<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?s=&#038;type=post&#038;topic=uvuvi-wa-kupita-kiasi" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/uvuvi-wa-kupita-kiasi/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 05 Sep 2026 00:00:40 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Vifaa vya uvuvi vilivyokatazwa vyateketezwa kupambana na uvuvi haramu Ziwa Tanganyika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/08/09/vifaa-vya-uvuvi-vilivyokatazwa-vyateketezwa-kupambana-na-uvuvi-haramu-ziwa-tanganyika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/08/09/vifaa-vya-uvuvi-vilivyokatazwa-vyateketezwa-kupambana-na-uvuvi-haramu-ziwa-tanganyika/#respond</comments>
					<pubDate>09 Agosti 2026 09:50:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Thérence Hategekimana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/08/09095305/Screenshot-2026-08-09-125222.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2405</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Burundi]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Makampuni Yanayokiuka Sheria za Mazingira, Mashirika Yanayokiuka Kanuni za Mazingira, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Uhalifu wa Mazingira, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Burundi imeteketeza boti ndogo saba na nyavu 97 za uvuvi zilizopigwa marufuku katika operesheni ya kupambana na uvuvi haramu iliyofanyika katika bandari ya Bujumbura, kando ya Ziwa Tanganyika. Operesheni hiyo iliongozwa na Godelieve Nininahazwe, Mamlaka ya Bahari, Bandari na Reli nchini Burundi (AMPF), ikiwa na lengo la kuhakikisha utekelezaji wa kanuni zilizopo na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/09/vifaa-vya-uvuvi-vilivyokatazwa-vyateketezwa-kupambana-na-uvuvi-haramu-ziwa-tanganyika/" data-wpel-link="internal">Vifaa vya uvuvi vilivyokatazwa vyateketezwa kupambana na uvuvi haramu Ziwa Tanganyika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Burundi imeteketeza boti ndogo saba na nyavu 97 za uvuvi zilizopigwa marufuku katika operesheni ya kupambana na uvuvi haramu iliyofanyika katika bandari ya Bujumbura, kando ya Ziwa Tanganyika. Operesheni hiyo iliongozwa na Godelieve Nininahazwe, Mamlaka ya Bahari, Bandari na Reli nchini Burundi (AMPF), ikiwa na lengo la kuhakikisha utekelezaji wa kanuni zilizopo na kulinda rasilimali za uvuvi za ziwa ambazo zinatishiwa na matumizi ya vifaa visivyoruhusiwa. Vifaa vinavyotumiwa kwenye uvuvi haramu vilivyokamatwa vikiteketea kwa moto.Picha kwa hisani ya AMPF. Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa AMPF, Godelieve Nininahazwe, vifaa hivyo vilikamatwa wakati wa ukaguzi wa kila siku unaofanywa na idara za usalama kwenye maji kwa ushirikiano na vyombo vya ulinzi na usalama. Akizungumza wakati wa tukio hilo, Nininahazwe alisema kuwa zana za uvuvi zilizopigwa marufuku si salama kwa ustawi wa samaki. &#8220;Zana hizi zinakamata bila ubaguzi. Samaki wakubwa na wadogo, wote hunaswa, jambo ambalo linahatarisha uzalishaji upya wa mazalia ya samaki na kuvuruga uwiano wa mfumo wa ikolojia wa ziwa,&#8221; alisema Nininahazwe. Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa la Chakula na Kilimo (FAO), rasilimali za uvuvi katika Ziwa Tanganyika zinatumika kupita kiasi kutokana na idadi kubwa ya wavuvi; matumizi ya zana haramu za uvuvi zinazokamata kwa wingi samaki ambao bado hawajakomaa; uvuvi katika maeneo nyeti kama maeneo ya mazalia au maeneo ya hifadhi ya spishi zilizo hatarini, pamoja na ongezeko kubwa la idadi ya watu. &#8220;Uvuvi haramu pia unachangia kupungua kwa idadi ya samaki, kudhoofisha bayoanuwai ya majini na kuhatarisha maisha ya maelfu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/08/09/vifaa-vya-uvuvi-vilivyokatazwa-vyateketezwa-kupambana-na-uvuvi-haramu-ziwa-tanganyika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/08/09/vifaa-vya-uvuvi-vilivyokatazwa-vyateketezwa-kupambana-na-uvuvi-haramu-ziwa-tanganyika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/#respond</comments>
