<?xml version="1.0" encoding="UTF-8"?><rss version="2.0" xmlns:content="http://purl.org/rss/1.0/modules/content/" xmlns:wfw="http://wellformedweb.org/CommentAPI/" xmlns:dc="http://purl.org/dc/elements/1.1/" xmlns:atom="http://www.w3.org/2005/Atom" xmlns:sy="http://purl.org/rss/1.0/modules/syndication/" xmlns:slash="http://purl.org/rss/1.0/modules/slash/" >

	<channel>
		<title>Habari za uhifadhi</title>
		<atom:link href="https://swahili.mongabay.com/feed/" rel="self" type="application/rss+xml" />
		<link>https://swahili.mongabay.com/</link>
		<description></description>
		<lastBuildDate>Wed, 06 May 2026 17:10:06 +0000</lastBuildDate>
		<language>sw</language>
		<sy:updatePeriod>hourly</sy:updatePeriod>
		<sy:updateFrequency>1</sy:updateFrequency>
		<generator>https://wordpress.org/?v=6.9.4</generator>
				<item>
					<title>Mahakama ya Kenya yaruhusu kesi ya kihistoria ya taka za sumu ya BP kuendelea</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/#respond</comments>
					<pubDate>06 Mei 2026 13:26:49 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dalle Abraham]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/06170355/Screenshot-2026-05-06-200329-768x497.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1525</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uchafuzi, Uchimbaji wa Mafuta, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo Kenya, imeamuru kwamba kesi ya hatua ya ngazi ya juu dhidi ya kampuni kubwa ya mafuta ya Uingereza ya BP inaweza kuendelea kusikizwa kikamilifu. Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa taka za sumu zilizoachwa kutokana na uchimbaji wa mafuta katika miaka ya 1980 zilichafua maji ya ardhini kaskazini mwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/" data-wpel-link="internal">Mahakama ya Kenya yaruhusu kesi ya kihistoria ya taka za sumu ya BP kuendelea</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo Kenya, imeamuru kwamba kesi ya hatua ya ngazi ya juu dhidi ya kampuni kubwa ya mafuta ya Uingereza ya BP inaweza kuendelea kusikizwa kikamilifu. Katika kesi hiyo, inadaiwa kuwa taka za sumu zilizoachwa kutokana na uchimbaji wa mafuta katika miaka ya 1980 zilichafua maji ya ardhini kaskazini mwa Kenya, na kuua zaidi ya watu 500 na maelfu ya mifugo. Kesi hiyo, iliyofunguliwa Februari na walalamikaji 299 katika Mahakama ya Mazingira na Ardhi mjini Isiolo, ilifikishwa mahakamani na wakazi wa Kargi na Kalacha, makazi mawili yaliyoko katika kaunti ya Marsabit. Inadaiwa katika kesi hiyo kuwa shughuli za uchimbaji wa mafuta zilizofanywa kati ya mwaka 1985 na mwaka 1993 kaskazini na kaskazini-magharibi mwa Kenya na Shirika la Amoco, ambalo lilinunuliwa na BP mwaka wa 1998, vichafuzi hatari na sumu vilimwagwa kwenye mazingira, na kuchafua maji ya ardhini ambayo jamii hutegemea kwa kunywa na kwa mifugo yao. Hati za korti zinadai kuwa taka za kuchimba visima zilizo na isotopu za radiamu, aseniki, madini ya risasi na nitrati, zilitupwa kwenye mashimo yaliyoachwa wazi au ambayo hayakuwekwa katika hali inayotakiwa kiusalama. Katika kesi hiyo, washitakiwa ni pamoja na kampuni ya British Petroleum PLC ambayo ni mshitakiwa wa kwanza, huku wengine 11 wakiwa ni Shirika la Kitaifa la Mafuta la Kenya; mawaziri wa mazingira, maji, afya na madini; Mamlaka ya Rasilimali za Maji; serikali ya kaunti ya Marsabit; mwanasheria mkuu; Mamlaka ya Kitaifa ya Usimamizi wa Mazingira; Mamlaka ya Udhibiti wa nishati ya Nyuklia ya Kenya pamoja na Taasisi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/06/mahakama-ya-kenya-yaruhusu-kesi-ya-kihistoria-ya-taka-za-sumu-ya-bp-kuendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/#respond</comments>
					<pubDate>05 Mei 2026 22:27:36 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[David AkanaRhett Ayers Butler]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/05212300/Screenshot-2026-05-06-000526-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1504</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika ya Kati, Bonde la Kongo, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na  Kongo]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Maendeleo Endelevu, Mamalia, Mazingira, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uharibifu wa Misitu ya Mvua, Uhifadhi, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Je, unadhani asili inaweza kuushinda mgogoro unaoendelea Mashariki mwa Kongo?</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Katika sehemu ya Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, majadiliano ya uhifadhi mara nyingi yanahusisha hasara: misitu iliyokatwa, wanyamapori wanaopungua, migogoro inayoenea katika mandhari ambayo hapo awali ilisaidia baadhi ya mifumo tajiri zaidi ya ikolojia ulimwenguni. Katika Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga, shinikizo hilo limekolezwa. Mbuga hiyo, ambayo ni kongwe zaidi barani Afrika, ina barafu, volkeno, misitu, na ardhi oevu ndani ya eneo moja lililohifadhiwa. Pia ipo ndani ya mazingira iliyoundwa kwa miongo kadhaa ya ukosefu wa utulivu, ambapo makundi yaliojihami kwa silaha, uchumi usio rasmi, na utawala dhaifu ni sehemu ya maisha ya kila siku. Hifadhi ya Kitaifa ya Virunga. Picha kwa hisani ya Bitini Ndiyanabo Kanane. Emmanuel de Merode, ambaye ameiongoza Virunga tangu mwaka wa 2008, haanzii na ikolojia. Mafunzo yake ni ya anthropolojia, hali inayounda namna anavyoelezea hifadhi. Anapendekeza kuwa hali ya wanyamapori hutokana na nguvu za kina. Upotevu wa misitu, ujangili, na ukosefu wa usalama sio shida za mazingira pekee. Yanatokana na namna watu wanavyopata riziki, namna mamlaka inavyofanya kazi, na jinsi pesa na rasilimali zinavyozunguka. Katika sehemu ya Mashariki mwa Kongo, uhifadhi hauwezi kutenganishwa na uchumi. Kwa jamii nyingi zinazoizunguka Virunga, chaguo lao ni la haraka. Kuifyeka misitu kwa ajili ya ukulima au kutengeza mkaa kunaweza kuzalisha kipato cha kuendesha maisha. Faida za uhifadhi ni ngumu kuonekana na mara nyingi huonekana zaidi nje ya eneo hilo. Ukosefu wa usawa unajitokeza katika maamuzi ya kila siku kuhusu mafuta, chakula na upatikanaji wa ardhi. Kama De Merode anavyoelezea, mfumo unawalazimisha baadhi ya watu maskini zaidi kubeba gharama ya kulinda mali zinazothaminiwa kimataifa. Shinikizo kwenye mbuga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/05/je-unadhani-asili-inaweza-kuushinda-mgogoro-mashariki-mwa-kongo/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/#respond</comments>
					<pubDate>04 Mei 2026 13:28:14 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Spoorthy Raman]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/04145740/Screenshot-2026-05-04-160903.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1493</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Kaskazini, Afrika Magharibi, Asia, Asia ya Kusini-mashariki, Guinea, Indonesia, Mali, Msumbiji, Senegal, Singapore, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Aina Vamizi, Biashara ya Wanyamapori, Bioanuai, Magonjwa, Matumizi ya Wanyamapori, Mazingira, Ndege, Ugonjwa wa Kuambukiza wa Wanyamapori, Uhalifu, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Ndege 1,000,000 walisafirishwa kutoka Afrika hadi Asia katika kipindi cha miaka 15; chiriku waongoza orodha</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ulimwenguni kote, watu hununua na kuwinda karibu nusu ya spishi 11,000 za ndege waliopo. Katika mabara ya Asia, Ulaya, Amerika Kaskazini na Amerika Kusini, ndege wa kuimba na kasuku ni ndege wa kufugwa nyumbani wanaotamanika sana. Wafugaji wa ndege hao hulipa pesa nyingi sana kwa spishi adimu au ndege wenye sauti nzuri ili kushindana katika mashindano ya uimbaji wa hali ya juu. Wafugaji wa ndege aina ya vipanga na wawindaji wa michezo hukamata au kuua ndege wa porini. Matambiko ya imani za jadi katika Afrika Magharibi hujumuisha viwiliwili vya tai. Wanunuzi kutoka Marekani ya Kaskazini hutafuta hondohondo na ndege mvumaji waliokufa kama mapambo ya nyumbani. Orodha inaendelea. Biashara hii kubwa inatisha zaidi ya spishi 200 za ndege kutoweka. Sasa, huku masoko ya mtandaoni yakiongezeka, wateja wanaweza kuagiza ndege kwa kubonyeza simu zao za mkononi kutoka mahali popote katika sayari. Kusafirisha ndege kote ulimwenguni pia husambaza magonjwa hatari, kama vile homa ya ndege na virusi vwa circovirus, na wakati ndege wasio wa asili wanapotoroka au kuachiliwa, wanaweza kuongezeka kuwashinda spishi za asili. &#8220;Kuna ukosefu wa ufahamu na kuthamini ukubwa wa biashara hii, na umakini mchache sana juu ya athari ambazo hii inaweza kuwa nayo kwa wakazi wa porini au hatari za kuenea kwa viumbe vamizi na magonjwa ya kuambukiza,&#8221; Rowan Martin ni mkurugenzi wa biashara ya ndege katika shirika lisilo la faida la World Parrot Trust. &#8220;Ikiwa watu hawajui kwamba hili linafanyika, basi tutawezaje kupunguza hatari zinazohusiana nayo?&#8221; Katika kujaribu kuelewa ukubwa wa biashara ya ndege hai, Martin na wenzake walitumia hifadhidata ya Umoja wa Mataifa ya Comtrade (UN Comtrade), hifadhidata inayojumlisha taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/04/takriban-ndege-milioni-moja-walisafirishwa-kutoka-afrika-hadi-asia-katika-kipindi-cha-miaka-15-chiriku-waongoza-orodha/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/#respond</comments>
					<pubDate>01 Mei 2026 15:34:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/01152749/Antoine-Moses-akipanda-miche-ya-miti-ya-mikoko-katika-eneo-la-Tudor-Mombasa.-Picha-kwa-hisani-ya-Wizara-ya-Mazingira-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1485</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bahari, Baharini, Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maji, Mazingira, Mikoko, Misitu, Miti, Samaki, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada avunja rekodi kwa kupanda mikoko 47,460 kwa saa 24 Kenya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kenya wiki hii imekuwa kitovu cha harakati za kuvunja rekodi za dunia za Guinness baada ya mwanaharakati wa mazingira kutoka Canada, Antoine Moses, kuvunja rekodi yake mwenyewe ya kupanda miche 47,460 ya mikoko ndani ya saa 24 tu. Idadi hiyo ilithibitishwa Mei 1, saa 8:01, muda mfupi baada ya kukamilisha zoezi hilo. Antoine alikuwa nchini humo kwa siku 10 kabla ya tukio hilo, ambapo alipanda miti mingine 13,600 ili kujenga stamina katika maandalizi ya rekodi mpya. “Tumekuwa Kenya kwa siku 10 zilizopita tukipanda mikoko, tukijifunza kutoka kwa jamii na kutengeneza kumbukumbu zisizosahaulika na marafiki wapya,” alisema kabla ya jaribio hilo, na kuongeza: “Baada ya kufikia miti 10,000 chini ya saa nne wakati wa mazoezi, nilijua tuko tayari kusonga mbele zaidi.” Waziri wa Mazingira wa Kenya, Deborah Barasa, alimkaribisha Antoine na alikuwepo alipokuwa akipanda mche wake wa kwanza. Alisema: “Kenya imepata heshima kumkaribisha Antoine Moses… Jaribio lake la kijasiri la kupanda mikoko 40,000 ndani ya saa 24 katika eneo la Tudor Creek, Kaunti ya Mombasa, halimaanishi tu kuweka rekodi mpya, bali ni kubadili mwenendo wa uharibifu wa misitu kabla haujafikia hatua ya hatari. Uwepo wake unaimarisha nafasi ya Kenya kama kiongozi anayeaminika katika juhudi za kimataifa za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.” Timu iliyoratibiwa ya wanajamii, wahifadhi wa mazingira, maafisa wa Huduma ya Misitu Kenya, akiwemo Katibu Mkuu Gitonga Mugambi, pamoja na washirika kutoka Earthlungs, walimpa hamasa, wakitembea pamoja naye ili kumsaidia kutimiza malengo yake. Awali, Antoine aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram kwamba malengo yake ni kupanda miche 35,500 ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/mwanaharakazi-wa-mazingira-kutoka-canada-apanda-miti-ya-mikoko-47460-kwa-saa-20-katika-pwani-ya-kenya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya yawapokea Swala wa milimani adimu waliorudishwa kutoka bustani za wanyama Ulaya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/#respond</comments>
