<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=sekta-ya-chakula&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/sekta-ya-chakula/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Tue, 01 Sep 2026 14:42:19 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Usalama wa chakula mashakani: Namna mvutano wa Ghuba unavyotikisa upatikanaji wa mbolea nchini Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>06 Julai 2026 16:53:00 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Achieng’ Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/06163255/Screenshot-2026-07-06-193237-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2014</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Kilimo, Chakula, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Maji, Mazao ya kilimo kimoja, Mimea, Msukosuko wa chakula, Safiri, Sekta ya Chakula, Siasa, upatikanaji wa chakula, na  Vita]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mzee Philip Kitur anatembea katikati ya safu nadhifu za mabua ya mahindi, huku majani yanayoanza kuchipua yakitoa ishara ya mavuno tele. Mkulima huyo mwenye umri wa miaka 72 anamiliki shamba la ekari 41 katika kijiji cha Kipkeikei, Kaunti ya Trans-Nzoia. Hata hivyo, nyuma ya tabasamu la Kitur kuna hofu ya kupoteza sehemu kubwa ya mavuno [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Usalama wa chakula mashakani: Namna mvutano wa Ghuba unavyotikisa upatikanaji wa mbolea nchini Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mzee Philip Kitur anatembea katikati ya safu nadhifu za mabua ya mahindi, huku majani yanayoanza kuchipua yakitoa ishara ya mavuno tele. Mkulima huyo mwenye umri wa miaka 72 anamiliki shamba la ekari 41 katika kijiji cha Kipkeikei, Kaunti ya Trans-Nzoia. Hata hivyo, nyuma ya tabasamu la Kitur kuna hofu ya kupoteza sehemu kubwa ya mavuno iwapo hatopata mbolea. &#8220;Mazao yanahitaji kuongezewa mbolea ya kukuzia, lakini sijapata mbolea ya aina ya urea; bila hiyo, naweza kupoteza hadi asilimia 30 ya mavuno yangu,&#8221; aliambia Mongabay. Mutahi Kagwe, Waziri wa Kilimo nchini Kenya, anasema nchi ina akiba ya kutosha ya mbolea, ikiwa ni pamoja na mifuko milioni 2 ya mbolea ya nyongeza. Anasema Kenya inatafuta vyanzo mbadala vya mbolea ili kuhakikisha usalama wa chakula licha ya misukosuko ya kimataifa iliyosababishwa na mvutano kati ya Iran na Marekani. &#8220;Ingawa hatuwezi kutabiri mgogoro wa Mashariki ya Kati utachukua muda gani, tumejadiliana kuhusu kupata mbolea ya urea kutoka Algeria na aina nyingine za mbolea kutoka Morocco,&#8221; Kagwe aliambia Mongabay katika mahojiano yaliyofanyika kwa njia ya mtandao. Shamba la mahindi linalomilikiwa na Dennis Chemonges, mkulima wa Cherengani, katika kaunti ya Trans-Nzoia nchini Kenya. Mazao hayo yanahitaji kuwekewa mbolea ya kukuzia. Picha na Achieng’ Otieno, Mongabay. Eneo kuu la uzalishaji wa chakula Kaunti ya Trans-Nzoia ni mojawapo ya maeneo makuu ya uzalishaji wa chakula nchini Kenya, hasa mahindi, ambayo ni chakula kikuu. Kulingana na Ripoti ya Kitaifa ya Uzalishaji wa Kilimo ya mwaka 2025 kutoka Shirika la Kitaifa la Takwimu za Kenya, Trans-Nzoia ilichangia tani 423,156 (asilimia 10.5) kati ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/06/usalama-wa-chakula-mashakani-namna-mvutano-wa-ghuba-unavyotikisa-upatikanaji-wa-mbolea-nchini-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jitihada  za Ethiopia kuingiza zao la kienyeji la enseti kwenye lishe</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/#respond</comments>
