<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=sera-za-tabianchi&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 06 Aug 2026 18:12:10 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.2</generator>
				<item>
					<title>Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/#respond</comments>
					<pubDate>17 Julai 2026 19:39:13 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ouma Elvine Tina]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/17192647/Screenshot-2026-07-17-221755.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2139</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Akili Mnemba, Biashara ya Kilimo, Chakula, Jinsia na Uhifadhi, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Taka, wanawake na haki za kimazingira: Ana kwa ana na mwanaharakati wa mazingira Malasen Hamida</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Malasen Hamida, mwanamke Muislamu kutoka jamii ya Wanubi katika mtaa wa Kibera, jijini Nairobi, ni mwanasiasa mtarajiwa na mwanaharakati wa mazingira mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 25 katika utetezi. Kibera, jina ambalo katika lugha ya Kinubi linamaanisha “ardhi ya misitu”, ndilo eneo kubwa zaidi la makazi yasiyo rasmi nchini Kenya; lililoko kwenye ardhi ambayo serikali ya ukoloni ya Uingereza iliitengea jamii ya Wanubi baada ya mababu zao kutumikia kama askari kwenye jeshi la King’s African Rifles. Awali, eneo hilo lilikuwa na ukubwa wa hekta 1,698 (ekari 4,197). Leo, kutokana na ukuaji wa miji, kufukuzwa kwa nguvu, uporaji wa ardhi na miradi mbalimbali ya serikali iliyotekelezwa kwa nyakati tofauti, ni hekta 116 (ekari 288) pekee zilizosalia mikononi mwa Wanubi, bila wao kuwahi kulipwa fidia yoyote. Kupitia Mazingira Women Initiative, Hamida ametumia zaidi ya miaka 25 kujihusisha na masuala ya usimamizi wa taka, kilimo kinachotumia teknolojia za kisasa, haki za kumiliki ardhi, na uongozi wa wanawake. Pia amewahi kugombea ubunge mara tatu katika eneo bunge la Kibera na ana mpango wa kugombea tena mwaka wa 2027. Hamida alizungumza na Mongabay mchana wa Jumamosi ya baridi, wakati alipokuwa akiondoka kwenye msikiti mkubwa zaidi katika eneo bunge la Kibera. Ofisi zake zilikuwa karibu, mwendo mfupi tu kutoka hapo. Tulipokuwa tukielekea huko, watu kadhaa walimsimamisha ili kumsalimia. Aliwajibu kila mmoja kwa kusema &#8220;Assalaamu aleikum,&#8221; akasimama kidogo ili kupiga nao gumzo, na akamshika msichana mdogo usoni kwa upole. Aliniongoza kupitia lango la mabati hadi kwenye eneo tulivu lenye nyumba zenye kuta za udongo na paa za mabati. Eneo hilo lilikuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/17/taka-wanawake-na-haki-za-kimazingira-ana-kwa-ana-na-mwanaharakati-wa-mazingira-malasen-hamida/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>10 Novemba 2025 09:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[John Cannon]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/12101218/Screenshot-2025-11-12-131027-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=769</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Hali ya Hewa, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mazingira, Nishati safi, Sera za tabianchi, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Tabianchi, Uchafuzi, Ufadhili wa tabianchi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko haki ya nishati yamaanisha nini kwa Afrika?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati waandishi wawili wa Mongabay walipokitembelea kijiji cha Lukwangulo kwenye Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, walipatana na hali halisi ambayo ni ya kawaida katika maeneo mengi ya vijijini barani Afrika: Familia hutumia muda wa thamani kuchanja kuni katika misitu kwa sababu ya kupikia, mara nyingi moja ya vyanzo vyao au hata wakati mwingine,- chanzo chao pekee cha kupata nishati. Wengine wanaweza kuchangisha pesa za kutosha kwa paneli ya jua ambayo inaweza kuchajisha simu ya mkononi, kuwasha redio na kutoa mwanga kidogo kwa watoto kutwalii. Lakini kwa kawaida haitoshi kwa kazi ya msingi ya kupikia. Tofauti kubwa kati ya hali hii na ulimwengu mpana zaidi unaotumia nishati hiyo inaonekana wazi kwa walio na uwezo finyu au wasiokuwa na uwezo kabisa wa kuufikia. &#8220;Unatokea mjini &#8211; una umeme, una taa. Kwa nini wewe na sio sisi?&#8221; Mukalay Ngoyi, kiongozi kutoka kijiji cha Lukwangulo, aliiambia Mongabay. &#8220;Sisi ni wanadamu kama wewe, na tunahitaji umeme pia.&#8221; Mnamo Novemba 10, Mkutano wa 30 (COP30) wa Nchi Wanachama wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi (UNFCCC),utakuwa Belém, Brazili, kutathmini maendeleo ya kimataifa kuelekea kukabiliana na mabadiliko ya hali ya hewa kwa kupunguza uzalishaji wa kaboni. Cha msingi katika kupunguza uzalishaji huo na kufikia lengo la kuweka halijoto duniani kuwa chini ya nyuzi 2° (3.6° Fahrenheit) juu ya viwango vya kabla ya kuanza kwa viwanda ni jinsi tunavyokidhi kuongezeka kwa mahitaji ya nishati, kote duniani na katika maeneo kama kijiji cha Lukwangulo. Lakini viongozi wengi wa jamii hawatakuwa Belém, badala yake wanategemea wengine kuwawakilisha&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/11/10/mabadiliko-haki-ya-nishati-yamaanisha-nini-kwa-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>