					<pubDate>01 Mei 2026 10:52:01 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/05/01105311/Swala-wa-milimani-aliye-hatarini-kutoweka-akiwa-kwenye-Bustani-ya-Chester-Cheshire-Uingereza.-Picha-kwa-hisani-ya-Chester-Zoo-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1481</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Kuzuia Kutoweka kwa Spishi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, Misitu, Spishi, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wiki hii Kenya imepokea kundi la swala wa milimani walio katika hatari kubwa ya kutoweka, wakitokea Jamhuri ya Czech ambako walikuwa wakihifadhiwa chini ya usimamizi wa Bustani ya Wanyama ya Zoo Dvůr Králové. Urejeshaji wa swala hao wanne dume, waliokulia katika bustani mbalimbali za wanyama chini ya mpango wa uhifadhi nchini Uingereza, ni hatua muhimu [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/" data-wpel-link="internal">Kenya yawapokea Swala wa milimani adimu waliorudishwa kutoka bustani za wanyama Ulaya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wiki hii Kenya imepokea kundi la swala wa milimani walio katika hatari kubwa ya kutoweka, wakitokea Jamhuri ya Czech ambako walikuwa wakihifadhiwa chini ya usimamizi wa Bustani ya Wanyama ya Zoo Dvůr Králové. Urejeshaji wa swala hao wanne dume, waliokulia katika bustani mbalimbali za wanyama chini ya mpango wa uhifadhi nchini Uingereza, ni hatua muhimu katika juhudi za Kenya kurejesha wanyama ambao kiasili wana nguvu na hupenda kuzunguka milimani kwa uhuru katika makazi yao ya asili. Hatua hii pia inaendana na mkakati wa kitaifa wa urejeshaji wa mwaka 2019–2023 unaolenga kuokoa spishi hiyo iliyokuwa hatarini kutoweka, juhudi ambazo zimeendelea hata miaka kadhaa baadaye. Swala hao watahifadhiwa katika Kituo cha Uhifadhi wa Wanyamapori cha Mount Kenya (MKWC), kilichopo katika maeneo ya milimani ya Laikipia. Uhamisho huo uliongozwa na wataalamu kutoka Bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa ushirikiano na Huduma ya Wanyamapori Kenya (KWS) pamoja na Chama cha Ulaya cha Bustani za Wanyama na Hifadhi za Majini. Akizungumza wakati wa kupokea swala hao waliowasili kwa ndege ya mizigo ya KLM katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi, Waziri Mkuu Msaidizi na Waziri wa Mambo ya Nje na Masuala ya Diaspora, Musalia Mudavadi, alisema kuwa simulizi ya swala wa milimani inaakisi hali pana ya mazingira nchini humo. Alisema: “Waliwahi kustawi katika misitu ya milimani, kuanzia Aberdares hadi Mlima Kenya, Mau na Eburu, lakini sasa spishi hii ya kipekee inakabiliwa na ukweli mchungu wa kuwa katika hatari ya kutoweka kabisa.” Wadau wengine kadhaa waliokuwepo ni pamoja na Waziri&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/05/01/kenya-yawapokea-kihistoria-swala-wa-milimani-adimu-waliorudishwa-kutoka-bustani-za-wanyama-ulaya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/#respond</comments>
					<pubDate>30 Aprili 2026 20:54:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/30202905/MTERA-6-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1470</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Afya, Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Maji, Maji ya kunywa, Mazingira, Maziwa, Samaki, Samaki wa Maji safi, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi wa Maji, Uvuvi, na  Uvuvi Haramu]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mabadiliko ya tabianchi yanavyoathiri sekta ya uvuvi nchini Tanzania na mikakati ya kujenga ustahimilivu</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Ni Jumamosi alfajiri. Jamal, ameketi kando ya mtumbwi wake, akiwa ameshika tama, macho yake yametizama mto Kilombero ambao miaka yote umempa fahari mbele ya familia yake. Pembeni yake zimeegeshwa nyavu ambazo kwa miaka mingi zimekuwa tegemea la maisha yake, lakini safari hii zimerudi tupu. Kwa muda mrefu uvuvi ulikuwa fahari yake kuu na chanzo cha mapato, lakini katika miaka ya hivi karibuni hali imebadilika, samaki wamepungua kwa kiasi kikubwa majini. Kimya kimya anaijuliza, ikiwa leo hakuna samaki, kesho kutwa, mtondo na mtondogoo hali itakuwaje? Mashaka haya hayamkabili Jamal pekee, bali pia wavuvi wengi nchini kote. Kilio cha wavuvi Kilio cha wavuvi nchini Tanzania ni matokeo ya athari za mabadiliko ya tabianchi ambayo yameitikisa vibaya sekta ya uvuvi kwa namna mbalimbali ikiwa ni pamoja na kusababisha kiwango cha samaki kupungua huku baadhi ya aina ya samaki wakitoweka kabisa. Victor Tondelo, Mtaalamu Mtafiti wa Madiliko ya Tabianchi, aliiambia Mongabay kuwa athari za mabadiliko ya tabianchi zimejidhihirisha zaidi katika rasilimali za maji (water resources) hasa kwenye mito, mabwawa na maziwa. “Kwa sababu ya kupungua kwa mvua inayonyesha na misimu inayotabirika, maji yamepungua na hivyo idadi ya samaki ambao maisha yao ni majini pia imepungua,” alieleza. Aliongeza kuwa kuwepo kwa maji machache pia husababisha joto kubwa wakati wa kiangazi na samaki na viumbe wengine wa majini hufa kutokana na joto kali. Uchunguzi wa Mongabay kuhusu athari za mabadiliko ya tabianchi kwenye sekta ya uvuvi, ulijikita katika mikoa mitatu ya Morogoro, Iringa na Pwani. Katika mkoa wa Morogoro ulihusisha mto Kilombero, Luipa, Ruhudji na Mto&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/30/mabadiliko-ya-tabianchi-yanavyoathiri-sekta-ya-uvuvi-nchini-tanzania-na-mikakati-ya-kujenga-ustahimilivu/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi kilimo kandokando ya vyanzo vya maji kinavyoathiri Ziwa Victoria</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/29/jinsi-kilimo-kandokando-ya-vyanzo-vya-maji-kinavyoathiri-ziwa-victoria/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/29/jinsi-kilimo-kandokando-ya-vyanzo-vya-maji-kinavyoathiri-ziwa-victoria/#respond</comments>
					<pubDate>29 Aprili 2026 15:54:22 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Mutayoba Arbogast]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/29153109/SHUGHU2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1461</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Uvuvi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Pembezoni mwa wilaya ya Missenyi, mkoani Kagera nchini Tanzania, kipo kijiji cha Kashenye kinachopakana na Ziwa Victoria. Ziwa hili ndilo kubwa zaidi barani Afrika, na pili duniani, likiwa na maji baridi. Ziwa Victoria ndio chanzo cha Mto Naili. Lina shughuli nyingi za kiuchumi, hasa uvuvi wa samaki aina ya dagaa, sato, sangara na wengineo. Amina [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/29/jinsi-kilimo-kandokando-ya-vyanzo-vya-maji-kinavyoathiri-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Jinsi kilimo kandokando ya vyanzo vya maji kinavyoathiri Ziwa Victoria</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Pembezoni mwa wilaya ya Missenyi, mkoani Kagera nchini Tanzania, kipo kijiji cha Kashenye kinachopakana na Ziwa Victoria. Ziwa hili ndilo kubwa zaidi barani Afrika, na pili duniani, likiwa na maji baridi. Ziwa Victoria ndio chanzo cha Mto Naili. Lina shughuli nyingi za kiuchumi, hasa uvuvi wa samaki aina ya dagaa, sato, sangara na wengineo. Amina Juma, mama wa watoto wanne, ambaye pia ni mjane, na anayejulikana zaidi kama Mama Koku, anaishi kijiji hiki, akijishughulisha na kilimo cha mbogamboga katika kitongoji jirani cha Kaishebo. Mama Koku na watoto wake watatu wana wiki nzima hawajapata kitoweo cha samaki, na wamekuwa wakitumia mboga ya &#8216;Sukuma wiki&#8217;, mchicha na matembele. Siku moja jioni baada ya kutoka shambani, Mama Koku anafungua fundo la kitenge chake alichokuwa amekipachika kwenye mlango wa chumba chake, anachukua noti pekee aliyokuwa amebaki nayo kama akiba ya nyumbani, TSh10,000 ($3.8), na kumpatia mtoto wake wa kiume, Ruta (11), akimbie mwaloni kununua samaki. Kutokana na hamu ya kupata kitoweo cha samaki, mtoto anapiga mbio hadi mwalo wa Kabindi, na kama wasemavyo Waswahili, &#8216; Mgaagaa na upwa hali wali mkavu&#8217;, kijana anajipatia samaki watatu aina ya sato, aliowaona wamenona, kwa TSh8,000. Mama Koku anapokea samaki kwa furaha na kutayarisha mlo wa usiku. Hata hivyo, baadaye usiku, hali inakuwa si shwari tena kwani watoto wanaanza kulalamikia maumivu ya tumbo, kuharisha na pia kuhisi kizunguzungu, madhila yanayomkumba mama yao pia. Asubuhi wanaamkia zahanati ya kata na majibu ya daktari yanaonyesha wamekula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu. Hata hivyo Mama Koku anasema daktari hakuthibitisha kama maradhi&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/29/jinsi-kilimo-kandokando-ya-vyanzo-vya-maji-kinavyoathiri-ziwa-victoria/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/29/jinsi-kilimo-kandokando-ya-vyanzo-vya-maji-kinavyoathiri-ziwa-victoria/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kufutwa kwa leseni 40 za utafiti wa madini Tanzania kwafichua ukweli wa athari za mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/#respond</comments>
					<pubDate>28 Aprili 2026 21:53:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Nkwimba Nkwimba]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/28213333/Madini-3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1452</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Ikolojia, Kijani, Mazingira, Misitu, Uchimbaji Dhahabu, Uchimbaji Madini, Uchimbaji Madini Haramu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Sekta ya madini nchini Tanzania imetikiswa na hatua ya Serikali kuzifutia leseni za utafiti wa madini kampuni 40 huku ikitoa muda wa siku 30 kwa kampuni nyingine 43 kurekebisha mapungufu yao, la sivyo nazo zitapoteza leseni zao. Wakati watu wengi wameunga mkono hatua hiyo kwa kuangalia matokeo ya uamuzi huo kwa mtazamo wa kiuchumi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/" data-wpel-link="internal">Kufutwa kwa leseni 40 za utafiti wa madini Tanzania kwafichua ukweli wa athari za mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Sekta ya madini nchini Tanzania imetikiswa na hatua ya Serikali kuzifutia leseni za utafiti wa madini kampuni 40 huku ikitoa muda wa siku 30 kwa kampuni nyingine 43 kurekebisha mapungufu yao, la sivyo nazo zitapoteza leseni zao. Wakati watu wengi wameunga mkono hatua hiyo kwa kuangalia matokeo ya uamuzi huo kwa mtazamo wa kiuchumi na uwajibikaji, watetezi wa mazingira wameibua hoja nzito kuhusu uharibifu mkubwa wa mazingira unaotokea pindi leseni za utafiti zinapotelekezwa. Waziri wa Madini Antony Mavunde, katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika katika makao makuu ya Tanzania, jijini Dodoma, alitaja mambo kadhaa ambayo kampuni hizo zimeshindwa kutekeleza licha ya kupewa onyo na muda wa kurekebisha kasoro zilizobainishwa. Alibainisha kuwa leseni hizo zilifutwa kufuatia ukiukwaji mkubwa wa masharti, ikiwemo kuhodhi maeneo bila kuyaendeleza, kushindwa kulipa ada stahiki, kutotekeleza wajibu wa ushirikishwaji wa Watanzania pamoja na kupuuza miradi ya uwajibikaji kwa jamii. “Tunashuhudia baadhi ya watu wanamiliki leseni kwa miaka mingi bila uwekezaji wowote unaoonekana. Hii si tu inapoteza fursa za kiuchumi bali pia inachochea uharibifu wa mazingira na migogoro katika jamii,” alisema Waziri. Kwa mujibu wa waziri huyo, leseni 40 za utafiti wa madini zilizofutwa ni sawa na eneo lenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 900 sawa na hekari 188,163. Uharibirifu wa mazingira Simulizi za watu tofauti wakiwemo wachimbaji wadogo katika maeneo mbalimbali zinaonyesha jinsi mazingira yanavyoharibiwa iwe katika hatua ya utafiti wa madini ama uchimbaji wenyewe. “Usiku mvua ikinyesha kidogo tu… asubuhi tunakuta shimo limejaa maji na kuta zimeporomoka,” anasema Emmanuel Joseph, mchimbaji mdogo katika Mkoa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/28/kufutwa-kwa-leseni-40-za-utafiti-wa-madini-nchini-tanzania-namna-mazingira-yanavyolipa-gharama-pale-maeneo-ya-uchimbaji-yanapotelekezwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mwanaume Kenya avunja rekodi ya dunia ya Guinness kwa kupanda miti 23,326 ndani ya saa 24</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/24/mwanaume-kenya-avunja-rekodi-ya-dunia-ya-guinness-kwa-kupanda-miti-23326-ndani-ya-saa-24/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/24/mwanaume-kenya-avunja-rekodi-ya-dunia-ya-guinness-kwa-kupanda-miti-23326-ndani-ya-saa-24/#respond</comments>
