<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?location=botswana&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/botswana/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Mon, 31 Aug 2026 14:23:41 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/#respond</comments>
					<pubDate>18 Agosti 2026 06:16:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mary Rice]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/18060350/Screenshot-2026-08-18-090213-768x492.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2511</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika ya Kati, Angola, Asia, Botswana, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Msumbiji, Namibia, Nigeria, Tanzania, Vietnam, na  Zambia]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Haramu, Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyama Wanyama, Cites, Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Spishi, Tembo, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhalifu uliopangwa, na  Usafirishaji wa Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Kuhusu pembe za ndovu, fuatilia mitandao ya usafirishaji haramu, si vichwa vya habari tu (maoni)</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mwanzoni mwa Machi 2026, mamlaka za Zambia zilikamata mzigo wa zaidi ya kilo 500 (zaidi ya paundi 1,100) za pembe za ndovu — hatua iliyofuata taarifa za kijasusi zilizotolewa na shirika langu, Environmental Investigation Agency (EIA) la Uingereza. Pamoja na mzigo huo, mshukiwa mwenye historia ndefu ya usafirishaji haramu wa pembe za ndovu katika eneo hilo alikamatwa pia. Mshukiwa huyo alikuwa amehukumiwa mwaka 2019 kwa kumiliki zaidi ya kilo 200 (karibu paundi 441) za pembe za ndovu, na mwaka 2020 alipewa kifungo cha miaka mitano gerezani. Hata hivyo, aliachiwa huru baada ya miezi michache tu, na tangu wakati huo amekuwa akiendelea na biashara hiyo haramu. Zambia imekuwa ikitumiwa vibaya na mitandao ya wahalifu tangu angalau mwaka 2002, na sasa iko tena chini ya mwanga wa uchunguzi. Kinachosumbua hasa ni ushiriki wa makundi ya wahalifu kutoka Kongo, ambayo yanafanya kazi kwa uhuru mkubwa ndani ya Zambia na nchi jirani. Makundi hayo yanakusanya na kusafirisha bidhaa za wanyamapori — pembe za ndovu za tembo, pembe za kifaru, magamba ya pangolin na paka wakubwa — kupitia njia ngumu za kimataifa kuelekea Asia, huku Vietnam mara nyingi ikitumika kama kituo muhimu cha kupitishia. Mitandao hii inajinufaisha na ukosefu wa nia ya kisiasa, utekelezaji dhaifu wa sheria, maafisa wafisadi na jamii zilizotengwa. Inaandaa misafara ya ujangili katika nchi jirani na kutumia wasuluhishi wa Zambia kupanua minyororo yake ya biashara haramu. Ukamataji wa Zambia — ukijumlishwa na matukio mawili ya ukamataji mkubwa uliofanywa Tanzania na Botswana mnamo Aprili na Mei mtawalia — unaleta jumla ya pembe za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/18/kuhusu-pembe-za-ndovu-fuatilia-mitandao-ya-usafirishaji-haramu-si-vichwa-vya-habari-tu-maoni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri ujangili unavyoendelea, Tanzania inaongeza silaha mpya: mbwa wa kunusa nyara za wanyamapori</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/#respond</comments>
					<pubDate>17 Mechi 2026 21:53:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/17230956/Screenshot-2026-03-18-020613-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1111</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Mashariki, Botswana, Kenya, Msumbiji, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Misitu, Sera za Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR-ES-SALAAM, Tanzania &#8211; Licha ya utajiri wake, ikiwa ni pamoja na uwekezaji wa mamilioni katika uhifadhi, Tanzania inakabiliwa na ongezeko la ujangili na biashara haramu za nyara, kama ilivyofichuliwa na Operesheni Thunder 2025 ya Interpol. Ili kukabiliana na janga hilo, imekuwa muhimu kutumia silaha zaidi, nchi hiyo sasa ikijumuisha ujuzi wa askari wa uhifadhi na mbwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/" data-wpel-link="internal">Kadri ujangili unavyoendelea, Tanzania inaongeza silaha mpya: mbwa wa kunusa nyara za wanyamapori</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR-ES-SALAAM, Tanzania &#8211; Licha ya utajiri wake, ikiwa ni pamoja na uwekezaji wa mamilioni katika uhifadhi, Tanzania inakabiliwa na ongezeko la ujangili na biashara haramu za nyara, kama ilivyofichuliwa na Operesheni Thunder 2025 ya Interpol. Ili kukabiliana na janga hilo, imekuwa muhimu kutumia silaha zaidi, nchi hiyo sasa ikijumuisha ujuzi wa askari wa uhifadhi na mbwa wenye mafunzo maalum ya kunusa nyara. Takwimu za sensa ya hivi karibuni zinaonesha kuwa Tanzania bado ina idadi kubwa zaidi ya nyati na simba barani Afrika. Mnamo Juni, 2024, Wizara ya Maliasili na Utalii nchini iliwasilisha taarifa katika bunge ikisema kuwa Tanzania ina simba takribani 17,000, nyati 225,000 na chui 20,000. Hata hivyo, Operesheni Thunder 2025, iliyofanywa kuanzia Septemba 15 hadi Oktoba 15, ilihusisha vyombo vya kutekeleza sheria pamoja na mamlaka za wanyamapori na misitu katika biashara haramu, ambapo maofisa wa nchi jirani ya Kenya walikamata zaidi ya kilo 400 za nyama za twiga, na wa Tanzania kupata nyama na ngozi za pundamilia na swala, zenye thamani ya takriban $10,000. Mwanzoni mwa Februari 2026, Mongabay ilizuru Shirika la Kuru Conservation Dogs, maarufu shule ya mbwa, iliyopo nchini Tanzania, na kuona jinsi huduma mbalimbali, zikiwemo chakula na matibabu, zilipita kwenye kila chumba cha mbwa. Wahudumu waliwaita kwa majina, nao wakatulia mara moja, na kuacha kubweka, tayari kupokea huduma zao. Mongabay ilishuhudia makumi ya vyumba ambavyo watoa huduma walipita kufanya usafi na kuwapa mbwa huduma hizo. Afisa wa Kikosi cha mbwa nusa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini Tanzania [TAWA] akiwa moja ya mbwa waliopewa mafunzo na Shirika la Kuru&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>