<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?post_type=post&#038;byline=dann-okoth" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Thu, 11 Jun 2026 19:44:46 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=6.9.4</generator>
				<item>
					<title>Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 19:43:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11194040/Vijana-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1846</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Fedha, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kenya yawa nchi ya kwanza barani Afrika kupokea ufadhili wa kukabiliana na majanga ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya imekuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na ufadhili huo wa kukabiliana na majanga ya tabianchi, msaada unaolenga kusaidia waliopata hasara na uharibifu unaotokana na mabadiliko ya tabianchi katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Fedha hizo, kiasi cha KSh90 milioni ($700,000) kutoka Santiago Network on Loss and Damage, mfumo wa Umoja wa Mataifa wenye makao yake nchini Uswisi unaofadhiliwa kupitia michango ya hiari kutoka kwa nchi zilizoendelea na jumuiya ya kimataifa, zitatolewa kupitia serikali na kusambazwa kwa jamii mbalimbali nchini zinazokabiliwa na majanga mbalimbali yanayochochewa na mabadiliko ya tabianchi. Majanga hayo ni pamoja na ukame wa mara kwa mara, mafuriko, kupungua kwa uzalishaji wa mazao, uharibifu wa mazao na matukio mengine ya hali mbaya ya hewa. Katibu Mkuu wa Wizara ya Mazingira, Mabadiliko ya Tabianchi na Misitu wa Kenya, Festus Ng’eno, alisema msaada huo ni hatua muhimu sana. Ng’eno alisema hatua hiyo inaifanya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika na ya pili duniani kunufaika na mfuko huo. Vanuatu, taifa la funguvisiwa lenye maeneo mengi ya mwinuko wa chini, ndiyo iliyokuwa nchi ya kwanza duniani kupata ufadhili huo. Ng’eno alitoa taarifa hiyo katika mazungumzo yaliyofanyika sambamba na mazungumzo ya kiufundi ya tabianchi ya UNFCCC Subsidiary Bodies (SB64) yanayoendelea huko Bonn, Ujerumani. Katika taarifa aliyochapisha mtandaoni, akithibitisha habari iliyochapishwa na gazeti la People Daily mnamo Juni 10, Dkt Ng’eno alisema kuwa licha ya Kenya kupitia baadhi ya majanga makubwa zaidi ya tabianchi katika Afrika Mashariki, nchi hiyo haijawahi kupima kikamilifu kiwango halisi cha hasara iliyopata kutokana na majanga hayo. &#8220;Hali hiyo sasa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/kenya-yawa-nchi-ya-kwanza-barani-afrika-kupokea-ufadhili-wa-kukabiliana-na-majanga-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 13:46:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ashoka Mukpo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11131849/Screenshot-2026-06-11-161609.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1841</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Urusi, Zambia, na  Zimbabwe]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchafuzi wa Hewa, Uhalifu wa Mazingira, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Matumizi ya makaa ya mawe duniani yapungua mwaka 2025 huku uwezo wa mitambo ukiendelea kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Matumizi ya makaa ya mawe duniani kote yaliendelea kupungua mnamo mwaka 2025, lakini kulikuwa na ongezeko la uwezo wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe, kulingana na ripoti ya kila mwaka ya kikundi cha uchambuzi wa data Global Energy Monitor. Uzalishaji wa umeme kutoka kwa makaa ya mawe kwa ujumla ulipungua kwa 0.6% mwaka jana, lakini uwezo wa akiba wa mitambo ya makaa ya mawe unaoweza kutumika wakati wa mahitaji makubwa ya umeme uliongezeka kwa 3.5%. Sehemu kubwa ya ongezeko hilo ilitokea nchini Uchina, ambapo uwezo wa ziada wa kuzalisha umeme kwa kutumia makaa ya mawe unazidi kuchukuliwa kuwa chaguo mbadala ili kuhakikisha usalama wa nishati. Wakati Uchina iliongeza gigawati 78.1 za uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo 2025, matumizi yake halisi ya nishati ya makaa ya mawe yalipungua kwa 1.2%. Kupungua huku kulidhihirika wazi kwani kulikuja huku kukiwa na ongezeko la jumla la mahitaji ya nishati ya Uchina. Kulingana na ripoti hiyo, zaidi ya 90% ya ongezeko hilo la mahitaji ya nishati lilikidhiwa na nishati ya upepo na jua badala ya makaa ya mawe. Wakati Uchina inasalia kuwa mtumiaji mkubwa zaidi wa makaa ya mawe duniani, mahitaji yake zaidi ya nishati yanatimizwa kwa njia mbadala. India ilirekodi ongezeko la pili kwa ukubwa la uwezo wa nishati ya makaa ya mawe mnamo mwaka 2025, lakini pia ilionyesha harakati kuelekea gridi safi zaidi. Pamoja na nyongeza za rekodi za nishati ya jua na upepo, nishati jadidifu zilichangia zaidi ya nusu ya uwezo wa jumla wa nishati nchini kwa mara ya kwanza. Christine Shearer, mtafiti&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/matumizi-ya-makaa-ya-mawe-duniani-yapungua-mwaka-wa-2025-huku-uwezo-wa-mitambo-ukiendelea-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/#respond</comments>
					<pubDate>11 Juni 2026 11:57:25 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Manuel Fonseca]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/11113159/Screenshot-2026-06-11-143059.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1834</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Misitu, Moto, Moto wa Misitu, Reptilia, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Namna marufuku ya biashara ya wanyama na juhudi za uhifadhi zilivyosaidia kuokoa mijusi ya samawati</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Uzuri ni laana &#8211; angalau kwa mjusi mdogo wa rangi ya samawati (turquoise dwarf gecko) anayepatikana katikati mwa Tanzania. Kati ya Desemba 2004 na Julai 2009, mahitaji ya mjusi huyu kutoka kwa wakusanyaji wa wanyama barani Ulaya yaliongezeka sana, jambo lililosababisha kukamatwa na kusafirishwa nje ya Tanzania kwa takriban mijusi 40,000 ya aina hii iliyokuwa na mwonekano wa kuvutia. “Nakumbuka nilipowaona kwa mara ya kwanza katika maonyesho ya wanyama, bei yao ilikuwa dola za Marekani 700 kwa kila mmoja ambazo ni sawa na zaidi ya shilingi za Tanzania milioni 1.8,” alisema Dennis Rödder, mtaalamu wa wanyama watambaao kutoka Leibniz Institute for the Analysis of Biodiversity Change nchini Ujerumani, katika mahojiano na Mongabay yaliyofanyika kwa njia ya video. “Nadhani ndani ya miaka mitatu au minne, spishi hii ilikuwa imeenea kote Ulaya. Ilikuwa ni rahisi kuinunua kutoka duka lolote la wanyama wa kufugwa.” Mijusi hawa wanaojulikana kisayansi kama (Lygodactylus williamsi) hukua hadi kufikia urefu wa sentimita 6–9 (takriban inchi 2.5–3.5). Wanapatikana tu katika maeneo mawili madogo ya misitu nchini Tanzania: Hifadhi ya Misitu ya Kimboza na Hifadhi ya Ruvu. Maeneo haya yaliyohifadhiwa yana ukubwa wa jumla ya kilomita za mraba 34 (takriban maili za mraba 13). Majike waliokomaa wana rangi ya kijani-kahawia inayofanana na majani ya miti wanayoishi, jambo linalowasaidia kujificha dhidi ya maadui. Hata hivyo, madume huwa na ngozi ya samawati ang’avu inayovutia sana. Rangi hii ni miongoni mwa rangi adimu zaidi kupatikana kiasili, na hutumika kuwavutia majike wakati wa uzazi. Mjusi mdogo wa rangi ya samawati (Lygodactylus williamsi). Picha: © Simon kupitia iNaturalist (CC&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/11/namna-marufuku-ya-biashara-ya-wanyama-na-juhudi-za-uhifadhi-zilivyosaidia-kuokoa-mijusi-ya-samawati/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/#respond</comments>
					<pubDate>10 Juni 2026 18:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/10161044/Meno-ya-tembo-2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1830</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ikolojia, Kupambana na ujangili, Mamalia, Mamalia Wakubwa, Sheria ya Mazingira, Tembo, Uhifadhi wa Wanyamapori, Ujangili, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na meno ya tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yapigwa tarehe tena</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili raia mmoja wa Korea Kaskazini, Un Hyok Ra (37), anayeshitakiwa kwa kukutwa akimiliki nyara za Serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni, imepigwa tarehe tena kwa madai kuwa upelelezi wake haujakamilika. Shauri hilo limetajwa leo Juni 9, 2026 katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Jijini Dar es Salaam mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mwasha. Akiwakilisha upande wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Florida Wenceslaus aliomba mahakama ipange tarehe nyingine ya kutajwa kwa kesi hiyo kwa kile alichoeleza kuwa upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika. Mshtakiwa, ambaye anaendelea kusota rumande, hakuwepo mahakamani leo kama ilivyokuwa wakati kesi hiyo ilipotajwa Mei 25, na pia hakuwa na mwakilishi. Hakimu Mwasha alikubali ombi la upande wa mashitaka na akaahirisha shauri hilo hadi Juni 23 mwaka huu, kesi itakapotajwa tena. Mshtakiwa Ra alipanda kizimbani kwa mara ya kwanza mwanzoni mwa Mei mwaka huu. Shauri lilipotajwa baada ya siku 14, yaani Mei 25 mwaka huu, mshtakiwa huyo hakufikishwa mahakamani na badala yake shauri liliahirishwa bila yeye kuwepo. Kabla ya kuahirisha kesi hiyo, hakimu aliamuru hati ya kumfikisha mshtakiwa kortini itolewe ili kesi itakapotajwa Juni 9, 2026, mshtakiwa aletwe kortini. Hata hivyo leo mshtakiwa hakufikishwa kortini na hakuna maelezo yoyote yaliyotolewa kwa nini mshatakiwa hakuwepo. Awali upande wa Jamhuri ulidai katika hati ya mashtaka kuwa mshtakiwa anakabiliwa na mashtaka mawili, kukutwa akimiliki nyara za Serikali na kujihusisha na biashara hiyo bila kibali. Ilidaiwa kuwa Aprili 19, 2026 katika eneo la Hoteli ya Golden Tulip–Masaki,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/10/kesi-ya-kukutwa-na-meno-ya-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yapigwa-tarehe-tena/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 19:10:28 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Victoria Schneider]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09143738/EACOP-Main-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1826</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Maziwa, Mgogoro wa Mazingira, Mimea, Samaki, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhalifu wa Mazingira, Uhifadhi, Utawala, Uvuvi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">EACOP latishia mifumo ya maji safi na njia za uhamaji wa wanyamapori, ripoti yabaini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) linaloanzia kwenye vitalu vya mafuta ya Ziwa Albert nchini Uganda hadi mji wa bandari wa Tanga nchini Tanzania, limeanza tena kuchunguzwa kwa karibu baada ya kutolewa kwa ripoti mpya inayobainisha maeneo ya bioanuwai na makazi ya wanyamapori ambayo bomba hilo linapitia au ambayo liko karibu nayo. Kwa kutumia takwimu za ramani na makadirio ya thamani ya kiuchumi, ripoti ya Earth Insight, shirika lisilo la kiserikali lenye makao yake makuu nchini Marekani, inaonyesha kuwa bomba hilo lenye urefu wa kilomita 1,443 liko karibu na maeneo muhimu kwa maisha ya mamilioni ya watu na usalama wa maji, na pia sehemu ambazo hutumika kama njia za uhamaji wa wanyama. Kutokana na uchambuzi huo, ripoti hiyo inahitimisha kuwa ujenzi wa bomba hilo tayari umeathiri jamii na mazingira, na kwamba usafirishaji wa mafuta