<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/?post_type=post&#038;byline=blaise-kasereka-makuta" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Tue, 21 Apr 2026 06:39:00 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=6.9.4</generator>
				<item>
					<title>Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/#respond</comments>
					<pubDate>21 Aprili 2026 00:42:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20151506/Screenshot-2026-04-20-165755-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1399</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kaskazini mwa Kenya, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni mzunguko usiokwisha wa kutafuta malisho na maji. Lakini ndani ya moyo wa jangwa hili, kumeibuka hadithi inayopinga mantiki ya asili &#8211; ya upendo uliopitiliza, hatari iliyojificha, na mipaka inayofifia kati ya binadamu na mnyama mwitu mwenye kasi kubwa. Ni hadithi ya Bishara Abdirahman Omar, mama wa watoto tisa, ambaye kwa zaidi ya miaka miwili alifanya jambo ambalo wengi wangeliona kama hukumu ya kifo. Mama huyu aliishi na duma ndani ya nyumba kama sehemu ya familia yake. Bishara anakumbuka siku hiyo kwa uwazi kabisa, kana kwamba ilitokea jana. Ilikuwa ni asubuhi yenye joto kali, na yeye alikuwa akitembea porini kutafuta kuni na kuangalia mifugo yake. Katika kichaka kimoja cha miiba, alisikia sauti dhaifu; kilio kidogo kilichofanana na kile cha mtoto wa paka aliyeishiwa nguvu. Aliposogea, alimkuta mtoto wa duma, akiwa mdogo kiasi cha kutoshea kwenye viganja vyake, macho yake yakiwa bado na ukungu wa upofu wa utotoni. “Alikuwa hana msaada kabisa. Nilimwangalia, nikatazama huku na huko nikitarajia kumuona mama yake, lakini hapakuwa na dalili yoyote. Alikuwa ameachwa peke yake kufa kwa njaa au kuliwa na fisi,” Bishara alisimulia, huku akitazama upeo wa macho. Kwa Bishara, hakuona mnyama hatari, bali aliona kiumbe aliyehitaji maziwa na joto. Bila&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kifo cha mtalii Zanzibar: Athari zake kwa utalii na uhifadhi wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 21:16:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asterius Banzi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20205836/MTALII-ALIYEKUFA-ZANZIBAR.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1415</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Utalii]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Aprili 09, Ashley Robinson, mwenye umri wa miaka 31, Mmarekani aliyekuwa kwenye kisiwa cha Unguja na mchumba wake kwa ajili ya mapumziko, alifariki hospitalini alipokimbizwa baada ya kukutwa akiwa mahututi katika villa aliyokuwa anaishi. Chanzo cha kifo hicho bado kimegubikwa na utata. Tukio hilo limewagusa watu mbalimbali kwa namna tofauti. Kwa familia na rafiki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Kifo cha mtalii Zanzibar: Athari zake kwa utalii na uhifadhi wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Aprili 09, Ashley Robinson, mwenye umri wa miaka 31, Mmarekani aliyekuwa kwenye kisiwa cha Unguja na mchumba wake kwa ajili ya mapumziko, alifariki hospitalini alipokimbizwa baada ya kukutwa akiwa mahututi katika villa aliyokuwa anaishi. Chanzo cha kifo hicho bado kimegubikwa na utata. Tukio hilo limewagusa watu mbalimbali kwa namna tofauti. Kwa familia na rafiki zake, kifo hicho kimeleta majonzi makubwa. Kifo hicho pia kimekuwa pigo kwa wafuasi wake mitandaoni, kwa sababu Ashley alikuwa ni mtu maarufu kwenye mitandao ya kijamii, aliyetumiwa na taasisi mbalimbali kama influencer kutokana na nguvu ya ushawishi aliyokuwa nayo. Kwa wadau wa sekta ya utalii na uhifadhi wa mazingira, kifo cha mtalii kinaibua maswali mazito kuhusu mustakabali wa sekta hizo. Baada ya kutokea kwa kifo hicho, Zuberi Chembela, ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika jeshi la polisi Zanzibar, alikaririwa na vyombo vya habari akisema wanamshikilia mchumba wa marehemu Ashley Joseph Isaac McCannon, na kwamba wamechukua pasi yake ya kusafiria, wakati uchunguzi ukiendelea. Kwa mujibu wa Chembela, tayari familia ya Ashley imeteua taasisi maarufu ya uchunguzi wa vifo vya ghafla na vyenye utata, ili kutafiti chanzo cha kifo hicho kwa kushirikiana na serikali ya Zanzibar, kwa lengo la kubaini kama alijiua au aliuawa. Kifo cha Ashley kinahusiana vipi na uhifadhi? Hubert Kilangali, mmoja wa watafiti wa utalii Zanzibar, anasema kuwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Biodiversity Finance Initiative (BIOFIN), asilimia 45 ya kila ada inayolipwa na mtalii kule Zanzibar inakwenda katika kuimarisha na kulinda uhifadhi. BIOFIN ni mpango wa Shirika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi Tanzania inavyoweza kubadili athari za mabadiliko ya tabianchi kuwa chanzo endelevu cha maji</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 20:58:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20205640/Picha1--768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1416</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, na  Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR es SALAAM, Tanzania &#8211; Mvua imenyesha bila kukoma usiku kucha. Nyumba zimejaa maji, nyingine zimesombwa kabisa. Katikati ya taharuki hiyo, Salehe na familia yake wanajaribu kujiokoa kwa kushikilia chochote kilicho karibu nao, wengine wanashikilia miti, wengine magodoro na makabati yanayoelea juu ya maji. Hata hivyo, taswira inayotia uchungu zaidi ni ya madumu yale yale ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/" data-wpel-link="internal">Jinsi Tanzania inavyoweza kubadili athari za mabadiliko ya tabianchi kuwa chanzo endelevu cha maji</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR es SALAAM, Tanzania &#8211; Mvua imenyesha bila kukoma usiku kucha. Nyumba zimejaa maji, nyingine zimesombwa kabisa. Katikati ya taharuki hiyo, Salehe na familia yake wanajaribu kujiokoa kwa kushikilia chochote kilicho karibu nao, wengine wanashikilia miti, wengine magodoro na makabati yanayoelea juu ya maji. Hata hivyo, taswira inayotia uchungu zaidi ni ya madumu yale yale ya njano ambayo hutumika wakati wa ukame kununulia maji, sasa yanaelea juu ya maji mengi kupita kiasi. Ni picha inayobeba ukweli mchungu: katika enzi ya mabadiliko ya tabianchi, jamii zinakabiliwa na ukame na mafuriko kwa wakati mmoja. Swali la msingi ni: Ni kwa namna gani kero ya mvua kubwa inaweza kugeuzwa kuwa suluhisho endelevu la changamoto ya upatikanaji wa maji? Hilo ndilo swali la msingi kwa sasa, ambalo baadhi ya wataalam wanalijibu katika makala haya. Taarifa za mamlaka kuhusu mvua za masika Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu mvua za masika. Katika taarifa yake ya mwelekeo wa mvua za masika Machi-Mei, 2026 inasema kuwa mvua hizo katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (kanda ya Ziwa Victoria, nyanda za juu Kaskazini mashariki, Pwani ya kaskazini pamoja na maeneo yaliyopo kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) katika kipindi cha miezi hiyo, vipindi vifupi vya mvua kubwa vinaweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi. Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Ladislaus Chang’a anasema matukio haya yanaweza kuleta uharibifu wa miundombinu na mazingira, milipuko ya magonjwa, pamoja na upotevu wa mali na maisha. Anahimiza Idara ya Usimamizi wa Maafa, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 15:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Gerald Ahairwe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20185806/IMG_5205-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1409</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Maji, Mamalia, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchimbaji wa Mafuta, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru wa kuandamana. Saa nne asubuhi, ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Buganda Road, Katikati mwa jiji la Kampala nchini Uganda, wanaharakati wa mazingira na wanafunzi wanane walifikishwa kizimbani. Wanafunzi hao wanatoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini Uganda, na wamekuwa gerezani tangu Agosti 1, 2025, baada ya kukamatwa wakiandamana kupinga mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP. Nje ya Mahakama, kulikuwa na rasharasha za mvua. Wasiwasi ulitanda miongoni mwa wanafunzi wa vuguvugu la “Students Against EACOP” waliokuwa wamefika pale ili kuhudhuria hukumu ya Mahakama hiyo dhidi ya wenzao. Hakimu Mkazi alitangaza kuahirishwa kwa hukumu yao hadi saa nane mchana. Lakini nyakati za chakula cha mchana, kabla ya saa nane, wanafunzi walio nje waliambiwa kwamba wenzao wanane wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma (common nuisance). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Sylvia Muwonge katika chumba chake kwenye Mahakama ya Buganda Road. Mawakili, umma au hata waandishi wa habari hawakuhudhuria. Upande wa utetezi umepinga hukumu hiyo, ukisema kuwa wanafunzi hao wamenyimwa haki ya kupewa dhamana, na vile vile kunyimwa nafasi ya kuridhisha kujitetea. Kato Tumusiime, wakili wa wanaharakati hao, anaelekeza kidole cha lawama kwa upendeleo uliokuwepo katika kesi hiyo tangu mwanzo. “Hukumu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushoroba wa Kwakuchinja: Manufaa yake kwa Uhifadhi na Jamii Kaskazini mwa Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 08:59:43 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Isack Dickson]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20075539/Tembo-kwenye-ushoroba-wa-Kwakuchinja-upande-wa-Ziwa-Manyara.-Picha-na-Isack-Dikson.