					<pubDate>21 Julai 2026 17:56:03 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Kelvin Matuku]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/21171918/Screenshot-2026-07-21-201312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2148</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Fedha ya mfumo wa ikolojia, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Uchafuzi, Uchafuzi wa Maji, Uchumi wa Mazingira, Ufugaji Samaki, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Kadri akiba ya samaki inavyozidi kupungua katika Ziwa Victoria, wavuvi wageukia vizimba kama tumaini jipya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati wa mapambazuko katika ufukwe wa Paga, Kaunti ya Kisumu, wavuvi wanaonekana wakivuta boti zao hadi ufuoni baada ya kukesha usiku mzima katika Ziwa Victoria. Lakini tofauti na miaka iliyopita, wengi wao walirejea na samaki wachache sana. Mvuvi Hesbone Otieno anasema kupungua kwa akiba ya samaki hakutishii tu riziki zao bali pia kunalazimisha jamii zinazotegemea ziwa hilo kutafakari upya mustakabali wa uvuvi katika ziwa hilo, ambalo ndilo kubwa zaidi barani Afrika. “Wakati mwingine nakaa ziwani usiku mzima na kurudi na kati ya samaki 300 na 359 pekee,” anasema Otieno, ambaye amevua katika Ziwa Victoria kwa miongo kadhaa. “Samaki ni wachache na kipato pia kinapungua. Kama mvuvi, naona njia ambayo imebakia ni kukumbatia vizimba vya samaki ili tuweze kuendelea kuishi.” Ufukwe wa Paga kwenye Ziwa Victoria. Picha na Kelvin Matuku, Mongabay. Ziwa Victoria ni chanzo cha kujikimu kwa jamii za wavuvi nchini Kenya, Uganda na Tanzania, kupitia uvuvi na biashara zinazohusiana nao. Hata hivyo, kwa mujibu wa utafiti uliochapishwa mwaka 2023, katika miaka ya hivi karibuni, Ziwa Victoria na eneo lake la vyanzo vya maji vimeathirika vibaya kutokana na “uvuvi kupita kiasi, umwagikaji wa mafuta, utiririshaji wa taka ambazo hazijatibiwa, kuenea kwa spishi vamizi, uchotaji wa maji kupita kiasi kutoka bonde la ziwa, na mabadiliko ya tabianchi, miongoni mwa sababu nyingine.” Kushuka kwa uzalishaji wa samaki Kwa mujibu wa Shirika la Huduma za Uvuvi Kenya (KeFS), uzalishaji wa samaki katika Ziwa Victoria umeshuka kutoka takriban tani za metriki 94,349 mwaka wa 2021 hadi 67,575 mwaka wa 2024. Huu ni upungufu wa zaidi ya tani 27,700 katika kipindi cha miaka mitatu. Upungufu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/21/kadri-akiba-ya-samaki-inavyopungua-katika-ziwa-victoria-wavuvi-wageukia-vizimba-kama-tumaini-jipya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/#respond</comments>
					<pubDate>15 Julai 2026 11:11:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/07/14191215/Namakongoro-4-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=2075</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Ikolojia, Irejeshaji wa Mfumo wa Ikolojia, Maziwa, Mifumo ya Ikolojia, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Ushirikishwaji wa jamii, wadau warejesha ikolojia ya bahari Namakongoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Miaka minne iliyopita, ikolojia ya bahari katika kijiji cha Namakongoro kilichopo katika Kata ya Limaliyao, Wilaya ya Kilwa, Mkoa wa Lindi, kwenye ukanda wa kusini wa Bahari ya Hindi, ikiwamo matumbawe, nyasi bahari na mikoko iliharibika vibaya kutokana na kukithiri kwa matukio ya uvuvi haramu hasa wa kutumia vilipuzi kama baruti. Hali hiyo ilisababisha uharibifu mkubwa wa makazi ya viumbe baharini, hivyo kupunguza idadi ya samaki, pweza na viumbe wengine wanaotegemea mazingira hayo kuishi na kuzaliana. Baadhi ya viumbe walihamia kwenye maeneo yenye kina kirefu, jambo lililovuruga mfumo wa ikolojia wa bahari na kupunguza bioanuwai. Hata hivyo, tangu mwaka 2021 hali ilianza kubadilika kufuatia juhudi