<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?topic=kaboni-ya-udongo&#038;type=post" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/kaboni-ya-udongo/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 10 Sep 2026 09:32:13 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Kenya Kaskazini: Shirika la ufadhili linaloendeshwa na jamii lakumbwa na mgogoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/05/20/kenya-kaskazini-shirika-la-ufadhili-linaloendeshwa-na-jamii-lakumbwa-na-mgogoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/05/20/kenya-kaskazini-shirika-la-ufadhili-linaloendeshwa-na-jamii-lakumbwa-na-mgogoro/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2025 09:54:10 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/13095255/NRT25_3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=80</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Kaboni, Fedha za Kaboni, Kaboni, Kaboni ya Udongo, Mifugo, Mikopo ya Kaboni, Soko ya Kaboni, Ufadhili, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>GOTU, Kenya — Ni saa ya alasiri kwenye mji mdogo wa Gotu, kaskazini mwa Kenya. Kivulini mwa mti mmoja wa mkakaya (mwatiko, mgunga), kundi la wazee limekusanyika kujadili masuala ya kijamii. Mji huu mdogo uliopo umbali wa takribani kilomita 52 kutoka mji wa Isiolo una shughuli nyingi za ulishaji wa mifugo. Kila unapopita, utawaona vijana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/20/kenya-kaskazini-shirika-la-ufadhili-linaloendeshwa-na-jamii-lakumbwa-na-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Kenya Kaskazini: Shirika la ufadhili linaloendeshwa na jamii lakumbwa na mgogoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[GOTU, Kenya — Ni saa ya alasiri kwenye mji mdogo wa Gotu, kaskazini mwa Kenya. Kivulini mwa mti mmoja wa mkakaya (mwatiko, mgunga), kundi la wazee limekusanyika kujadili masuala ya kijamii. Mji huu mdogo uliopo umbali wa takribani kilomita 52 kutoka mji wa Isiolo una shughuli nyingi za ulishaji wa mifugo. Kila unapopita, utawaona vijana wakichunga makundi ya ngamia kando ya barabara, huku mbuzi wakila majani mabichi na mimea karibu na makao yaliyojengwa kwa matofali, au udongo, na yenye paa za mabati. Mto uliokuwa karibu sana unaelekea kukauka kufuatia kiangazi. Umebakia mkondo mwembamba tu, huku jamii zikitarajia mvua kila kunapokucha. Rashid Susa, mwenye umri wa miaka 70, ni mmoja wa wafugaji hawa wanaojadili masuala ya mifugo. Rashid, aliye na ndevu zilizopakwa rangi nyekundu, anaunga mkono shirika moja lisilo la kiserikali, maarufu kama Northern Rangelands Trust (NRT), ambalo linajihusisha na uhifadhi. Mzee huyu anasema kwa miaka 14 sasa, shirika hili la NRT limesaidia jamii nyingi katika eneo la Gomu. Anaorodhesha faida kama vile mishahara kwa walinzi wa wanyamapori wanaotoka kwenye jamii, ufadhili wa masomo kutokana na malipo ya mikopo ya kaboni, pamoja na usaidizi kuhakikisha kuwa mifugo iliyoibwa baada ya uvamizi wa jamii jirani, imefuatwa na kurudishwa kwa wamiliki. Wazee wengine wote wanatikisa vichwa vyao, ishara kuwa wanakubaliana na Susa. Mji huo mdogo ni sehemu ya hifadhi ya Nakuprat-Gotu, ambayo ni mojawapo ya hifadhi 45, ambazo pia ni wanachama wa NRT nchini Kenya na Uganda. Mchungaji akiwa na mbuzi wake mjini Gotu. Picha na Ashoka Mukpo wa Mongabay. Angalau katika kundi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/05/20/kenya-kaskazini-shirika-la-ufadhili-linaloendeshwa-na-jamii-lakumbwa-na-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/05/20/kenya-kaskazini-shirika-la-ufadhili-linaloendeshwa-na-jamii-lakumbwa-na-mgogoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>