<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?s=&#038;type=post&#038;topic=kilimo-ikolojia" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/kilimo-ikolojia/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 05 Sep 2026 00:00:40 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/#respond</comments>
					<pubDate>17 Juni 2026 13:26:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/17130445/Screenshot-2026-06-17-160345-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1868</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, Kenya, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Biashara ya Kilimo, Bioanuai wa Baharini, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo-ikolojia, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mimea, Mimea yenye Tiba, na  Uhifadhi wa Baharini]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mbinu za uchakachuaji wa mwani zaongeza juhudi za kuimarisha soko nchini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Kila siku asubuhi maji yanapopungua katika ufuo wa bahari wa Kibuyuni, Kaunti ya Kwale kusini mwa pwani ya Kenya, Salim Ahmed na wakulima wenzake wa mwani huelekea baharini kuangalia mashamba yao. Ahmed amefanya ukulima wa mwani kwa miaka mitatu sasa. Ukosefu wa ajira na uhaba wa fursa za kiuchumi vilimsukuma kutafuta njia mbadala ya kujikimu kimaisha. Kilimo cha mwani kikawa jibu lake, akaamua kujiunga na wanakijiji wenzake wanaofanya ukulima huo. Mwani ni kundi la viumbe wa majini wanaofanana na mimea inayokua katika maji ya chumvi, hasa maeneo ya pwani yenye kina kifupi. Hupandwa kwa kufungwa kwenye vitiji na kamba baharini. Mwani huchukua kati ya siku 45 na 60 kufikia kiwango cha kuvunwa. Mwani hutumika kutengeneza bidhaa mbalimbali kama vile vipodozi, sabuni, dawa, virutubisho vya lishe, vinywaji na malighafi za viwandani. What is seagrass and why is it important? Kwa wakulima wengi wa mwani katika eneo la Kwale, baada ya kuvuna wao huukausha kisha kuuuza kupitia chama cha ushirika cha mwani katika eneo la Kibuyuni. Ukulima wa mwani ulishirikisha wanawake wengi katika eneo la Kibuyuni ili wapate fursa ya kupata manufaa ya bahari ambayo imekuwa tegemeo la upatikanaji wa riziki kwa familia nyingi eneo la Pwani. Hii ni kutokana na kuwepo kwa mila na tamaduni zilizomwekea vikwazo mwanamke kuingia baharini kuvua samaki. Wakulima wa Mwani wakitayarisha Kamba tayari kwa mafunzo kuhusu upandaji wa Mwani eneo la Shanga, Lamu, Kenya. Picha na Mohamed Fuad Mohamed. Lakini ukulima huo sasa umeanza kuvutia hata wanaume kama Ahmed, kutokana na faida ambazo wameziona kwa wanawake, wakiwa na matumaini ya kupata kipato cha kujiendeleza kimaisha.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/17/mbinu-za-uchakachuaji-wa-mwani-zaongeza-juhudi-za-kuimarisha-soko-nchini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mjini Kivu nchini DRC, Moringa unatoa manufaa muhimu kiafya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/#respond</comments>
					<pubDate>09 Oktoba 2025 19:27:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Blaise Kasereka Makuta]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/11/03193952/Screenshot-2025-11-03-223837-768x473.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=725</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Ikolojia, Kilimo, Kilimo-ikolojia, Maarifa ya Jadi, Mazingira, Mimea, Mimea yenye Tiba, Misitu, Miti, Sheria ya Mazingira, Ufugaji, Ufugaji wa Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Moringa, mti ambao mara nyingi huhusishwa na eneo lake la asili la taifa la India, pia ni mmea wenye thamani unaopatikana maelfu ya maili kutoka eneo la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ndani ya nchi, mti wa Moringa huchukua jukumu muhimu la utengenezaji wa dawa za jadi, za jadi-kileo (mchanganyiko wa dawa za [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/" data-wpel-link="internal">Mjini Kivu nchini DRC, Moringa unatoa manufaa muhimu kiafya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Moringa, mti