na Tarangire, mstari kwenye ramani peke yake haukuwahi kuwa wa kutosha. Tembo, nyumbu, na wanyama wengine walipita kwenye ardhi iliyotumiwa na wafugaji na wakulima, ardhi ambayo barabara, mashamba na makazi yalikuwa yakizidi kusambaa. Kulinda ushoroba huo kulihitaji zaidi ya kuweka mipaka: kulihitaji kuwashawishi watu waliokaa hapo kwamba wanyamapori walikuwa na nafasi katika mustakabali wao. Kulihitaji kukabiliana na hasara ya mifugo iliyouawa na wanyama wakali, migogoro kuhusu mgawanyo wa mapato, na kazi ngumu ya kuimarisha taasisi za mitaa. John Gospel Yonazi Salehe, aliyefariki tarehe 19 Juni akiwa na umri wa miaka 71, alitumia sehemu kubwa ya maisha yake ya kazi kushughulikia changamoto kama hizo. Mtanzania huyu, aliyefunzwa katika taaluma ya misitu, alifanya kazi serikalini, kisha katika FAO, UNDP, WWF, na hatimaye African Wildlife Foundation, ambako alihudumu kama mkurugenzi wa Tanzania. Alifanya kazi kwa zaidi ya miongo minne katika sekta za misitu, maeneo ya wanyamapori, na miradi ya maendeleo katika Afrika Mashariki. Kwa Salehe, uhifadhi ulikuwa wa vitendo na wenye msingi imara wa kijamii. Katika Nyanda za Maasai, alijikita katika kulinda ushoroba wa wanyamapori na kuimarisha Maeneo ya Usimamizi wa Wanyamapori yanayosimamiwa na jamii. Alitaka faida za uhifadhi ziwafikie wanajamii, akiunga mkono ujenzi wa mazizi yaliyoimarishwa ili kulinda mifugo dhidi ya wanyama wakali, na utoaji wa fidia kwa hasara zilizosababishwa na wanyamapori. Kwa mtazamo wake, jamii haikuwa hadhira inayosubiri maamuzi ya wengine; ilikuwa nguzo ya msingi ya jinsi uhifadhi unavyopaswa kufanya kazi. Mtazamo huo huo uliongoza kazi yake katika sekta ya misitu. Katika maeneo ya kati ya Tanzania, ambapo uzalishaji wa mkaa na kilimo viliongeza shinikizo kubwa kwa misitu, Salehe alisisitiza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/17/mwanauhifadhi-john-salehe-aliyepigania-uhifadhi-shirikishi-tanzaia-afariki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 12:22:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30073721/Magari2-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2264</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Halijoto, Kaboni, Mabadiliko ya Tabianchi, Maliasili, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Siasa za Tabianchi, Teknolojia, Uendelevu, na  Ufanisi wa nishati]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya kuhamia matumizi ya nishati safi kwenye vyombo vya usafiri kwa kuzielekeza taasisi zote za umma kuanza kujumuisha ununuzi wa magari yanayotumia umeme na gesi asilia katika mipango na bajeti zao. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omari, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupunguza gharama kubwa za kununua mafuta. Bajaji zinazotumia umeme. Picha ya Jenifer Gilla, Mongabay. Hatua hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050  na Michango ya Taifa Iliyoamuliwa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris ambapo Tanzania imeahidi kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kupitia sekta za nishati na usafiri. Uzalishaji wa hewa ya ukaa Mpango wa kutumia nishati safi kwenye vyombo vya usafiri nchini Tanzania, iwapo utafanikiwa, utapunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi. Msololo Onditi, Mtaalam wa mabadiliko ya tabianchi na Mshauri wa Masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika Shirika la Maendeleo la Ujerumani Tanzania (GIZ), anasema kila lita moja ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jitihada  za Ethiopia kuingiza zao la kienyeji la enseti kwenye lishe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/#respond</comments>