utaleta hatari zaidi za muda mrefu. EACOP ni mradi wa ubia kati ya  kampuni ya TotalEnergies yenye asilimia 62 ya hisa, serikali za Uganda na Tanzania kila moja ikiwa na asilimia 15, pamoja na China National Offshore Oil Corporation (CNOOC) yenye asilimia 8. EACOP itasafirisha mafuta yanayochimbwa kutoka vitalu viwili kwenye bonde la Ziwa Albert: Kingfisher, linalomilikiwa na CNOOC; na Tilenga, linalomilikiwa na TotalEnergies. Ujenzi wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) nchini Uganda. Picha kwa hisani ya Thomas Lewton. Kwa mujibu wa Earth Insight, mradi huo unakaribia kukamilika na mafuta ya kwanza yataanza kusafirishwa mapema mwaka 2026. “Linapita moja kwa moja katika maeneo ya viumbe walio hatarini kutoweka, na eneo muhimu zaidi ni la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/eacop-latishia-mifumo-ya-maji-safi-na-njia-za-uhamaji-wa-wanyamapori-ripoti-yabaini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 14:29:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Isack Dickson]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09125042/3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1810</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Kupungua kwa ushoroba wa Kwakuchinja kwatishia uhamaji wa wanyamapori</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ushoroba wa Kwakuchinja, ambao katika toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu manufaa ya ushoroba nchini Tanzania, ulielezwa kuleta manufaa makubwa kwa uhifadhi na pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge, uko hatarini kutokana na kuendelea kupungua siku hadi siku. Ushoroba huo uko Kaskazini mwa Tanzania, kati ya Hifadhi za Taifa za Tarangire na Ziwa Manyara, na unaokatiza maeneo ya Babati, Monduli na Simanjiro, umeendelea kuwa kiunganishi muhimu cha mifumo ya ikolojia katika ukanda huo wenye utajiri mkubwa wa viumbe hai. Kwa miongo kadhaa umekuwa njia muhimu ya kupita kwa wanyamapori wanaohama kutoka eneo moja kwenda lingine. Wanyama aina ya pundamilia wakiwa katika ushoroba wa Kwakuchinja. Picha na Isack Dickson. Revocatus Meney, mtafiti kutoka TAWIRI, anasema ushoroba huo umekuwa ukipungua siku hadi siku kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu. Makazi, kilimo na mifugo vinaendelea kuubana mwaka hadi mwaka na kuufanya uwe finyu. Kwa mujibu wa tafiti za TAWIRI, miaka ya 1970, ushoroba wa Kwakuchinja ulikuwa na ukubwa unaofikia kilomita za mraba 600. Hata hivyo, Meney anasema kutokana na ongezeko la shughuli za kibinadamu ikiwemo makazi, kilimo na matumizi mengine ya ardhi, eneo hilo limeendelea kupungua na kufikia takribani kilomita za mraba 274.45 kwa sasa. Kupungua huku kunamaanisha kuwa zaidi ya nusu ya eneo la awali la ushoroba limepotea ndani ya kipindi cha takribani miongo mitano. Meney anasema hakuna kiwango kimoja cha upana kinachotumika kwa ushoroba kwa sababu hutegemea aina ya wanyama wanaoutumia na mazingira husika. Hata hivyo, anasema kadri ushoroba unavyokuwa mpana na usio na vikwazo vya shughuli&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/kupungua-kwa-ushoroba-wa-kwakuchinja-kwatishia-uhamaji-wa-wanyamapori/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 13:12:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Akana]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09111629/Screenshot-2026-06-09-141545.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1799</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, na  Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Hifadhi, Hifadhi za Taifa, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uhifadhi wa Misitu wa Mvua, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Alinusurika shambulio hatari, sasa anataka mazingira bora ya kazi kwa walinzi wa mbuga nchini DRC</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Afrika ya kati, kulinda asili kunaweza kugharimu maisha yako. Kwa miaka mingi, walinzi wanaofanya kazi katika mbuga za wanyamapori kama Virunga na Kahuzi-Biega wamefanya kazi katikati ya makundi yenye silaha, usafirishaji haramu wa maliasili, mivutano ya kijamii na vurugu za kudumu ambazo tayari zimegharimu maisha ya mamia ya wenzao. Hata hivyo, licha ya jukumu lao kuu katika kulinda bayoanuwai na baadhi ya misitu muhimu zaidi ulimwenguni, wengi wanaendelea kufanya kazi wakiwa na usaidizi mdogo, mishahara midogo, na hali hatarishi sana. Kwa Emmanuel Bahati Lukoo, ukweli huu ni wa kibinafsi sana. Aliwahi kuwa mlinzi katika mbuga ya kitaifa ya Virunga ambapo kwa sasa ni afisa katika Hifadhi ya Kitaifa ya Kahuzi-Biega, alinusurika kifo katika shambulizi la kushutukizia mnamo mwaka wa 2018 na kikundi cha wanamgambo wa jamii kinachojulikana kama Mai-Mai. Wenzake kadhaa waliuawa kwa kuviziwa. Alipigwa risasi, alijeruhiwa na kupata kiwewe cha kisaikolojia, na baadaye kufunguliwa mashitaka mbele ya mahakama ya kijeshi katika kesi iliyohusishwa na ulinzi wa hifadhi, angeweza kuondoka. Badala yake, Bahati alichagua kusimulia hadithi yake katika kitabu kiitwacho Conservation at the Cost of My Youth: The Survival of a Ranger, simulizi ghafi ya dhabihu, hofu, shinikizo za kisiasa, na mara nyingi hali halisi isiyoonekana inayowakabili walinzi wa misitu mashariki mwa DRC. Kwenye mahojiano ya ana kwa ana na Mongabay, Bahati anatafakari safari yake, shambulizi lililokaribia kumuua, kiwewe walichopata walinzi, migogoro kati ya uhifadhi na maisha ya jamii ya eneo hilo, na uingiliaji wa kisiasa unaotatiza ulinzi wa maeneo yaliyohifadhiwa. Zaidi ya hadithi ya kibinafsi,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/alinusurika-shambulio-hatari-sasa-anataka-mazingira-bora-ya-kazi-kwa-walinzi-wa-mbuga-nchini-jamhuri-ya-kidemokrasia-ya-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yatishia ikolojia ya bahari Zanzibar &#8211; Serikali</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/#respond</comments>
					<pubDate>09 Juni 2026 11:55:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/09103711/ZANZIBAR-ECOLOGY.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1795</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Huduma za Mazingira, Ikolojia, Irejeshaji wa Mfumo wa Ikolojia, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Urejeshaji wa Ikolojia, Utawala, na  Uzuri wa Kiikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Licha ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhifadhi ikolojia ya bahari kupitia usimamizi endelevu wa rasilimali zake, mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuwa tishio kubwa kwa mazingira hayo na ustawi wa jamii zinazoyategemea. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, amesema athari za mabadiliko ya tabianchi zinahatarisha mafanikio ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yatishia ikolojia ya bahari Zanzibar &#8211; Serikali</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Licha ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi Zanzibar kuhifadhi ikolojia ya bahari kupitia usimamizi endelevu wa rasilimali zake, mabadiliko ya tabianchi yanaendelea kuwa tishio kubwa kwa mazingira hayo na ustawi wa jamii zinazoyategemea. Makamu wa Pili wa Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, amesema athari za mabadiliko ya tabianchi zinahatarisha mafanikio ya uchumi wa buluu kutokana na kuongezeka kwa kina cha bahari, kupauka kwa miamba ya matumbawe, dhoruba kali pamoja na kupungua kwa samaki baharini. Kulinda ikolojia ya Zanzibar ni hatua muhimu katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na kujenga uchumi wa buluu wenye tija. Picha kutoka mtandaoni. Aliyasema hayo katika Warsha ya 29 ya Mwaka ya Utafiti iliyoandaliwa na Taasisi ya Utafiti na Kupunguza Umasikini [REPOA], iliyowaweka pamoja serikali za Tanzania bara na Zanzibar pamoja na wadau wa bahari kujadili namna ya kuimarisha ikolojia hiyo. Abdulla alisema Zanzibar imekuwa kivutio kikubwa cha utalii duniani kutokana na utajiri wa ikolojia yake ya bahari, utamaduni wa watu wake na mazingira ya amani na utulivu lakini ongezeko la joto duniani linaendelea kuathiri mifumo ya bahari inayochangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa Zanzibar kupitia utalii, uvuvi na shughuli nyingine za kiuchumi zinazotegemea bahari. Nini kifanyike Makamu wa Pili wa Rais alishauri kujengwa kwa miundombinu himilivu  na mifumo madhubuti ya tahadhari ya mapema ili kulinda ikolojia ya bahari na maisha ya wananchi. Alishauri kuwepo ushirikiano kati ya taasisi za mafunzo ya uvuvi na bahari pamoja na vyuo vikuu katika kuendeleza uchumi wa buluu kwa muda mrefu, sambamba na kuingiza elimu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/09/mabadiliko-ya-tabianchi-yatishia-ikolojia-ya-bahari-zanzibar/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 20:21:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05201200/Screenshot-2026-06-05-231142-768x490.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1791</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Mikoko, Nishati, Siasa za Nishati, Uchafuzi, na  Uchafuzi wa Maji]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Ripoti: Njia za meli kubwa za kusafirisha gesi nchini Tanzania zitapita katika maeneo nyeti kiikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Serikali ya Tanzania ikijiandaa kutia saini makubaliano ya mwisho kabla ya kusainiwa kwa makubaliano ya mwisho wa mradi wa kuchakata na kusafirisha gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG), ripoti mpya iliyotolewa na mashirika zaidi ya kumi imeweka wazi athari mbalimbali zinazoweza kusababishwa na upanuzi wa miradi ya mafuta na gesi katika maeneo ya pwani na baharini. Ripoti hiyo inayojulikana kama “Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk” pamoja na mambo mengine, inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa sakafu ya bahari (deep-sea mining) pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Ripoti hiyo ilitolewa Juni 4, 2026 na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia, ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya maadhimisho ya Siku ya Bahari Duniani inayoadhimishwa Juni 8. Ripoti iliandaliwa kutokana na utafiti uliohusisha nchi 11 kutoka sehemu mbalimbali duniani ikiwemo Tanzania. Katika utafiti huo, Tanzania imetajwa kuwa miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Nchi nyingine zilizotajwa ni Kenya, Australia, Cameroon, Indonesia, Jamaica, Norway, Trinidad na Tobago, Argentina na Mexico. Kwa Tanzania, mradi huo unapangwa kujengwa katika eneo la Likong’o, kusini mwa mkoa wa Lindi. Lengo ni kuchakata gesi asilia inayopatikana baharini na kuibadilisha kuwa gesi asilia iliyoyeyushwa (LNG) kwa ajili ya kuuzwa katika masoko ya kimataifa. Ripoti hiyo imetolewa siku chache baada ya Waziri wa Nishati, Dkt Deogratius Ndejembi, kuliambia Bunge kwamba makubaliano ya kibiashara na kodi kati ya serikali na wawekezaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/ripoti-njia-za-meli-kubwa-za-kusafirisha-gesi-nchini-tanzania-zitapita-katika-maeneo-nyeti-kiikolojia-na-kibaiolojia/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/#respond</comments>
