<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=botania&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/botania/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 28 Aug 2026 16:47:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Aloyce Mwakisoma, mhifadhi wa maarifa ya misitu katika Milima ya Udzungwa, afariki na miaka 45</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/aloyce-mwakisoma-mhifadhi-wa-maarifa-ya-misitu-katika-milima-ya-udzungwa-tanzania-afariki-na-miaka-45/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/aloyce-mwakisoma-mhifadhi-wa-maarifa-ya-misitu-katika-milima-ya-udzungwa-tanzania-afariki-na-miaka-45/#respond</comments>
					<pubDate>15 Oktoba 2025 14:37:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Rhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/11150049/Screenshot-2025-11-11-175813-768x476.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=763</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Botania, Mazingira, na  Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>15 Oct 2025 Habari Fupi za Waanzilishi Alizaliwa katika misitu ambayo baadaye ingekuwa sehemu muhimu ya maisha yake. Katika Bonde la Kilombero, nchini Tanzania, ambako ukungu hushuka kutoka Milima ya Udzungwa, kijana Aloyce Mwakisoma alijifunza majina ya mimea kabla hata ya kujua majina ya kisayansi ya mimea hiyo kwa lugha ya Kilatini. Baba yake, ambaye [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/aloyce-mwakisoma-mhifadhi-wa-maarifa-ya-misitu-katika-milima-ya-udzungwa-tanzania-afariki-na-miaka-45/" data-wpel-link="internal">Aloyce Mwakisoma, mhifadhi wa maarifa ya misitu katika Milima ya Udzungwa, afariki na miaka 45</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[15 Oct 2025 Habari Fupi za Waanzilishi Alizaliwa katika misitu ambayo baadaye ingekuwa sehemu muhimu ya maisha yake. Katika Bonde la Kilombero, nchini Tanzania, ambako ukungu hushuka kutoka Milima ya Udzungwa, kijana Aloyce Mwakisoma alijifunza majina ya mimea kabla hata ya kujua majina ya kisayansi ya mimea hiyo kwa lugha ya Kilatini. Baba yake, ambaye hapo awali alikuwa mwindaji, aligeuka kuwa msaidizi wa watafiti baada ya uwindaji kupigwa marufuku katika miaka ya 1990, akiwaongoza wanasayansi kupitia msitu wenye kijani kibichi kama maficho. Aloyce alimfuata, akijifunza lugha ya sayansi pamoja na hekima ya kale ya wazee wa Kihehe, ambao kwao kila mmea ulikuwa na jina, matumizi, na hadithi yake. Akiwa mvulana, alikuwa akifuatana na baba yake na wanasayansi waliokuwa wakitembelea eneo hilo msituni, akisikiliza majadiliano yao kuhusu spishi na vipimo, huku yeye akikumbuka majina ya kienyeji na magonjwa ambayo kila jani au mzizi ungeweza kutibu. Baadaye, yeye mwenyewe alikuja kuwa mtafiti msaidizi. Wakati fulaini, alipokuwa akifuatilia tumbili wekundu wa Udzungwa kwa ajili ya utafiti, chui aliruka kutoka kwenye vichaka na kumkamata tumbili jike akiwa umbali wa mita chache tu kutoka alipokuwa amepumzika, tukio hilo lilimkumbusha hali halisi ya pori na maajabu yasiyotabirika ya msitu alioufahamu vizuri. Aloyce Mwakisoma. Picha na Andrea Bianchi. Kadri miaka ilivyopita, ndivyo alivyoendelea kujiimarisha hadi akawa mmoja wa wataalamu wa mimea na utafiti wanaoheshimika zaidi katika Milima ya Tao la Mashariki, safu ya milima yenye wingi wa viumbe hai iliyoenea kote Tanzania. Uelewa wake wa kina, uliosheheni maarifa ya kiasili kuhusu maisha ya msituni, ulimfanya awe mtu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/aloyce-mwakisoma-mhifadhi-wa-maarifa-ya-misitu-katika-milima-ya-udzungwa-tanzania-afariki-na-miaka-45/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/15/aloyce-mwakisoma-mhifadhi-wa-maarifa-ya-misitu-katika-milima-ya-udzungwa-tanzania-afariki-na-miaka-45/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ili