--768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1384</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati miale ya jua asubuhi ikiangaza wilaya ya Babati kaskazini mwa Tanzania, watoto kutoka kijiji cha Sangaiwe wanapita katika njia zilizopo katikati ya misitu ya asili na kwingine mashambani. Ni umbali isiozidi nusu kilomita kuelekea shule ya Msingi Burunge. Katarina Claudi mwenye umri wa miaka 12, na rafiki yake Magdalena Gabriel ni miongoni mwa wanafunzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Ushoroba wa Kwakuchinja: Manufaa yake kwa Uhifadhi na Jamii Kaskazini mwa Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati miale ya jua asubuhi ikiangaza wilaya ya Babati kaskazini mwa Tanzania, watoto kutoka kijiji cha Sangaiwe wanapita katika njia zilizopo katikati ya misitu ya asili na kwingine mashambani. Ni umbali isiozidi nusu kilomita kuelekea shule ya Msingi Burunge. Katarina Claudi mwenye umri wa miaka 12, na rafiki yake Magdalena Gabriel ni miongoni mwa wanafunzi wa shule hiyo. Kutoka nyumbani kwao hadi hapo shuleni wanatumia dakika 20 tu. Ukiwa katikati ya madarasa ya shule hiyo iliyopo kwenye mteremko wa mlima mdogo wenye mawe makubwa kwa madogo, utasikia sauti za watoto wakiimba na kukariri masomo yao zikiwa zimechanganyikana na sauti za ndege wa porini, na kutengeneza taswira ya kipekee ya maisha yanayoendelea pembezoni mwa moja kati ya mapito muhimu zaidi ya wanyamapori nchini Tanzania. Ushoroba wa Kwakuchinja ni njia muhimu ya asili inayounganisha Hifadhi za Taifa za Tarangire na Ziwa Manyara. Wanyamapori kama tembo, nyumbu, pundamilia na twiga huutumia kuhama kwa uhuru kutoka sehemu moja kwenda nyingine kutafuta maji na malisho. Manufaa ya ushoroba Wilfred Mariani Makamu mwenyekiti wa hifadhi ya Burunge, anasema kuwepo kwa ushoroba kwa huo kumeleta manufaa makubwa si kwa uhifadhi tu, bali pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge. Anasema kutokana na kuwepo kwa ushoroba huo wananchi kwanza wananufaika na mapato yanayopatikana kupitia utalii ambayo kwa usimamizi mzuri wa Jumuiya ya Hifadhi ya Jamii ya Burunge, (Burunge WMA) hurudi moja kwa moja kwa wananchi kupitia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na miradi ya maendeleo, kielimu na kijamii. Kwa mfano, kupitia ushoroba huo, shule mbili; sekondari ya Burunge&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 19:32:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/14182846/mawe2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1351</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Sera za Mazingira, Uchafuzi, Uharibifu wa Makazi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), bado uchimbaji holela wa mawe umeendelea kuwa jinamizi linalowaumiza wakazi jijini Mwanza. Akizungumzia sababu za hali hiyo kuendelea, Laurent Kitogo, Afisa wa Mazingira kutoka Environmental Management and Economic Development Organization (EMEDO), anataja udhaifu katika usimamizi pamoja na utekelezaji wa sheria kuwa kikwazo kikubwa. “Sheria ni eneo moja na usimamizi wake ni jambo jingine. Tunazo mamlaka kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na maeneo yote ambayo watu wanaishi. Sheria imeelekeza kabisa kwamba kutakuwa na maafisa wa mazingira kuanzia ngazi ya mtaa, lakini ukiangalia kwa uhalisia ulivyo, utaona maafisa wa mazingira wanaanzia ngazi ya halmashauri. Huwezi kumkuta afisa wa mazingira katika ngazi ya kata,” anasema. David Joseph, Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira jijini Mwanza, anasema kuwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hakuna eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa mawe, na kwamba wanaochimba, baadhi wanakuwa wanasawazisha viwanja vyao kutokana na kuwa na asili ya miamba, au ni wavamizi ambao wameona hiyo kama fursa ya ujasiriamali. “Watu wanachimba mawe katika miktadha kuu miwili. Moja, asili ya Mwanza ni milima, na sehemu nyingi zina mawe. Hata kama ni tambarare, utakuta kuna mawe…kwa hiyo watu wengine wanachimba yale mawe ili kusawazisha viwanja vyao…hayo mawe&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uchimbaji holela wa mawe Mwanza waathiri mazingira na jamii</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 18:39:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/15174750/Screenshot-2026-04-14-231107.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1346</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ardhi iliyoharibika, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Mageuzi ya Ardhi, Mimea, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Makazi, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la pili hapa. Ni asubuhi, na kwa mbali jua linaanza kuchomoza juu ya vilima vya Jiji la Mwanza. Juma anaingia kazini, katikati ya miamba mikubwa ya mawe, mahali anapopaita ofisi yake. Kila siku hufika hapo kutafuta riziki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/" data-wpel-link="internal">Uchimbaji holela wa mawe Mwanza waathiri mazingira na jamii</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la pili hapa. Ni asubuhi, na kwa mbali jua linaanza kuchomoza juu ya vilima vya Jiji la Mwanza. Juma anaingia kazini, katikati ya miamba mikubwa ya mawe, mahali anapopaita ofisi yake. Kila siku hufika hapo kutafuta riziki kwa kuponda mawe na kuyauza. Kabla hajapiga nyundo yake kwenye jiwe la kwanza, anafunga macho kwa sekunde chache, moyo wake umejaa hofu na mashaka. Ameshuhudia wenzake wakipoteza maisha baada ya kupondwa na mawe au kufukiwa na vifusi bila msaada. Kwa Juma, maisha yake ni bahati nasibu. Kila siku ni uchaguzi kati ya uhai na kifo. Juma ni miongoni mwa wakazi wengi wa Jiji la Mwanza ambao wanaishi kwa kujishughulisha na upasuaji na uuzaji wa mawe, shughuli ambayo licha ya kuwa na madhara mengi kwa mazingira, afya, jamii na hata kusababisha vifo, vita dhidi yake inaendelea kuwa ngumu kutokana na changamoto mbalimbali. Mchakato hatari wa uchimbaji mawe Jiji la Mwanza nchini Tanzania limeendelea kukua kwa kasi, likichochewa na ongezeko la watu na mahitaji ya makazi pamoja na miundombinu. Jiji hili lenye asili ya milima na miamba linafanya uchimbaji kuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku, ukitoa ajira na kuchangia upatikanaji wa malighafi za ujenzi zinazohitajika. Hata hivyo, nyuma ya faida hizi za kiuchumi, shughuli hizi zinatishia utunzaji wa mazingira na jamii, kwa kuathiri ardhi, bioanuai, usalama wa wachimbaji wenyewe pamoja na wakazi wanaoishi karibu na maeneo ya uchimbaji. Hatari ya kwanza ya shughuli hii inatokana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/#respond</comments>
					<pubDate>12 Aprili 2026 14:52:07 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/12143649/Green-Climate-Fund.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1342</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Fedha na .Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  tabianchi. Kwa mujibu wa taarifa ya GCF kwa Mongabay, kwa sasa mfuko huo unaunga mkono miradi minne nchini Kenya na miradi 23 ya kikanda inayohusisha nchi nyingi. “GCF hutoa ufadhili kupitia washirika waliothibitishwa; taasisi za kifedha zilizoidhinishwa kufanya kazi na mfuko huu. Taasisi hizi zinakidhi viwango vya GCF na zinaendana na dhamira ya mfuko ya kuleta mabadiliko chanya katika kukabiliana na tabianchi,” alisema Catherine Koffman, Mkurugenzi wa Idara ya Kanda ya Afrika wa GCF. Katika barua pepe kwa Mongabay, Rebecca Phwitiko, Mtaalamu wa Mawasiliano wa GCF (Vyombo vya Habari na Maudhui), alieleza kuwa maeneo makubwa wanayolenga kufanyia kazi yanajumuisha kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo inayostahimili mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yenye ukame. Mengine ni kurejesha maeneo ya malisho na vyanzo vya maji vilivyoharibika ili kuboresha upatikanaji wa maji na maisha ya watu, kupanua matumizi ya nishati jadidifu na nishati safi za kupikia, pamoja na kufungua fursa za ufadhili mseto kwa teknolojia rafiki kwa tabianchi kupitia taasisi za kifedha za ndani. Miradi inayoungwa mkono na GCF nchini Kenya yenye thamani ya $493 milioni inalenga kuleta manufaa makubwa, “ikiwa ni pamoja na kuboresha usalama wa chakula, kuimarisha ustahimilivu wa maji, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbinu ya kutumia pilipili kufukuza tembo inasaidia uhifadhi na kupunguza migogoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/#respond</comments>
					<pubDate>07 Aprili 2026 19:57:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/07192518/Meneja-Mradi-wa-Tembopilipili-Francis-Ndelema-akionesha-jinsi-ya-kuzungushia-wigo-wa-pilipili-shambani-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1325</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mgogoro wa Binadam na Tembo]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MANYARA, Tanzania &#8211; Emmanuel Mwita, mkulima katika Kijiji cha Vilima Viwili, wilayani Babati katika Mkoa wa Manyara, Kaskazini mwa Tanzania, anakumbuka uharibifu mkubwa aliokuwa akifanyiwa na tembo katika shamba lake la mahindi. “Kuna wakati tembo walikuwa wanaingia na kula kila kitu, shamba lote linabaki kama uwanja. Sikuwa navuna kitu. Nilibaki na njaa tu,” anasema Mwita, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/" data-wpel-link="internal">Mbinu ya kutumia pilipili kufukuza tembo inasaidia uhifadhi na kupunguza migogoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MANYARA, Tanzania &#8211; Emmanuel Mwita, mkulima katika Kijiji cha Vilima Viwili, wilayani Babati katika Mkoa wa Manyara, Kaskazini mwa Tanzania, anakumbuka uharibifu mkubwa aliokuwa akifanyiwa na tembo katika shamba lake la mahindi. “Kuna wakati tembo walikuwa wanaingia na kula kila kitu, shamba lote linabaki kama uwanja. Sikuwa navuna kitu. Nilibaki na njaa tu,” anasema Mwita, na kuongeza: “Niliwachukia sana wanyama hao kwa kunirudisha nyuma.” Matukio ya migogoro kati ya wanyama, hususan tembo, na binadamu mara nyingi yamekuwa yakisababisha hasara kwa wakulima, majeruhi na hata vifo kwa upande wa binadamu na kwa upande wa tembo. Wengine wamekuwa wakiuawa na wananchi waliokasirishwa na uharibifu wa wanyama hao. Tembo Pilipili inavyooanisha dhana zinazokinzana Katika kuoanisha dhana mbili ambazo kwa kawaida hukinzana; kupambana na wanyama waharibifu kwa upande mmoja na uhifadhi kwa upande mwingine, asasi ya Tembo Pilipili ilibuni mradi unaoendeleza uhifadhi wa wanyama walio hatarini kutoweka, hasa tembo, na papo hapo kuondoa migogoro baina ya tembo na binadamu. Tembo Pilipili ni mradi ulioanzishwa mwaka 2021 ukilenga kutumia mbinu za kijamii kusaidia tembo na binadamu kuishi kwa pamoja bila migogoro. Ukiendeshwa na asasi inayojulikana kama Tembo Pilipili (TPP), mradi unafanya kazi katika maeneo yanayopakana na hifadhi za wanyama kama vile Tarangire, Ruaha, Selous, Serengeti na Mikumi. Licha ya kudhibiti migogoro, mradi huo unasaidia wakulima kuzuia tembo wasiharibu mazao yao bila kuwadhuru. Pilipili-ikiwa-imeanikwa-kabla-ya-kuitumia. Picha kwa hisani ya mradi wa Tembo Pilipili. Francis Ndemela, Meneja wa Mradi wa Tembo Pilipili, anasema: “Tulibuni mbinu hizi kwa ajili ya kusaidia uhifadhi na wakati huohuo kuondoa migogoro baina ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/#respond</comments>
