<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=malisho-ya-ngombe&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/malisho-ya-ngombe/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Tue, 01 Sep 2026 14:42:19 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mradi unaoongozwa na wafugaji wa Kitanzania washinda tuzo ya kimataifa kwa kuimarisha uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>16 Desemba 2025 17:39:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/12/23182123/Screenshot-2025-12-23-204447-768x467.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=850</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Akili Mnemba, Ardhi iliyoharibika, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Mageuzi ya Ardhi, Malisho ya Ng'ombe, Mazingira, Mifugo, Mimea, Nyasi, Suluhisho za Asili, Teknolojia, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Ufugaji, Ufugaji wa Ng'ombe, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, na  Vikundi vya Jamii za Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wafugaji kutoka maeneo ya vijijini nchini Tanzania wametambuliwa kimataifa kwa kufanikiwa kuweka pamoja maarifa ya asili na teknolojia mpya katika juhudi za kurejesha ardhi iliyoharibika na kuhakikisha upatikanaji wa malisho. Mradi huo unaoongozwa na jamii, ujulikanao kama Sustainable Rangelands Initiative (SRI), ulibuniwa na shirika la African People &#38; Wildlife (APW). Hivi karibuni, ulishinda tuzo katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mradi unaoongozwa na wafugaji wa Kitanzania washinda tuzo ya kimataifa kwa kuimarisha uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wafugaji kutoka maeneo ya vijijini nchini Tanzania wametambuliwa kimataifa kwa kufanikiwa kuweka pamoja maarifa ya asili na teknolojia mpya katika juhudi za kurejesha ardhi iliyoharibika na kuhakikisha upatikanaji wa malisho. Mradi huo unaoongozwa na jamii, ujulikanao kama Sustainable Rangelands Initiative (SRI), ulibuniwa na shirika la African People &amp; Wildlife (APW). Hivi karibuni, ulishinda tuzo katika kipengele cha NatureTech Stewards kwenye uzinduzi wa tuzo za IUCN Tech4Nature, wakati wa Mkutano wa Dunia wa Uhifadhi wa Mazingira wa IUCN, uliofanyika Abu Dhabi Oktoba mwaka huu wa 2025. Mpango wa Sustainable Rangelands Initiative (SRI) unatekelezwa Kaskazini na Kati mwa Tanzania katika wilaya za Simanjiro, Babati, Longido, Same, Monduli, Ngorogoro, na Mwanga. Mkurugenzi wa Uhifadhi wa Jamii na Mazingira wa APW, Neovitus Sianga, anasema maeneo haya yalichaguliwa kwa kuwa ni muhimu kwa shughuli za mifugo na wanyamapori. Kupitia mpango huu, unaotekelezwa na APW kwa kushirikiana na jamii za maeneo husika, kamati za malisho za vijiji pamoja na wafuatiliaji wa maeneo ya malisho waliopatiwa mafunzo, hutumia zana za kidijitali zikiwemo simu za mkononi kukusanya taarifa kuhusu vyanzo vya maji, uoto wa asili, kasi ya ukuaji wa nyasi, afya ya udongo pamoja na uwepo wa vimelea au spishi vamizi. Nasma Mustafa, mmoja wa wafuatiliaji wa malisho kutoka Kijiji cha Engaluka, anaeleza hatua kuu za zoezi hilo: “Tunatumia kipimo cha tepu ya kupimia, kamba na simu. Kamba hulazwa juu ya ardhi kwa urefu wa mita 100, sambamba na kipimo chenye alama tano. Kisha tunaangalia ni alama zipi kati ya hizo tano zinazogusa uoto wa asili na zipi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Suluhu ya simu kwa mifugo ya wafugaji wa Kenya, afueni kwa wanyamapori pia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/11/06/suluhu-ya-simu-kwa-mifugo-ya-wafugaji-wa-kenya-afuenikwa-wanyamapori-pia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/11/06/suluhu-ya-simu-kwa-mifugo-ya-wafugaji-wa-kenya-afuenikwa-wanyamapori-pia/#respond</comments>