za pamoja za jamii, Serikali, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU) na taasisi ya Sea Sense, inayojihusisha na uhifadhi wa mazingira ya bahari na ukanda wa pwani, kuanzisha mikakati ya uhifadhi wa bahari. Wavuvi wa Namakongoro wakipewa mafunzo ya uhifadhi bahari kupitia njia za uvuvi endelevu na Maofisa wa Halmashauri ya Namakongoro pamoja na Taasisi ya Seasense. Picha kwa hisani ya SeaSense. Juhudi hizo zimeleta mabadiliko makubwa ikiwa ni pamoja na kusaidia kurejesha matumbawe, kuongeza wingi wa samaki waliokuwa wamepungua pamoja na kupungua kwa kiwango kikubwa kwa uvuvi haramu. Kurejesha uhai wa bahari Mafanikio ya kurejesha uhai wa bahari Namakongoro yametokana na ushirikiano wa karibu kati ya wanakijiji, Kitengo cha Usimamizi Shirikishi wa Ufukwe (BMU), Sea Sense na Serikali. Baada ya kubaini kuwa chanzo kikuu cha uharibifu huo kilikuwa ni uvuvi haramu, taasisi ya Sea Sense iliingia katika kijiji cha Namakongoro. Mratibu wa Mradi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/07/15/ushirikishwaji-wa-jamii-wadau-warejesha-ikolojia-ya-bahari-namakongoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>30 Juni 2026 18:54:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/30183954/Screenshot-2026-06-30-213942-768x489.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1962</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Biashara Endelevu, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Fedha, Haki ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Halijoto, Hifadhi, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mikoko, Misitu ya Kitropiki, Ongezeko la Joto Baharini, Uhifadhi wa Baharini, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Wanawake wapiga doria katika bahari ya Pemba katika juhudi za jamii za kulinda rasilimali za baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[PEMBA, Tanzania — Kufanya doria baharini si aina ya kazi ambayo wanawake wengi katika Kisiwa cha Pemba nchini Tanzania wanatarajiwa kufanya. Hata hivyo, kwa Amina Gharib Issa, amekuwa akifanya kazi hiyo katika miaka ya hivi karibuni. Issa, mwenye umri wa miaka 55, ametumia muda mwingi baharini akiwa mvuvi. Lakini samaki walipoanza kupungua na jamii ilipoanza kutekeleza vipindi vya kufunga maeneo ya uvuvi kwa muda ili kuruhusu viumbe vya baharini kuzaliana tena na kurejesha idadi yake, alichukua jukumu la kusaidia doria katika maji ili kuhakikisha sheria zinafuatwa. Yeye ni mmoja wa watu saba katika timu ya doria ya jamii ambayo huenda kufanya doria baharini mara nane kwa mwezi, kuangalia boti, zana za uvuvi na leseni. Kazi hiyo inachukua muda mrefu majini, wakati mwingine katika hali mbaya, kwa malipo ya takriban $8 kwa siku. Katika sehemu kubwa ya Pemba, wanawake hushiriki sana katika uvuvi, lakini kupiga doria mbali na ufukwe na wanaume ni jambo jingine. Jamii hiyo ina idadi kubwa ya Waislamu, na majukumu ya kijinsia yanaweza kuchunguzwa kwa karibu. &#8220;Baadhi ya wanawake hawaruhusiwi na waume zao,&#8221; Ali Said Hamad, mjumbe wa timu ya Mwambao, alisema, akielezea mojawapo ya sababu zinazowafanya wanawake wengi wasijiunge. Hamad ametumia muda mwingi baharini, si kama afisa wa utekelezaji bali akisaidia kutekeleza programu za uhifadhi zinazoongozwa na jamii. Kwa wanawake wanaofanya doria baharini, usaidizi wa familia unaweza kuleta mabadiliko. Issa alisema mume wake aliuunga mkono uamuzi wake wa kushiriki. Kazi yake ni sehemu ya juhudi pana za uhifadhi zinazoongozwa na jamii zinazoungwa mkono na Kikundi cha Jamii za Pwani (Mwambao&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/30/wanawake-wapiga-doria-katika-bahari-ya-pemba-tanzania-katika-juhudi-zinazoongozwa-na-jamii-kulinda-rasilimali-za-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/#respond</comments>
