<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=fedha&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 31 Jul 2026 11:04:46 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 19:43:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11194040/Vijana-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1846</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Fedha, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa Umoja wa Mataifa wenye makao yake nchini Uswisi unaofadhiliwa kupitia michango ya hiari kutoka kwa nchi zilizoendelea na jumuiya ya kimataifa, zitatolewa kupitia serikali na kusambazwa kwa jamii mbalimbali nchini zinazokabiliwa na majanga mbalimbali yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi. Majanga hayo ni pamoja na ukame wa mara kwa mara, mafuriko, kupungua kwa uzalishaji wa mazao, uharibifu wa mazao na matukio mengine ya hali mbaya ya hewa. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Misitu wa Kenya, Festus Ng’eno, alisema msaada huo ni hatua muhimu sana. Ng’eno alisema hatua hiyo inaifanya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na mfuko huo. Vanuatu, taifa la funguvisiwa lenye maeneo mengi ya mwinuko wa chini, ndiyo iliyokuwa nchi ya kwanza duniani kupata ufadhili huo. Ng’eno alitoa taarifa hiyo katika mazungumzo yaliyofanyika sambamba na mazungumzo ya kiufundi ya tabianchi ya UNFCCC Subsidiary Bodies (SB64) yanayoendelea huko Bonn, Ujerumani. Katika taarifa aliyochapisha mtandaoni, akithibitisha habari iliyochapishwa na gazeti la People Daily mnamo Juni 10, Dkt Ng’eno alisema kuwa licha ya Kenya kupitia baadhi ya majanga makubwa zaidi ya tabianchi katika Afrika Mashariki, nchi hiyo haijawahi kupima kikamilifu kiwango halisi cha hasara iliyopata kutokana na majanga hayo. &#8220;Hali hiyo sasa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/#respond</comments>
					<pubDate>12 Aprili 2026 14:52:07 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/12143649/Green-Climate-Fund.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1342</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Fedha na .Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  tabianchi. Kwa mujibu wa taarifa ya GCF kwa Mongabay, kwa sasa mfuko huo unaunga mkono miradi minne nchini Kenya na miradi 23 ya kikanda inayohusisha nchi nyingi. “GCF hutoa ufadhili kupitia washirika waliothibitishwa; taasisi za kifedha zilizoidhinishwa kufanya kazi na mfuko huu. Taasisi hizi zinakidhi viwango vya GCF na zinaendana na dhamira ya mfuko ya kuleta mabadiliko chanya katika kukabiliana na tabianchi,” alisema Catherine Koffman, Mkurugenzi wa Idara ya Kanda ya Afrika wa GCF. Katika barua pepe kwa Mongabay, Rebecca Phwitiko, Mtaalamu wa Mawasiliano wa GCF (Vyombo vya Habari na Maudhui), alieleza kuwa maeneo makubwa wanayolenga kufanyia kazi yanajumuisha kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo inayostahimili mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yenye ukame. Mengine ni kurejesha maeneo ya malisho na vyanzo vya maji vilivyoharibika ili kuboresha upatikanaji wa maji na maisha ya watu, kupanua matumizi ya nishati jadidifu na nishati safi za kupikia, pamoja na kufungua fursa za ufadhili mseto kwa teknolojia rafiki kwa tabianchi kupitia taasisi za kifedha za ndani. Miradi inayoungwa mkono na GCF nchini Kenya yenye thamani ya $493 milioni inalenga kuleta manufaa makubwa, “ikiwa ni pamoja na kuboresha usalama wa chakula, kuimarisha ustahimilivu wa maji, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>