					<pubDate>24 Aprili 2026 13:21:39 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/24153344/Screenshot-2026-04-24-183249-768x492.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1441</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Misitu, Misitu ya Kitropiki, Suluhu za Uhifadhi, Uanaharakati, Uanaharakati wa tabianchi, Uharakati wa Mazingira, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi wa Misitu, Upandaji Miti, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya mazingira, ameweka rekodi mpya ya dunia kwa kupanda miti 23,326 ndani ya saa 24, akivunja rekodi ya awali ya Guinness ya kupanda miti 23,060. Hillary Kiplagat Kibiwott alianzia zoezi hilo katika Kituo cha Misitu cha Kessup kilichoko katika kaunti ya Elgeyo-Marakwet, tarehe 22 [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/24/mwanaume-kenya-avunja-rekodi-ya-dunia-ya-guinness-kwa-kupanda-miti-23326-ndani-ya-saa-24/" data-wpel-link="internal">Mwanaume Kenya avunja rekodi ya dunia ya Guinness kwa kupanda miti 23,326 ndani ya saa 24</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kijana mwenye umri wa miaka 29 ambaye ni mwanaharakati wa masuala ya mazingira, ameweka rekodi mpya ya dunia kwa kupanda miti 23,326 ndani ya saa 24, akivunja rekodi ya awali ya Guinness ya kupanda miti 23,060. Hillary Kiplagat Kibiwott alianzia zoezi hilo katika Kituo cha Misitu cha Kessup kilichoko katika kaunti ya Elgeyo-Marakwet, tarehe 22 Aprili, 2026 chini ya uangalizi mkali wa wawakilishi wa Guinness World Records, Huduma ya Misitu ya Kenya (Kenya Forest Service) pamoja na wahudumu wa afya. Alikamilisha zoezi hilo Alhamisi, tarehe 23 Aprili. Hillary Kibiwott baada ya kukamilisha zoezi la kupanda miti 24,000 ndani ya saa 24 tu. Picha na Uzalendo News. Timu yake kuu ilijumuisha vijana waliokuwa wakichimba mashimo katika eneo la msitu lililoharibiwa lenye ukubwa wa ekari 30 na kumpa miche ya miti, pamoja na baba yake ambaye alimwelekeza na kumsaidia wakati wa zoezi hilo. Akihamasishwa na umati wa watu waliokuwa wakiimba na kushangilia huku wakitaja jina lake, wakiwemo wanafunzi wa shule za msingi, Hillary alipanda wastani wa miche 16 kwa dakika. Zoezi hilo lilikuwa likirushwa moja kwa moja mtandaoni. Wakati anafikia mwisho wa zoezi hilo, alikuwa amechoka sana kiasi kwamba alisafirishwa kwa gari la wagonjwa, lakini alirejea baada ya zaidi ya saa moja akiwa tayari kuzungumza na waandishi wa habari na umati uliokuwa ukimsubiri. Alisema lengo lake lilikuwa kuonyesha kuwa mpango wa kupanda miti bilioni 15 uliozinduliwa na Rais wa Kenya, William Ruto, unawezekana. Kuhusu changamoto wakati wa zoezi hilo, alitaja ardhi yenye milima, joto kali la mchana na baridi ya usiku kuwa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/24/mwanaume-kenya-avunja-rekodi-ya-dunia-ya-guinness-kwa-kupanda-miti-23326-ndani-ya-saa-24/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/24/mwanaume-kenya-avunja-rekodi-ya-dunia-ya-guinness-kwa-kupanda-miti-23326-ndani-ya-saa-24/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/#respond</comments>
					<pubDate>22 Aprili 2026 21:25:41 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/22211810/Screenshot-2026-04-23-001707.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1429</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maji, Mazingira, Sheria ya Mazingira, Uchafuzi, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">&#8216;Earth Day&#8217; yaadhimishwa huku wataalam wakipendekeza namna ya kudhibiti maporomoko</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Aprili 22 ni siku ambayo mataifa 193 duniani yanaadhimisha &#8216;Earth Day&#8217; kwa kufanya mambo mbalimbali, wengine wakipanda miti, kusafisha mazingira, kuondoa takataka za plastiki kwenye mifereji na shughuli nyingine zinazodhihirisha wajibu wa kila mmoja katika kulinda na kutunza mazingira. Lakini katika kitongoji cha Wage, kijiji cha Dimilo, kata ya Kibungo Juu, mkoani Morogoro, zaidi ya kaya 15 zinaadhimisha siku hiyo bila kuwa na makazi baada ya kuzikimbia nyumba zao kufuatia maporomoko ya tope  yaliyokumba eneo lao hivi karibuni. Huko wilayani Rungwe, wanasherehekea siku hii huku wakiwa na majonzi mazito kufuatia kupoteza ndugu na jamaa zao zaidi ya watu 20 waliofariki katika maporomoko yaliyosababishwa na mafuriko yaliyotokea Machi 15, 2026. Kutokea kwa maporomoko ni miongoni mwa majanga yaliyoelezwa na Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)  katika taarifa yake kuhusu mwelekeo wa mvua za masika Machi-Mei, 2026. Katika taarifa hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Dkt. Ladislaus Chang’a alisema maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (kanda ya Ziwa Victoria, nyanda za juu Kaskazini-mashariki, Pwani ya kaskazini pamoja na maeneo yaliyopo kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) katika kipindi cha miezi hiyo, vipindi vifupi vya mvua kubwa vingeweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi. Alisema matukio hayo yangeweza kuleta uharibifu wa miundombinu na mazingira, milipuko ya magonjwa, pamoja na upotevu wa mali na maisha. Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC ) nalo lilitoa tahadhari kuhusu hatari ya mvua kubwa na maporomoko ya ardhi ambayo yangeweza kusababisha uharibifu mkubwa. Mkurugenzi Mkuu wa NEMC, Immaculate Semesi, akizungumza na vyombo&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/22/earth-day-yaadhimishwa-huku-wataalam-wakipendekeza-namna-ya-kudhibiti-maporomoko-yanayosababisha-vifo-majeraha-na-kusomba-makazi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/#respond</comments>
					<pubDate>21 Aprili 2026 00:42:09 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anne Ngugi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20151506/Screenshot-2026-04-20-165755-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1399</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, Kaskazini mwa Kenya, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bustani za wanyama, Elimu ya Mazingira, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sheria ya Mazingira, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, Usafirishaji wa Wanyamapori, Wanyama, Wanyama maarufu, Wanyama wanaokula nyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Penzi hatari la mwanamke aliyeishi na duma kama mwanawe kwa miaka miwili</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[WAJIR, Kenya &#8211; Katika maeneo kame ya kaskazini mwa Kenya, maisha hayapimwi kwa saa au dakika, bali kwa uvumilivu wa nafsi dhidi ya mazingira. Hapa, katika Kaunti ya Wajir, ardhi imepasuka kwa jua kali, na upepo wa vumbi hubeba harufu ya jasho la mifugo na matumaini ya mvua isiyotabirika. Maisha ya jamii za wafugaji ni mzunguko usiokwisha wa kutafuta malisho na maji. Lakini ndani ya moyo wa jangwa hili, kumeibuka hadithi inayopinga mantiki ya asili &#8211; ya upendo uliopitiliza, hatari iliyojificha, na mipaka inayofifia kati ya binadamu na mnyama mwitu mwenye kasi kubwa. Ni hadithi ya Bishara Abdirahman Omar, mama wa watoto tisa, ambaye kwa zaidi ya miaka miwili alifanya jambo ambalo wengi wangeliona kama hukumu ya kifo. Mama huyu aliishi na duma ndani ya nyumba kama sehemu ya familia yake. Bishara anakumbuka siku hiyo kwa uwazi kabisa, kana kwamba ilitokea jana. Ilikuwa ni asubuhi yenye joto kali, na yeye alikuwa akitembea porini kutafuta kuni na kuangalia mifugo yake. Katika kichaka kimoja cha miiba, alisikia sauti dhaifu; kilio kidogo kilichofanana na kile cha mtoto wa paka aliyeishiwa nguvu. Aliposogea, alimkuta mtoto wa duma, akiwa mdogo kiasi cha kutoshea kwenye viganja vyake, macho yake yakiwa bado na ukungu wa upofu wa utotoni. “Alikuwa hana msaada kabisa. Nilimwangalia, nikatazama huku na huko nikitarajia kumuona mama yake, lakini hapakuwa na dalili yoyote. Alikuwa ameachwa peke yake kufa kwa njaa au kuliwa na fisi,” Bishara alisimulia, huku akitazama upeo wa macho. Kwa Bishara, hakuona mnyama hatari, bali aliona kiumbe aliyehitaji maziwa na joto. Bila&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/21/penzi-hatari-la-mwanamke-aliyeishi-na-duma-kama-mwanawe-kwa-miaka-miwili/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kifo cha mtalii Zanzibar: Athari zake kwa utalii na uhifadhi wa mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 21:16:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Asterius Banzi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20205836/MTALII-ALIYEKUFA-ZANZIBAR.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1415</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Utalii]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Mnamo Aprili 09, Ashley Robinson, mwenye umri wa miaka 31, Mmarekani aliyekuwa kwenye kisiwa cha Unguja na mchumba wake kwa ajili ya mapumziko, alifariki hospitalini alipokimbizwa baada ya kukutwa akiwa mahututi katika villa aliyokuwa anaishi. Chanzo cha kifo hicho bado kimegubikwa na utata. Tukio hilo limewagusa watu mbalimbali kwa namna tofauti. Kwa familia na rafiki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Kifo cha mtalii Zanzibar: Athari zake kwa utalii na uhifadhi wa mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Mnamo Aprili 09, Ashley Robinson, mwenye umri wa miaka 31, Mmarekani aliyekuwa kwenye kisiwa cha Unguja na mchumba wake kwa ajili ya mapumziko, alifariki hospitalini alipokimbizwa baada ya kukutwa akiwa mahututi katika villa aliyokuwa anaishi. Chanzo cha kifo hicho bado kimegubikwa na utata. Tukio hilo limewagusa watu mbalimbali kwa namna tofauti. Kwa familia na rafiki zake, kifo hicho kimeleta majonzi makubwa. Kifo hicho pia kimekuwa pigo kwa wafuasi wake mitandaoni, kwa sababu Ashley alikuwa ni mtu maarufu kwenye mitandao ya kijamii, aliyetumiwa na taasisi mbalimbali kama influencer kutokana na nguvu ya ushawishi aliyokuwa nayo. Kwa wadau wa sekta ya utalii na uhifadhi wa mazingira, kifo cha mtalii kinaibua maswali mazito kuhusu mustakabali wa sekta hizo. Baada ya kutokea kwa kifo hicho, Zuberi Chembela, ambaye ni Naibu Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai katika jeshi la polisi Zanzibar, alikaririwa na vyombo vya habari akisema wanamshikilia mchumba wa marehemu Ashley Joseph Isaac McCannon, na kwamba wamechukua pasi yake ya kusafiria, wakati uchunguzi ukiendelea. Kwa mujibu wa Chembela, tayari familia ya Ashley imeteua taasisi maarufu ya uchunguzi wa vifo vya ghafla na vyenye utata, ili kutafiti chanzo cha kifo hicho kwa kushirikiana na serikali ya Zanzibar, kwa lengo la kubaini kama alijiua au