					<pubDate>05 Juni 2026 15:09:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hellen Nachilongo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/05125337/Baadhi-ya-wavuvi-katika-eneo-la-Kigambani-wakipakia-chakula-yakiwemo-mafuta-ya-kula-na-mahindi-tayari-kwenda-Mafia-kuvua-samaki.-Picha-na-Hellen-Nachilongo.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1784</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maudhui ya mazingira yanayoonyesha mabadiliko chanya, Mazingira, Maziwa, Sera za Mazingira, na  Sheria ya Mazingira]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaadhimisha Siku ya Mazingira Duniani, huku uchafuzi wa Bahari ya Hindi ukizidi kuongezeka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati dunia ikiadhimisha Siku ya Mazingira Duniani tarehe 5 Juni mwaka huu kwa msisitizo wa kuchukua hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi, Tanzania inaungana na mataifa mengine kuadhimisha siku hiyo huku ikikabiliwa na changamoto kubwa ya kulinda Bahari ya Hindi inayozidi kuathiriwa na uchafuzi wa mazingira, hasa ongezeko la taka za plastiki, uvuvi usio endelevu pamoja na uharibifu wa mifumo ya ikolojia ya pwani. Hali ikoje? Remy Lema, Meneja wa Kiufundi wa mradi wa ‘Pamoja Tuhifadhi Bahari Yetu’ kutoka International Union for Conservation of Nature (IUCN), anasema sehemu kubwa ya uchafuzi wa bahari inatokana na taka ngumu. Anasema kuwa kwa sasa zaidi ya asilimia 80 ya uchafuzi unaopatikana baharini unatokana na taka ngumu, huku asilimia 10 hadi 12 ikihusishwa na vimiminika mbalimbali, yakiwemo mafuta, kemikali na taka nyingine za majimaji zinazomwagika kwenye mazingira ya bahari. “Bila hatua za haraka za kulinda bahari, Tanzania inaweza kupoteza moja ya rasilimali zake muhimu zaidi za kiikolojia na kiuchumi katika miaka ijayo,” anasema Lema. Uchafuzi wa bahari umegeuka kilio kwa wavuvi. Salum Khamis, anayefanyia kazi zake za uvuvi katika maeneo ya Kunduchi amelalamikia kuongezeka kwa uchafuzi wa bahari, akisema hali hiyo imeanza kuathiri shughuli zao za kila siku na kupunguza kipato kinachotegemea uvuvi. “Kwa sasa plastiki nyingi zinaelea baharini na nyingine huzama. Samaki wanakufa au kuhama maeneo haya…hii inaathiri sana kiasi cha samaki kinachopatikana,” anasema. Mvuvi mwingine kutoka eneo la Feri, Juma Said, anasema mara nyingi nyavu zao hunasa takataka badala ya samaki, jambo linalowaongezea gharama za matengenezo ya vifaa. “Zamani tulikuwa tukipata&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/05/tanzania-yaadhimisha-siku-ya-mazingira-duniani-huku-uchafuzi-wa-bahari-ya-hindi-ukizidi-kuongezeka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/#respond</comments>
					<pubDate>04 Juni 2026 12:55:05 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/04131449/Screenshot-2026-06-04-161427.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1773</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Bahari ya Hindi, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Gesi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuta, Mafuta ya Kisukuku, Maji, Mazingira, Mgogoro wa Mazingira ya Baharini, Miamba ya Matumbawe, Mifumo Ikolojia ya Pwani, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Utafiti, Utawala, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Utafiti: Mifumo nyeti ya bahari ya Kenya imo ndani ya maeneo yaliyopangiwa miradi ya mafuta na gesi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ripoti mpya imebainisha kuwa asilimia 100 ya miamba ya matumbawe, misitu ya mikoko, maeneo ya hifadhi za baharini pamoja na maeneo muhimu ya bayoanuwai katika ukanda wa pwani ya Kenya yamo ndani ya maeneo yaliyotengwa kwa shughuli za utafutaji wa mafuta na gesi. Maeneo hayo pia ni sehemu za bahari ambazo ni muhimu kiikolojia na kibayolojia. Ripoti hiyo iliyopewa jina la Fossil Fuel Threats to the Ocean: Marine Life and Coastal Communities at Risk ilitolewa leo, siku chache kabla ya mkutano wa 11 unaohusu masuala ya bahari, mkutano wa ‘Our Ocean Conference’ unaotarajiwa kufanyika kuanzia Juni 16 hadi 18 mjini Mombasa, Kenya. Ripoti hiyo inaeleza kuwa upanuzi wa shughuli za mafuta na gesi baharini unaweza kusababisha madhara makubwa yatokanayo na uchimbaji wa visima, umwagikaji wa mafuta, uchimbaji wa kina cha bahari pamoja na kuongezeka kwa shughuli za usafirishaji wa meli. Bonde la Lamu limetajwa kuwa eneo linalopewa kipaumbele, ambapo miradi minane ya mafuta inayotarajiwa kuanza baadaye mwaka huu, imepangwa kutekelezwa katika ukanda huo wa pwani wenye historia na utajiri mkubwa wa kiikolojia. “Uchambuzi wetu unaonesha kuwa asilimia 100 ya Miamba ya matumbawe na misitu ya mikoko katika eneo hili imefunikwa na vitalu vya mafuta na gesi. Kwa asilimia 100, maeneo haya ni ya hifadhi za baharini na pwani lakini pia ni muhimu kwa bayoanuwai,” ripoti hiyo imeeleza. Katika ripoti hiyo, Kenya imetajwa kuwa ni miongoni mwa nchi ambazo zinaendelea kuhamasisha uwekezaji mkubwa katika sekta ya mafuta na gesi. Ripoti hiyo ilitolewa na shirika la Earth Insight kwa ushirikiano na mashirika 12 ya kiraia,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/04/ripoti-mpya-yafichua-miradi-ya-mafuta-baharini-kenya-ni-hatari-kwa-mifumo-muhimu-ya-ikolojia-ya-pwani/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 15:48:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Benjamin Jumbe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03150618/Screenshot-2026-06-03-180555-768x498.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1759</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Tembo, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Tembo warudi upande wa Uganda wa Mlima Elgon baada ya zaidi ya miongo minne</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kulingana na taarifa zilizopatikana kupitia kola za kufuatilia na Wakfu wa Mlima Elgon (MEF), mwaka jana tembo wasiopungua 60 walivuka kutoka Kenya hadi upande wa Uganda wa Mlima Elgon, mlima mkubwa wa volkeno ulioko mpakani mwa Uganda na Kenya, na kurudi kwenye sehemu ya asili yao ambapo hawajaonekana kwa zaidi ya miaka 40. MEF hufadhili miradi ya jamii inayolenga kupunguza uharibifu wa misitu na kuongeza ufahamu wa masuala ya mazingira, pamoja na timu ya maskauti wa jamii 18 katika upande wa Kenya wa mlima, sehemu ya Mradi wa Tembo wa Mlima Elgon unaotekelezwa na Shirika la Wanyamapori la Afrika Mashariki. Mwenyekiti wa wakfu wa MEF, Chris Powles, aliiambia Mongabay kwamba mnamo mwaka 2022, maskauti walifuatilia tembo wanne wakivuka mto Suam, ambao unaashiria mpaka kati ya nchi hizo mbili. Picha za video zilizorekodiwa kwa ndege isiyo na rubani zikionyesha tembo upande wa Uganda wa Mlima Elgon. Picha kwa hisani ya UWA. Katika mahojiano kupitia barua pepe, Powles alisema sababu kadhaa zinaweza kuelezea kurudi kwa tembo, ingawa haiwezekani kusema kwa uhakika ni nini kiliwachochea kurejea katika eneo hilo. &#8220;[Hizi] ni pamoja na ongezeko la idadi ya tembo upande wa Kenya, kuongezeka kwa shinikizo la binadamu kwa upande wa Kenya, usalama wanaoupata wakiwa upande wa Uganda, ambako eneo hilo lote liko ndani ya mbuga ya taifa, tofauti na upande wa Kenya,&#8221; aliandika. &#8220;Na, labda, tembo walio hai tangu wakati wengine wao waliuawa nchini Uganda sasa wamekufa kawaida na hivyo huenda kumbukumbu ya hatari zilizowakabili nchini Uganda imefifia kadri vizazi vilivyobadilika.&#8221; Mwishoni mwa miaka ya 1970 na mwanzoni mwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/tembo-warudi-upande-wa-uganda-wa-mlima-elgon-baada-ya-zaidi-ya-miongo-minne/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 12:56:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Penzi Nyamungumi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03130042/Screenshot-2026-06-03-160011.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1754</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chembechembe ndogo za plastiki, Elimu ya Mazingira, Mazingira, Plastiki, Sheria ya Mazingira, na  Uchafuzi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Biashara ya chupa za plastiki yaleta mageuzi katika juhudi za uhifadhi wa mazingira mijini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR ES SALAAM, Tanzania &#8211; Kushamiri kwa biashara ya uokotaji wa taka hasa chupa za plastiki katika maeneo ya mijini, huenda kuleta mageuzi katika kushughulikia changamoto za mazingira katika miji mikubwa likiwemo la Dar es Salaam. Kwa muda mrefu, chupa za plastiki zimekuwa zikitajwa kuwa chanzo kikubwa cha uchafuzi wa mazingira mijini. Zile ambazo hutupwa kwenye mifereji zimekuwa zikiziba njia za maji na kuchangia mafuriko. Aidha, chupa zinapochomwa, moshi wake husababisha maradhi na pia kuathiri mazingira kutokana na asili yake ya kuchelewa kuoza. Hata hivyo, kuibuka na kukua kwa biashara ya chupa za plastiki zilizotumika, ambayo mara nyingi hufanywa na akinamama na vijana, kunaendelea kubadilisha historia. Hivi sasa badala ya kushuhudia barabara zenye mifereji iliyojaa chupa tupu, kinachoonekana ni akinamama na vijana waliobeba viroba vikubwa vyenye chupa hizo. Wakusanyaji wadogo huuza chupa hizo kwa wakusanyaji wakubwa au kwa kampuni zinazojishughulisha na ukusanyaji na urejelezaji wa chupa hizo baada ya matumizi. Taimuru Hamad, Meneja Uzingatiaji Sheria kutoka Baraza la Taifa la Usimamizi na Uhifadhi wa Mazingira (NEMC), anakiri kwamba biashara hiyo imeleta faida kubwa katika ustawi na ulinzi wa mazingira. Chupa za plastiki zilizokusanywa kutoka maeneo mbalimbali Jijini Dar es Salaam zikiwa zimefungwa kwenye mifuko mikubwa kwa ajili ya kupelekwa kwa wanunuzi. Picha na Joyce Bazira. “Kuokotwa kwa hizi chupa kunasaidia sana. Kwanza, kunasaidia katika suala zima la ustawi wa mazingira, lakini pia kwenye suala la usafi. Kama zingekuwa haziokotwi, mazingira yangeendelea kuathirika sana na pia yangekuwa machafu sana,” alisema Taimuru katika mahojiano na Mongabay. Chupa za rangi Pamoja na kazi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/biashara-ya-chupa-za-plastiki-yaleta-mageuzi-katika-juhudi-za-uhifadhi-wa-mazingira-mijini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/#respond</comments>
					<pubDate>03 Juni 2026 10:41:59 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Naina Rao]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/03103608/Screenshot-2026-06-03-132733-768x475.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1749</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Amerika ya Kaskazini, Marekani, na  Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Halijoto, Kudhibiti Ongezeko la Joto Duniani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Ongezeko la Joto Duniani, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Hatua za FIFA kukabiliana na joto katika Kombe la Dunia huenda zisitoshe, mtaalamu anaonya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hatua zinazopendekezwa na waandaaji wa Kombe la Dunia lijalo la FIFA hazitatosha kuwalinda wachezaji na mashabiki dhidi ya hatari ya joto kali na unyevunyevu unaotarajiwa katika mashindano ya mwaka huu, mtaalamu wa matibabu anaonya. Mnamo Desemba mwaka 2025, FIFA ilitangaza kuwa kutakuwa na mapumziko ya dakika tatu kwa ajili ya kunywa maji kwa wachezaji katika kila nusu ya kila mchezo &#8220;ili kuhakikisha hali bora zaidi kwa wachezaji&#8221;. Hata hivyo, uchambuzi wa hivi majuzi unasema Kombe la Dunia la 2026, lililoandaliwa kwa pamoja na Marekani, Meksiko na Kanada, litakuwa na joto kali zaidi kuliko mashindano ya Marekani ya &#8217;94. Wanasayansi kutoka World Weather Attribution (WWA), mtandao wa kimataifa wa watafiti wanaochunguza mchango wa mabadiliko ya tabianchi katika matukio ya hali mbaya ya hewa, wanaonya kuwa mabadiliko ya tabianchi yameongeza karibu mara mbili uwezekano wa joto kali tangu wakati huo. Hiyo inafanya iwe vigumu zaidi kuondoa joto mwilini, alisema Chris Mullington, mshauri wa kutia ganzi na mhadhiri mkuu wa kliniki katika Imperial College London. &#8220;Hiyo ni muhimu kwa sababu wanasoka huzalisha kiasi kikubwa cha joto mwilini wanapokimbia mara kwa mara, kuongeza kasi na kucheza kwa kiwango cha juu cha ushindani,&#8221; alisema katika mkutano na waandishi wa habari. &#8220;WBGT inapoongezeka, mifumo ya kawaida ya kupoeza ya mwili inakuwa dhaifu.&#8221; WBGT ni kipimo cha joto kinachojumuisha halijoto ya hewa, unyevunyevu, mionzi ya jua na kasi ya upepo, na hutoa &#8220;hisia halisi&#8221; ya joto kwenye mwili wa mwanadamu. Mullington alisema viwango vya juu vya WBGT vinaweza kulazimisha wachezaji &#8220;kupunguza kasi ya kukimbia mara kwa mara, kujiendesha kwa uangalifu&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/03/hatua-za-fifa-kukabiliana-na-joto-katika-kombe-la-dunia-huenda-zisitoshe-mtaalamu-anaonya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, akili bandia inaweza kubadilisha miradi ya kaboni barani Afrika? </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/#respond</comments>
