- Visiwa maarufu vya Tanzania vya Zanzibar vinaendelea kupanua wigo wake wa utalii hadi visiwa jirani yake kama vile Pemba bila kuzingatia mazingira, tahariri mpya inasema.
- Matatizo makubwa ya uhifadhi ni pamoja na ubomoaji wa visiwa vidogo kwa ajili ya ujenzi wa nyumba za mapumziko, uharibifu wa karibu robo ya eneo la hifadhi ya Kisiwa cha Pemba ili kujenga “majengo ya mapumziko ya mazingira,” na mipango ya kuendeleza kisiwa muhimu kiikolojia cha Misali.
- “Sasa ni wakati wa serikali ya Zanzibar kuangalia upya maamuzi ya uwekezaji yaliyopita na yajayo ili kuhakikisha yanaheshimu turathi asili ya Zanzibar na kuiuhifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo,” anaandika mwandishi.
- Chapisho hili ni maoni. Maoni yaliyotolewa ni yale ya mwandishi, sio lazima yaendane na ya Mongabay.
Kisiwa cha Zanzibar kina sifa ya kuwa kisiwa cha paradiso katika Bahari ya Hindi. Kikiwa kipo kilomita 20 (maili 12) kutoka Bara la Afrika Mashariki, kisiwa hico kinatawaliwa kama sehemu isio na uhuru wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kina visiwa viwili vikubwa – Unguja (kilomita za mraba 1,666, au maili za mraba 643) kwa upande wa kusini, na Pemba (km2 988, au 381 mi2) upande wa kaskazini magharibi mwao, kila moja ni ndogo upande wa magharibi.
Visiwa hivyo ni mojawapo ya maeneo yenye wakazi wengi zaidi barani Afrika, ikiwa na jumla ya wakazi milioni 1.9, kulingana na hesabu ya watu ya mwaka 2022. Kikiwa na kiwango cha ukuaji wa watu kwa 3.8% kwa mwaka na wastani wa ukubwa wa makazi ya watu watano, kuna shinikizo kubwa kwa maliasili. Hata hivyo, visiwa hivyo bado vina misitu ya pwani ya kitropiki yenye majani mapana, miti ya zamani, na mikoko yenye spishi adimu na za kawaida. Pia, jamii bado zinategemea kwa kiasi kikubwa misitu.
Maamuzi kinzani yameibuka kati ya maendeleo na uhifadhi wa visiwa hivi: katika kipindi cha miaka 30 iliyopita, sekta kubwa ya utalii imestawi Unguja na fukwe zake za mchanga (zaidi ya hoteli 500), ingawa sio Pemba na ufuo wake mwingi wa mashaza (yenye takriban hoteli 20). Visiwa hivi sasa hupokea wageni zaidi ya 100,000 kwa mwezi katika msimu wa likizo, na wageni 106,108 mnamo Julai 2025 waliwakilisha ongezeko la 31% kutoka 2024.
Wengi wa wageni hawa huenda Unguja, ambako maendeleo mengi ya watalii yametokea bila kuzingatia mazingira. Mifano ni pamoja na barabara mpya za lami zinazopita katika Hifadhi ya Msitu wa Masingini unaohifadhiwa na kupitia msitu wa mikoko unaokamata kaboni kwenye Peninsula ya Uzi kwa Unguja – maendeleo ya haraka ambayo yanasukumwa kwa muda mfupi wa mjadala.

Sasa, serikali inataka kuwekeza kwa kiasi kikubwa Pemba, lakini kuna viongozi wa serikali na viongozi wa jamii kwenye visiwa vyote viwili wanaona maendeleo ya haraka ya miundombinu ya Unguja na utegemezi mkubwa wa sekta ya utalii kuwa ni mfano mbaya. Badala yake, wanatambua kwamba utalii mkubwa umeleta mabadiliko makubwa ya kitamaduni katika kisiwa cha kusini, na kuwasili kwa masarobaro wa pwani, pombe na dawa za kulevya kwenye hoteli za pwani, kutasababisha wasiwasi mkubwa miongoni mwa wakazi.
Kilichoko aratini kwa sasa ni iwapo mfumo wa kijamii wa Pemba utahatarishwa vivyo hivyo, na iwapo maendeleo ya kiuchumi yanayoweza kuepukika yanayotokana na utalii yatahatarisha uwezo wa vizazi vijavyo vya jamii ya Wazanzibari kufurahia yale mabaki ya turathi zao za asili na kiutamaduni.
Sehemu kubwa ya visiwa vyote viwili vinaendeleza kilimo mseto kwa ajili ya uzalishaji wa matunda, nazi na viungovya mapishi, iliyochanganyikana na mabonde kwa ajili ya kilimo cha mpunga na nyanya, na udongo mkavu wa matumbawe unaotolewa kwa ajili ya uzalishaji wa maharagwe, mihogo na karanga.
