<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?s=&#038;type=post&#038;topic=upaukaji-wa-matumbawe" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/upaukaji-wa-matumbawe/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 05 Sep 2026 00:00:40 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2026 21:58:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/31214131/Atuwa-akiwa-amezamia-bahari-kwenye-kazi-ya-kurekebisha-matumbawe-kwenye-bahari-ya-kisiwa-cha-Mnemba-Zanzibar.jpeg-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1733</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Barafu ya bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Upaukaji wa Matumbawe, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa bluu, njano na kijani hupita juu ya kichwa chake huku mwanga wa jua ukionekana kwa mbali ndani ya maji. Juu ya uso wa bahari, watalii huwa wanazunguka katika maji bila kufahamu kuhusu mfumo dhaifu wa ikolojia unaopambana kuendelea kuishi chini yake. Kwa mujibu wa waajiri wake, Atuwa, mwenye umri wa miaka 23, anaelezwa kuwa mwanamke pekee Zanzibar anayeshiriki kazi hiyo ya uzamiaji wa urejeshaji wa matumbawe. Mamlaka za Zanzibar zinaeleza kuwa miaka mitatu iliyopita, eneo la Mnemba ambako Atuwa hufanya kazi, ambalo lina baadhi ya miamba muhimu ya matumbawe ya Zanzibar, liliharibika. Makame Omar Makame, Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi Baharini Zanzibar, anasema eneo hilo la Mnemba liliathiriwa na shughuli za kibinadamu zilizokithiri. “Kulikuwa na shughuli nyingi za uvuvi zisizofuata utaratibu, msongamano wa watalii, ambapo takribani boti 200 zenye watalii zilikuwa zikiingia katika eneo la mita 200 za ukanda wa pwani kila siku,” Makame aliieleza Mongabay. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, ili kulinda mazingira, Serikali ya Zanzibar iliamua kupunguza idadi ya wageni hadi 80 kwa siku na kuongeza ada ya uhifadhi kutoka $3 hadi $25 kwa mtalii mmoja, kusitisha kwa muda shughuli za uvuvi na pia kutoa elimu kwa jamii. Hilo lilikuwa jambo muhimu kwa Atuwa na wenzake ambao wanaamini jamii zao zilihitaji mazingira&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>‘Haina maana’: Mwanabiolojia Kenya apinga mpango wa ujenzi wa kiwanda cha nyuklia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/08/29/haina-maana-mwanabiolojia-kenya-apinga-mpango-wa-ujenzi-wa-kiwanda-cha-nyuklia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/08/29/haina-maana-mwanabiolojia-kenya-apinga-mpango-wa-ujenzi-wa-kiwanda-cha-nyuklia/#respond</comments>
					<pubDate>29 Agosti 2025 14:37:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/24143952/Screenshot-2025-09-24-173905-768x471.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=500</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai wa Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Upaukaji wa Matumbawe, na  Wanyama wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya iko katika mchakato wa kujenga kituo chake cha kwanza kabisa cha nishati ya nyuklia. Kwa mujibu wa makadirio ya Shirika la Nguvu za Nyuklia na Nishati la Kenya (NuPEA), ujenzi unatarajiwa kuanza ifikapo mwaka 2027 na kituo hicho kitazalisha megawati 1,000 za umeme. Mji wa Uyombo, ulioko katika kaunti ya Kilifi, pwani ya Kenya, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/29/haina-maana-mwanabiolojia-kenya-apinga-mpango-wa-ujenzi-wa-kiwanda-cha-nyuklia/" data-wpel-link="internal">‘Haina maana’: Mwanabiolojia Kenya apinga mpango wa ujenzi wa kiwanda cha nyuklia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya iko katika mchakato wa kujenga kituo chake cha kwanza kabisa cha nishati ya nyuklia. Kwa mujibu wa makadirio ya Shirika la Nguvu za Nyuklia na Nishati la Kenya (NuPEA), ujenzi unatarajiwa kuanza ifikapo mwaka 2027 na kituo hicho kitazalisha megawati 1,000 za umeme. Mji wa Uyombo, ulioko katika kaunti ya Kilifi, pwani ya Kenya, ni moja ya maeneo matatu yanayofikiriwa na NuPEA kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Lakini tayari kuna pingamizi. Wananchi wakijitokeza kwa sauti moja na kusema kuwa hawataki umeme ya nyuklia. Walisema, “Sitaki Nuclear”. Maandamano yalizuka kabla ya kesi ya kisheria kuwasilishwa mahakamani na wananchi hao. Kesi hiyo ilitupiliwa mbali. Ombi la mtandaoni pia halikufaulu kukomesha mradi huo, kwa kuwa unaendelea mbele, jambo ambalo linawatia wasiwasi wakazi na baadhi ya wanaharakati wa mazingira nchini Kenya. Kijiji cha Uyombo kimezungukwa na mikoko ya Mida Creek, na kiko umbali wa kilomita chache tu kutoka Hifadhi ya Msitu wa Arabuko Sokoke – msitu mkubwa zaidi wa pwani uliosalia Afrika Mashariki, na ambao unatambulika kama kitovu cha bioanuai nchini, kwa sababu ya wingi wa spishi asilia na upotevu wa makazi ya viumbe kwingineko. Uyombo pia imepakana na Hifadhi ya Bahari ya Taifa ya Watamu, ambayo inatambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) kama Hifadhi ya Biosfera (Biosphere Reserve) ikizingatiwa kwamba ina miamba ya matumbawe na wingi wa viumbe wa baharini, kama vile papa wakubwa nyangumi (Rhincodon typus) na samaki wakubwa aina ya manta (Manta alfredi). Je, mradi huu unaweza kuwa na athari gani kwa bioanuai?