					<pubDate>07 Aprili 2026 13:39:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/15164710/Screenshot-2026-04-15-194412-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1359</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi wa Ritz-Carlton, Masai Mara Safari Camp, inayoendeshwa na Lazizi Mara Ltd. “Mahakama inaona haina mamlaka ya kushughulikia suala hili kwa sababu kuna mifumo mbadala ya utatuzi wa migogoro ambayo haikutumiwa na mlalamikaji, hivyo kesi hii iliwasilishwa kabla ya muda wake, na mahakama imeondolewa mamlaka ya kuisikiliza. Bila mamlaka, mikono ya mahakama imefungwa,” uamuzi wa mahakama unasema. Uamuzi wa mahakama unaeleza kuwa mlalamikaji, kabla ya kufungua shauri, alipaswa kuwasilisha malalamiko chini ya Kifungu cha 117 cha Sheria ya Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori, ambacho kinataka njia zote za utatuzi, ikiwa ni pamoja na zile za kijamii, zitumike, na pia kukata rufaa chini ya Kifungu cha 129 cha Sheria ya Usimamizi na Uratibu wa Mazingira. Ili kupata taarifa zaidi, Mongabay iliwasiliana na mahakama ya Narok na mamlaka za kaunti, lakini hawakujibu ombi letu la kufanyiwa mahojiano. Kwa mtazamo wa wahifadhi wa mazingira kama Johnson Yiamat, uamuzi huo unatuma ujumbe usio sahihi. “Ninahisi kwamba matokeo ya kiutaratibu hayapaswi kufunika kiini cha hoja zilizowasilishwa,” alisema kupitia ujumbe aliotuma kwa Mongabay. Yiamat ni Mmasai na mwanzilishi wa Osotua Green Alliance, shirika linaloongozwa na jamii lililojikita katika masuala ya uhifadhi wa bioanuwai, hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na uwezeshaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama barani Ulaya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/#respond</comments>
					<pubDate>03 Aprili 2026 21:12:34 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/07185248/Swala-wa-milimani.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1322</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Kimazingira, Maendeleo Endelevu, Maeneo yaliyolindwa, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya &#8211; Hifadhi ya Wanyamapori ya Mount Kenya (MKWC) iko mbioni kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama za Ulaya, hatua inayolenga kuongeza idadi ya miongoni mwa swala walio hatarini zaidi kutoweka barani Afrika. Uhamisho wa swala hao wa kiume uliongozwa na wataalamu kutoka bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/" data-wpel-link="internal">Kenya kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama barani Ulaya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya &#8211; Hifadhi ya Wanyamapori ya Mount Kenya (MKWC) iko mbioni kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama za Ulaya, hatua inayolenga kuongeza idadi ya miongoni mwa swala walio hatarini zaidi kutoweka barani Afrika. Uhamisho wa swala hao wa kiume uliongozwa na wataalamu kutoka bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa ushirikiano na Shirika la Huduma za Wanyamapori la Kenya (KWS) pamoja na European Association of Zoos and Aquaria (EAZA), na the European Association of Zoos and Aquariums. Katika taarifa iliyotumwa kwa Mongabay, Bustani ya Chester ilisema wataalamu wake walitumia zaidi ya miaka 11 kuratibu mpango wa uzalishaji (breeding program) katika bustani za uhifadhi barani Ulaya. “Swala hawa wanne wa kiume walioteuliwa kwa kuzingatia umri, afya na vinasaba: watakuwa wa kwanza kabisa kuhamishwa kutoka bustani za wanyama za Ulaya kwenda Kenya kama sehemu ya juhudi za kurejesha spishi hii porini.” “Ushirikiano kama huu ni muhimu sana ikiwa tunataka kuzuia spishi hii adimu kutoweka kabisa,” Nick Davis, Meneja Mkuu wa Mamalia katika Bustani ya wanyama ya Chester na mratibu wa mpango wa uzalishaji wa Ulaya, alisema katika taarifa hiyo. “Unaonyesha jinsi bustani za kisasa za wanyama zinazoongozwa na sayansi zinavyochangia kwa kiasi ikubwa urejeshaji wa spishi hizi zilizo katika hatari ya kutoweka”. Tathmini ya mwaka 2016 ya IUCN ilibainisha kuwa swala hawa wanaoishi misituni walikuwa katika hatari kubwa ya kutoweka ambapo idadi ya wale waliofikia umri wa kukomaa waliobaki porini walikuwa kati ya 70 hadi 80. Idadi hii ilikuwa ya wanyama wote wa aina hii walioko nchini&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Udhibiti wa ukataji misitu nchini Tanzania: Ni vita kati ya uhai na uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 22:38:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31201251/MKAA-1-12-machi9-2026-768x498.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1289</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Misitu, Miti, Nishati, Nishati Endelevu, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Ni Alfajiri, siku ya Jumamosi, Mariana anadamkia kwenye kibanda chake cha kuuza mkaa ili kupakua mkaa kutoka kwenye magunia na kuuweka kwenye mifuko midogo midogo ili ifikapo asubuhi, awe tayari kuwauzia wateja wa rejareja. Anafahamu mkaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Udhibiti wa ukataji misitu nchini Tanzania: Ni vita kati ya uhai na uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Ni Alfajiri, siku ya Jumamosi, Mariana anadamkia kwenye kibanda chake cha kuuza mkaa ili kupakua mkaa kutoka kwenye magunia na kuuweka kwenye mifuko midogo midogo ili ifikapo asubuhi, awe tayari kuwauzia wateja wa rejareja. Anafahamu mkaa unaharibu misitu, lakini hana njia nyingine ya kupata riziki ya kila siku kwa ajili yake na watoto wake watatu. Kwa Mariana, kila mfuko anaouza, ni chakula kwa watoto wake, lakini kwa upande wa uhifadhi, ni kifo kwa misitu zaidi katika eneo lake. Hadithi ya Mariana ni kielelezo cha kweli kinachoonyesha hali halisi inayoendelea kwenye jamii mbalimbali nchini Tanzania, ambazo licha ya jitihada na miradi mbalimbali inayoendelea kulinda na kuhifadhi misitu, bado wanaendelea kukata miti kwa matumizi mbalimbali. Kwa Mariana na jamii nyingi nchini, kuacha kukata misitu ni kuchagua uhifadhi badala ya uhai wao. Hii ina maana kwamba hatua hiyo itawafanya wapoteze njia pekee ya kujipatia riziki. Misitu ni msingi wa maisha bora kwa wanadamu na viumbe hai vingine, na pia husaidia kujenga uhusiano wa kutegemeana baina ya mifumo mbalimbali ya maisha. Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO), misitu ni nyezo muhimu ya kuondoa umaskini katika jamii zenye kipato cha chini au zisizokuwa na kipato cha kueleweka, kwani huzikinga na majanga mbalimbali ya kiuchumi na kimazingira. Kulingana na Benki ya Dunia, maisha ya watu wapatao bilioni 1.6, ambayo ni zaidi ya asilimia 25 ya watu maskini duniani, hutegemea misitu katika maisha yao,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 22:09:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31212151/MSARAZA-PWANI-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1301</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Misitu, Miti, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka 1998.  Sera hii imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara ili kukabiliana na changamoto za wakati huu, na pitio la mwisho lilifanyika mwaka 2017. Miongoni mwa hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa, Kideghesho anasema ni pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kama gesi na gesi asilia, gesi inayotokana na kinyesi cha wanyama. Taarifa zaidi zinaonyesha serikali imedhamiria kurejesha misitu katika eneo la hekta milioni 5.2 ambalo ardhi yake imepoteza ubora kutokana na kukatwa miti hovyo. Kuanzia mwaka 2023, serikali kwa kushirikiana na asasi za kiraia imekuwa ikitekeleza mradi mkubwa wa mageuzi ya matumizi ya nishati itokanayo na miti wenye lengo la kuboresha usimamizi na uvunaji endelevu wa misitu. Wanakijiji wa Msaraza Wilaya ya Pangani wakiandaa udongo kwaajili ya kutengeneza vitalu vya mitiche ya miti ya asili. Picha kwa hisani ya CAN Tanzania. Mradi wa Mchakato Jumuishi wa Kuleta Mabadiliko Katika Mnyororo wa Thamani wa Nishati ya Kuni (Integrated Approach for Transformation of Tanzania Fuel Wood Value Chain Project), ni mmoja wa miradi inayolenga kuboresha ustawi wa jamii zilizo pembezoni na kuhifadhi na kulinda misitu. Mradi huo unaotekelezwa katika wilaya 16 zilizopo kwenye mikoa ya Tabora, Dar es Salaam, Mwanza, Pwani, Tanga na Morogoro, unafadhiliwa na Umoja wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Baadhi ya wadau wazikataa ripoti, wadai maoni ya wananchi hayakuingizwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 21:18:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31184733/Ngorongoro3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1283</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Baada ya tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro na nyingine kuchunguza migogoro ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/" data-wpel-link="internal">Baadhi ya wadau wazikataa ripoti, wadai maoni ya wananchi hayakuingizwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Baada ya tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro na nyingine kuchunguza migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo, kuwasilisha ripoti zake pamoja na kutoa mapendekezo, watu mbalimbali wametoa maoni yao. Hawa ni pamoja na wenyeji wa wilaya ya Ngorongoro, wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali, Muungano wa Kutetea Haki za Wamasai (MISA), na wataalamu kutoka ndani na nje ya Tanzania. Baadhi wameyakataa mapendekezo ya tume hizo. Charles Odero, Mwanaharakati na Mkurugenzi wa Shirika la Civil and Legal Aid Organization CILAO, ambaye amekuwa akipambania haki za binadamu katika eneo la Ngorongoro, anasema kuwa hajaridhishwa kabisa na mapendekezo ya tume zote mbili. “Kama mdau sijaridhika na mapendekezo ya tume kwa sababu mbalimbali lakini moja ni kwamba yamehalalisha uporaji wa haki za jamii ya wafugaji wa asili (Wahadazabe, Wadatogana Maasai) ambao wanategemea ardhi ya Ngorongoro, Loliondo na Natron kama msingi na tegemeo la maisha yao,” anasema. Kundi la Kondoo katika kijiji cha Ololosokwan baada ya kuondolewa ndani ya kilometa za mraba 1502. Kijiji cha Ololosokwan ni miongoni mwa vijiji vilivyoathirika baada ya eneo la pori la akiba la Parloleti kuchukuliwa kutoka kwa wananchi. Picha na Yohani Gwangway. Akizungumzia suala la uhamaji wa hiari, Odero anakiri kuwa zoezi lilikuwa na kasoro nyingine na kushauri mapungufu hayo yaliyoainishwa na tume yafanyiwe kazi mara moja.