aliuawa. Kifo cha Ashley kinahusiana vipi na uhifadhi? Hubert Kilangali, mmoja wa watafiti wa utalii Zanzibar, anasema kuwa kwa mujibu wa utaratibu uliowekwa na Biodiversity Finance Initiative (BIOFIN), asilimia 45 ya kila ada inayolipwa na mtalii kule Zanzibar inakwenda katika kuimarisha na kulinda uhifadhi. BIOFIN ni mpango wa Shirika&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/athari-za-kifo-cha-mtalii-zanzibar-athari-zake-kwa-utalii-na-uhifadhi-wa-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Jinsi Tanzania inavyoweza kubadili athari za mabadiliko ya tabianchi kuwa chanzo endelevu cha maji</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 20:58:38 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20205640/Picha1--768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1416</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Haki za Binadamu, Kukabiliana na Mabadiliko ya Tabianchi, Mabadiliko ya Tabianchi, Mazingira, na  Uhifadhi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>DAR es SALAAM, Tanzania &#8211; Mvua imenyesha bila kukoma usiku kucha. Nyumba zimejaa maji, nyingine zimesombwa kabisa. Katikati ya taharuki hiyo, Salehe na familia yake wanajaribu kujiokoa kwa kushikilia chochote kilicho karibu nao, wengine wanashikilia miti, wengine magodoro na makabati yanayoelea juu ya maji. Hata hivyo, taswira inayotia uchungu zaidi ni ya madumu yale yale ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/" data-wpel-link="internal">Jinsi Tanzania inavyoweza kubadili athari za mabadiliko ya tabianchi kuwa chanzo endelevu cha maji</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[DAR es SALAAM, Tanzania &#8211; Mvua imenyesha bila kukoma usiku kucha. Nyumba zimejaa maji, nyingine zimesombwa kabisa. Katikati ya taharuki hiyo, Salehe na familia yake wanajaribu kujiokoa kwa kushikilia chochote kilicho karibu nao, wengine wanashikilia miti, wengine magodoro na makabati yanayoelea juu ya maji. Hata hivyo, taswira inayotia uchungu zaidi ni ya madumu yale yale ya njano ambayo hutumika wakati wa ukame kununulia maji, sasa yanaelea juu ya maji mengi kupita kiasi. Ni picha inayobeba ukweli mchungu: katika enzi ya mabadiliko ya tabianchi, jamii zinakabiliwa na ukame na mafuriko kwa wakati mmoja. Swali la msingi ni: Ni kwa namna gani kero ya mvua kubwa inaweza kugeuzwa kuwa suluhisho endelevu la changamoto ya upatikanaji wa maji? Hilo ndilo swali la msingi kwa sasa, ambalo baadhi ya wataalam wanalijibu katika makala haya. Taarifa za mamlaka kuhusu mvua za masika Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa taarifa kuhusu mvua za masika. Katika taarifa yake ya mwelekeo wa mvua za masika Machi-Mei, 2026 inasema kuwa mvua hizo katika maeneo yanayopata misimu miwili ya mvua kwa mwaka (kanda ya Ziwa Victoria, nyanda za juu Kaskazini mashariki, Pwani ya kaskazini pamoja na maeneo yaliyopo kaskazini mwa mkoa wa Kigoma) katika kipindi cha miezi hiyo, vipindi vifupi vya mvua kubwa vinaweza kujitokeza na kusababisha mafuriko na maporomoko ya ardhi. Mkurugenzi Mkuu wa TMA, Ladislaus Chang’a anasema matukio haya yanaweza kuleta uharibifu wa miundombinu na mazingira, milipuko ya magonjwa, pamoja na upotevu wa mali na maisha. Anahimiza Idara ya Usimamizi wa Maafa, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/jinsi-tanzania-inavyoweza-kubadili-athari-za-mabadiliko-ya-tabianchi-kuwa-chanzo-endelevu-cha-maji/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 15:36:08 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Gerald Ahairwe]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20185806/IMG_5205-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1409</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Haki ya Tabianchi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kijamii, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maeneo yaliyolindwa, Mafuta, Maji, Mamalia, Mazingira, Maziwa, Mimea, Misitu, Samaki, Siasa za Mazingira, Uchimbaji wa Mafuta, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Wanafunzi wanane wafungwa nchini Uganda kwa kupinga EACOP</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[KAMPALA, Uganda &#8211; Wanafunzi wanane na wanaharakati wa mazingira wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela nchini Uganda kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma baada ya kuandamana kupinga mradi wa bomba la mafuta ghafi la Afrika Mashariki (East African Crude Oil Pipeline &#8211; EACOP), huku hukumu hiyo ikizua maswali mapya kuhusu haki za binadamu na uhuru wa kuandamana. Saa nne asubuhi, ndani ya Mahakama ya Hakimu Mkazi wa Buganda Road, Katikati mwa jiji la Kampala nchini Uganda, wanaharakati wa mazingira na wanafunzi wanane walifikishwa kizimbani. Wanafunzi hao wanatoka katika vyuo vikuu mbalimbali nchini Uganda, na wamekuwa gerezani tangu Agosti 1, 2025, baada ya kukamatwa wakiandamana kupinga mradi wa ujenzi wa bomba la mafuta ghafi la EACOP. Nje ya Mahakama, kulikuwa na rasharasha za mvua. Wasiwasi ulitanda miongoni mwa wanafunzi wa vuguvugu la “Students Against EACOP” waliokuwa wamefika pale ili kuhudhuria hukumu ya Mahakama hiyo dhidi ya wenzao. Hakimu Mkazi alitangaza kuahirishwa kwa hukumu yao hadi saa nane mchana. Lakini nyakati za chakula cha mchana, kabla ya saa nane, wanafunzi walio nje waliambiwa kwamba wenzao wanane wamehukumiwa kifungo cha miezi 11 jela kwa kosa la kusababisha usumbufu wa umma (common nuisance). Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Mkazi Sylvia Muwonge katika chumba chake kwenye Mahakama ya Buganda Road. Mawakili, umma au hata waandishi wa habari hawakuhudhuria. Upande wa utetezi umepinga hukumu hiyo, ukisema kuwa wanafunzi hao wamenyimwa haki ya kupewa dhamana, na vile vile kunyimwa nafasi ya kuridhisha kujitetea. Kato Tumusiime, wakili wa wanaharakati hao, anaelekeza kidole cha lawama kwa upendeleo uliokuwepo katika kesi hiyo tangu mwanzo. “Hukumu ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/wanafunzi-wanane-wafungwa-nchini-uganda-kwa-kupinga-eacop-huku-maswali-ya-mazingira-na-haki-yakizidi-kuibuka/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ushoroba wa Kwakuchinja: Manufaa yake kwa Uhifadhi na Jamii Kaskazini mwa Tanzania</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/#respond</comments>
					<pubDate>20 Aprili 2026 08:59:43 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Isack Dickson]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/20075539/Tembo-kwenye-ushoroba-wa-Kwakuchinja-upande-wa-Ziwa-Manyara.-Picha-na-Isack-Dikson.--768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1384</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati miale ya jua asubuhi ikiangaza wilaya ya Babati kaskazini mwa Tanzania, watoto kutoka kijiji cha Sangaiwe wanapita katika njia zilizopo katikati ya misitu ya asili na kwingine mashambani. Ni umbali isiozidi nusu kilomita kuelekea shule ya Msingi Burunge. Katarina Claudi mwenye umri wa miaka 12, na rafiki yake Magdalena Gabriel ni miongoni mwa wanafunzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Ushoroba wa Kwakuchinja: Manufaa yake kwa Uhifadhi na Jamii Kaskazini mwa Tanzania</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati miale ya jua asubuhi ikiangaza wilaya ya Babati kaskazini mwa Tanzania, watoto kutoka kijiji cha Sangaiwe wanapita katika njia zilizopo katikati ya misitu ya asili na kwingine mashambani. Ni umbali isiozidi nusu kilomita kuelekea shule ya Msingi Burunge. Katarina Claudi mwenye umri wa miaka 12, na rafiki yake Magdalena Gabriel ni miongoni mwa wanafunzi wa shule hiyo. Kutoka nyumbani kwao hadi hapo shuleni wanatumia dakika 20 tu. Ukiwa katikati ya madarasa ya shule hiyo iliyopo kwenye mteremko wa mlima mdogo wenye mawe makubwa kwa madogo, utasikia sauti za watoto wakiimba na kukariri masomo yao zikiwa zimechanganyikana na sauti za ndege wa porini, na kutengeneza taswira ya kipekee ya maisha yanayoendelea pembezoni mwa moja kati ya mapito muhimu zaidi ya wanyamapori nchini Tanzania. Ushoroba wa Kwakuchinja ni njia muhimu ya asili inayounganisha Hifadhi za Taifa za Tarangire na Ziwa Manyara. Wanyamapori kama tembo, nyumbu, pundamilia na twiga huutumia kuhama kwa uhuru kutoka sehemu moja kwenda nyingine kutafuta maji na malisho. Manufaa ya ushoroba Wilfred Mariani Makamu mwenyekiti wa hifadhi ya Burunge, anasema kuwepo kwa ushoroba kwa huo kumeleta manufaa makubwa si kwa uhifadhi tu, bali pia kwa jamii zinazozunguka hifadhi ya Burunge. Anasema kutokana na kuwepo kwa ushoroba huo wananchi kwanza wananufaika na mapato yanayopatikana kupitia utalii ambayo kwa usimamizi mzuri wa Jumuiya ya Hifadhi ya Jamii ya Burunge, (Burunge WMA) hurudi moja kwa moja kwa wananchi kupitia njia mbalimbali ikiwa ni pamoja na miradi ya maendeleo, kielimu na kijamii. Kwa mfano, kupitia ushoroba huo, shule mbili; sekondari ya Burunge&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/20/ushoroba-wa-kwakuchinja-manufaa-yake-kwa-uhifadhi-na-jamii-kaskazini-mwa-tanzania/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uhasama waikumba jamii adimu ya sokwe katika mbuga ya kitaifa ya Uganda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/#respond</comments>
					<pubDate>17 Aprili 2026 07:28:46 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Keith Anthony Fabro]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/23073935/Screenshot-2026-04-23-103518-768x507.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1433</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Uganda]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bustani za wanyama, Ikolojia, Magonjwa ya Zoonotiki, Mazingira, Misitu, Sokwe, Tabia za Wanyama, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Jamii ya sokwe katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale nchini Uganda iligawanyika katika makundi hasimu na kushambulia washirika wa zamani, katika kile watafiti wanakifafanua kuwa ni &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya nadra vya sokwe. Utafiti huo mpya, uliochapishwa kwenye jarida la Science, unaangazia uchunguzi wa takriban miongo mitatu kwenye tovuti ya utafiti wa sokwe wa Ngogo, ukiongozwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/" data-wpel-link="internal">Uhasama waikumba jamii adimu ya sokwe katika mbuga ya kitaifa ya Uganda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Jamii ya sokwe katika Mbuga ya Kitaifa ya Kibale nchini Uganda iligawanyika katika makundi hasimu na kushambulia washirika wa zamani, katika kile watafiti wanakifafanua kuwa ni &#8220;vita vya wenyewe kwa wenyewe&#8221; vya nadra vya sokwe. Utafiti huo mpya, uliochapishwa kwenye jarida la Science, unaangazia uchunguzi wa takriban miongo mitatu kwenye tovuti ya utafiti wa sokwe wa Ngogo, ukiongozwa na mtaalamu wa wanyama Aaron A. Sandel wa Chuo Kikuu cha Texas huko Austin, nchini Marekani. Yeye na wenzake wanasema hili ni tukio la nadra linaloweza kutokea mara moja tu kila baada ya miaka 500. Limezingatiwa mara moja tu awali na wanadamu. Kabla ya mgawanyiko huo, jamii ya Ngogo ilikuwa kubwa isivyo kawaida, ikiwa na takriban sokwe 150 hadi 200 (Pan troglodytes), na kuifanya kuwa mojawapo ya makundi makubwa zaidi ya sokwe kuwahi kurekodiwa porini. Baada ya mpasuko huo, jamii iligawanyika katika makundi mawili, ambayo watafiti wameyaita makundi ya Kati na Magharibi, yaliyopewa jina la sehemu za misitu walimoishi. Kabla ya sokwe wa Ngogo kugawanywa katika makundi mawili, ilikuwa mojawapo ya makundi makubwa zaidi kuwahi kurekodiwa: kati ya wanyama 150 &#8211; 200. Picha na Aaron Sandel. Kati ya mwaka 2018 na mwaka 2024, kundi