Ingawa jamii nyingi hutunza misitu ya jamii kwa ajili ya uzalishaji wa kuni, matunda na mbao, kuna misitu michache iliyohifadhiwa. Kwa Unguja, hifadhi hizi zinajumuisha Hifadhi ya Kitaifa ya Jozani-Chwaka, maarufu kwa wakazi wake wa aina ya kima punju wa Zanzibar (Piliocolobus kirkii), na hifadhi tatu za misitu, lakini hizi hazina ulinzi wa kiutendaji kutokana na ufadhili mdogo.
Kwa upande wa Pemba, kuna hifadhi tatu tu: Msitu Mkuu, Ras Kiuyu, na vito vya bioanuwai visiwani humo, Hifadhi ya Msitu wa Asili ya Ngezi-Vumawimbi, sehemu kubwa zaidi iliyosalia ya msitu wa mvua ya pwani wa Zanzibar ambao umezeeka. Lakini hata maeneo haya si salama tena katika mazingira haya mapya ya sera.
Tishio hilo kwa Zanzibar linatokana na Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar (ZIPA), chombo kilichoteuliwa na Serikali kuwatafutia wawekezaji kwa ajili ya kuendeleza hoteli katika visiwa vidogo vinavyozunguka Pemba na Unguja, kwa sababu fursa zinakwenda Unguja. Mamlaka ya ZIPA sasa inatafuta wawekezaji wa kubadilisha visiwa hivi vya pwani, na imebainisha 15 kati ya hivi kwa uwekezaji wa hoteli.
Nyingi ni maficho kwa ajili ya maisha ya ndege na popo bawa wa kawaida, na 12 kati yao ni kimbilio la mwisho la kaa maalum aina ya (Birgus latro), spishi zilizoorodheshwa kuwa katika hatari ya kutoweka. Hata hivyo, msukumo wa kuongeza vitanda umesababisha upotevu wa mimea na kusawazisha kujenga miji mikubwa, kama inavyoonekana kwenye visiwa vya Bawe na Pamunda. Usafishaji wa hivi majuzi wa kisiwa kingine ckwa jina Chapwani, umekinyima kisiwa hicho maeneo ya kutagia popo bawa wa matunda na korongo, jambo linalosababisha upotevu wa mapato kwa wasimamizi wa watalii kisiwani humo.

Kama vile inashangaza mradi wa kubadilisha sehemu kubwa ya Hifadhi ya Msitu wa Ngezi kuwa eneo la shamba: mradi wa Montuli utachukua makadirio ya ajabu ya 17% ya eneo la hifadhi, na 23% ya msitu wa juu wa hifadhi hiyo, na zaidi ya miundo 100 itajengwa, ikipendekeza eneo la maendeleo badala ya “mapumziko ya mazingira.”
Hakuna hakikisho lolote kwamba tathmini zinazoendelea za athari za mazingira – seti moja itakayofanywa na kampuni ambayo kwa kawaida huangazia miradi ya mijini – itaunda aina yoyote ya kizuizi kwa maendeleo haya, na hakuna dalili kwamba hitaji la kisheria la kutangaza msitu wa hifadhi itakuwa kikwazo, kwa kuzingatia jengo la matofali na karakana iliyojaa malori mapya yaliyoegeshwa karibu.
Ngezi imeteuliwa kama eneo muhimu la ndege, eneo euhimu la bayoanuwai lenye umuhimu wa kimataifa, na muungano wa eneo la kuzuia kutoweka kwake. Ngezi ya Kaskazini ni vito vya mimea, ikiwa na spishi sita hadi nane za mimea, msitu wa miti ya Intsia ambayo haipatikani kwingineko barani Afrika, aina ya spishi za ndege waliogunduliwa upya wanne wa kawaida, wote kwa sababu ya kuangamizwa kupitia eneo hili la mapumziko. Mashirika yasiyo ya kiserikali ya uhifadhi yanaelekea kuokoa miche kutoka kwenye msitu uliohifadhiwa ili kuepusha kutoweka!
Mazungumzo ya faragha na maafisa katika nyadhifa za serikali yanaonyesha kuwa wengi wamesikitishwa na mradi huu, ila wanahisi kutokuwa na uwezo wa kuuzuia, na mashauriano na jamii yanaonyesha kuna wasiwasi mkubwa wa kupoteza ufikiaji wa maeneo ya kutua kwa ufuo na usumbufu kwa jamii zao.
Zaidi ya hayo, maendeleo hayo yatasababisha ufukwe unaotumiwa na jamii ya Wapemba wengi kwa wikendi na sherehe za Ramadhani, na pia kwa safari za shule. Ingawa jamii ya Wapemba wengi wanathamini biashara ndogo ndogo za kitalii, unyakuzi wa ardhi ya ukubwa huu bila shaka hautakubalika kutokana na kuvurugika kwa shughuli za kiuchumi na kijamii.
Mpango wa tatu wa uwekezaji unaoonyesha kwa uwazi tofauti kati ya kulinda maliasili yenye thamani ya kitamaduni na kuwavutia wapenda likizo duniani uko kwenye eneo la Hifadhi ya Kisiwa cha Misali, kisiwa chenye umuhimu wa kidini na makazi ya popo wa pemba (Pteropus voeltzkowi) pamoja na kaa, kasa wanaotaga baharini na misubili iliyoko hatarini kutoweka.

