<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?location=asia&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 06 Aug 2026 18:12:10 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/#respond</comments>
					<pubDate>18 Juni 2026 08:35:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/18080931/Screenshot-2026-06-18-110907-768x439.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1874</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Asia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Asidi ya Bahari, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bahari ya Kina, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Fedha za Uhifadhi, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mashirika ya baharini yanayoongozwa na jamii za Kiafrika ni muhimu kwa mafanikio ya lengo la 30×30</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii, maelfu ya wajumbe wamekusanyika mjini Mombasa, Kenya, kwa Kongamano la kwanza la “Our Ocean” kuandaliwa katika ardhi ya Afrika. Kama inavyotarajiwa, mazungumzo mengi yatalenga shabaha ya kimataifa ya mfumo wa uhifadhi wa &#8220;30×30&#8221; &#8211; kulinda 30% ya ardhi, maji safi na bahari duniani ifikapo 2030. Hata hivyo, mbali na kumbi za mikutano, ahadi kubwa za kimataifa na za serikali, watu wengi wanaofanya kazi ya kila siku ya uhifadhi wa baharini ni mashirika ya kijamii yanayofanya kazi kwa bajeti ndogo katika ukanda wa pwani wa Afrika. Mara nyingi hufanya hivyo mbali na kuangaziwa, lakini mchango wao ni muhimu kwa nia ya kimataifa ya kuhifadhi nafasi za bahari. Mkataba wa Anuwai ya Kibiolojia (CBD), ambao chini yake Mfumo wa Bioanuwai wa Kunming-Montreal ulipitisha malengo ya mwaka 2030, unaonyesha kuwa mafanikio yanategemea sana ushirikishwaji wa jamii. Kote nchini Kenya, Tanzania na Namibia, vikundi vinne kama hivyo &#8211; Maendeleo ya Rasilimali za Pwani na Bahari (COMRED) Action for Ocean, Mwambao Coastal Community Network na Namibia Nature Foundation (NNF) &#8211; hutoa fursa ya kufahamu jinsi uhifadhi wa bahari unaoongozwa na jamii unavyotekelezwa kwa vitendo. Kazi yao inaweza kuwa na ufadhili wa chini, kutofautiana na wakati mwingine polepole, lakini inazidi kuwa msingi wa jinsi ulinzi wa baharini unavyowaziwa katika bara. Mifumo ya ikolojia ya baharini barani Afrika inasaidia uvuvi, utalii, uchukuzi, uhifadhi wa kaboni na ulinzi wa pwani huku ikiendeleza mamilioni ya riziki kutoka Bahari ya Hindi Magharibi hadi pwani ya Afrika ya Atlantiki na Mediterania. Katika Afrika Mashariki hasa, mikoko, miamba ya matumbawe, nyasi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/18/mashirika-ya-baharini-yanayoongozwa-na-jamii-za-kiafrika-ni-muhimu-kwa-mafanikio-ya-lengo-la-30x30/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/#respond</comments>
					<pubDate>16 Juni 2026 15:28:54 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/16152623/Aquatic-animal-production-from-aquaculture-topped-100-million-tonnes-for-the-first-time-in-2024-according-to-FAOs-latest-State-of-World-Fisheries-and-Aquaculture-report-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1861</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Asia, na  Bahari ya Hindi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Bahari, Baharini, Biashara ya Kimataifa, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Kasa wa baharini, Mamalia wa Baharini, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Uhifadhi wa Baharini, Utafiti, Uvuvi, Viwango vya Bahari, Wanyama wa Baharini, na  Wenyeji wa Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">FAO: Ufugaji wa viumbe vya majini waweka rekodi mpya huku biashara ya dunia ikifikia dola bilioni 