					<pubDate>29 Juni 2026 14:08:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/29134931/Screenshot-2026-06-29-164657-768x499.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1948</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Eneo Lililolindwa Baharini, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jinsia na Uhifadhi, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Ongezeko la Joto Baharini, Sehemu za Bioanuwai, Suluhisho za Asili, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Baharini, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Ndani, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, Viwango vya Bahari, na  Wanawake katika Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Katika Mkondo wa Mida nchini Kenya, wavuvi sasa wanakabiliana na mabadiliko ya bahari kwa matumaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WATAMU, Kenya &#8211; Kufikia adhuhuri, samaki walikuwa bado hawajafika. Tangu saa mbili asubuhi, Alice Kazungu alikuwa ameketi kwenye bandari ya samaki katika eneo la Mkondo wa Mida kwenye pwani ya Bahari ya Hindi ya Kenya, akisubiri wavuvi warudi kutoka majini. Saa kadhaa baadaye, alikuwa bado anasubiri. Karibu naye, mwanamke mwingine anaangalia mkondo ili kuona dalili za mitumbwi inayokaribia. Baadhi ya wavuvi walikuwa tayari wamerudi mikono mitupu. Wengine walikuwa hawajarudi kabisa. Kwa Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo kipya cha Usimamizi wa Pwani wa Mida (BMU), kusubiri kwa muda mrefu kumekuwa sehemu ya maisha ya kila siku. Kitengo cha Usimamizi wa Pwani (BMU) ni mfumo wa usimamizi shirikishi wa uvuvi nchini Kenya, ukiwaleta pamoja wadau katika sekta hiyo wakiwemo wavuvi, wauza samaki na wafanyabiashara. Alice Kazungu, mfanyabiashara wa samaki na naibu mwenyekiti wa Kitengo cha Usimamizi wa Pwani ya Mida (BMU) kilichoanzishwa hivi karibuni huko Watamu, Kenya. Picha na David Akana/Mongabay. &#8220;Kuna wakati ambapo samaki walikuwa wengi hapa,&#8221; anasema, akionyesha mkondo wa bahari uliommzunguka. &#8220;Sasa [wavuvi] wanarudi na kilo mbili au tatu tu.&#8221; Kwa Kazungu, kupungua kwa samaki kumekuwa suala la kuishi. Akiwa ameolewa na mwenye watoto, anategemea karibu kabisa kuuza samaki ili kupata mapato. Wakati hakuna samaki, mara kwa mara anauza mnazi, aina ya mvinyo wa mitende kutoka kwa minazi. Lakini hiyo haitoshi kuchukua nafasi ya riziki iliyojengwa karibu na bahari. &#8220;Ninarejea nyumbani, watoto hutaka chakula,&#8221; anasema. &#8220;Hilo ndilo linalonitia wasiwasi.&#8221; Hadithi yake inaakisi hali ilivyo katika Mkondo wa Mida, mtandao mkubwa wa mikoko, matope na mifereji ya maji ambayo ni sehemu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/29/katika-mkondo-wa-mida-nchini-kenya-wavuvi-wanakabiliana-na-mabadiliko-ya-bahari-kwa-matumaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/#respond</comments>
					<pubDate>25 Juni 2026 23:31:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/25230559/Our-Ocean-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1930</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Magharibi, Afrika Mashariki, Afrika ya Ikweta, Afrika ya Kati, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai wa Baharini, Dawa ya Asili, Elimu, Elimu ya Mazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Kasa wa baharini, Maji, Maliasili, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Mikoko, Misitu ya Asili, Ongezeko la Joto Baharini, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhisho za Asili, Tamaduni za Kiasili, Uchafuzi wa Maji, Uhifadhi wa Baharini, Urejesho wa Asili, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Elimu asili yapewa nafasi muhimu katika juhudi za kimataifa za kulinda bahari</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jimmy Muranga kutoka Sokoke, kaunti ya Kilifi, Pwani ya Kenya, anakumbuka vizuri enzi za utoto wake, alipokuwa akikaa na babu yake na kuelezwa hadithi na kupewa mafunzo kuhusu utunzaji wa mazingira. Wazee walimueleza