					<pubDate>02 Juni 2026 09:54:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David Njagi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/06/02094948/Screenshot-2026-06-02-124936-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1742</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kaboni, Fedha za Kaboni, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kaboni, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Mikopo ya Kaboni, Siasa za Mazingira, Soko ya Kaboni, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Naito Leshao alionyesha hisia za kuchoshwa na miradi ya biashara ya fidia ya hewa ukaa katika mkutano wa kimataifa uitwao Global Landscapes Forum (GLF) wa mwaka 2026 uliofanyika Nairobi, Kenya. Akiwa na hisia kali, Leshao aliuliza maswali kadhaa: kwa nini miradi mikubwa ya kaboni inayodaiwa kuwa kwa ajili ya watu waliolinda ardhi kwa miaka mingi hupitia mikononi mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Je, akili bandia inaweza kubadilisha miradi ya kaboni barani Afrika? </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Naito Leshao alionyesha hisia za kuchoshwa na miradi ya biashara ya fidia ya hewa ukaa katika mkutano wa kimataifa uitwao Global Landscapes Forum (GLF) wa mwaka 2026 uliofanyika Nairobi, Kenya. Akiwa na hisia kali, Leshao aliuliza maswali kadhaa: kwa nini miradi mikubwa ya kaboni inayodaiwa kuwa kwa ajili ya watu waliolinda ardhi kwa miaka mingi hupitia mikononi mwa watu wengi kiasi kwamba malipo yanapowafikia wanajamii, wanapata kiasi kidogo sana? Leshao, aliyekuwa akiwakilisha jamii yake kutoka Maasai Mara, aliendelea kwa swali jingine: Je, mnatarajia jamii za kiasili ziendelee kuhifadhi ardhi huku zikilinda mifumo yao ya malisho, wakati matatizo yao hayasikilizwi kuhusu namna mabadiliko ya tabianchi yanavyowaathiri? Maswali tata Maswali yake si mapya katika mijadala ya uhifadhi wa mazingira. Yameendelea kujitokeza tangu Mkataba wa Paris ulipoweka msingi wa ushirikiano wa kimataifa katika biashara ya kaboni kupitia Kifungu cha 6 kama njia ya kupambana na ongezeko la joto duniani huku ukiwa na lengo la kupambana na ongezeko la joto duniani na kuzalisha mapato. Hata hivyo, vigezo vya mfumo huo mara nyingi vimekuwa vikionekana kuwa vya upendeleo, vikiegemea zaidi kwa waendelezaji wa miradi katika mnyororo wa biashara ya kaboni. “Wanakuja na asilimia fulani, lakini nani anaamua hizo asilimia? Nani anasema kwamba jamii hii inapaswa kupata asilimia 10 au 15? Unajuaje kwamba hicho ndicho kiasi kinachokidhi uendeshaji wa jamii hii? Pamoja na kukosekana kwa usawa katika mchakato huu, bado dunia inazihitaji jamii za kiasili kuhifadhi mazingira,” alisema Leshao. Hakukuwa na majibu ya haraka kwa maswali yake, licha ya makadirio mapya kuonyesha kwamba mapato yanayotokana na soko la kimataifa la&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/06/02/je-akili-bandia-inaweza-kubadilisha-miradi-ya-kaboni-barani-afrika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mei 2026 21:58:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/31214131/Atuwa-akiwa-amezamia-bahari-kwenye-kazi-ya-kurekebisha-matumbawe-kwenye-bahari-ya-kisiwa-cha-Mnemba-Zanzibar.jpeg-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1733</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Barafu ya bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Miamba ya Matumbawe, Samaki, Samaki wa Maji Chumvi, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Upaukaji wa Matumbawe, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Atuwa, mwanamke pekee Zanzibar anayezamia ili kurejesha miamba ya matumbawe iliyoharibika</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Zaidi ya futi 40 (takriban mita 12.2) chini ya Bahari ya Hindi, karibu na Kisiwa cha Mnemba kilichopo Zanzibar, Atuwa Omari na wahifadhi wengine huzama hadi kwenye sakafu ya bahari kwa lengo la kushiriki katika urejeshaji wa miamba ya matumbawe iliyoharibika. Anapokuwa katika eneo hilo, mawimbi humsukuma huku makundi ya samaki yenye rangi mbalimbali kama vile wa bluu, njano na kijani hupita juu ya kichwa chake huku mwanga wa jua ukionekana kwa mbali ndani ya maji. Juu ya uso wa bahari, watalii huwa wanazunguka katika maji bila kufahamu kuhusu mfumo dhaifu wa ikolojia unaopambana kuendelea kuishi chini yake. Kwa mujibu wa waajiri wake, Atuwa, mwenye umri wa miaka 23, anaelezwa kuwa mwanamke pekee Zanzibar anayeshiriki kazi hiyo ya uzamiaji wa urejeshaji wa matumbawe. Mamlaka za Zanzibar zinaeleza kuwa miaka mitatu iliyopita, eneo la Mnemba ambako Atuwa hufanya kazi, ambalo lina baadhi ya miamba muhimu ya matumbawe ya Zanzibar, liliharibika. Makame Omar Makame, Mkurugenzi wa Idara ya Uhifadhi Baharini Zanzibar, anasema eneo hilo la Mnemba liliathiriwa na shughuli za kibinadamu zilizokithiri. “Kulikuwa na shughuli nyingi za uvuvi zisizofuata utaratibu, msongamano wa watalii, ambapo takribani boti 200 zenye watalii zilikuwa zikiingia katika eneo la mita 200 za ukanda wa pwani kila siku,” Makame aliieleza Mongabay. Kwa mujibu wa mkurugenzi huyo, ili kulinda mazingira, Serikali ya Zanzibar iliamua kupunguza idadi ya wageni hadi 80 kwa siku na kuongeza ada ya uhifadhi kutoka $3 hadi $25 kwa mtalii mmoja, kusitisha kwa muda shughuli za uvuvi na pia kutoa elimu kwa jamii. Hilo lilikuwa jambo muhimu kwa Atuwa na wenzake ambao wanaamini jamii zao zilihitaji mazingira&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/31/atuwa-mwanamke-pekee-zanzibar-anayezamia-ili-kurejesha-miamba-ya-matumbawe-iliyoharibika/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kesi ya kukutwa na nyara za tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yatajwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/28/kesi-ya-kukutwa-na-nyara-za-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yatajwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/28/kesi-ya-kukutwa-na-nyara-za-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yatajwa/#respond</comments>
					<pubDate>28 Mei 2026 15:30:47 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Tumaini Mgeni]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/28152908/Tembo-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1727</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Biashara ya Pembe za Ndovu, Biashara ya Wanyamapori, Pembe za Ndovu, Sheria ya Mazingira, Tembo, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37), anayekabiliwa na mashtaka ya kukutwa akimiliki nyara za serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni anaendelea kusota rumande kufuatia upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika. Kesi hiyo imetajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam. Hata hivyo mshtakiwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/28/kesi-ya-kukutwa-na-nyara-za-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yatajwa/" data-wpel-link="internal">Kesi ya kukutwa na nyara za tembo dhidi ya raia wa Korea Kaskazini yatajwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Raia wa Korea Kaskazini Un Hyok Ra (37), anayekabiliwa na mashtaka ya kukutwa akimiliki nyara za serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6.4 bilioni anaendelea kusota rumande kufuatia upelelezi wa kesi hiyo kutokamilika. Kesi hiyo imetajwa leo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam. Hata hivyo mshtakiwa hakuwepo mahakamani. Un Hyok Ra anakabiliwa na mashtaka mawili: kukutwa akimiliki nyara za serikali na kujihusisha na biashara hiyo. Akiwakilisha upande wa Mashtaka, Wakili wa Serikali Mwandamizi, Florida Wancelaus amemwambia Hakimu Mkazi Mkuu Salome Mshasha anayesikiliza kesi hiyo kuwa upelelezi bado haujakamilika na akaomba shauri lipangiwe tarehe nyingine ya kutajwa. Hakimu Mshasha baada ya kusikiliza hoja za upande wa Mashtaka, aliamuru hati ya kumfikisha mshtakiwa mahakamani itolewe ili kesi itakapotajwa Juni 9, 2026, mshtakiwa aletwe kortini. Awali, ilidaiwa katika hati ya mashtaka kuwa Ra, ambaye ni mkazi wa Mikocheni, Dar es Salaam, Aprili 19, 2026, katika eneo la Hoteli ya Golden Tulip, Masaki, Wilaya ya Kinondoni, Mkoa wa Dar es Salaam, alikutwa akimiliki nyara za serikali ambazo ni vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6,476,534,750 ($2,481,433) mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bila kuwa na kibali wala leseni kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyamapori. Katika shtaka la pili, Ra anatuhumiwa kuwa tarehe hiyo na mahali hapo, alijihusisha na biashara haramu ya nyara za serikali kwa kuuza vipande 504 vya meno ya tembo vyenye thamani ya TSh6,476,534,750 ($2,481,433) mali ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, bila kuwa na kibali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/28/kesi-ya-kukutwa-na-nyara-za-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yatajwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/28/kesi-ya-kukutwa-na-nyara-za-tembo-dhidi-ya-raia-wa-korea-kaskazini-yatajwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mei 2026 17:35:57 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/26172956/Usenge-Beach-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1717</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kenya, Tanzania, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maji, Mazingira, Maziwa, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Nishati safi, Nishati ya Jua, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, upatikanaji wa chakula, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">NuPEA yaweka wazi msimamo wake kufuatia maandamano dhidi ya mradi wa nyuklia Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA) ya Kenya imetangaza mipango ya kufanya kampeni mpya za wazi, madhubuti na za ngazi mbalimbali za uelimishaji wa umma ili kutafuta muafaka juu ya wasiwasi uliopo kuhusu usalama wa nishati ya nyuklia, haki za ardhi, na maisha ya wananchi kabla ya kuanza kwa ujenzi wa mradi wa nishati ya nyuklia wenye thamani ya shilingi bilioni 500 za Kenya katika kaunti ya Siaya. “Kama wakala wa nishati ya nyuklia, tunasikia na kuheshimu sauti za wakazi wa Siaya. Ushiriki wa