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti za tume mbili kuhusu Ngorongoro zafichua ukweli kuhusu uhamaji wa hiari, chanzo cha mgogoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 20:58:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31183248/Ngorongoro-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1275</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Sera za Mazingira, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Hatimaye tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mnamo mwezi Desemba mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro, na nyingine kuchunguza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Ripoti za tume mbili kuhusu Ngorongoro zafichua ukweli kuhusu uhamaji wa hiari, chanzo cha mgogoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Hatimaye tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mnamo mwezi Desemba mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro, na nyingine kuchunguza migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo, zimewasilisha ripoti na kutoa mapendekezo yao. Tume hizo ziliundwa kwa lengo la kufanya tathmini ya kina na shirikishi kuhusu hali halisi ya migogoro ya muda mrefu katika eneo la Ngorongoro na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kupata suluhisho la kudumu. Tume ya kwanza iliongozwa na Musa Iyombe ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu. Wajumbe wengine saba na nafasi zao ni; Sihaba Nkinga- Katibu Mkuu Mstaafu; Alphayo Kidata; Mohamed Mtonga; Valentino Mlowola, Balozi na Mkurugenzi wa Amani, PCCB; George Madafa, Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC); Edward Maura Nduleti na Rehema Moisare wote wakazi wa Ngorongoro. Tume hii ilizinduliwa rasmi tarehe 20 mwezi Februari mwaka 2025 na kuanza kazi rasmi tarehe 25 Februari mwaka huo. Tume ya pili iliongozwa na Gerald Ndika ikiwa na wajumbe wengine ambao ni  Philemon Luhanjo ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu, Zakia Meghji ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Jaji George Masaju (Baadaye alijiondoa baada ya uteuzi wake kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani). Wengine ni Richard Muyungi ambaye ni Mshauri wa Rais katika masuala ya Mazingira pamoja na mabadiliko ya tabianchi, Salome Sijaona, Wilbard Kombe kutoka chuo Kikuu cha Ardhi; Emmanuel Luoga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taasisi ya utafiti na mafunzo ya wanyamapori yaelekeza nguvu kwenye mafunzo ya vitendo kulinda mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/#comments</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 20:30:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31172318/Graduation1-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1273</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mazingira, Sera za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyama pori ya Kenya (WRTI) imefanikiwa kuhamia katika mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia umahiri (Competency-Based Education and Training), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuandaa wataalamu ambao hawaelewi tu uhifadhi, bali pia wana ujuzi wa vitendo wa kulinda wanyama pori na rasilimali asilia za Kenya. Mkurugenzi na Mtendaji [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/" data-wpel-link="internal">Taasisi ya utafiti na mafunzo ya wanyamapori yaelekeza nguvu kwenye mafunzo ya vitendo kulinda mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyama pori ya Kenya (WRTI) imefanikiwa kuhamia katika mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia umahiri (Competency-Based Education and Training), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuandaa wataalamu ambao hawaelewi tu uhifadhi, bali pia wana ujuzi wa vitendo wa kulinda wanyama pori na rasilimali asilia za Kenya. Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa WRTI, Patrick Omondi, alielezea hatua hiyo kama sehemu ya juhudi za kitaifa za kuimarisha uwezo wa kitaalamu katika uhifadhi na usimamizi wa wanyama pori, sambamba na kuhamia kutoka mfumo wa nadharia kwenda katika mbinu za vitendo zinazoendana na mahitaji ya soko la ajira. Omondi alitangaza mabadiliko hayo wakati wa mahafali ya 23 ya taasisi hiyo yaliyofanyika Machi 27, ambapo wahitimu wapatao 499 walitunukiwa vyeti. Mhitimu mmoja ambaye alifariki dunia kabla ya mahafali hayo, alitunukiwa cheti kwa heshima. “Tumepitia upya mitaala yetu ili kuhakikisha inabaki kuwa na uhalisia, na tunaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau muhimu ili kuongeza ubora wa mafunzo na kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu wetu. &#8220;Mapitio yanayoendelea ya programu za ngazi ya tano yataendelea kutuunganisha na mfumo wa kitaifa wa TVET na kuwezesha wanafunzi wetu kuendelea na masomo kwa urahisi,” alisema Omondi katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wadau wa uhifadhi kutoka serikalini, sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali. Baadhi ya wanufaika wa kozi fupi zilizozinduliwa hivi karibuni, zinazolenga kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta ya wanyamapori, ni pamoja na waongoza watalii, ambao wanatarajiwa kuthibitishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Utalii ya Kenya (TRA). Ili kuhimiza ushirikiano kati ya uhifadhi rasmi na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 17:49:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Diana Wanyonyi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://swahili.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/Screenshot-2026-03-27-200514.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1250</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Filosofia ya Uhifadhi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Hifadhi, Hifadhi za Jamii za Asili, Maendeleo ya Jamii, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Misitu ya Kitropiki, Nyani, Primates, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tumbili, Tumbili wa Msituni, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia hiyo ya asili imeundwa kupitia shughuli za kila siku za binadamu, magari, baiskeli na pikipiki zinazoitumia mara kwa mara. Pia kuna wanyamapori wanaotumia njia hiyo wakienda kutafuta maji na malisho. Mongabay iliona kinyesi cha ndovu kilichokuwa kimesambaa barabarani na kukauka, huku vingine vikiwa bado vibichi na vikitoa harufu kali. Mbegu za mimea na majani yaliyosagika yalionekana ndani ya kinyesi hicho kilichokuwa ardhini. Kwa wakazi wa Baomo, kinyesi hicho si uchafu bali ni ujumbe kuwa wanaishi kwa ukaribu na wanyamapori wakubwa zaidi barani Afrika: ndovu. Kijiji cha Baomo kilichoko katika Kaunti ya Tana River, pwani ya Kenya, kipo karibu na Mto Tana na kimezungukwa na msitu unaohifadhi wanyamapori mbalimbali, wakiwemo fisi, tumbili, ndovu, nyati, dikdik, nyani, twiga, ndege, nyoka na wanyama wengine. Mpalawasi hawezi kukudhuru Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Baomo. Picha na Diana Wanyonyi, Mongabay. Matawi ya miti yalipoanza kutikisika mbele yangu, Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, aliyekuja kunipokea, aliniambia: “Mwanangu usiogope, wala usihofu. Hao ni tumbili ambao pia ni jamii yetu. Sisi kama jamii ya Pokomo tunawaita ‘Mpalawasi’. Hatakudhuru kabisa, anasubiri nimwimbie wimbo wake afurahie aende zake. Subiri nimwimbie:&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 16:47:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/06171705/Screenshot-2026-04-06-201423-768x503.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1312</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Sheria ya Mazingira, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana zaidi, ambao kulingana na wahifadhi wa mazingira, unaoonyesha jinsi hatma ya papa na samaki jamii ya pweza walio hatarini, ilivyofungamana kwa karibu na maisha ya wavuvi wanaojitafutia kipato katika Bahari ya Hindi ya Magharibi. Mnamo Februari, ili kuweka mpango kazi unaotekelezeka wa uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza nchini Kenya, kundi la watunga sera, wanasayansi na viongozi wa jamii walichapisha mkakati wenye malengo 19. Kati ya hayo, zaidi ya malengo 12 yanawahusisha moja kwa moja wavuvi wadogo au yanakusudia kuwashirikisha ili kuhakikisha mafanikio yake. Malengo hayo yanajumuisha kuanzisha maeneo zaidi ya bahari yanayosimamiwa na jamii, kuwashirikisha wavuvi katika maamuzi ya uhifadhi, na kuimarisha utekelezaji wa sheria kuhusu zana za uvuvi na uvuvi wa spishi zilizo hatarini. Tangu mwaka 2023, Kenya tayari ina sera ya uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza — Mpango wa Kitaifa wa Hatua za Uhifadhi na Usimamizi wa Papa (NPOA-Sharks). Hata hivyo, mpango huo bado unasubiri kuidhinishwa rasmi na serikali. Mkakati uliopendekezwa na wadau unatoa njia ya jinsi ya kuutekeleza. Papa aina ya scalloped hammerhead (Sphyrna lewini), aliyepigwa picha Yonaguni, Japan. Kulingana na utafiti, spishi hii huvuliwa mara kwa mara na wavuvi wadogo nchini Kenya. Picha na Masayuki Agawa kupitia Ocean Image Bank.