&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/08/29/haina-maana-mwanabiolojia-kenya-apinga-mpango-wa-ujenzi-wa-kiwanda-cha-nyuklia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/08/29/haina-maana-mwanabiolojia-kenya-apinga-mpango-wa-ujenzi-wa-kiwanda-cha-nyuklia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kujengwa kwa bandari mpya Kenya, tishio kwa viumbe baharini, vitega uchumi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/06/23/kujengwa-kwa-bandari-mpya-kenya-tishio-kwa-viumbe-baharini-vitega-uchumi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/06/23/kujengwa-kwa-bandari-mpya-kenya-tishio-kwa-viumbe-baharini-vitega-uchumi/#respond</comments>
					<pubDate>23 Juni 2025 06:30:40 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/22061221/Screenshot-2025-08-22-091123-768x479.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=183</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Bahari ya Kina, Haki za Kimazingira, Jamii Asili, Kilimo, Maendeleo, Maeneo yaliyolindwa, Mazao, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Miundombinu, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Siasa za Mazingira, Uanaharakati wa tabianchi, Ufugaji Samaki, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, Upaukaji wa Matumbawe, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>SHIMONI, Kenya — Nyuma ya lango la shamba dogo lenye msitu kando ya bahari huko Shimoni, mji mdogo ulioko pwani ya kusini mwa Kenya, maandalizi ya kurejesha matumbawe yalikuwa yakiendelea alasiri moja mwezi Machi. Sehemu moja ya kiwanja ilikuwa imetapakaa kwa sinki za zege, ngome za chuma na plastiki na vizuizi vya kupachika. Vijana wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/23/kujengwa-kwa-bandari-mpya-kenya-tishio-kwa-viumbe-baharini-vitega-uchumi/" data-wpel-link="internal">Kujengwa kwa bandari mpya Kenya, tishio kwa viumbe baharini, vitega uchumi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[SHIMONI, Kenya — Nyuma ya lango la shamba dogo lenye msitu kando ya bahari huko Shimoni, mji mdogo ulioko pwani ya kusini mwa Kenya, maandalizi ya kurejesha matumbawe yalikuwa yakiendelea alasiri moja mwezi Machi. Sehemu moja ya kiwanja ilikuwa imetapakaa kwa sinki za zege, ngome za chuma na plastiki na vizuizi vya kupachika. Vijana wa kiume na wa kike walitumia fursa ya kivuli kufanya kazi wakiwa wamekingwa na jua kali la pwani. Walikuwa wakijenga miundo ya miamba ya kushikilia matumbawe machanga ambayo hivi karibuni wangepanda karibu sana na baharini, sehemu ya mradi unaoongozwa na tawi dogo la Shirika lisilokuwa la kiserikali la Uholanzi, REEFlution. Tangu mwaka 2018, mradi huo umeweka miundo 3,600 ya miamba bandia ili kurejesha miamba ya matumbawe kwenye zaidi ya mita za mraba 5,000 (futi za mraba 54,000) za Mkondo wa Wasini. Kwa mbali kidogo magharibi mwa kiwanja cha REEFolution, pia kwenye Chaneli ya Wasini, bandari mpya ya uvuvi inakuja. Majengo yake makubwa ya rangi ya samawati na nyeupe yametawala mandhari. Jeti mpya imefunika ile ya awali iliyokuwa inatumiwa na wavuvi wa ndani. Hivi karibuni, wenyeji wataanza kuona meli kubwa za kimataifa za uvuvi zikitia nanga kwenye bandari hiyo. Mradi huo wa bandari, ambao umeungwa mkono na Rais wa Kenya, William Ruto, uliigharimu serikali shilingi bilioni 2.6 za Kenya (sawa na dola za Marekani milioni 20) na unatarajiwa kukamilika mwezi Juni. Huku serikali ikiwaahidi wenyeji fursa za ajira na biashara pindi shughuli zikianza, wakazi wengine wanaona madhara zaidi kuliko faida kutokana bandari hiyo. Shughuli za uhifadhi na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/06/23/kujengwa-kwa-bandari-mpya-kenya-tishio-kwa-viumbe-baharini-vitega-uchumi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/06/23/kujengwa-kwa-bandari-mpya-kenya-tishio-kwa-viumbe-baharini-vitega-uchumi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>