umma si jambo la kufuata taratibu tu. Ni haki ya kikatiba,” shirika hilo lilisema katika taarifa yake. Taarifa hiyo ilitolewa siku mbili baada ya wakazi wa Sakwa, Bondo katika Kaunti ya Siaya inayopakana na Ziwa Victoria, kuandamana kupinga mradi huo. Wakazi hao walieleza hofu kuhusu hatari za kimazingira iwapo ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika na lenye utajiri mkubwa wa ikolojia litachafuliwa. Pia walitaja hofu ya kupoteza riziki, chakula na mahitaji mengine muhimu. Katika taarifa yake ya kujibu maandamano hayo, iliyotiwa saini na Afisa Mkuu Mtendaji wa NuPEA, Justus Wabuyabom, shirika hilo lilisema kuwa ujenzi wa mradi huo hautaanza hadi wakazi wa Siaya waelimishwe kikamilifu na wakubaliane na mradi huo. NuPEA kubadili mkakati NuPEA iliongeza kuwa itabadilisha mkakati wake “kutoka mipango ya kitaasisi ya ngazi za juu kwenda katika uhamasishaji wa kina kwa wananchi wa vijijini” kuhusu mradi huo unaotarajiwa kuzalisha megawati 2,000. Wakati huohuo, Power Shift Africa (PSA) imekosoa msisitizo wa kutumia nishati ya nyuklia kama chanzo cha umeme, ikisema kuwa hatua hiyo inaweza&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/26/nupea-yajibu-maandamano-kupinga-ujenzi-wa-mtambo-wa-nyuklia-yaahidi-majadiliano-zaidi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Katika ikolojia tete, mwanamme mmoja aendeleza juhudi za kuleta mshikamano kati ya binadamu na nyoka</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/katika-ikolojia-tete-mwanamme-mmoja-aendeleza-juhudi-za-kuleta-mshikamano-kati-ya-binadamu-na-nyoka-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/katika-ikolojia-tete-mwanamme-mmoja-aendeleza-juhudi-za-kuleta-mshikamano-kati-ya-binadamu-na-nyoka-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>25 Mei 2026 14:00:30 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Linah Mwamachi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/25123328/Black-Mamba-Snake-2-Courtesy-Inncocent-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1687</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Misitu, Nyoka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kama wanajamii wengine katika vijiji vya milima ya Taita, John Maghanga, maarufu kama John wa Nyoka, aliwaogopa nyoka akiamini kuwa wanapaswa kuuawa pindi wanapoonekana. Mwaka 2019, akiwa katika ziara zake msituni katika milima ya Taita, Maghanga alimgusa nyoka kwa mikono yake kimakosa. Alijawa na hofu akijiuliza: “Kama angeniuma ingekuwaje?” Kabla ya nyoka huyo kuteleza na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/katika-ikolojia-tete-mwanamme-mmoja-aendeleza-juhudi-za-kuleta-mshikamano-kati-ya-binadamu-na-nyoka-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Katika ikolojia tete, mwanamme mmoja aendeleza juhudi za kuleta mshikamano kati ya binadamu na nyoka</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kama wanajamii wengine katika vijiji vya milima ya Taita, John Maghanga, maarufu kama John wa Nyoka, aliwaogopa nyoka akiamini kuwa wanapaswa kuuawa pindi wanapoonekana. Mwaka 2019, akiwa katika ziara zake msituni katika milima ya Taita, Maghanga alimgusa nyoka kwa mikono yake kimakosa. Alijawa na hofu akijiuliza: “Kama angeniuma ingekuwaje?” Kabla ya nyoka huyo kuteleza na kupotelea mitini, Maghanga alichukua simu na kupiga picha yake, aliyochapisha kwenye Facebook. Lengo lake lilikuwa kufahamu mengi kuhusu nyoka huyo. Alistaajabu kugundua kuwa nyoka huyo alikuwa mwenye sumu kali. Mongabay ilimtembelea Maghanga na kumpata akiwa ametoka kuhamasisha wanajamii kuhusu nyoka na jinsi ya kuishi nao kwa amani. Alielezea jinsi tukio hilo lilibadili mienendo yake: “Baada ya tukio hilo, uoga wangu kwa nyoka ulianza kufifia, na polepole nikataka kufahamu zaidi kuwahusu. Sasa mimi ni mshauri na mtaalamu wa kukamata nyoka na kuwahamisha sehemu salama.” John Maghanga akimtoa nyoka aliyekuwa ameingia kwa nyumba ya mkaazi wa Taita Taveta. Picha na Linah Mwamachi. Katika vijiji vilivyo milimani na tambarare zinazopakana na mbuga za wanyama za Tsavo Mashariki na Tsavo Magharibi, kusini mashariki mwa Kenya, wengi wamepoteza maisha kwa kukosa huduma muhimu kwa upesi na wengine kuachwa na makovu ya ulemavu. Migogoro kati ya binadamu na nyoka mara nyingi hutokea katika msimu wa mvua, wanyama hao wanapotoroka hifadhi zao na kutangamana na binadamu. Katika maeneo yaliyopakana na mbuga za wanyamapori za Tsavo Mashariki na Tsavo Magharibi, binadamu pia huwaua nyoka kiholela, kutokana na uoga wa kuumwa, japo si nyoka wote ni hatari. Kupitia shirika la Snake Community Action Now (SCAN) Maghanga sasa anahamasisha umma jinsi ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/katika-ikolojia-tete-mwanamme-mmoja-aendeleza-juhudi-za-kuleta-mshikamano-kati-ya-binadamu-na-nyoka-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/katika-ikolojia-tete-mwanamme-mmoja-aendeleza-juhudi-za-kuleta-mshikamano-kati-ya-binadamu-na-nyoka-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania kuandaa mwongozo wa kuhakikisha shughuli za uvuvi na ufugaji haziathiri mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/serikali-kuandaa-mwongozo-wa-kuhakikisha-shughuli-za-uvuvi-na-ufugaji-haziathiri-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/serikali-kuandaa-mwongozo-wa-kuhakikisha-shughuli-za-uvuvi-na-ufugaji-haziathiri-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>25 Mei 2026 13:35:19 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/25133402/Screenshot-2026-05-25-163250.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1712</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Haki za Kimazingira, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Uhifadhi, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ili kuhakikisha shughuli zinazofanywa na sekta ya mifugo na uvuvi zinazingatia uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali, serikali ya Tanzania imepanga kuandaa mwongozo utakaoweka mikakati ya uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Bashiru Ally, amesema mpango huo wa kwanza wa usimamizi wa mazingira utakaotekelezwa kwa miaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/serikali-kuandaa-mwongozo-wa-kuhakikisha-shughuli-za-uvuvi-na-ufugaji-haziathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Tanzania kuandaa mwongozo wa kuhakikisha shughuli za uvuvi na ufugaji haziathiri mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ili kuhakikisha shughuli zinazofanywa na sekta ya mifugo na uvuvi zinazingatia uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali, serikali ya Tanzania imepanga kuandaa mwongozo utakaoweka mikakati ya uhifadhi wa mazingira na matumizi endelevu ya rasilimali. Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Balozi Bashiru Ally, amesema mpango huo wa kwanza wa usimamizi wa mazingira utakaotekelezwa kwa miaka mitano kuanzia mwaka 2027/2028 hadi 2032/2033, pia utatoa miongozo kuhusu matumizi endelevu ya rasilimali na namna ya kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Akiwasilisha hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2026/2027 ya wizara yake, akiwa katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika makao makuu ya nchi, Dodoma, Bashiru alisema katika kipindi cha mwaka 2026/2027, Wizara ya Mifugo na Uvuvi pia imepanga kufanya tathmini ya athari za mazingira katika miradi ya ujenzi wa minada ya mifugo, mialo na masoko ya samaki. Kwa mujibu wa Bashiru, mpango mwingine utakaofanywa na wizara yake katika kipindi cha mwaka wa fedha 2026/2027 ni kutoa elimu kwa wafugaji na wavuvi 1,000 katika ukanda wa pwani, kaskazini na nyanda za juu kusini kuhusu utunzaji wa mazingira kwa uvuvi na ufugaji unaostahimili mabadiliko ya tabianchi. “Vilevile, Wizara itaendelea kufanya tathmini ya athari za mabadiliko ya tabianchi na kuandaa mpango wa kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi kwa ukanda wa pwani,” alisema Bashiru. Alisema katika mwaka 2026/2027, wizara yake itafanya ukaguzi wa mazingira kwa miradi 10 ya uwekezaji katika sekta za mifugo na uvuvi ili kuhakikisha uzingatiaji wa sheria, kanuni na miongozo ya usimamizi wa mazingira. Pia, wizara hiyo itaendelea na utekelezaji wa Mkakati wa Kitaifa wa Matumizi ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/serikali-kuandaa-mwongozo-wa-kuhakikisha-shughuli-za-uvuvi-na-ufugaji-haziathiri-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/25/serikali-kuandaa-mwongozo-wa-kuhakikisha-shughuli-za-uvuvi-na-ufugaji-haziathiri-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>23 Mei 2026 21:35:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/23214326/Screenshot-2026-05-24-004210-768x468.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1696</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maji, Mazingira, Maziwa, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uhifadhi, na  Umeme]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jamii za Kenya zapinga mpango wa ujenzi wa kinu cha nyuklia karibu na Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Mei 21, wakazi wa Sakwa Kusini Mashariki mwa Kenya, walikusanyika kupinga mpango wa Serikali wa kujenga kinu cha kuzalisha umeme wa nyuklia karibu na makazi yao, kandokando ya Ziwa Victoria. Sakwa, iliyopo katika kaunti ya Siaya, ni makazi ya jamii ya Waluo na iko kwenye mwambao wa ziwa hilo kubwa zaidi lenye maji safi barani Afrika, ambalo linapatikana Kenya, Uganda na Tanzania. Mwisho wa Machi 2026, wakati wa kongamano la kimataifa kuhusu nishati ya nyuklia, Rais wa Kenya William Ruto alitangaza ujenzi wa kinu cha nyuklia chenye uwezo wa kuzalisha megawati 2,000 katika eneo hilo. Kwa sasa hakuna taarifa rasmi kuhusu mpango huo kwenye tovuti ya Nuclear Power and Energy Agency (NuPEA). Hata hivyo, Ruto alisema ujenzi utaanza mwaka ujao na kinu hicho kinatarajiwa kuanza kuzalisha umeme mwaka 2034. “Hakuna nchi yoyote duniani iliyowahi kufanikisha malengo yake ya maendeleo bila kuwa na nishati ya kutosha na ya kuaminika,” alisema Ruto. Pia alisisitiza kuwa nishati ya nyuklia inatambuliwa na Umoja wa Mataifa kama chanzo cha nishati chenye kiwango kidogo cha uzalishaji wa hewa ukaa na muhimu katika kufanikisha Agenda ya Maendeleo Endelevu ya 2030. “Kuunganisha nishati ya nyuklia katika gridi ya taifa ni hatua ya kimkakati ya kupata suluhisho la muda mrefu litakalokidhi ongezeko la mahitaji ya umeme nchini Kenya,” alisema. Katika hotuba yake, Ruto alifafanua kuwa tayari alikuwa ameshauriana na wakazi wa Siaya na kujiridhisha kuwa jamii za eneo hilo zinaunga mkono mradi huo. Hata hivyo, maandamano ya hivi karibuni yanaonyesha hali halisi ni tofauti. Aidha, ombi la kupinga mradi huo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/23/wakazi-wa-sakwa-wapinga-mpango-wa-kujenga-kinu-cha-nyuklia-karibu-na-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Bioanuwai hatarini: Uhamisho wa kituo cha wanyama yatima wazua wasiwasi miongoni mwa wahifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/22/bioanuwai-hatarini-uhamisho-wa-kituo-cha-wanyama-yatima-cha-nairobi-wazua-wasiwasi-miongoni-mwa-wahifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/22/bioanuwai-hatarini-uhamisho-wa-kituo-cha-wanyama-yatima-cha-nairobi-wazua-wasiwasi-miongoni-mwa-wahifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Mei 2026 03:00:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Achieng’ Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20183609/0a16e98a-b5ab-48a2-8fb8-694e881b7670-1_all_26564-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1658</guid>

					
					