kukusanya mbegu za asili bora, wataalamu wa mimea Uganda hukwea miti mirefu ya msituni</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/05/28/ili-kukusanya-mbegu-za-asili-bora-wataalamu-wa-mimea-uganda-hukwea-miti-mirefu-ya-msituni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/05/28/ili-kukusanya-mbegu-za-asili-bora-wataalamu-wa-mimea-uganda-hukwea-miti-mirefu-ya-msituni/#respond</comments>
					<pubDate>28 Mei 2025 13:25:12 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Kamnitzer]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/21131106/Screenshot-2025-08-21-154153-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=120</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Botania, Mazingira, Misitu, Miti, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Uokoaji wa Misitu, Urejeshaji, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Usimamizi wa Misitu wa Jamii]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mvule (Milicia excelsa) ni mti mkubwa sana, unaoweza kufikia urefu wa hadi mita 50 (futi 165), ukiwa na shina lenye mzunguko wa hadi mita 6 (futi 20). Ili kukusanya mbegu kutoka mti mkubwa wa aina hii, wapandaji hufanya kazi kwa timu ya watu watatu, anaeleza Sebastian Walaita, ambaye ni msimamizi wa Bustani ya Mimea ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/28/ili-kukusanya-mbegu-za-asili-bora-wataalamu-wa-mimea-uganda-hukwea-miti-mirefu-ya-msituni/" data-wpel-link="internal">Ili kukusanya mbegu za asili bora, wataalamu wa mimea Uganda hukwea miti mirefu ya msituni</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mvule (Milicia excelsa) ni mti mkubwa sana, unaoweza kufikia urefu wa hadi mita 50 (futi 165), ukiwa na shina lenye mzunguko wa hadi mita 6 (futi 20). Ili kukusanya mbegu kutoka mti mkubwa wa aina hii, wapandaji hufanya kazi kwa timu ya watu watatu, anaeleza Sebastian Walaita, ambaye ni msimamizi wa Bustani ya Mimea ya Tooro nchini Uganda. Wakiwa wamejipanga kwa usawa kuzunguka shina la mti, hupanda kwa pamoja wakitumia mfumo wa kamba, mikanda ya usalama na misumari ya kupandia. Wanapofika kwenye taji la mti, hupeana ishara na kutawanyika kwenye matawi huku wakikusanya mbegu zilizoiva na kuziweka kwenye mifuko yao kabla ya kushuka chini. Walaita alijifunza kwa mara ya kwanza kupanda miti mirefu kwa ajili ya ukusanyaji wa mbegu zaidi ya miaka 25 iliyopita, kupitia kozi iliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Denmark, DANIDA Forest Seed Centre, na tangu wakati huo ameendelea kuboresha ujuzi wake. Kwa miaka mingi, ametoa mafunzo kwa kada ya wataalamu wa mimea kutoka Tooro nchini humo, ambao sasa wanaweza kukusanya mbegu kwa usalama kutoka hata miti migumu zaidi ili  kuboresha uwezo wao wa kueneza spishi asilia, anasema. “Ni mapenzi ya dhati,” anaeleza Walaita. Kukusanya mbegu za miti ya asili kwa ajili ya urejeshaji wa misitu Kupitia Mpango wa Afrika wa Urejeshaji wa Mandhari ya Misitu (AFR100), serikali kote barani zimeahidi kurejesha hekta milioni 100 (sawa na ekari milioni 247) za ardhi ifikapo mwaka 2030. Kuna uelewa unaokua miongoni mwa wahifadhi kuwa ni bora kupanda tena maeneo yaliyoharibiwa kwa kutumia spishi za asili ili kuhifadhi bioanuwai. Aidha,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/28/ili-kukusanya-mbegu-za-asili-bora-wataalamu-wa-mimea-uganda-hukwea-miti-mirefu-ya-msituni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/05/28/ili-kukusanya-mbegu-za-asili-bora-wataalamu-wa-mimea-uganda-hukwea-miti-mirefu-ya-msituni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>`Mlima