jinsi maeneo mbalimbali ya bahari, mikoko na misitu ya pwani ilivyo na umuhimu mkubwa kwa maisha ya binadamu. Kupitia simulizi hizo, Muranga alijifunza kuwa mazingira si rasilimali za kutumia tu, bali ni urithi wa kulindwa kwa ajili ya vizazi vijavyo. Nchini Kenya, ukanda wa pwani wenye urefu wa takriban kilomita 640 ni kitovu cha uchumi wa buluu unaojumuisha uvuvi, utalii, usafiri wa baharini na biashara nyingine zinazotegemea bahari. Karibu watu milioni nne wanaishi katika eneo la pwani, huku maelfu ya wavuvi na makumi ya maelfu ya kaya wakitegemea rasilimali za bahari kwa riziki zao. Hali hiyo inaifanya uhifadhi wa bahari kuwa muhimu si tu kwa mazingira bali pia kwa ustawi wa uchumi wa taifa. Muranga, ambaye sasa ni mvuvi na pia mwenyekiti wa kikundi cha kijamii cha kulinda misitu cha Sokoke, ana jukumu la kuhakikisha kuwa anapitisha elimu hiyo kwa jamii, hasa kwa vizazi vichanga, ili ihifadhiwe kwa vizazi vijavyo. Mwonekano wa sehemu ya Bahari ya Hindi jijini Mombasa, huku mikoko ikionekana upande wa kushoto. Picha na Malavika Vyawahare, Mongabay. Mikoko ni misitu ya kipekee inayostawi katika maeneo ya maji ya chumvi kwenye fukwe za bahari za kanda za kitropiki. Misitu hii huunganisha nchi kavu na bahari, ikifanya kazi muhimu katika kulinda mazingira na ustawi wa jamii za pwani. “Zamani tulikuwa tukikalishwa na mababu zetu tukisimuliwa hadithi na kanuni za kijamii ambazo zilikuwa zinalinda&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/25/elimu-asili-yapewa-nafasi-muhimu-katika-juhudi-za-kimataifa-za-kulinda-bahari/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 16:47:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/06171705/Screenshot-2026-04-06-201423-768x503.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1312</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Sheria ya Mazingira, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana zaidi, ambao kulingana na wahifadhi wa mazingira, unaoonyesha jinsi hatma ya papa na samaki jamii ya pweza walio hatarini, ilivyofungamana kwa karibu na maisha ya wavuvi wanaojitafutia kipato katika Bahari ya Hindi ya Magharibi. Mnamo Februari, ili kuweka mpango kazi unaotekelezeka wa uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza nchini Kenya, kundi la watunga sera, wanasayansi na viongozi wa jamii walichapisha mkakati wenye malengo 19. Kati ya hayo, zaidi ya malengo 12 yanawahusisha moja kwa moja wavuvi wadogo au yanakusudia kuwashirikisha ili kuhakikisha mafanikio yake. Malengo hayo yanajumuisha kuanzisha maeneo zaidi ya bahari yanayosimamiwa na jamii, kuwashirikisha wavuvi katika maamuzi ya uhifadhi, na kuimarisha utekelezaji wa sheria kuhusu zana za uvuvi na uvuvi wa spishi zilizo hatarini. Tangu mwaka 2023, Kenya tayari ina sera ya uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza — Mpango wa Kitaifa wa Hatua za Uhifadhi na Usimamizi wa Papa (NPOA-Sharks). Hata hivyo, mpango huo bado unasubiri kuidhinishwa rasmi na serikali. Mkakati uliopendekezwa na wadau unatoa njia ya jinsi ya kuutekeleza. Papa aina ya scalloped hammerhead (Sphyrna lewini), aliyepigwa picha Yonaguni, Japan. Kulingana na utafiti, spishi hii huvuliwa mara kwa mara na wavuvi wadogo nchini Kenya. Picha na Masayuki Agawa kupitia Ocean Image Bank.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>04 Januari 2026 19:23:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/04190953/kuruwitu1-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=871</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara, Biashara Endelevu, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Hifadhi za Jamii za Asili, Jamii Asili, Mazingira, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Takwimu, Ufugaji, Ufugaji Samaki, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Uhifadhi wa mazingira ya bahari kupitia tengefu unaleta matumaini kwa wavuvi katika pwani ya Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kwa zaidi ya miongo miwili sasa, eneo la Kuruwitu limejulikana sana kwa uhifadhi wa mazingira ya Bahari kiasi kwamba kizazi kipya cha rika la vijana (hususan Gen Z), wanalitambua. Hii ilidhihirika wazi pale nilipotua kituo cha basi cha Shariani, barabara kuu ya kutoka Mombasa kuelekea Malindi, na kuulizia mwelekeo kufika baharini. &#8220;Unaenda Kuruwitu ile ya uhifadhi wa mazingira ya baharini?