					<pubDate>06 Novemba 2023 04:18:16 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/10/05044012/Screenshot-2025-10-05-070556-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=616</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kilimo, Malisho ya Ng'ombe, Marejesho ya Mandhari, Mifumo ya Ikolojia, Ng'ombe, Suluhu za Uhifadhi, Ufugaji wa Ng'ombe, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ukanda wa Wanyamapori, Urejeshaji, Urejeshaji wa Ikolojia, Utalii wa Mazingira, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ENONKISHU, Kenya — Bernard Leshinga, mfugaji wa jamii ya Kimasai kutoka kusini mwa Kenya, anapenda siku isio na bughdha zozote kuendesha biashara yake ya ufugaji. Lakini hadi hivi majuzi, Leshinga hakuwa amewazia namna ya kusaidia mifugo yake kushindana kwenye malisho na wanyamapori, au kukaa kando salama dhidi ya wanyama wanaowinda wanyama wengine; wakati wafugaji walio na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/11/06/suluhu-ya-simu-kwa-mifugo-ya-wafugaji-wa-kenya-afuenikwa-wanyamapori-pia/" data-wpel-link="internal">Suluhu ya simu kwa mifugo ya wafugaji wa Kenya, afueni kwa wanyamapori pia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ENONKISHU, Kenya — Bernard Leshinga, mfugaji wa jamii ya Kimasai kutoka kusini mwa Kenya, anapenda siku isio na bughdha zozote kuendesha biashara yake ya ufugaji. Lakini hadi hivi majuzi, Leshinga hakuwa amewazia namna ya kusaidia mifugo yake kushindana kwenye malisho na wanyamapori, au kukaa kando salama dhidi ya wanyama wanaowinda wanyama wengine; wakati wafugaji walio na makazi hapa mara nyingi hujenga boma (mazizi ya kudumu au mabanda) kulinda mifugo yao nyakati za usiku, watu kama yeye ambao hutoka mbali na nyumbani mara nyingi hujitahidi kuzuia uwindaji. Na wakati nyanda za malisho zinaharibiwa na malisho ya wanyama porini kupungua kwa idadi, wanyama wanaokula wenzao katika eneo tata la Maasai Mara nchini Kenya hulenga mifugo mara kwa mara. Mafanikio kwa wafugaji kama Leshinga yalikuja mwaka wa 2017, wakati maboma ya kuhamishika yalipoanzishwa katika Hifadhi ya Enonkishu. Haya ni maboma yanayoweza kusogezwa, yenye matundu ya waya ambayo wafugaji huhifadhi mifugo yao usiku, salama dhidi ya wanyama wanaowinda wanyama wengine. Kila baada ya siku 10 wakati wa msimu wa kiangazi, wenyeji wanaowajibikia boma hizo hukusanya nguvu kazi yao ili kuhamisha shehena za maboma hadi kwenye sehemu mpya, kwa kawaida wakiwa na mikokoteni au kubeba vipande kwa mikono. Wakati wa msimu wa mvua, hufanya kazi hii kila baada ya wiki mbili. Bernard Leshinga, mfugaji wa jamii ya Kimasai aliyezaliwa katika ardhi ambayo sasa imezungukwa na Hifadhi ya jamii ya Enonkishu, yenye maboma yanayoweza kuhamishwa. Picha na David Njagi wa Mongabay. &#8220;Katika siku za nyuma, kulikuwa na ongezeko la uvamizi wa wanyama wanaowinda mifugo yetu kwa sababu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/11/06/suluhu-ya-simu-kwa-mifugo-ya-wafugaji-wa-kenya-afuenikwa-wanyamapori-pia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/11/06/suluhu-ya-simu-kwa-mifugo-ya-wafugaji-wa-kenya-afuenikwa-wanyamapori-pia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>