<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?s=&#038;type=post&#038;topic=dioksidi-ya-kaboni" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/list/dioksidi-ya-kaboni/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Sat, 05 Sep 2026 00:00:40 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=7.0.4</generator>
				<item>
					<title>Kenya yaanzisha mabasi ya umeme kukabili uchafuzi wa hewa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/#respond</comments>
					<pubDate>12 Desemba 2024 17:05:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Stephanie Wangari]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2025/08/25105127/c2bb7b40-27ce-4f07-b856-41df9afa1f36-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=249</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Dioksidi ya kaboni, Maendeleo, Maendeleo Endelevu, Mafuta, Mazingira, na  Uchafuzi wa Hewa]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI — Zaidi ya mabasi 22,000 huwa kwenye mitaa yenye msongamano jijini Nairobi, yakibeba sehemu kubwa ya wakazi milioni 5.3 wa mji huo mkuu wa Kenya. Mabasi ya abiria, maarufu kama matatu ya Nairobi, ambayo ni mali ya watu binafsi, yanajulikana kwa kupambwa kwa rangi kali na picha za wasanii wa muziki wa rap au [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/" data-wpel-link="internal">Kenya yaanzisha mabasi ya umeme kukabili uchafuzi wa hewa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI — Zaidi ya mabasi 22,000 huwa kwenye mitaa yenye msongamano jijini Nairobi, yakibeba sehemu kubwa ya wakazi milioni 5.3 wa mji huo mkuu wa Kenya. Mabasi ya abiria, maarufu kama matatu ya Nairobi, ambayo ni mali ya watu binafsi, yanajulikana kwa kupambwa kwa rangi kali na picha za wasanii wa muziki wa rap au vilabu vya soka vya Uingereza. Miongoni mwa haya magari yanayotumia dizeli yenye kelele nyingi na kutoa moshi mzito, sasa kuna wageni wapya 35 ambao hawana kelele; wageni hao ni mabasi ya umeme yaliyounganishwa na kampuni ya humo humo nchini iitwayo BasiGo. Kwa miaka sita sasa, Isaac Kamau amekuwa akihudumu kama dereva wa basi jijini Nairobi, akisafirisha abiria kutoka katikati mwa jiji hadi maeneo ya makazi. Mwaka 2022, alipata fursa ya kupewa mafunzo maalum ya kuendesha basi la umeme. “Kila mhitimu alitakiwa kuwa na historia nzuri ya kazi ili kupata nafasi kama hii,” Kamau aliiambia Mongabay. Mafunzo yake yalilenga zaidi uendeshaji rafiki kwa mazingira na usalama, na sasa anafurahia gari lake jipya. “Abiria wanapendelea mabasi ya umeme kuliko yale yanayotumia mafuta. Hawahitaji kushawishiwa kupanda. Yanafariji zaidi, ni ya haraka na hayana kelele.” Basi la Kamau ni miongoni mwa mabasi 35 ya umeme yanayofanya kazi jijini, huku mengine 14 yakitarajiwa kuongezwa mjini humo mwishoni mwa mwaka 2024. Kampuni ya BasiGo, ambayo huunganisha mabasi nchini Kenya kwa kutumia sehemu zinazotengenezwa na kampuni ya China ya CHTC, inasema tayari imepokea maagizo ya awali 500 kutoka kwa waendeshaji wa mabasi. Matatu za Nairobi ni zaidi ya chombo cha usafiri wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2024/12/12/kenya-yaanzisha-mabasi-ya-umeme-kukabili-uchafuzi-wa-hewa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>