<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=nyasi&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/nyasi/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Fri, 28 Aug 2026 16:47:28 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mradi unaoongozwa na wafugaji wa Kitanzania washinda tuzo ya kimataifa kwa kuimarisha uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>16 Desemba 2025 17:39:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/12/23182123/Screenshot-2025-12-23-204447-768x467.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=850</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Akili Mnemba, Ardhi iliyoharibika, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Mageuzi ya Ardhi, Malisho ya Ng'ombe, Mazingira, Mifugo, Mimea, Nyasi, Suluhisho za Asili, Teknolojia, Teknolojia ya Uhifadhi Mazingira ya Porini, Ufugaji, Ufugaji wa Ng'ombe, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, na  Vikundi vya Jamii za Asili]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wafugaji kutoka maeneo ya vijijini nchini Tanzania wametambuliwa kimataifa kwa kufanikiwa kuweka pamoja maarifa ya asili na teknolojia mpya katika juhudi za kurejesha ardhi iliyoharibika na kuhakikisha upatikanaji wa malisho. Mradi huo unaoongozwa na jamii, ujulikanao kama Sustainable Rangelands Initiative (SRI), ulibuniwa na shirika la African People &#38; Wildlife (APW). Hivi karibuni, ulishinda tuzo katika [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mradi unaoongozwa na wafugaji wa Kitanzania washinda tuzo ya kimataifa kwa kuimarisha uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wafugaji kutoka maeneo ya vijijini nchini Tanzania wametambuliwa kimataifa kwa kufanikiwa kuweka pamoja maarifa ya asili na teknolojia mpya katika juhudi za kurejesha ardhi iliyoharibika na kuhakikisha upatikanaji wa malisho. Mradi huo unaoongozwa na jamii, ujulikanao kama Sustainable Rangelands Initiative (SRI), ulibuniwa na shirika la African People &amp; Wildlife (APW). Hivi karibuni, ulishinda tuzo katika kipengele cha NatureTech Stewards kwenye uzinduzi wa tuzo za IUCN Tech4Nature, wakati wa Mkutano wa Dunia wa Uhifadhi wa Mazingira wa IUCN, uliofanyika Abu Dhabi Oktoba mwaka huu wa 2025. Mpango wa Sustainable Rangelands Initiative (SRI) unatekelezwa Kaskazini na Kati mwa Tanzania katika wilaya za Simanjiro, Babati, Longido, Same, Monduli, Ngorogoro, na Mwanga. Mkurugenzi wa Uhifadhi wa Jamii na Mazingira wa APW, Neovitus Sianga, anasema maeneo haya yalichaguliwa kwa kuwa ni muhimu kwa shughuli za mifugo na wanyamapori. Kupitia mpango huu, unaotekelezwa na APW kwa kushirikiana na jamii za maeneo husika, kamati za malisho za vijiji pamoja na wafuatiliaji wa maeneo ya malisho waliopatiwa mafunzo, hutumia zana za kidijitali zikiwemo simu za mkononi kukusanya taarifa kuhusu vyanzo vya maji, uoto wa asili, kasi ya ukuaji wa nyasi, afya ya udongo pamoja na uwepo wa vimelea au spishi vamizi. Nasma Mustafa, mmoja wa wafuatiliaji wa malisho kutoka Kijiji cha Engaluka, anaeleza hatua kuu za zoezi hilo: “Tunatumia kipimo cha tepu ya kupimia, kamba na simu. Kamba hulazwa juu ya ardhi kwa urefu wa mita 100, sambamba na kipimo chenye alama tano. Kisha tunaangalia ni alama zipi kati ya hizo tano zinazogusa uoto wa asili na zipi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/12/16/mradi-wa-kibunifu-unaoongozwa-na-wafugaji-wa-kitanzania-washinda-tuzo-ya-kimataifa-kwa-kuimarisha-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>