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kifo cha Waziri Lukuvi wa Tanzania chaacha pengo katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi na uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mechi 2026 20:25:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/26202110/Lukuvi-1-768x470.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1247</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu wa Tanzania, William Vangimembe Lukuvi, si tu pigo la kisiasa bali pia pengo kubwa kwa juhudi za uhifadhi wa mazingira nchini humo. Alipofariki dunia Machi 25, 2026, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alikuwa bado anahudumu. Aliacha nyuma urithi unaotambulika katika kusuluhisha migogoro ya ardhi katika eneo nyeti linalogusa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Kifo cha Waziri Lukuvi wa Tanzania chaacha pengo katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi na uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu wa Tanzania, William Vangimembe Lukuvi, si tu pigo la kisiasa bali pia pengo kubwa kwa juhudi za uhifadhi wa mazingira nchini humo. Alipofariki dunia Machi 25, 2026, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alikuwa bado anahudumu. Aliacha nyuma urithi unaotambulika katika kusuluhisha migogoro ya ardhi katika eneo nyeti linalogusa moja kwa moja mustakabali wa rasilimali asili, hifadhi za taifa, na maisha ya jamii zinazozitegemea. Mjane wake amepoteza mume, watoto wamepoteza baba na Watanzania wamempoteza mbunge na mwanasiasa maarufu na mkongwe. Lakini kwa wapenda mazingira nchini, kifo chake kinaamsha kumbukumbu za matumaini kuhusu mafunzo aliyoyaacha katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi, hasa kati ya wakulima na wafugaji na katika maeneo yanayopakana na hifadhi za taifa. Taarifa ya kifo cha Lukuvi, ambaye alikuwa pia Mbunge wa Jimbo la Isimani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), ilitangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka. “Kwa wengine, Lukuvi alikuwa na kofia nyingi tofauti. Lakini kwetu wapenda mazingira, tunamwona kama shujaa wa usimamizi endelevu wa raslimali asili. Wote tunafahamu migogoro ya ardhi mara nyingi husababisha matumizi mabaya ya maeneo ya hifadhi, uharibifu wa vyanzo vya maji na misitu. Lakini pia hupelekea kupotea kwa makazi ya wanyama pori au mimea ya asili. “Kwa ujumla, usuluhishi wa migogoro ya ardhi ni kiini cha usimamizi endelevu wa rasilimali asili. Ndiyo maana tunamuona Lukuvi kama shujaa, kwa kutambua na kuyasimamia yote hayo,’’ anasema Paul Mphizi, mwanaharakati wa masuala ya mazingira. Katika nafasi yake ya uwaziri katika wizara tofauti, Lukuvi alisimamia kikamilifu masuala ya utatuzi wa migogoro ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Askari wa hifadhi wa Kenya, zaidi ya kazi ya usalama, akumbukwa kwa umahiri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mechi 2026 19:17:55 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/26185528/WhatsApp-Image-2026-03-16-at-15.24.45-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1242</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Maeneo yaliyolindwa, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati mwili wa John Tanui unashushwa katika kaburi katika eneo moja la Bonde la Ufa nchini Kenya tarehe 25 Machi, 2026, simulizi kuhusu mwanamume ambaye wengi walitamani awe na maisha marefu duniani, ziliendelea kujadiliwa ndani na nje ya nchi. Tanui alifanya kazi kama Afisa wa Mawasiliano ya Usalama katika Hifadhi ya Wanyapori ya Lewa kuanzia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/" data-wpel-link="internal">Askari wa hifadhi wa Kenya, zaidi ya kazi ya usalama, akumbukwa kwa umahiri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati mwili wa John Tanui unashushwa katika kaburi katika eneo moja la Bonde la Ufa nchini Kenya tarehe 25 Machi, 2026, simulizi kuhusu mwanamume ambaye wengi walitamani awe na maisha marefu duniani, ziliendelea kujadiliwa ndani na nje ya nchi. Tanui alifanya kazi kama Afisa wa Mawasiliano ya Usalama katika Hifadhi ya Wanyapori ya Lewa kuanzia mwaka 1995 hadi 2024. “Tanui amekuwa Lewa kwa zaidi ya miaka 23, akisaidia kuboresha operesheni za timu za kupambana na ujangili na wafanyakazi wa hifadhi. Kama mtaalamu wa teknolojia, ndiye aliyeongoza mawasiliano ya kupambana na ujangili Lewa,” Ripoti kuhusu Athari  iliyochapishwa mwaka 2017 na hifadhi hiyo, ilieleza. John Tanui akiwa kazini. Picha na Martin Buzora kwa hisani ya Lewa Wildlife Conservancy. Ripoti hiyo pia ilibainisha kuwa ujuzi wa Tanui kuhusu wanyamapori na ndege ulikuwa wa kuvutia na kwamba alikuwa mahiri na mtu wa kujituma kuwasaidia wageni wa Lewa ambako alikuwa kama mwongozaji wao. “Kifaru wake aliyempenda zaidi ni Elvis.” Tanui alikuwa mtu ambaye alivutiwa na kushangazwa na mandhari ya wanyamapori, japo walikuwa wale wale ambao amekuwa akiwashuhudia kwa miongo kadhaa. Siku moja jioni, alipokuwa akizunguka hifadhi hiyo akiwa na mgeni, walitazama kundi la simba likipanda juu ya mti uliokuwa umeanguka. Jinsi ambavyo Tanui alishangazwa na ustadi wa simba hao kulimshtua mgeni huyo, zaidi ya kuwaona hao wanyama wenyewe. Wote wawili walitazama simba hao kwa takriban saa moja. Mgeni huyo alikuwa mkurugenzi wa EarthRanger, Jes Lefcourt. “Sijawahi kumwona akifurahia kama alivyokuwa akitazama simba hao. Hapo ndipo unapoona upendo wa kweli na kujitolea,” alisema Lefcourt katika taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Tanzania yakamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa umemejua wa MW 50 Kishapu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/tanzania-yakamilisha-awamu-ya-kwanza-ya-mradi-wa-umemejua-wa-mw-50-kishapu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/tanzania-yakamilisha-awamu-ya-kwanza-ya-mradi-wa-umemejua-wa-mw-50-kishapu/#respond</comments>
					<pubDate>25 Mechi 2026 20:14:23 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/25171845/UMEMEJUA1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1236</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Umeme]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Serikali ya Tanzania imekamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa kuzalisha umeme wa jua wenye uwezo wa kutoa megawati 50 uliogharimu Shilingi za Tanzania Bilioni 118.6 (Dola za Marekani Milioni 47.44). Mradi huo uliojengwa katika kijiji cha Ngunga, wilaya ya Kishapu, mkoa wa Shinyanga, unalenga kuongeza uzalishaji wa nishati safi na kuimarisha uthabiti wa gridi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/tanzania-yakamilisha-awamu-ya-kwanza-ya-mradi-wa-umemejua-wa-mw-50-kishapu/" data-wpel-link="internal">Tanzania yakamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa umemejua wa MW 50 Kishapu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Serikali ya Tanzania imekamilisha awamu ya kwanza ya mradi wa kuzalisha umeme wa jua wenye uwezo wa kutoa megawati 50 uliogharimu Shilingi za Tanzania Bilioni 118.6 (Dola za Marekani Milioni 47.44). Mradi huo uliojengwa katika kijiji cha Ngunga, wilaya ya Kishapu, mkoa wa Shinyanga, unalenga kuongeza uzalishaji wa nishati safi na kuimarisha uthabiti wa gridi ya taifa. Ulianza kutumika rasmi Februari, mwaka huu. Hatua hiyo ni utekelezaji wa Tamko la Dar es Salaam la Misheni 300 la mwaka 2025, ambapo Tanzania iliahidi kuongeza mchango wa nishati mbadala katika uzalishaji wa umeme kwenye gridi ya taifa hadi asilimia 75 kufikia mwaka 2030, kutoka kiwango cha sasa cha  asilimia 61.8. Tamko la Misheni 300 ni utekelezaji wa Dira ya Taifa ya mwaka 2025, inayosisitiza matumizi ya nishati safi endelevu na Mpango wa Kitaifa wa Mchango wa Taifa (NDC) katika Mkataba wa Paris. Mkataba wa Paris ni makubaliano ya kimataifa yaliyoanzishwa mwaka 2015 chini ya Umoja wa Mataifa, yakilenga kupunguza ongezeko la joto duniani hadi chini ya nyuzi joto 2°C, na ikiwezekana 1.5°C, kwa kupunguza uzalishaji wa gesi chafu. Kupitia mkataba huo, nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, hutakiwa kuandaa na kutekeleza mipango yao ya kitaifa  ya kupunguza uzalishaji wa hewa chafu na kujenga ustahimilivu dhidi ya athari za mabadiliko ya tabianchi (NDCs). Chini ya mpango huo, Tanzania imeahidi kukuza matumizi ya teknolojia za nishati safi katika uzalishaji wa umeme na shughuli za viwanda, kwa lengo la kupunguza utegemezi wa nishati chafu kama mafuta, gesi na kuni, ambavyo huchangia uchafuzi wa mazingira na kuongeza uzalishaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/tanzania-yakamilisha-awamu-ya-kwanza-ya-mradi-wa-umemejua-wa-mw-50-kishapu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/25/tanzania-yakamilisha-awamu-ya-kwanza-ya-mradi-wa-umemejua-wa-mw-50-kishapu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanawake na mabadiliko ya tabianchi: Athari, changamoto na ushiriki wao katika mipango na maamuzi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/wanawake-na-mabadiliko-ya-tabianchi-athari-changamoto-na-ushiriki-wao-katika-mipango-na-maamuzi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/wanawake-na-mabadiliko-ya-tabianchi-athari-changamoto-na-ushiriki-wao-katika-mipango-na-maamuzi/#respond</comments>