la sokwe wa Magharibi lilifanya mashambulizi 24 kwenye kundi la sokwe wa Kati, na kuua angalau wanaume wazima saba na watoto wachanga 17. Sandel aliiarifu Mongabay kuwa mzozo huo bado unaendelea na huenda ukawa na matokeo ya kudumu kwa idadi ya sokwe. &#8220;Kundi la sokwe wa Kati liko hatarini &#8211; wamekuwa na ongezeko kubwa la vifo,&#8221; Sandel alisema. &#8220;Swali kuu ni: Je,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/17/uhasama-waikumba-jamii-adimu-ya-sokwe-katika-mbuga-ya-kitaifa-ya-uganda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 19:32:53 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/14182846/mawe2-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1351</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Sera za Mazingira, Uchafuzi, Uharibifu wa Makazi, Uharibifu wa Makazi ya Asili, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Vita dhidi ya uchimbaji holela wa mawe Mwanza yahitaji elimu na uwajibikaji kuishinda</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la kwanza hapa. Licha ya kuwepo kwa Sera ya Taifa ya Mazingira ya mwaka 2021, Sheria ya Usimamizi wa Mazingira ya mwaka 2004 pamoja na mikakati mbalimbali ya usimamizi wa mazingira, ikiwemo Mpango Kabambe wa Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (2022-2032), bado uchimbaji holela wa mawe umeendelea kuwa jinamizi linalowaumiza wakazi jijini Mwanza. Akizungumzia sababu za hali hiyo kuendelea, Laurent Kitogo, Afisa wa Mazingira kutoka Environmental Management and Economic Development Organization (EMEDO), anataja udhaifu katika usimamizi pamoja na utekelezaji wa sheria kuwa kikwazo kikubwa. “Sheria ni eneo moja na usimamizi wake ni jambo jingine. Tunazo mamlaka kuanzia ngazi za mitaa, vijiji na maeneo yote ambayo watu wanaishi. Sheria imeelekeza kabisa kwamba kutakuwa na maafisa wa mazingira kuanzia ngazi ya mtaa, lakini ukiangalia kwa uhalisia ulivyo, utaona maafisa wa mazingira wanaanzia ngazi ya halmashauri. Huwezi kumkuta afisa wa mazingira katika ngazi ya kata,” anasema. David Joseph, Mkuu wa Idara ya Maliasili na Mazingira jijini Mwanza, anasema kuwa katika Halmashauri ya Jiji la Mwanza hakuna eneo lililotengwa kwa ajili ya uchimbaji wa mawe, na kwamba wanaochimba, baadhi wanakuwa wanasawazisha viwanja vyao kutokana na kuwa na asili ya miamba, au ni wavamizi ambao wameona hiyo kama fursa ya ujasiriamali. “Watu wanachimba mawe katika miktadha kuu miwili. Moja, asili ya Mwanza ni milima, na sehemu nyingi zina mawe. Hata kama ni tambarare, utakuta kuna mawe…kwa hiyo watu wengine wanachimba yale mawe ili kusawazisha viwanja vyao…hayo mawe&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-vita-inayohitaji-elimu-na-uwajibikaji-kuishinda/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Uchimbaji holela wa mawe Mwanza waathiri mazingira na jamii</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/#respond</comments>
					<pubDate>14 Aprili 2026 18:39:24 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Dominic Allen]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/15174750/Screenshot-2026-04-14-231107.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1346</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Ardhi iliyoharibika, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Mageuzi ya Ardhi, Mimea, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Makazi, Utawala, na  Wanyama]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la pili hapa. Ni asubuhi, na kwa mbali jua linaanza kuchomoza juu ya vilima vya Jiji la Mwanza. Juma anaingia kazini, katikati ya miamba mikubwa ya mawe, mahali anapopaita ofisi yake. Kila siku hufika hapo kutafuta riziki [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/" data-wpel-link="internal">Uchimbaji holela wa mawe Mwanza waathiri mazingira na jamii</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza la mfululizo wa makala kuhusu uchimbaji holela wa mawe jijini Mwanza. Soma toleo la pili hapa. Ni asubuhi, na kwa mbali jua linaanza kuchomoza juu ya vilima vya Jiji la Mwanza. Juma anaingia kazini, katikati ya miamba mikubwa ya mawe, mahali anapopaita ofisi yake. Kila siku hufika hapo kutafuta riziki kwa kuponda mawe na kuyauza. Kabla hajapiga nyundo yake kwenye jiwe la kwanza, anafunga macho kwa sekunde chache, moyo wake umejaa hofu na mashaka. Ameshuhudia wenzake wakipoteza maisha baada ya kupondwa na mawe au kufukiwa na vifusi bila msaada. Kwa Juma, maisha yake ni bahati nasibu. Kila siku ni uchaguzi kati ya uhai na kifo. Juma ni miongoni mwa wakazi wengi wa Jiji la Mwanza ambao wanaishi kwa kujishughulisha na upasuaji na uuzaji wa mawe, shughuli ambayo licha ya kuwa na madhara mengi kwa mazingira, afya, jamii na hata kusababisha vifo, vita dhidi yake inaendelea kuwa ngumu kutokana na changamoto mbalimbali. Mchakato hatari wa uchimbaji mawe Jiji la Mwanza nchini Tanzania limeendelea kukua kwa kasi, likichochewa na ongezeko la watu na mahitaji ya makazi pamoja na miundombinu. Jiji hili lenye asili ya milima na miamba linafanya uchimbaji kuwa sehemu muhimu ya maisha ya kila siku, ukitoa ajira na kuchangia upatikanaji wa malighafi za ujenzi zinazohitajika. Hata hivyo, nyuma ya faida hizi za kiuchumi, shughuli hizi zinatishia utunzaji wa mazingira na jamii, kwa kuathiri ardhi, bioanuai, usalama wa wachimbaji wenyewe pamoja na wakazi wanaoishi karibu na maeneo ya uchimbaji. Hatari ya kwanza ya shughuli hii inatokana&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/14/uchimbaji-holela-wa-mawe-jijini-mwanza-jinamizi-linalofumbiwa-macho/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/#respond</comments>
					<pubDate>12 Aprili 2026 14:52:07 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/12143649/Green-Climate-Fund.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1342</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Fedha na .Mabadiliko ya Tabianchi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">GCF yaongeza washirika hadi 168 huku Kenya ikipata miradi ya tabianchi ya $493 milioni</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Green Climate Fund (GCF) kwa sasa una washirika 168 waliothibitishwa, baada ya kuongeza washirika 10 zaidi katika kikao cha bodi kilichofanyika katika makao makuu yake nchini Korea Kusini mwishoni mwa Machi 2026. Hii inaongeza idadi ya nchi zinazoendelea na wadau wanaoshirikiana na mfuko huo kubaini maeneo na njia bora zaidi ya kuleta mabadiliko chanya kwenye  tabianchi. Kwa mujibu wa taarifa ya GCF kwa Mongabay, kwa sasa mfuko huo unaunga mkono miradi minne nchini Kenya na miradi 23 ya kikanda inayohusisha nchi nyingi. “GCF hutoa ufadhili kupitia washirika waliothibitishwa; taasisi za kifedha zilizoidhinishwa kufanya kazi na mfuko huu. Taasisi hizi zinakidhi viwango vya GCF na zinaendana na dhamira ya mfuko ya kuleta mabadiliko chanya katika kukabiliana na tabianchi,” alisema Catherine Koffman, Mkurugenzi wa Idara ya Kanda ya Afrika wa GCF. Katika barua pepe kwa Mongabay, Rebecca Phwitiko, Mtaalamu wa Mawasiliano wa GCF (Vyombo vya Habari na Maudhui), alieleza kuwa maeneo makubwa wanayolenga kufanyia kazi yanajumuisha kuimarisha minyororo ya thamani ya kilimo inayostahimili mabadiliko ya tabianchi katika maeneo yenye ukame. Mengine ni kurejesha maeneo ya malisho na vyanzo vya maji vilivyoharibika ili kuboresha upatikanaji wa maji na maisha ya watu, kupanua matumizi ya nishati jadidifu na nishati safi za kupikia, pamoja na kufungua fursa za ufadhili mseto kwa teknolojia rafiki kwa tabianchi kupitia taasisi za kifedha za ndani. Miradi inayoungwa mkono na GCF nchini Kenya yenye thamani ya $493 milioni inalenga kuleta manufaa makubwa, “ikiwa ni pamoja na kuboresha usalama wa chakula, kuimarisha ustahimilivu wa maji, kupunguza uzalishaji wa hewa ukaa, na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/12/gcf-yaongeza-washirika-hadi-168-huku-kenya-ikipata-miradi-ya-tabianchi-ya-493-milioni/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mbinu ya kutumia pilipili kufukuza tembo inasaidia uhifadhi na kupunguza migogoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/#respond</comments>
					<pubDate>07 Aprili 2026 19:57:21 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Christopher Kidanka]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/07192518/Meneja-Mradi-wa-Tembopilipili-Francis-Ndelema-akionesha-jinsi-ya-kuzungushia-wigo-wa-pilipili-shambani-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1325</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Mgogoro wa Binadam na Tembo]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>MANYARA, Tanzania &#8211; Emmanuel Mwita, mkulima katika Kijiji cha Vilima Viwili, wilayani Babati katika Mkoa wa Manyara, Kaskazini mwa Tanzania, anakumbuka uharibifu mkubwa aliokuwa akifanyiwa na tembo katika shamba lake la mahindi. “Kuna wakati tembo walikuwa wanaingia na kula kila kitu, shamba lote linabaki kama uwanja. Sikuwa navuna kitu. Nilibaki na njaa tu,” anasema Mwita, [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/" data-wpel-link="internal">Mbinu ya kutumia pilipili kufukuza tembo inasaidia uhifadhi na kupunguza migogoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[MANYARA, Tanzania &#8211; Emmanuel Mwita, mkulima katika Kijiji cha Vilima Viwili, wilayani Babati katika Mkoa wa Manyara, Kaskazini mwa Tanzania, anakumbuka uharibifu mkubwa aliokuwa akifanyiwa na tembo katika shamba lake la mahindi. “Kuna wakati tembo walikuwa wanaingia na kula kila kitu, shamba lote linabaki kama uwanja. Sikuwa navuna kitu. Nilibaki na njaa tu,” anasema Mwita, na kuongeza: “Niliwachukia sana wanyama hao kwa kunirudisha nyuma.” Matukio ya migogoro kati ya wanyama, hususan tembo, na binadamu mara nyingi yamekuwa yakisababisha hasara kwa wakulima, majeruhi na hata vifo kwa upande wa binadamu na kwa upande wa tembo. Wengine wamekuwa wakiuawa na wananchi waliokasirishwa na uharibifu wa wanyama hao. Tembo Pilipili inavyooanisha dhana zinazokinzana Katika kuoanisha dhana mbili ambazo kwa kawaida hukinzana; kupambana na wanyama waharibifu kwa upande mmoja na uhifadhi kwa upande mwingine, asasi ya Tembo Pilipili ilibuni mradi unaoendeleza uhifadhi wa wanyama walio hatarini kutoweka, hasa tembo, na papo hapo kuondoa migogoro baina ya tembo na binadamu. Tembo Pilipili ni mradi ulioanzishwa mwaka 2021 ukilenga kutumia mbinu za kijamii kusaidia tembo na binadamu kuishi kwa pamoja bila migogoro. Ukiendeshwa na asasi inayojulikana kama Tembo Pilipili (TPP), mradi unafanya kazi katika maeneo yanayopakana na hifadhi za wanyama kama vile Tarangire, Ruaha, Selous, Serengeti na Mikumi. Licha ya kudhibiti migogoro, mradi huo unasaidia wakulima kuzuia tembo wasiharibu mazao yao bila kuwadhuru. Pilipili-ikiwa-imeanikwa-kabla-ya-kuitumia. Picha kwa hisani ya mradi wa Tembo Pilipili. Francis Ndemela, Meneja wa Mradi wa Tembo Pilipili, anasema: “Tulibuni mbinu hizi kwa ajili ya kusaidia uhifadhi na wakati huohuo kuondoa migogoro baina ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/mbinu-ya-kutumia-pilipili-kufukuza-tembo-inasaidia-uhifadhi-na-kupunguza-migogoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/#respond</comments>