ambao mara nyingi huhusishwa na eneo lake la asili la taifa la India, pia ni mmea wenye thamani unaopatikana maelfu ya maili kutoka eneo la Kivu katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo. Ndani ya nchi, mti wa Moringa huchukua jukumu muhimu la utengenezaji wa dawa za jadi, za jadi-kileo (mchanganyiko wa dawa za zamani na mpya) na za kisasa. Kulingana na watabibu na wagonjwa kadhaa wa kienyeji, kutokana na sifa zake za matibabu, moringa unaweza kutumika kutibu magonjwa mbalimbali kama vile kisukari, maumivu ya misuli, udhaifu wa kijinsia na mengine mengi. &#8220;Kando na sifa zake za dawa, moringa una faida nyingi; ni mti wa asili unaorutubisha,&#8221; Jackeline Muderwa, mwanamke mwenye umri wa miaka 69 na mtabibu kutoka mtaa wa Mugunga huko Goma, alielezea katika mahojiano na Mongabay. Anaihusisha na kipindi cha ukoloni wa Ubelgiji karibu katikati ya karne ya 20. &#8220;Wabelgiji waliipanda miti ya moringa kwenye bustani zao na kuitumia kutibu magonjwa yao fulani. Naamini hapo ndipo tulipofahamu manufaa yake. Mara nyingi hata msituni, uwepo wake ulidhihirisha uwepo wa babu wa mtu mahali hapo ambaye huenda alihama.&#8221; Moringa, kwa jina la kibayolojia Moringa oleifera, ni mti unaokua kwa haraka wa familia ya Moringaceae; jina la kibayolojia. Ingawa umeainishwa kimataifa kama spishi isiyojali sana kwenye Orodha Nyekundu ya shirika la IUCN, mti huu unahitaji uangalizi maalum. Hulimwa hasa katika maeneo ya nusu-kame, kitropiki na maeneo ya nusu-tropiki. (Kushoto) Spishi ya Moringa, kwa jina la kibayolojia Moringa oleifera, ni spishi ya miti asili wa India lakini pia inatumika DRC kwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2025/10/09/mjini-kivu-nchini-drc-moringa-unatoa-manufaa-muhimu-kiafya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Wamaasai wa Tanzania yabidi wapunguze mifugo, waongeze miti</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/10/30/kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-wamaasai-wa-tanzania-yabidi-wapunguze-mifugo-waongeze-miti/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/10/30/kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-wamaasai-wa-tanzania-yabidi-wapunguze-mifugo-waongeze-miti/#respond</comments>
					<pubDate>30 Oktoba 2024 00:10:03 +0000</pubDate>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/27235720/Screenshot-2025-08-28-025223-768x472.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=274</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Kilimo, Kilimo-ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo ya Jamii, Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Mazingira, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, na  Uhifadhi Unaofanywa na Jamii]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kijiji cha Terrat, ambacho kina wakazi wapatao 14,000 waishio eneo lenye ukame kiasi na misitu ya mikunga katika Ukanda wa Wamaasai, ni miongoni mwa vijiji vingi kaskazini mwa Tanzania vilivyoathiriwa na ukame mkali wa mara kwa mara. Wakazi wa Terrat — wakulima na wafugaji — wanajitahidi kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa msaada [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/10/30/kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-wamaasai-wa-tanzania-yabidi-wapunguze-mifugo-waongeze-miti/" data-wpel-link="internal">Kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Wamaasai wa Tanzania yabidi wapunguze mifugo, waongeze miti</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kijiji cha Terrat, ambacho kina wakazi wapatao 14,000 waishio eneo lenye ukame kiasi na misitu ya mikunga katika Ukanda wa Wamaasai, ni miongoni mwa vijiji vingi kaskazini mwa Tanzania vilivyoathiriwa na ukame mkali wa mara kwa mara. Wakazi wa Terrat — wakulima na wafugaji — wanajitahidi kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi kwa msaada wa shirika linalosaidia upandaji miti sambamba na kutoa mbinu mpya za kilimo na fursa za kiuchumi. Ukame si jambo geni katika wilaya ya Simanjiro, ambako ndiko Terrat