Tena, hii ni seemu iliyohifadhiwa ambayo imepangwa kwa ajili ya maendeleo ya utalii ambayo itakuwa na athari isiyojulikana kwa kasa wanaozalia viota, miamba ya matumbawe, na baadhi ya msitu wa matumbawe usioharibika zaidi (msitu uliodumaa unaostawi kwenye chokaa ya korali isiyo na kina kirefu) kwenye pwani ya Afrika Mashariki. Warsha moja iliyowaleta pamoja wanamazingira na viongozi wa dini mwezi Aprili 2025, ambayo ilikuza wazo la kuifanya Misali kuwa Hifadhi ya Taifa ya Pemba, inahitaji kufuatiliwa na viongozi wa serikali wanaotaka kuifanya Pemba kuwa kivutio halisi cha ikolojia kwa muda mrefu. Maafisa wanaotaka kuulinda Misali wanahisi kutengwa na wengine katika serikali yao, ingawa.
Kwa bahati nzuri, kuna baadhi ya dalili kwamba sekta ya utalii kisiwani Zanzibar inataka kulinda maeneo ya mazingira na mambo ya kale. Mudrick Ramadhan Soraga, Waziri wa Utalii wa Zanzibar, amesema, “Maono yetu ya muda mrefu yanasisitiza utalii wa hali ya chini na wa thamani ya juu. Kwa kutetea maeneo ya mapumziko yanayozingatia mazingira juu ya mifano ya watalii wengi, tunalenga kulinda mazingira yetu na utambulisho wetu wa kitamaduni kwa vizazi vijavyo.”
Hata hivyo, baadhi ya watendaji wanahatarisha hili kwa maono tofauti ambayo hayana uwezo wa kuona mbele, akili timamu na wajibu kwa jamii za wenyeji, na badala yake wanafikiri kwamba ardhi yoyote “isiyotumiwa” inapaswa kufanywa kuzalisha pesa.
Shida moja ni kuamua ni maeneo gani ya mapumziko ya mazingira yanawakilisha. Kwa baadhi ya serikali na sekta ya utalii, haya yanajumuisha hoteli nzuri au majengo ya ghorofa yanayohudumia utalii wa kiwango kikubwa, lakini yamejengwa katika maeneo safi.
Kwa wengine, ni nyumba ndogo za kulala wageni zinazoathiriwa na ikolojia na vitanda vichache, njia mbadala iliyofanikiwa kuanzishwa katika maeneo machache Zanzibar kama vile bustani ya Chumbe Island Coral.

Iwapo aina ya mwisho ya hifadhi ya mazingira ingeagizwa na kufuatwa, kungekuwa na nafasi ya maelewano kati ya wale wanaotaka kutengeneza ajira mpya kwa muda mfupi, na wale wanaofikiria mustakabali wa muda mrefu wa mazingira asilia ya Pemba na uadilifu wa kitamaduni wa Zanzibar.
Muundo wa maendeleo unahitaji kufikiriwa upya ili kujumuisha kutoza kodi ya utalii kwa faida, si idadi ya vitanda (ili kuhimiza hoteli za hali ya juu, si miji mikubwa), kushauriana kwa umakini zaidi na jamii ili kubaini mahitaji yao halisi, kuiga mfano wa maeneo ya mapumziko yaliyofaulu (kama vile Chumbe, ambayo yote yanalinda mazingira na kutoa huduma za jamii), kutafuta wawekezaji wenye sifa dhabiti za kutafuta pesa badala ya wale wanaokimbilia kutafuta pesa kwa haraka na kadhalika.
Kinadharia, maendeleo ya kiuchumi (pamoja na yale yanayotegemea utalii) yanaweza kuchukua shinikizo kwa bayoanuwai iliyosalia kwa kuwa inawezesha mseto wa maisha, lakini inahitaji maendeleo ya miundombinu ambayo kwa kawaida hayana usikivu wa mazingira. Suala ni kupata usawa. Kuna mifano ya matokeo ya ushindi kwa pande zote mbili, kama vile makubaliano ya kupunguza ukataji miti wakati wa uboreshaji wa sasa wa barabara ya Ngezi, ili iweze kufikiwa.
Baadhi serikalini wana nia ya kweli na chanya ya kuwa na utalii na maendeleo endelevu na yenye manufaa kwa jamii, lakini kuna vipengele ndani ya serikali ambavyo haviendani na hili, na vinaweza kuhatarisha mipango hii mizuri.
Sasa ni wakati muafaka kwa serikali ya Zanzibar kuangalia upya maamuzi ya uwekezaji yaliyopita na yajayo ili kuhakikisha yanaheshimu turati asilia ya jamii ya Zanzibar na kuihifadhi kwa ajili ya vizazi vijavyo.
Tim Caro ni mwanaikolojia wa kitabia/mageuzi na mwanabiolojia wa uhifadhi ambaye amefanya utafiti nchini Tanzania kwa miaka 30.
Maoni haya yalichapishwa kwa mara ya kwanza hapa, kwa Kiingereza tarehe 22/10/2025