					<pubDate>07 Aprili 2026 13:39:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Elodie Toto]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/15164710/Screenshot-2026-04-15-194412-768x504.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1359</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Haki za Ardhi, Haki za Kimazingira, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maeneo yaliyolindwa, Mamalia, Mazingira, Misitu, Sera za Mazingira, Sheria ya Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Wasiwasi kuhusu wanyamapori bado unaendelea licha ya uamuzi wa mahakama ya Kenya kuhusu Luxury Safari Camp</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Huu ni mwisho wa sakata ambalo limevutia wapenzi wa mazingira na utalii nchini Kenya kwa miezi sita iliyopita. Mahakama ya Mazingira na Ardhi, ikifanya kikao chake mjini Narok, ilitupilia mbali ombi lililowasilishwa Agosti 2025 na Meitamei Olol Dapash, mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Wamasai, Utafiti na Uhifadhi. Mhifadhi huyo wa mazingira alikuwa akipinga ufunguzi wa Ritz-Carlton, Masai Mara Safari Camp, inayoendeshwa na Lazizi Mara Ltd. “Mahakama inaona haina mamlaka ya kushughulikia suala hili kwa sababu kuna mifumo mbadala ya utatuzi wa migogoro ambayo haikutumiwa na mlalamikaji, hivyo kesi hii iliwasilishwa kabla ya muda wake, na mahakama imeondolewa mamlaka ya kuisikiliza. Bila mamlaka, mikono ya mahakama imefungwa,” uamuzi wa mahakama unasema. Uamuzi wa mahakama unaeleza kuwa mlalamikaji, kabla ya kufungua shauri, alipaswa kuwasilisha malalamiko chini ya Kifungu cha 117 cha Sheria ya Uhifadhi na Usimamizi wa Wanyamapori, ambacho kinataka njia zote za utatuzi, ikiwa ni pamoja na zile za kijamii, zitumike, na pia kukata rufaa chini ya Kifungu cha 129 cha Sheria ya Usimamizi na Uratibu wa Mazingira. Ili kupata taarifa zaidi, Mongabay iliwasiliana na mahakama ya Narok na mamlaka za kaunti, lakini hawakujibu ombi letu la kufanyiwa mahojiano. Kwa mtazamo wa wahifadhi wa mazingira kama Johnson Yiamat, uamuzi huo unatuma ujumbe usio sahihi. “Ninahisi kwamba matokeo ya kiutaratibu hayapaswi kufunika kiini cha hoja zilizowasilishwa,” alisema kupitia ujumbe aliotuma kwa Mongabay. Yiamat ni Mmasai na mwanzilishi wa Osotua Green Alliance, shirika linaloongozwa na jamii lililojikita katika masuala ya uhifadhi wa bioanuwai, hatua za kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi na uwezeshaji wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/07/wasiwasi-kuhusu-wanyamapori-bado-unaendelea-licha-ya-uamuzi-wa-mahakama-ya-kenya-kuhusu-luxury-safari-camp/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kenya kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama barani Ulaya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/#respond</comments>
					<pubDate>03 Aprili 2026 21:12:34 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/07185248/Swala-wa-milimani.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1322</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Haki za Kimazingira, Maendeleo Endelevu, Maeneo yaliyolindwa, Sayansi ya Uhifadhi wa Mazingira ya Kitropiki, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Ufugaji wa Uhifadhi, Uhifadhi, Uhifadhi nje ya Makazi ya Asili, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uongozi wa Uhifadhi, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya &#8211; Hifadhi ya Wanyamapori ya Mount Kenya (MKWC) iko mbioni kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama za Ulaya, hatua inayolenga kuongeza idadi ya miongoni mwa swala walio hatarini zaidi kutoweka barani Afrika. Uhamisho wa swala hao wa kiume uliongozwa na wataalamu kutoka bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/" data-wpel-link="internal">Kenya kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama barani Ulaya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya &#8211; Hifadhi ya Wanyamapori ya Mount Kenya (MKWC) iko mbioni kupokea swala wa milimani wanne kutoka bustani za wanyama za Ulaya, hatua inayolenga kuongeza idadi ya miongoni mwa swala walio hatarini zaidi kutoweka barani Afrika. Uhamisho wa swala hao wa kiume uliongozwa na wataalamu kutoka bustani ya Wanyama ya Chester nchini Uingereza, kwa ushirikiano na Shirika la Huduma za Wanyamapori la Kenya (KWS) pamoja na European Association of Zoos and Aquaria (EAZA), na the European Association of Zoos and Aquariums. Katika taarifa iliyotumwa kwa Mongabay, Bustani ya Chester ilisema wataalamu wake walitumia zaidi ya miaka 11 kuratibu mpango wa uzalishaji (breeding program) katika bustani za uhifadhi barani Ulaya. “Swala hawa wanne wa kiume walioteuliwa kwa kuzingatia umri, afya na vinasaba: watakuwa wa kwanza kabisa kuhamishwa kutoka bustani za wanyama za Ulaya kwenda Kenya kama sehemu ya juhudi za kurejesha spishi hii porini.” “Ushirikiano kama huu ni muhimu sana ikiwa tunataka kuzuia spishi hii adimu kutoweka kabisa,” Nick Davis, Meneja Mkuu wa Mamalia katika Bustani ya wanyama ya Chester na mratibu wa mpango wa uzalishaji wa Ulaya, alisema katika taarifa hiyo. “Unaonyesha jinsi bustani za kisasa za wanyama zinazoongozwa na sayansi zinavyochangia kwa kiasi ikubwa urejeshaji wa spishi hizi zilizo katika hatari ya kutoweka”. Tathmini ya mwaka 2016 ya IUCN ilibainisha kuwa swala hawa wanaoishi misituni walikuwa katika hatari kubwa ya kutoweka ambapo idadi ya wale waliofikia umri wa kukomaa waliobaki porini walikuwa kati ya 70 hadi 80. Idadi hii ilikuwa ya wanyama wote wa aina hii walioko nchini&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/04/03/kenya-kupokea-swala-wa-milimani-wanne-kutoka-bustani-za-wanyama-barani-ulaya/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Udhibiti wa ukataji misitu nchini Tanzania: Ni vita kati ya uhai na uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 22:38:48 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31201251/MKAA-1-12-machi9-2026-768x498.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1289</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Kijani, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Maendeleo Endelevu, Maendeleo ya Jamii, Mazingira, Misitu, Miti, Nishati, Nishati Endelevu, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Urejeshaji wa Ikolojia, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Ni Alfajiri, siku ya Jumamosi, Mariana anadamkia kwenye kibanda chake cha kuuza mkaa ili kupakua mkaa kutoka kwenye magunia na kuuweka kwenye mifuko midogo midogo ili ifikapo asubuhi, awe tayari kuwauzia wateja wa rejareja. Anafahamu mkaa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Udhibiti wa ukataji misitu nchini Tanzania: Ni vita kati ya uhai na uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Ni Alfajiri, siku ya Jumamosi, Mariana anadamkia kwenye kibanda chake cha kuuza mkaa ili kupakua mkaa kutoka kwenye magunia na kuuweka kwenye mifuko midogo midogo ili ifikapo asubuhi, awe tayari kuwauzia wateja wa rejareja. Anafahamu mkaa unaharibu misitu, lakini hana njia nyingine ya kupata riziki ya kila siku kwa ajili yake na watoto wake watatu. Kwa Mariana, kila mfuko anaouza, ni chakula kwa watoto wake, lakini kwa upande wa uhifadhi, ni kifo kwa misitu zaidi katika eneo lake. Hadithi ya Mariana ni kielelezo cha kweli kinachoonyesha hali halisi inayoendelea kwenye jamii mbalimbali nchini Tanzania, ambazo licha ya jitihada na miradi mbalimbali inayoendelea kulinda na kuhifadhi misitu, bado wanaendelea kukata miti kwa matumizi mbalimbali. Kwa Mariana na jamii nyingi nchini, kuacha kukata misitu ni kuchagua uhifadhi badala ya uhai wao. Hii ina maana kwamba hatua hiyo itawafanya wapoteze njia pekee ya kujipatia riziki. Misitu ni msingi wa maisha bora kwa wanadamu na viumbe hai vingine, na pia husaidia kujenga uhusiano wa kutegemeana baina ya mifumo mbalimbali ya maisha. Kwa mujibu wa Shirika la Chakula na Kilimo Duniani (FAO), misitu ni nyezo muhimu ya kuondoa umaskini katika jamii zenye kipato cha chini au zisizokuwa na kipato cha kueleweka, kwani huzikinga na majanga mbalimbali ya kiuchumi na kimazingira. Kulingana na Benki ya Dunia, maisha ya watu wapatao bilioni 1.6, ambayo ni zaidi ya asilimia 25 ya watu maskini duniani, hutegemea misitu katika maisha yao,&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/udhibiti-wa-ukataji-misitu-nchini-tanzania-ni-vita-kati-ya-uhai-na-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 22:09:02 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Deodatus Mfugale]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31212151/MSARAZA-PWANI-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1301</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Misitu, Miti, Nishati, Nishati Endelevu, Nishati Mbadala, Siasa za Mazingira, Siasa za Nishati, Suluhu za Uhifadhi, Uharibifu wa Misitu, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mikakati kuokoa misitu Tanzania: Mafanikio, changamoto na mipango ya baadaye</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu uharibifu wa misitu Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Tanzania imekuwa ikichukua hatua mbalimbali ili kupunguza au kumaliza kabisa ukataji ovyo wa misitu ambao kwa sasa ni tishio la kitaifa. Jitihada hizo zinaongozwa na sera na sheria ikiwemo Sera ya Misitu ya Tanzania ya mwaka 1998.  Sera hii imekuwa ikifanyiwa marekebisho mara kwa mara ili kukabiliana na changamoto za wakati huu, na pitio la mwisho lilifanyika mwaka 2017. Miongoni mwa hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa, Kideghesho anasema ni pamoja na kuhamasisha matumizi ya nishati mbadala kama gesi na gesi asilia, gesi inayotokana na kinyesi cha wanyama. Taarifa zaidi zinaonyesha serikali imedhamiria kurejesha misitu katika eneo la hekta milioni 5.2 ambalo ardhi yake imepoteza ubora kutokana na kukatwa miti hovyo. Kuanzia mwaka 2023, serikali kwa kushirikiana na asasi za kiraia imekuwa ikitekeleza mradi mkubwa wa mageuzi ya matumizi ya nishati itokanayo na miti wenye lengo la kuboresha usimamizi na uvunaji endelevu wa misitu. Wanakijiji wa Msaraza Wilaya ya Pangani wakiandaa udongo kwaajili ya kutengeneza vitalu vya mitiche ya miti ya asili. Picha kwa hisani ya CAN Tanzania. Mradi wa Mchakato Jumuishi wa Kuleta Mabadiliko Katika Mnyororo wa Thamani wa Nishati ya Kuni (Integrated Approach for Transformation of Tanzania Fuel Wood Value Chain Project), ni mmoja wa miradi inayolenga kuboresha ustawi wa jamii zilizo pembezoni na kuhifadhi na kulinda misitu. Mradi huo unaotekelezwa katika wilaya 16 zilizopo kwenye mikoa ya Tabora, Dar es Salaam, Mwanza, Pwani, Tanga na Morogoro, unafadhiliwa na Umoja wa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/mikakati-kuokoa-misitu-tanzania-mafanikio-changamoto-na-mipango-ya-baadaye/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Baadhi ya wadau wazikataa ripoti, wadai maoni ya wananchi hayakuingizwa</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 21:18:32 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31184733/Ngorongoro3-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1283</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Chakula, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Ikolojia, Jamii Asili, Maeneo yaliyolindwa, Mazingira, Siasa za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, Urejeshaji wa Ikolojia, Utafiti, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Baada ya tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro na nyingine kuchunguza migogoro ya [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/" data-wpel-link="internal">Baadhi ya wadau wazikataa ripoti, wadai maoni ya wananchi hayakuingizwa</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la pili katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la kwanza hapa. Baada ya tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro na nyingine kuchunguza migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo, kuwasilisha ripoti zake pamoja na kutoa mapendekezo, watu mbalimbali wametoa maoni yao. Hawa ni pamoja na wenyeji wa wilaya ya Ngorongoro, wadau kutoka mashirika yasiyo ya kiserikali, Muungano wa Kutetea Haki za Wamasai (MISA), na wataalamu kutoka ndani na nje ya Tanzania. Baadhi wameyakataa mapendekezo ya tume hizo. Charles Odero, Mwanaharakati na Mkurugenzi wa Shirika la Civil and Legal Aid Organization CILAO, ambaye amekuwa akipambania haki za binadamu katika eneo la Ngorongoro, anasema kuwa hajaridhishwa kabisa na mapendekezo ya tume zote mbili. “Kama mdau sijaridhika na mapendekezo ya tume kwa sababu mbalimbali lakini moja ni kwamba yamehalalisha uporaji wa haki za jamii ya wafugaji wa asili (Wahadazabe, Wadatogana Maasai) ambao wanategemea ardhi ya Ngorongoro, Loliondo na Natron kama msingi na tegemeo la maisha yao,” anasema. Kundi la Kondoo katika kijiji cha Ololosokwan baada ya kuondolewa ndani ya kilometa za mraba 1502. Kijiji cha Ololosokwan ni miongoni mwa vijiji vilivyoathirika baada ya eneo la pori la akiba la Parloleti kuchukuliwa kutoka kwa wananchi. Picha na Yohani Gwangway. Akizungumzia suala la uhamaji wa hiari, Odero anakiri kuwa zoezi lilikuwa na kasoro nyingine na kushauri mapungufu hayo yaliyoainishwa na tume yafanyiwe kazi mara moja.