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya &#8211; Huku dunia ikisherehekea Siku ya Kimataifa ya Bioanuwai, tangazo la kuhamishwa kwa kituo cha Nairobi Animal Orphanage linazua mjadala mkubwa kati ya Huduma ya Wanyamapori Kenya (Kenya Wildlife Service &#8211; KWS) na makundi ya wanaharakati wa mazingira ambao wameishutumu serikali ya Kenya kwa kutumia mamlaka yake kupita kiasi bila kuzingatia maoni ya wadau [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/22/bioanuwai-hatarini-uhamisho-wa-kituo-cha-wanyama-yatima-cha-nairobi-wazua-wasiwasi-miongoni-mwa-wahifadhi/" data-wpel-link="internal">Bioanuwai hatarini: Uhamisho wa kituo cha wanyama yatima wazua wasiwasi miongoni mwa wahifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya &#8211; Huku dunia ikisherehekea Siku ya Kimataifa ya Bioanuwai, tangazo la kuhamishwa kwa kituo cha Nairobi Animal Orphanage linazua mjadala mkubwa kati ya Huduma ya Wanyamapori Kenya (Kenya Wildlife Service &#8211; KWS) na makundi ya wanaharakati wa mazingira ambao wameishutumu serikali ya Kenya kwa kutumia mamlaka yake kupita kiasi bila kuzingatia maoni ya wadau wengine. Tayari kundi moja la utetezi nchini limewasilisha ombi mahakamani kutaka mahakama itoe amri kuizuia serikali kuhamisha Nairobi Animal Orphanage, kwa madai kuwa mpango huo ni njia ya kuficha njama za kugawa isivyo halali hekta 31 za ardhi kutoka Hifadhi ya Taifa ya Nairobi. Shauri hilo liliwasilishwa na Kituo cha Sheria pamoja na taasisi ya Just Act katika Mahakama ya Mazingira na Ardhi, na likapewa kesi nambari E019 ya 2026. Walalamikiwa katika kesi hiyo ni KWS, Shirika la Bomas la Kenya, Wizara ya Ulinzi, Mamlaka ya Taifa ya Usimamizi wa Mazingira, Tume ya Taifa ya Ardhi, na Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Walalamikaji wanaitaka mahakama kusitisha leseni ya Tathmini ya Athari kwa Mazingira (EIA) nambari NEMA/ENVIS/CPR/LIC-0940, hatua ambayo itazuia ukataji wa msitu wa asili ndani ya hifadhi hiyo, ambayo ni makazi muhimu kwa faru weusi walio katika hatari kubwa ya kutoweka. Katika hati ya kiapo iliyowasilishwa mahakamani, Kituo cha Sheria, kupitia kwa Mkurugenzi Mtendaji Wambua Kituku, ilishutumu serikali ya Kenya kwa kile ilichokiita matumizi mabaya makubwa ya fedha, pamoja na kukosekana kwa ushirikishwaji wa umma katika mpango wa kuhamisha kituo hicho cha wanyama. “Mlalamikaji mbele ya mahakama hii anatafuta kulinda wanyamapori na mazingira dhidi ya unyonyaji usio na msingi na usio endelevu, akitimiza wajibu wake&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/22/bioanuwai-hatarini-uhamisho-wa-kituo-cha-wanyama-yatima-cha-nairobi-wazua-wasiwasi-miongoni-mwa-wahifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/22/bioanuwai-hatarini-uhamisho-wa-kituo-cha-wanyama-yatima-cha-nairobi-wazua-wasiwasi-miongoni-mwa-wahifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mradi wa mazingira mashuleni warejesha miti na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/21/mradi-wa-mazingira-mashuleni-warejesha-miti-na-kujenga-ustahimilivu-wa-mabadiliko-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/21/mradi-wa-mazingira-mashuleni-warejesha-miti-na-kujenga-ustahimilivu-wa-mabadiliko-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>21 Mei 2026 16:53:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/21160452/2-Iringa-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1680</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Mimea, Misitu, Miti, Upandaji Miti, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati Tanzania ikiendelea kupoteza misitu kwa kasi kutokana na sababu mbalimbali, mradi wa kuhifadhi mazingira mashuleni umeanza kuleta mabadiliko kwa kurejesha miti iliyoanza kutoweka na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi. Takwimu za Global Forest Watch zinaonyesha kuwa Tanzania  ilipoteza hekta milioni 3.48 za uoto wa miti kati ya mwaka 2001 na 2024, kwa mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/21/mradi-wa-mazingira-mashuleni-warejesha-miti-na-kujenga-ustahimilivu-wa-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mradi wa mazingira mashuleni warejesha miti na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati Tanzania ikiendelea kupoteza misitu kwa kasi kutokana na sababu mbalimbali, mradi wa kuhifadhi mazingira mashuleni umeanza kuleta mabadiliko kwa kurejesha miti iliyoanza kutoweka na kujenga ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi. Takwimu za Global Forest Watch zinaonyesha kuwa Tanzania  ilipoteza hekta milioni 3.48 za uoto wa miti kati ya mwaka 2001 na 2024, kwa mwaka 2024 pekee, ikipoteza hekta 271,000. Sababu zinazotajwa kuchangia upotevu huo ni pamoja na shughuli za binadamu zinazochochewa na hitaji la kuni na mkaa kwa ajili ya kupikia, kupanuka kwa miji na ukataji wa miti kwa ajili ya kujengea nyumba. Chanzo kikuu ni utegemezi mkubwa wa nishati itokayo na miti ambapo zaidi ya asilimia 85 ya kaya nchini Tanzania hutegemea mkaa na kuni kwa ajili ya kupikia. Dk Elikana John, Meneja wa Misitu kutoka Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), anasema ili kuingilia kati uharibifu huo, TFS ikishirikiana na taasisi na wadau wa mazingira nchini, imekuwa ikitoa miche ya matunda na ya vivuli ili kutekeleza miradi ya kupanda miti sehemu mbalimbali ikiwemo mashuleni, hospitalini na majumbani. Mwanafunzi Charles Godfrey wa Shule ya Msingi Makweli, Kata ya Vugiri, Halmashauri ya Korogwe akipanda miti katika eneo la shule ikiwa ni utekelezaji wa mradi wa Eco-Schools. Picha na Jenifer Gilla. Katika mikoa ya Morogoro, Iringa na Tanga, baadhi ya shule za msingi na sekondari zimeanzisha utaratibu wa kurejesha miti iliyotoweka kupitia programu ya Eco-Schools ambapo wanafunzi ni washiriki wakuu katika uhifadhi wa mazingira. Programu hiyo inafadhiliwa na Shirika la uhifadhi wa misitu la Tanzania Forest Conservation Group (TFCG).&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/21/mradi-wa-mazingira-mashuleni-warejesha-miti-na-kujenga-ustahimilivu-wa-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/21/mradi-wa-mazingira-mashuleni-warejesha-miti-na-kujenga-ustahimilivu-wa-mabadiliko-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yaathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi nchini Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2026 20:07:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20200154/Picture2.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1672</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DODOMA, Tanzania &#8211; Mabadiliko ya tabianchi yametajwa kama changamoto kubwa iliyoathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026. Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi Tanzania, Abdallah Ulega, wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, mnamo Mei 20, katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika Makao [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yaathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi nchini Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DODOMA, Tanzania &#8211; Mabadiliko ya tabianchi yametajwa kama changamoto kubwa iliyoathiri utekelezaji wa majukumu ya Wizara ya Ujenzi katika kipindi cha mwaka wa fedha 2025/2026. Hayo yamesemwa na Waziri wa Ujenzi Tanzania, Abdallah Ulega, wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, mnamo Mei 20, katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika Makao Makuu ya Nchi, Dodoma. Amesema majanga yaliyosababishwa na mabadiliko ya tabianchi, kama vile mafuriko, yalisababisha uharibifu wa miundombinu ya barabara na madaraja katika maeneo mbalimbali nchini. Ili kukabiliana na hali kama hiyo, Waziri alisema wizara yake inaboresha miongozo ya usanifu na matumizi ya malighafi za ujenzi kwa kuzingatia uhimilivu wa miundombinu. Upandaji miti kando ya barabara kuu ni miongoni mwa hatua zinazochukuliwa na Serikali kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi. Picha kwa hisani ya Wizara ya Ujenzi Tanzania. “Vilevile, wizara imepanga kupanda miti 40,000 katika barabara kuu na barabara za mikoa, na kuanza maandalizi ya mpango wa kuhimili mabadiliko ya tabianchi wa Sekta ya Ujenzi,” amesema waziri. Aidha, amesema wizara itaendelea kuchukua hatua za haraka kurejesha na kujenga upya miundombinu iliyoharibiwa na mafuriko pamoja na athari nyingine za mabadiliko ya tabianchi. Gharama za uharibifu “Barabara na madaraja yaliyoathirika yatajengwa kwa viwango vinavyoweza kuhimili majanga hayo, ili kuepuka kuongeza mzigo kwa serikali kugharamia uharibifu unaojitokeza kila msimu wa mvua kubwa na kuhakikisha barabara zetu zinapitika majira yote ya mwaka hata wakati wa changamoto za hali ya hewa,” amesema Waziri. Kauli hiyo ya Waziri imekuja kipindi ambacho taifa bado linaugulia maumivu ya hasara kubwa zilizosababishwa na athari za mabadiliko ya tabianchi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/mabadiliko-ya-tabianchi-yaathiri-utekelezaji-wa-majukumu-ya-wizara-ya-ujenzi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mei 2026 12:50:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/20124420/Waziri-Shemdoe-1-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1650</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Ikolojia, Maji, Mazingira, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Taka, Uchafuzi, Uhalifu wa Mazingira, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaandaa mkakati wa usimamizi wa taka ngumu kwa ajili kutunza mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imeandaa Mkakati wa Taifa wa Usimamizi wa Taka (2025-2030) ambao unalenga kupunguza uzalishaji wa taka kwa kutumia dhana ya uchumi wa mzunguko ili kutunza mazingira, kuimarisha afya ya jamii na kukuza maendeleo endelevu ya miji. Mkakati huo umekuja kipindi ambacho uzalishaji wa taka ngumu unazidi kuongezeka nchini huku usimamizi wake ukiwa wa kiwango cha chini. Kwa mujibu wa Ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira), Tanzania huzalisha kati ya tani milioni 14.4 hadi milioni 20.7 za taka ngumu kila mwaka. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Riziki Shemdoe, jijini Dodoma katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira mijini. Mkutano huo uliwakutanisha viongozi waandamizi wa serikali, washirika wa maendeleo, na wataalamu wa mazingira kwa lengo la kutathmini maendeleo yaliyofikiwa na kuweka mikakati ya kuboresha mifumo ya usimamizi wa taka. Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Profesa Riziki Shemdoe na wadau wa usimamizi wa taka wakifuatilia mijadala katika Mkutano wa Mwaka wa Tathmini ya Utekelezaji wa Afua za Usimamizi wa Taka Ngumu na Usafi wa Mazingira katika Jiji la Dodoma. Picha: Maktaba ya Wizara. Taka na fursa za kiuchumi Waziri Riziki alisema kuwa usimamizi wa taka unapaswa kuingizwa katika mikakati mipana ya uwezeshaji wa kiuchumi kwa kuwa taka zinapaswa kuonekana kama rasilimali ya kiuchumi inayoweza kuzalisha ajira na kipato ikiwa zitasimamiwa ipasavyo. Aliziagiza mamlaka za serikali za&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/20/tanzania-yaandaa-mkakati-wa-usimamizi-wa-taka-ngumu-kwa-ajili-kutunza-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Teknolojia ya satelaiti yatumika kubaini na kudhibiti moto kwenye hifadhi za misitu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/18/teknolojia-ya-satelaiti-yatumika-kubaini-na-kudhibiti-moto-kwenye-hifadhi-za-misitu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/18/teknolojia-ya-satelaiti-yatumika-kubaini-na-kudhibiti-moto-kwenye-hifadhi-za-misitu/#respond</comments>