					<pubDate>20 Agosti 2025 12:53:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Solomon Yimer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23115134/Screenshot-2025-09-23-145101-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=436</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Hali ya Hewa, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ARBA MINCH, Ethiopia — Mwishoni mwa mwezi Mei, muda wa asubuhi, wakati baridi ya alfajiri ilipokuwa ikipungua, na jua likianza kuchomoza na kupasha joto vilima vya kijiji cha Hareba kusini mwa Ethiopia, Almaz Achamo, mwanamke mwenye umri wa miaka 56, alikuwa akihudumia mmea mrefu, unaofanana na ndizi ambao umesaidia jamii yake kwa vizazi vingi. Mmea huu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/" data-wpel-link="internal">Jitihada  za Ethiopia kuingiza zao la kienyeji la enseti kwenye lishe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ARBA MINCH, Ethiopia — Mwishoni mwa mwezi Mei, muda wa asubuhi, wakati baridi ya alfajiri ilipokuwa ikipungua, na jua likianza kuchomoza na kupasha joto vilima vya kijiji cha Hareba kusini mwa Ethiopia, Almaz Achamo, mwanamke mwenye umri wa miaka 56, alikuwa akihudumia mmea mrefu, unaofanana na ndizi ambao umesaidia jamii yake kwa vizazi vingi. Mmea huu wa kitamaduni unaostahimili hali ya hewa umesaidia familia kustahimili ukame na upungufu wa chakula. &#8220;Enseti ni mmea muhimu zaidi kwa familia yangu. Tunapata chakula chetu chote kutoka kwenye mmea huu,&#8221; Almaz anasema, huku akiondoa kwa taratibu majani yaliyoharibiwa ili kuweka mazao kuwa na afya. Wanategemea enseti kwa sababu unaweza kuvunwa mwaka mzima na kuwaendeleza katika nyakati ngumu. &#8220;Mazao mengine yanaposhindwa, enseti haituruhusu tufe kwa njaa,&#8221; Almaz anaiambia Mongabay. Ustahimilivu huu ndio umesababisha watafiti kuuita mti huu &#8220;mti dhidi ya njaa.&#8221; Hata hivyo, zao hilo limeendelea kupuuzwa, kwa kiasi kikubwa, na sera za ndani za kilimo na wadau wa kimataifa. Lakini wakati mabadiliko ya hali ya hewa na shinikizo nyingine zinavyoathiri mifumo ya chakula cha asili katika maeneo ya vijijini, Ethiopia inajitahidi kufufua mmea wa enseti. Baada ya kuwekwa kando, mmea wa enseti sasa ni sehemu ya programu za kitaifa na ubunifu unaoongozwa na chuo kikuu unaolenga kuimarisha usalama wa chakula, kuboresha maisha, na kuunda mustakabali wa chakula nchini. Watafiti na wavumbuzi wanaendeleza teknolojia mpya za kilimo na usindikaji ili kukabiliana na changamoto kuu katika uzalishaji wa enseti, kwa lengo la kulibadilisha kuwa zao la biashara linaloweza kuhimili ushindani na kupanua matumizi yake zaidi ya maeneo ya jadi ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/#respond</comments>
					<pubDate>02 Agosti 2023 12:48:18 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/05054458/Screenshot-2025-10-05-083758-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=607</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Kijani, Kilimo, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Kupunguza Umaskini, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Ufugaji Samaki, Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, huku shamba lake lililosalia, likisaidia mifugo na mazao ya chakula kama maharage ya kijani, mtama, uwele na mahindi. Tangu mwaka 2013, ni nusu ekari tu ya eneo lake ambayo imemnufaisha zaidi. &#8220;Samaki ninaowafuga hapa ni kwa ajili ya matumizi ya ndani. Pia ninapata mapato mazuri ninapouza samaki katika soko la huku nchini. Sioni wasiwasi wakati mazao yangu ya chakula yanaposhindwa kutoa mavuno,&#8221; alisema baba huyo wa watoto watano mwenye umri wa miaka 51, anayefuga ngege na kambare. Japheth Nthiga anafuga samaki aina ya ngege na kambare katika mabwawa ya samaki kwenye shamba lake eneo la kati ya Kenya. Picha na David Njagi wa Mongabay.  Ni rahisi kuelewa vizuri hisia za Nthiga. Kijiji chake, ambacho kiko takriban kilomita 150 (sawa na maili 90) kutoka ukingo wa Msitu wa Mlima Kenya, kimekumbwa na ukame wa muda mrefu na wa mara kwa mara kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita. Ili kukabiliana na msimu wa kiangazi, wakulima, hasa wale wanaotoka katika nyanda za juu za mito, wamezidisha matumizi yao ya mbolea ili kuongeza mavuno, na kwa kufanya hivyo, wamesababisha uchafuzi wa mito na kupoteza rutuba ya udongo katika eneo hilo, kulingana na Venter Mwongera, ambaye ni mratibu wa mawasiliano&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>