&#8221; aliniuliza kijana wa rika, mwendesha pikipiki. Na baada ya dakika kama saba, nilikuwa nimefika eneo hilo. Mkurugenzi mkuu wa shirika la Kuruwitu Conservation Welfare and Association Daniel Mwangunya alikuwa ameshawasili tayari kuhojiwa kuhusu shughuli zao za uhifadhi wa mazingira ya bahari katika bandari ya Kinuni. Lakini kwanza aliomba tumsubiri mkuu wa kitengo cha uhifadhi wa matumbawe, ambaye kwa wakati huo alikuwa amepeleka wageni kuzama na kutalii mandhari ndani ya bahari. Tengefu ni eneo la bahari lililotengwa na kusimamiwa na wanajamii kwa ajili ya uhifadhi wa viumbe na mazingira ya baharini. Eneo lililohifadhiwa na jamii ya Kuruwitu kwa ajili ya kuongeza samaki na kuhifadhi matumbawe. Picha na Ruth Keah. Katika mantiki ya tengefu, hili ni eneo ambalo uvuvi wa samaki hauruhusiwi. Eneo hili linalindwa na wanajamii, hivyo kusababisha samaki kuwa na mazingira mwafaka ya kuzaana na kuongezeka. Wanapokuwa wengi, wanamiminika hadi sehemu ambazo wavuvi wanaruhusiwa kuvua, hivyo basi kuongeza kipato. Utulivu ulionikaribisha hapo ni ishara kwamba hakuna shughuli za uvuvi zinazoendelea, bali ni pilkapilka za kupokea wageni, kutayarisha vifaa kama vile mashua na zana za kuzamia kwenye bahari. Katana Ngala ni mzaliwa wa kijiji cha Kuruwitu, na ni miongoni mwa waanzilishi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/01/04/uhifadhi-wa-mazingira-ya-bahari-kupitia-tengefu-unaleta-matumaini-kwa-wavuvi-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/#respond</comments>
					<pubDate>30 Desemba 2025 14:08:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mongabay.com]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/01/13140426/Screenshot-2026-01-13-165604-768x482.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=922</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Maji, Mazingira, Maziwa, Mito, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, Uvuvi Haramu, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mageuzi ya kisasa katika uvuvi yawaacha wavuvi wadogo wa Tanzania wakihangaika kukabiliana na maisha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KILWA, Tanzania &#8211; Baadhi ya wavuvi katika wilaya ya Kilwa nchini Tanzania, ambao ni miongoni mwa watu wa kwanza kupokea boti za uvuvi kupitia mpango wa serikali, vyombo hivyo sasa vimegeuka kuwa mzigo na kuwatwisha gharama kubwa badala ya kuwa msaada. Mpango huo, uliozinduliwa Novemba mwaka 2023 na Wizara ya Mifugo na Uvuvi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ulilenga kuboresha sekta ya uvuvi kwa kubadilisha boti za mbao zilizopitwa na wakati kwa vyombo vya kisasa vya kuvulia. Rais Samia alipotembelea Kilwa miezi miwili kabla ya uzinduzi wa mpango huo, aliahidi kuwa wavuvi wadogo wangepewa boti hizo kupitia mikopo yenye riba nafuu. Ahadi hiyo iliibua matumaini makubwa miongoni mwa jamii za wavuvi ambazo kwa muda mrefu zimekuwa zikikabiliwa na changamoto za boti chakavu na ukosefu wa mtaji wa kununua vyombo vipya. Ili kufadhili mpango huo, serikali ilishirikiana na Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB), ambayo hutoa mikopo nafuu kwa vikundi vya wavuvi. Mikopo hiyo ina viwango vya riba vya chini, inatoa muda mrefu kwa marejesho, na inajumuisha kipindi cha msamaha wa malipo cha takribani miaka mitano hadi kumi kabla ya kuanza kulipa. “Tunatoa tangazo linalowafikia watu nchi nzima pindi boti zinapopatikana,” alisema Mohammed Sheikh, Mkurugenzi wa Uvuvi katika