<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=kilimo-mseto&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/kilimo-mseto/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 28 Aug 2026 16:47:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/#respond</comments>
					<pubDate>17 Julai 2026 19:39:13 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ouma Elvine Tina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/17192647/Screenshot-2026-07-17-221755.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2139</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Akili Mnemba, Biashara ya Kilimo, Chakula, Jinsia na Uhifadhi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo serikali ya ukoloni ya Uingereza iliitengea jamii ya Wanubi baada ya mababu zao kutumikia kama askari kwenye jeshi la King’s African Rifles. Awali, eneo hilo lilikuwa na ukubwa wa hekta 1,698 (ekari 4,197). Leo, kutokana na ukuaji wa miji, kufukuzwa kwa nguvu, uporaji wa ardhi na miradi mbalimbali ya serikali iliyotekelezwa kwa nyakati tofauti, ni hekta 116 (ekari 288) pekee zilizosalia mikononi mwa Wanubi, bila wao kuwahi kulipwa fidia yoyote. Kupitia Mazingira Women Initiative, Hamida ametumia zaidi ya miaka 25 kujihusisha na masuala ya usimamizi wa taka, kilimo kinachotumia teknolojia za kisasa, haki za kumiliki ardhi, na uongozi wa wanawake. Pia amewahi kugombea ubunge mara tatu katika eneo bunge la Kibera na ana mpango wa kugombea tena mwaka wa 2027. Hamida alizungumza na Mongabay mchana wa Jumamosi ya baridi, wakati alipokuwa akiondoka kwenye msikiti mkubwa zaidi katika eneo bunge la Kibera. Ofisi zake zilikuwa karibu, mwendo mfupi tu kutoka hapo. Tulipokuwa tukielekea huko, watu kadhaa walimsimamisha ili kumsalimia. Aliwajibu kila mmoja kwa kusema &#8220;Assalaamu aleikum,&#8221; akasimama kidogo ili kupiga nao gumzo, na akamshika msichana mdogo usoni kwa upole. Aliniongoza kupitia lango la mabati hadi kwenye eneo tulivu lenye nyumba zenye kuta za udongo na paa za mabati. Eneo hilo lilikuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/#comments</comments>
					<pubDate>08 Julai 2026 18:36:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/08182238/2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2033</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Aina Vamizi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Mazao ya kilimo kimoja, Mgogoro wa Binadam na Tembo, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Migogoro, Mimea, Mimea yenye Tiba, Tabia za Wanyama, Tembo, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Ustawi wa Wanyama, Wanyama, Wanyama maarufu, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Pilipili na usingizi wa amani: Kinamama wa Maasai Mara waandika upya hadithi ya kuishi na tembo waharibifu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nyimbo za jadi za Kimaasai zinasikika taratibu katika Enkutoto, eneo la Maasai Mara, ambalo kwa miaka mingi limeishi katika kivuli cha migogoro mikali kati ya binadamu na tembo. Chini ya jua kali la mchana, wanawake wameinama mashambani. Mikono yao inasonga kwa ustadi ikipalilia mistari mirefu ya pilipili, rosemary, mti wa chai, na lavender. Mabadiliko makubwa ya mandhari yameshuhudiwa hapa. Badala ya mashamba mapana ya mahindi pekee kama ilivyokuwa zamani, ardhi sasa imepambwa na rangi ya kijivu, kijani kibichi na zambarau, ya mimea hii ya manukato. Wanawake hapa wana matumaini mapya, si tu ya kulinda maisha yao, bali ya kuendeleza kilimo chenye tija ya kiuchumi. Miongoni mwa wanawake hao ni Nelly Musana kutoka Enkutoto, na mwanachama wa kikundi cha kina mama cha Oloisesiai Self Help Group. Karibu yake yupo Mama Arami Musekenya, mama wa watoto sita, mfugaji na mkulima mzaliwa wa Maasai Mara ambaye maisha yake yote ameshuhudia migogoro kati ya binadamu na wanyamapori. Kwa miaka mingi, wanawake hawa waliishi kwa hofu kubwa. Hofu hiyo haikuja mchana; ilikuja usiku, hasa wakati mahindi yalipoanza kuzaa na kukomaa. “Tembo walikuwa wakija bila hodi,” anasema Musekenya, huku akitazama shamba lililojaa rosemary. “Kitu kibaya si kuona tembo; ni kuamka asubuhi ukute hakuna kitu kabisa.” Kiwango cha uharibifu unaofanywa na wanyama hawa wakubwa ni jambo la kutia wasiwasi mkubwa na linaloacha familia katika umaskini wa ghafla. Musekenya anasimulia kuwa kuna nyakati ambapo kundi la tembo watano tu linaweza kuingia shambani na ndani ya usiku mmoja tu, wanamaliza kabisa ekari tano za mahindi. Uharibifu huo wa kasi ya ajabu unamaanisha kuwa jasho&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/08/pilipili-na-usingizi-wa-amani-kinamama-wa-maasai-mara-waandika-upya-hadithi-ya-kuishi-na-tembo-waharibifu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/#respond</comments>
					<pubDate>02 Agosti 2023 12:48:18 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/05054458/Screenshot-2025-10-05-083758-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=607</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Kijani, Kilimo, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Kupunguza Umaskini, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Ufugaji Samaki, Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, huku shamba lake lililosalia, likisaidia mifugo na mazao ya chakula kama maharage ya kijani, mtama, uwele na mahindi. Tangu mwaka 2013, ni nusu ekari tu ya eneo lake ambayo imemnufaisha zaidi. &#8220;Samaki ninaowafuga hapa ni kwa ajili ya matumizi ya ndani. Pia ninapata mapato mazuri ninapouza samaki katika soko la huku nchini. Sioni wasiwasi wakati mazao yangu ya chakula yanaposhindwa kutoa mavuno,&#8221; alisema baba huyo wa watoto watano mwenye umri wa miaka 51, anayefuga ngege na kambare. Japheth Nthiga anafuga samaki aina ya ngege na kambare katika mabwawa ya samaki kwenye shamba lake eneo la kati ya Kenya. Picha na David Njagi wa Mongabay.  Ni rahisi kuelewa vizuri hisia za Nthiga. Kijiji chake, ambacho kiko takriban kilomita 150 (sawa na maili 90) kutoka ukingo wa Msitu wa Mlima Kenya, kimekumbwa na ukame wa muda mrefu na wa mara kwa mara kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita. Ili kukabiliana na msimu wa kiangazi, wakulima, hasa wale wanaotoka katika nyanda za juu za mito, wamezidisha matumizi yao ya mbolea ili kuongeza mavuno, na kwa kufanya hivyo, wamesababisha uchafuzi wa mito na kupoteza rutuba ya udongo katika eneo hilo, kulingana na Venter Mwongera, ambaye ni mratibu wa mawasiliano&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>