<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=halijoto&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/halijoto/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 14:23:41 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/#respond</comments>
					<pubDate>26 Agosti 2026 20:21:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Sean Mowbray]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/26193037/Screenshot-2026-08-26-222742-768x495.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2618</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Amazon, Amerika ya Kaskazini, Amerika ya Kati, Amerika ya Kusini, Asia, Ethiopia, India, Sri Lanka, Ukraine, Ulaya, Ulimwenguni, na  Urusi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Elimu ya Mazingira, Halijoto, Huduma za Mazingira, Mafuriko, Magonjwa, Maji, Maji ya kunywa, Mazao, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, Uhamishaji, Ukame, upatikanaji wa chakula, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Sharti dunia ijifunze kwa yaliyopita ili kujiandaa kwa tukio lisilo la kawaida la El Niño linaloweza kutokea</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mataifa ulimwenguni kote yanajiandaa kwa tukio la El Niño ambalo linazidi kuonekana kuwa ya kihistoria; mifumo ya kisasa ya utabiri ikionyesha kuwa tukio la 2026-2027 huenda likawa na nguvu zaidi kuwahi kuripotiwa, na huenda likavunja rekodi kwa kiwango kikubwa na cha hatari. Mashirika ya kimataifa, yakiwemo Shirika la Afya Duniani (WHO), Shirika la Hali ya Hewa Duniani (WMO) na Shirika la Umoja wa Mataifa la Mpango wa Chakula Duniani (WFP), yanazihimiza mataifa kujiandaa kwa hali mbaya ya hewa na athari zitakazofuata katika sekta za afya, chakula na nishati. Tayari baadhi ya mataifa yanachukua hatua: Brazil imeajiri wazima moto wengi kupambana na moto wa misitu unaotarajiwa katika Amazon. Peru, iliyokumbwa na mvua kubwa, mafuriko na maporomoko ya ardhi katika matukio ya El Niño yaliyopita, imetangaza hali ya hatari katika 40% ya maeneo ya nchi hiyo. Sri Lanka imepanga kuwapatia maji watu karibu 72,000 katika wilaya saba zinazokabiliwa na ukame, na India inalenga wilaya 300 zinazokabiliwa na ukame, ikiimarisha mipango ya dharura ya kilimo na kuongeza mipango ya umwagiliaji. Umoja wa Afrika unatoa wito kwa nchi wanachama kuimarisha mifumo ya tahadhari za mapema ili kulinda &#8220;maisha, riziki na uchumi katika miezi ijayo.&#8221; Ukame mkali nchini Ethiopia  wakati wa tukio la El Niño mwaka 2015 ulisababisha mgogoro wa kibinadamu uliowaathiri zaidi ya watu milioni 10. Hapa, Umoja wa Ulaya (EU) na shirika lisilo la kiserikali la Oxfam zinasambaza lori la kusafirisha maji ili kutoa maji ya dharura nayohitajika. Picha na ©EU/ECHO/Anouk Delafortrie kupitia Flickr (CC BY-NC-ND 2.0). Hata hivyo, nchi nyingi hazijajiandaa: Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) limetoa wito wa dharura wa $202 milioni kwa ajili ya Wito wa pamoja wa kuchukua&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/26/sharti-dunia-ijifunze-kwa-yaliyopita-ili-kujiandaa-kwa-tukio-lisilo-la-kawaida-la-el-nino-linaloweza-kutokea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/#respond</comments>
					<pubDate>30 Julai 2026 12:22:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/30073721/Magari2-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2264</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Halijoto, Kaboni, Mabadiliko ya Tabianchi, Maliasili, Mazingira, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, Sera za Mazingira, Serikali, Sheria, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Siasa za Tabianchi, Teknolojia, Uendelevu, na  Ufanisi wa nishati]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Safari ya Tanzania kuelekea matumizi ya nishati safi katika usafiri: Nini kimefanyika hadi sasa?