					<pubDate>18 Mei 2026 20:49:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/18204618/moto1.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1647</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Misitu, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika juhudi za kubaini matukio ya moto mapema na kuudhibiti kabla ya kuenea na kusababisha madhara makubwa katika hifadhi za misitu, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unafanya ufuatiliaji wa moto nchi nzima kwa kutumia teknolojia ya satelaiti. Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Ashatu Kijaji wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/18/teknolojia-ya-satelaiti-yatumika-kubaini-na-kudhibiti-moto-kwenye-hifadhi-za-misitu/" data-wpel-link="internal">Teknolojia ya satelaiti yatumika kubaini na kudhibiti moto kwenye hifadhi za misitu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika juhudi za kubaini matukio ya moto mapema na kuudhibiti kabla ya kuenea na kusababisha madhara makubwa katika hifadhi za misitu, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania unafanya ufuatiliaji wa moto nchi nzima kwa kutumia teknolojia ya satelaiti. Hayo yamesemwa na Waziri wa Maliasili na Utalii Ashatu Kijaji wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027 mnamo Mei 15, katika kikao cha bajeti kinachoendelea katika mji mkuu wa nchi, Dodoma. Kijaji alisema kupitia juhudi hizo, matukio ya moto yamepungua kwa wastani wa asilimia 11 kwa mwaka. Aidha, ukubwa wa maeneo yanayoathirika na moto kila mwaka unaendelea kupungua. Katika hotuba yake, Waziri alisema pia kuwa Wakala umesafisha njia za kuzuia moto zenye urefu wa kilomita 2,723, kusimamia minara 17 ya kuangalizia moto pamoja na vituo saba vya kufuatilia na kudhibiti moto katika maeneo ya hifadhi, huku ukidhibiti matukio 92 ya moto. Waziri huyo aliongeza kuwa Wakala umetoa mafunzo ya mbinu za kukabiliana na kudhibiti moto kwa vikosi 45 vyenye jumla ya watu 705. Vilevile, mafunzo yametolewa kwa wananchi 20,297 kutoka vijiji 245 vinavyopakana na hifadhi za misitu na mashamba ya miti yaliyopo katika maeneo mbalimbali nchini. “Wakala utaendelea kuzuia na kupambana na matukio ya moto kwa kufanya kampeni 295 za kuzuia moto katika vijiji 337 pamoja na kuunda vikundi 49 vyenye jumla ya watu 588 kwa ajili ya kuzuia na kudhibiti moto kwenye hifadhi za misitu,” Kijaji alisema katika hotuba yake. Aidha, kwa mujibu wa Kijaji, Wakala utafungua kilomita 114 za njia mpya za kuzuia moto na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/18/teknolojia-ya-satelaiti-yatumika-kubaini-na-kudhibiti-moto-kwenye-hifadhi-za-misitu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/18/teknolojia-ya-satelaiti-yatumika-kubaini-na-kudhibiti-moto-kwenye-hifadhi-za-misitu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yaahidi kuendeleza ushirikiano na Norway katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/tanzania-yaahidi-kuendeleza-ushirikiano-na-norway-katika-kukabiliana-na-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/tanzania-yaahidi-kuendeleza-ushirikiano-na-norway-katika-kukabiliana-na-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi/#respond</comments>
					<pubDate>17 Mei 2026 21:04:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/17210626/Screenshot-2026-05-18-000557.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1643</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mabadiliko ya Tabianchi, na  Maendeleo Endelevu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na nchi ya Norway katika kuendeleza hatua za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, uhamishaji wa teknolojia, uwekezaji wa kijani pamoja na ulinzi wa mazingira. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Hamad Yussuf Masauni wakati akizungumza kwenye [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/tanzania-yaahidi-kuendeleza-ushirikiano-na-norway-katika-kukabiliana-na-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Tanzania yaahidi kuendeleza ushirikiano na Norway katika kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kushirikiana na nchi ya Norway katika kuendeleza hatua za kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi, uhamishaji wa teknolojia, uwekezaji wa kijani pamoja na ulinzi wa mazingira. Hayo yamesemwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, Hamad Yussuf Masauni wakati akizungumza kwenye Maadhimisho ya Siku ya Katiba ya Norway yaliyofanyika jijini Dar es Salaam Mei 15, 2026. Alisema Serikali ya Tanzania inaipongeza Norway kwa kuendelea kuwa kinara duniani katika ufadhili wa masuala ya tabianchi na maendeleo endelevu. Akimkaribisha mgeni rasmi, Balozi wa Norway nchini Tanzania, Tone Tinnes, alisema maneno machache kuhusu umuhimu wa siku hiyo pamoja na urafiki na mshikamano kati ya nchi hizo mbili. Uwekezaji zaidi Masauni alisema kuwa wakati Tanzania ikiendelea kutekeleza dira yake ya maendeleo ya 2050 na kuendeleza ukuaji wa kijani pamoja na ustawi shirikishi, inakaribisha kwa moyo mkunjufu ushirikiano zaidi, uwekezaji zaidi, na kuimarishwa kwa mahusiano kati ya mataifa hayo mawili. Masuala ya uhifadhi wa mazingira na ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi ni miongoni mwa vipaumbele katika Dira ya Maendeleo ya Taifa 2050, iliyozinduliwa Julai 2025 na Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan. “Kwa zaidi ya miongo sita, nchi zetu zimejenga urafiki uliotokana na kuaminiana, ukaimarishwa na mshikamano, na kuendelea kudumishwa na maadili ya pamoja. Ni urafiki ambao umeendelea kudumu licha ya mabadiliko ya siasa za kimataifa na mageuzi katika uchumi wa dunia,” alisema waziri huyo. Aliongeza kuwa Tanzania inathamini kwa dhati ushirikiano endelevu wa Norway katika maeneo kama ustahimilivu wa mabadiliko ya tabianchi, nishati jadidifu, kilimo endelevu, elimu, na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/tanzania-yaahidi-kuendeleza-ushirikiano-na-norway-katika-kukabiliana-na-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/tanzania-yaahidi-kuendeleza-ushirikiano-na-norway-katika-kukabiliana-na-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake sita wanaobadilisha mapambano ya mazingira duniani washinda Tuzo ya Goldman 2026</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/wanawake-sita-wanaobadilisha-mapambano-ya-mazingira-duniani-washinda-tuzo-ya-goldman-2026/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/wanawake-sita-wanaobadilisha-mapambano-ya-mazingira-duniani-washinda-tuzo-ya-goldman-2026/#respond</comments>
					<pubDate>17 Mei 2026 04:00:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Liz Kimbrough]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/15150736/Screenshot-2026-05-15-141515-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1632</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Ulimwenguni]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Ikolojia, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Misitu, Miti, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Uongozi wa Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wanaharakati sita wa mazingira kutoka ulimwenguni kote walitunukiwa Tuzo ya Mazingira ya Goldman tarehe 20 Aprili. Ikitambulika kama &#8220;Tuzo ya Nobel ya Kijani,&#8221; Tuzo ya Goldman huwaheshimu wanaharakati kutoka kanda sita za mabara yenye wakazi. Kwa mara ya kwanza katika historia, washindi wote sita ni wanawake. Washindi wa mwaka huu walipambana kulinda popo adimu nchini Nigeria [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/wanawake-sita-wanaobadilisha-mapambano-ya-mazingira-duniani-washinda-tuzo-ya-goldman-2026/" data-wpel-link="internal">Wanawake sita wanaobadilisha mapambano ya mazingira duniani washinda Tuzo ya Goldman 2026</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wanaharakati sita wa mazingira kutoka ulimwenguni kote walitunukiwa Tuzo ya Mazingira ya Goldman tarehe 20 Aprili. Ikitambulika kama &#8220;Tuzo ya Nobel ya Kijani,&#8221; Tuzo ya Goldman huwaheshimu wanaharakati kutoka kanda sita za mabara yenye wakazi. Kwa mara ya kwanza katika historia, washindi wote sita ni wanawake. Washindi wa mwaka huu walipambana kulinda popo adimu nchini Nigeria kwa kutoa mafunzo kwa wanajamii kuhusu kuzuia moto katika maeneo ya nyika; walishinda kesi ya kihistoria mahakamani nchini Korea Kusini na kulazimisha serikali kuweka malengo madhubuti ya hali ya hewa; walisimamisha mradi wa kuchimba mafuta nchini Uingereza baada ya miaka kumi ya vita vya kisheria; waliishinikiza kampuni kubwa ya uchimbaji madini duniani kusafisha mgodi ulioachwa wenye sumu huko Papua New Guinea; walizuia mgodi mkubwa wa shimo wazi uliopendekezwa katika historia ya Marekani Kaskazini huko Alaska; na wakasaidia kusimamisha miradi ya uchimbaji mafuta kwa mbinu ya kupasua miamba nchini Colombia. &#8220;Wakati tunaendelea kupigana kulinda mazingira na kutekeleza sera za hali ya hewa za kuokoa maisha nchini Marekani na duniani kote, ni wazi kwamba viongozi wa kweli wako miongoni mwetu,&#8221; alisema John Goldman, makamu wa rais wa wakfu wa mazingira wa Goldman. &#8220;Nimefurahi sana kuheshimu kundi letu la kwanza kabisa la wanawake sita, kwani hili ni onyesho kubwa la nafasi ambayo wanawake wanaendelea kuchukua katika jamii ya mazingira ulimwenguni.&#8221; Washindi walitunukiwa katika hafla iliyofanyika San Francisco nchini Marekani tarehe 20 Aprili, iliyoandaliwa na mtangazaji wa Telemundo Vanessa Hauc, pamoja na burudani ya muziki kutoka kundi la Caminos Flamencos. Tukio hilo lilionyeshwa moja kwa moja kuanzia saa 5:30&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/wanawake-sita-wanaobadilisha-mapambano-ya-mazingira-duniani-washinda-tuzo-ya-goldman-2026/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/17/wanawake-sita-wanaobadilisha-mapambano-ya-mazingira-duniani-washinda-tuzo-ya-goldman-2026/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mfumo wa malipo ya fidia kwa wananchi walioathirika na matukio ya uharibifu wa wanyamapori waboreshwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/#respond</comments>