					<pubDate>20 Agosti 2025 12:53:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Solomon Yimer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/23115134/Screenshot-2025-09-23-145101-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=436</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Ethiopia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Hali ya Hewa, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ARBA MINCH, Ethiopia — Mwishoni mwa mwezi Mei, muda wa asubuhi, wakati baridi ya alfajiri ilipokuwa ikipungua, na jua likianza kuchomoza na kupasha joto vilima vya kijiji cha Hareba kusini mwa Ethiopia, Almaz Achamo, mwanamke mwenye umri wa miaka 56, alikuwa akihudumia mmea mrefu, unaofanana na ndizi ambao umesaidia jamii yake kwa vizazi vingi. Mmea huu wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/" data-wpel-link="internal">Jitihada  za Ethiopia kuingiza zao la kienyeji la enseti kwenye lishe</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ARBA MINCH, Ethiopia — Mwishoni mwa mwezi Mei, muda wa asubuhi, wakati baridi ya alfajiri ilipokuwa ikipungua, na jua likianza kuchomoza na kupasha joto vilima vya kijiji cha Hareba kusini mwa Ethiopia, Almaz Achamo, mwanamke mwenye umri wa miaka 56, alikuwa akihudumia mmea mrefu, unaofanana na ndizi ambao umesaidia jamii yake kwa vizazi vingi. Mmea huu wa kitamaduni unaostahimili hali ya hewa umesaidia familia kustahimili ukame na upungufu wa chakula. &#8220;Enseti ni mmea muhimu zaidi kwa familia yangu. Tunapata chakula chetu chote kutoka kwenye mmea huu,&#8221; Almaz anasema, huku akiondoa kwa taratibu majani yaliyoharibiwa ili kuweka mazao kuwa na afya. Wanategemea enseti kwa sababu unaweza kuvunwa mwaka mzima na kuwaendeleza katika nyakati ngumu. &#8220;Mazao mengine yanaposhindwa, enseti haituruhusu tufe kwa njaa,&#8221; Almaz anaiambia Mongabay. Ustahimilivu huu ndio umesababisha watafiti kuuita mti huu &#8220;mti dhidi ya njaa.&#8221; Hata hivyo, zao hilo limeendelea kupuuzwa, kwa kiasi kikubwa, na sera za ndani za kilimo na wadau wa kimataifa. Lakini wakati mabadiliko ya hali ya hewa na shinikizo nyingine zinavyoathiri mifumo ya chakula cha asili katika maeneo ya vijijini, Ethiopia inajitahidi kufufua mmea wa enseti. Baada ya kuwekwa kando, mmea wa enseti sasa ni sehemu ya programu za kitaifa na ubunifu unaoongozwa na chuo kikuu unaolenga kuimarisha usalama wa chakula, kuboresha maisha, na kuunda mustakabali wa chakula nchini. Watafiti na wavumbuzi wanaendeleza teknolojia mpya za kilimo na usindikaji ili kukabiliana na changamoto kuu katika uzalishaji wa enseti, kwa lengo la kulibadilisha kuwa zao la biashara linaloweza kuhimili ushindani na kupanua matumizi yake zaidi ya maeneo ya jadi ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/20/jitihada-za-ethiopia-kuingiza-zao-la-kienyeji-la-enseti-kwenye-lishe/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wadogo Afrika wanufaika na matumizi ya nishati jadidifu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/03/31/wakulima-wadogo-afrika-wanufaika-na-matumizi-ya-nishati-jadidifu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/03/31/wakulima-wadogo-afrika-wanufaika-na-matumizi-ya-nishati-jadidifu/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2025 06:51:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Aimable Twahirwa]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/22085712/featured-1-768x477.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=193</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Rwanda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Kilimo, Mazingira, Nishati, Nishati Mbadala, Nishati ya Jua, Sekta ya Chakula, Suluhu za Uhifadhi, na  Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KIREHE, Rwanda &#8211; Kwa miaka mingi Victor Ndwaniye, mkulima mdogo kutoka kijiji cha Nasho kilichopo kandokando ya ziwa katika wilaya ya Kirehe mashariki mwa Rwanda, alikuwa akimwagilia shamba lake lenye aina mbalimbali za mboga kwa kutumia ndoo. Hata hivyo, kuanzia mwaka 2020, Ndwaniye ambaye ni baba wa watoto sita, amekuwa akitumia njia ya kisasa ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/31/wakulima-wadogo-afrika-wanufaika-na-matumizi-ya-nishati-jadidifu/" data-wpel-link="internal">Wakulima wadogo