184</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kufikia mwaka 2024, biashara ya bidhaa za majini duniani ilifika $186 bilioni. Kati ya hizo, $184 bilioni zilihusishwa na biashara ya bidhaa za majini pekee, ilhali $2 bilioni zilihusishwa na biashara ya mwani na mazao mengine. Biashara hiyo ilihusisha maeneo ya kiuchumi 230 kote ulimwenguni. Hii ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa [FAO] ambayo pia imeeleza kuwa sekta hiyo inayohusiana na uvuvi na ufugaji wa samaki na viumbe wengine wa majini iliajiri wafanyakazi zaidi ya milioni 65, na hivyo kuwa tegemeo la maisha ya watu zaidi ya milioni 600 kote duniani. FAO ilizindua ripoti hiyo mpya ya Hali ya Uvuvi na Ufugaji wa Viumbe vya Majini Duniani (SOFIA 2026) kwenye mkutano wa 11 wa Bahari Yetu [11th Our Ocean Conference] uliofanyika jijini Mombasa, nchini Kenya. Ripoti hiyo imeeleza kuwa uzalishaji wa uvuvi na ufugaji wa viumbe vya majini duniani ulifikia rekodi ya tani milioni 235 kwa mwaka 2024. Pia uzalishaji wa wanyama wa majini ulifikia tani milioni 195 na umeendelea kukua kwa wastani wa asilimia 3.2 kwa mwaka tangu miaka ya 1950. Pia ripoti ya shirika hilo la Umoja wa Mataifa imeonyesha kuwa uvuvi wa asili umeendelea kuwa thabiti kwa kiasi kikubwa tangu mwishoni mwa miaka ya 1980, hali inayochangiwa na juhudi za usimamizi wa uvuvi na uhifadhi wa mazingira katika baadhi ya maeneo. Aidha, ilibainika kuwa ufugaji wa viumbe vya majini ulizalisha tani milioni 103 za wanyama wa majini, rekodi ya juu zaidi kuwahi kushuhudiwa. Hii ni sawa na asilimia 53 ya uzalishaji wote wa viumbe vya majini duniani, na zaidi ya asilimia 59&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/16/fao-ufugaji-wa-viumbe-vya-majini-waweka-rekodi-mpya-huku-biashara-ya-dunia-ikifikia-dola-bilioni-184/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/#respond</comments>
					<pubDate>04 Mei 2026 13:28:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/04145740/Screenshot-2026-05-04-160903.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1493</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi, Asia, Asia ya Kusini-mashariki, Guinea, Indonesia, Mali, Msumbiji, Senegal, Singapore, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Magonjwa, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Ndege, Ugonjwa wa Kuambukiza wa Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano ya uimbaji wa hali ya juu. Wafugaji wa ndege aina ya vipanga na wawindaji wa michezo hukamata au kuua ndege wa porini. Matambiko ya imani za jadi katika Afrika Magharibi hujumuisha viwiliwili vya tai. Wanunuzi kutoka Marekani ya Kaskazini hutafuta hondohondo na ndege mvumaji waliokufa kama mapambo ya nyumbani. Orodha inaendelea. Biashara hii kubwa inatisha zaidi ya spishi 200 za ndege kutoweka. Sasa, huku masoko ya mtandaoni yakiongezeka, wateja wanaweza kuagiza ndege kwa kubonyeza simu zao za mkononi kutoka mahali popote katika sayari. Kusafirisha ndege kote ulimwenguni pia husambaza magonjwa hatari, kama vile homa ya ndege na virusi vwa circovirus, na wakati ndege wasio wa asili wanapotoroka au kuachiliwa, wanaweza kuongezeka kuwashinda spishi za asili. &#8220;Kuna ukosefu wa ufahamu na kuthamini ukubwa wa biashara hii, na umakini mchache sana juu ya athari ambazo hii inaweza kuwa nayo kwa wakazi wa porini au hatari za kuenea kwa viumbe vamizi na magonjwa ya kuambukiza,&#8221; Rowan Martin ni mkurugenzi wa biashara ya ndege katika shirika lisilo la faida la World Parrot Trust. &#8220;Ikiwa watu hawajui kwamba hili linafanyika, basi tutawezaje kupunguza hatari zinazohusiana nayo?&#8221; Katika kujaribu kuelewa ukubwa wa biashara ya ndege hai, Martin na wenzake walitumia hifadhidata ya Umoja wa Mataifa ya Comtrade (UN Comtrade), hifadhidata inayojumlisha taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Chui waliosahaulika wazidi kutoweka kwenye kivuli cha uwindaji haramu na biashara</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/06/26/chui-waliosahaulika-wazidi-kutoweka-kweye-kivuli-cha-uwindaji-haramu-na-biashara/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/06/26/chui-waliosahaulika-wazidi-kutoweka-kweye-kivuli-cha-uwindaji-haramu-na-biashara/#respond</comments>