ilipo, lakini kuanzia mwanzoni mwa miaka ya 2000, eneo hili la Tanzania lilishuhudia kipindi cha zaidi ya miaka 20 cha upungufu mkubwa wa mvua. Hili lilileta changamoto kubwa kwa takriban asilimia 80 ya wakazi wa Terrat ambao ni wafugaji wanaotegemea mvua kwa ajili ya malisho ya mifugo yao. Mwenyekiti wa kijiji cha Terrat, Kone Medukenya, aliiambia Mongabay kuwa kutokana na uhaba wa malisho na vyanzo vingi vya maji kukauka, ng’ombe walidhoofika na wengi kufa, na kwamba ni mbuzi peke yake walioweza kustahimili. Hii ilipunguza chanzo kikuu cha mapato kwa wafugaji. Wafugaji walilazimika kusafiri umbali mrefu kutafuta maeneo ya malisho, mara nyingi wakiingia kwenye maeneo ya jamii jirani, jambo lililosababisha migogoro kuhusu rasilimali zinazozidi kupungua. Ukame pia ulisababisha kupanda kwa bei ya chakula katika sehemu hii ya Tanzania. Bei ya gunia la mahindi la kilo 100 (sawa na pauni 220) ilipanda kutoka dola za Marekani 11 mwaka 2004 hadi dola 66 mwaka 2008, na iliendelea kupanda kwa takriban miaka 10. Kwa mujibu wa wakazi wa Simanjiro, katika kipindi hicho, kuna wakati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/10/30/kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-wamaasai-wa-tanzania-yabidi-wapunguze-mifugo-waongeze-miti/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/10/30/kukabiliana-na-mabadiliko-ya-tabianchi-wamaasai-wa-tanzania-yabidi-wapunguze-mifugo-waongeze-miti/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/#respond</comments>
					<pubDate>02 Agosti 2023 12:48:18 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/09/05054458/Screenshot-2025-10-05-083758-768x477.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=607</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Kijani, Kilimo, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Kupunguza Umaskini, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mifumo ya Ikolojia ya Maji Baridi, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sekta ya Chakula, Uendelevu, Ufugaji Samaki, Uhifadhi, na  upatikanaji wa chakula]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Ufugaji endelevu wa samaki na kilimohai vyaimarisha jamii za Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[GATUNGA, Kenya — Msimu wa ukame ambao uliisumbua Kenya kwa miaka michache iliyopita umetikisa mifumo ya chakula vijijini nchini humo. Lakini Japheth Nthiga, mkulima kutoka kijiji cha Karethani sehemu ya kati ya Kenya, amekuwa akipata faraja wakati wa kipindi kigumu. Hiyo ni kwa sababu Nthiga amebadilisha sehemu ya ardhi yake kuwa mabwawa ya kufugia samaki, huku shamba lake lililosalia, likisaidia mifugo na mazao ya chakula kama maharage ya kijani, mtama, uwele na mahindi. Tangu mwaka 2013, ni nusu ekari tu ya eneo lake ambayo imemnufaisha zaidi. &#8220;Samaki ninaowafuga hapa ni kwa ajili ya matumizi ya ndani. Pia ninapata mapato mazuri ninapouza samaki katika soko la huku nchini. Sioni wasiwasi wakati mazao yangu ya chakula yanaposhindwa kutoa mavuno,&#8221; alisema baba huyo wa watoto watano mwenye umri wa miaka 51, anayefuga ngege na kambare. Japheth Nthiga anafuga samaki aina ya ngege na kambare katika mabwawa ya samaki kwenye shamba lake eneo la kati ya Kenya. Picha na David Njagi wa Mongabay.  Ni rahisi kuelewa vizuri hisia za Nthiga. Kijiji chake, ambacho kiko takriban kilomita 150 (sawa na maili 90) kutoka ukingo wa Msitu wa Mlima Kenya, kimekumbwa na ukame wa muda mrefu na wa mara kwa mara kwa zaidi ya muongo mmoja uliopita. Ili kukabiliana na msimu wa kiangazi, wakulima, hasa wale wanaotoka katika nyanda za juu za mito, wamezidisha matumizi yao ya mbolea ili kuongeza mavuno, na kwa kufanya hivyo, wamesababisha uchafuzi wa mito na kupoteza rutuba ya udongo katika eneo hilo, kulingana na Venter Mwongera, ambaye ni mratibu wa mawasiliano&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2023/08/02/viongozi-wapendekeza-suluhisho-zilizobuniwa-ndani-kwenye-mkutano-wa-hali-ya-hewa-afrika-na-dola-bilioni-100-kuzitekeleza/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>