Afrika wanufaika na matumizi ya nishati jadidifu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KIREHE, Rwanda &#8211; Kwa miaka mingi Victor Ndwaniye, mkulima mdogo kutoka kijiji cha Nasho kilichopo kandokando ya ziwa katika wilaya ya Kirehe mashariki mwa Rwanda, alikuwa akimwagilia shamba lake lenye aina mbalimbali za mboga kwa kutumia ndoo. Hata hivyo, kuanzia mwaka 2020, Ndwaniye ambaye ni baba wa watoto sita, amekuwa akitumia njia ya kisasa ya umwagiliaji akitumia mfumo wa umeme jua. “Umwagiliaji wa kutumia ndoo haukuwa na tija. Haukukidhi mahitaji ya wakulima wengi wadogo na ulitoa mazao hafifu,” alieleza Ndwaniye wakati wa mahojiano na Mongabay. Kwa sasa hali ya wakulima nchini Rwanda imebadilika baada ya kuanza kilimo cha umwagiliaji kinachotumia nishati jadidifu ya umemejua. Teknolojia hii mpya inatumika katika hatua mbalimbali katika mnyororo wa thamani katika kilimo na ni mkombozi wa wakulima wadogo. Maafisa wa kilimo sasa wameweka lengo la kuongeza ukubwa wa mashamba yanayotumia kilimo cha umwagiliaji kupitia umemejua kutoka hekta 646 (ekari 1,600) za sasa hadi kufikia hekta 1,146 (eka 2,830) ifikapo 2029. Nchi nyingine kama Bangladesh na India nazo zimepiga hatua kubwa katika kilimo cha umwagiliaji kinachotumia umemejua na zina malengo ya kuongeza ukubwa wa mashamba yanayotumia teknolojia hii ya umwagiliaji. Katika hatua za mwanzo, wakulima wanatakiwa kulipa gharama za utunzaji wa mifumo na miundombinu ya umwagiliaji. Katika hatua hii pia serikali na wadau wengine hutoa msaada wa fedha kuwawezesha wakulima kugharamia teknolojia hii ingawa bado gharama inaonekana kubwa kwa wakulima. Kulingana na Bodi ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo ya Rwanda (Rwanda Agriculture and Animal Resources Development Board), mpango huu unalenga kuwajenga wakulima wadogo kuhimili majanga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/03/31/wakulima-wadogo-afrika-wanufaika-na-matumizi-ya-nishati-jadidifu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/03/31/wakulima-wadogo-afrika-wanufaika-na-matumizi-ya-nishati-jadidifu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/#respond</comments>
					<pubDate>02 Agosti 2023 12:48:18 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/05054458/Screenshot-2025-10-05-083758-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=607</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Kijani, Kilimo, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Kupunguza Umaskini, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Ufugaji Samaki, Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, huku shamba lake lililosalia, likisaidia mifugo na mazao ya chakula kama maharage ya kijani, mtama, uwele na mahindi. Tangu mwaka 2013, ni nusu ekari tu ya eneo lake ambayo imemnufaisha zaidi. &#8220;Samaki ninaowafuga hapa ni kwa ajili ya matumizi ya ndani. Pia ninapata mapato mazuri ninapouza samaki katika soko la huku nchini. Sioni wasiwasi wakati mazao yangu ya chakula yanaposhindwa kutoa mavuno,&#8221; alisema baba huyo wa watoto watano mwenye umri wa miaka 51, anayefuga ngege na kambare. Japheth Nthiga anafuga samaki aina ya ngege na kambare katika mabwawa ya samaki kwenye shamba lake eneo la kati ya Kenya. Picha na David Njagi wa Mongabay.  Ni rahisi kuelewa vizuri hisia za Nthiga. Kijiji chake, ambacho kiko takriban kilomita 150 (sawa na maili 90) kutoka ukingo wa Msitu wa Mlima Kenya, kimekumbwa na ukame wa muda mrefu na wa mara kwa mara kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita. Ili kukabiliana na msimu wa kiangazi, wakulima, hasa wale wanaotoka katika nyanda za juu za mito, wamezidisha matumizi yao ya mbolea ili kuongeza mavuno, na kwa kufanya hivyo, wamesababisha uchafuzi wa mito na kupoteza rutuba ya udongo katika eneo hilo, kulingana na Venter Mwongera, ambaye ni mratibu wa mawasiliano&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>