					<pubDate>15 Mei 2026 14:49:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/15142508/Baadhi-ya-wanyama-wanaopatikana-katika-mbuga-nchini-Tanzania.-Picha-kutoka-tovuti-ya-TANAPA-768x500.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1629</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bustani za wanyama, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Wenyeji wa Asili, Mgogoro wa Binadamu na Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha mfumo wa Problem Animals Information System (PAIS), mahsusi ulioundwa kusimamia taarifa za matukio ya wanyamapori wakali pamoja na kuratibu na kuwezesha ulipaji wa vifuta jasho/machozi kwa wananchi wanaoathirika na matukio hayo. Hayo yamesemwa na Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/" data-wpel-link="internal">Mfumo wa malipo ya fidia kwa wananchi walioathirika na matukio ya uharibifu wa wanyamapori waboreshwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wizara ya Maliasili na Utalii imeanzisha mfumo wa Problem Animals Information System (PAIS), mahsusi ulioundwa kusimamia taarifa za matukio ya wanyamapori wakali pamoja na kuratibu na kuwezesha ulipaji wa vifuta jasho/machozi kwa wananchi wanaoathirika na matukio hayo. Hayo yamesemwa na Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, katika kikao cha bajeti kinachoendelea makao makuu ya nchi, Dodoma. Amesema mfumo huo wa kisasa umerahisisha ukusanyaji, uwasilishwaji wa taarifa sahihi na kuepuka udanganyifu. Umeboresha pia uchakataji na utunzaji wa taarifa za matukio ya uharibifu wa wanyamapori wakali na waharibifu. Vilevile, mfumo umerahisisha malipo ya kifuta jasho na machozi kwa wananchi waliopata madhara ya wanyamapori wakali na waharibifu. “Kwa sasa taratibu za malipo zinachukua siku saba hadi 14 tofauti na taratibu za awali ambapo malipo yalikuwa yakichukua miezi sita hadi 12,” amesema. Sambamba na hilo, waziri amesema mfumo umeongeza uwazi na uwajibikaji kwani unawezesha kufuatilia kila muamala. Kwa mujibu wa Waziri, hadi kufikia Aprili mwaka 2026, Wizara imelipa kiasi cha TSh8,149,314,750 ($3,134,351) ikiwa ni kifuta jasho na machozi kwa wananchi 22,696 waliopatwa na madhara ya wanyamapori katika Halmashauri za Wilaya 81 ikilinganishwa na 43 katika kipindi kama hiki cha Mwaka wa Fedha 2024/2025 ambapo jumla ya TSh4,604,909,750 ($1,771,119) zililipwa kwa wananchi 16,939. Waziri Ashatu Kijazi wakati akiwasilisha hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa mwaka 2026/2027, Mei 15, katika kikao cha bajeti kinachoendelea makao makuu ya nchi, Dodoma. Taarifa hiyo ya Kijazi kuhusu maboresho kwenye utaratibu wa malipo ya fidia huenda ikawa mkombozi kwa wananchi ambao wamekuwa wakitumia muda mrefu kufuatilia malipo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/mfumo-wa-malipo-ya-fidia-kwa-wananchi-walioathirika-na-matukio-ya-uharibifu-wa-wanyamapori-waboreshwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/#respond</comments>
					<pubDate>15 Mei 2026 10:00:23 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/13194410/IMG-20260513-WA0002-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1602</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mazingira, Migogoro, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Kutoka kuchunga ng’ombe hadi usukani wa helikopta: Safari ya kijana anayelinda tembo na jamii Maasai Mara</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika nyanda za Olemoncho, ndani ya upeo mpana wa Maasai Mara, maisha huanza mapema. Kwa wengi, maisha hayo huanza ardhini. Kuna mdundo wa kipekee ndani ya nyika za Olemoncho; mdundo wa kengele za ng’ombe na nyayo zinazochora njia kwenye udongo mnyevunyevu baada ya mvua zinazoendelea kunyesha. Kwa muda mrefu, anga la Maasai Mara lilitawaliwa na tai na ndege kubwa za kitalii, lakini leo, kuna mlio mpya wa helikopta unaoashiria mabadiliko ya zama. Hapa ndipo ilipoanzia safari ya Wilson Sairowua &#8216;Tate&#8217;; kijana ambaye mikono yake, iliyozoea kushika fimbo ya uchungaji huku akitembea miguu peku katika mfumo huu wa ekolojia, sasa imeshika usukani wa teknolojia ya kisasa. Wilson si rubani tu, ni daraja la amani linalotumia mbingu kulinda urithi wa ardhi ambapo hatima ya binadamu na tembo zimeunganishwa. Rubani Wilson Sairowua akiwa pamoja na askari wa MEP katika makao makuu ya MEP kwenye eneo la hifadhi la Lemek wakati wa mafunzo ya matumizi ya droni. Picha kwa hisani ya MEP. Kabla hajavaa jaketi la rubani lenye nembo ya shirika la Mara Elephant Project (MEP), au kushika usukani wa helikopta, Wilson alikuwa kijana wa kawaida wa Kimaasai, mchungaji mdogo, mara nyingi akitembea miguu peku, akifuatilia mifugo chini ya jua kali la mchana. Alijua kila mti na kila njia ya siri ya maji, na alikuwa hodari wa kutafsiri nyayo za wanyamapori. Vazi lake lilikuwa shuka na kaptula. Suruali ya kwanza aliivaa akiwa na umri wa miaka 14, alipoingia shule ya upili. “Tulikuwa tunatembea umbali mrefu sana kwenda shule. Wengine wetu hata hatukuwa na viatu. Nikiwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/15/kutoka-kuchunga-ngombe-hadi-angani-safari-ya-rubani-wa-kimasai-anayeunganisha-binadamu-na-tembo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Urejeshwaji wa mikoko Bagamoyo waongeza kasi licha ya ukosefu wa takwimu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/14/urejeshwaji-wa-mikoko-bagamoyo-waongeza-kasi-licha-ya-ukosefu-wa-takwimu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/14/urejeshwaji-wa-mikoko-bagamoyo-waongeza-kasi-licha-ya-ukosefu-wa-takwimu/#respond</comments>
					<pubDate>14 Mei 2026 16:50:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Hellen Nachilongo]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/14161934/Mwanachi-Kisutu-2-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1617</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Ikolojia, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mifumo Ikolojia ya Pwani, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Karibu maeneo yote ya ukanda wa pwani wa Tanzania yanaendelea kukabiliwa na shinikizo linalotokana na maendeleo ya pwani, uvunaji wa kuni na athari za mabadiliko ya tabianchi. Hata hivyo, Bagamoyo inaonyesha dalili za mafanikio katika juhudi za urejeshaji wa mikoko zinazoungwa mkono na jamii pamoja na mashirika ya uhifadhi. Tanzania inakadiriwa kuwa na takribani hekta [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/14/urejeshwaji-wa-mikoko-bagamoyo-waongeza-kasi-licha-ya-ukosefu-wa-takwimu/" data-wpel-link="internal">Urejeshwaji wa mikoko Bagamoyo waongeza kasi licha ya ukosefu wa takwimu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Karibu maeneo yote ya ukanda wa pwani wa Tanzania yanaendelea kukabiliwa na shinikizo linalotokana na maendeleo ya pwani, uvunaji wa kuni na athari za mabadiliko ya tabianchi. Hata hivyo, Bagamoyo inaonyesha dalili za mafanikio katika juhudi za urejeshaji wa mikoko zinazoungwa mkono na jamii pamoja na mashirika ya uhifadhi. Tanzania inakadiriwa kuwa na takribani hekta 158,000 za misitu ya mikoko, huku Bagamoyo ikichangia karibu hekta 5,636 zinazoambaa kwenye ukanda wa karibu kilomita 100 za pwani. Ingawa baadhi ya maeneo yanaonekana kuwa na mianya au upungufu wa mikoko wataalamu wanafafanua si maeneo kuwa na mianya au uwazi hakumaanishi kwamba yameharibika kabisa, kwani mikoko inaweza kujirejesha yenyewe endapo mazingira yatakuwa rafiki. Katika kata za Kisutu, Magomeni, Makurunga, Zinga, Kaole, Dunda na Mapinga, ambazo zina wakazi zaidi ya 205,000, shughuli za urejeshaji zinaendelea kwenye maeneo yaliyokuwa yameharibika hapo awali. Katika maeneo ambayo mikoko mipya imepandwa, wananchi wameanza kushuhudia dalili za urejeshwaji wa ikolojia na kuimarika kwa mazingira ingawa bado kuna changamoto zinazoendelea kuwepo. Tangu mwaka 2022, inakadiriwa kuwa miche kati ya 42,000 hadi 46,000 ya mikoko imepandwa wilayani Bagamoyo kupitia programu za pamoja za urejeshaji zinazolenga kufufua mifumo ikolojia ya pwani iliyoharibika. Wananchi katika wilaya ya Bagamoyo kata ya Kisutu wakipanda mikoko. Picha kwa hisani ya Aga Khan Foundation. Akizungumza na Mongabay, Meneja wa Mradi wa Sustainable Ocean Alliance (SOA) Tanzania, Yusufu Issa, alisema juhudi hizo zimeelekezwa zaidi katika maeneo yaliyoharibika sana ambayo urejeshaji wa asili hauwezekani tena. “Tunajikita katika maeneo ya ambayo urejeshaji wa asili hauwezekani tena. Maeneo tunayashughulikia kwa sasa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/14/urejeshwaji-wa-mikoko-bagamoyo-waongeza-kasi-licha-ya-ukosefu-wa-takwimu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/14/urejeshwaji-wa-mikoko-bagamoyo-waongeza-kasi-licha-ya-ukosefu-wa-takwimu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uendelezaji wa viwanda vya kijani na haki ya tabianchi zaongoza mjadala katika Africa Forward Summit</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/13/uendelezaji-wa-viwanda-vya-kijani-na-haki-ya-tabianchi-zaongoza-mjadala-katika-mkutano-wa-africa-forward/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/13/uendelezaji-wa-viwanda-vya-kijani-na-haki-ya-tabianchi-zaongoza-mjadala-katika-mkutano-wa-africa-forward/#respond</comments>
					<pubDate>13 Mei 2026 21:59:31 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/13211054/XXX-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1601</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Kusini, Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara, Afrika Magharibi, na  Afrika Mashariki]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mkutano wa Africa Forward Summit ulifungwa jijini Nairobi Mei 12 kwa tamko la pamoja la kisiasa lililosisitiza kuwa Afrika inapaswa kutambuliwa “siyo tu kama soko la baadaye, bali kama mshirika katika uzalishaji, ubunifu na uongozi wa uchumi wa dunia.” Mkutano huo uliandaliwa kwa ushirikiano wa Kenya na Ufaransa. Ulihudhuriwa na wakuu wa nchi takribani 30, wafanyabiashara wakubwa, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/13/uendelezaji-wa-viwanda-vya-kijani-na-haki-ya-tabianchi-zaongoza-mjadala-katika-mkutano-wa-africa-forward/" data-wpel-link="internal">Uendelezaji wa viwanda vya kijani na haki ya tabianchi zaongoza mjadala katika Africa Forward Summit</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mkutano wa Africa Forward Summit ulifungwa jijini Nairobi Mei 12 kwa tamko la pamoja la kisiasa lililosisitiza kuwa Afrika inapaswa kutambuliwa “siyo tu kama soko la baadaye, bali kama mshirika katika uzalishaji, ubunifu na uongozi wa uchumi wa dunia.” Mkutano huo uliandaliwa kwa ushirikiano wa Kenya na Ufaransa. Ulihudhuriwa na wakuu wa nchi takribani 30, wafanyabiashara wakubwa, watunga sera, taasisi za kimataifa, na wadau wa masuala ya tabianchi, mijadala iligusa mpito wa nishati ya kijani na umuhimu wa kuhakikisha makosa ya zamani ya uchimbaji na unyonyaji wa rasilimali hayarudiwi. Badala yake, mjadala ulisisitiza haki ya tabianchi, upatikanaji sawa wa fedha na teknolojia, pamoja na ulinzi wa mazingira. Awali, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres, alipohutubia kikao cha ngazi ya juu katika mkutano huo, alisisitiza suala la haki ya tabianchi. Alieleza mchango mdogo wa Afrika katika ongezeko la joto duniani, na akibainisha kuwa licha ya hali hiyo, bara hilo bado linaendelea kuathirika zaidi na madhara ya mabadiliko ya tabianchi. Hali hiyo iliakisiwa katika tamko la mwisho la mkutano huo, ambalo liliahidi “kuendeleza mifumo ya haki na usawa katika ufadhili wa miradi ya tabianchi na maendeleo endelevu, wakati Afrika ikipewa sauti kubwa zaidi katika maamuzi ya kimataifa, utawala, uwekaji wa viwango na utungaji wa sheria.” Guterres pia alizungumzia uwezo mkubwa wa Afrika katika nishati jadidifu, akisema kuwa kuna pengo kubwa la uwekezaji katika sekta ya nishati safi duniani. “Afrika ina asilimia 60 ya maeneo bora zaidi duniani kwa uzalishaji wa nishati ya jua lakini inapokea asilimia 2 pekee ya uwekezaji wa kimataifa katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/13/uendelezaji-wa-viwanda-vya-kijani-na-haki-ya-tabianchi-zaongoza-mjadala-katika-mkutano-wa-africa-forward/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/13/uendelezaji-wa-viwanda-vya-kijani-na-haki-ya-tabianchi-zaongoza-mjadala-katika-mkutano-wa-africa-forward/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>