wa jongoo’ wa Tanzania watoa spishi sita mpya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/03/26/mlima-wa-jongoo-wa-tanzania-watoa-spishi-sita-mpya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/03/26/mlima-wa-jongoo-wa-tanzania-watoa-spishi-sita-mpya/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mechi 2024 11:48:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ryan Truscott]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/19114720/AlainSenghorKNguteProcessingMillipedeSpecimen_HamiduMnendendo-MEDIUM-2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=417</guid>

					
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Botania, Mazingira, Mimea, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Miti, Spishi Mpya, Ugunduzi Mpya, Ugunduzi wa Spishi, Uharibifu wa Makazi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utafiti, Wadudu, Wanyama, Wanyama wasio na Mifupa ya Mgongo, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wanasayansi hivi karibuni walibainisha spishi sita mpya za jongoo, ikiwemo moja kutoka kwenye jenasi mpya kabisa, katika Safu ya Milima ya Mashariki ya Tanzania. Ugunduzi huu umefanya idadi ya spishi mpya zilizopatikana katika Milima ya Udzungwa tangu mwaka 2014 kufikia 81 — jambo linalothibitisha kwa mara nyingine utajiri mkubwa wa bioanuwai katika safu hizi za [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/03/26/mlima-wa-jongoo-wa-tanzania-watoa-spishi-sita-mpya/" data-wpel-link="internal">`Mlima wa jongoo’ wa Tanzania watoa spishi sita mpya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wanasayansi hivi karibuni walibainisha spishi sita mpya za jongoo, ikiwemo moja kutoka kwenye jenasi mpya kabisa, katika Safu ya Milima ya Mashariki ya Tanzania. Ugunduzi huu umefanya idadi ya spishi mpya zilizopatikana katika Milima ya Udzungwa tangu mwaka 2014 kufikia 81 — jambo linalothibitisha kwa mara nyingine utajiri mkubwa wa bioanuwai katika safu hizi za milima zilizojitenga na maeneo mengine. Jongoo hao waliogunduliwa hivi karibuni wanawasaidia watafiti kutathmini urejeshwaji wa mfumo wa ikolojia. Jongoo mmoja kati ya waliogunduliwa hivi karibuni, ambaye kwa kitaalam anajulikana kama, Udzungwastreptus marianae, hukua hadi kufikia urefu wa takriban sentimita 3, na hupatikana katika misitu iliyoko juu ya mita 1,000 kutoka usawa wa bahari. Profesa wa mfumo wa kisayansi wa wanyama na jiografia ya wanyama katika Makumbusho ya Historia Asilia ya Denmark, Henrik Enghoff, ambaye ameelezea spishi 69 kati ya 81 zilizogunduliwa katika milima hiyo, anasema jenasi hiyo imepewa jina Udzungwastreptus kama njia ya kutambua utajiri wa ajabu wa viumbehai katika Milima ya Udzungwa. Milima ya Udzungwa ni sehemu ya Safu ya Milima ya Mashariki ya Tanzania, ambayo ni kisiwa chenye safu ya milima yenye vilele vilivyofunikwa na misitu, vinavyoyeosha umbali wa kilomita 900 (maili 560) kuanzia mashariki hadi kusini mwa Tanzania. Picha na Marc Veraart kupitia Flickr (CC BY 2.0) Udzungwastreptus marianae, ambao ni aina mpya ya jongoo iliyogunduliwa hivi karibuni katika Milima ya Udzungwa, Tanzania, na jongoo wengine hutambaa juu ya sakafu ya msitu kama vichwa vidogo vya treni, huku wakila mabaki ya mimea iliyokufa na takataka za kikaboni. “Baadhi ya jongoo walikuwa na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/03/26/mlima-wa-jongoo-wa-tanzania-watoa-spishi-sita-mpya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/03/26/mlima-wa-jongoo-wa-tanzania-watoa-spishi-sita-mpya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>