<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?s=&#038;type=post&#038;topic=makaa-ya-mawe" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/makaa-ya-mawe/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 05 Sep 2026 00:00:40 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mahakama Kenya yathibitisha kufutwa kwa leseni ya mradi wa umeme wa makaa ya mawe megawati 1,050</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/11/06/mahakama-kenya-yathibitisha-kufutwa-kwa-leseni-ya-mradi-wa-umeme-wa-makaa-ya-mawe-megawati-1050/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/11/06/mahakama-kenya-yathibitisha-kufutwa-kwa-leseni-ya-mradi-wa-umeme-wa-makaa-ya-mawe-megawati-1050/#respond</comments>
					<pubDate>06 Novemba 2025 22:05:43 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/18221150/Screenshot-2025-11-19-011134-768x478.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=813</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Kimazingira, Jamii Asili, Maji, Makaa ya Mawe, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi wa Maji, na  Visukuku]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama inayosimamia masuala ya Mazingira na Ardhi nchini Kenya, imethibitisha uamuzi ulitolewa mwaka 2019, ambao ulibatilisha leseni ya mazingira iliyokuwa imetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kiwanda cha umeme unaotokana na makaa ya mawe cha Lamu chenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1,050. Kwa uamuzi huo, mradi huo uliogubikwa na utata umesitishwa rasmi. [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/06/mahakama-kenya-yathibitisha-kufutwa-kwa-leseni-ya-mradi-wa-umeme-wa-makaa-ya-mawe-megawati-1050/" data-wpel-link="internal">Mahakama Kenya yathibitisha kufutwa kwa leseni ya mradi wa umeme wa makaa ya mawe megawati 1,050</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama inayosimamia masuala ya Mazingira na Ardhi nchini Kenya, imethibitisha uamuzi ulitolewa mwaka 2019, ambao ulibatilisha leseni ya mazingira iliyokuwa imetolewa kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa kiwanda cha umeme unaotokana na makaa ya mawe cha Lamu chenye uwezo wa kuzalisha umeme wa megawati 1,050. Kwa uamuzi huo, mradi huo uliogubikwa na utata umesitishwa rasmi. Jaji Francis Njoroge aliitupilia mbali rufaa iliyowasilishwa na kampuni ya Amu Power kwa hoja kwamba tathimini ya athari za mazingira na kijamii (ESIA) ya mradi huo, haikujitosheleza na wala haikuwashirikisha kikamilifu wananchi. Uamuzi huo umemaliza mgogoro wa kisheria wa miaka mingi na upinzani kutoka kwa wenyeji dhidi ya kiwanda hicho kilichopangwa kujengwa kwenye safu ya visiwa vya Lamu nchini Kenya. Safu hiyo ya visiwa ni eneo la Urithi wa Dunia la UNESCO lenye utajiri wa mikoko, mazalia ya nyasi za baharini na miamba ya matumbawe, ambavyo ni mhimili wa uvuvi na utalii. Mnamo mwaka 2016, Mamlaka ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mazingira ya Kenya (NEMA), ilitoa leseni ya awali ya mradi huo kwa kampuni ya Amu Power. Hata hivyo, hatua hiyo ilipokelewa kwa upinzani mkubwa kutoka kwa Save Lamu, muungano wa mashirika yapatayo 40 ya kiraia pamoja na kampeni ya deCOALonize, harakati za kikanda zinayopinga uendelezaji wa makaa ya mawe. Madai makubwa ya makundi hayo ni kwamba thathmini ya ESIA ilipuuzia athari za mradi huo kwa afya ya bayoanuai na pia ushirikishwaji wa wananchi haukuwa wa kuridhisha. Mnamo mwaka 2019, Mahakama ya Mazingira ya Kitaifa (NET) ilifuta leseni hiyo kwa hoja kwamba utoaji wa taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/11/06/mahakama-kenya-yathibitisha-kufutwa-kwa-leseni-ya-mradi-wa-umeme-wa-makaa-ya-mawe-megawati-1050/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/11/06/mahakama-kenya-yathibitisha-kufutwa-kwa-leseni-ya-mradi-wa-umeme-wa-makaa-ya-mawe-megawati-1050/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>