					<pubDate>26 Juni 2025 09:26:18 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/11152203/leopard-leopard-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=68</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Asia, Asia ya Kusini, Asia ya Kusini-mashariki, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara Haramu, Biashara ya Wanyamapori ya China, Bioanuai, Chui, Cites, Kanuni, Paka, Paka Wakubwa, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Ujangili, Usafirishaji wa Wanyamapori, Utafiti, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Chui ni mnyama anayependa faragha, mwenye tabia ya kuficha mambo, anayependa kuwinda usiku, huku akijitenga na jamii. Kimaumbile, ana manyoya ya rangi ya dhahabu yenye madoadoa meusi. Mnyama huyu ni mmoja kati ya paka wakubwa wa porini, na wameenea sana kote duniani. Kwa mara nyingi, chui waanapatikana katika mazingira kama vile misitu ya mvua, milima [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/26/chui-waliosahaulika-wazidi-kutoweka-kweye-kivuli-cha-uwindaji-haramu-na-biashara/" data-wpel-link="internal">Chui waliosahaulika wazidi kutoweka kwenye kivuli cha uwindaji haramu na biashara</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Chui ni mnyama anayependa faragha, mwenye tabia ya kuficha mambo, anayependa kuwinda usiku, huku akijitenga na jamii. Kimaumbile, ana manyoya ya rangi ya dhahabu yenye madoadoa meusi. Mnyama huyu ni mmoja kati ya paka wakubwa wa porini, na wameenea sana kote duniani. Kwa mara nyingi, chui waanapatikana katika mazingira kama vile misitu ya mvua, milima yenye miamba, nyika, nyanda na hata jangwani, katika hali ya joto na pia hata baridi. Kwa jumla, kuna aina ndogo nane za chui duniani, zilizogawanywa kulingana na maeneo wanayoishi na muonekano wao. Kumbukumbu za kihistoria zinaonyesha kuwa chui walienea Asia na Afrika, Kusini mwa Jangwa la Sahara, lakini kwa sasa, eneo lao limepungua zaidi. Chui (Panthera pardus) sasa wanapatikana Asia ya Kati, Kusini mwa Asia, Afrika, na maeneo madogo Mashariki na Kusini-Mashariki mwa Asia. India pia ina idadi ya chui wengi zaidi duniani, takriban 14,000, ambao wanaishi porini. Licha ya kuwepo kwao kwenye kiambatisho cha CITES (Huu ni mkataba wa kimataifa wa biashara ya wanyamapori na mimea pori vilivyo hatarini kutoweka) — ambao umepiga marufuku biashara ya kimataifa ya mnyama huyu — chui wamethibitishwa kuwa paka mwitu wa pili kuuzwa zaidi duniani, wakitanguliwa na simba, ambao biashara yao inadhibitiwa. Hata hivyo, vitisho dhidi ya chui havijapewa kipaumbele, licha ya tamaa kubwa ya viungo vyao, ambayo imechochea biashara na uwindaji haramu. “Serikali nyingi zinatoa taarifa zaidi kuhusu chui milia (tigers) kuliko chui wa kawaida,” anasema Debbie Banks, ambaye ni kiongozi wa kampeni dhidi ya uhalifu wa wanyamapori kwenye shirika la Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/26/chui-waliosahaulika-wazidi-kutoweka-kweye-kivuli-cha-uwindaji-haramu-na-biashara/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/06/26/chui-waliosahaulika-wazidi-kutoweka-kweye-kivuli-cha-uwindaji-haramu-na-biashara/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>