					<pubDate>24 Mechi 2026 19:03:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/24185056/TABIANCHI1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1218</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Majadiliano kuhusu Mabadiliko ya Tabianchi, Sera ya Mabadiliko ya Tabianchi, na  Siasa za Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kukabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, mijadala mingi imekuwa ikijikita katika athari zake kwa ujumla, bila kuangalia namna makundi tofauti yanavyoathirika. Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Machi 8, 2026, Mongabay ilifanya mahojiano ya ana kwa ana na Leonard Chakupewa Soza, Mtaalamu wa Masuala ya Jinsia na Mazingira, ili [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/wanawake-na-mabadiliko-ya-tabianchi-athari-changamoto-na-ushiriki-wao-katika-mipango-na-maamuzi/" data-wpel-link="internal">Wanawake na mabadiliko ya tabianchi: Athari, changamoto na ushiriki wao katika mipango na maamuzi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika kipindi ambacho dunia inaendelea kukabiliwa na changamoto za mabadiliko ya tabianchi, mijadala mingi imekuwa ikijikita katika athari zake kwa ujumla, bila kuangalia namna makundi tofauti yanavyoathirika. Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Machi 8, 2026, Mongabay ilifanya mahojiano ya ana kwa ana na Leonard Chakupewa Soza, Mtaalamu wa Masuala ya Jinsia na Mazingira, ili kuchambua kwa kina uhusiano kati ya mabadiliko ya tabianchi na usawa wa kijinsia. Mahojiano haya yanalenga kuangalia nafasi ya wanawake katika mipango na harakati za kukabiliana na athari hizo na kwa nini ni muhimu kuhakikisha sauti zao zinajumuishwa katika maamuzi, sera, mipango na sheria. Yafuatayo ni mahojiano kati ya mwandishi wa Mongabay na Leonard Chakupewa Soza. Leonard Chakupewa Soza, Mtaalamu wa Masuala ya Jinsia na Mazingira. Picha na Joyce Bazira, Mongabay.  Mongabay: Mabadiliko ya tabianchi yanawaathiri vipi wanawake kwa namna tofauti na wanaume katika nchi zinazoendelea, zikiwemo za Afrika Mashariki? Leonard:  Ili kuelewa athari za mabadiliko ya tabianchi kwa wanawake, ni muhimu kuanza kwa kuangalia nafasi yao katika jamii. Wanawake katika nchi nyingi za Afrika ni kundi kubwa. Kwa mfano, katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 inaonyesha kati ya watu 61,741,120 waliohesabiwa. Wanaume walikuwa 30,053,130, sawa na asilimia 49 ya watu wote, huku wanawake wakiwa 31,687,990, sawa na asilimia 51. Asilimia 60 ya watu wanaojishughulisha na kilimo ni wanawake, ikimaanisha kwamba wao ndio wanaolisha taifa. Wanawake pia hubeba mzigo mzito wa malezi ya watoto na utunzaji wa wazee na wagonjwa. Kutokana na mlundikano huo wa majukumu ya kifamilia na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/wanawake-na-mabadiliko-ya-tabianchi-athari-changamoto-na-ushiriki-wao-katika-mipango-na-maamuzi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/wanawake-na-mabadiliko-ya-tabianchi-athari-changamoto-na-ushiriki-wao-katika-mipango-na-maamuzi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yaadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani huku vifo kutokana na mafuriko vikifikia 81</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/#respond</comments>
					<pubDate>24 Mechi 2026 17:49:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/24174838/Vehicles-partially-submerged-in-at-a-flooded-parking-lot-in-Nairobi-Kenya-after-days-of-heavy-rainfall-on-March-06-2026.-Photo-Courtesy-of-AA.com_.tr_-1-768x487.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1212</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, na  Uhifadhi wa Misitu wa Mvua]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Machi 23, 2026 ni siku ya kuadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani kwa kutambua mchango wa sayansi katika kusaidia binadamu kuelewa na kutabiri hali ya hewa. Huku maadhimisho haya yakiendelea, familia kadhaa kutoka Mashariki mwa Kenya zinaomboleza vifo vya ndugu zao. Watu wawili waliopoteza maisha baada ya ukuta uliolowa kwa maji ya mvua kuwaangukia, na msichana mdogo [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/" data-wpel-link="internal">Kenya yaadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani huku vifo kutokana na mafuriko vikifikia 81</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Machi 23, 2026 ni siku ya kuadhimisha Siku ya Hali ya Hewa Duniani kwa kutambua mchango wa sayansi katika kusaidia binadamu kuelewa na kutabiri hali ya hewa. Huku maadhimisho haya yakiendelea, familia kadhaa kutoka Mashariki mwa Kenya zinaomboleza vifo vya ndugu zao. Watu wawili waliopoteza maisha baada ya ukuta uliolowa kwa maji ya mvua kuwaangukia, na msichana mdogo pia akachukuliwa na maji alipokuwa akichunga mifugo katika eneo hilo. Katika Kaunti ya Baringo, iliyoko Bonde la Ufa, mwanamke mmoja na mtoto wa miaka minne walifariki baada ya maporomoko ya ardhi kuisomba nyumba yao. Vifo vingine vinavyohusishwa na msimu huu wa mvua vinaendelea kuripotiwa kote nchini, huku matukio ya karibuni yakifanya idadi ya vifo vilivyotokea hadi sasa kufikia 81. Kwa mujibu wa taarifa za ReliefWeb, takribani kaunti 21 kati ya 47 za nchini humo, ukiwemo mji mkuu Nairobi, zimeathirika. Taarifa hiyo imefafanua kuwa “takribani watu 70,000 wamehamishwa makazi yao”. Kabla ya kuanza kwa msimu wa mvua, Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya ilitoa tahadhari. Idara hiyo ilitabiri mvua kubwa, zaidi ya milimita 20 ndani ya saa 24 katika maeneo mbalimbali, na kutoa onyo kuhusu mafuriko, maporomoko ya ardhi, na mwonekano hafifu. Idara hiyo imeendelea kutoa utabiri zaidi wa hali ya hewa kila siku. Athari za mvua kubwa zinahusishwa na sababu mbalimbali, ikiwemo mabadiliko ya tabianchi, upangaji wa miji, na mabadiliko ya matumizi ya ardhi. Pia kumekuwepo madai ya mapungufu katika utawala bora, kama ilivyoripotiwa Gazeti la The Daily Nation. Wakati wa maadhimisho ya jana, Edward Muriuki, Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Hali ya Hewa ya Kenya, alisema taasisi hiyo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/24/kenya-yaadhimisha-siku-ya-hali-ya-hewa-duniani-huku-vifo-kutokana-na-mafuriko-vikifikia-81/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 17:31:42 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Ruth Keah]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20141013/Screenshot-2026-03-20-171000-768x509.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1178</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Baharini, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maji, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Safari ya mvuvi wa pwani ya Kenya anayeongoza juhudi za vijana za kuokoa kasa wa baharini</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KWALE, Kenya &#8211; Akiwa na umri wa miaka nane, na akiwa katika darasa la pili, ilikuwa kawaida kwa familia ya Farid Abdallah kula nyama ya kasa. Hii ni kutokana na kwamba baba yake alikuwa mvuvi. &#8220;Baba yangu alikuwa akija nyumbani na nyama ya kasa karibu kila siku. Kama sio yeye aliyemshika, basi ni wavuvi wenzake. Nyama yake ilikuwa ikigawanywa kwa jamii kama ilivyokuwa desturi. Nyama ya kasa ni tamu sana, na tulikuwa tunafurahia sana kitoweo chake,” alisema Abdallah. Kasa katika ufuo wa bahari Shimoni picha na Dzivula Gube Miaka 35 baadaye, Abdallah, ambaye amefanya uvuvi kwa miaka tisa sasa katika eneo la Shimoni, amekuwa mkereketwa mkubwa wa masuala ya kuhifadhi kasa katika kijiji chake. Abdallah pia anashirikiana na kikundi cha vijana cha Shimoni Turtle Watch kilichoko wadi ya Pongwe-Kikoneni, Shimoni, eneo bunge la Lunga Lunga katika Kaunti ya Kwale, ambacho kimefanya kazi hiyo ya uhifadhi wa kasa kwa miaka saba sasa. Hii ni kutokana na tishio la kupotea kwa kasa kutokana na uchafuzi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi, shughuli za uvuvi na ujenzi kwenye fuo za bahari. Wavuvi wanaochinja kasa waliokufa Zaidi, Abdallah na kikundi hicho walisema wamechukua hatua hiyo ya kumlinda kasa kutokana na tishio kwamba kuna wavuvi wengine ambao wanapokutana na kasa amekufa humchinja na kugawia watu nyama yake, hatua ambayo inahatarisha afya ya jamii. Farid Abdallah Mvuvi akionyesha aina ya karatasi za plastiki zipatikanazo baharini ambazo kasa hupenda kula na ni hatari kwao. Picha na Ruth Keah, Mongabay. Kasa ni aina ya kobe wakubwa wanaoishi baharini. Mnyama huyo hutaga mayai yake ardhini hasa katika ufukwe wa bahari, na kuyafukia humo kwa kati&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/safari-ya-mvuvi-wa-pwani-ya-kenya-anayeongoza-juhudi-za-kidijitali-za-kuokoa-kasa-wa-baharini/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Engaroni: Njia ya asili inayosaidia ulinzi wa ardhi na mifumo ya ikolojia</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/engaroni-njia-ya-asili-inayosaidia-ulinzi-wa-ardhi-na-mifumo-ya-ikolojia__trashed/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/engaroni-njia-ya-asili-inayosaidia-ulinzi-wa-ardhi-na-mifumo-ya-ikolojia__trashed/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 15:00:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/24182422/Screenshot-2026-03-24-212318.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1187</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Ufugaji, Ufugaji wa Ng'ombe, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ukame unaochechewa na mabadiliko ya tabianchi unazidi kuathiri maisha ya wafugaji na mifumo ya ikolojia Kaskazini mwa Tanzania. Hata hivyo, tofauti na miaka ya nyuma, safari hii, jamii za Kimasai hazina wasiwasi mkubwa wa kupoteza mifugo kutokana na kukosa malisho. Mfumo wa jadi unaowawezesha kuhifadhi maeneo ya malisho wakati wa msimu wa mvua na kuyafungua [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/engaroni-njia-ya-asili-inayosaidia-ulinzi-wa-ardhi-na-mifumo-ya-ikolojia__trashed/" data-wpel-link="internal">Engaroni: Njia ya asili inayosaidia ulinzi wa ardhi na mifumo ya ikolojia</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ukame unaochechewa na mabadiliko ya tabianchi unazidi kuathiri maisha ya wafugaji na mifumo ya ikolojia Kaskazini mwa Tanzania. Hata hivyo, tofauti na miaka ya nyuma, safari hii, jamii za Kimasai hazina wasiwasi mkubwa wa kupoteza mifugo kutokana na kukosa malisho. Mfumo wa jadi unaowawezesha kuhifadhi maeneo ya malisho wakati wa msimu wa mvua na kuyafungua wakati wa kiangazi, umekuwa mkombozi kwao na mifugo yao. Mfumo huo wa malisho ya kuhamahama, unaojulikana kama Engaroni kwa lugha ya Kimasai, unawawezesha wafugaji kutenga ardhi katika nyanda mbalimbali. Ardhi hiyo hutumika kwa nyakati tofauti kulingana na msimu. Chini ya mfumo huo, wafugaji hufunga baadhi ya maeneo wakati wa msimu wa mvua ili nyasi zikue na kurejesha rutuba na kuyafungua wakati wa kiangazi au ukame kwa ajili ya kulisha mifugo na kuiokoa isife kwa kukosa malisho. Mfumo huo wa kugawa kanda za malisho pia unajumuisha kugawa kanda kwa ajili ya ndama au wanyama wengine ambao hawawezi kutembea umbali mrefu. Mbinu ya kutenga maeneo kwa ajili ya ndama hujulikana kama Oloipolili. Mbinu zote mbili husaidia ardhi kujirutubisha na majani kuota vizuri baada ya kuacha kuitumia kwa kipindi fulani. Akizungumza na Mongabay, Nyamyak Saibulu, mfugaji kutoka kijiji cha Orbamba wilaya ya Longido, mkoani Arusha, anasema desturi hii imekuwa ikitumika kwa muda mrefu katika jamii za wafugaji lakini hivi sasa utamaduni huo umehuishwa kwa kujumuisha mikakati ya kisasa kama upandaji wa miti na majani katika maeneo yaliyotengwa. Wanafunzi katika shule ya msingi Lengijape wakishiriki katika zoezi la upandaji miti. Picha kwa hisani ya UCRT. Wilaya za Monduli na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/engaroni-njia-ya-asili-inayosaidia-ulinzi-wa-ardhi-na-mifumo-ya-ikolojia__trashed/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/engaroni-njia-ya-asili-inayosaidia-ulinzi-wa-ardhi-na-mifumo-ya-ikolojia__trashed/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/#respond</comments>
