<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=tropiki&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Tue, 04 Aug 2026 18:45:21 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Olivier Nsengimana wa Rwanda ahamasisha ulinzi wa Korongo wa Kijivu Afrika Mashariki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/04/30/olivier-nsengimana-wa-rwanda-ahamasisha-ulinzi-wa-korongo-wa-kijivu-afrika-mashariki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/04/30/olivier-nsengimana-wa-rwanda-ahamasisha-ulinzi-wa-korongo-wa-kijivu-afrika-mashariki/#respond</comments>
					<pubDate>30 Aprili 2025 06:52:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Musinguzi Blanshe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
		<category><![CDATA[Afrika]]></category>
		<category><![CDATA[Afrika Mashariki]]></category>
		<category><![CDATA[Ardhi iliyoharibika]]></category>
		<category><![CDATA[Mabwawa]]></category>
		<category><![CDATA[Maeneo ya tropiki]]></category>
		<category><![CDATA[Maji]]></category>
		<category><![CDATA[Makazioevu]]></category>
		<category><![CDATA[Mazingira]]></category>
		<category><![CDATA[Ndege]]></category>
		<category><![CDATA[Rwanda]]></category>
		<category><![CDATA[Sera ya mazingira]]></category>
		<category><![CDATA[Spishi hatarini kutoweka]]></category>
		<category><![CDATA[Uganda]]></category>
		<category><![CDATA[Uhai anuai]]></category>
		<category><![CDATA[Uhifadhi]]></category>
		<category><![CDATA[Utawala]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/21062755/RO1-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=105</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Rwanda, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ardhi iliyoharibika, Bioanuai, Maeneo Oevu, Maji, Mazingira, Ndege, Sera za Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tropiki, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Shirika la Uhifadhi wa Wanyamapori Rwanda (Rwanda Wildlife Conservation Association &#8211; RWCA), linaloongozwa na daktari wa wanyama Olivier Nsengimana, limekuwa mstari wa mbele katika kampeni ya kukomesha tabia ya kufuga korongo kama wanyama wa kufugwa majumbani, likiwa limefanikiwa kuwahifadhi tena na kuwaachilia huru ndege wengi waliokuwa mateka. Shirika hilo pia linawahusisha wanajamii katika kuimarisha ulinzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/30/olivier-nsengimana-wa-rwanda-ahamasisha-ulinzi-wa-korongo-wa-kijivu-afrika-mashariki/" data-wpel-link="internal">Olivier Nsengimana wa Rwanda ahamasisha ulinzi wa Korongo wa Kijivu Afrika Mashariki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Shirika la Uhifadhi wa Wanyamapori Rwanda (Rwanda Wildlife Conservation Association &#8211; RWCA), linaloongozwa na daktari wa wanyama Olivier Nsengimana, limekuwa mstari wa mbele katika kampeni ya kukomesha tabia ya kufuga korongo kama wanyama wa kufugwa majumbani, likiwa limefanikiwa kuwahifadhi tena na kuwaachilia huru ndege wengi waliokuwa mateka. Shirika hilo pia linawahusisha wanajamii katika kuimarisha ulinzi wa makazi ya korongo kwenye maeneo ya mabwawa dhidi ya uvamizi na uharibifu — mbinu ambayo sasa inaenezwa hadi nchi jirani kupitia ushirikiano na mashirika mengine yasiyo ya kiserikali. Kwa juhudi hizi, Nsengimana ametunukiwa Tuzo ya Dhahabu ya Whitley ya mwaka 2025, na hivyo kuwa mshindi wa tuzo hiyo kwa mara ya pili baada ya kuipokea kwa mara ya kwanza mwaka 2018. Miaka 10 tu iliyopita, kuona korongo wa rangi ya kijivu katika maeneo oevu ya Rwanda lilikuwa jambo la kawaida. Ndege hawa wa kifahari &#8211; warefu na wenye sura nzuri, wakiwa na manyoya ya dhahabu vichwani mwao &#8211; waliwahi kusitawi Afrika Mashariki. Lakini kufikia katikati ya muongo uliopita, idadi yao nchini Rwanda ilikuwa imepungua sana. &#8220;Ilinishtua,&#8221; anasema Olivier Nsengimana, daktari wa mifugo na mhifadhi wa Rwanda ambaye alianzisha RWCA. Anasema sensa ya mwaka 2017 ilihesabu chini ya ndege 500 kote nchini. &#8220;Tulikuwa na korongo wengi katika nyumba za watu kuliko walivyokuwa porini.