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-kuhusu-ngorongoro-baadhi-ya-wadau-wazikataa-ripoti-wadai-maoni-ya-wananchi-hayakuingizwa/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Ripoti za tume mbili kuhusu Ngorongoro zafichua ukweli kuhusu uhamaji wa hiari, chanzo cha mgogoro</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/#respond</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 20:58:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Yohani Gwangway]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31183248/Ngorongoro-1-768x512.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1275</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Ikolojia, Jamii Asili, Kijani, Maendeleo ya Jamii, Maeneo yaliyolindwa, Sera za Mazingira, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Hatimaye tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mnamo mwezi Desemba mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro, na nyingine kuchunguza [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Ripoti za tume mbili kuhusu Ngorongoro zafichua ukweli kuhusu uhamaji wa hiari, chanzo cha mgogoro</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Hili ni toleo la kwanza katika mfululizo wa makala kuhusu mgogoro wa Ngorongoro, Kaskazini mwa Tanzania. Soma toleo la pili hapa. Hatimaye tume mbili zilizoundwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan mnamo mwezi Desemba mwaka 2024, moja kuchunguza zoezi la kuhama kwa hiari kwa wakazi wa Ngorongoro, na nyingine kuchunguza migogoro ya ardhi katika wilaya hiyo, zimewasilisha ripoti na kutoa mapendekezo yao. Tume hizo ziliundwa kwa lengo la kufanya tathmini ya kina na shirikishi kuhusu hali halisi ya migogoro ya muda mrefu katika eneo la Ngorongoro na kutoa mapendekezo yatakayosaidia kupata suluhisho la kudumu. Tume ya kwanza iliongozwa na Musa Iyombe ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu. Wajumbe wengine saba na nafasi zao ni; Sihaba Nkinga- Katibu Mkuu Mstaafu; Alphayo Kidata; Mohamed Mtonga; Valentino Mlowola, Balozi na Mkurugenzi wa Amani, PCCB; George Madafa, Mkurugenzi wa zamani wa Shirika la Nyumba la Taifa (NHC); Edward Maura Nduleti na Rehema Moisare wote wakazi wa Ngorongoro. Tume hii ilizinduliwa rasmi tarehe 20 mwezi Februari mwaka 2025 na kuanza kazi rasmi tarehe 25 Februari mwaka huo. Tume ya pili iliongozwa na Gerald Ndika ikiwa na wajumbe wengine ambao ni  Philemon Luhanjo ambaye ni Katibu Mkuu Mstaafu, Zakia Meghji ambaye aliwahi kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii, Jaji George Masaju (Baadaye alijiondoa baada ya uteuzi wake kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani). Wengine ni Richard Muyungi ambaye ni Mshauri wa Rais katika masuala ya Mazingira pamoja na mabadiliko ya tabianchi, Salome Sijaona, Wilbard Kombe kutoka chuo Kikuu cha Ardhi; Emmanuel Luoga&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/ripoti-za-tume-mbili-kuhusu-ngorongoro-zafichua-ukweli-kuhusu-uhamaji-wa-hiari-chanzo-cha-mgogoro/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Taasisi ya utafiti na mafunzo ya wanyamapori yaelekeza nguvu kwenye mafunzo ya vitendo kulinda mazingira</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/#comments</comments>
					<pubDate>31 Mechi 2026 20:30:06 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/31172318/Graduation1-768x512.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1273</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Ikolojia, Mazingira, Sera za Mazingira, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Utawala, Wanyama, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyama pori ya Kenya (WRTI) imefanikiwa kuhamia katika mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia umahiri (Competency-Based Education and Training), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuandaa wataalamu ambao hawaelewi tu uhifadhi, bali pia wana ujuzi wa vitendo wa kulinda wanyama pori na rasilimali asilia za Kenya. Mkurugenzi na Mtendaji [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/" data-wpel-link="internal">Taasisi ya utafiti na mafunzo ya wanyamapori yaelekeza nguvu kwenye mafunzo ya vitendo kulinda mazingira</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Taasisi ya Utafiti na Mafunzo ya Wanyama pori ya Kenya (WRTI) imefanikiwa kuhamia katika mfumo wa elimu na mafunzo unaozingatia umahiri (Competency-Based Education and Training), ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuandaa wataalamu ambao hawaelewi tu uhifadhi, bali pia wana ujuzi wa vitendo wa kulinda wanyama pori na rasilimali asilia za Kenya. Mkurugenzi na Mtendaji Mkuu wa WRTI, Patrick Omondi, alielezea hatua hiyo kama sehemu ya juhudi za kitaifa za kuimarisha uwezo wa kitaalamu katika uhifadhi na usimamizi wa wanyama pori, sambamba na kuhamia kutoka mfumo wa nadharia kwenda katika mbinu za vitendo zinazoendana na mahitaji ya soko la ajira. Omondi alitangaza mabadiliko hayo wakati wa mahafali ya 23 ya taasisi hiyo yaliyofanyika Machi 27, ambapo wahitimu wapatao 499 walitunukiwa vyeti. Mhitimu mmoja ambaye alifariki dunia kabla ya mahafali hayo, alitunukiwa cheti kwa heshima. “Tumepitia upya mitaala yetu ili kuhakikisha inabaki kuwa na uhalisia, na tunaendelea kuimarisha ushirikiano na wadau muhimu ili kuongeza ubora wa mafunzo na kuongeza fursa za ajira kwa wahitimu wetu. &#8220;Mapitio yanayoendelea ya programu za ngazi ya tano yataendelea kutuunganisha na mfumo wa kitaifa wa TVET na kuwezesha wanafunzi wetu kuendelea na masomo kwa urahisi,” alisema Omondi katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na wadau wa uhifadhi kutoka serikalini, sekta binafsi na mashirika yasiyo ya kiserikali. Baadhi ya wanufaika wa kozi fupi zilizozinduliwa hivi karibuni, zinazolenga kuwajengea uwezo wataalamu wa sekta ya wanyamapori, ni pamoja na waongoza watalii, ambao wanatarajiwa kuthibitishwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Utalii ya Kenya (TRA). Ili kuhimiza ushirikiano kati ya uhifadhi rasmi na&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/31/kuziba-pengo-la-ujuzi-na-uhifadhi-taasisi-ya-wanyama-pori-kenya-yaelekeza-nguvu-kwenye-mafunzo-ya-vitendo-kulinda-mazingira/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>1</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/#respond</comments>
					<pubDate>29 Mechi 2026 20:07:58 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Jackson Okata]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/29194055/Screenshot-2026-03-29-223905.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1262</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Biashara ya Kilimo, Bioanuai, Chakula, Ikolojia, Kilimo, Kilimo cha Kujikimu, Kilimo mseto, Kilimo-ikolojia, Maji, Mimea, Misitu, Miti, Sera za Mazingira, Siasa za Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uchafuzi, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi Unaofanywa na Jamii, na  Urejeshaji wa Ikolojia]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Wakulima wa kahawa Kenya bado wako gizani kuhusu EUDR huku ukataji miti ukiendelea kimyakimya</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NYERI, Kenya – Wakati Kenya ilipoadhimisha usafirishaji wake wa kwanza wa kahawa inayokidhi viwango vya EUDR kwenda nchini Poland tarehe 25 Machi, hali halisi kwenye maeneo ya uzalishaji ilikuwa tofauti huku ikigubikwa na ugumu usioelezeka. Huku serikali ikisherehekea kusafirisha mzigo wa magunia 320, kila moja likiwa na uzito wa kilo 60 na kutoka katika vyama 13 vya ushirika, hatua hii iliashiria mafanikio, lakini pia shinikizo. Wakulima wengi bado hawajajiandaa kwa masharti makali dhidi ya ukataji miti ambayo sasa yanaamua upatikanaji wa soko lenye faida la Ulaya. Hili ni jaribio. Mkulima wa kahawa akata mti wa mmea huo ili kuuwezesha kumea upya. Picha na Jacson Ambole, Mongabay. Chini ya jua kali la mchana katika kijiji cha Gaturere, Kaunti ya Nyeri, takribani maili 95 kaskazini-mashariki mwa Nairobi, Nichodemus Muchangi, baba ya watoto wanne, yuko shambani, akili yake ikiwa imetawaliwa na kuhudumia kahawa, jambo ambalo amefanya kwa zaidi ya miongo mitatu. Akiwa na miti 400 ya kahawa katika shamba lake la nusu ekari, Muchangi anasema hajawahi kufanya kazi nyingine tangu aliporithi ardhi hiyo kutoka kwa baba yake alipokuwa na umri wa miaka 13. Sasa ana umri wa miaka 43. Kwa mujibu wa Bruno Linyuri, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Kilimo na Chakula ya Kenya, Kenya ina takribani wakulima wadogo wa kahawa 800,000 walioko katika maeneo 33 ya uzalishaji. Wakulima hawa huzalisha takribani asilimia 70 ya kahawa ya Kenya, ambayo pia ni moja ya vyanzo vikuu vya mapato ya fedha za kigeni nchini. Maeneo ya kilimo cha kahawa nchini Kenya yanajumuisha baadhi ya maeneo muhimu sana kiikolojia, ikiwa ni&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/29/eudr-wakulima-wa-kahawa-kenya-wakabiliwa-na-kanuni-za-umoja-wa-ulaya-kuhusu-ukataji-miti-wakati-upotevu-wa-misitu-unaendelea/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 17:49:56 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Diana Wanyonyi]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://swahili.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/Screenshot-2026-03-27-200514.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1250</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Athari za Mabadiliko ya Tabianchi, Bioanuai, Elimu ya Mazingira, Filosofia ya Uhifadhi, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Hifadhi, Hifadhi za Jamii za Asili, Maendeleo ya Jamii, Mahojiano na washikadau wa uhifadhi, Misitu ya Kitropiki, Nyani, Primates, Spishi zilizo Hatarini Kutoweka, Suluhu za Uhifadhi, Tumbili, Tumbili wa Msituni, Uharibifu wa Misitu, Uhifadhi, Uhifadhi wa Wanyamapori, Usimamizi wa Misitu wa Jamii, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mangabey: Nyimbo za jadi zinavyoimarisha uhusiano wa binadamu na tumbili adimu katika misitu ya Tana</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[TANA RIVER, Kenya &#8211; Ni siku ya Jumamosi, majira ya asubuhi. Kwa mbali jua limeanza kuchomoza juu ya msitu wa Tana River, na kijiji cha Baomo kinaanza kuamka polepole. Ukimya wa asubuhi unapambwa na sauti za ndege. Ili kuingia katika kijiji hicho, kilichozungukwa na msitu, kuna njia nyembamba inayokatiza msitu na mashamba, ambayo inaelekea Baomo. Njia hiyo ya asili imeundwa kupitia shughuli za kila siku za binadamu, magari, baiskeli na pikipiki zinazoitumia mara kwa mara. Pia kuna wanyamapori wanaotumia njia hiyo wakienda kutafuta maji na malisho. Mongabay iliona kinyesi cha ndovu kilichokuwa kimesambaa barabarani na kukauka, huku vingine vikiwa bado vibichi na vikitoa harufu kali. Mbegu za mimea na majani yaliyosagika yalionekana ndani ya kinyesi hicho kilichokuwa ardhini. Kwa wakazi wa Baomo, kinyesi hicho si uchafu bali ni ujumbe kuwa wanaishi kwa ukaribu na wanyamapori wakubwa zaidi barani Afrika: ndovu. Kijiji cha Baomo kilichoko katika Kaunti ya Tana River, pwani ya Kenya, kipo karibu na Mto Tana na kimezungukwa na msitu unaohifadhi wanyamapori mbalimbali, wakiwemo fisi, tumbili, ndovu, nyati, dikdik, nyani, twiga, ndege, nyoka na wanyama wengine. Mpalawasi hawezi kukudhuru Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, na ambaye ni mkazi wa kijiji cha Baomo. Picha na Diana Wanyonyi, Mongabay. Matawi ya miti yalipoanza kutikisika mbele yangu, Mwanahamisi Kandugu Sidi, mama wa umri wa miaka 65, aliyekuja kunipokea, aliniambia: “Mwanangu usiogope, wala usihofu. Hao ni tumbili ambao pia ni jamii yetu. Sisi kama jamii ya Pokomo tunawaita ‘Mpalawasi’. Hatakudhuru kabisa, anasubiri nimwimbie wimbo wake afurahie aende zake. Subiri nimwimbie:&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/nyimbo-za-jadi-zawaunganisha-wana-ndera-na-tumbili-aina-ya-mangabey-na-red-colobus/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/#respond</comments>