					<pubDate>20 Mechi 2026 14:00:29 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/20164352/Screenshot-2026-03-20-194312.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1189</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Kasa, Kasa wa baharini, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Maji, Mamalia wa Baharini, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Baharini, na  Uongozi wa Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Kasa 350 wawekwa katika viota maalum kufuatia hatari ya kutoweka katika bahari ya Zanzibar</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[ZANZIBAR, Tanzania &#8211; Nchini Tanzania, katika visiwa vya Zanzibar, zaidi ya kasa 350 wamehifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe, hatua ambayo wataalamu wanadai ni muhimu katika kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu zinazoendelea katika maeneo ya pwani. Hata hivyo, wahifadhi wa mazingira wanaonya kwamba kulinda viota pekee hakutatosha kubadili kile wanachoeleza kuwa ni kupungua kwa kiasi kikubwa kwa idadi ya kasa, hasa katika pwani ya kaskazini-mashariki ya Unguja, ambako hapo awali kulishuhudiwa kasa wengi. Casper Morch, ambaye ni mwanaikolojia na msimamizi wa miradi wa Taasisi ya Under the Wave iliyopo Zanzibar, anasema kuna utafiti mdogo sana wa kisayansi kuhusu kasa wa baharini Zanzibar, lakini idadi ya kasa imepungua mara dufu katika miaka ya hivi karibuni. Morch anasema: “Tunajua kumekuwa na upungufu mkubwa wa kuonekana kwa kasa. Zamani wapiga mbizi walikuwa wanaona kasa 30 hadi 40 kwa wiki, lakini sasa wanajiona wenye bahati wakiona hata mmoja tu.” Mmoja wa kasa zaidi ya 350 wa Zanzibar waliohifadhiwa katika viota maalum kwenye fukwe ili kuwalinda dhidi ya ujangili, wanyama wanaowinda, na shughuli nyingi za kibinadamu. Picha kwa hisani ya Under the Wave. Taasisi ya Under the Wave, ikishirikiana na mamlaka za Zanzibar, ilianza uhifadhi wa kasa mwaka 2020, mwaka ambao walibaini kuwa idadi ya kasa ilikuwa ikipungua kwa kasi. “Tulianzisha mara moja viota (aquaria) ambavyo hadi sasa vina kasa takribani 350. Lakini hawawezi kuzaliana kama walivyokuwa wakiishi kwenye makazi yao ya asilia. Hili ni jambo tunalolitambua na tutahakikisha wanarejea na kuwa salama,” anasema Morch. Taasisi hiyo inasema kasa wanahitaji kurudi walipotoka, lakini hilo litakuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/20/kasa-350-wawekwa-katika-viota-maalum-kufuatia-hatari-ya-kutoweka-katika-bahari-ya-zanzibar/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wataalamu wa mazingira: Huenda maporomoko ya ardhi Chesongoch yaliathiri spishi adimu na mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/wataalamu-wa-mazingira-huenda-maporomoko-ya-ardhi-chesongoch-yaliathiri-spishi-adimu-na-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/wataalamu-wa-mazingira-huenda-maporomoko-ya-ardhi-chesongoch-yaliathiri-spishi-adimu-na-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>18 Mechi 2026 21:25:40 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dann Okoth]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/18211623/Screenshot-2026-03-19-001515.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1170</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Ikolojia, Mifumo ya Ikolojia, Uharibifu wa Makazi, na  Uharibifu wa Misitu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni sehemu ya pili ya nakala hii kuhusu maporomoko ya ardhi yaliyotokea nchini Kenya baada ya musimu wa mvua. Soma sehemu ya kwanza hapa. KERIO VALLEY &#8211; Kenya. Siku chache baada ya mvua kubwa ya mfululizo kunyesha kwenye vilima vilivyokatwa miti, juu ya kijiji cha Chesongoch, Marakwet Mashariki, katika Bonde la Ufa nchini Kenya, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/wataalamu-wa-mazingira-huenda-maporomoko-ya-ardhi-chesongoch-yaliathiri-spishi-adimu-na-mazingira/" data-wpel-link="internal">Wataalamu wa mazingira: Huenda maporomoko ya ardhi Chesongoch yaliathiri spishi adimu na mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni sehemu ya pili ya nakala hii kuhusu maporomoko ya ardhi yaliyotokea nchini Kenya baada ya musimu wa mvua. Soma sehemu ya kwanza hapa. KERIO VALLEY &#8211; Kenya. Siku chache baada ya mvua kubwa ya mfululizo kunyesha kwenye vilima vilivyokatwa miti, juu ya kijiji cha Chesongoch, Marakwet Mashariki, katika Bonde la Ufa nchini Kenya, udongo mwepesi wa volkeno uliteleza na kuporomoka. Kilichoanza kama mtikisiko mdogo wa ardhi mara kiligeuka kuwa jinamizi la vifusi vilivyoanguka na makazi ya watu kusombwa. Takwimu zinazotolewa kuhusu idadi ya vifo vilivyotokana na kadhia hiyo, zinatofautiana huku baadhi ya watu wakisema waliofariki ni 26, wengine wakitaja 31 na 39. Zaidi ya familia 600 ziliripotiwa kukosa makazi katika janga hilo lililotokea Novemba mwaka 2025, ambalo wanasayansi wamelihusisha na mabadiliko ya tabianchi, jiolojia pamoja na shughuli za binadamu, ikiwemo uharibifu wa kasi wa mifumo ya ikolojia katika maendeo ya nyanda za juu. Wahifadhi wa mazingira wanaeleza kuwa majanga kama maporomoko ya ardhi ya Chesongoch yana athari mengi zaidi ya vifo na uharibifu wa mali unaoripotiwa mara kwa mara. Philip Muruthi, Makamu wa Rais wa Uhifadhi wa Spishi na Sayansi katika African Wildlife Foundation, yenye makao yake jijini Nairobi, anasema mara nyingi msisitizo mkubwa huwekwa kwenye athari za kijamii na kiuchumi kwa binadamu, huku madhara kwa bioanuwai yakipuuzwa. Mti uliosalia baada ya maporomoko ya ardhi katika kijiji cha Chesongoch, Marakwet Mashariki, katika Bonde la Kerio. Picha na Dann Okoth, Mongabay. Madhara ya kiikolojia ya maporomopo Moja ya athari hizo, anasema, ni kuvurugika kwa njia za uhamaji wa wanyamapori, tatizo ambalo huenda&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/wataalamu-wa-mazingira-huenda-maporomoko-ya-ardhi-chesongoch-yaliathiri-spishi-adimu-na-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/wataalamu-wa-mazingira-huenda-maporomoko-ya-ardhi-chesongoch-yaliathiri-spishi-adimu-na-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jamii ya Bonde la Kerio inatumainia suluhisho la kudumu baada ya maporomoko ya ardhi kila mara </title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/jamii-ya-bonde-la-kerio-inatumainia-suluhisho-la-kudumu-baada-ya-maporomoko-ya-ardhi-ya-mara-kwa-mara/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/jamii-ya-bonde-la-kerio-inatumainia-suluhisho-la-kudumu-baada-ya-maporomoko-ya-ardhi-ya-mara-kwa-mara/#respond</comments>
					<pubDate>18 Mechi 2026 20:28:11 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dann Okoth]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/18191437/Screenshot-2026-03-18-220925-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1154</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Chakula, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kilimo, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Matumizi ya Ardhi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Mimea, Misitu, Miti, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mabadiliko ya Tabianchi, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Ukataji Miti, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hii ni sehemu ya kwanza ya nakala hii kuhusu maporomoko ya ardhi yaliyotokea nchini Kenya baada ya msimu wa mvua Novemba 2025. Soma sehemu ya pili hapa. KERIO VALLEY, Kenya &#8211; Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini Kenya tangu Februari zinazidi kuacha alama zisizofutika kwa watu mijini na vijijini, huku jamii zikikabiliana na majanga. Tayari barabara [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/jamii-ya-bonde-la-kerio-inatumainia-suluhisho-la-kudumu-baada-ya-maporomoko-ya-ardhi-ya-mara-kwa-mara/" data-wpel-link="internal">Jamii ya Bonde la Kerio inatumainia suluhisho la kudumu baada ya maporomoko ya ardhi kila mara </a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hii ni sehemu ya kwanza ya nakala hii kuhusu maporomoko ya ardhi yaliyotokea nchini Kenya baada ya msimu wa mvua Novemba 2025. Soma sehemu ya pili hapa. KERIO VALLEY, Kenya &#8211; Mvua kubwa zinazoendelea kunyesha nchini Kenya tangu Februari zinazidi kuacha alama zisizofutika kwa watu mijini na vijijini, huku jamii zikikabiliana na majanga. Tayari barabara zimezibwa, madaraja yameanguka, huku mashamba yakijaa maji na mafuriko yakizua hofu ya vifo zaidi. Zaidi ya watu 70 wameripotiwa kufariki kote nchini kutokana na mafuriko yaliyosababishwa na mvua tangu Februari 2026. Maelfu ya familia pia yamepoteza makazi yao, na wengine wengi kuathirika kwa njia nyingine mbalimbali. Lakini hata kabla ya mvua na mafuriko ya 2026 ambayo yamegonga vichwa vya habari, Bonde la Kerio lililoko magharibi mwa Kenya, lilikuwa limeshuhudia vifo vya takriban watu 39 katika mazingira ya kutatanisha. Ilikuwa Oktoba 31, mwaka jana, wakati ghafla maporomoko ya ardhi yalisomba nyumba, miti, na mashamba ya wakazi wa kijiji cha Chesongoch, Elgeyo Marakwet na kuwazika wengi wakiwa bado hai. Hadi sasa, zaidi ya familia 600, ambazo ni baadhi ya wale walioathiriwa, bado zinaishi kwenye makambi ya wahamiaji wa ndani, huku hofu ya mikasa zaidi ikitanda, hasa baada ya Idara ya Hali ya Hewa kutangaza uwezekano wa mvua zaidi. Hata hivyo, historia ya maporomoko ya ardhi katika eneo hili ni ndefu na yenye mafunzo ya dhahiri. Tukio hilo la mwaka 2025 liliashiria hatari iliyojirudia: mwaka 2010 vifo 14, na mwaka 2012 vifo 26. Mongabay kwenye eneo la tukio Mwezi Februari, 2026, timu ya Mongabay ilitembelea nyumbani kwa Mathias Chelimo katika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/jamii-ya-bonde-la-kerio-inatumainia-suluhisho-la-kudumu-baada-ya-maporomoko-ya-ardhi-ya-mara-kwa-mara/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/18/jamii-ya-bonde-la-kerio-inatumainia-suluhisho-la-kudumu-baada-ya-maporomoko-ya-ardhi-ya-mara-kwa-mara/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kadri ujangili unavyoendelea, Tanzania inaongeza silaha mpya: mbwa wa kunusa nyara za wanyamapori</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/#respond</comments>
