<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=kasa&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/kasa/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 28 Aug 2026 16:47:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 17:31:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20141013/Screenshot-2026-03-20-171000-768x509.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1178</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Baharini, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maji, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii kama ilivyokuwa desturi. Nyama ya kasa ni tamu sana, na tulikuwa tunafurahia sana kitoweo chake,” alisema Abdallah. Kasa katika ufuo wa bahari Shimoni picha na Dzivula Gube Miaka 35 baadaye, Abdallah, ambaye amefanya uvuvi kwa miaka tisa sasa katika eneo la Shimoni, amekuwa mkereketwa mkubwa wa masuala ya kuhifadhi kasa katika kijiji chake. Abdallah pia anashirikiana na kikundi cha vijana cha Shimoni Turtle Watch kilichoko wadi ya Pongwe-Kikoneni, Shimoni, eneo bunge la Lunga Lunga katika Kaunti ya Kwale, ambacho kimefanya kazi hiyo ya uhifadhi wa kasa kwa miaka saba sasa. Hii ni kutokana na tishio la kupotea kwa kasa kutokana na uchafuzi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi, shughuli za uvuvi na ujenzi kwenye fuo za bahari. Wavuvi wanaochinja kasa waliokufa Zaidi, Abdallah na kikundi hicho walisema wamechukua hatua hiyo ya kumlinda kasa kutokana na tishio kwamba kuna wavuvi wengine ambao wanapokutana na kasa amekufa humchinja na kugawia watu nyama yake, hatua ambayo inahatarisha afya ya jamii. Farid Abdallah Mvuvi akionyesha aina ya karatasi za plastiki zipatikanazo baharini ambazo kasa hupenda kula na ni hatari kwao. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kasa ni aina ya kobe wakubwa wanaoishi baharini. Mnyama huyo hutaga mayai yake ardhini hasa katika ufukwe wa bahari, na kuyafukia humo kwa kati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 14:00:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20164352/Screenshot-2026-03-20-194312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1189</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Mamalia wa Baharini, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uongozi wa Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile wanachoeleza kuwa ni kupungua kwa kiasi kikubwa kwa idadi ya kasa, hasa katika pwani ya kaskazini-mashariki ya Unguja, ambako hapo awali kulishuhudiwa kasa wengi. Casper Morch, ambaye ni mwanaikolojia na msimamizi wa miradi wa Taasisi ya Under the Wave iliyopo Zanzibar, anasema kuna utafiti mdogo sana wa kisayansi kuhusu kasa wa baharini Zanzibar, lakini idadi ya kasa imepungua mara dufu katika miaka ya hivi karibuni. Morch anasema: “Tunajua kumekuwa na upungufu mkubwa wa kuonekana kwa kasa. Zamani wapiga mbizi walikuwa wanaona kasa 30 hadi 40 kwa wiki, lakini sasa wanajiona wenye bahati wakiona hata mmoja tu.” Mmoja wa kasa zaidi ya 350 wa Zanzibar waliohifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe ili kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu. Picha kwa hisani ya Under the Wave. Taasisi ya Under the Wave, ikishirikiana na mamlaka za Zanzibar, ilianza uhifadhi wa kasa mwaka 2020, mwaka ambao walibaini kuwa idadi ya kasa ilikuwa ikipungua kwa kasi. “Tulianzisha mara moja viota (aquaria) ambavyo hadi sasa vina kasa takribani 350. Lakini hawawezi kuzaliana kama walivyokuwa wakiishi kwenye makazi yao ya asilia. Hili ni jambo tunalolitambua na tutahakikisha wanarejea na kuwa salama,” anasema Morch. Taasisi hiyo inasema kasa wanahitaji kurudi walipotoka, lakini hilo litakuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>