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Na Mpango wa Tanzania wa kuhamia matumizi ya nishati safi katika usafiri ili kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari, umeanza kutekelezwa. Hadi sasa baadhi ya hatua za mpango huo zinaendelea kutekelezwa kwa mafanikio ingawa pia kuna changamoto kadhaa zinazohitaji kushughulikiwa. Juni 12, mwaka huu, serikali ya Tanzania ilitangaza dhamira yake ya kuhamia matumizi ya nishati safi kwenye vyombo vya usafiri kwa kuzielekeza taasisi zote za umma kuanza kujumuisha ununuzi wa magari yanayotumia umeme na gesi asilia katika mipango na bajeti zao. Waziri wa Fedha, Balozi Khamis Mussa Omari, wakati akiwasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2026/2027 bungeni jijini Dodoma, alisema lengo la mpango huo ni kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na kupunguza gharama kubwa za kununua mafuta. Bajaji zinazotumia umeme. Picha ya Jenifer Gilla, Mongabay. Hatua hiyo pia ni sehemu ya utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050  na Michango ya Taifa Iliyoamuliwa (NDCs) chini ya Mkataba wa Paris ambapo Tanzania imeahidi kupunguza uzalishaji wa gesi chafu kupitia sekta za nishati na usafiri. Uzalishaji wa hewa ya ukaa Mpango wa kutumia nishati safi kwenye vyombo vya usafiri nchini Tanzania, iwapo utafanikiwa, utapunguza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa hewa ukaa inayotokana na mafuta ya magari ambayo huchochea athari za mabadiliko ya tabianchi. Msololo Onditi, Mtaalam wa mabadiliko ya tabianchi na Mshauri wa Masuala ya mabadiliko ya tabianchi katika Shirika la Maendeleo la Ujerumani Tanzania (GIZ), anasema kila lita moja ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/30/safari-ya-tanzania-kuelekea-matumizi-ya-nishati-safi-katika-usafiri-nini-kimefanyika-hadi-sasa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 10:41:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Naina Rao]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03103608/Screenshot-2026-06-03-132733-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1749</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Amerika ya Kaskazini, Marekani, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Halijoto, Kudhibiti Ongezeko la Joto Duniani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila nusu ya kila mchezo &#8220;ili kuhakikisha hali bora zaidi kwa wachezaji&#8221;. Hata hivyo, uchambuzi wa hivi majuzi unasema Kombe la Dunia la 2026, lililoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Meksiko na Kanada, litakuwa na joto kali zaidi kuliko mashindano ya Marekani ya &#8217;94. Wanasayansi kutoka World Weather Attribution (WWA), mtandao wa kimataifa wa watafiti wanaochunguza mchango wa mabadiliko ya tabianchi katika matukio ya hali mbaya ya hewa, wanaonya kuwa mabadiliko ya tabianchi yameongeza karibu mara mbili uwezekano wa joto kali tangu wakati huo. Hiyo inafanya iwe vigumu zaidi kuondoa joto mwilini, alisema Chris Mullington, mshauri wa kutia ganzi na mhadhiri mkuu wa kliniki katika Imperial College London. &#8220;Hiyo ni muhimu kwa sababu wanasoka huzalisha kiasi kikubwa cha joto mwilini wanapokimbia mara kwa mara, kuongeza kasi na kucheza kwa kiwango cha juu cha ushindani,&#8221; alisema katika mkutano na waandishi wa habari. &#8220;WBGT inapoongezeka, mifumo ya kawaida ya kupoeza ya mwili inakuwa dhaifu.&#8221; WBGT ni kipimo cha joto kinachojumuisha halijoto ya hewa, unyevunyevu, mionzi ya jua na kasi ya upepo, na hutoa &#8220;hisia halisi&#8221; ya joto kwenye mwili wa mwanadamu. Mullington alisema viwango vya juu vya WBGT vinaweza kulazimisha wachezaji &#8220;kupunguza kasi ya kukimbia mara kwa mara, kujiendesha kwa uangalifu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>