					<pubDate>17 Mechi 2026 21:53:33 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Las Junior]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/17230956/Screenshot-2026-03-18-020613-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1111</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kusini, Afrika Mashariki, Botswana, Kenya, Msumbiji, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Misitu, Sera za Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR-ES-SALAAM, Tanzania &#8211; Licha ya utajiri wake, ikiwa ni pamoja na uwekezaji wa mamilioni katika uhifadhi, Tanzania inakabiliwa na ongezeko la ujangili na biashara haramu za nyara, kama ilivyofichuliwa na Operesheni Thunder 2025 ya Interpol. Ili kukabiliana na janga hilo, imekuwa muhimu kutumia silaha zaidi, nchi hiyo sasa ikijumuisha ujuzi wa askari wa uhifadhi na mbwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/" data-wpel-link="internal">Kadri ujangili unavyoendelea, Tanzania inaongeza silaha mpya: mbwa wa kunusa nyara za wanyamapori</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR-ES-SALAAM, Tanzania &#8211; Licha ya utajiri wake, ikiwa ni pamoja na uwekezaji wa mamilioni katika uhifadhi, Tanzania inakabiliwa na ongezeko la ujangili na biashara haramu za nyara, kama ilivyofichuliwa na Operesheni Thunder 2025 ya Interpol. Ili kukabiliana na janga hilo, imekuwa muhimu kutumia silaha zaidi, nchi hiyo sasa ikijumuisha ujuzi wa askari wa uhifadhi na mbwa wenye mafunzo maalum ya kunusa nyara. Takwimu za sensa ya hivi karibuni zinaonesha kuwa Tanzania bado ina idadi kubwa zaidi ya nyati na simba barani Afrika. Mnamo Juni, 2024, Wizara ya Maliasili na Utalii nchini iliwasilisha taarifa katika bunge ikisema kuwa Tanzania ina simba takribani 17,000, nyati 225,000 na chui 20,000. Hata hivyo, Operesheni Thunder 2025, iliyofanywa kuanzia Septemba 15 hadi Oktoba 15, ilihusisha vyombo vya kutekeleza sheria pamoja na mamlaka za wanyamapori na misitu katika biashara haramu, ambapo maofisa wa nchi jirani ya Kenya walikamata zaidi ya kilo 400 za nyama za twiga, na wa Tanzania kupata nyama na ngozi za pundamilia na swala, zenye thamani ya takriban $10,000. Mwanzoni mwa Februari 2026, Mongabay ilizuru Shirika la Kuru Conservation Dogs, maarufu shule ya mbwa, iliyopo nchini Tanzania, na kuona jinsi huduma mbalimbali, zikiwemo chakula na matibabu, zilipita kwenye kila chumba cha mbwa. Wahudumu waliwaita kwa majina, nao wakatulia mara moja, na kuacha kubweka, tayari kupokea huduma zao. Mongabay ilishuhudia makumi ya vyumba ambavyo watoa huduma walipita kufanya usafi na kuwapa mbwa huduma hizo. Afisa wa Kikosi cha mbwa nusa wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori nchini Tanzania [TAWA] akiwa moja ya mbwa waliopewa mafunzo na Shirika la Kuru&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/17/kadri-ujangili-unavyoendelea-tanzania-inaongeza-silaha-mpya-mbwa-wa-kunusa-nyara/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kutoka taka hadi thamani: Jinsi mradi unavyogeuza taka kuwa silaha dhidi ya mabadiliko ya tabianchi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/11/kutoka-taka-hadi-thamani-jinsi-mradi-unavyogeuza-taka-kuwa-silaha-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/11/kutoka-taka-hadi-thamani-jinsi-mradi-unavyogeuza-taka-kuwa-silaha-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/#comments</comments>
					<pubDate>11 Mechi 2026 16:52:26 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jenifer Gilla]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/11163742/6.-Ukusanyaji-taka-bila-kutengenishwa-majumbani-unapingwa-na-wadau-wa-mazingira-ukielezwa-kuwa-husababisha-taka-nyingi-kutupwa-dampo.-Picha-Jenifer-Gilla-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1088</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Huduma za Mazingira, Ikolojia, Kilimo, Maendeleo Endelevu, Mashujaa wa Mazingira, Mazingira, Taka, na  Uhifadhi Unaofanywa na Jamii]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Nchini Tanzania, kaya nyingi huona taka kama uchafu usio na thamani. Mabaki ya chakula yanapooza na kutoa harufu kali na plastiki zinazotapakaa karibu na makazi, familia nyingi mijini huwa na wasiwasi wa kupata athari za kiafya, hivyo hukimbilia kuzichoma, kuzitupa ovyo au kuzikusanya kwenye magari ili zipelekwe dampo. Vitendo hivyo huchafua mazingira, na kuchochea uzalishaji [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/11/kutoka-taka-hadi-thamani-jinsi-mradi-unavyogeuza-taka-kuwa-silaha-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Kutoka taka hadi thamani: Jinsi mradi unavyogeuza taka kuwa silaha dhidi ya mabadiliko ya tabianchi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Nchini Tanzania, kaya nyingi huona taka kama uchafu usio na thamani. Mabaki ya chakula yanapooza na kutoa harufu kali na plastiki zinazotapakaa karibu na makazi, familia nyingi mijini huwa na wasiwasi wa kupata athari za kiafya, hivyo hukimbilia kuzichoma, kuzitupa ovyo au kuzikusanya kwenye magari ili zipelekwe dampo. Vitendo hivyo huchafua mazingira, na kuchochea uzalishaji wa gesi aina ya Methane, ambayo hutokana na vitu vya kikaboni kama mabaki ya vyakula na taka vinapooza. Gesi hii huchangia kwa kiasi kikubwa athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo yanaathiri maisha ya kiuchumi na kijamii ya wanadamu. Taarifa ya Ofisi ya Makamu wa Rais iliyowekwa kwenye Mkakati wa Kitaifa wa Usimamizi wa Taka (2025), inasema Tanzania huzalisha kati ya tani milioni 14.4 hadi 20.7 za taka ngumu kwa mwaka. Kati ya hizo, zaidi ya asilimia 60 ni taka za kikaboni, ikiwemo mabaki ya chakula, majani Ripoti ya Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) ya mwaka 2020, inaonyesha kuwa Jiji la Dar es Salaam linaongoza kwa uzalishaji wa taka ambapo kwa mwezi linazalisha taka tani 400,000, kati ya hizo, asilimia 75 huzalishwa majumbani na ni asilimia 30 tu hutupwa kwenye dampo lililopo Pugu Kinyamwezi, Wilaya ya Ilala. Zile zilizosalia huishia kwenye vyanzo vya maji kama vile mifereji, mito, mabwawa na baharini. Boniface Kyaruzi, Mtaalam wa taka na Ofisa Mkuu wa Mazingira NEMC, anasema taka zinapotupwa ovyo mitaani bila kuwa na usimamizi thabiti, huchafua mazingira na kuyasababisha yakose mvuto. Anasema taka hizo zinapokuwa zimezagaa barabarani, maji ya mvua huzipekeka kwenye mito na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/11/kutoka-taka-hadi-thamani-jinsi-mradi-unavyogeuza-taka-kuwa-silaha-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/11/kutoka-taka-hadi-thamani-jinsi-mradi-unavyogeuza-taka-kuwa-silaha-dhidi-ya-mabadiliko-ya-tabianchi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/#comments</comments>
					<pubDate>03 Mechi 2026 19:17:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/03185644/Sehemu-ya-mtambo-wa-kuzalisha-maji-wa-Ruvu-Chini-2-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1074</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki ya Tabianchi, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mafuriko, Maji, Maji ya kunywa, Shida ya Maji, na  Ukame]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Wataalam washauri suluhisho kukabili mabadiliko ya tabianchi yaletayo ukame na mafuriko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni usiku mkubwa wa saa nane, Mama Amina ananyakuka kitandani taratibu na kuelekea uani ambako anafungua bomba kuona kama maji yanatoka. Anaambulia patupu na kurudi tena kitandani. Anazinduka tena baada ya saa moja na kukuta hali ni ile ile. Hadi asubuhi, bomba halitatoa hata tone moja ya maji. Alfajiri pikipiki zilizobeba madumu ya njano ya plastiki yenye maji, zinapishana mtaani. Wanawake, akiwemo Mama Amina, wanazikimbilia kununua maji ambayo yanauzwa kuanzia TSh500 hadi TSh1,000 kwa dumu lenye ujazo wa lita 20. Mama Amina ni miongoni mwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, lenye wakazi karibu 7,000,000, ambao mara kwa mara hukabiliwa na uhaba wa maji. Wakati viongozi wa Serikali ya Tanzania wanahaha kutembelea vyanzo vikuu vya maji vinavyohudumia Jiji la Dar es Salaam kujionea wenyewe namna vilivyokauka, watalaam wa masuala ya maji wanasema ukame huo ambao kwa kiasi kikubwa unachochewa na mabadiliko ya tabianchi, unaweza kupatiwa ufumbuzi wa kudumu iwapo ushauri wa kitalaam utafuatwa. Jiji la Dar es salaam ndilo lenye wakazi wengi zaidi nchini Tanzania. Kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, mkoa huo ulikuwa na watu 5,380,000, ukifuatiwa na mkoa wa Mwanza uliokuwa na watu 3,690,000. Kuanzia Novemba hadi Desemba mwaka 2025, Jiji la Dar es Slaam limekumbwa na uhaba mkubwa wa maji uliosababishwa na kupungua kwa kina cha maji cha Mto Ruvu &#8211; chanzo kikuu cha maji ya jiji hilo. Hali hiyo ilisababisha watu wenye visiwa kuuza maji kwa bei ya hadi TSh1,000 (takriban $0.5) kwa dumu la lita 20. Mamlaka ya Maji&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/03/wataalam-washauri-suluhisho-kukabili-mabadiliko-ya-tabianchi-yaletayo-ukame-mafuriko/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>