Wizara ya Mifugo na Uvuvi. “Vyama vya ushirika vinavyovutiwa vinatuma maombi, na vikikubaliwa, hupokea boti ambazo zinakuwa zimewekewa bima kamili na ziko tayari kwa matumizi.” Thamani ya kila boti hutegemea ukubwa wake (kwa kawaida boti yenye ukubwa wa kati ya mita 5 hadi 14, (futi 16 hadi 46), gharama yake ni takribani shilingi milioni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/12/30/mageuzi-ya-kisasa-katika-uvuvi-yawaacha-wavuvi-wadogo-wa-tanzania-wakihangaika-kukabiliana-na-maisha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanakijiji Kenya waonyesha namna ya kuvuna pweza wengi kwa kuvua kidogo</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/01/24/wanakijiji-kenya-waonyesha-namna-ya-kuvuna-pweza-wengi-kwa-kuvua-kidogo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/01/24/wanakijiji-kenya-waonyesha-namna-ya-kuvuna-pweza-wengi-kwa-kuvua-kidogo/#respond</comments>
					<pubDate>24 Januari 2024 16:02:00 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Diana Wanyonyi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/24160343/Screenshot-2025-09-24-190302-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=511</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Chakula, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uvuvi, Uvuvi wa Kupita Kiasi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MUNJE, Kenya — Kuanzia katikati ya mwaka 2023, eneo maarufu la kuvua samaki aina ya pweza lililoko karibu na pwani ya kijiji cha Munje lilionekana wazi na tulivu kwa namna ya kushangaza. Wanachama wa kikundi cha usimamizi wa fukwe cha kijiji hicho (BMU) walikuwa wakililinda kwa umakini ili kuhakikisha hakuna anayevua pweza katika sehemu hiyo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/01/24/wanakijiji-kenya-waonyesha-namna-ya-kuvuna-pweza-wengi-kwa-kuvua-kidogo/" data-wpel-link="internal">Wanakijiji Kenya waonyesha namna ya kuvuna pweza wengi kwa kuvua kidogo</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MUNJE, Kenya — Kuanzia katikati ya mwaka 2023, eneo maarufu la kuvua samaki aina ya pweza lililoko karibu na pwani ya kijiji cha Munje lilionekana wazi na tulivu kwa namna ya kushangaza. Wanachama wa kikundi cha usimamizi wa fukwe cha kijiji hicho (BMU) walikuwa wakililinda kwa umakini ili kuhakikisha hakuna anayevua pweza katika sehemu hiyo ya miamba. Mwishoni mwa mwezi Oktoba, kikundi hicho cha BMU kilijitosa baharini kuvuna matunda ya uvumilivu wao. Munje ni kijiji kidogo cha wavuvi kilichopo kwenye pwani ya Bahari ya Hindi, takribani kilomita 60 kusini mwa bandari ya Mombasa. Wakazi wake wanategemea kilimo na uvuvi kama vyanzo vya chakula na mapato. Uvuvi wa pweza, hasa aina ya Octopus vulgaris, kwenye miamba ya baharini ni miongoni mwa shughuli zenye faida kubwa zaidi kwao. Hata hivyo, pweza walikuwa wakipungua kwa kasi kutokana na uvunaji uliopitiliza na uharibifu wa miamba ya matumbawe ambayo ndiyo makazi yao.  “Enzi za baba zetu, kulikuwa na pweza wengi sana hapa, lakini siku hizi mvuvi akienda kuvua, anapotoka baharini, anarudi na kilo moja au mbili tu za pweza,” alisema Mwenyekiti wa BMU, Hamisi Bakari Chimete, wakati akizungumza na Mongabay mwezi Agosti. “Hii ndiyo sababu iliyotufanya tuamue kufunga eneo moja la uvuvi wetu ili kuwapa pweza nafasi ya kuzaliana na kuongezeka, na pia kuruhusu miamba ya matumbawe kujirekebisha.” Maelezo ya bango lililopo katika ofisi ya BMU ya Munje yakionyesha mzunguko wa maisha ya pweza. Kufunga eneo la kuvua pweza kunaruhusu idadi yao kuongezeka upya kati ya vipindi vya uvunaji. Picha na Terna Gyuse kwa niaba ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/01/24/wanakijiji-kenya-waonyesha-namna-ya-kuvuna-pweza-wengi-kwa-kuvua-kidogo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/01/24/wanakijiji-kenya-waonyesha-namna-ya-kuvuna-pweza-wengi-kwa-kuvua-kidogo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>