&#8221; Wakikabiliwa na upotevu wa makazi, kutekwa kwa biashara haramu kama wanyama wa kufugwa majumbani, na vitisho vingine, korongo wa rangi ya kijivu (Balearica regulorum) alikuwa akitoweka kimya kimya na kutoweka kabisa nchini Rwanda. Hadithi kama hiyo ilikuwa ikitokea katika nchi jirani, zikiwemo Burundi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/04/30/olivier-nsengimana-wa-rwanda-ahamasisha-ulinzi-wa-korongo-wa-kijivu-afrika-mashariki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/04/30/olivier-nsengimana-wa-rwanda-ahamasisha-ulinzi-wa-korongo-wa-kijivu-afrika-mashariki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatua ndogo zafungua njia kwa lengo kubwa la kuhifadhi maeneo oevu ya Afrika Mashariki</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/08/06/hatua-ndogo-zafungua-njia-kwa-lengo-kubwa-la-kuhifadhi-maeneo-oevu-ya-afrika-mashariki/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/08/06/hatua-ndogo-zafungua-njia-kwa-lengo-kubwa-la-kuhifadhi-maeneo-oevu-ya-afrika-mashariki/#respond</comments>
					<pubDate>06 Agosti 2024 15:32:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Petro Kotzé]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/01134847/262edbfc-d376-4841-bfe7-23d02866f032-768x371.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=305</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, Ethiopia, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ardhi iliyoharibika, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo Oevu, Maji, Mazingira, Maziwa, Mito, Sera za Mazingira, Tropiki, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miaka mitatu baada ya mradi wenye matumaini makubwa ya kurejesha ubora wa ardhi oevu katika maeneo ya Afrika Mashariki, Mhifadhi Julie Milonga anasema kuwa amejifunza mambo mengi kuhusu thamati ya hatua moja baada ya nyingine, japo ni ndogo, katika kufikia malengo makubwa ya uhifandi na utunzaji wa mazingira. Mradi wa Kutoka Chanzo mpaka Bharini ulilenga kutunza na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/08/06/hatua-ndogo-zafungua-njia-kwa-lengo-kubwa-la-kuhifadhi-maeneo-oevu-ya-afrika-mashariki/" data-wpel-link="internal">Hatua ndogo zafungua njia kwa lengo kubwa la kuhifadhi maeneo oevu ya Afrika Mashariki</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miaka mitatu baada ya mradi wenye matumaini makubwa ya kurejesha ubora wa ardhi oevu katika maeneo ya Afrika Mashariki, Mhifadhi Julie Milonga anasema kuwa amejifunza mambo mengi kuhusu thamati ya hatua moja baada ya nyingine, japo ni ndogo, katika kufikia malengo makubwa ya uhifandi na utunzaji wa mazingira. Mradi wa Kutoka Chanzo mpaka Bharini ulilenga kutunza na kulinda maeneo ya ardhi oevu yaliyoko katika Bonde la Ufa na mikoko inayopatikana na Bahari ya Hindi na wakati huo huo kuboresha maisha ya jamii zilizoko katika maeneo ya mradi na kuwajengea uwezo wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi. “Tulianza na maono makubwa katika kutekeleza mradi huu,” anasema Mulonga, ambaye ndiye Mkurugenzi wa Wetlands International kwa upande wa Afrika Mashariki, “lakini nikiangalia tulipoanzia nakiri kuwa tulikuwa na malengo makubwa mno ambayo tulitarajia kuyafikia mapema mno.” Mradi ulianza kutekelezwa mwaka 2021 ukihusisha maeneo makubwa ya kiikologia ambayo ni Eneo la Maziwa yaliyoko katika Bonde la Ufa, likianzia kutoka Ziwa Albert na Nyanda za Juu za Ethiopia kwa upande wa kaskazini hadi Ziwa Tanganyika kwa upande wa Kusini na eneo la kiikologia la mikoko la Afrika Mashariki likianzia kusini mwa Somalia mpaka Msumbiji likijumuisha eneo la Lamu nchini Kenya, Delta ya Rufiji iliyoko Tanzania na Delta ya Mto Zambezi nchini Msumbiji. Delta ya Rufiji nchini Tanzania (Picha: Olly Wright kupitia Flickr (CC BY-NC 2.0) Mradi wa Kutoka Chanzo Mpaka Baharini (The Source to Sea Project) unahusisha maziwa ya Bonde la Ufa nchini Ethiopia na Uganda, (ambako ndege huyu aina ya korongo mwenye kichwa cheusi alipigwa picha) na kuenea hadi kusini mwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/08/06/hatua-ndogo-zafungua-njia-kwa-lengo-kubwa-la-kuhifadhi-maeneo-oevu-ya-afrika-mashariki/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/08/06/hatua-ndogo-zafungua-njia-kwa-lengo-kubwa-la-kuhifadhi-maeneo-oevu-ya-afrika-mashariki/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>