					<pubDate>27 Mechi 2026 16:47:15 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Anthony Langat]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/04/06171705/Screenshot-2026-04-06-201423-768x503.png" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1312</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bahari, Baharini, Bioanuai, Bioanuai wa Baharini, Chakula, Elimu ya Mazingira, Haki za Binadamu, Haki za Wenyeji wa Asili, Ikolojia, Jamii Asili, Maendeleo Endelevu, Mazingira, Mfumo Ikolojia wa Baharini, Samaki, Sheria ya Mazingira, Uhifadhi wa Baharini, Urejeshaji wa Ikolojia, Uvuvi, na  Uvuvi wa Kupita Kiasi]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mkakati mpya wa kudhibiti upungufu wa papa nchini Kenya unalenga kuwashirikisha wavuvi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[NAIROBI, Kenya — Katika pwani ya mashariki mwa Kenya, mvuvi mdogo hubeba samaki waliovuliwa siku hiyo na kuwaweka mezani kwa ajili ya kuwakatakata tayari kwa kuuzwa. Kuna uwezekano mkubwa miongoni mwa samaki hao zimo spishi zilizo hatarini zaidi kama papa aina ya scalloped hammerhead na samaki aina ya white-spotted guitarfish. Huu ni mfano mmoja tu wa mwenendo mpana zaidi, ambao kulingana na wahifadhi wa mazingira, unaoonyesha jinsi hatma ya papa na samaki jamii ya pweza walio hatarini, ilivyofungamana kwa karibu na maisha ya wavuvi wanaojitafutia kipato katika Bahari ya Hindi ya Magharibi. Mnamo Februari, ili kuweka mpango kazi unaotekelezeka wa uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza nchini Kenya, kundi la watunga sera, wanasayansi na viongozi wa jamii walichapisha mkakati wenye malengo 19. Kati ya hayo, zaidi ya malengo 12 yanawahusisha moja kwa moja wavuvi wadogo au yanakusudia kuwashirikisha ili kuhakikisha mafanikio yake. Malengo hayo yanajumuisha kuanzisha maeneo zaidi ya bahari yanayosimamiwa na jamii, kuwashirikisha wavuvi katika maamuzi ya uhifadhi, na kuimarisha utekelezaji wa sheria kuhusu zana za uvuvi na uvuvi wa spishi zilizo hatarini. Tangu mwaka 2023, Kenya tayari ina sera ya uhifadhi wa papa na samaki jamii ya pweza — Mpango wa Kitaifa wa Hatua za Uhifadhi na Usimamizi wa Papa (NPOA-Sharks). Hata hivyo, mpango huo bado unasubiri kuidhinishwa rasmi na serikali. Mkakati uliopendekezwa na wadau unatoa njia ya jinsi ya kuutekeleza. Papa aina ya scalloped hammerhead (Sphyrna lewini), aliyepigwa picha Yonaguni, Japan. Kulingana na utafiti, spishi hii huvuliwa mara kwa mara na wavuvi wadogo nchini Kenya. Picha na Masayuki Agawa kupitia Ocean Image Bank.&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/27/mkakati-mpya-wa-kudhibiti-upungufu-wa-papa-nchini-kenya-unalenga-kuwashirikisha-wavuvi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Kifo cha Waziri Lukuvi wa Tanzania chaacha pengo katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi na uhifadhi</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mechi 2026 20:25:45 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Joyce Bazira]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Lynet]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/26202110/Lukuvi-1-768x470.jpg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1247</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Tanzania]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Elimu ya Mazingira, Haki za Ardhi, Haki za Binadamu, Haki za Kimazingira, Kilimo, Mabadiliko ya Tabianchi, Sheria ya Mazingira, Suluhu za Uhifadhi, Uhifadhi, na  Utawala]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu wa Tanzania, William Vangimembe Lukuvi, si tu pigo la kisiasa bali pia pengo kubwa kwa juhudi za uhifadhi wa mazingira nchini humo. Alipofariki dunia Machi 25, 2026, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alikuwa bado anahudumu. Aliacha nyuma urithi unaotambulika katika kusuluhisha migogoro ya ardhi katika eneo nyeti linalogusa [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Kifo cha Waziri Lukuvi wa Tanzania chaacha pengo katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi na uhifadhi</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Kifo cha aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu wa Tanzania, William Vangimembe Lukuvi, si tu pigo la kisiasa bali pia pengo kubwa kwa juhudi za uhifadhi wa mazingira nchini humo. Alipofariki dunia Machi 25, 2026, katika Hospitali ya Benjamin Mkapa, jijini Dodoma, alikuwa bado anahudumu. Aliacha nyuma urithi unaotambulika katika kusuluhisha migogoro ya ardhi katika eneo nyeti linalogusa moja kwa moja mustakabali wa rasilimali asili, hifadhi za taifa, na maisha ya jamii zinazozitegemea. Mjane wake amepoteza mume, watoto wamepoteza baba na Watanzania wamempoteza mbunge na mwanasiasa maarufu na mkongwe. Lakini kwa wapenda mazingira nchini, kifo chake kinaamsha kumbukumbu za matumaini kuhusu mafunzo aliyoyaacha katika usuluhishi wa migogoro ya ardhi, hasa kati ya wakulima na wafugaji na katika maeneo yanayopakana na hifadhi za taifa. Taarifa ya kifo cha Lukuvi, ambaye alikuwa pia Mbunge wa Jimbo la Isimani kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), ilitangazwa na Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Moses Kusiluka. “Kwa wengine, Lukuvi alikuwa na kofia nyingi tofauti. Lakini kwetu wapenda mazingira, tunamwona kama shujaa wa usimamizi endelevu wa raslimali asili. Wote tunafahamu migogoro ya ardhi mara nyingi husababisha matumizi mabaya ya maeneo ya hifadhi, uharibifu wa vyanzo vya maji na misitu. Lakini pia hupelekea kupotea kwa makazi ya wanyama pori au mimea ya asili. “Kwa ujumla, usuluhishi wa migogoro ya ardhi ni kiini cha usimamizi endelevu wa rasilimali asili. Ndiyo maana tunamuona Lukuvi kama shujaa, kwa kutambua na kuyasimamia yote hayo,’’ anasema Paul Mphizi, mwanaharakati wa masuala ya mazingira. Katika nafasi yake ya uwaziri katika wizara tofauti, Lukuvi alisimamia kikamilifu masuala ya utatuzi wa migogoro ya&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/kifo-cha-waziri-lukuvi-wa-tanzania-chaacha-pengo-katika-usuluhishi-wa-migogoro-ya-ardhi-na-uhifadhi/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
						<item>
					<title>Askari wa hifadhi wa Kenya, zaidi ya kazi ya usalama, akumbukwa kwa umahiri</title>
					<link>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/</link>
					<comments>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/#respond</comments>
					<pubDate>26 Mechi 2026 19:17:55 +0000</pubDate>
											<dc:creator>
							<![CDATA[Lynet Otieno]]>
						</dc:creator>
										<author>
						<![CDATA[Joycebazira]]>
					</author>
							<category><![CDATA[Uncategorized]]></category>
										<enclosure url="https://imgs.mongabay.com/wp-content/uploads/sites/37/2026/03/26185528/WhatsApp-Image-2026-03-16-at-15.24.45-1-768x512.jpeg" type="image/jpeg" />
					<guid isPermaLink="false">https://swahili.mongabay.com/?p=1242</guid>

					
											<locations>
							<![CDATA[Afrika, Afrika Mashariki, na  Kenya]]>
						</locations>
					
											<topic-tags>
							<![CDATA[Bioanuai, Maeneo yaliyolindwa, Misitu, Suluhu za Uhifadhi, Uhalifu kwa Wanyamapori, Uhifadhi wa Wanyamapori, Uokoaji wa Wanyamapori, na  Wanyamapori]]>
						</topic-tags>
					
					
											<description>
							<![CDATA[<p>Wakati mwili wa John Tanui unashushwa katika kaburi katika eneo moja la Bonde la Ufa nchini Kenya tarehe 25 Machi, 2026, simulizi kuhusu mwanamume ambaye wengi walitamani awe na maisha marefu duniani, ziliendelea kujadiliwa ndani na nje ya nchi. Tanui alifanya kazi kama Afisa wa Mawasiliano ya Usalama katika Hifadhi ya Wanyapori ya Lewa kuanzia [&#8230;]</p>
<p>The post <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/" data-wpel-link="internal">Askari wa hifadhi wa Kenya, zaidi ya kazi ya usalama, akumbukwa kwa umahiri</a> appeared first on <a href="https://swahili.mongabay.com" data-wpel-link="internal">Habari za uhifadhi</a>.</p>
]]>
						</description>
																					<content:encoded>
							<![CDATA[Wakati mwili wa John Tanui unashushwa katika kaburi katika eneo moja la Bonde la Ufa nchini Kenya tarehe 25 Machi, 2026, simulizi kuhusu mwanamume ambaye wengi walitamani awe na maisha marefu duniani, ziliendelea kujadiliwa ndani na nje ya nchi. Tanui alifanya kazi kama Afisa wa Mawasiliano ya Usalama katika Hifadhi ya Wanyapori ya Lewa kuanzia mwaka 1995 hadi 2024. “Tanui amekuwa Lewa kwa zaidi ya miaka 23, akisaidia kuboresha operesheni za timu za kupambana na ujangili na wafanyakazi wa hifadhi. Kama mtaalamu wa teknolojia, ndiye aliyeongoza mawasiliano ya kupambana na ujangili Lewa,” Ripoti kuhusu Athari  iliyochapishwa mwaka 2017 na hifadhi hiyo, ilieleza. John Tanui akiwa kazini. Picha na Martin Buzora kwa hisani ya Lewa Wildlife Conservancy. Ripoti hiyo pia ilibainisha kuwa ujuzi wa Tanui kuhusu wanyamapori na ndege ulikuwa wa kuvutia na kwamba alikuwa mahiri na mtu wa kujituma kuwasaidia wageni wa Lewa ambako alikuwa kama mwongozaji wao. “Kifaru wake aliyempenda zaidi ni Elvis.” Tanui alikuwa mtu ambaye alivutiwa na kushangazwa na mandhari ya wanyamapori, japo walikuwa wale wale ambao amekuwa akiwashuhudia kwa miongo kadhaa. Siku moja jioni, alipokuwa akizunguka hifadhi hiyo akiwa na mgeni, walitazama kundi la simba likipanda juu ya mti uliokuwa umeanguka. Jinsi ambavyo Tanui alishangazwa na ustadi wa simba hao kulimshtua mgeni huyo, zaidi ya kuwaona hao wanyama wenyewe. Wote wawili walitazama simba hao kwa takriban saa moja. Mgeni huyo alikuwa mkurugenzi wa EarthRanger, Jes Lefcourt. “Sijawahi kumwona akifurahia kama alivyokuwa akitazama simba hao. Hapo ndipo unapoona upendo wa kweli na kujitolea,” alisema Lefcourt katika taarifa&hellip;This article was originally published on <a href="https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/" data-wpel-link="internal">Mongabay</a>]]>
						</content:encoded>
										<wfw:commentRss>https://swahili.mongabay.com/2026/03/26/askari-wa-hifadhi-wa-kenya-zaidi-ya-kazi-ya-usalama-akumbukwa-kwa-umahiri/feed/</wfw:commentRss>
					<slash:comments>0</slash:comments>
														</item>
			</channel>
</rss>